You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
YA<br />
AL HABBIB SAYYEID
.<br />
NA<br />
Yamefasiriwa kwa Kiswahili na:<br />
<strong>Al</strong> habbib Sayyeid Umar Bin Sayyeid Abdallah<br />
(Mwinyi Baraka).<br />
First addition.<br />
03 Sept, 2005.<br />
28 Rajab, 1426. HR.<br />
i
MANAQIB YA AL-MAARUF<br />
Baada ya yote haya ni Manaqibu ya Walii Mkubwa kabisa<br />
aliyetajwa kwa jina hapo juu, yaliandikwa na mmoja katika<br />
makhalifa wake wakubwa Sayyid Ahmad bin Abdul Rahmani Ibn<br />
Sultan <strong>Al</strong>awi. Yalifasiriwa na <strong>Al</strong> <strong>Al</strong>lama Sayyid Kaab Ibn Sayyid<br />
Ahmad Zakiy <strong>Al</strong>-Masalah.<br />
Sasa inafasiriwa kwa Kiswahili na mtoto wa ndugu yake<br />
Walii huyo, Omar Abdallah Bin Sheikh Ahmad ambaye<br />
hujulikana kwa jina la Mwinyi Baraka.<br />
Huyu mfasiri kwa Kiswahili ameazimia dua zote aziache bila<br />
kufasiriwa kwani muhimu ni kulumiwa kama zilivyopokewa.<br />
ii.
MAISHA YAKE.<br />
Sasa naanzia:<br />
Utajo wa kuzaliwa kwake Mwenyi Ezi Mungu atakase siri<br />
yake Bwana <strong>Al</strong>-Maarufu alizaliwa mwaka Saf 1270 Hijra katika<br />
mtaa wa Bajanani, Moroni Ngazija.<br />
<strong>Al</strong>izaliwa katika nyumba iitwayo "Shashanyongo". Baba<br />
yake ndiye aliyemlea. <strong>Al</strong>isoma kuran Ngazija akawa anasoma<br />
kwa Tajwidi.<br />
Baadaye Baba yake alimpeleka Zanzibar si kwa<br />
jingine lolote ila kutafuta ilmu. <strong>Al</strong>ikaa Unguja kiasi ya miaka<br />
mine, takriban akazijua vilivyo fani za Tajwidi, Fiqih, Nahw na<br />
kiasi cha kutosha katika ilmu za hadithi na kuran. Ilmu zote hizi<br />
alizichukua kutokana na mjomba wake Sayyid <strong>Al</strong>i Bin Sultan<br />
Ahmad.<br />
Wakati wa safari yake, Babu yake upande wa mama<br />
yake Sultan Ahmad alimwambia; "Tutafutie ilmu ya haqiq<br />
(undani wa mambo yaliyohusiana na Uungu) kwani sisi hatujui<br />
vilivyo".<br />
Baada ya kusoma ilmu hizo alirejea Ngazija, akashughulika<br />
kukunjua ilmu zote hizi na kuita watu kwa Mwenyi Ezi Mungu<br />
katika msikiti wa Ijumaa. <strong>Al</strong>ianza kusomesha katika tafsiri ya<br />
kuran Jalalain katika wanafunzi wake waliosoma kwake fanni ni<br />
mwalimu wake wa Tajwidi Musa Bin Ahmad.<br />
Muhimu:<br />
Baba yake Sayyid, Mungu amuie Radhi ilikuwa<br />
hakupata mtoto mwanaume. Basi alipohiji akakusudia Madina<br />
kumzuru babu yake, Rehema ya Mwenyi Ezi Mungu na Amani<br />
yake ziwe juu yake, alimuomba Mwenyi Ezi Mungu katika Quba<br />
la mtume (SAW) amruzuku mtoto mwanaume kwa mke wake<br />
mlahirifu Mwana mkuu Bint Sultan Ahmad. <strong>Al</strong>iweka nadhiri<br />
hapo ikiwa Mwenyi Ezi Mungu kamruzuku mtoto mwanamme<br />
1.
