constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
24<br />
Elisha Ochieng; (Ziwani resident) Anatuaribia maisha, mnikiwa na pesa yangu kidogo, anaenda kuita serikali, hati sijui nini na<br />
nini.<br />
Wengi wetu wazazi hawafanyi kazi, ningeomba kuwa shule, watoto wawachiliwe wasome bure, hata kama ni mpaka standard<br />
8.<br />
Matibabu pia iwe bure.<br />
Julius Mwangi: Kwanza nataka kushukuru, <strong>commission</strong>ers kwa kazi nzuri wamefanya na uvumilivu wao.<br />
Sheria zaa ardhi zilizopo sasa zinafinya wanainchi wa kawaida sana, kwa sababu wengi hawana ardhi na watu wale wakubwa<br />
walikuwa tangu wakati wa ukoloni wakinyakua ardhi iliyokuweko na mpaka wakati huu wamezidi kabisa. Tuna taka sheria<br />
ambayo itatumiwa ile kila mwanainchi au familia ipate mahali itaita nyumbani.<br />
Kwa vile kwa mfano, tajiri akija apate mahali mnafanyia kazi, nyinyi ni watu kumi mko pale, mnafanya kazi mnajisaidia na<br />
inasaidi watoto wenu, serikali ina haki ya kuja na kuwafukuza kutoka mahali pale na iwaonyeshi mahali mtaende, sasa iyo<br />
inalete ufukara zaidi. Watu wanazidi kudidimia.<br />
Polisi; wakati polisi wanawashika watu, hasa wanaume wakiwashika wanawake, na kuwapeleka cell, wanawake huwa<br />
wanaumia sana. Mara nyingine wakifika kule, hao wanaume wanawalizimish kufagia, na saa ingine wanaanywa kufagia usiku.<br />
Na saa ingine hao wanawake wanaazimishwa kujipeana mwili zao ili wanunuwe uhuru wao. Kwa hivyo wanawake wawe<br />
wakishikwa na askari wanawake, na wakati wako kwa cell wawe, wanajibika maswala yote kwa askari wanawake.<br />
Interruption: Kuhusu hii maneno ya polisi, je mngetaka warudishwe shule ama, kwa vile wa<strong>kenya</strong> wengi wanalalamika kuwa<br />
polisi wanaumiza watu.<br />
Julius Mwangi: Ninaonelea ya kwamba, kuwe na utaratibu au <strong>commission</strong> ingine. Kama committee, lakini iwe ni serikali,<br />
sijui iwekwe majeshi ndio watakua juu, wapewe uwezo wa kutawala polisi. Ili wewe ukigandamizwa na polisi, unaweza<br />
kuwastaki kwa hawa, sababu sasa ukudhulumiwa na polisi unaweza kuenda kustaki wapi Wamekuwa wabaya sana na<br />
wamezidi kabisa. Hata unyangaywi ile inafanywa siku hizi, ni hao wanafanya. Na hata ukijua hauna mahali ya kuenda<br />
kuwashtaki.<br />
Mimi ni mhuzaji wa makaa na nimetembea mahali nyingi sana katika Kenya, na hii biashara ilikuwa imefungwa lakini kule<br />
kufungwa nikusema inaendelea kwa njia mbaya, hata kama imefungwa. Ningeuliza serikali iwe ikiwaruhusu watu mahali<br />
wanaishi, kama ni zile miti zimeanguka, zile zimeoza na mahali wanakubaliwa kusafisha mashamba wawe legalized kuwa<br />
wakichoma izo miti, na iwe ni huru mahali wanapeleka wasiulizwe.