Download TPS, East Africa 2008 Annual Report - Serena Hotels
Download TPS, East Africa 2008 Annual Report - Serena Hotels
Download TPS, East Africa 2008 Annual Report - Serena Hotels
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Taarifa ya Mwenyekiti (yaendelea)<br />
Sehemu ya nje ya Hoteli ya Ngorongoro <strong>Serena</strong><br />
Hatimaye, kwa mara nyingine, Hoteli za <strong>Serena</strong> zilitwaa<br />
nafasi za juu kwenye shindano la jarida la Travel News<br />
Magazine kwa utuzaji bora. Mpango huu wa uzawadiaji<br />
unatekelezwa kupitia utafiti wa wateja, utendaji bora katika<br />
sekta mbali mbali za utalii Afrika Mashariki. Hata kama<br />
kulikuwa na changamoto zilizotajwa hapo awali, ukarabati<br />
mdogo ulitekelezwa katika raslimali mbali mbali za Kundi<br />
kuhakikisha kuwepo kwa utekelezaji bora wa shughuli bila<br />
kuathiri ubora wa sura ya majumba.<br />
Kujitolea kwa <strong>Serena</strong> kuzindua mkakati wa habari na<br />
mawasiliano ambao unakamilisha mikakati mingine ya<br />
biashara na mipango uliendelea mwaka <strong>2008</strong>. Ningependa<br />
kufafanua kwamba ingawa mwaka ulikuwa mgumu,<br />
usimamizi haukusitisha uzinduzi wa mipango muhimu<br />
ambayo endapo ingecheleweshwa ingehatarisha ushindani<br />
wa muda mrefu wa Kampuni. Kwa sababu hiyo, Kampuni<br />
sasa inatoa huduma za mawasiliano ya mtandao ya moja kwa<br />
moja kwa wageni wake katika hoteli zake. Mpango wa<br />
kuweka pamoja habari uko katika hatua za mwisho za<br />
uzinduzi baina ya afisi kuu mbili nchini Kenya na Tanzania<br />
ambao utasaidia kuafikia ulipiaji huduma/vyumba mapema<br />
na mifumo ya fedha na kupelekea kuwepo kwa utendaji bora<br />
wa kazi, usimamizi na uthibiti bora. Mwisho, ufanisi<br />
umepatikana kuhusiana na uuzaji wa biashara kupitia mfumo<br />
wa elektroniki ambapo hoteli za <strong>Serena</strong> zilianza kutumia<br />
mbinu hiyo mwezi Agosti mwaka <strong>2008</strong> huku kukiwa na<br />
mfumo wa utumaji maombi unaopatikana kupitia wavuti wa<br />
makundi yote ya hoteli yaliyoko mijini na fuo za bahari.<br />
Kundi linazidi kuamini kwamba wafanyakazi wake ni raslimali<br />
muhimu katika hazina ya biashara mambo yanapokuwa<br />
magumu. Licha ya changamoto za kibiashara, utuzaji wa<br />
wafanyakazi, utoaji mafunzo ya hali ya juu, uimarishaji wa<br />
uwezo ulibakia kuwa swala lililopewa kipaumbele. Wakati<br />
wa kipindi hiki cha mwaka, Kundi lilimwajiri Meneja wa<br />
Utoaji Mafunzo na Maendeleo ambaye kwa sasa anaendesha<br />
mkakati wa kuimarisha uzalishaji.<br />
Kama mnavyofahamu, wasafiri wa sasa wamejitolea<br />
kuhakikisha raslimali wanazotumia zinatoa mchango wao<br />
kuimarisha maendeleo miongoni mwake kupitia uhifadhi wa<br />
mifumo ya ikolojia na kuongoza katika ustawi bora wa utalii.<br />
Kundi linazidi kutekeleza wajibu wake katika jamii kwa<br />
kuhusisha pamoja shughuli hizo kwenye mkakati wake wa<br />
kibiashara. Kufikia sasa, shughuli za Kampuni katika wajibu<br />
wa jamii zinazidi kuangazia utalii wa ikolojia, uhifadhi wa<br />
mazingira, utoaji mafunzo, Afya ya Umma na maendeleo ya<br />
jamii. Mnamo mwezi Juni <strong>2008</strong>, <strong>TPS</strong>EA ilichapisha jarida lake<br />
la pili la wajibu wake kwa jamii linalojulikana kama <strong>Serena</strong><br />
Outreach to Society (SOS) ambalo linaangazia shughuli hizi.<br />
Kwa maelezo zaidi kuhusiana na wajibu wa Kampuni kwa<br />
jamii tafadhali rejelea ukurasa 20 na 21 wa ripoti hii.<br />
Kundi limebakia kuwa mchangiaji mkuu kwa hazina ya<br />
serikali za Kenya, Tanzania na Zanzibar. Kwa wastani Kundi<br />
lililipa kiwango sawa na Shilingi milioni 648 pesa za Kenya<br />
kwa ushuru wa moja kwa moja au usio wa moja kwa moja.<br />
Pia lilitoa Shilingi milioni 121 kwa mabaraza ya serikali za<br />
wilaya kama ada ya nia njema/ukodishaji katika miliki mbali<br />
mbali mwaka <strong>2008</strong>.<br />
Halmashauri na wasimamizi wanakadiria kuwepo kwa<br />
mazingira magumu ya biashara mwaka 2009 na athari za<br />
kushuka kwa uchumi wa dunia na kuzidi kuwepo kwa wasi<br />
wasi wa kifedha. Hali hii inatarajiwa kuchochewa na maswala<br />
mengine, masoko yasiyoaminika na kushuka kwa imani<br />
miongoni mwa wateja hali inayotarajia kuendelea kuathiri<br />
mahitaji ya utalii duniani kwa muda wa miezi 12 ijayo.<br />
Kama ilivyoshuhudiwa muhula wa kwanza wa mwaka 2009,<br />
kipindi cha mwaka kilichosalia kitazidi kukumbwa na<br />
changamoto ambazo zitaathiri gharama za uendeshaji<br />
biashara kutokana na ugumu wa maisha unaosababishwa na<br />
mfumuko wa bei, njaa iliyoko na gharama zilisizotarajiwa za<br />
kawi. Kwa sasa, majibu kutoka kwa waendeshaji wakuu wa<br />
biashara kuhusiana na maagizo ya vyumba katika vituo vyote<br />
vya mapumziko ni ya kutia shaka. Wasimamizi wametambua<br />
ukodishaji wa vyumba kwa muda mfupi siku za hivi karibuni.<br />
Hali hii ni ya kutia moyo.<br />
Chajio kando ya moto katika Hoteli ya Ngorongoro <strong>Serena</strong><br />
12 <strong>TPS</strong> EASTERN AFRICA LIMITED | ANNUAL REPORT AND FINANCIAL STATEMENTS <strong>2008</strong>