30.01.2013 Views

Hadithi ya Betty Utambulisho - Raising Voices

Hadithi ya Betty Utambulisho - Raising Voices

Hadithi ya Betty Utambulisho - Raising Voices

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

<strong>Utambulisho</strong><br />

A1


<strong>Utambulisho</strong><br />

Jina langu naitwa <strong>Betty</strong>. Nina umri wa miaka 9 na ngozi <strong>ya</strong>ngu ni nyeusi na nyororo kama imepakwa<br />

mafuta <strong>ya</strong> samli. Shingo <strong>ya</strong>ngu ndefu na mwan<strong>ya</strong> kwenye meno <strong>ya</strong>ngu vinanifan<strong>ya</strong> nionekane binti<br />

mrembo kuliko wote darasani mwetu. Ninapenda kusoma, hasa somo la sa<strong>ya</strong>nsi, ambalo napenda<br />

kuliko yote. Rafiki <strong>ya</strong>ngu wa karibu, Fauzia hukaa karibu na mimi tukiwa darasani. Pia anaishi karibu<br />

na nyumbani kwetu na kila siku tunaenda shuleni na kurudi tukiwa pamoja na wanafunzi wengine,<br />

wavulana kwa wasichana. Wavulana wanapofika nyumbani wanaanza kucheza au kusoma vitabu<br />

v<strong>ya</strong>o. Wakati mwingine wanapaswa kusaidia kukata kuni. Wasichana wote wanatakiwa kwenda jikoni<br />

kupika. Muda pekee tulio nao wa kusoma vitabu vyetu ni wakati tunapokuwa shuleni, lakini hali hii<br />

haitufanyi mimi na Fauzia tuache kusoma. Tutakapokuwa wakubwa tutafan<strong>ya</strong> kazi katika kiwanda<br />

kimojawapo kikubwa huko mjini. Ni ndoto yetu kuwa siku moja tutaenda jijini.<br />

Kijiji chetu ni kidogo sana na karibu watu wote wanafahamiana. Nyumba zimejengwa katika makundi<br />

au miji, na kila nyumba ina jiko la kupikia kwa nje, pamoja na maliwato <strong>ya</strong> pamoja. Familia nyingi zina<br />

bustani <strong>ya</strong> pamoja yenye v<strong>ya</strong>kula vingi sana. Ninaishi na wazazi wangu, kaka zangu wakubwa wawili<br />

na dada yetu mdogo mmoja. Shangazi zangu, wajomba na binamu zangu wanaishi kwenye kundi<br />

la nyumba au mji unaofuatia. Mama <strong>ya</strong>ngu, shangazi <strong>ya</strong>ngu, na karibu wanawake wote wa kijijini<br />

kwetu wanakaa nyumbani wakifan<strong>ya</strong> kazi za bustani na kulea watoto wadogo. Binamu zangu huwa<br />

wananiambia nifute ndoto za kufan<strong>ya</strong> kazi kiwandani kwa sababu wasichana wa kijijini husubiriwa<br />

wakue ili waolewe na kuwa kina mama wa nyumbani. Huwa nawacheka na kuwaambia maisha <strong>ya</strong>ngu<br />

kamwe ha<strong>ya</strong>takuwa hivyo. Sijali wanachokisema binamu zangu lakini…<br />

Nenda kwenye Ukatili Watokea na uchukue kadi namba 1.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B1


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Ukatili Watokea 1<br />

A2


Ukatili Watokea 1<br />

Leo wewe na Fauzia mnakimbia mkirudi nyumbani kutoka shuleni huku mmejitwika vizuri kichwani vitabu<br />

vyenu kuona ni nani atafika wa kwanza pasipo vitabu v<strong>ya</strong>ke kuanguka. Unapofika nyumbani mama <strong>ya</strong>ko<br />

anakwambia kesho asubuhi mtaamka mapema na mtaenda sehemu fulani maalumu. Hupati picha halisi<br />

juu <strong>ya</strong> jambo analozungumzia, lakini huna uhuru wa kumuuliza maswali mengi.<br />

Umelala tongo macho kwa shauku uliyonayo, na leo badala <strong>ya</strong> kwenda shuleni, mama <strong>ya</strong>ko anakuongoza<br />

kuelekea njia iendayo sokoni. Unawazia kwamba huenda anaenda kukununulia nguo mp<strong>ya</strong>. Mnasimama<br />

kwenye kibanda kilichopambwa vizuri. Unawaona wanawake vikongwe wawili wamesimama mlangoni.<br />

Mmoja wao ni mganga anayetibu wanawake kule kijijini. Mwanamke huyo ni maarufu sana na watu<br />

wanasema ndiye mwanamke tajiri sana kuliko wote kijijini. Mama <strong>ya</strong>ko anakukumbatia na kukutakia kila<br />

la heri. Kichwa chako kinaanza kuwa<strong>ya</strong>wa<strong>ya</strong> huku ukikaribishwa uani ambako kumetapakaa wanawake<br />

wengi wagonjwa. Huko ndani unaona beseni lenye maji, na beseni jingine lina maji <strong>ya</strong> kijani, visu<br />

viwili, na chini kuna pia sahani yenye pamba. Mwanamke mmoja anakwambia ulale chini. Mwanamke<br />

mwingine anakaribia na kukushika miguu na mikono kwa kuikandamiza chini kwa nguvu. Kabla hujajua<br />

kinachoendelea, ta<strong>ya</strong>ri imeshavuliwa chupi <strong>ya</strong>ko na yule mganga ameanza kukata. Huwezi kuelezea<br />

maumivu makali unayo<strong>ya</strong>pata mwilini, utafikiri kaa la moto limewekwa sehemu zako za siri. Unatoa macho<br />

na kuanza kupiga kelele kwa maumivu lakini mwanamke mmoja anakuziba mdomo, akikwambia maumivu<br />

