18.06.2013 Views

Download TPS, East Africa 2008 Annual Report - Serena Hotels

Download TPS, East Africa 2008 Annual Report - Serena Hotels

Download TPS, East Africa 2008 Annual Report - Serena Hotels

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Taarifa ya Mwenyekiti (yaendelea)<br />

Sehemu ya nje ya Hoteli ya Ngorongoro <strong>Serena</strong><br />

Hatimaye, kwa mara nyingine, Hoteli za <strong>Serena</strong> zilitwaa<br />

nafasi za juu kwenye shindano la jarida la Travel News<br />

Magazine kwa utuzaji bora. Mpango huu wa uzawadiaji<br />

unatekelezwa kupitia utafiti wa wateja, utendaji bora katika<br />

sekta mbali mbali za utalii Afrika Mashariki. Hata kama<br />

kulikuwa na changamoto zilizotajwa hapo awali, ukarabati<br />

mdogo ulitekelezwa katika raslimali mbali mbali za Kundi<br />

kuhakikisha kuwepo kwa utekelezaji bora wa shughuli bila<br />

kuathiri ubora wa sura ya majumba.<br />

Kujitolea kwa <strong>Serena</strong> kuzindua mkakati wa habari na<br />

mawasiliano ambao unakamilisha mikakati mingine ya<br />

biashara na mipango uliendelea mwaka <strong>2008</strong>. Ningependa<br />

kufafanua kwamba ingawa mwaka ulikuwa mgumu,<br />

usimamizi haukusitisha uzinduzi wa mipango muhimu<br />

ambayo endapo ingecheleweshwa ingehatarisha ushindani<br />

wa muda mrefu wa Kampuni. Kwa sababu hiyo, Kampuni<br />

sasa inatoa huduma za mawasiliano ya mtandao ya moja kwa<br />

moja kwa wageni wake katika hoteli zake. Mpango wa<br />

kuweka pamoja habari uko katika hatua za mwisho za<br />

uzinduzi baina ya afisi kuu mbili nchini Kenya na Tanzania<br />

ambao utasaidia kuafikia ulipiaji huduma/vyumba mapema<br />

na mifumo ya fedha na kupelekea kuwepo kwa utendaji bora<br />

wa kazi, usimamizi na uthibiti bora. Mwisho, ufanisi<br />

umepatikana kuhusiana na uuzaji wa biashara kupitia mfumo<br />

wa elektroniki ambapo hoteli za <strong>Serena</strong> zilianza kutumia<br />

mbinu hiyo mwezi Agosti mwaka <strong>2008</strong> huku kukiwa na<br />

mfumo wa utumaji maombi unaopatikana kupitia wavuti wa<br />

makundi yote ya hoteli yaliyoko mijini na fuo za bahari.<br />

Kundi linazidi kuamini kwamba wafanyakazi wake ni raslimali<br />

muhimu katika hazina ya biashara mambo yanapokuwa<br />

magumu. Licha ya changamoto za kibiashara, utuzaji wa<br />

wafanyakazi, utoaji mafunzo ya hali ya juu, uimarishaji wa<br />

uwezo ulibakia kuwa swala lililopewa kipaumbele. Wakati<br />

wa kipindi hiki cha mwaka, Kundi lilimwajiri Meneja wa<br />

Utoaji Mafunzo na Maendeleo ambaye kwa sasa anaendesha<br />

mkakati wa kuimarisha uzalishaji.<br />

Kama mnavyofahamu, wasafiri wa sasa wamejitolea<br />

kuhakikisha raslimali wanazotumia zinatoa mchango wao<br />

kuimarisha maendeleo miongoni mwake kupitia uhifadhi wa<br />

mifumo ya ikolojia na kuongoza katika ustawi bora wa utalii.<br />

Kundi linazidi kutekeleza wajibu wake katika jamii kwa<br />

kuhusisha pamoja shughuli hizo kwenye mkakati wake wa<br />

kibiashara. Kufikia sasa, shughuli za Kampuni katika wajibu<br />

wa jamii zinazidi kuangazia utalii wa ikolojia, uhifadhi wa<br />

mazingira, utoaji mafunzo, Afya ya Umma na maendeleo ya<br />

jamii. Mnamo mwezi Juni <strong>2008</strong>, <strong>TPS</strong>EA ilichapisha jarida lake<br />

la pili la wajibu wake kwa jamii linalojulikana kama <strong>Serena</strong><br />

Outreach to Society (SOS) ambalo linaangazia shughuli hizi.<br />

Kwa maelezo zaidi kuhusiana na wajibu wa Kampuni kwa<br />

jamii tafadhali rejelea ukurasa 20 na 21 wa ripoti hii.<br />

Kundi limebakia kuwa mchangiaji mkuu kwa hazina ya<br />

serikali za Kenya, Tanzania na Zanzibar. Kwa wastani Kundi<br />

lililipa kiwango sawa na Shilingi milioni 648 pesa za Kenya<br />

kwa ushuru wa moja kwa moja au usio wa moja kwa moja.<br />

Pia lilitoa Shilingi milioni 121 kwa mabaraza ya serikali za<br />

wilaya kama ada ya nia njema/ukodishaji katika miliki mbali<br />

mbali mwaka <strong>2008</strong>.<br />

Halmashauri na wasimamizi wanakadiria kuwepo kwa<br />

mazingira magumu ya biashara mwaka 2009 na athari za<br />

kushuka kwa uchumi wa dunia na kuzidi kuwepo kwa wasi<br />

wasi wa kifedha. Hali hii inatarajiwa kuchochewa na maswala<br />

mengine, masoko yasiyoaminika na kushuka kwa imani<br />

miongoni mwa wateja hali inayotarajia kuendelea kuathiri<br />

mahitaji ya utalii duniani kwa muda wa miezi 12 ijayo.<br />

Kama ilivyoshuhudiwa muhula wa kwanza wa mwaka 2009,<br />

kipindi cha mwaka kilichosalia kitazidi kukumbwa na<br />

changamoto ambazo zitaathiri gharama za uendeshaji<br />

biashara kutokana na ugumu wa maisha unaosababishwa na<br />

mfumuko wa bei, njaa iliyoko na gharama zilisizotarajiwa za<br />

kawi. Kwa sasa, majibu kutoka kwa waendeshaji wakuu wa<br />

biashara kuhusiana na maagizo ya vyumba katika vituo vyote<br />

vya mapumziko ni ya kutia shaka. Wasimamizi wametambua<br />

ukodishaji wa vyumba kwa muda mfupi siku za hivi karibuni.<br />

Hali hii ni ya kutia moyo.<br />

Chajio kando ya moto katika Hoteli ya Ngorongoro <strong>Serena</strong><br />

12 <strong>TPS</strong> EASTERN AFRICA LIMITED | ANNUAL REPORT AND FINANCIAL STATEMENTS <strong>2008</strong>

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!