atapeleka pesa kidogo kwenye kuba la Mtume (SAW) kwa<br />
matumizi ya watumikiao alipolala Mtume. Mwenyi Ezi Mungu<br />
alipokea dua yake. Baada ya kurejea Ngazijah, mkewe alishika<br />
mimba akamzaa anayeandikwa habari zake hapa. Baba yake<br />
alimwita MA'ARUF. Na akapeleka zile pesa Madina kutekeleza<br />
nadhiri yake.<br />
Nasabu yake tukufu yeye ni Bwana wangu (Mwenyi<br />
Ezi Mungu atakase siri yake kubwa), Muhammed Bin Sheikh<br />
Ahmad Bin Sayyid Abubakar Bin Sayyid Ahmad Bin Sayyid<br />
Abubakar Bin Sayyid Abdallah Bin Sayyid Salim Bin Sayyid<br />
Ahmad Bin Sayyid Abdallah Bin Sayyid <strong>Al</strong>i Bin <strong>Al</strong>fakhir Ash-<br />
Sheikh Abubakar Bin Salim, <strong>Al</strong>iyetawafu Einat katika<br />
Hadhramaut. Hii ni kwa upande wa Baba yake, na kwa puande<br />
wa Mama yake, yeye ni mtoto wa Mwana Mkuu Bint Sultan<br />
Seyyid Ahmad na yeye ana nasibika na Abubakar Bin Salim.<br />
Ama mabibi zake wataharifu, mama yake baba yake Wamwinyi<br />
Bint Sayyid Eidarus anaye jukuliwa na Abubakar Bin Salim na<br />
mama yake ni Sayyidat Khadija Bin Sheikh Salim; na yeye vile<br />
vile anajukuliwa na Abubakar Bin Salim. Basi imejulikana kuwa<br />
nasabu yake amezungukwa na Sheikh Abubakar Bin Salim<br />
upande wa mabababa na upande wa mamama Mwenyi Ezi<br />
Mungu atunufaishe na yeye na wazee wake Amin.<br />
Wake zake watahilifu na utajo wa kubariki baba yake. Mke<br />
wake wa mwanzo ni mtoto wa ndugu yake mama yake Sayyidat<br />
Sittinaa Bint Sultan Sayyid Omar Bin Sayyid Hassan katika<br />
kabila ya <strong>Al</strong>masaiha BA-ALAWI ambaye baba yake ndie<br />
aliemposea na akamuoza baba yake mkewe Sultan Sayyid Omar<br />
alietajwa hapo juu kwa mahari ya wanawake mfano wake aliingia<br />
nyumbani hapo Moroni. Siku ya Tisa tangu kuingia nyumbani<br />
baba yake alifariki (Faida; Ijumaa ya mwanzo baada ya kuingia<br />
nyumbani Sayyidina Muhammed Bin Sheikh alimtuma mtu<br />
akamtakie Jokho kwa baba yake ili avae kwenda kuhudhuria sala.<br />
Sheikh Ahmad alimjibu "Mwambie mwanangu asubiri kwani<br />
Jokho hilo litakuwa lake baada ya siku chache. Siku hizo hizo<br />
mzee akafariki.- Nyongeza hii ni ya Mfasiri).<br />
Bibi huyu yaani Sayyidat Sittinaa alizaa nae watoto watatu<br />
Khadija, Hawdhat na Shama. Baadaye alimuoa Maryam Bint<br />
Beja, akazaa naye Sayyid Ahmad. Tena alimuoa Bint Sayyid<br />
Aqil na mwishoni kwa Ngazijah alimuoa bibi Halimah Bint Ilyas.<br />
2.
Unguja alimuoa Bibi Khadijah Bint <strong>Al</strong>i aliezaliwa Ngazija na<br />
mama yake ni Mngazija alizaa naye Sayyid <strong>Al</strong>i na Sayyidat<br />
Batul. Baadaye alimuoa Bint Naqib Assayf <strong>Al</strong>-Kisadi akazaa<br />
naye Sayyidat Sharifah na Ismail ambaye alikufa mtoto hata baba<br />
yake hakuwahi kumuona ama Sharifah alikufa baada ya kufariki<br />
baba yake.<br />
Safari zake:<br />
Mwanzo alikwenda Unguja kutafuta elimu kama<br />
ilivyotajwa kabla katika safari zake. (Mwenyi Ezi Mungu amuilie<br />
radhi na amwidhishe). Ni safari ya Makka tukufu alikwenda<br />
kuhiji pamoja na mama yake na ukhti yake Sayyidat <strong>Al</strong>awiyya na<br />
waliyofuatana nae alipokuwa Makka alikutana na mmoja katika<br />
Mawalii wakubwa akawa humtukuza akamuusia achukue Tarika<br />
ya AL IMAM ASH-SHADHIL akampa khabari kuwa<br />
kufunguliwa kwake kumo katika Tarika hiyo mambo yakawa<br />
kama alivyomkhubiria Walii huyo, katika baadhi ya mikusanyiko<br />
yake na Walii huyo huyu Walii alimuuliza "Umekuja kwa sababu<br />
ya yule mgonjwa wa akili ambaye anazunguka Ngazija?" Na<br />
ilikuwa niya ya As-Sayyid ni kumuombea dua, yule walii<br />
alimkashif. Jawabu yake ilikuwa: "Naam". Akamjibu keshapona.<br />
<strong>Al</strong>iporejea kamkuta kweli keshapona kama alivyomwombea,<br />
Mwenyi Ezi Mungu atanufaishe kwa siri zao. Katika safari hii<br />
alikusudia Madina iliyojazwa Nuru ili kumzuru babu yake<br />
(S.A.W) huko alipokea vilitokea kwa Mungu kuletewa mbele ya<br />
Muhammed. <strong>Al</strong>ikaa Madina siku kadha wa kadha katika baadhi<br />
ya ziara zake ndani ya Kuba la Mtume takatifu aliingia yeye na<br />
mama yake. Mama yake aliona ndani ya Kuba Mtu anapendeza,<br />
mzuri, anatabasam. Mama yake alimuuliza mtoto wake "Nani<br />
huyu? As-Sayyid <strong>Al</strong>imuashiria mama yake anyamaze. Walipo<br />
rejea huko walikoshukia alimwambia mamake "Yule mtu<br />
uliyemuona ni Mtume (S.A.W) mwenyewe kwani mahali pale<br />
haingii mtu.<br />
<strong>Al</strong>ipomaliza ibada zake za hija na ziara aliingia Anzwani<br />
pamoja na mama yake na ukhti yake wakakaa huko siku kadha<br />
wa kadha yeye ndie wa mwanzo kuwapelekea Maulid ya<br />
Barzanji alikuwa anapenda kuyasoma na kuyahudhuria kwa<br />
taadhim na heshima kubwa alikuwa akikataza kucheka na<br />
kucheza na kutafuna tambuu wakati wa kuyasoma kwa<br />
kumuadhimisha mjumbe wa Mwenyi Ezi Mungu (S.A.W).<br />
Baada ya hapo alirejea kwenye watani wake hali ya kuwa ni<br />
3
mwenye kutizamwa kwa jicho la kusaidiwa na kutengenezewa<br />
