22.04.2014 Views

1lzXuhv

1lzXuhv

1lzXuhv

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Taarifa ya Mwenyekiti (Yaendelea)<br />

Wakurugenzi Wakuu wasio tekeleza majukumu ya siku<br />

hadi siku.<br />

Misingi ya Halmashauri ya KCB inaweka msisitizo<br />

kwenye majukumu nyeti ya kibiashara na hutoa fursa<br />

kwa Halmashauri ya Wakurugenzi kujifahamisha vyema<br />

na biashara ili kutekeleza majukumu yao kikamilifu. Tuna<br />

imani kuwa biashara inasimamiwa kwa busara na kwa<br />

kuzingatia masharti yote ya kisheria.<br />

Mwaka wa 2013 kulifanyika mabadiliko katika<br />

Halmashauri ya Wakurugenzi. Kulingana na Kanuni za<br />

Huduma za Wakurugenzi, Bw. Joseph Isaac Adongo<br />

alistaafu kutoka kwa Halmashauri. Bw. Tom Ipomai<br />

ambaye mlimchagua katika Mkutano Mkuu wa Mwaka<br />

uliopita alijiunga na Halmashauri ya Wakurugenzi.<br />

Pamoja na hayo, Bi. Catherine Adongo Kola na<br />

Prof. Peter Kiko Kimuyu walichaguliwa tena kwenye<br />

Halmashauri. Aidha, Halmashauri pia ilimchagua<br />

mwenyekiti mpya, Bw. Ngeny Biwott, ambaye alichukua<br />

hatamu kutoka kwa Mhandisi Musa Ndeto. Bw. Collins<br />

Otiwu aliteuliwa kwenye Halmashauri kufuatia kuajiriwa<br />

kwake kuwa Msimamizi Mkuu wa Fedha. Halmashauri<br />

pia ilimteua Bw. Joseph Kania kuwa Katibu mpya wa<br />

Kampuni. Nawakaribisha Wakurugenzi wapya kwenye<br />

Halmashauri na kuwashukuru wale wote wanaoondoka<br />

kwa mchango wao.<br />

Kama mnavyofahamu, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni,<br />

Bw. Joshua Oigara, alichukua hatamu Januari, 2013.<br />

Katikati ya 2013, Halmashauri ilichunguza upya ajira<br />

za wasimamizi wakuu katika Kamati Simamizi (EXCO)<br />

ambazo ziliidhinishwa pia na Benki Kuu ya Kenya. Kamati<br />

Simamizi ya Kampuni (EXCO) sasa inawajumuisha<br />

Mkurugenzi Mkuu, Msimamizi Mkuu wa Fedha, Afisa<br />

Mkuu wa Biashara nchini Kenya, Mkurugenzi wa<br />

Mikopo wa Kampuni, Mkurugenzi wa Wafanyakazi,<br />

Mkurugenzi wa dhidi ya athari za kifedha, Mkururgenzi<br />

Mkuu wa Teknolojia na Katibu wa Kampuni. Hili ni kundi<br />

la watu wachache na lenye ujuzi mkubwa wa kufanya<br />

kazi lililoundwa kuambatana na mikakati ya sera ya<br />

Kampuni. Halmashauri ina imani kamili na kundi hilo<br />

linapoanza kuielekeza KCB kutoka mkondo wa kuwa<br />

benki bora hadi ule wa kuwa benki thabiti zaidi.<br />

Safari endelevu<br />

Mnamo 2013 Halmashauri ya Kampuni ya KCB<br />

iliidhinisha Mfumo Endelevu kwa Benki.<br />

Halmashauri imejitolea kutoa rasilimali<br />

zifaazo kwa utekelezaji wa mipango<br />

ambayo itahakikisha uzingativu wa Benki<br />

kwa Kanuni Endelevu.<br />

Kutoka kushoto; Mkurugenzi wa KCB wa Biashara Rejareja, Annastacia Kimtai, Mwenyekiti<br />

wa Kampuni ya KCB, Bw. Ngeny Biwott, Mke wa Naibu Rais, Bi. Rachel Ruto na Dkt.<br />

Solomon Joloimat, wakati Bi. Ruto alipotembelea ofisi ya Mwenyekiti.<br />

Halmashauri inahusika moja kwa moja<br />

katika utekelezaji sahihi wa Maendeleo<br />

Endelevu ya Kijamii, Mazingira Endelevu,<br />

Uchumi Endelevu na Uthabiti wa<br />

Kifedha. Hii itahakikisha kuwa Kampuni<br />

ya KCB itakuwa taasisi endelevu<br />

miongo inayokuja. Pia tutafanya kazi na<br />

washikadau kuendeleza ajenda yetu kwa<br />

kutumia ushirika uliopo katika juhudi zetu<br />

za kuafikia ulimwengu endelevu. Katika<br />

kuafikia hili, Benki itaendelea kuwekeza<br />

27 16<br />

K C B 2 0 1 3 A n n u a l R e p o r t a n d F i n a n c i a l S t a t e m e n t s

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!