01.01.2015 Views

CONTENTS - Investing In Africa

CONTENTS - Investing In Africa

CONTENTS - Investing In Africa

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

TAARIFA YA MWENYEKITI kuendelea<br />

KCB JUBA<br />

Outside view of KCB Juba branch.<br />

Viwango vya riba baina ya mabenki katika kipindi hicho<br />

hicho viliongezeka kutoka asili mia 6.3 mwishoni mwa 2006<br />

hadi asili mia 7.0 mwezi Desemba 2007. Viwango vya riba<br />

vilivyodumishwa viliendelea kuwa muhimu katika mipango<br />

ya uwekezaji.<br />

MASOKO YA KIFEDHA<br />

Shilingi ya Kenya ilikuwa na imariko kuu dhidi ya sarafu<br />

muhimu za kimataifa na kuwa na viwango vya chini zaidi vya<br />

ubadilishanaji ikilinganishwa na miaka iliyotangulia. Shilingi<br />

iliimarika dhidi ya Dola ya Marekani, Pauni ya Uingereza na<br />

Euro mwezi Desemba mwaka wa 2007 hadi Shilingi 62.50,<br />

Shilingi 124.80 na Shilingi 89.90 kulinganishwa na Shilingi<br />

69.40, Shilingi 136.30 na Shilingi 91.40 mwezi Desemba<br />

mwaka wa 2006 mtawalio. Kuimarika kwa Shilingi kuliakisi<br />

kuingia kwa fedha za kigeni katika kipindi cha mwaka<br />

huo. Ufanisi huu umedhoofishwa na ghasia za baada ya<br />

uchaguzi na kupelekea kudidimia kwa thamani ya Shilingi.<br />

Biashara katika Soko la Hisa ilionyesha viwango vya chini<br />

kutokana na hali ya sintofahamu miongoni mwa wawekezaji<br />

wakati wa mwaka wa uchaguzi. Kigezo cha kampuni<br />

bora 20 katika soko la Hisa la Nairobi kilipungua kwa asili<br />

mia 4 kutoka alama 5,645.7 mwezi Desemba, 2006 hadi<br />

alama 5,444.8 mwezi Desemba 2007. Hata hivyo mtaji<br />

wa jumla wa soko hilo uliongezeka kutoka Shilingi bilioni<br />

792 mwishoni mwa 2006 hadi Shilingi bilioni 851. Thamani<br />

ya jumla ya hisa zilizouzwa katika soko la Hisa la Nairobi<br />

ilipungua kwa asili mia 7 kutoka Shilingi bilioni 95 mwishoni<br />

mwa mwaka wa 2006 hadi Shilingi bilioni 89 mwaka wa<br />

2007, lakini jumla ya hisa zilizouzwa ziliongezeka kwa kiasi<br />

kikubwa ikilinganishwa na miaka iliyotangulia.<br />

Hisa za KCB ambazo kufuatia gawanyiko zilikuwa zikiuzwa<br />

kwa shilingi 24 ziliimarika na kufikia shilingi 28.50. Mtaji wa<br />

jumla uliongezeka hadi shilingi bilioni 56.9 mwaka wa 2007<br />

kutoka shilingi bilioni 48.1 mwaka wa 2006. Ongezeko hili<br />

lilikuwa linaakisi shinikizo la kuimarika kwa bei ya hisa na<br />

kiasi kikubwa cha hisa zilizotolewa. Kutoka na gawanyo<br />

hilo, hisa zilizotolewa ziliongezeka kutoka hisa milioni 199.6<br />

hadi hisa milioni 1,996.<br />

Kuambatana na imariko la uchumi, sekta ya benki iliendelea<br />

kuonyesha ukuaji bora mwaka wa 2007. Wakati wa kipindi<br />

hicho, mali za sekta hiyo ziliongezeka kutoka kiwango<br />

kikubwa cha shilingi bilioni 760 mwaka wa 2006 hadi<br />

shilingi bilioni 910 mwaka wa 2007. Hii hasa ilitokana na<br />

ongezeko la fedha kwenye akaunti, mtaji wa ziada pamoja<br />

na hifadhi ya faida iliyotoa nafasi zaidi ya uwekezaji katika<br />

hati za dhamana za serikali na ukopeshaji.<br />

Aidha kulikuwa na imariko la jumla la mikopo iliyolipwa<br />

huku visa vya kutolipwa kwa mikopo vikipungua, ongezeko<br />

la thamani ya mali na toshelezo la uwiano wa mtaji pamoja<br />

na kuimarika kwa faida katika sekta kwa jumla.<br />

UPANUZI WA MAENEO NA MASHIRIKA<br />

Ili tuwe benki ya kanda, Halmashauri iliidhinisha kuanzishwa<br />

kwa tawi la benki nchini Uganda na ikaanza shughuli zake<br />

mwishoni mwa mwezi Novemba mjini Kampala. Soko<br />

limepokea vyema biashara hiyo mpya na Halmashauri<br />

imekubaliana na mipango ya Usimamizi ya kuongeza<br />

matawi zaidi nchini humo.<br />

Matawi mengine ya kanda yanaonyesha dalili njema na<br />

kuna mipango ya kuongeza huduma zaidi Kusini mwa<br />

Sudani ambapo tuna mipango ya kufungua matawi manne<br />

zaidi mwaka wa 2008 na Tanzania ambapo kuna mipango<br />

ya kuongeza matawi 20 zaidi katika muda wa miaka miwili<br />

ijayo. KCB-U inatarajia kuwa na matawi sita mwaka wa<br />

2008.<br />

Kwa ujumla, matawi hayo ya benki kwa pamoja yalikuwa<br />

na faida ya shilingi milioni 363 kabla ya kodi licha ya<br />

faida kiasi kutoka KCB-T(Shilingi milioni 0.2) na hasara ya<br />

shilingi milioni 49.2 kutoka KCB-U kutokana na gharama za<br />

kuianzisha. Shirika la S&L liliendelea kuimarika huku faida<br />

yake ikiongezeka maradufu wakati wa kipindi hicho kutoka<br />

shilingi milioni 130 mwaka wa 2006 hadi shilingi milioni<br />

277 mwaka wa 2007. Shirika hili ambalo linaongoza kwa<br />

utoaji wa mikopo ya ujenzi wa nyumba nchini lina mpango<br />

wa kupanua huduma zake katika mataifa ya kanda ndani<br />

ya mwaka wa 2008 na tunaamini kwa kuwa lina ushindani<br />

16 KCB ANNUAL REPORT & FINANCIAL STATEMENTS 2007

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!