kutokana na bwana Muumbaji khalafu alisafiri kwenda Zanzibar<br />
akakutana na Sheikh Uways na akachukua Tarika ya Qadiria<br />
kutokana naye akarejea Ngazija baadaye akenda Nzwani wakati<br />
huo anadhikri kwa Tarika ya Qadiriya wala hakumpa yeyote Ijaza<br />
ya Tarika hiyo, bali baadhi ya nyakati alikuwa hujitenga faragha<br />
akadhikiri peke yake baadae hurejea kwa wapenzi wake.<br />
<strong>Al</strong>iporejea Ngazija haikuchukua muda mrefu ila alifika<br />
Sheikh Abdallah Darwesh alikuwa kafuatana na ndugu yake<br />
Sayyid Abdal Rahman Bin Sheikh na mama yake Sayyidat<br />
Mwana Mkuu wakaja katika jahazi moja.<br />
Sayyid alikutana na Sheikh Abdallah Darwesh alie<br />
mchukulia amana na pakapatikana baina yao mahaba kwa<br />
mtizamano wa mwanzo.<br />
Hayo yalitokea kwa hekima ya Mwenye Ezi Mungu<br />
aliyeumba akatengeneza kila jambo na vipawa vya kukusudiwa.<br />
Sheikh Abdallah alitelemka kwenye kisiwa cha Ngazija<br />
akaingia katika vingi katika vijiji vyake. <strong>Al</strong>ipokuwa anazunguka<br />
katika vijiji hivyo aliona katika baadhi ya njia zake ndege wawili,<br />
mmoja akatoa ubait huu:<br />
شرتث شراب السر مه خمر الصفاء<br />
Wapili nae akatoa ubait huu:<br />
فسكرت لو حقا ومالي منا زعا<br />
Sheikh akaongeza juu ya ubait huu Abyat nyingine kama ilivyo<br />
katika kasida ijulikanayo Ubait wa mwanzo wa qasida hiyo ni:<br />
سقاء في سعاىاالحثية فلم ارى<br />
سواه علي اال طالقا فىاكون المع<br />
mpaka mwisho.<br />
Baadae Sheikh Abdallah alifanya makazi mahali alipozaliwa.<br />
Itsandaa mjini (Huko ndiko alipozaliwa mrithi wa Ahwal za<br />
Mawalii na Maqamat yao Seyyidna <strong>Al</strong>-Habib Omar Bin Ahmad<br />
Bin Sumeit رضوان هللا عايو na baba yake alizaliwa huko huko,<br />
babu yake <strong>Al</strong>-Habib Abubakar ndiye aliyetoka Shibam<br />
Hadhramaut kuja Ngazija- Mfasiri).<br />
Huko kwao Itsandaa Sheikh Abdallah alifungua chuo<br />
cha kusomesha watoto kur-an tukufu na baadhi ya vyuo vidogo<br />
vidogo. Baadhi ya watoto walikua wakikhitimu kuran takatifu<br />
kwa muda wa chini ya miezi sita kwa baraka zake hata wengi<br />
4
katika watu wa Moroni waliwapeleka watoto wao ili<br />
awasomeshe vile vile alifungua Daira ya Dhikri huko aliwapa<br />
watu ijaza katika Tarika ya Shadhili – Yashrutii khabari ilifika<br />
Moroni Bwana wangu (anakusudia <strong>Al</strong> Ma`aruf ) akakusudia<br />
Itsandaa kwa kutaka Ijaza akapewa Ijaza na Ukhalifa katika<br />
Tarika Shadhiliyya Yashrutyya. Sanad yake katika Tarika<br />
(NjiaTarika iliyomfikilia kutokana na Mtume (S.A.W) <strong>Al</strong>ichukua<br />
Tarika kutokana na Abu Saith Arif Billah (amjuaye Mungu)<br />
Sheikh Abdallah Bin Said ajulikanae kwa jina la Darwesh yeye<br />
huyu akapokea kutokana na Ustadh mkamilifu kabisa Sayyid <strong>Al</strong>i<br />
<strong>Al</strong>-Yashruti (Bwana huyu alitoka Afrika ya kaskazini akaja Akka<br />
katika Flastin akafanya makazi Sheikh Abdalllah Darweshi katika<br />
mzunguko wake kumtafuta Khutbu <strong>Al</strong> –Ghawth alifika huka<br />
Akka, akakaa chini na Sayyidina <strong>Al</strong>i <strong>Al</strong>-Yashruti kwa miaka hata<br />
akapata <strong>Al</strong> Fat-hu <strong>Al</strong> Akbar. Akapewa ruhusa arejee Ngazija<br />
kama wasita baina ya Sayyidina <strong>Al</strong>i na Sayyidina <strong>Al</strong> Ma`aruf,<br />
yeye Sheikh Abdallah Darwesh alipompa <strong>Al</strong> Ma`aruf amana yake<br />
alimwambia “Hii kazi yenu nyinyi Ahl- Bait Rasulillah. Mfasiri).<br />
Yeye Sayyidina <strong>Al</strong>i <strong>Al</strong>-Yashruti alipokea kwa khutbu wa zama<br />
zake As Sayyid Muhammed Bin Hamza Dhafir <strong>Al</strong>-Madani<br />
kutokana na Sharif <strong>Al</strong> Husainy baba yake Ahmad <strong>Al</strong> Arab<br />
Addarqawi kutokana na <strong>Al</strong>i <strong>Al</strong>-Imran kutokana na <strong>Al</strong> Arab Bin<br />
Ahmad Bin Abdallah kutokana na baba yake Ahmad Bin<br />
Abdallah kutokana na Qassim <strong>Al</strong> Khassas kutokana na Abdul<br />
Rahman <strong>Al</strong> fasi kutokana na Muhammed Bin Abdallah <strong>Al</strong> Kabir<br />
baba yake Sayyidina Ahmad na wao wote wawili kutokana na<br />
Yusuf <strong>Al</strong> Fasi kutokana na Abdul Rahman <strong>Al</strong> Majdhub kutokana<br />
na <strong>Al</strong>i As-Sanhaji, kutokana na Ahmad Zarruq (Bwan huyu ni<br />
katika nguzo kubwa kabisa za Silsila hii alikusanya kila namna za<br />
elimu hata Falsafa, Mantiq (Logic) Sayansi na Mathematic.<br />
Kasema maneno makubwa makubwa kama alivyosema Sultan <strong>Al</strong><br />
Awliyaa Seyyidina Abdul Qadir Jailan- Mfasiri)<br />
Zarruq alikuwa khalifa wa Ahmad Bin Uqba <strong>Al</strong><br />
Hadhrami bwana huyu alilelewa Tarim Hadharamawt na<br />
Seyyidna Abdallah Bin Abubakar <strong>Al</strong>-Aidarus akafikilia daraja<br />
kuwa katika Uwalii Mwenyi Enzi Mungu akamchagua awe<br />
mmoja katika Mqutbu wa Silsila hii ya Shadhili akampeleka<br />
Misri akalazimiya na Yahya <strong>Al</strong>-Qadiri alipofariki huyo alirithiwa<br />
na <strong>Al</strong> Hadhrami –Mfasiri).<br />
5.