<strong>ya</strong>tapoa muda si mrefu. Hatimaye maumivu <strong>ya</strong>napungua taratibu na wale wanawake wanakuweka pamba<br />

yenye unyevunyevu kwenye sehemu za maumivu. Maumivu <strong>ya</strong>naonekana kusambaa mwili mzima. Mtu<br />

fulani anakun<strong>ya</strong>nyua kutoka chini kwenye uchafu na kukuingiza ndani kwenye mkeka ambapo unalala<br />

kwa maumizi tele.<br />

Masaa <strong>ya</strong>napozidi kwendelea unawaona wasichana wengine wakiingia na kutoka ndani <strong>ya</strong> nyumba hiyo.<br />

Moyo wako unashtuka unapomuona Fauzia akiingia, lakini huna nguvu za kumuita akipita na kuingia<br />

kwenye chumba kingine chenye giza. Unapitiwa na usingizi na kulala mpaka wakati wanapokuja kukusafisha<br />

kidonda chako. Pia wanawaletea chakula kizuri mpate kula, lakini hata hivyo maumivu ha<strong>ya</strong>toweki.<br />

Ikiwa unataka kumtafuta Fauzia, nenda kwenye Marafiki na Majirani na uchukue kadi namba 1.<br />

Ikiwa unaamua kwenda nyumbani kumuona mama <strong>ya</strong>ko, nenda kwenye Familia na uchukue kadi<br />

namba 1.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B2


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Marafiki na Majirani 1<br />

A3


Marafiki na Majirani 1<br />

Unachowaza ni kumtafuta Fauzia, lakini kila ukijaribu kuinuka ili ukamtafute, maumivu kwenye uke<br />

wako <strong>ya</strong>nakuwa makali sana. Hivyo, unalala tena chini kwenye giza peke <strong>ya</strong>ko huku ukijiuliza ni kwa<br />

nini mama <strong>ya</strong>ko alikuleta huku. Unaogopa sana kwa sababu maumivu ha<strong>ya</strong>ishi na huwezi kufan<strong>ya</strong><br />

lolote zaidi <strong>ya</strong> kuendelea kulia tu. Hatimaye baada <strong>ya</strong> siku tatu ndefu, unaanza kutembea pole pole<br />

uani ukimtafuta Fauzia. Maumivu <strong>ya</strong>nasambaa miguuni kama moto. Baadaye unamuona amekaa<br />

chini <strong>ya</strong> mti akinywa chai. Anatabasamu kwa udhaifu anapokuona. Mnakaa pamoja lakini hakuna<br />

anayeongea sana kati yenu huku wale vikongwe wakiendelea kuwaangalia kwa ukali. Unataka<br />

kumsimulia kuhusu maumivu makali <strong>ya</strong> kisu ambayo amekua nayo mwilini tangu siku hiyo. Unataka<br />

kujua ikiwa yeye pia alitaka kupiga mayowe na wakamziba mdomo.<br />

Baada <strong>ya</strong> dakika chache Fauzia anasema anataka kujilaza chini. Unatambua kwamba hata yeye<br />

anapitia maumivu makali sana. Unamshika mkono wakati analala na mnamuomba Mungu kwamba<br />

wote mpone kwa haraka. Kwa siku kadhaa zinazofuatia, wewe, Fauzia na wasichana wengine walioko<br />

pale mnajifunza mengi zaidi kuhusu namna <strong>ya</strong> kuwa mwanamke. Wanawake wale wakongwe<br />

wanawapaka dawa za miti shamba kwenye vidonda vyenu kila siku jioni, lakini cha kwako hakionekani<br />

kupona. Fauzia anaendelea kukujulia hali, na hatimaye mnaweza kutembea bila kuhisi maumivu<br />

makali. Balaa linaonekana kufikia mwisho pale mnapoambiwa ni wakati wa kurudi shuleni.<br />

Huku ukifurahia kurudi tena shuleni na kuendeleza ndoto <strong>ya</strong>ko aa kufan<strong>ya</strong> kazi kwenye kiwanda kule<br />

jijini, maumivu kwenye kidonda <strong>ya</strong>naendelea kukutisha kama ha<strong>ya</strong>taishia.<br />

Miaka inapita.<br />

Sasa unakaribia kushuhudia ndoto zako zikitimia. Unatimiza miaka kumi na mitatu, kwa maana hiyo<br />

mwaka unaofuatia utaanza kusoma shule <strong>ya</strong> sekondari. Lakini kabla <strong>ya</strong> hapo…<br />

Nenda kwenye Ukatili Watokea na uchukue kadi namba 2.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B3


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Familia 1<br />

A4


Familia 1<br />

Zimepita siku chache tangu ukeketwe na kutembea kurudi nyumbani ni maumivu makali sana. Mama<br />

