12.08.2021 Views

Mema Magzine Edition 2 #FursaKidijitali

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Waja leo, huondoki leo

ABBASI ISMAIL

Mambo vipi washikaji? Naitwa Abbasi maarufu Abby boy. Ni

mzaliwa na mkazi wa Muheza, mkoani Tanga. Leo

nakutembeza Muheza ujue yale usiyoyajua. Muheza ni wilaya

kongwe nchini ilianzishwa mwaka 1976. Kihistoria kulipiganwa

vita kati ya Wabondei na Wadigo katika pwani ya Tanga.

Wabondei walichakazwa na kukimbilia maeneo ya Muheza na

walipofika hapo walisema “Hanu Mheza” ikimaanisha hapa

mmekwisha. Kweli Wadigo waliufuata moto kwani

walitembezewa kichapo na kurudi pwani ya Tanga na mpaka

leo Wadigo wapo wengi Tanga mjini na Wabondei wakabaki

kama wenyeji hapa Muheza.

Ukipita Muheza utakuta imepambwa na mandhari ya kuvutia

yenye milima, mito na majengo ya kihistoria yaliyoachwa na

wakoloni. Wilaya ya Muheza ina mitaa mingi maarufu ikiwemo

Magila ambapo kuna shule ya kwanza ya msingi kujengwa

hapa nchini wakati wa ukoloni. Mitaa mingine ni Tongwe,

Ngomeni, Pande, Mtimbwane n.k. Wilaya yetu ina ukubwa wa

eneo la kilomita za mraba 1,470.

Mishe za kibiashara zipo kibao, muhimu kuchangamkia fursa.

Kuna mishe za kilimo kama machungwa, katani n.k. Muheza

ina vivutio vingi vya utalii ikiwemo misitu maarufu ya Amani na

Magoroto maarufu Bali of Africa. Huko kuna mambo mengi ya

kupendeza ambayo huwezi kujutia ikiwemo maporomoko ya

maji, bwawa zuri la kuogelea, wanyama kama farasi na ndege

wengi wazuri. Msitu wa hifadhi ya Amani una vipepeo wa

pekee duniani ambao wananchi huwafuga na kuwauza nje ya

nchi.

5 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE

Hamis Mwinjuma maarufu Mwana FA ni

mbunge na moja ya watu maarufu kutoka

Muheza.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!