Yahya <strong>Al</strong>-Qadiria alipokea <strong>Al</strong>i Wafaa na yeye aliwapokea<br />
kutokana na baba yake Bahr Safa kutokana na Daud <strong>Al</strong>-Bakhili<br />
kutokana na Ahmad Bin Attaillah Assakandari kutokana Abi <strong>Al</strong>-<br />
Abbas <strong>Al</strong> Mursi (Huyu kaitwa <strong>Al</strong> Mursi kwa sababu alizaliwa<br />
Mercia, Spain wakati Spain ilikuwa ya kiislam baada ya waislamu<br />
kukaa huko kwa miaka wakatia misingi ya kila namna ya masomo<br />
na ustaarab huko ulaya. <strong>Al</strong>-Mursi alikuwa anakwenda kuhiji Jahazi<br />
ilivunjika wakazama watu wote akaokotwa hapo alipokuwa Qutba<br />
mkubwa kabisa Sayyidina Abdul Hassan Ash-Shadhili alimlazimu<br />
bwana huyu hata akawa yeye ndiye khalifa wake mkubwa kabisa -<br />
Mfasiri).<br />
Seyyidina <strong>Al</strong>-Imam Abdul Hassan alimrithi Abdu<br />
Ssalaam Bin Mashish na yeye alipokea kwa Abdulrahman <strong>Al</strong><br />
Madani Azzayyat kutokana na Taqiyyuddin <strong>Al</strong> Fuqayyir kutokana<br />
na <strong>Al</strong> Qutb Fakhruddin kutokana na Qutb Nuruddin Abdul Hassan<br />
kutokana na <strong>Al</strong> Qutb Tajuddin kutokana <strong>Al</strong> Qutb Shamsuddin<br />
Assiwasi kutokana na <strong>Al</strong> Qutb Zainuddin <strong>Al</strong> Qazwimi kutokana na<br />
<strong>Al</strong> Qutb Abi Is-Haq Ibrahim <strong>Al</strong>i Bisry kutokana na <strong>Al</strong> Qutb Abu<br />
Qassim Ahmad <strong>Al</strong> Marwany kutokana na Qutb Abu Muhammed<br />
Said kutokana na <strong>Al</strong> Qutb Saad kutokana na <strong>Al</strong> Qutb Fathu Suud<br />
kutokana na <strong>Al</strong> Qutb Said <strong>Al</strong> Qazzani kutokana na <strong>Al</strong> Qutb Abi<br />
Muhammed Jabir kutokana na Qutb wa mwanzo Sayyiduna <strong>Al</strong><br />
Hassan kutokana na baba yake Sayyidina <strong>Al</strong>i Bin Abi Twalib na<br />
yeye kapokea kwa Bwana wa mwanzo na wa mwisho Bwana wetu<br />
Muhammed S.A.W. Hapa Silsila imemalizika.<br />
Sheikh Abdallah alimwambia <strong>Al</strong> Maaruf "Chukueni kazi<br />
yenu hii nyinyi Ahl Bait Rasulillah. Sisi ni watumishi wenu katika<br />
kazi hii".<br />
<strong>Al</strong> Maaruf alipopewa ukhalifa alirejea Moroni akasimamisha<br />
Daira na akawa anawapa watu Ijaza wakakusanyika kwake watu<br />
namna nyingi Sheikh Abdallah alikuwa huja Moroni na<br />
kuhudhuria Daira pamoja naye hata bwana wangu (Siri yake<br />
imetakaswa alimchukua Sheikh Abdallah nyumbani kwake ili<br />
awape Ijaza watu wa huko nyumbani Sheikh Abdallah akampa<br />
ijaza mama yake Assayid na ndugu zake wanawake Sayyidat<br />
<strong>Al</strong>awiyyah, Sayyidat Batul, Sayyidat Fatuma na Sayyidat Ihsan<br />
ndugu zake baba mmoja mama mmoja aliendelea Sheikh<br />
Abdallah kwenda Moroni na kurudi Itsandaa.<br />
6
Siku moja alipikiwa chakula Moroni, akasema: "Mwenye<br />
kula chakula hiki ataingia peponi, na mwenye kukila kwa nia<br />
yoyote atapata muradi wake". Akachukua kila mmoja katika<br />
walio kuwepo tonge tonge akawachukulia watu wa nyumbani.<br />
Palikuwa na mwanamke Tasa akala kwa nia Mwenyi Ezi Mungu<br />
ampe mtoto na Mungu akampa na hekaya hii inajulikana<br />
Ngazijah na imeenea kwenye watu wa huko.<br />
Baadaye alimpelekea Assayyid khabari asafiri<br />
aende Hinzwani Sayyid akamjibu kuwa, "hapana marikebu<br />
inayokwenda huko". Akamjibu "Andaeni safari kwani nyinyi<br />
mtasafiri kesho inshaallah". Wala hapakuwa merikebu pwani<br />
ilipokuja siku aliyowaambia kuwa safari yao itakuwa, alisikia<br />
mjini kuwa pamedhihiri jahazi ya matanga pwani lakini jahazi<br />
hiyo haikusogea mjini watu walitoka kuiangalia wakaikuta kama<br />
ilivyosemwa. Paliteremshwa Ngalawa kutoka Jahazini<br />
wakateremka baadhi ya waliokuwa na katika wao alikuwa<br />