<strong>ya</strong>ko anashangaa kukuona. Anakuuliza umekuja kufan<strong>ya</strong> nini nyumbani na ni nani aliyekuruhusu<br />

kurudi, kwani ulitarajiwa kubaki kwa wale wanawake vikongwe mpaka baada juma moja kupita.<br />

Unaanza kulia huku unamshikilia. “Lazima urudi,” anakwambia. “Watapata wasiwasi, huwezi kurudi<br />

nyumbani mpaka kazi ikamilike.” Unaelezea <strong>ya</strong>liyokufikia kwa kukeketwa na kisu, ukidhani mama<br />

<strong>ya</strong>ko hakuwaruhusu wakukekete alipokwambia mlikuwa mnaenda mahali maalumu.<br />

Unamwambia kuhusu maumivu makali unayopata, kwamba hata kutoa mkojo ni vigumu sana.<br />

Anakusikiliza kwa makini na anakupaka dawa fulani za miti shamba kwenye kidonda. Unaumia<br />

kidogo lakini anakuhakikishia kwamba dawa hiyo itakupon<strong>ya</strong>. Daima anaendelea kukwambia juu <strong>ya</strong><br />

jinsi ananvyojivunia juu <strong>ya</strong>ko kwa hutoaibisha familia. Anasema kwamba sasa wewe ni mwanamke<br />

halisi na kwamba wanaume wengi watatamani kukuoa kwa sababu ulitunza ujana wako. Huelewi<br />

chochote lakini anaahidi kukupikia chakula kile ukipendacho utakaporudi nyumbani kwa sababu<br />

wewe ni binti jasiri. Kisha anakusindikiza nje <strong>ya</strong> lango na kukuambia ni muhimu urudi kule haraka na<br />

ukaungane na wasichana wenzako walioko huko. Anakuambia ujikaze na usijali sana maumivu kwa<br />

kuwa wanawake wote lazima wateseke.<br />

Unarudi kule kibandani bila kugunduliwa na mnafundishwa jinsi <strong>ya</strong> kuwa mke halisi pamoja na kuwa<br />

mama. Polepole maumivu <strong>ya</strong>naanza kupungua, na wasichana wengi wanapopona, kunafanyika<br />

sherehe kubwa ambapo watu wote kijijini wanakuja kusherehekea kupatikana kwa wanawake wap<strong>ya</strong>.<br />

Unaporudi shuleni, walimu wako wanakutambua kwa namna mp<strong>ya</strong> na wewe anaanza kujivunia kwa<br />

kukeketwa. Majuma <strong>ya</strong>nageuka miezi, na kila muhula unapopita, unapata shauku zaidi <strong>ya</strong> kujiunga<br />

na shule <strong>ya</strong> sekondari, lakini…<br />

Nenda kwenye Ukatili Watokea na uchukue kadi namba 2.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B4


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Ukatili Watokea 2<br />

A5


Ukatili Watokea 2<br />

Hujui hata kidogo kwamba kuna hatima tofauti inayokungoja. Kwenye siku <strong>ya</strong> mwisho <strong>ya</strong> kumaliza shule <strong>ya</strong><br />

msingi, unarudi nyumbani ukiwazia juu <strong>ya</strong> kujiunga na shule <strong>ya</strong> sekondari. Kwa siku chache za mwanzo wa<br />

likizo, unawasaidia wanawake wengine katika kazi za nyumbani na unazungumza na Fauzia. Siku moja usiku,<br />

ukiwa unaanza kupata usingizi, unamsikia juujuu mama <strong>ya</strong>ko akiongea na shangazi zako. Unan<strong>ya</strong>tia karibu na<br />

kuwasikiliza kisiri huku wakipanga maandalizi <strong>ya</strong> harusi <strong>ya</strong>ko. Unaamka na kuwauliza juu <strong>ya</strong> nini kinachoendelea.<br />

Mama <strong>ya</strong>ko anakwambia, “Kuna tajiri mmoja kijijini ambaye anataka kutoa mahari kwa ajili <strong>ya</strong>ko! Anataka<br />

mke atakayemzalia mtoto wa kiume. Wake zake wengine wawili wamemzalia watoto wa kike tu. <strong>Betty</strong> tunajua<br />

utailetea sifa familia hii.” Unakosa la kusema.<br />

Asubuhi inayofuatia, kila mtu anajiandaa ta<strong>ya</strong>ri kwa harusi <strong>ya</strong>ko. Wanawake wanapaka mwili wako kwa<br />

mafuta na manukato za mitishamba kukuandaa kwa harusi <strong>ya</strong>ko jioni hiyo na nguo nzuri sana zimeshonwa<br />

kwa ajili <strong>ya</strong>ko. Siku <strong>ya</strong> harusi <strong>ya</strong>ko ndipo unakutana na mumeo kwa mara <strong>ya</strong> kwanza. Ni mzee sana. Watu<br />

wanaokuzunguka wanafurahi na kusherehekea. Wewe huelewi kihalisi aina <strong>ya</strong> maisha utakayoishi na mzee<br />

huyu. Unajawa na hofu.<br />

Usiku wa kwanza wa ngono baada <strong>ya</strong> harusi kuisha anatoboa utando wa ngozi ulioziba pamoja na kovu<br />

lililotokana na kukeketwa. Maumivu unayopata wakati wa kushiriki tendo la kujamiana ni makali sana karibu<br />

sawa na <strong>ya</strong>le <strong>ya</strong> wakati ulipokeketwa. Lakini unajaribu kuvumilia na kutimiza wajibu wako kwa uadilifu, ukifan<strong>ya</strong><br />

kazi za bustani kwa bidii, kutunza mji, na kujaribu kadri uwezavyo kujizuia kulia kwa maumivu unayopata wakati<br />

wa kujamiana. Kuna siku nyingine unahisi kama uke wako unapasuliwa lakini unajua kwamba kama mke wa<br />

mtu hupaswi kulalamika.<br />

Ni pale tu maumivu <strong>ya</strong>napongezeka zaidi ambapo unaamua kutafuta msaada.<br />

