17.02.2015 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

YA<br />

AL HABBIB SAYYEID


.<br />

NA<br />

Yamefasiriwa kwa Kiswahili na:<br />

<strong>Al</strong> habbib Sayyeid Umar Bin Sayyeid Abdallah<br />

(Mwinyi Baraka).<br />

First addition.<br />

03 Sept, 2005.<br />

28 Rajab, 1426. HR.<br />

i


MANAQIB YA AL-MAARUF<br />

Baada ya yote haya ni Manaqibu ya Walii Mkubwa kabisa<br />

aliyetajwa kwa jina hapo juu, yaliandikwa na mmoja katika<br />

makhalifa wake wakubwa Sayyid Ahmad bin Abdul Rahmani Ibn<br />

Sultan <strong>Al</strong>awi. Yalifasiriwa na <strong>Al</strong> <strong>Al</strong>lama Sayyid Kaab Ibn Sayyid<br />

Ahmad Zakiy <strong>Al</strong>-Masalah.<br />

Sasa inafasiriwa kwa Kiswahili na mtoto wa ndugu yake<br />

Walii huyo, Omar Abdallah Bin Sheikh Ahmad ambaye<br />

hujulikana kwa jina la Mwinyi Baraka.<br />

Huyu mfasiri kwa Kiswahili ameazimia dua zote aziache bila<br />

kufasiriwa kwani muhimu ni kulumiwa kama zilivyopokewa.<br />

ii.


MAISHA YAKE.<br />

Sasa naanzia:<br />

Utajo wa kuzaliwa kwake Mwenyi Ezi Mungu atakase siri<br />

yake Bwana <strong>Al</strong>-Maarufu alizaliwa mwaka Saf 1270 Hijra katika<br />

mtaa wa Bajanani, Moroni Ngazija.<br />

<strong>Al</strong>izaliwa katika nyumba iitwayo "Shashanyongo". Baba<br />

yake ndiye aliyemlea. <strong>Al</strong>isoma kuran Ngazija akawa anasoma<br />

kwa Tajwidi.<br />

Baadaye Baba yake alimpeleka Zanzibar si kwa<br />

jingine lolote ila kutafuta ilmu. <strong>Al</strong>ikaa Unguja kiasi ya miaka<br />

mine, takriban akazijua vilivyo fani za Tajwidi, Fiqih, Nahw na<br />

kiasi cha kutosha katika ilmu za hadithi na kuran. Ilmu zote hizi<br />

alizichukua kutokana na mjomba wake Sayyid <strong>Al</strong>i Bin Sultan<br />

Ahmad.<br />

Wakati wa safari yake, Babu yake upande wa mama<br />

yake Sultan Ahmad alimwambia; "Tutafutie ilmu ya haqiq<br />

(undani wa mambo yaliyohusiana na Uungu) kwani sisi hatujui<br />

vilivyo".<br />

Baada ya kusoma ilmu hizo alirejea Ngazija, akashughulika<br />

kukunjua ilmu zote hizi na kuita watu kwa Mwenyi Ezi Mungu<br />

katika msikiti wa Ijumaa. <strong>Al</strong>ianza kusomesha katika tafsiri ya<br />

kuran Jalalain katika wanafunzi wake waliosoma kwake fanni ni<br />

mwalimu wake wa Tajwidi Musa Bin Ahmad.<br />

Muhimu:<br />

Baba yake Sayyid, Mungu amuie Radhi ilikuwa<br />

hakupata mtoto mwanaume. Basi alipohiji akakusudia Madina<br />

kumzuru babu yake, Rehema ya Mwenyi Ezi Mungu na Amani<br />

yake ziwe juu yake, alimuomba Mwenyi Ezi Mungu katika Quba<br />

la mtume (SAW) amruzuku mtoto mwanaume kwa mke wake<br />

mlahirifu Mwana mkuu Bint Sultan Ahmad. <strong>Al</strong>iweka nadhiri<br />

hapo ikiwa Mwenyi Ezi Mungu kamruzuku mtoto mwanamme<br />

1.


