Sustainability Performance: At a glance (31 March 2012) - Safaricom
Sustainability Performance: At a glance (31 March 2012) - Safaricom
Sustainability Performance: At a glance (31 March 2012) - Safaricom
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Executive summary<br />
Ni mwanzo wa safari ya kusisimua<br />
Nafurahia mno fursa ya kuwasilisha kwenu taarifa hii ya kwanza ya<br />
kudumisha usitawi inayoashiria mfululizo wa mafanikio. Ni tukio muhimu<br />
na la kusisimua kwetu sisi kama Shirika la hapa Kenya, kwa vile ni<br />
dhihirisho la kujitolea kwetu kuzidi kupania faida na kuwajibika kusimamia<br />
vyema mchango wetu katika uchumi, jamii, mazingira na kwenye jumuiya<br />
tunakoendeshea shughuli zetu na tunakoendelea kuungwa mkono.<br />
Kwa vile hii ni taarifa yetu zinduzi, ndiposa ikawa na taswira ya safari<br />
ya kusisimua ambayo sisi kama kampuni na pia kama watu binafsi<br />
tumeianza. Kudumisha usitawi na kuripotiwa kwake kunajumuisha mengi<br />
zaidi ya utaratibu, sera na desturi za kibiashara, ni falsafa na mpangilio wa<br />
maadili yanayoongoza na kufafanua maamuzi kwote katika kampuni, na<br />
inaonyesha hali mambo itakavyokuwa katika mstakabala wetu.<br />
Ujumbe Wa<br />
Mwenyekiti<br />
Bw. Nicholas Nganga<br />
Ubunifu bado unasalia<br />
kuwa kichocheo<br />
muhimu cha ukuaji na<br />
tunaendelea kuangazia<br />
utoaji wa bidhaa na<br />
huduma zinazoongezea<br />
thamani katika maisha<br />
ya wakenya<br />
Tunawasilisha kwenu taarifa hii tukiwa na<br />
msimamo huo, taarifa yenye maelezo yaliyo wazi<br />
na yanayojumlisha hali halisi ya mafanikio yetu na<br />
malengo yetu katika siku zijazo. Hii ni moja tu kati<br />
ya ripoti nyingi zitakazokujieni, na inawakilisha<br />
kigezo kinachoonyesha mahala tulipo sasa na<br />
mwanzo wa gumzo linaloendelea juu ya safari ya<br />
kusisimua tunayodhamiria kuanza.<br />
Mambo mapya yanayojiri na<br />
Mashaka yake<br />
Hali yetu ya siku zijazo inategemea zaidi<br />
baadhi ya matukio yanayojiri humu nchini<br />
na katika eneo hili. La muhimu kutajwa<br />
hapa ni mwelekeo wa athari ya mabadiliko<br />
ya uchumi wa ulimwengu, teknolojia yenye<br />
kasi inayobadilika kila kunapokucha na huku<br />
mipaka ikiendelea kunywea. Miongoni mwa<br />
baadhi ya mashaka yanayotukabili kwa<br />
sasa ni, kupanda mara kwa mara kwa bei ya<br />
mafuta na kubadilikabadilika kwa kima cha<br />
ubadilishanaji pesa za kigeni hali ambayo<br />
inaathiri mno mazingira ya biashara yetu, lakini<br />
tumeendelea kuwasilisha matokeo mazuri na<br />
faida tunayopata tumeitumia kuwekeza zaidi<br />
katika muundo msingi wetu, kukiwa na zaidi ya<br />
KShs Bilioni 25 za faida itokanayo na mauzo ya<br />
rasilimali zikiwekezwa katika kipindi cha mwaka<br />
wa kifedha wa <strong>2012</strong>/13<br />
Ni jambo lililo wazi kuwa utekelezaji wa<br />
sheria pia unaathiri udumishaji wa usitawi<br />
wetu na tuko mstari wa mbele kuanzisha<br />
mashauriano na serikali pamoja na mamlaka<br />
mbali mbali za kusimamia utekelezaji kanuni,<br />
huku tukilinda na kusaidia biashara hii kwa<br />
ujumla kupitia kuimarisha maelewano na<br />
mipango yenye manufaa.<br />
Ubunifu unaendelea kuwa<br />
kichocheo muhimu<br />
Ubunifu bado unasalia kuwa kichocheo<br />
muhimu cha ukuaji na tunaendelea kuangazia<br />
utoaji wa bidhaa na huduma zinazoongezea<br />
thamani katika maisha ya wakenya. Mfano<br />
mzuri wa ubunifu wetu ni M-PESA, huduma<br />
yetu ya uhawilishaji pesa kupitia simu ya<br />
mkononi. Kukiwa na wateja zaidi ya milioni<br />
15 na mawakala zaidi ya 39, 000, M-PESA<br />
inaendelea kupata ukuaji imara na kuchangia<br />
pakubwa kuboresha hali ya wakenya na jinsi<br />
wanavyoendesha shughuli zao za kila siku.<br />
Kutekeleza uwajibikaji wa<br />
maswala ya jamii<br />
Vile vile tunajivunia mchango ambao taasisi<br />
ya <strong>Safaricom</strong> Foundation inaendelea<br />
kutoa katika kuboresha maisha ya<br />
wakenya. <strong>Safaricom</strong> Foundation, ambayo<br />
ilisajiliwa mwaka wa 2003, ni taasisi huru<br />
ya kuchangisha pesa za kusaidia wale<br />
wasiojiweza katika jamii. Ni hazina ya<br />
amana inayotusaidi kutekeleza ahadi yetu ya<br />
kuwekeza katika uwajibikaji kwenye Jumuiya<br />
na inaangazia masuala mbali mbali ya kijamii<br />
kama vile afya, elimu, uwezo wa kiuchumi na<br />
ulindaji wa mazingira. Mpango unaostahili sifa<br />
hapa, ni ile kampeni ya Kenyans for Kenya<br />
ambapo <strong>Safaricom</strong> Foundation na idara zote<br />
za <strong>Safaricom</strong> kwa ujumla walihusika sana<br />
katika kuhamisisha wakenya kuchangia pesa<br />
za kusaidia wahanga wa baa la njaa.<br />
Mtazamo wa siku zijazo<br />
Mambo tunayoyapa umuhimu zaidi mwakani<br />
yanategemea ari yetu wa kuboresha huduma,<br />
bidhaa bora zinazotutofautisha na washindani<br />
wetu, kuongeza thamani kwenye hudunma na<br />
utoaji huduma za kipekee kwa wateja. Tutafikia<br />
haya huku tukizingatia zaidi athari yetu kwenye<br />
mazingira yetu, kwenye biashara hii na uchumi<br />
wa Kenya kwa ujumla, haya yote yakienda<br />
sambamba na ahadi yetu ya kuwa shirika<br />
linalochukuana na matakwa ya raia.<br />
16 <strong>Safaricom</strong> <strong>Sustainability</strong> Report <strong>2012</strong> <strong>Safaricom</strong> <strong>Sustainability</strong> Report <strong>2012</strong> 17<br />
”<br />
“<br />
Executive summary