01.01.2015 Views

CONTENTS - Investing In Africa

CONTENTS - Investing In Africa

CONTENTS - Investing In Africa

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

TAARIFA YA MKURUGENZI MKUU kuendelea<br />

DONATION<br />

Maria Immaculate Children’s Centre<br />

celebrate upon recieving their donation<br />

from KCB.<br />

kutumia mfumo huo mpya kufika robo ya tatu ya mwaka<br />

wa 2008.<br />

Nembo yetu inaendelea kuwa thabiti katika soko ambapo<br />

uchunguzi wa hivi majuzi uliofanywa na kampuni ya<br />

Steadman iliorodhesha KCB ya nne miongoni mwa nembo<br />

maarufu zaidi kwenye soko kwa alama 75 (Safaricom-85,<br />

Kenya Airways-78, Coca Cola-77). Tutaendelea kuimarisha<br />

utambuzi wa nembo yetu kupitia kwa udhamini wetu mkuu<br />

kama vile KCB Kenyan National Rally Championships,<br />

KCB Safari Rally, KCB Pro-AM Golf Tour na KCB/Athletics<br />

Kenya National Cross Country Championships, miongoni<br />

mwa shughuli nyingine za kibiashara.<br />

Pia tuliwekeza kwa kiasi kikubwa katika shughuli za<br />

maendeleo ya kijamii za kuhifadhi mazingira, kupitia<br />

mikakati yetu ya upanzi wa miti, maendeleo ya uwaminishi<br />

na mikakati ya shughuli za maslahi ya jamii.<br />

Wafanyakazi wetu walihusika katika upanzi wa miti kama<br />

sehemu ya siku ya jamii ya KCB na katika kusaidia shule<br />

zenye mahitaji wakati wa wiki ya jamii ya KCB.<br />

Ili kuimarisha uwezo wa wafanyakazi wetu wa kutoa<br />

huduma bora zaidi, tuliendelea kuwapa mafunzo ya hali<br />

ya juu katika huduma kwa wateja na nyanja nyingine za<br />

usaidizi wa kibiashara. Uchunguzi wa kuangalia kuridhika<br />

kwa wateja uliotolewa hivi majuzi unaonyesha imariko la<br />

jumla katika kuridhika kwa wafanyakazi katika nyanja zote<br />

zilizoangaziwa na kuimarika kwa kiasi kikubwa kwa ubora<br />

wa uongozi katika bashara.<br />

Kulikuwa na mabadiliko kadhaa katika wasimamizi wakuu<br />

wa biashara baada ya kuondoka kwa Mkurugenzi Mkuu<br />

wa zamani, Terry Davidson na kuteuliwa kwangu kuchukua<br />

mahali pake. Nimefurahishwa na usaidizi ninaopokea<br />

kutoka kwa Halmashauri na Wasimamizi wakuu na nina<br />

imani kwamba nina kundi thabiti la kuelekeza Benki hii<br />

katika ufanisi wa baadaye. Katika kufanya marekebisho,<br />

Halmashauri ilibuni nyadhifa za naibu wa mkurugenzi mkuu,<br />

Biashara za kundi na Uthibiti wa biashara na kumteua<br />

Peter Munyiri na Samuel Kimani kusimamia vitengo hivyo.<br />

Wakurugenzi wawili wa idara(Philip Ilako-Huduma za benki<br />

kwa mashirika na Kalyan Mukherjee-Hazina) pia walitoka<br />

kwenye kampuni baada ya kumalizika kwa vipindi vyao vya<br />

kuhudumu na nafasi zao kutwaliwa na John Mark Wandolo<br />

na Timothy Kabiru, mtawalio.<br />

Ningependa kuwashukuru washirika wote kwa usaidizi<br />

wao ambao umepelekea ufanisi huu mkubwa na hasa<br />

wafanyakazi wa KCB kwa juhudi zao na kujitolea katika<br />

ufanisi huu. Aidha nina wingi wa shukrani kwa wateja na<br />

wenyehisa kwa imani yao kwetu.<br />

Shukrani zangu za dhati ziwaendee Wakurugenzi wa<br />

Halmashauri kwa kutupa majukumu ya kusimamia shirika hili<br />

na kwa kuendelea kutuunga mkono na kutupa mwelekeo.<br />

Tuna imani kwamba tunaweza kudumisha msukumo huu<br />

katika siku zijazo na kwa pamoja kuifanya KCB kuwa benki<br />

bora zaidi katika kanda na kwingineko.<br />

Asanteni.<br />

24 KCB ANNUAL REPORT & FINANCIAL STATEMENTS 2007

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!