atapeleka pesa kidogo kwenye kuba la Mtume (SAW) kwa<br />

matumizi ya watumikiao alipolala Mtume. Mwenyi Ezi Mungu<br />

alipokea dua yake. Baada ya kurejea Ngazijah, mkewe alishika<br />

mimba akamzaa anayeandikwa habari zake hapa. Baba yake<br />

alimwita MA'ARUF. Na akapeleka zile pesa Madina kutekeleza<br />

nadhiri yake.<br />

Nasabu yake tukufu yeye ni Bwana wangu (Mwenyi<br />

Ezi Mungu atakase siri yake kubwa), Muhammed Bin Sheikh<br />

Ahmad Bin Sayyid Abubakar Bin Sayyid Ahmad Bin Sayyid<br />

Abubakar Bin Sayyid Abdallah Bin Sayyid Salim Bin Sayyid<br />

Ahmad Bin Sayyid Abdallah Bin Sayyid <strong>Al</strong>i Bin <strong>Al</strong>fakhir Ash-<br />

Sheikh Abubakar Bin Salim, <strong>Al</strong>iyetawafu Einat katika<br />

Hadhramaut. Hii ni kwa upande wa Baba yake, na kwa puande<br />

wa Mama yake, yeye ni mtoto wa Mwana Mkuu Bint Sultan<br />

Seyyid Ahmad na yeye ana nasibika na Abubakar Bin Salim.<br />

Ama mabibi zake wataharifu, mama yake baba yake Wamwinyi<br />

Bint Sayyid Eidarus anaye jukuliwa na Abubakar Bin Salim na<br />

mama yake ni Sayyidat Khadija Bin Sheikh Salim; na yeye vile<br />

vile anajukuliwa na Abubakar Bin Salim. Basi imejulikana kuwa<br />

nasabu yake amezungukwa na Sheikh Abubakar Bin Salim<br />

upande wa mabababa na upande wa mamama Mwenyi Ezi<br />

Mungu atunufaishe na yeye na wazee wake Amin.<br />

Wake zake watahilifu na utajo wa kubariki baba yake. Mke<br />

wake wa mwanzo ni mtoto wa ndugu yake mama yake Sayyidat<br />

Sittinaa Bint Sultan Sayyid Omar Bin Sayyid Hassan katika<br />

kabila ya <strong>Al</strong>masaiha BA-ALAWI ambaye baba yake ndie<br />

aliemposea na akamuoza baba yake mkewe Sultan Sayyid Omar<br />

alietajwa hapo juu kwa mahari ya wanawake mfano wake aliingia<br />

nyumbani hapo Moroni. Siku ya Tisa tangu kuingia nyumbani<br />

baba yake alifariki (Faida; Ijumaa ya mwanzo baada ya kuingia<br />

nyumbani Sayyidina Muhammed Bin Sheikh alimtuma mtu<br />

akamtakie Jokho kwa baba yake ili avae kwenda kuhudhuria sala.<br />

Sheikh Ahmad alimjibu "Mwambie mwanangu asubiri kwani<br />

Jokho hilo litakuwa lake baada ya siku chache. Siku hizo hizo<br />

mzee akafariki.- Nyongeza hii ni ya Mfasiri).<br />

Bibi huyu yaani Sayyidat Sittinaa alizaa nae watoto watatu<br />

Khadija, Hawdhat na Shama. Baadaye alimuoa Maryam Bint<br />

Beja, akazaa naye Sayyid Ahmad. Tena alimuoa Bint Sayyid<br />

Aqil na mwishoni kwa Ngazijah alimuoa bibi Halimah Bint Ilyas.<br />

2.


Unguja alimuoa Bibi Khadijah Bint <strong>Al</strong>i aliezaliwa Ngazija na<br />

mama yake ni Mngazija alizaa naye Sayyid <strong>Al</strong>i na Sayyidat<br />

Batul. Baadaye alimuoa Bint Naqib Assayf <strong>Al</strong>-Kisadi akazaa<br />

naye Sayyidat Sharifah na Ismail ambaye alikufa mtoto hata baba<br />

yake hakuwahi kumuona ama Sharifah alikufa baada ya kufariki<br />

baba yake.<br />

Safari zake:<br />

Mwanzo alikwenda Unguja kutafuta elimu kama<br />

ilivyotajwa kabla katika safari zake. (Mwenyi Ezi Mungu amuilie<br />

radhi na amwidhishe). Ni safari ya Makka tukufu alikwenda<br />

kuhiji pamoja na mama yake na ukhti yake Sayyidat <strong>Al</strong>awiyya na<br />

