12.08.2021 Views

Mema Magzine Edition 2 #FursaKidijitali

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Naitwa Rigeye Ally, ni mwanafunzi wa kidato

cha nne shule ya sekondari Mikocheni. Nilikuwa

pia rais wa Mema Club kuanzia mwaka 2019

mpaka 2021. Mimi ni kiongozi na nina jiamini

katika kuongoza. Ndoto yangu ni kuwa daktari

wa binadamu na kiongozi. Wanafunzi

wenzangu huniita Mema, kwa sababu nilikuwa

rais wa Mema Club tangu nikiwa kidato cha pili

mpaka cha nne. Awali sikuwa najua kama nina

karama ya uongozi.

Mara nyingi nilikuwa mstari wa mbele kutuliza

kelele katika klabu na kujitolea kufundisha

wengine masuala ya hedhi. Wanafunzi

wenzangu walianza kuvutiwa na mimi na kisha

wakanichagua kuwa kiongozi wao. Kujitolea

katika kufundisha wenzangu, kunyamazisha

kelele na kuhudhuria siku za klabu kulisaidia

kuaminiwa na kuchaguliwa kuwa kiongozi wa

klabu. Umaarufu wa uongozi wangu ulichochea

pia kuchaguliwa kuwa kiongozi wa mazingira

na afya shuleni.

Kujitolea katika kufundisha

wenzangu,kunyamazisha kelele

na kuhudhuria siku za klabu

kulisaidia kuaminiwa na

kuchaguliwa kuwa kiongozi wa

klabu.

Changamoto niliyopitia kubwa ni

wakati wa COVID19. Wasimamizi

wetu hawakuwa wanakuja kwa

tahadhari ya mikusanyiko na

mwalimu mlezi alienda

masomoni. Klabu ikawa haiendi

sawa. Baadhi ya viongozi

walihama klabu. Ila nilisimama

sana imara wakati huo.

Niliendelea kusimamia na

kufundisha kupitia vitabu vya

afya ya uzazi Mema Tanzania

walivyotuachia.Ilinisaidia sana

kunijenga kujiamini na kuwa

kiongozi bora zaidi.

Klabu yetu imekuwa inatupa

motisha kufanya vyema katika

mitihani. Kuwa kiongozi wa

Mema Club kumenipa motisha

ya kuamini naweza kuwa

kiongozi.

Rigeye Ally

Ndoto yangu ni udaktari

20 | AUG 2021MEMA MAGAZINE

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!