CONTENTS - Investing In Africa
CONTENTS - Investing In Africa
CONTENTS - Investing In Africa
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
TAARIFA YA MKURUGENZI MKUU<br />
Faida kabla ya kodi iliongezeka<br />
kutoka Shilingi bilioni 3.2 mwaka<br />
wa 2006 hadi Shilingi bilioni 4.2<br />
hali ambayo iliakisi utendaji bora<br />
katika sekta zote za biashara.<br />
Martin Oduor-Otieno,<br />
Mkurugenzi Mkuu<br />
Mwaka wa 2007 ulikuwa na ufanisisi ambapo maendeleo<br />
ya kasi ya biashara yalipelekea ongezeko la faida la asili mia<br />
33. Faida kabla ya kodi iliongezeka kutoka Shilingi bilioni<br />
3.2 mwaka wa 2006 hadi Shilingi bilioni 4.2 hali ambayo<br />
iliakisi utendaji bora katika sekta zote za biashara.<br />
Kufuatia utendaji bora huu, Halmashauri imependekeza<br />
mgao wa faida wa Shilingi 0.70(senti 70) kwa kila hisa hili<br />
likiwa ni ongezeko la asili mia 17 kulinganishwa na mwaka<br />
wa 2006.<br />
Utendaji huu ulisukumwa na mazingira bora ya kiuchumi<br />
ambayo yaliweka msingi bora wa riba na viwango vya<br />
ubadilishanaji fedha za kigeni.<br />
Jumla ya mapato ya shughuli zetu yaliongezeka kwa asili<br />
mia 22 kutoka Shilingi bilioni 12.1 mwaka wa 2006 hadi<br />
Shilingi bilioni 14.8 kutokana na ukuaji thabiti wa mapato<br />
ya riba. Jumla ya mapato ya riba yaliongezeka kwa kima<br />
cha kupendeza cha asili mia 34 kutoka Shilingi bilioni 6.3<br />
hadi Shilingi bilioni 8.5. Mapato kutokana na ubadilishaji<br />
wa fedha za kigeni na ada yalichangia Shilingi milioni 839<br />
(nyongeza ya asili mia 27 mwaka wa 2006) na Shilingi bilioni<br />
4.5( ongezeko la asili mia 20 mwaka wa 2006) kwenye kima<br />
cha msingi cha Kundi.<br />
na mikakati ya huduma kwa wateja. Kiasi kikubwa cha<br />
fedha katika mkondo huu zimetumika katika kuimarisha<br />
muundo msingi na shughuli inayoendelea ya kutekeleza<br />
shughuli zetu kuu za mtandao wa benki.<br />
Tunatarajia kuendelea kutumia fedha katika upanuzi wa<br />
matawi na mashini za ATM kote katika kanda katika jitihada<br />
za kufanya huduma zetu kupatikana zaidi katika soko.<br />
Kulikuwa na ongezeko kubwa la faida katika mashirika<br />
ambayo kwa pamoja yalichangia faida ya jumla ya Shilingi<br />
milioni 268 kwa Kundi. Huku KCB-T na KCB-S zikipata<br />
kasi ya biashara tunatarija mchango mkubwa zaidi kutoka<br />
kwao katika siku za zinazokuja.<br />
Mali ya Kundi ilikuwa kwa asili mia 30 na kuongezeka<br />
kutoka Shilingi bilioni 92.5 hadi Shilingi bilioni 120.5, na<br />
kuiweka KCB miongoni mwa Benki chache katika kanda<br />
zenye mali ya kiasi hicho. Hii ilitokana na ongezeko kubwa<br />
la mali zetu na madeni.<br />
Jumla ya mikopo iliyotolewa iliongezeka kwa asili mia 42<br />
kutoka Shilingi bilioni 45.3 mwaka wa 2006 hadi Shilingi<br />
bilioni 64.3 mwaka wa 2007 kutokana na ongezeko la juhudi<br />
za masoko na utekelezaji wa mfumo bora wa kutayarisha<br />
mikopo.<br />
Tulishuhudia ongezeko la asili mia 20 la gharama za utendaji<br />
kutoka Shilingi bilioni 7.8 mwaka wa 2006 hadi Shilingi<br />
bilioni 9.4 mwaka wa 2007 kwa sababu ya ongezeko la<br />
shughuli za kibiashara, ikiwa ni pamoja na mauzo, mafunzo<br />
Fedha zilizowekwa na wateja ziliongezeka kwa Shilingi<br />
bilioni 17.2 wakati wa kipindi cha mwaka kutoka Shilingi<br />
bilioni 77.2 hadi Shilingi bilioni 94.4 huku kiasi kikubwa<br />
kikiwa ni kutoka kwa akaunti za hundi(Shilingi bilioni 8.9),<br />
22 KCB ANNUAL REPORT & FINANCIAL STATEMENTS 2007