waliyofuatana nae alipokuwa Makka alikutana na mmoja katika<br />

Mawalii wakubwa akawa humtukuza akamuusia achukue Tarika<br />

ya AL IMAM ASH-SHADHIL akampa khabari kuwa<br />

kufunguliwa kwake kumo katika Tarika hiyo mambo yakawa<br />

kama alivyomkhubiria Walii huyo, katika baadhi ya mikusanyiko<br />

yake na Walii huyo huyu Walii alimuuliza "Umekuja kwa sababu<br />

ya yule mgonjwa wa akili ambaye anazunguka Ngazija?" Na<br />

ilikuwa niya ya As-Sayyid ni kumuombea dua, yule walii<br />

alimkashif. Jawabu yake ilikuwa: "Naam". Akamjibu keshapona.<br />

<strong>Al</strong>iporejea kamkuta kweli keshapona kama alivyomwombea,<br />

Mwenyi Ezi Mungu atanufaishe kwa siri zao. Katika safari hii<br />

alikusudia Madina iliyojazwa Nuru ili kumzuru babu yake<br />

(S.A.W) huko alipokea vilitokea kwa Mungu kuletewa mbele ya<br />

Muhammed. <strong>Al</strong>ikaa Madina siku kadha wa kadha katika baadhi<br />

ya ziara zake ndani ya Kuba la Mtume takatifu aliingia yeye na<br />

mama yake. Mama yake aliona ndani ya Kuba Mtu anapendeza,<br />

mzuri, anatabasam. Mama yake alimuuliza mtoto wake "Nani<br />

huyu? As-Sayyid <strong>Al</strong>imuashiria mama yake anyamaze. Walipo<br />

rejea huko walikoshukia alimwambia mamake "Yule mtu<br />

uliyemuona ni Mtume (S.A.W) mwenyewe kwani mahali pale<br />

haingii mtu.<br />

<strong>Al</strong>ipomaliza ibada zake za hija na ziara aliingia Anzwani<br />

pamoja na mama yake na ukhti yake wakakaa huko siku kadha<br />

wa kadha yeye ndie wa mwanzo kuwapelekea Maulid ya<br />

Barzanji alikuwa anapenda kuyasoma na kuyahudhuria kwa<br />

taadhim na heshima kubwa alikuwa akikataza kucheka na<br />

kucheza na kutafuna tambuu wakati wa kuyasoma kwa<br />

kumuadhimisha mjumbe wa Mwenyi Ezi Mungu (S.A.W).<br />

Baada ya hapo alirejea kwenye watani wake hali ya kuwa ni<br />

3


mwenye kutizamwa kwa jicho la kusaidiwa na kutengenezewa<br />

kutokana na bwana Muumbaji khalafu alisafiri kwenda Zanzibar<br />

akakutana na Sheikh Uways na akachukua Tarika ya Qadiria<br />

kutokana naye akarejea Ngazija baadaye akenda Nzwani wakati<br />

huo anadhikri kwa Tarika ya Qadiriya wala hakumpa yeyote Ijaza<br />

ya Tarika hiyo, bali baadhi ya nyakati alikuwa hujitenga faragha<br />

akadhikiri peke yake baadae hurejea kwa wapenzi wake.<br />

<strong>Al</strong>iporejea Ngazija haikuchukua muda mrefu ila alifika<br />

Sheikh Abdallah Darwesh alikuwa kafuatana na ndugu yake<br />

Sayyid Abdal Rahman Bin Sheikh na mama yake Sayyidat<br />

Mwana Mkuu wakaja katika jahazi moja.<br />

Sayyid alikutana na Sheikh Abdallah Darwesh alie<br />

mchukulia amana na pakapatikana baina yao mahaba kwa<br />

mtizamano wa mwanzo.<br />

Hayo yalitokea kwa hekima ya Mwenye Ezi Mungu<br />

aliyeumba akatengeneza kila jambo na vipawa vya kukusudiwa.<br />

Sheikh Abdallah alitelemka kwenye kisiwa cha Ngazija<br />

akaingia katika vingi katika vijiji vyake. <strong>Al</strong>ipokuwa anazunguka<br />

