CONTENTS - Investing In Africa
CONTENTS - Investing In Africa
CONTENTS - Investing In Africa
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
RIPOTI YA WAKAGUZI - WAHASIBU<br />
Taarifa zilizoambatanishwa za Benki ya<br />
Kenya Commercial na mashirika yake kama<br />
zilivyoonyeshwa kwenye ukurasa wa 35 hadi 76,<br />
ambazo zinahusisha hesabu ya Kundi na Benki kufikia<br />
tarehe 31 Disemba 2007 na taarifa ya mapato ya Kundi<br />
na Benki, taarifa ya mabadiliko katika hisa za Kundi na<br />
Benki, taarifa ya matumizi ya fedha ya Kundi kwa mwaka<br />
uliomalizika katika kipindi hicho na muktasari wa sera<br />
muhimu za uhasibu na maelezo mengine.<br />
WAJIBU WA WAKURUGENZI KWA TAARIFA ZA<br />
UHASIBU<br />
Wakurugenzi wanawajibikia utayarishaji na uwasilishaji<br />
wa taarifa za uhasibu wa haki kuambatana na kanuni na<br />
viwango vya kimataifa vya uhasibu na mahitaji ya sheria<br />
za kampuni za Kenya. Wajibu huu ni pamoja na upangaji,<br />
utekelezaji na kudumisha udhibiti ambao ni muhimu kwa<br />
utayarishaji na uwasilishaji wa haki wa taarifa za uhasibu<br />
ambazo ziko huru kutokana na upungufu, ama kwa sababu<br />
ya ulaghai au makosa,kuchagua na kutumia sera zinazofaa<br />
za uhasibu na kufanya makadirio ya uhasibu ambayo<br />
yanakubalika kwa wakati huo.<br />
za wahasibu ambazo zinafaa kwa hali hiyo, lakini sio kwa<br />
minajili ya kuwasilisha maoni kuhusu uwezo wa Kundi wa<br />
kudhibiti shughuli zake.<br />
Uhasibu pia unahusisha kutathimini sera sawa za uhasibu<br />
zilizotumika na kukubalika kwa makadirio ya uhasibu<br />
uliofanywa na Wakurugenzi, pamoja na kutathimini<br />
uwasilishaji wa jumla wa taarifa za uhasibu.<br />
Tunaamini kwamba ushahidi wa uhasibu tuliopata unatosha<br />
na unafaa kutoa msingi wa maoni yetu ya uhasibu.<br />
MAONI<br />
Kwa maoni yetu taarifa za uhasibu zilizoambatanishwa<br />
zinaeleza hali halisi ya kifedha katika Kundi hili na Benki<br />
kufikia tarehe 31 mwezi Disemba 2007 na ile ya faida kwa<br />
Kundi hili na matumizi na mapato ya fedha kwa kundi hili<br />
kwa mwaka uliomalizika kuambatana na mahitaji ya sheria<br />
za makampuni nchini Kenya na viwango vya kimataifa vya<br />
kutoa ripoti za uhasibu.<br />
Ripoti kuhusu mahitaji mengine ya kisheria<br />
WAJIBU WA WAHASIBU<br />
Wajibu wetu ni kuelezea maoni huru kuhusu taarifa hizi za<br />
uhasibu kwa msingi wa hesabu zetu. Tulifanya uhasibu<br />
wetu kuambatana na viwango vya kimataifa vya uhasibu.<br />
Viwango hivyo vinatuhitaji kuafiki maadili na kupanga na<br />
kutekeleza hesabu ili kupata hakikisho linalokubalika iwapo<br />
taarifa za uhasibu zimeelezwa kikamilifu.<br />
Uhasibu unahusisha utekelezaji wa kanuni ili kupata<br />
ushahidi wa hesabu kuhusu kiwango cha fedha na<br />
maelezo katika taarifa za uhasibu. Kanuni zilizochaguliwa<br />
zinategemea uamuzi wa wahasibu, ikiwa ni pamoja na<br />
ukadiriaji wa kasoro za taarifa za uhasibu zisizo kamilifu<br />
ama kwa sababu ya udanganyifu au makosa. Katika<br />
kufanya maamuzi hayo, mhasibu anatilia maanani udhibiti<br />
wa kampuni ambao ni muhimu katika utayarishaji na<br />
uwasilishaji wa haki wa taarifa za kifedha ili kubuni kanuni<br />
Kama inavyohitajika na sheria za makampuni nchini Kenya,<br />
tunaripoti kwenu, kuambatana na uhasibu wetu kwamba:<br />
i) Tumepata taarifa zote na maelezo ambazo kadri<br />
tunavyoelewa na kuamini zilikuwa muhimu kwa minajili<br />
ya kufanya uhasibu wetu;<br />
ii) Kwa maoni yetu, vitabu sahihi vya hasibu vimewekwa<br />
na Kundi na Benki, kwa jinsi tulivyoona kutokana na<br />
uchunguzi wa vitabu hivyo;<br />
iii) Hesabu za Kundi na Benki zinawiana na vitabu vya<br />
hesabu.<br />
Nairobi<br />
28 Februari 2008<br />
34 KCB ANNUAL REPORT & FINANCIAL STATEMENTS 2007