07.12.2012 Views

Sustainability Performance: At a glance (31 March 2012) - Safaricom

Sustainability Performance: At a glance (31 March 2012) - Safaricom

Sustainability Performance: At a glance (31 March 2012) - Safaricom

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Executive summary<br />

Ni mwanzo wa safari ya kusisimua<br />

Nafurahia mno fursa ya kuwasilisha kwenu taarifa hii ya kwanza ya<br />

kudumisha usitawi inayoashiria mfululizo wa mafanikio. Ni tukio muhimu<br />

na la kusisimua kwetu sisi kama Shirika la hapa Kenya, kwa vile ni<br />

dhihirisho la kujitolea kwetu kuzidi kupania faida na kuwajibika kusimamia<br />

vyema mchango wetu katika uchumi, jamii, mazingira na kwenye jumuiya<br />

tunakoendeshea shughuli zetu na tunakoendelea kuungwa mkono.<br />

Kwa vile hii ni taarifa yetu zinduzi, ndiposa ikawa na taswira ya safari<br />

ya kusisimua ambayo sisi kama kampuni na pia kama watu binafsi<br />

tumeianza. Kudumisha usitawi na kuripotiwa kwake kunajumuisha mengi<br />

zaidi ya utaratibu, sera na desturi za kibiashara, ni falsafa na mpangilio wa<br />

maadili yanayoongoza na kufafanua maamuzi kwote katika kampuni, na<br />

inaonyesha hali mambo itakavyokuwa katika mstakabala wetu.<br />

Ujumbe Wa<br />

Mwenyekiti<br />

Bw. Nicholas Nganga<br />

Ubunifu bado unasalia<br />

kuwa kichocheo<br />

muhimu cha ukuaji na<br />

tunaendelea kuangazia<br />

utoaji wa bidhaa na<br />

huduma zinazoongezea<br />

thamani katika maisha<br />

ya wakenya<br />

Tunawasilisha kwenu taarifa hii tukiwa na<br />

msimamo huo, taarifa yenye maelezo yaliyo wazi<br />

na yanayojumlisha hali halisi ya mafanikio yetu na<br />

malengo yetu katika siku zijazo. Hii ni moja tu kati<br />

ya ripoti nyingi zitakazokujieni, na inawakilisha<br />

kigezo kinachoonyesha mahala tulipo sasa na<br />

mwanzo wa gumzo linaloendelea juu ya safari ya<br />

kusisimua tunayodhamiria kuanza.<br />

Mambo mapya yanayojiri na<br />

Mashaka yake<br />

Hali yetu ya siku zijazo inategemea zaidi<br />

baadhi ya matukio yanayojiri humu nchini<br />

na katika eneo hili. La muhimu kutajwa<br />

hapa ni mwelekeo wa athari ya mabadiliko<br />

ya uchumi wa ulimwengu, teknolojia yenye<br />

kasi inayobadilika kila kunapokucha na huku<br />

mipaka ikiendelea kunywea. Miongoni mwa<br />

baadhi ya mashaka yanayotukabili kwa<br />

sasa ni, kupanda mara kwa mara kwa bei ya<br />

mafuta na kubadilikabadilika kwa kima cha<br />

ubadilishanaji pesa za kigeni hali ambayo<br />

inaathiri mno mazingira ya biashara yetu, lakini<br />

tumeendelea kuwasilisha matokeo mazuri na<br />

faida tunayopata tumeitumia kuwekeza zaidi<br />

katika muundo msingi wetu, kukiwa na zaidi ya<br />

KShs Bilioni 25 za faida itokanayo na mauzo ya<br />

rasilimali zikiwekezwa katika kipindi cha mwaka<br />

wa kifedha wa <strong>2012</strong>/13<br />

Ni jambo lililo wazi kuwa utekelezaji wa<br />

sheria pia unaathiri udumishaji wa usitawi<br />

wetu na tuko mstari wa mbele kuanzisha<br />

mashauriano na serikali pamoja na mamlaka<br />

mbali mbali za kusimamia utekelezaji kanuni,<br />

huku tukilinda na kusaidia biashara hii kwa<br />

ujumla kupitia kuimarisha maelewano na<br />

mipango yenye manufaa.<br />

Ubunifu unaendelea kuwa<br />

kichocheo muhimu<br />

Ubunifu bado unasalia kuwa kichocheo<br />

muhimu cha ukuaji na tunaendelea kuangazia<br />

utoaji wa bidhaa na huduma zinazoongezea<br />

thamani katika maisha ya wakenya. Mfano<br />

mzuri wa ubunifu wetu ni M-PESA, huduma<br />

yetu ya uhawilishaji pesa kupitia simu ya<br />

mkononi. Kukiwa na wateja zaidi ya milioni<br />

15 na mawakala zaidi ya 39, 000, M-PESA<br />

inaendelea kupata ukuaji imara na kuchangia<br />

pakubwa kuboresha hali ya wakenya na jinsi<br />

wanavyoendesha shughuli zao za kila siku.<br />

Kutekeleza uwajibikaji wa<br />

maswala ya jamii<br />

Vile vile tunajivunia mchango ambao taasisi<br />

ya <strong>Safaricom</strong> Foundation inaendelea<br />

kutoa katika kuboresha maisha ya<br />

wakenya. <strong>Safaricom</strong> Foundation, ambayo<br />

ilisajiliwa mwaka wa 2003, ni taasisi huru<br />

ya kuchangisha pesa za kusaidia wale<br />

wasiojiweza katika jamii. Ni hazina ya<br />

amana inayotusaidi kutekeleza ahadi yetu ya<br />

kuwekeza katika uwajibikaji kwenye Jumuiya<br />

na inaangazia masuala mbali mbali ya kijamii<br />

kama vile afya, elimu, uwezo wa kiuchumi na<br />

ulindaji wa mazingira. Mpango unaostahili sifa<br />

hapa, ni ile kampeni ya Kenyans for Kenya<br />

ambapo <strong>Safaricom</strong> Foundation na idara zote<br />

za <strong>Safaricom</strong> kwa ujumla walihusika sana<br />

katika kuhamisisha wakenya kuchangia pesa<br />

za kusaidia wahanga wa baa la njaa.<br />

Mtazamo wa siku zijazo<br />

Mambo tunayoyapa umuhimu zaidi mwakani<br />

yanategemea ari yetu wa kuboresha huduma,<br />

bidhaa bora zinazotutofautisha na washindani<br />

wetu, kuongeza thamani kwenye hudunma na<br />

utoaji huduma za kipekee kwa wateja. Tutafikia<br />

haya huku tukizingatia zaidi athari yetu kwenye<br />

mazingira yetu, kwenye biashara hii na uchumi<br />

wa Kenya kwa ujumla, haya yote yakienda<br />

sambamba na ahadi yetu ya kuwa shirika<br />

linalochukuana na matakwa ya raia.<br />

16 <strong>Safaricom</strong> <strong>Sustainability</strong> Report <strong>2012</strong> <strong>Safaricom</strong> <strong>Sustainability</strong> Report <strong>2012</strong> 17<br />

”<br />

“<br />

Executive summary

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!