Masuala Yaliyojadiliwa - Coastal Forests of Kenya and Tanzania
Masuala Yaliyojadiliwa - Coastal Forests of Kenya and Tanzania
Masuala Yaliyojadiliwa - Coastal Forests of Kenya and Tanzania
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
REMP Technical Report 38 Muhitasari wa Majumuisho ya warsha ya utawala bora Twasalie, Rufiji<br />
• Hatuna usafiri wa haraka kama vile boti wala mtumbwi na shughuli zetu za baharini samaki na<br />
mikoko.<br />
• Mipaka sahihi haijapatikana<br />
• Ukosefu wa unifomu<br />
• Kutopewa posho ya kazi na kijiji<br />
• Kutohusishwa katika vikao vyote<br />
• Kutohusishwa katika kamati zote<br />
• Akikamatwa adui anapopelekwa kijijini siku ya pili anaondoka sababu hatuielewi.<br />
• Serikali ya kijiji yote haijui wajibu wake<br />
4.2.5 Kero za kundi la Wanawake<br />
• Hakuna miradi midogo midogo katika kijiji<br />
• Kutokuwa na huduma nzuri za jamii kama hospitali, wakunga na wahudumu wa afya<br />
• Vikao vya kijiji havipangwi na kufikia utekelezaji wake kama suala fulani likiongolewa<br />
halitekelezwi.<br />
• Kutodhibitiwa kwa wanyama waharibifu<br />
• Hakuna utekelezaji toka kwa waliopata mafunzo mbalimbali hata kwa wao kuonyesha mifano ili<br />
wananchi wajifunze kwao<br />
• Serikali ya kijiji haiitishi vikao au mikutano ya hadhara<br />
• Halmashauri ya wilaya kutoleta walimu kwani mwalimu yupo mmoja kwa jina siyo kwa kufanya<br />
kazi<br />
• Sisi wote tumehesabiwa kama jamii ya jinsi moja bila kujali jinsia, lakini kuna mganga mmoja wa<br />
kiume ambaye masuala yote yanayohusu wanawake hafanyi kama vile kupima ujauzito kupima<br />
watoto na kuzalisha<br />
• Wananchi kutokujulishwa mapato na matumizi ya fedha za serikali ya kijiji<br />
• Mwenyekiti wa serikali ya kijiji vikao vikiitishwa huwa haudhurii mara nyingi anaendelea na yake<br />
bila taarifa zozote.<br />
• Kikundi cha umoja wa kinamama hakina nguvu kwa kukosa fedhaa/elimu ya kukiinua.<br />
• Serikali haijatoa msukumo/elimu yoyote baada ya zao la minazi kufa na korosho kutokuzaa ili<br />
kupata mazao mbadala.<br />
• Vikiitishwa vikao na kualika mheshimiwa Diwani, Afisa mtendaji Kata hawahudhurii.<br />
• Vijana hawajishughulishi na mradi wa MUMARU hapa kijijini.<br />
4.2.6 Kero za kundi la Mambwiga<br />
• Wenyeviti wa vitongoji hawana muamko katika shughuli za maendeleo.<br />
• Mambwiga wengine hawafuatilii utoaji na upokeaji taarifa.<br />
• Wananchi wengi hawaitikii taarifa zinazotelewa na Mabwiga kama vile kuitikia mikutano au<br />
masomo.<br />
• Mradi hautoi motisha kwa mabwiga kama vile kupewa sare za nguo (k<strong>of</strong>ia shirt, khanga)<br />
4.2.7 Kero za kundi la Vijana<br />
• Wazee hawataki tushiriki katika mradi .<br />
a) Baada ya mawasilisho ya kila kikundi, yapo masuala yaliyojitokeza ambayo yalitolewa maswali na<br />
majibu kwa washiriki. Kwa kuwa Afisa Mtendaji Kata alikuwepo siku ya kwanza ya warsha, suala la<br />
kutoshirikishwa kijiji cha Twasalie na kijiji cha Msala katika uwekaji wa mipaka ya kijiji, lilisemwa wazi<br />
na lilionyesha kukera sana washiriki wengi hasa kundi la wazee. Afisa Mtendaji wa kata alilaumiwa sana<br />
kuwa hajashirikisha wahusika yaani wanavijiji wa vijiji vyote viwili, mjadala huu ulichukua muda katika<br />
kujadiliwa, mwishoni mwezeshaji aliwaomba washiriki wasuburi na badaye itakap<strong>of</strong>ikia wakati wake<br />
waweke mikakati ya kuondoa hitilafu iliyotokea katika utatuzi wa mipaka.<br />
4