08.06.2013 Views

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Hakuna shaka yoyote kwamba Unyakuo wa kanisa utafanyika wakati fulani katika hiyo<br />

miaka saba, au karibu na hiyo miaka saba.<br />

Je, Unyakuo Ni Lini Hasa?<br />

Swali ambalo mara nyingi linawagawa Wakristo ni wakati hasa wa Unyakuo. Kuna<br />

wanaosema kwamba Unyakuo utatokea kabla ya ile miaka saba ya dhiki. Kwa maana<br />

hiyo, unaweza kutokea wakati wowote. Wengine wanasema utatokea katikati ya ile<br />

miaka saba ya dhiki. <strong>Na</strong> wengine tena wanasema utatokea punde tu baada ya dhiki ya<br />

miaka saba kufika katikati. <strong>Na</strong> kuna wengine nao wanaosema kwamba Unyakuo utatokea<br />

wakati wa Yesu kurudi na ghadhabu nyingi, mwishoni mwa kipindi cha Dhiki.<br />

Hilo si swala la kugawanyikia, na makundi yote manne yanapaswa kukumbuka<br />

kwamba yote yanakubali kwamba Unyakuo utatokea wakati fulani katika kipindi hicho<br />

cha baadaye cha dhiki ya miaka saba, au karibu nacho. Hilo ni dirisha dogo sana katika<br />

upana wa miaka maelfu ya historia. Hivyo, badala ya kugawanyika kutokana na<br />

kutokubaliana kwetu, ni afadhali tufurahie makubaliano yetu! Tena, si kitu tunaamini nini<br />

maana haitabadilisha kitakachotokea.<br />

Baada ya kusema hayo, sina budi kusema kwamba, kwa miaka ishirini na mitano ya<br />

kwanza katika maisha yangu ya Kikristo, niliamini kwamba Unyakuo utatokea kabla ya<br />

Dhiki ile ya miaka saba. Niliamini hivyo kwa sababu ndivyo nilivyofundishwa, na pia<br />

kwa sababu sikutaka kupitia mambo ninayosoma habari zake katika Kitabu cha Ufunuo!<br />

Ila, nilipoendelea kujifunza Maandiko, nilianza kupata mtazamo tofauti. Hebu kwa<br />

pamoja tutazame Biblia inavyosema, na tuone tutafikia maamuzi gani. Hata kama<br />

sitafanikiwa kukushawishi ujiunge na upande wangu, hebu tuendelee kupendana!<br />

Mafundisho Pale Mlima Wa Mizeituni<br />

Hebu tuanze kwa kutazama sura ya 24 ya Injili ya Mathayo, sehemu ya Maandiko<br />

ambayo ni ya msingi sana kwa habari ya matukio ya nyakati za mwisho na kurudi kwa<br />

Yesu. Pamoja na sura ya 25, sehemu hiyo huitwa Mafundisho Pale Mlima Wa Mizeituni,<br />

kwa sababu sura hizo mbili ni taarifa ya mahubiri ambayo Yesu alitoa kwa baadhi ya<br />

wanafunzi Wake wa karibu sana 3 hapo mlimani. Tunaposoma mafundisho hayo,<br />

tutajifunza kuhusu matukio mengi ya nyakati za mwisho, nasi tutaona uwezekano wa<br />

wanafunzi wa Yesu kufikiri muda wa Unyakuo ni upi, waliposikia mafundisho yenyewe.<br />

Yesu akaenda zake, akatoka hekaluni. <strong>Wanafunzi</strong> wake wakamwendea ili<br />

kumwonyesha majengo ya hekalu. <strong>Na</strong>ye akajibu akawaambia, ‘Hamyaoni<br />

haya yote? Amin nawaambieni, halitasalia hapa jiwe juu ya jiwe ambalo<br />

halitabomoshwa.’Hata alipokuwa ameketi katika mlima wa Mizeituni,<br />

wanafunzi wake wakamwendea kwa faragha wakisema, ‘Tuambie! Mambo<br />

hayo yatakuwa lini? <strong>Na</strong>yo ni nini dalili ya kuja kwako, na ya mwisho wa<br />

dunia?’ (Mathayo 24:1-3).<br />

3 Katika Marko 13:3 wanatajwa wale wanne waliokuwepo: Petro, <strong>Ya</strong>kobo, Yohana na Andrea. Mafundisho<br />

ya pale Mlima wa Mizeituni yanapatikanapia katika Marko 13:1-37 na Luka 21:5-36. Utapata habari kama<br />

hizo katika Luka 17:22-37 pia.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!