Ikiwa unataka kwenda kwenye kituo cha af<strong>ya</strong> kilicho karibu na wewe, nenda kwenye Huduma za Matibabu<br />

na uchukue kadi namba 1.<br />

Ikiwa unaamua kuomba ushauri kutoka kwa wazee wa kijiji, nenda kwenye Viongozi wa Kijadi na uchukue<br />

kadi namba 1.<br />

Ikiwa unaamua kuongea na mama <strong>ya</strong>ko, nenda kwenye Familia na uchukue kadi namba 2.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B5


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Huduma za Matibabu 1<br />

A6


Huduma za Matibabu 1<br />

Unafika kituo cha af<strong>ya</strong>. Kimefurika na watu kama kawaida kwa sababu matibabu ni bure, lakini hata<br />

hivyo unapata sehemu <strong>ya</strong> kukaa. Unahisi maumivu makali. Ni kama vile unachomwa chomwa na visu<br />

mwili mzima. Daktari anapokufikia, anakupa kipimo cha mimba. Pia anakumiminia dawa kwenye<br />

kidonda na anakuelezea kuwa ni kawaida kidonda kuhuishwa hapo mwanamke anaposhiriki kitendo<br />

cha kujamiana kwa mara <strong>ya</strong> kwanza baada <strong>ya</strong> kukeketwa. Anakwambia ujikaze na usilalamike, kwa<br />

sababu tatizo hilo hutokea kwa wanawake wengi. Pia daktari anakwambia una ujauzito. Unafurahia<br />

sana. Unawazia kwamba hatimaye angalau jambo zuri limetokea katika ndoa <strong>ya</strong>ko iliyojaa machungu.<br />

Unaamini kwamba kwa sababu una ujauzito mume wako hatataka kulala na wewe tena.<br />

Maumivu uliyokuwanayo <strong>ya</strong>napungua unapowazia kupata mtoto wako. Unajaribu hata kuota hali<br />

itakavyokuwa ikiwa utapata mtoto wa kiume. Labda mume wako atakuruhusu umalizie masomo<br />

<strong>ya</strong>ko! Unatamania kuwaambia mume wako na mama <strong>ya</strong>ko kuhusu mimba <strong>ya</strong>ko. Unaanza kuchagua<br />

majina <strong>ya</strong> kiume. Baada <strong>ya</strong> kumshukuru sana kila mtu, unatoka nje na kurudi nyumbani. Ghafla dunia<br />

haionekani kuwa mba<strong>ya</strong> sana kwako kama wakati ulipoingia hapo hospitalini. Kama Fauzia angekuwa<br />

anaishi eneo jirani, angefurahia sana kusikia habari zako njema, lakini anaishi mbali sana pamoja na<br />

mume wake wa hivi majuzi. Unajiuliza kama yeye amekwisha mpata mtoto au bado. Unaharakisha<br />

kurudi nyumbani ili ukampashe habari hizi mume wako.<br />

Nenda kwenye Kurudi Nyumbani na uchukue kadi namba 1.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B6


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Familia 2<br />

A7


Familia 2<br />

Mama <strong>ya</strong>ko anakusikiliza na kukuhurumia. Hata hivyo, anakwambia kwamba ni jambo la kawaida<br />

kuhisi maumivu wakati wa kujamiana, na kwamba maadamu utazaa mtoto wa kiume, tunza mji<br />

wako, usije ukaleta aibu kwa mume wako, kila kitu kitakuwa sawa. Anakukumbusha kwamba<br />

mumeo alilipa mahari nzito na anakuuliza iwapo umemfanyia jambo lolote lililomuudhi mume<br />

wako. Unapomwambia kwamba ulikuwa mtiifu kwa kila kitu, ndipo anakwambia ukae kwake kwa<br />

siku kadhaa mpaka utakapopata nafuu. Anakuon<strong>ya</strong> kwamba ni lazima urudi kwa mume wako baada<br />

<strong>ya</strong> majeraha kupona.<br />

Unaangalia vitabu v<strong>ya</strong>ko v<strong>ya</strong> shule <strong>ya</strong> msingi, unafunuafunua kwa shauku lakini ghafla unavitupia<br />

nje kwa hasira kwa sababu unajua hutavitumia tena. Unaviwashia kiberiti na kuvitazama vikiteketea<br />

kwa moto kama <strong>ya</strong>livyo maisha <strong>ya</strong>ko. Unawaza kuhusu Fauzia ambaye pia amekwishaolewa na<br />

hujui anaendeleaje, na pia kama mume wake anaishi naye kwa raha, au kama ndoa <strong>ya</strong>ko ndiyo hali<br />

kielelezo <strong>ya</strong> wanawake wote walioolewa.<br />

Mama <strong>ya</strong>ko anahisi moshi na anataka nje kukuchungulia. Anapoona vitabu vinateketea hadi kuwa<br />

majivu, anakaa chini pembeni na wewe. “Ni bora kuziacha ndoto hizo ziteketee, <strong>Betty</strong>. Unatakiwa<br />

kuzingatia kupata watoto. Isitoshe, kwa nini kesho usiende hospitali kupimwa kama una ujauzito?”<br />