mwenye Jahazi, Muhammed Bin Silim yeye alikua ana mke na<br />
marafiki Moroni ilipita kuwazuru tu. Assayyid alimuuliza<br />
mnaendea wapi? " akajibu Muwali" akasema "Sisi tunataka<br />
kusafiri pamoja na nyinyi" Jawabu ilikuwa kwa mapenzi na<br />
Ukarim akasafiri siku hiyo pamoja na Sheikh Abdallah <strong>Al</strong>i fundi<br />
na Ahmad Bin Nakhodha hata wakafika Muwali wakateremka<br />
baadae walisafiri kwenda Hinzwani katika Jahazi nyingineyo<br />
wakateremka Bamoni wakapita njia ya barabara hata wakifika<br />
Mtsamudu. Siku hiyo ilikuwa Ijumaa Mwezi 24 mfungo Tisa<br />
mwaka 1299 Hijriyya walipofika hapo alikutana na Ssayyid<br />
Ahmad <strong>Al</strong>-Kabir Muhammed <strong>Al</strong> Arab na Muhammed Abood na<br />
Abdu-Rab na wote wakawa katika Muridi wa Kishadhili.<br />
Baadaye Sayyid alijiweka kuwapa Ijaza kila alietaka wakachukua<br />
Ijaza kutokana naye watu namna nyingi, alikuwa husimamisha<br />
Daira msikiti wa Ijumaa kila usiku baada ya sala ya Isha. Watu<br />
wa msikitini walimwambia: "Ungeligura ukenda mahali pengine<br />
ingelikuwa bora kwani sisi tunashawishika ikisimamishwa Daira<br />
hapa na sisi tuna nyiradi hatuwezi kuzisoma". Kwa hiyo alihamia<br />
Masjid Ar-rhmani hakuwa akisimamisha Daira msikiti wa<br />
Ijumaa ila baada ya sala ya Ijumaa na sikukuu zote mbili.<br />
Baadae alielekea Wani ili kutoa Ijaza akakaa huko kiasi ya<br />
wiki walichukua Ijaza kwake aghlabu ya watu wa huko akampa<br />
Sheikh Muhammed Bin Abubakar Ukhalifa juu yao.<br />
7
<strong>Al</strong>irejea tena Mtsamudu, lakini hakukaa hapo mda mrefu<br />
akatakiwa kwenda Bombo akaenda pamoja na baadhi ya Muridi,<br />
akakaa huko siku kadha wa kadha aliwapa Ijaza huko watu wengi<br />
akafanya khalifa juu yao Sayyid Jaafar baadae alirejea Mtsamudu<br />
akadumu katika Masjid Ar hmani katika kumtaja Rabbu wake.<br />
Hakuwa akienda msikiti wa Ijumaa ila siku ya Ijumaa.<br />
Kupingwa na Sheikh Fadhil na Jawabu ya Sayyid na<br />
yaliyopita baina yao kwa ufupi.<br />
(Mungu awalie Radhi wote wawili na atunufaishe kwa wote)<br />
katika muda huu Sheikh Fadhili alimpinga Sayyid katika<br />
kuwapa Ijaza ya Tarika watu wa Hunzuwani pamoja na kuwa<br />
wao si Ahli kama alivyodai yeye hali ya kutoa Dalili kwa hadithi<br />
"Msiwape hekima wasiostahiki msije mkadhulumu" na katika<br />
hadithi nyingine au utimilifu wa hii au hadith khutba na mimi<br />
ndie Mufti wa Sawahil yote tangu Ras hafun mpaka Ras torfi na<br />
mimi nimezuia dhikri juu yenu au kuisoma mbele yangu. Seyyid<br />
alisimama akasema "Huna njia ya kuzuia dhikri", wakati huo<br />
zogo lilizuka kwa wingi msikitini watu walisimama na kelele<br />
zikaja juu. Kila mmoja akakamata silaha yake, Sayyid nae<br />
alinyanyua upanga wake Sayyid Abdallah Bin Sheikh alitoa nje<br />
upanga wake Sayyid Abdallah Bin Omar Khajar lake akelekea<br />
kwa Sayyid Abdallah Bin Omar aliyeitwa Abood Bin<br />
Muhammad Bin Omar, mtoto wa nduguye Abdallah Bin Omar ni<br />
katika Muridi wa Sayyid. Hapo hapo alimpiga kofi Ami yake<br />
kwa sababu ya wivu juu ya Sheikh wake hivi ndo anavyokuwa<br />
Muridi. Sultan Abdallah alikuwapo msikitini askari wake<br />
wakamzunguka Sayyid akatoka nje ya msikiti akanadi anaetaka<br />
Ijaza na ahudhurie wakahudhuria mbele yake wengi na yeye<br />
pamoja waliokua pamoja naye wanataka jina la Mwenyi Ezi<br />
Mungu. Baadae alitoa sauti akatoa nje upanga wake mbele ya<br />
Sultan Abdallah. Askari walipoona upanga walikimbia, Sayyid<br />
alimshika Sultan mkono akamwambia: "Sema <strong>Al</strong>lah" akawa<br />
anasema pamoja naye wakafuatana nyumbani na waliokuwapo<br />
waliwafuata na wote wanataja jina tukufu mpaka Sultan akaingia<br />
nyumbani kwake.<br />
Assayyid alielekea Mirontsi na kikundi katika Muridi wake<br />
walimfuata lakini hawakufika pamoja naye kwenye msikiti wa<br />
8.