katika vijiji hivyo aliona katika baadhi ya njia zake ndege wawili,<br />

mmoja akatoa ubait huu:<br />

شرتث شراب السر مه خمر الصفاء<br />

Wapili nae akatoa ubait huu:<br />

فسكرت لو حقا ومالي منا زعا<br />

Sheikh akaongeza juu ya ubait huu Abyat nyingine kama ilivyo<br />

katika kasida ijulikanayo Ubait wa mwanzo wa qasida hiyo ni:<br />

سقاء في سعاىاالحثية فلم ارى<br />

سواه علي اال طالقا فىاكون المع<br />

mpaka mwisho.<br />

Baadae Sheikh Abdallah alifanya makazi mahali alipozaliwa.<br />

Itsandaa mjini (Huko ndiko alipozaliwa mrithi wa Ahwal za<br />

Mawalii na Maqamat yao Seyyidna <strong>Al</strong>-Habib Omar Bin Ahmad<br />

Bin Sumeit رضوان هللا عايو na baba yake alizaliwa huko huko,<br />

babu yake <strong>Al</strong>-Habib Abubakar ndiye aliyetoka Shibam<br />

Hadhramaut kuja Ngazija- Mfasiri).<br />

Huko kwao Itsandaa Sheikh Abdallah alifungua chuo<br />

cha kusomesha watoto kur-an tukufu na baadhi ya vyuo vidogo<br />

vidogo. Baadhi ya watoto walikua wakikhitimu kuran takatifu<br />

kwa muda wa chini ya miezi sita kwa baraka zake hata wengi<br />

4


katika watu wa Moroni waliwapeleka watoto wao ili<br />

awasomeshe vile vile alifungua Daira ya Dhikri huko aliwapa<br />

watu ijaza katika Tarika ya Shadhili – Yashrutii khabari ilifika<br />

Moroni Bwana wangu (anakusudia <strong>Al</strong> Ma`aruf ) akakusudia<br />

Itsandaa kwa kutaka Ijaza akapewa Ijaza na Ukhalifa katika<br />

Tarika Shadhiliyya Yashrutyya. Sanad yake katika Tarika<br />

(NjiaTarika iliyomfikilia kutokana na Mtume (S.A.W) <strong>Al</strong>ichukua<br />

Tarika kutokana na Abu Saith Arif Billah (amjuaye Mungu)<br />

Sheikh Abdallah Bin Said ajulikanae kwa jina la Darwesh yeye<br />

huyu akapokea kutokana na Ustadh mkamilifu kabisa Sayyid <strong>Al</strong>i<br />

<strong>Al</strong>-Yashruti (Bwana huyu alitoka Afrika ya kaskazini akaja Akka<br />

katika Flastin akafanya makazi Sheikh Abdalllah Darweshi katika<br />

mzunguko wake kumtafuta Khutbu <strong>Al</strong> –Ghawth alifika huka<br />

Akka, akakaa chini na Sayyidina <strong>Al</strong>i <strong>Al</strong>-Yashruti kwa miaka hata<br />

akapata <strong>Al</strong> Fat-hu <strong>Al</strong> Akbar. Akapewa ruhusa arejee Ngazija<br />

kama wasita baina ya Sayyidina <strong>Al</strong>i na Sayyidina <strong>Al</strong> Ma`aruf,<br />

yeye Sheikh Abdallah Darwesh alipompa <strong>Al</strong> Ma`aruf amana yake<br />

alimwambia “Hii kazi yenu nyinyi Ahl- Bait Rasulillah. Mfasiri).<br />

Yeye Sayyidina <strong>Al</strong>i <strong>Al</strong>-Yashruti alipokea kwa khutbu wa zama<br />

zake As Sayyid Muhammed Bin Hamza Dhafir <strong>Al</strong>-Madani<br />

kutokana na Sharif <strong>Al</strong> Husainy baba yake Ahmad <strong>Al</strong> Arab<br />

Addarqawi kutokana na <strong>Al</strong>i <strong>Al</strong>-Imran kutokana na <strong>Al</strong> Arab Bin<br />