Ikiwa unaamua kwenda kuongea na wazee wa kijijji, nenda kwenye Viongozi wa Kijadi na uchukue<br />

kadi namba 1.<br />

Ikiwa unaamua kwenda moja kwa moja kwenye kliniki, nenda kwenye Huduma za Matibabu na<br />

uchukue kadi namba 1.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B7


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Kiongozi wa Jadi 1<br />

A8


Kiongozi wa Jadi 1<br />

Wakati wowote kunapotokea tatizo kubwa kijijini, watu huenda kuzungumza na wazee. Una<strong>ya</strong>kumbuka<br />

macho <strong>ya</strong> ukarimu <strong>ya</strong> Bwana Moses tangu ukiwa bado mdogo sana. Unaamua kwenda nyumbani<br />

kwake kuzungumza naye.<br />

Unapofika nyumbani kwake, unamkuta akiwa na mtu mwingine wa kutoka kijijini kwenu. Msichana<br />

anakuletea kigoda na unaketi kivulini ukisubiri amalize mazungumzo <strong>ya</strong>ke. Anapomaliza na<br />

kukupungia mkono uje kwake, unapiga magoti kumtukuza na kumsalimia. Anainamisha kichwa chake<br />

na kisha anakuuliza ni tatizo gani limekufan<strong>ya</strong> uende kumuona. Unamwelezea kwamba uliachishwa<br />

masomo na kulazimishwa kuolewa na mwanamume mzee sana, na kwamba mwili wako unakuuma,<br />

na umepoteza fursa <strong>ya</strong>ko <strong>ya</strong> kupata elimu. Anacheka kicheko cha chinichini na kukupapasa kichwani<br />

kama vile bado u mtoto mdogo. “<strong>Betty</strong>,” anafunga macho <strong>ya</strong>ke wakati anaongea na wewe, “Hili ni<br />

jukumu lako katika maisha – kuwa mke mzuri na mama pia. Bwana tajiri sana amekulipia mahari<br />

kubwa kwa ajili <strong>ya</strong>ko, hivyo lazima uwe mtiifu kwa mumeo na usilete aibu kwa kijiji chetu.”<br />

Unainamisha kichwa chako kwa huzuni. Unajua huwezi kujadiliana naye suala la maumivu unayopata<br />

kwa sababu ni mtu wa heshima sana kama yeye, hivyo unamshukuru na kumwomba uondoke.<br />

Unapotembea kurudi nyumbani unawazia juu <strong>ya</strong> nini utachofan<strong>ya</strong>. Hutaki kuleta aibu kwa familia<br />

<strong>ya</strong>ko, lakini pia hutaki kuishi katika maumivu <strong>ya</strong> kudumu. Uamuzi wako wa mwisho ni kwenda<br />

hospitalini iliyo karibu ili upate kusaidiwa.<br />

Nenda kwenye Huduma za Matibabu na uchukue kadi namba 1.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B8


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Kurudi Nyumbani 1<br />

A9


Kurudi Nyumbani 1<br />

Leo ni siku tofauti na siku nyingine unapohofia kurudi kwa mume wako. Leo unamwandalia chakula<br />

akipendacho zaidi, n<strong>ya</strong>ma <strong>ya</strong> mbuzi, mboga za majani, siagi <strong>ya</strong> karanga pamoja na viazi vikuu.<br />

Anakula chakula chake akiwa amekaa kwenye kigoda huku wewe ukiwa unamsubiri kwa heshima<br />

amalize kula. Anapomaliza kula, unamshirikisha habari mp<strong>ya</strong> kwamba una ujauzito. Kwa mara <strong>ya</strong><br />

kwanza tangu uanze kuishi naye anatabasamu, na anaonyesha kwa dhati furaha <strong>ya</strong>ke kwako.<br />

“Asante kwa kunizalia mtoto wa kiume, najua atakuwa wa kiume kwa sababu nililipa mahari kubwa<br />

sana kukuoa wewe. Najua hatimaye nitapata mrithi.”<br />

Anaendeleza burudani kwa kukunyenyua na kukuingiza chumba cha kulala. Unamwambia jinsi<br />

unahisi maumivu kutokana na majeraha <strong>ya</strong> hivi karibuni na kwamba daktari amesema unahitaji<br />

kupumzika kwa muda mpaka upone. Hakusikilizi. Anajijali yeye mwenyewe. “Hakuna sababu <strong>ya</strong><br />

kuwa na wasiwasi,” anakwambia. Unapoendelea kukataa na kugeukia pembeni, anapata hasira.<br />

Anakuamuru utulie na anakukandamizia kitandani huku ukilia na kumwomba akuache.<br />

Miezi inapita wakati mimba <strong>ya</strong>ko inazidi kuwa kubwa kila siku. Ulifikiri mimba <strong>ya</strong>ko itamridhisha<br />

mumeo na aache kujamiana na wewe, lakini anaendelea kukulazimisha kufan<strong>ya</strong> ngono. Umejifunza<br />

kutolia wala kulalamika kwa sababu ukifan<strong>ya</strong> hivyo inamfan<strong>ya</strong> awe mkorofi zaidi. Unaendelea kuamini<br />

kwamba kuna wakati mimba itakuwa kubwa zaidi kiasi cha kumfan<strong>ya</strong> awe mbali nawe kwa ngono.<br />

