12.08.2021 Views

Mema Magzine Edition 2 #FursaKidijitali

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Nilipofika chuo, nilianza kufanya comedy

kwa kuji-record video fupi kisha naziweka

katika akaunti yangu ya Instagram. Baadae

kazi zangu zilianza kufuatiliwa sana na

nikaona nahitaji kukua zaidi. Nikaanza

kushiriki katika vichekesho vya jukwaani

(stand-up comedy). Awali nilifanya kama

msanii wa kujitegema baadae nikapata

bahati ya kuwa sehemu ya familia ya Watu

Baki, japo bado sijawa mwaanachama rasmi.

Watu Baki imekuwa ni familia, najifunza

mambo mengi kutoka kwao. Ni kundi lenye

vipaji lukuki na wengine tayari wameshakuwa

na majina makubwa.

Watu Baki nafanya nao mazoezi na kushiriki

katika tamasha linalofanyika The Base Club

kila alhamis. Mwaka huu kuna rafiki yangu ni

mchekeshaji pia alikuja na wazo la kuanzisha

kundi letu litakalo husisha wanachuo wenye

vipaji vya uchekeshaji, ndipo Unicomedy

ilipoanza. Tumekuwa tukiandaa matamasha

yetu wenyewe yanayofanyika chuoni na nje

ya chuo. Kazi yangu imenipa heshima kwa

mwaka huu kupewa tuzo ya mchekeshaji

bora chuoni kwetu.

Mwaka huu Unicomedy tumefanikiwa

kuandaa matamasha mawili na yote

yalifanya vizuri. Mwanzoni tulifanyia London

Lounge, Ubungo. Watu walihudhuria wengi na

baadhi kukosa viti. La pili tukahamia ukumbi

mwingine.

Kati ya vitu ambavyo haviwezi kuepukika ni

mitandao ya kijamii. Mitandao ya kijamii

inasaidia sana kusukuma kazi zangu kufika

mbali. Japo changamoto ukishakuwa

maarufu watu wanaanza kutumia jina lako

hali inayowapa ugumu watu wanaponitafuta.

Mitandao imesaidia sana kujenga brand

yangu na kuonyesha uwezo wangu kwa

watu. Napgia simu na kupata mialiko kuperform

katika sherehe tofauti.

Mitandao pia imenikutanisha na ma-star

wakubwa, wengine ni role model wangu.

Mfano Kendrick Mulamula kutoka Kenya,

tuliwasiliana kupitia mitandao ya kijamii na

kubadilishana namba. Mpaka leo

tunawasiliana vizuri tu. Mpaka sasa

nimefanikiwa kufanya kazi na wasanii

wakubwa tofauti kama Idris Sultan ambaye ni

role model wangu, Francis Nalimi na wengine

kutoka Watu Baki.

Comedy kwa sasa sio kama zamani ambapo

ili uonekane mchekshaji uvae kiajabu ajabu

na watu kukuona kama kituko. Na ilichangia

sana malipo madogo ukilinagnisha na

wasanii wengine wa bongo movie kwa

sababu tulionekana kama vituko tu.

Mtazamo hasa kwa Dar umebadilika sana.

Changamoto bado mikoani kama kule kwetu

Simiyu bado waigizaji wengi wamekuwa na

mtazamo wa vituko badala ya vichekesho.

Kama mwanafunzi changamoto kubwa

nayopitia ni kupigana vizinga, wanafunzi

wengi wanafikiri nina hela nyingi. Wakiona na

star mkubwa wanajua jamaa

ameshayapatia, ukimnyima hela anahisi

umemkazia. Pia nyumbani wana-support

lakini kwa mashaka. Wazazi wananilipia ada

wanahisi sanaa inaweza kuniharibia masomo.

Ila taratibu wanazidi kuelea hii ni kazi na kwa

upande wa masomo haina athari yoyote ile.

22 | AUG 2021MEMA MAGAZINE

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!