1lzXuhv
1lzXuhv
1lzXuhv
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Taarifa ya Mwenyekiti (Yaendelea)<br />
Wakurugenzi Wakuu wasio tekeleza majukumu ya siku<br />
hadi siku.<br />
Misingi ya Halmashauri ya KCB inaweka msisitizo<br />
kwenye majukumu nyeti ya kibiashara na hutoa fursa<br />
kwa Halmashauri ya Wakurugenzi kujifahamisha vyema<br />
na biashara ili kutekeleza majukumu yao kikamilifu. Tuna<br />
imani kuwa biashara inasimamiwa kwa busara na kwa<br />
kuzingatia masharti yote ya kisheria.<br />
Mwaka wa 2013 kulifanyika mabadiliko katika<br />
Halmashauri ya Wakurugenzi. Kulingana na Kanuni za<br />
Huduma za Wakurugenzi, Bw. Joseph Isaac Adongo<br />
alistaafu kutoka kwa Halmashauri. Bw. Tom Ipomai<br />
ambaye mlimchagua katika Mkutano Mkuu wa Mwaka<br />
uliopita alijiunga na Halmashauri ya Wakurugenzi.<br />
Pamoja na hayo, Bi. Catherine Adongo Kola na<br />
Prof. Peter Kiko Kimuyu walichaguliwa tena kwenye<br />
Halmashauri. Aidha, Halmashauri pia ilimchagua<br />
mwenyekiti mpya, Bw. Ngeny Biwott, ambaye alichukua<br />
hatamu kutoka kwa Mhandisi Musa Ndeto. Bw. Collins<br />
Otiwu aliteuliwa kwenye Halmashauri kufuatia kuajiriwa<br />
kwake kuwa Msimamizi Mkuu wa Fedha. Halmashauri<br />
pia ilimteua Bw. Joseph Kania kuwa Katibu mpya wa<br />
Kampuni. Nawakaribisha Wakurugenzi wapya kwenye<br />
Halmashauri na kuwashukuru wale wote wanaoondoka<br />
kwa mchango wao.<br />
Kama mnavyofahamu, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni,<br />
Bw. Joshua Oigara, alichukua hatamu Januari, 2013.<br />
Katikati ya 2013, Halmashauri ilichunguza upya ajira<br />
za wasimamizi wakuu katika Kamati Simamizi (EXCO)<br />
ambazo ziliidhinishwa pia na Benki Kuu ya Kenya. Kamati<br />
Simamizi ya Kampuni (EXCO) sasa inawajumuisha<br />
Mkurugenzi Mkuu, Msimamizi Mkuu wa Fedha, Afisa<br />
Mkuu wa Biashara nchini Kenya, Mkurugenzi wa<br />
Mikopo wa Kampuni, Mkurugenzi wa Wafanyakazi,<br />
Mkurugenzi wa dhidi ya athari za kifedha, Mkururgenzi<br />
Mkuu wa Teknolojia na Katibu wa Kampuni. Hili ni kundi<br />
la watu wachache na lenye ujuzi mkubwa wa kufanya<br />
kazi lililoundwa kuambatana na mikakati ya sera ya<br />
Kampuni. Halmashauri ina imani kamili na kundi hilo<br />
linapoanza kuielekeza KCB kutoka mkondo wa kuwa<br />
benki bora hadi ule wa kuwa benki thabiti zaidi.<br />
Safari endelevu<br />
Mnamo 2013 Halmashauri ya Kampuni ya KCB<br />
iliidhinisha Mfumo Endelevu kwa Benki.<br />
Halmashauri imejitolea kutoa rasilimali<br />
zifaazo kwa utekelezaji wa mipango<br />
ambayo itahakikisha uzingativu wa Benki<br />
kwa Kanuni Endelevu.<br />
Kutoka kushoto; Mkurugenzi wa KCB wa Biashara Rejareja, Annastacia Kimtai, Mwenyekiti<br />
wa Kampuni ya KCB, Bw. Ngeny Biwott, Mke wa Naibu Rais, Bi. Rachel Ruto na Dkt.<br />
Solomon Joloimat, wakati Bi. Ruto alipotembelea ofisi ya Mwenyekiti.<br />
Halmashauri inahusika moja kwa moja<br />
katika utekelezaji sahihi wa Maendeleo<br />
Endelevu ya Kijamii, Mazingira Endelevu,<br />
Uchumi Endelevu na Uthabiti wa<br />
Kifedha. Hii itahakikisha kuwa Kampuni<br />
ya KCB itakuwa taasisi endelevu<br />
miongo inayokuja. Pia tutafanya kazi na<br />
washikadau kuendeleza ajenda yetu kwa<br />
kutumia ushirika uliopo katika juhudi zetu<br />
za kuafikia ulimwengu endelevu. Katika<br />
kuafikia hili, Benki itaendelea kuwekeza<br />
27 16<br />
K C B 2 0 1 3 A n n u a l R e p o r t a n d F i n a n c i a l S t a t e m e n t s