Mara muda wa kujifungua kwako umefika. Wake wenzio wanamleta mkunga wa kijadi akuhudumie.<br />

Uchungu wa kujifungua unakushika kwa muda mrefu sana, zaidi <strong>ya</strong> siku mbili. Hatimaye, mkunga<br />

wako anamshauri mumeo akupeleke hospitalini.<br />

Nenda kwenye Huduma za Matibabu na uchukue kadi namba 2.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B9


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Huduma za Matibabu 2<br />

A10


Huduma za Matibabu 2<br />

Hospitalini, daktari anakusaidia kujifungua. Hatimaye mtoto anapotoka, ni mtoto wa kiume, lakini kwa<br />

bahati mba<strong>ya</strong> amefariki. Unalia sana wala huwezi kun<strong>ya</strong>maza. Daktari anajaribu kukueleza kwamba<br />

ni jambo la kawaida kwa msichana mwenye umri mdogo kujifungua kwa shida na kwamba kichanga<br />

chako kilikwama kwenye njia <strong>ya</strong> uzazi. Mama <strong>ya</strong>ko na wake wenzio wanajaribu kukun<strong>ya</strong>mazisha na<br />

kukuambia kwamba usihofie kwani bado unafursa <strong>ya</strong> kujaribu tena, lakini huachi kujilaumu na kuhisi<br />

kuwa ni amkosa <strong>ya</strong>ko.<br />

Unataka tu kurudi nyumbani, lakini hali bado haijawa nzuri sana. Akiongea na wewe pamoja na<br />

mama <strong>ya</strong>ko kwa faragha, daktari anawaarifu kuwa hapo wakati wa kujifungua umepata tundu ukeni,<br />

<strong>ya</strong>ani fistula na hivyo hutaweza kudhibiti mkojo. Mkojo utakuwa tu unatiririka mfululizo.<br />

Unakasirishwa sana na taarifa hiyo kiasi kwamba hakuna mtu anayeweza kukufariji tena. Unatumaini<br />

mume wako atalipia gharama za kukufanyia upasuaji na kuziba sehemu yenye tundu ili usije ukawa<br />

unatoa harufu mba<strong>ya</strong> na kusumbuliwa kama daktari alivyokuelezea. Lakini mumeo anazipokea<br />

habari hizo shingo upande…<br />

Nenda kwenye Ukatili Watokea na uchukue kadi namba 3.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B10


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Familia 3<br />

A11


Familia 3<br />

Wake wenza wanakukaribisha, lakini wanaonyesha chuki. Wanakushutumu kwamba unajivunia<br />

ilihali umeshindwa kumzalia mumeo mtoto wa kiume. Wanasema kutiririka mkojo ndiyo malipo<br />

unayostahili. Unatoa harufu mba<strong>ya</strong> sana kiasi kwamba wanakutenga mbali wakati wa chakula.<br />

Haupiti muda mrefu, harufu <strong>ya</strong>ko mba<strong>ya</strong> inazidi kuwa kali zaidi na utunzaji wa kila siku ambao<br />

unahitaji unawakera sana wake wenza na wanakulazimu uanze kulala nje ambako harufu <strong>ya</strong>ko<br />

haitawasumbua na kuwafan<strong>ya</strong> wakeshe bila sababu. Wakati wote wanakuzungumzia wewe na jinsi<br />

ambavyo umechezea maisha <strong>ya</strong>ko kwa sababu hakuna mwanamume ambaye anaweza kukutaka<br />

tena.<br />

Hatimaye mmoja wao anakwambia,“Unanuka sana kiasi kwamba hatuwezi tena kulimana na<br />

wewe bustanini. Hatuwezi kufuatana na wewe hadi madukani kwa sababu unatuaibisha. Watu<br />

hawatutembelei tena kwa sababu <strong>ya</strong>ko. Unatakiwa uondoke.” Asubuhi <strong>ya</strong>ke unafungasha kifurushi<br />

kidogo cha nguo zako na kuondoka mapema kabla hakujapambazuka.<br />

Ikiwa unaamua kwenda kwa wazazi wako, nenda kwenye Familia na uchukue kadi namba 4.<br />

Ikiwa unataka fursa nyingine kwa kuruhusiwa kumrudia mumeo, nenda kwenye Fursa na uchukue<br />

kadi namba 1.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B11


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Ukatili Watokea 3<br />

A12


Ukatili Watokea 3<br />

Unapofika nyumbani unakuta mume wako anakusubiri kwa hamu. Anapopata taarifa kwamba<br />

umejifungua mtoto wa kiume aliyekufa, anaghadhabika. Anakufokea na kukutupia bakuli kichwani.<br />

Anakushutumu kwamba wewe ni mchawi aliyeolewa ili umtese na anasema hakuna kilichobaki kati<br />

yenu. Akikusukumia pembeni, anakuambia upotelee mbali na ukatafute sehemu mahali pengine pa<br />

kuishi.<br />

Hupati hata fursa <strong>ya</strong> kumwambia kuhusu fistula wala kumuomba akulipie gharama za upasuaji kabla<br />

haja kutimua nje na kukutupia nguo zako uondoke.<br />

Ikiwa unaamua kwenda kuishi na wake wenza, nenda kwenye Familia na uchukue kadi namba 3.<br />