Ahmad Bin Abdallah kutokana na baba yake Ahmad Bin<br />

Abdallah kutokana na Qassim <strong>Al</strong> Khassas kutokana na Abdul<br />

Rahman <strong>Al</strong> fasi kutokana na Muhammed Bin Abdallah <strong>Al</strong> Kabir<br />

baba yake Sayyidina Ahmad na wao wote wawili kutokana na<br />

Yusuf <strong>Al</strong> Fasi kutokana na Abdul Rahman <strong>Al</strong> Majdhub kutokana<br />

na <strong>Al</strong>i As-Sanhaji, kutokana na Ahmad Zarruq (Bwan huyu ni<br />

katika nguzo kubwa kabisa za Silsila hii alikusanya kila namna za<br />

elimu hata Falsafa, Mantiq (Logic) Sayansi na Mathematic.<br />

Kasema maneno makubwa makubwa kama alivyosema Sultan <strong>Al</strong><br />

Awliyaa Seyyidina Abdul Qadir Jailan- Mfasiri)<br />

Zarruq alikuwa khalifa wa Ahmad Bin Uqba <strong>Al</strong><br />

Hadhrami bwana huyu alilelewa Tarim Hadharamawt na<br />

Seyyidna Abdallah Bin Abubakar <strong>Al</strong>-Aidarus akafikilia daraja<br />

kuwa katika Uwalii Mwenyi Enzi Mungu akamchagua awe<br />

mmoja katika Mqutbu wa Silsila hii ya Shadhili akampeleka<br />

Misri akalazimiya na Yahya <strong>Al</strong>-Qadiri alipofariki huyo alirithiwa<br />

na <strong>Al</strong> Hadhrami –Mfasiri).<br />

5.


Yahya <strong>Al</strong>-Qadiria alipokea <strong>Al</strong>i Wafaa na yeye aliwapokea<br />

kutokana na baba yake Bahr Safa kutokana na Daud <strong>Al</strong>-Bakhili<br />

kutokana na Ahmad Bin Attaillah Assakandari kutokana Abi <strong>Al</strong>-<br />

Abbas <strong>Al</strong> Mursi (Huyu kaitwa <strong>Al</strong> Mursi kwa sababu alizaliwa<br />

Mercia, Spain wakati Spain ilikuwa ya kiislam baada ya waislamu<br />

kukaa huko kwa miaka wakatia misingi ya kila namna ya masomo<br />

na ustaarab huko ulaya. <strong>Al</strong>-Mursi alikuwa anakwenda kuhiji Jahazi<br />

ilivunjika wakazama watu wote akaokotwa hapo alipokuwa Qutba<br />

mkubwa kabisa Sayyidina Abdul Hassan Ash-Shadhili alimlazimu<br />

bwana huyu hata akawa yeye ndiye khalifa wake mkubwa kabisa -<br />

Mfasiri).<br />

Seyyidina <strong>Al</strong>-Imam Abdul Hassan alimrithi Abdu<br />

Ssalaam Bin Mashish na yeye alipokea kwa Abdulrahman <strong>Al</strong><br />

Madani Azzayyat kutokana na Taqiyyuddin <strong>Al</strong> Fuqayyir kutokana<br />

na <strong>Al</strong> Qutb Fakhruddin kutokana na Qutb Nuruddin Abdul Hassan<br />

kutokana na <strong>Al</strong> Qutb Tajuddin kutokana <strong>Al</strong> Qutb Shamsuddin<br />

Assiwasi kutokana na <strong>Al</strong> Qutb Zainuddin <strong>Al</strong> Qazwimi kutokana na<br />

<strong>Al</strong> Qutb Abi Is-Haq Ibrahim <strong>Al</strong>i Bisry kutokana na <strong>Al</strong> Qutb Abu<br />

Qassim Ahmad <strong>Al</strong> Marwany kutokana na Qutb Abu Muhammed<br />

Said kutokana na <strong>Al</strong> Qutb Saad kutokana na <strong>Al</strong> Qutb Fathu Suud<br />

kutokana na <strong>Al</strong> Qutb Said <strong>Al</strong> Qazzani kutokana na <strong>Al</strong> Qutb Abi<br />

Muhammed Jabir kutokana na Qutb wa mwanzo Sayyiduna <strong>Al</strong><br />

Hassan kutokana na baba yake Sayyidina <strong>Al</strong>i Bin Abi Twalib na<br />

yeye kapokea kwa Bwana wa mwanzo na wa mwisho Bwana wetu<br />

Muhammed S.A.W. Hapa Silsila imemalizika.<br />

Sheikh Abdallah alimwambia <strong>Al</strong> Maaruf "Chukueni kazi<br />

yenu hii nyinyi Ahl Bait Rasulillah. Sisi ni watumishi wenu katika<br />

kazi hii".<br />

<strong>Al</strong> Maaruf alipopewa ukhalifa alirejea Moroni akasimamisha<br />

Daira na akawa anawapa watu Ijaza wakakusanyika kwake watu<br />

namna nyingi Sheikh Abdallah alikuwa huja Moroni na<br />

kuhudhuria Daira pamoja naye hata bwana wangu (Siri yake<br />

imetakaswa alimchukua Sheikh Abdallah nyumbani kwake ili<br />

awape Ijaza watu wa huko nyumbani Sheikh Abdallah akampa<br />

ijaza mama yake Assayid na ndugu zake wanawake Sayyidat<br />

<strong>Al</strong>awiyyah, Sayyidat Batul, Sayyidat Fatuma na Sayyidat Ihsan<br />