Mironts ila watu kumi katika hao ni nduguye Sayyid <strong>Al</strong>i.<br />
Hapakupita ila dakika chache mara ukawafikia mwito<br />
kutokana na askari wa Sultan Abdallah, waliokuwa<br />
wamemzunguka wakamwambia amnilikie Sultan, yeye akajibu<br />
" Ndivyo" .<strong>Al</strong>ipotoka Msikitini wale askari walitaka kuchukua<br />
upanga wake na yeye akajizuia. Nduguye Sayyid <strong>Al</strong>i<br />
akamwambia: "Hii ni amri ya Sultan anahitajia tuitii". Hapo<br />
akawapa upanga baadae alichukuliwa pamoja na aliokua nao<br />
kutoka Morots na huko wanapigwa na kutolewa maneno na<br />
msukumo mkubwa hata mwisho Sayyid alitupwa baharini<br />
akatupiwa mawe. Baharini palikuwa Jahazi ya baadhi ya wahindi<br />
Sayyid alipanda akabaki humo siku saba baadae akasafiri pamoja<br />
nao mpaka Nusbee.<br />
Ijumaa ya mwanzo baada ya vituko hivyo walikuja<br />
watu wake kutoka Bambao na katika hao ni Sayyid Jaafar na<br />
Sayyid Salim Bin Sultan Abdallah wakamkuta kesha safiri<br />
wakahudhuria Sala na wakasimamisha Daira. Waliapa kuwa<br />
ataewaingilia watamuuwa. Hapana aliewaingilia., Daira ilidumu<br />
kama ilivyokuwa katika Masjid Ar rahmani kila Ijumaa na<br />
sikukuu mbili ilikuwa ikisimamishwa Msikiti wa Ijumaa.<br />
Sayyid alirejea kutoka Nusbee akateremka Maote<br />
alimuamrisha Sayyid Ahmad Bin Abdulrahman na Abood Bin<br />
Muhammad warejee Hinzwan na yeye mwenyewe alielekea<br />
Ngazijah pamoja na nduguye Sayyid <strong>Al</strong>i na Muhammad <strong>Al</strong> arab.<br />
<strong>Al</strong>ipofika Ngazijah alipokelewa na Sheikh Abdallah Darwesh na<br />
alikuwa pamoja nae kwa namna iliokuwa njema kabisa kuliko<br />
walivyopata kuwa.<br />
Baadae alimpeleka nduguye Hinzwani ili afanye<br />
upya mfungano wao na Tarika akampa Ijaza. Yeye alikaa<br />
Hinzwani miezi. Siku yane na ya tano ya kufika kwake Hinzwani<br />
alifariki Sheikh Fadhil ( Mungu amrehemu). (Sayyid alitoa amri<br />
asomewe wadhifa aombewe dua. Haya yanaonyesha kuwa Sheikh<br />
Fadhil hakumpinga Sayyid kwa inadi bali jitihada. <strong>Al</strong>ijitahidi<br />
akakosana, na Sayyid akamuombea Dua aghufuriwe - Mfasiri)<br />
Sayyid <strong>Al</strong>i alirejea Ngazija akamkuta Sheikh Abdallah<br />
Darwesh kasafiri kwenda Zanzibar baada ya kufariki Sayyidat<br />
<strong>Al</strong>awiyya. Bibi huyo alikuwa na cheo kikubwa kwa Bwana ambae<br />
maisha yake yanaandikwa. Hapa mauti yalipomhudhuria alikuwa<br />
anataja jina tukufu la Mwenyi Ezi Mungu. Sayyid alimwambia:<br />
"Msalie Mtume" Bibi alijibu "Huyu hapa Mjumbe<br />
9
wa Mwenyi Ezi Mungu ananiamrisha nitaje Ismul-Jalala".<br />
Sayyidat <strong>Al</strong>awiyya huyu ndiye ambaye Sheikh Abdallah<br />
Darwesh alisema katika kumtaja kumpa cheo chake:<br />
"Wangegawika Muridi mimi ningekuwa pamoja na kikundi<br />
alichomo Sayyidati <strong>Al</strong>awiyya".<br />
Katika siku hizo alikwenda Sayyid kwenye Bustani ya<br />
mama yake ijulikanayo kwa jina la Buzini akakaa huko siku<br />
nyingi awemo ndani ya Khalwa (Muepukano na kila kitu kwa<br />
kushughulika na Mwenyi Ezi Mungu) Hapo ilimjilia kwa daraja<br />
kubwa hali wapatao Mawalii wakubwa ilirejea nayo Mironi<br />
akaingia nyumbani kwa Sheikh Abdallah Bin Himid, akabaki<br />
pamoja naye huko siku tatu bila ya kuingia huko nyumba yoyote.<br />
Baada ya hapo alitoka Sheikh Abdallah Bin Himid<br />
na Sayyid akapanda juu ya sakafu ya nyumba akafika ukingoni<br />
akaanguka, nduguye Sayyid alimchukua mpaka nyumbani kwa<br />
mama yake akabaki nyumbani kiasi ya miezi sita na Ahwal zake<br />
zikizidi hatuwezi kukisia aliyoyapata katika yajayo kutoka na<br />
