CONTENTS - Investing In Africa
CONTENTS - Investing In Africa
CONTENTS - Investing In Africa
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
TAARIFA YA MWENYEKITI kuendelea<br />
KCB JUBA<br />
Outside view of KCB Juba branch.<br />
Viwango vya riba baina ya mabenki katika kipindi hicho<br />
hicho viliongezeka kutoka asili mia 6.3 mwishoni mwa 2006<br />
hadi asili mia 7.0 mwezi Desemba 2007. Viwango vya riba<br />
vilivyodumishwa viliendelea kuwa muhimu katika mipango<br />
ya uwekezaji.<br />
MASOKO YA KIFEDHA<br />
Shilingi ya Kenya ilikuwa na imariko kuu dhidi ya sarafu<br />
muhimu za kimataifa na kuwa na viwango vya chini zaidi vya<br />
ubadilishanaji ikilinganishwa na miaka iliyotangulia. Shilingi<br />
iliimarika dhidi ya Dola ya Marekani, Pauni ya Uingereza na<br />
Euro mwezi Desemba mwaka wa 2007 hadi Shilingi 62.50,<br />
Shilingi 124.80 na Shilingi 89.90 kulinganishwa na Shilingi<br />
69.40, Shilingi 136.30 na Shilingi 91.40 mwezi Desemba<br />
mwaka wa 2006 mtawalio. Kuimarika kwa Shilingi kuliakisi<br />
kuingia kwa fedha za kigeni katika kipindi cha mwaka<br />
huo. Ufanisi huu umedhoofishwa na ghasia za baada ya<br />
uchaguzi na kupelekea kudidimia kwa thamani ya Shilingi.<br />
Biashara katika Soko la Hisa ilionyesha viwango vya chini<br />
kutokana na hali ya sintofahamu miongoni mwa wawekezaji<br />
wakati wa mwaka wa uchaguzi. Kigezo cha kampuni<br />
bora 20 katika soko la Hisa la Nairobi kilipungua kwa asili<br />
mia 4 kutoka alama 5,645.7 mwezi Desemba, 2006 hadi<br />
alama 5,444.8 mwezi Desemba 2007. Hata hivyo mtaji<br />
wa jumla wa soko hilo uliongezeka kutoka Shilingi bilioni<br />
792 mwishoni mwa 2006 hadi Shilingi bilioni 851. Thamani<br />
ya jumla ya hisa zilizouzwa katika soko la Hisa la Nairobi<br />
ilipungua kwa asili mia 7 kutoka Shilingi bilioni 95 mwishoni<br />
mwa mwaka wa 2006 hadi Shilingi bilioni 89 mwaka wa<br />
2007, lakini jumla ya hisa zilizouzwa ziliongezeka kwa kiasi<br />
kikubwa ikilinganishwa na miaka iliyotangulia.<br />
Hisa za KCB ambazo kufuatia gawanyiko zilikuwa zikiuzwa<br />
kwa shilingi 24 ziliimarika na kufikia shilingi 28.50. Mtaji wa<br />
jumla uliongezeka hadi shilingi bilioni 56.9 mwaka wa 2007<br />
kutoka shilingi bilioni 48.1 mwaka wa 2006. Ongezeko hili<br />
lilikuwa linaakisi shinikizo la kuimarika kwa bei ya hisa na<br />
kiasi kikubwa cha hisa zilizotolewa. Kutoka na gawanyo<br />
hilo, hisa zilizotolewa ziliongezeka kutoka hisa milioni 199.6<br />
hadi hisa milioni 1,996.<br />
Kuambatana na imariko la uchumi, sekta ya benki iliendelea<br />
kuonyesha ukuaji bora mwaka wa 2007. Wakati wa kipindi<br />
hicho, mali za sekta hiyo ziliongezeka kutoka kiwango<br />
kikubwa cha shilingi bilioni 760 mwaka wa 2006 hadi<br />
shilingi bilioni 910 mwaka wa 2007. Hii hasa ilitokana na<br />
ongezeko la fedha kwenye akaunti, mtaji wa ziada pamoja<br />
na hifadhi ya faida iliyotoa nafasi zaidi ya uwekezaji katika<br />
hati za dhamana za serikali na ukopeshaji.<br />
Aidha kulikuwa na imariko la jumla la mikopo iliyolipwa<br />
huku visa vya kutolipwa kwa mikopo vikipungua, ongezeko<br />
la thamani ya mali na toshelezo la uwiano wa mtaji pamoja<br />
na kuimarika kwa faida katika sekta kwa jumla.<br />
UPANUZI WA MAENEO NA MASHIRIKA<br />
Ili tuwe benki ya kanda, Halmashauri iliidhinisha kuanzishwa<br />
kwa tawi la benki nchini Uganda na ikaanza shughuli zake<br />
mwishoni mwa mwezi Novemba mjini Kampala. Soko<br />
limepokea vyema biashara hiyo mpya na Halmashauri<br />
imekubaliana na mipango ya Usimamizi ya kuongeza<br />
matawi zaidi nchini humo.<br />
Matawi mengine ya kanda yanaonyesha dalili njema na<br />
kuna mipango ya kuongeza huduma zaidi Kusini mwa<br />
Sudani ambapo tuna mipango ya kufungua matawi manne<br />
zaidi mwaka wa 2008 na Tanzania ambapo kuna mipango<br />
ya kuongeza matawi 20 zaidi katika muda wa miaka miwili<br />
ijayo. KCB-U inatarajia kuwa na matawi sita mwaka wa<br />
2008.<br />
Kwa ujumla, matawi hayo ya benki kwa pamoja yalikuwa<br />
na faida ya shilingi milioni 363 kabla ya kodi licha ya<br />
faida kiasi kutoka KCB-T(Shilingi milioni 0.2) na hasara ya<br />
shilingi milioni 49.2 kutoka KCB-U kutokana na gharama za<br />
kuianzisha. Shirika la S&L liliendelea kuimarika huku faida<br />
yake ikiongezeka maradufu wakati wa kipindi hicho kutoka<br />
shilingi milioni 130 mwaka wa 2006 hadi shilingi milioni<br />
277 mwaka wa 2007. Shirika hili ambalo linaongoza kwa<br />
utoaji wa mikopo ya ujenzi wa nyumba nchini lina mpango<br />
wa kupanua huduma zake katika mataifa ya kanda ndani<br />
ya mwaka wa 2008 na tunaamini kwa kuwa lina ushindani<br />
16 KCB ANNUAL REPORT & FINANCIAL STATEMENTS 2007