Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Naitwa Rigeye Ally, ni mwanafunzi wa kidato
cha nne shule ya sekondari Mikocheni. Nilikuwa
pia rais wa Mema Club kuanzia mwaka 2019
mpaka 2021. Mimi ni kiongozi na nina jiamini
katika kuongoza. Ndoto yangu ni kuwa daktari
wa binadamu na kiongozi. Wanafunzi
wenzangu huniita Mema, kwa sababu nilikuwa
rais wa Mema Club tangu nikiwa kidato cha pili
mpaka cha nne. Awali sikuwa najua kama nina
karama ya uongozi.
Mara nyingi nilikuwa mstari wa mbele kutuliza
kelele katika klabu na kujitolea kufundisha
wengine masuala ya hedhi. Wanafunzi
wenzangu walianza kuvutiwa na mimi na kisha
wakanichagua kuwa kiongozi wao. Kujitolea
katika kufundisha wenzangu, kunyamazisha
kelele na kuhudhuria siku za klabu kulisaidia
kuaminiwa na kuchaguliwa kuwa kiongozi wa
klabu. Umaarufu wa uongozi wangu ulichochea
pia kuchaguliwa kuwa kiongozi wa mazingira
na afya shuleni.
Kujitolea katika kufundisha
wenzangu,kunyamazisha kelele
na kuhudhuria siku za klabu
kulisaidia kuaminiwa na
kuchaguliwa kuwa kiongozi wa
klabu.
Changamoto niliyopitia kubwa ni
wakati wa COVID19. Wasimamizi
wetu hawakuwa wanakuja kwa
tahadhari ya mikusanyiko na
mwalimu mlezi alienda
masomoni. Klabu ikawa haiendi
sawa. Baadhi ya viongozi
walihama klabu. Ila nilisimama
sana imara wakati huo.
Niliendelea kusimamia na
kufundisha kupitia vitabu vya
afya ya uzazi Mema Tanzania
walivyotuachia.Ilinisaidia sana
kunijenga kujiamini na kuwa
kiongozi bora zaidi.
Klabu yetu imekuwa inatupa
motisha kufanya vyema katika
mitihani. Kuwa kiongozi wa
Mema Club kumenipa motisha
ya kuamini naweza kuwa
kiongozi.
Rigeye Ally
Ndoto yangu ni udaktari
20 | AUG 2021MEMA MAGAZINE