ndugu zake baba mmoja mama mmoja aliendelea Sheikh<br />

Abdallah kwenda Moroni na kurudi Itsandaa.<br />

6


Siku moja alipikiwa chakula Moroni, akasema: "Mwenye<br />

kula chakula hiki ataingia peponi, na mwenye kukila kwa nia<br />

yoyote atapata muradi wake". Akachukua kila mmoja katika<br />

walio kuwepo tonge tonge akawachukulia watu wa nyumbani.<br />

Palikuwa na mwanamke Tasa akala kwa nia Mwenyi Ezi Mungu<br />

ampe mtoto na Mungu akampa na hekaya hii inajulikana<br />

Ngazijah na imeenea kwenye watu wa huko.<br />

Baadaye alimpelekea Assayyid khabari asafiri<br />

aende Hinzwani Sayyid akamjibu kuwa, "hapana marikebu<br />

inayokwenda huko". Akamjibu "Andaeni safari kwani nyinyi<br />

mtasafiri kesho inshaallah". Wala hapakuwa merikebu pwani<br />

ilipokuja siku aliyowaambia kuwa safari yao itakuwa, alisikia<br />

mjini kuwa pamedhihiri jahazi ya matanga pwani lakini jahazi<br />

hiyo haikusogea mjini watu walitoka kuiangalia wakaikuta kama<br />

ilivyosemwa. Paliteremshwa Ngalawa kutoka Jahazini<br />

wakateremka baadhi ya waliokuwa na katika wao alikuwa<br />

mwenye Jahazi, Muhammed Bin Silim yeye alikua ana mke na<br />

marafiki Moroni ilipita kuwazuru tu. Assayyid alimuuliza<br />

mnaendea wapi? " akajibu Muwali" akasema "Sisi tunataka<br />

kusafiri pamoja na nyinyi" Jawabu ilikuwa kwa mapenzi na<br />

Ukarim akasafiri siku hiyo pamoja na Sheikh Abdallah <strong>Al</strong>i fundi<br />

na Ahmad Bin Nakhodha hata wakafika Muwali wakateremka<br />

baadae walisafiri kwenda Hinzwani katika Jahazi nyingineyo<br />

wakateremka Bamoni wakapita njia ya barabara hata wakifika<br />

Mtsamudu. Siku hiyo ilikuwa Ijumaa Mwezi 24 mfungo Tisa<br />

mwaka 1299 Hijriyya walipofika hapo alikutana na Ssayyid<br />

Ahmad <strong>Al</strong>-Kabir Muhammed <strong>Al</strong> Arab na Muhammed Abood na<br />

