46Munge Kago: Sasa kijana mwenye nguvu, anashinda pale town, ati anauza mali mali, ati ni biashara, na anatoka na shilingiishirini pekeee yake. Na labda angelima, tungekuwa hatuna njaa, na hata ukiangalia hii mambo ya industries yote inatokana naukulima wa mchanga. Biashara inatokana kwa mchanga. Kwa hivyo sisi tungefikiria mambo ya mchanga tu, tuaache kufikiriamambo mingi, ati tujenge magari, tujenge mandege ya kufanya nini? Tulime. Sasa hiyo tu ndiyo ilikuwa maoni yangu.Com. Charles Maranga: Asante. Asante Mzee wangu. Asante, weka sahihi, thank you very much. Gichaiga Isaac. Yournames first and be very brief to the point.Isaac Githaiga: My names are Isaac Githaiga.Interjection – Com Charles Maranga: Okey, siyo Gichaiga.Isaac Githaiga: You have said ch. It is th. Thank you very much.Nina machache tu kidogo nataka kugusia. Ya kwanza ni system <strong>of</strong> government. Ningependekeza, tuendelee na democracy.Lakini iwe ni democracy, isiwe ni kitu kama democracy. Pili ningetaka kugusia kuhusu wale watu ambao wamekuwa kwamilitary, iwe ni paramilitary ama ni military yenyewe, whatever the case, wasiwe wanastaafu when they are still young. Kwasababu, naonelea kutoka kwao wakiwa bado hawajaendelea kwa miaka, pengine ndiyo kunaleta uharibifu mwingi kwa sababuwanajua kutumia silaha na wanataka kuishi.Ningependekeza pia chama ambacho kinasimamia Workers Union, ambacho umbrella body ni COTU, Rais asiwe anahusikakuchagua Secretary General.Ningependekeza pia, Rais apunguziwe mamlaka. Isiwe yeye ndiye ana-appoint heads <strong>of</strong> parastatals.Niseme pia lingine.The three organs ambazo zinaongoza serikali yetu, which is the Judiciary, Parliament na Executive body, ziwe kila moja ikiwaindependent, bila kuhusika ingine kwa ingine.Kuhusu soko, hii vile imesemeka ati Tumekuwa na soko huru. Soko huru haisaidii common person. Inasaidia wale ambaowanazo. Unaona Tumetoa merchandise kutoka ng’ambo na zina- punguzwa bei, halafu zile tuko nazo hapa, kama ni mahindiama whatever the case, zinakuwa floating, zinakosa soko. Ni hayo tu niko nayo.Com. Charles Maranga: Asante Bwana Githaiga. Asante na weka memorandum yako, na uweke sahihi. Thank you verymuch. Mwingine ninayemuita ni Kiptoo Rep. Is it Kiptoo Rep? Yah, come.
47Kiptoo Rop: Asante sana mwenye kiti wa Tume ya Katiba. Jina langu naitwa Paul Kiptoo Rop. Kwanza kabisa, hii mamboya private schools, ningependa serikali ama Katiba, iondoe mambo ya private schools, kwa sababu kulingana na sasa vilemaisha ya Kenya iko, wananchi wengi hawana kazi na matajiri wetu wanapeleka watoto kwa private schools. Hawa wananchiwa kawaida watoto wao hawawezi kupata masomo ya hali ya juu. Sasa hizi private schools, ambazo ni za girls and boys,zitupiliwe mbali kabisa, halafu turudishiwe tu moja ya serikali pekeee yake.Kwa mambo ya hosipitali, tungependa tu kuwe na hospitali za serekali pekeee yake. Kwa sababu hizi private hospitals, kunamadawa nyingi sana zinaibiwa kwa serikali zinapelekwa kwa private hospitals.Halafu, kwa mambo ya powers za President, Rais asiwe above the law. Kwa sababu Rais wenye wamekuwa sasawakiongoza hawa wawili wamepita, wamekuwa wakitumia mamlaka yao vibaya.Kwa mambo ya waalimu na madaktari, madaktari waongezewe pesa, kwa sababu hawa ndio wanatibu wananchi. Mkiachiliamadaktari, hawawezi kushugulikia wananchi wa kawaida. Sina mengi ni hayo tu.Com. Charles Maranga: Thank you. Asante