Ikiwa unaamua kutafuta msaada kutoka kwa mganga wa jadi kijijini kwenu, nenda kwenye Mganga<br />

wa Jadi na uchukue kadi namba 1.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B12


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Mganga wa Jadi 1<br />

A13


Mganga wa Jadi 1<br />

Unamkumbuka mwanamke aliyekukeketa miaka mingi iliyopita na kwamba wanajamii wanamuamini<br />

kuwa ni mganga bora kuliko wengine pale kijijini. Baada <strong>ya</strong> kukukeketa aliahidi kwamba unaweza<br />

kwenda kumuona wakati wowote unapokuwa na shida. Unaamini atakusaidia kutibu tatizo lako.<br />

Unarundi kwenye mazingira <strong>ya</strong> nyumba ambapo uliumia na kuishi kwa maumivu makali ulipokuwa<br />

bado mdogo, na unasita kidogo wakati unavuta kumbukumbu, lakini unaendelea kwenda na<br />

kumuona huyo mama ambaye sura <strong>ya</strong>ke utaikumbuka daima. “Shikamoo, ni mimi <strong>Betty</strong>,”unataja jina<br />

lako ukitarajia atakukumbuka. Lakini sura <strong>ya</strong>ke inaonesha hakumbuki kitu na kisha anaonesha kuhisi<br />

viba<strong>ya</strong> anaposikia harufu <strong>ya</strong> mkojo. Unafan<strong>ya</strong> haraka kumwambia kilichokupata na unamuomba<br />

akusaidie. Anakutazama kuanzia juu mpaka chini, anaangalia mikono <strong>ya</strong>ko mitupu pamoja na sketi<br />

<strong>ya</strong>ko iliyolowa mkojo. “Siwezi kukusaidia,”anakwambia huku akitikisa kichwa. “Hakuna chochote<br />

ninachoweza kukufanyia. Harufu hiyo ni mba<strong>ya</strong> sana kwangu na unaweza kuharibu dawa zangu.<br />

Unatakiwa kuondoka sasa hivi.” Anakuashiria uondoke halafu anakwenda zake.<br />

Ni mateso makali sana kwa ahadi na ndoto ulizokuwa nazo. Unahisi upweke usio na matumaini<br />

yoyote.<br />

Ikiwa unaamua kujaribu kuona kama wake wenza watakubali uishi nao, nenda kwenye Familia na<br />

uchukue kadi namba 3.<br />

Ikiwa unaamua kwamba mtu pekee atakaye kupokea kwa sasa ni mama <strong>ya</strong>ko, nenda kwenye<br />

Familia na uchukue kadi namba 4.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B13


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Fursa 1<br />

A14


Fursa 1<br />

Huoni kama kutakuwa na maendeleo yoyote iwapo hutafanikiwa kufanyiwa upasuaji na kutibiwa<br />

fistula. Kimbilio lako pekee ni mume wako, hivyo unakwenda kwenye nyumba <strong>ya</strong>ke wakati akiwa<br />

bado hajarudi na unamuandalia chakula maalumu cha jioni. Anapofika nyumbani, anakuona na<br />

kutaka kujua unafan<strong>ya</strong> nini hapo nyumbani. Humjibu chochote, lakini unamuomba akusikilize.<br />

Anakupuuza mwanzoni lakini hukati tamaa kwa kuendelea kumsihi mpaka hatimaye anakusikiliza.<br />

Unamwelezea jinsi utakavyomzalia mrithi. Unamkumbusha kwamba umeshazaa mtoto wa kwanza<br />

wa kiume, lakini ni kukosekana kwa huduma nzuri za kitabibu ambako kumesababisha kifo cha<br />

mtoto huyo. Unamwahidi kwamba iwapo atakupa fursa nyingine tena, utajitunza vizuri pamoja na<br />

kutapata huduma bora za kitibabu. Unamuona akianza kushawishika, na unamhakikishia kabisa<br />

kwamba utamzalia mtoto wa kiume. Hatimaye anakubali kulipa gharama za kufanyiwa upasuaji ili<br />

kuziba fistula na anakuruhusu urudi tena kukaa kwenye nyumba <strong>ya</strong>ke.<br />

Kwa bahati nzuri, upasuaji unafanyika kwa mafanikio. Na muda si mrefu unashika mimba nyingine.<br />

Safari hii mumeo anajitoa kwa gharama zote kuhakikisha anapata mtoto wa kiume mwenye af<strong>ya</strong><br />

nzuri na ambaye atarithi mali zake kwa sababu yeye amezeeka.<br />

Anakupa matunzo mazuri sana kwa kuwatowajali wake zake wengine, jambo ambalo linawafan<strong>ya</strong><br />

wakuchukie zaidi. Wanakwambia unajivuna na huna shukurani, lakini unajitahidi kutowajali sana.<br />

Unajihisi kama vile umepewa fursa nyingine, lakini…<br />

Nenda kwenye Ukatili Watokea na uchukue kadi namba 4.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B14


