08.06.2013 Views

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

wote waliosadiki katika siku ile, (kwa sababu ushuhuda wetu ulisadikiwa<br />

kwenu). (2Wathes. 1:6-10. Maneno mepesi kukazia)<br />

Paulo alisema kwamba wakati ambao Yesu angerudi kuwapa nafuu Wathesalonike<br />

waliokuwa wanateswa (ona 1Wathes. 1:4, 5), angetokea “pamoja na malaika wake katika<br />

mwali wa moto” ili kuwaadhibu wale waliokuwa wanawatesa wao, kutoa hukumu ya<br />

haki, inayostahili. Hii haifanani na kile kinachosemwa na wengi, kwamba Unyakuo<br />

utatokea kabla ya dhiki, na kanisa kunyakuliwa na Kristo kabla ya kile kipindi cha dhiki<br />

cha miaka saba kuanza. Hii pia huitwa kuja kwa siri kwa Yesu ili kunyakua kanisa Lake.<br />

Hapana kabisa! Maelezo haya yanafanana na kile ambacho Yesu alieleza katika Mathayo<br />

24:30, 31 – kurudi Kwake karibu au mwishoni mwa kipindi cha dhiki kuu –<br />

anapowanyakua waaminio na kumimina hasira <strong>Ya</strong>ke juu ya wasoiamini.<br />

Siku <strong>Ya</strong> Bwana<br />

Baadaye, katika barua hiyo hiyo, Paulo aliandika hivi:<br />

Basi ndugu, tunakusihini, kwa habari ya kuja kwake Bwana wetu Yesu<br />

Kristo, na kukusanyika kwetu mbele zake, kwamba msifadhaishwe upesi<br />

hata kuiacha nia yenu, wala msisitushwe, kwa roho, wala kwa neno, wala<br />

kwa waraka unaodhaniwa kuwa ni wetu, kana kwamba siku ya Bwana<br />

imekwisha kuwapo (2Wathes. 2:1, 2).<br />

Kwanza: Ona kwamba mada ya Paulo ni kurudi kwa Kristo na Unyakuo. Aliandika<br />

kuhusu “kukusanyika kwetu mbele zake,” akitumia maneno yale yale ambayo Yesu<br />

alitumia katika Mathayo 24:31, alipozungumza juu ya malaika ambao “wangekusanya”<br />

wateule Wake “kutoka mwisho huu wa mbingu mpaka mwisho ule.”<br />

Pili: Ona kwamba Paulo anayaita matukio hayo kuwa ni “siku ya Bwana,” sawa na<br />

alivyofanya katika 1Wathesalonike 4:13 hadi 5:2. Hilo liko wazi kabisa.<br />

Kisha anaendelea hivi:<br />

Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yoyote; maana haiji, usipokuja<br />

kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa<br />

uharibifu; yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho<br />

Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la<br />

Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu (2Wathes.<br />

2:3, 4. Maneno mepesi kukazia).<br />

Wakristo Wathesalonike walikuwa wanadanganywa kwa namna fulani kwamba siku<br />

ya bwana – ambayo kulingana na Paulo lazima ianze kwa Unyakuo na kurudi kwa Kristo<br />

– ilikuwa imekwisha fika. Akatamka wazi wazi kwamba haiji mpaka baada ya ule<br />

ukengeufu (labda ndiyo kule kurudi nyuma ambako Yesu alizungumzia katika Mathayo<br />

24:10) na baada ya mpingakristo kujitangaza kwamba ni Mungu kutoka hekalu la<br />

Yerusalemu. Basi, Paulo anawaambia waamini Wathesalonike wazi wazi kwamba

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!