Mwenyi Ezi Mungu pamoja na yanayoteremka na miminio<br />
alipokuwa katika hali hiyo mara yumo ndani ya صحو mara<br />
nyingine محو pengine huwa عينةkatika na pengine katika<br />
(Maneno haya hayafasirika kwani ni Istilahi za Mabwana حضو ر<br />
Masufi. Hayana maana ya lugha wenyewe wanatambua kwa<br />
Dhawq. Kuyaonja na ekspiriense. - Mfasiri). <strong>Al</strong>iendelea hata<br />
akapata ambayo hatwezi kuyatambua vilivyo na tunahemewa na<br />
kudiriki hakika yake.<br />
Jadhba hii ni mash-hur Ngazija kwa Muridi wote. Yeye<br />
Sayyid alisema wakati katika Jadhba yake "Mimi ni kitu Azizi<br />
mimi ni kitu kilichotokana na Mtume (S.A.W) na ni hasha<br />
Mtume kumpa baba yangu kitu kidhalilifu". <strong>Al</strong>isema:<br />
(Mwenyi Ezi Mungu atunufaishe kwa baraka zake ) "Ingekuwa<br />
bahari ni wino na miti kalamu ili kudhibiti niliyoyaona<br />
bahari ingekwisha na miti ingemalizika kabla ya kumalizika<br />
mambo niliyoyaona katika Jadhba yangu hii".<br />
Baada ya hapo alirejea kukaa na watu kama ada yake ya<br />
mwanzo akasafiri kwenda Hinzwani akateremka Mtsamudu.<br />
Sultan Abdallah alikuwa Bambao alimtaka Sayyid aende huko na<br />
yeye akenda pamoja na baadhi ya Muridi. Sultan Abdallah<br />
akampokea kwa taadhima na mtukuzo, na yeye alikuwa<br />
akijihisabu kuwa ni katika jumla ya Muridu. Katika baadhi ya<br />
10.
siku alimwonyesha mkono Sayyid kwa kutaka kumpa<br />
mapesa. Sayyid alisema: "Nimepokea zawadi yako, lakini<br />
sasa sina haja ya kitu basi kaa nayo mpaka wakati wa haja".<br />
Baadae alifika Sheikh Abdallah bin Himid kutoka<br />
Ngazija akakutana na Sayyid akampa khabari ya kifo cha<br />
Sayyidat Fatuma Bint Sheikh Ahmad. Ukhti yake Sayyid<br />
baba mmoja mama mmoja, alimuomba arejee Ngazija.<br />
akakubali akasafiri pamoja. Hii ndio safari ya mwisho ya<br />
Hinzwani hakurejea tena.<br />
Baada ya kufika Ngazija, watu wa huko walikhtalifiana<br />
na mfalme wao Sultan Sayyid <strong>Al</strong>i Bin Sultan Sayyid Omar<br />
<strong>Al</strong>-Masily walimtaka Sayyid awe pamoja nao na<br />
walimkhubiri kuwa watamuuzulu Sayyid <strong>Al</strong>i. Wakati huo<br />
ada ilikurubia kutoa kabisa hukumu za sheria iliyo<br />
tahirishwa jambo ambalo haridhii nalo Mwenyi Ezi Mungu<br />
na Mjumbe wake. Sayyid mara nyingi alikuwa akiyataja<br />
lakini hakumpata wa kunusuru sheria kwa hiyo alipotakiwa<br />
awe pamoja na alietaka kumuuzulu Sultan Sayyid <strong>Al</strong>i,<br />
waliomtaka walimpa miadi madhubuti kuwa watabatilisha<br />
ada yenye kwenda kinyume na sheria, watasimamisha<br />
sheria imara. <strong>Al</strong>iwakubalia na ikawa sababu kubwa ya<br />
kusalimika Sulatn Sayyid <strong>Al</strong>i nafsi yake kwani wale<br />
waliotaka kumuuzulu, walikusudia kumuua, lakini Sayyid<br />
hakuwaachia bali alibaki anawarairai na anawachukua kwa<br />
upole na kuwalainishia maneno kwa kumuonea huruma<br />
mtoto wa ndugu mama yake (Hakika ya mambo alihisi<br />
kuwa kisharia hakustahiki kuuliwa. Ingelikuwa sii hivyo<br />
angeliwaachia wakamuua kwani yeye ni wa mbele katika<br />
ambao hawatizami mhusiano mbele ya sheria ya Mungu -<br />
Mfasiri).<br />
Azma ya kumuuzulu iliposhika nguvu walimuamrisha<br />
khatibu asimtaje katika khutba ya <strong>Al</strong>jumua na yeye alukhutubu<br />
pasina kumuombea dua, ilipothibiti kwa Sultan Sayyid <strong>Al</strong>i kuwa<br />
waliloliazimia na jambo la matatizo alisafiri kwa kujificha mpaka<br />
Muali, na kutoka huko mpaka Maote akaifikishia dolla ya<br />
kifaransa yaliyomfika. Dola ya kifaransa iliandalia marikebo<br />
ikachukua idadi ya askari marekebo iliingia Ngazija ikateremsha<br />
11.