sana na weka sahihi. Next.Mary Njambi- (deaf): Kwa majina yangu naitwa Mary Jambi. Ningependelea Katiba mpya ikitengenezwa, kuwe serikaliikitukumbuka sana. Kwa sababu kama sisi viziwi, hatutambuliwi, katika serikali, tukiwa na kama MP akiwa akitushirikishakatika mambo yetu tutafurahia.Na kulingana na mambo ya shule, kama sisi viziwi shule zetu zimekuwa bei ghali sana, na wazazi wetu, wengine ni masikini,hawawezi tulipia shule. For example anasema yeye alifika Std. 8 na wazazi wake wakakosa pesa ya karo. Kwa hivyoangependelea serikali, elimu yao ikuwe ya bure. Atafurahia sana. Asante.Com. Charles Maranga: Asante sana. Kuna mwingine? Okey.Rose Muthoni - (deaf): Kwa majina yangu naitwa Rose Muthoni. Ameonelea na yeye Katiba mpya itakayo rekebishwa, iweikihusisha the deaf kwa kazi yoyote ya serikali, ili maisha yetu sisi kama viziwi ikuwe inalingana na hearing people.Kama viziwi wenye wako mashambani, nao wako na shida sana kwa sababu wazazi wao hawajaelewa shida zao, nahawajatambua kama kuna elimu ya viziwi. Ningependelea nayo serikali iangalie mambo yetu.Com. Charles Maranga: Thank you. Muambie asante. Next.
- Page 1 and 2: CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMIS
- Page 3 and 4: 3RECORD OF CONSTITUENCY PUBLIC HEAR
- Page 5 and 6: 5John Kirui: Emero, thank you.Cylus
- Page 7 and 8: 7Bwana Mwangi alisema namna hii, Bw
- Page 9: 9The exercise of registration of vo
- Page 12 and 13: 12Ya mwisho ni uchaguzi wa viongozi
- Page 14 and 15: 14Col. Hastings Muhindi: Asante. Ni
- Page 16 and 17: 16wangelipwa mshahara ambao unatosh
- Page 18 and 19: 18Moja kabisa unasema ati Wakenya w
- Page 20 and 21: 20The other point is that there bei
- Page 22 and 23: 22behalf and you will be remedized.
- Page 24 and 25: 24akishakufa wanalia sana, hata lod
- Page 26 and 27: 26mtu ambaye amemkanyanga mkia ya k
- Page 28 and 29: 28On the Federal government, I wish
- Page 30 and 31: 30Summarize the main points. Watu w
- Page 32 and 33: 32Com. Abida Ali-Aroni: Stephen, ul
- Page 34 and 35: 34Parliament should also have power
- Page 36 and 37: 36Katiba itatoka kutokana na maoni
- Page 38 and 39: 38placing the country above oneself
- Page 40 and 41: 40Senate represents the society, an
- Page 42 and 43: 42Tatu, nitaenda kwa Cabinet. Wakat
- Page 44 and 45: 44Francis Musyoka: Hii elimu iwe ya
- Page 48 and 49: 48Truphena Awuor: Asante sana Commi
- Page 50 and 51: 50jailed for life. Hence, what they
- Page 52 and 53: 52Com. Abida Ali-Aroni Aroni: Bwana
- Page 54 and 55: 54Com. Charles Maranga: Your last p
- Page 56 and 57: 56will be encouraged by every ethni
- Page 58 and 59: 58harambee ya mia mbili, mia moja.
- Page 61: 61Com. Charles Maranga: Hiyo ni ya
- Page 64 and 65: 64Family Law succession. Acts Cap 1
- Page 66 and 67: 66njaa. Kwa sababu ya nini? Mashamb
- Page 68 and 69: 68ya gari ya matatu. Unatakiwa ulip
- Page 70 and 71: 70Geoffrey Njiraini: Asanteni sana.
- Page 72 and 73: 72Josephat Waititu: So as I was say
- Page 74 and 75: 74kitaifa, anaongea maneno ya kitai
- Page 76 and 77: 76walifika hapa, lilibadilika kutok
- Page 78 and 79: 78The other thing is that the const
- Page 80 and 81: 80hawatengenezi. Na hawa ndiyo tu w
- Page 82 and 83: 82andika waalimu elfu hamsini. Hiyo
- Page 84 and 85: 84Com. Charles Maranga: The last po
- Page 86 and 87: 86Muhindi mwenye ako next shop, kam
- Page 88 and 89: 88Ingine ni upande wa drug abuse. U