08.06.2013 Views

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

kusakwa na kuuawa. Ndiyo sababu Yesu aliwaambia waamini wa Uyahudi wakimbilie<br />

milimani bila kukawia, wakiomba kwamba kutoroka kwao kusizuiwe na sababu yoyote<br />

ile.<br />

Wazo langu ni kwamba ingekuwa vizuri kwa waamini wote duniani kukimbilia<br />

maeneo yaliyofichika wakati huo, maana tukio hilo litatangazwa duniani kote kwa njia ya<br />

televisheni. Maandiko yanatuambia kwamba dunia nzima itadanganywa na mpingakristo<br />

na kudhani yeye ndiye Kristo wao, nao watampa mamlaka na heshima zote.<br />

Atakapojitangaza kwamba ni Mungu, watamwamini na kumwabudu. Atakaponena<br />

makufuru dhidi ya Mungu wa kweli – Mungu wa Wakristo – atashawishi dunia yote<br />

iliyodanganyika ili kuwachukia wale wanaokataa kumwabudu (ona Ufunuo 13:1-8).<br />

Yesu aliahidi ukombozi kwa ajili ya watu Wake mwenyewe kwa “kukatisha” hizo<br />

siku za dhiki, vinginevyo, “asingeokoka mtu yeyote” (24:22). Huko “kukatizwa” siku<br />

hizo <strong>Na</strong>ye “kwa ajili ya wateule” bila shaka ni kitu kinachohusu Yeye kuwakomboa<br />

wakati atakapoonekana na kuwakusanya mawinguni. Yesu hata hivyo hatuambii hapa<br />

kwamba ukombozi huo utatokea muda gani baada ya mpingakristo kujitangazia uungu.<br />

Vyovyote vile – tunarudia kusema hapa tena kwamba Yesu aliwaacha wasikilizaji<br />

Wake siku hiyo wakiwa wanajua kwamba wangeishi na kumwona mpingakristo<br />

akitangaza uungu wake, na kupigana vita na Wakristo. Hili linapingana kabisa na wazo la<br />

wale wanaosemakwamba waamini watanyakuliwa kabla ya tukio hilo. Kama<br />

ungemwuliza Petro, <strong>Ya</strong>kobo au hata Yohana kwamba Yesu angerudi kuwaokoa kabla ya<br />

tamko la mpingakristo kwamba ni Mungu, wangekujibu, “Si hivyo”.<br />

Vita Dhidi <strong>Ya</strong> Watakatifu<br />

Katika sehemu zingine, Maandiko yanatabiri juu ya mateso ya mpingakristo kwa<br />

waamini. Kwa mfano: Yohana alifunuliwa, naye akaandika hivi katika kitabu cha<br />

Ufunuo:<br />

<strong>Na</strong>ye [mpingakristo] akapewa kinywa cha kunena maneno makuu, ya<br />

makufuru. Akapewa uwezo wa kufanya kazi yake miezi arobaini na miwili.<br />

Akafunua kinywa chake amtukane Mungu, na kulitukana jina lake, na<br />

maskani yake, nao wakaao mbinguni. Tena akapewa kufanya vita na<br />

watakatifu na kuwashinda, akapewa uwezo juu ya kila kabila na jamaa na<br />

lugha na taifa (Ufunuo 13:5-7. Maneno mepesi kukazia).<br />

Ona hapo kwamba mpingakristo atapewa “uwezo wa kufanya kazi yake” kwa miezi<br />

arobaini na mbili, au, miaka mitatu na nusu kamili. Huu ndiyo wakati unaoitwa nusu ya<br />

wakati wa kipindi cha Dhiki ya miaka saba. Ni sawa kabisa kufikiri kwamba ni ile miezi<br />

arobaini na mbili ya mwisho ya Dhiki, ndipo mpingakristo atakapopewa “uwezo wa<br />

kufanya kazi yake,” kwa sababu mamlaka yake yataondolewa kabisa wakati Kristo<br />

atakaporudi kufanya vita naye na majeshi yake wakati wa kumalizika kwa Dhiki.<br />

Ni dhahiri kwamba “uwezo wak ufanya kzi yake” kwa miezi arobaini na mbili maan<br />

ayake ni mamlaka maalum, maana mpingakristo atapewa mamlaka kiasi fulani na Mungu<br />

katika wakati wake wa kumiliki. Haya “mamlaka maalum ya kufanya kazi” yanaweza<br />

kuwa ni muda atakaopewa wa kuwashinda watakatifu, maana, tunasoma hivi katika<br />

kitabu cha Danieli:

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!