Abdu-Rab na wote wakawa katika Muridi wa Kishadhili.<br />

Baadaye Sayyid alijiweka kuwapa Ijaza kila alietaka wakachukua<br />

Ijaza kutokana naye watu namna nyingi, alikuwa husimamisha<br />

Daira msikiti wa Ijumaa kila usiku baada ya sala ya Isha. Watu<br />

wa msikitini walimwambia: "Ungeligura ukenda mahali pengine<br />

ingelikuwa bora kwani sisi tunashawishika ikisimamishwa Daira<br />

hapa na sisi tuna nyiradi hatuwezi kuzisoma". Kwa hiyo alihamia<br />

Masjid Ar-rhmani hakuwa akisimamisha Daira msikiti wa<br />

Ijumaa ila baada ya sala ya Ijumaa na sikukuu zote mbili.<br />

Baadae alielekea Wani ili kutoa Ijaza akakaa huko kiasi ya<br />

wiki walichukua Ijaza kwake aghlabu ya watu wa huko akampa<br />

Sheikh Muhammed Bin Abubakar Ukhalifa juu yao.<br />

7


<strong>Al</strong>irejea tena Mtsamudu, lakini hakukaa hapo mda mrefu<br />

akatakiwa kwenda Bombo akaenda pamoja na baadhi ya Muridi,<br />

akakaa huko siku kadha wa kadha aliwapa Ijaza huko watu wengi<br />

akafanya khalifa juu yao Sayyid Jaafar baadae alirejea Mtsamudu<br />

akadumu katika Masjid Ar hmani katika kumtaja Rabbu wake.<br />

Hakuwa akienda msikiti wa Ijumaa ila siku ya Ijumaa.<br />

Kupingwa na Sheikh Fadhil na Jawabu ya Sayyid na<br />

yaliyopita baina yao kwa ufupi.<br />

(Mungu awalie Radhi wote wawili na atunufaishe kwa wote)<br />

katika muda huu Sheikh Fadhili alimpinga Sayyid katika<br />

kuwapa Ijaza ya Tarika watu wa Hunzuwani pamoja na kuwa<br />

wao si Ahli kama alivyodai yeye hali ya kutoa Dalili kwa hadithi<br />

"Msiwape hekima wasiostahiki msije mkadhulumu" na katika<br />

hadithi nyingine au utimilifu wa hii au hadith khutba na mimi<br />

ndie Mufti wa Sawahil yote tangu Ras hafun mpaka Ras torfi na<br />

mimi nimezuia dhikri juu yenu au kuisoma mbele yangu. Seyyid<br />

alisimama akasema "Huna njia ya kuzuia dhikri", wakati huo<br />

zogo lilizuka kwa wingi msikitini watu walisimama na kelele<br />

zikaja juu. Kila mmoja akakamata silaha yake, Sayyid nae<br />

alinyanyua upanga wake Sayyid Abdallah Bin Sheikh alitoa nje<br />

upanga wake Sayyid Abdallah Bin Omar Khajar lake akelekea<br />

kwa Sayyid Abdallah Bin Omar aliyeitwa Abood Bin<br />

Muhammad Bin Omar, mtoto wa nduguye Abdallah Bin Omar ni<br />

katika Muridi wa Sayyid. Hapo hapo alimpiga kofi Ami yake<br />

kwa sababu ya wivu juu ya Sheikh wake hivi ndo anavyokuwa<br />

Muridi. Sultan Abdallah alikuwapo msikitini askari wake<br />

wakamzunguka Sayyid akatoka nje ya msikiti akanadi anaetaka<br />

Ijaza na ahudhurie wakahudhuria mbele yake wengi na yeye<br />

pamoja waliokua pamoja naye wanataka jina la Mwenyi Ezi<br />

Mungu. Baadae alitoa sauti akatoa nje upanga wake mbele ya<br />

Sultan Abdallah. Askari walipoona upanga walikimbia, Sayyid<br />

alimshika Sultan mkono akamwambia: "Sema <strong>Al</strong>lah" akawa<br />

anasema pamoja naye wakafuatana nyumbani na waliokuwapo<br />

waliwafuata na wote wanataja jina tukufu mpaka Sultan akaingia<br />

nyumbani kwake.<br />

Assayyid alielekea Mirontsi na kikundi katika Muridi wake<br />

walimfuata lakini hawakufika pamoja naye kwenye msikiti wa<br />

8.


Mironts ila watu kumi katika hao ni nduguye Sayyid <strong>Al</strong>i.<br />

Hapakupita ila dakika chache mara ukawafikia mwito<br />

kutokana na askari wa Sultan Abdallah, waliokuwa<br />

wamemzunguka wakamwambia amnilikie Sultan, yeye akajibu<br />

" Ndivyo" .<strong>Al</strong>ipotoka Msikitini wale askari walitaka kuchukua<br />