askari ambao walitafuta baadhi ya watu wajulikanao<br />
wakawachukua baadhi yao. Walimtafuta As-Sayyid lakini yeye<br />
alijificha hawakuweza kutambua alipokuwa. Mitsamhuli<br />
ilikuwapo jahazi inakwenda Zanzibar, Sayyid alipanda usiku<br />
wakati ambao wanaomtafuta wameghafilika walipokuwa<br />
hawakumpataSayyid, nchi kavu wazungu walipanda kwenye<br />
jahazi ili watizame ikiwa hajajificha humo jahazini. Walipoingia<br />
jahazini wakaanza kupekua, palivuma upepo mkali na mawimbi<br />
yakachafuka, hapo hapo waliteremka bila ya kumuona, "Na wapi<br />
jicho pofu litaona jua?" wakati huo mnyororo uliofungiwa jahazi<br />
na nanga ulikatika na Jahazi ikaingia baharini matanga<br />
yakapandishwa na jahazi ikatweka kuelekea Zanzibar.<br />
Imewachukua Sayyid na Muridi wake wawili Ahmad<br />
Nakhodha na Abdul-R-rabb jahazi ilipokuwa mbali na nchi kavu<br />
Sayyid alisimama juu ya sitaha akababaika mmoja katika muridi<br />
wake akasema: "Eeh bwana wangu, umejitokeza watu watakuua<br />
iwe sababu ya sisi kuangamia", akajibu "Usihuzunike na sisi kwa<br />
kupenda Mwenyi Ezi Mungu baada ya salat aljumaa tutaingia<br />
Zanzibar. Safari yake ilikuwa jioni ya jumanne. Ikatokea vile vile<br />
kama alivyosema kwani waliingia Zanzibar baada ya salat<br />
aljumaa.<br />
<strong>Al</strong>iishi Sayyid Unguja hata mpaka alipotolewa Sultan<br />
Sayyid <strong>Al</strong>i Ngazija Dola ya kifaransa ndio iliyomtoa. Hapo<br />
alirejea Ngazija na hakusafiri kamwe. Hakuondoka huko hata<br />
Mwenyi Ezi Mungu akamchukua hali ya kuwa yeye Sayyid<br />
karidhia na karidhiwa.<br />
منا فيو رض هللا عنو<br />
12.
Mtoto wa <strong>Al</strong> habbib Sayyeid Muhammed <strong>Al</strong> Ma`aruf aliyezaliwa<br />
Zanzibar.<br />
13.
<strong>Al</strong> habbib Sayyeid Muhammed Bin Sayyeid <strong>Al</strong>liy <strong>Al</strong> Ma`aruf.<br />
15.
Mfasiri kwa Kiswahili mtoto wa ndugu yake Sayyeid <strong>Al</strong> Ma`aruf.<br />
<strong>Al</strong> habbib Nassib Sayyeid Umar Bin Sayyeid Abdallah<br />
Mwinyibaraka.<br />
17
Khalifa wa mwanzo wa Majaalis-el ulaa – Mwinyi Baraka-<br />
Uwesia – Qa-diriyya. <strong>Al</strong> <strong>Faqeer</strong> Sheikh Ahmad Bin Sheikh<br />
Muhammed Msiha.<br />
18
Vitabu vilivyokwishatoka ni:<br />
*1. Maana halisi ya Imaan. (i) (1 st , 2nd & 3rd addition).<br />
*2. Njia nyepesi ya kuijua nafsi yako.<br />
*3. Njia nyepesi ya kujua kitu juu ya uongofu.<br />
*4. Knowledge vision & ecstacy.<br />
*5. Mwinyi Baraka katika ulimwengu wa kiislamu.<br />
*6. Waislamu na Sayansi - Ulu-m.<br />
*7. Kuhifadhi Burda.<br />
*8. Maana halisi ya Imaan (ii).<br />
*9. Muhammad SAW katika ulimwengu wa ghayb.<br />
*10. Siri ya Balaa.<br />
*11. El makhlouq (Viumbe)<br />
*12. Njia nyepesi ya kujua juu ya uongofu. (2nd addition)<br />
*13. Manaqib ya <strong>Al</strong> habbib Sayyeid <strong>Al</strong> Ma`aruf.<br />
Vitabu ambavyo tunategemea kuvitoa muda si mrefu<br />
(Insha <strong>Al</strong>lah) ni:<br />
*1. Waislamu na Sayansi - Ulu-m. (2nd addition)<br />
*2. Njia nyepesi ya kuijua nafsi yako. (2nd addition).<br />
*3. Mwinyi Baraka katika ulimwengu wa kiislamu ( 2nd. add).<br />
*4. Njia nyepesi ya kujua kitu juu ya Uongofu.<br />
*5. Some aspects of concepts of facility in medevial Islamic<br />
Philosophy by Mwinyibaraka.<br />
Kwa maulizo kuhusu vitabu wasiliana nasi:<br />
Majaalis El Ulaa-MwinyiBaraka-Uwesia- El Qadiriyya Sinza,<br />
P.o. Box 15170,<br />
Tel: 0747483553<br />
Tel: 0748595958.<br />
Tel: 0744 023703.<br />
Tel: 0741 235091.<br />
Tel: 0744 299597.<br />
Dar es salaam.