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Familia 4<br />

A15


Familia 4<br />

Harufu inayotoka mwilini mwako ni mba<strong>ya</strong> sana kiasi kwamba unaacha kukaa pamoja na watu kwa<br />

mazungumzo. Unajihisi kutengwa na mpweke. Watu hawakukaribishi tena majumbani mwao wala<br />

kwenye matukio muhimu <strong>ya</strong> kijamii. Tumaini lako pekee ni kwamba mama <strong>ya</strong>ko atapata suluhu <strong>ya</strong><br />

tatizo lako.<br />

Nyumbani kwa mama <strong>ya</strong>ko, unamsalimia na anakukaribisha ndani vizuri kwa ukarimu. Anakushika kwa<br />

muda kidogo na kuonyesha masikitiko <strong>ya</strong>ke juu <strong>ya</strong> mtoto wako uliyefariki. Anasema unakaribishwa<br />

nyumbani wakati wowote lakini hutakaa kwenye nyumba kuu kwa sababu harufu <strong>ya</strong>ko ile mba<strong>ya</strong><br />

itamsumbua baba <strong>ya</strong>ko. Kwa huzuni kubwa, anakusindikiza kwenye kibanda kidogo kilichopo nyuma<br />

<strong>ya</strong> nyumba na ambacho hakijatumika kwa miaka kadhaa iliyopita. Anakusaidia kufungua na kuweka<br />

vizuri nguo zako chache ulizokuja nazo na kisha anakuletea maji <strong>ya</strong> kuoga.<br />

Hivi ndivyo unavyoishi sasa – mpweke, aliyetengwa na jamii, na usiyekaa katika familia yoyote. Ndoto<br />

na matarajio <strong>ya</strong>ko yote vimegeuka kuwa kumbukumbu za ukatili.<br />

MWISHO<br />

Huu ndio mwisho wa hadithi <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong>. Tumia dakika chache kukaa kim<strong>ya</strong> na utafakari tajiriba <strong>ya</strong>ke<br />

<strong>Betty</strong>. Unapokuwa ta<strong>ya</strong>ri, muombe mwezeshaji akupe hadithi <strong>ya</strong> mwanamke mwingine.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B15


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Ukatili Watokea 4<br />

A16


Ukatili Watokea 4<br />

Unapokaribia kujifungua unapanga kwenda kwenye kituo cha af<strong>ya</strong> kilichoko karibu na mnakoishi,<br />

punde tu unapoanza kuhisi uchungu wa kujifungua.<br />

“Safari hii, kichanga chako kitakuwa salama,” unamhakikishia mumeo wakati unaondoka kwenda<br />

hospitalini. Bila kupata shida yoyote, daktari anakusaidia na masaa machache baadaye unajifungua<br />

mtoto wa kike mwenye af<strong>ya</strong> njema.<br />

Unafurahi kwamba mtoto ni mzima na kwamba hukupata shida yoyote katika kujifungua, lakini<br />

kujifungua mtoto wa kike kutaleta matatizo. Unamshika vizuri mtoto wako kama wahudumu<br />

wanavyokuelekeza na unaanza kumyonyesha.<br />

Unapofika nyumbani siku chache baadaye, mume wako anakataa hata kukuangalia wewe wala<br />

mwanae wa kike. Anawaambia wake wenzako wakutolee nje vitu v<strong>ya</strong>ko vyote kwa sababu<br />

hutaendelea kukaa kwenye nyumba <strong>ya</strong>ke tena. Safari hii, wake wenzio wanakubeza na kukuambia<br />

kwamba hawawezi kulea mtoto mwingine wakati na wao wana watoto. Huna njia mbadala isipokuwa<br />

kurudi nyumbani kwa mama <strong>ya</strong>ko.<br />

Nenda kwenye Familia na uchukue kadi namba 5.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B16


<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong><br />

Familia 5<br />

A17


Familia 5<br />

Unamlea binti <strong>ya</strong>ko ukiwa nyumbani kwa mama <strong>ya</strong>ko. Mama <strong>ya</strong>ko hakuulizi kwa nini mumeo<br />

amekufukuza, wala hakutupii lawama kwa nini umezaa mtoto wa kike. Badala <strong>ya</strong>ke, anakusaidia<br />

kumlea mtoto wako kwa malezi bora kadri inavyowezekana. Unampatia jina Muujiza kwa sababu<br />

kwako wewe, ni Muujiza ambao umekufundisha mambo mengi kuhusu mapenzi na maisha.<br />

Baada <strong>ya</strong> kumwachisha kunyon<strong>ya</strong>, unapata kibarua kwenye mkahawa wa pale kijijini kwa kusafisha<br />

pale baada <strong>ya</strong> kufunga. Unatumia pesa hizi japo ni kidogo, kugharamia mahitaji <strong>ya</strong> nyumbani na<br />

kuweka akiba kidogo kwa ajili <strong>ya</strong> kumsomeshea Muujiza. Japokuwa ndoto zako zimefutika, utafan<strong>ya</strong><br />

kila liwezekanalo kuhakikisha kwamba binti <strong>ya</strong>ko anapata elimu <strong>ya</strong> kutosha na pia kwamba hata<br />

ataweza kutembelea jiji.<br />

MWISHO<br />

Huu ndio mwisho wa hadithi <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong>. Tumia dakika chache kukaa kim<strong>ya</strong> na utafakari tajiriba <strong>ya</strong>ke<br />

<strong>Betty</strong>. Unapokuwa ta<strong>ya</strong>ri, muombe mwezeshaji akupe hadithi <strong>ya</strong> mwanamke mwingine.<br />

<strong>Hadithi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Betty</strong> B17

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!