upanga wake na yeye akajizuia. Nduguye Sayyid <strong>Al</strong>i<br />

akamwambia: "Hii ni amri ya Sultan anahitajia tuitii". Hapo<br />

akawapa upanga baadae alichukuliwa pamoja na aliokua nao<br />

kutoka Morots na huko wanapigwa na kutolewa maneno na<br />

msukumo mkubwa hata mwisho Sayyid alitupwa baharini<br />

akatupiwa mawe. Baharini palikuwa Jahazi ya baadhi ya wahindi<br />

Sayyid alipanda akabaki humo siku saba baadae akasafiri pamoja<br />

nao mpaka Nusbee.<br />

Ijumaa ya mwanzo baada ya vituko hivyo walikuja<br />

watu wake kutoka Bambao na katika hao ni Sayyid Jaafar na<br />

Sayyid Salim Bin Sultan Abdallah wakamkuta kesha safiri<br />

wakahudhuria Sala na wakasimamisha Daira. Waliapa kuwa<br />

ataewaingilia watamuuwa. Hapana aliewaingilia., Daira ilidumu<br />

kama ilivyokuwa katika Masjid Ar rahmani kila Ijumaa na<br />

sikukuu mbili ilikuwa ikisimamishwa Msikiti wa Ijumaa.<br />

Sayyid alirejea kutoka Nusbee akateremka Maote<br />

alimuamrisha Sayyid Ahmad Bin Abdulrahman na Abood Bin<br />

Muhammad warejee Hinzwan na yeye mwenyewe alielekea<br />

Ngazijah pamoja na nduguye Sayyid <strong>Al</strong>i na Muhammad <strong>Al</strong> arab.<br />

<strong>Al</strong>ipofika Ngazijah alipokelewa na Sheikh Abdallah Darwesh na<br />

alikuwa pamoja nae kwa namna iliokuwa njema kabisa kuliko<br />

walivyopata kuwa.<br />

Baadae alimpeleka nduguye Hinzwani ili afanye<br />

upya mfungano wao na Tarika akampa Ijaza. Yeye alikaa<br />

Hinzwani miezi. Siku yane na ya tano ya kufika kwake Hinzwani<br />

alifariki Sheikh Fadhil ( Mungu amrehemu). (Sayyid alitoa amri<br />

asomewe wadhifa aombewe dua. Haya yanaonyesha kuwa Sheikh<br />

Fadhil hakumpinga Sayyid kwa inadi bali jitihada. <strong>Al</strong>ijitahidi<br />

akakosana, na Sayyid akamuombea Dua aghufuriwe - Mfasiri)<br />

Sayyid <strong>Al</strong>i alirejea Ngazija akamkuta Sheikh Abdallah<br />

Darwesh kasafiri kwenda Zanzibar baada ya kufariki Sayyidat<br />

<strong>Al</strong>awiyya. Bibi huyo alikuwa na cheo kikubwa kwa Bwana ambae<br />

maisha yake yanaandikwa. Hapa mauti yalipomhudhuria alikuwa<br />

anataja jina tukufu la Mwenyi Ezi Mungu. Sayyid alimwambia:<br />

"Msalie Mtume" Bibi alijibu "Huyu hapa Mjumbe<br />

9


wa Mwenyi Ezi Mungu ananiamrisha nitaje Ismul-Jalala".<br />

Sayyidat <strong>Al</strong>awiyya huyu ndiye ambaye Sheikh Abdallah<br />

Darwesh alisema katika kumtaja kumpa cheo chake:<br />

"Wangegawika Muridi mimi ningekuwa pamoja na kikundi<br />

alichomo Sayyidati <strong>Al</strong>awiyya".<br />

Katika siku hizo alikwenda Sayyid kwenye Bustani ya<br />

mama yake ijulikanayo kwa jina la Buzini akakaa huko siku<br />

nyingi awemo ndani ya Khalwa (Muepukano na kila kitu kwa<br />

kushughulika na Mwenyi Ezi Mungu) Hapo ilimjilia kwa daraja<br />

kubwa hali wapatao Mawalii wakubwa ilirejea nayo Mironi<br />

akaingia nyumbani kwa Sheikh Abdallah Bin Himid, akabaki<br />

pamoja naye huko siku tatu bila ya kuingia huko nyumba yoyote.<br />

Baada ya hapo alitoka Sheikh Abdallah Bin Himid<br />

na Sayyid akapanda juu ya sakafu ya nyumba akafika ukingoni<br />

akaanguka, nduguye Sayyid alimchukua mpaka nyumbani kwa<br />

mama yake akabaki nyumbani kiasi ya miezi sita na Ahwal zake<br />

zikizidi hatuwezi kukisia aliyoyapata katika yajayo kutoka na<br />

Mwenyi Ezi Mungu pamoja na yanayoteremka na miminio<br />

alipokuwa katika hali hiyo mara yumo ndani ya صحو mara<br />

nyingine محو pengine huwa عينةkatika na pengine katika<br />

(Maneno haya hayafasirika kwani ni Istilahi za Mabwana حضو ر<br />

Masufi. Hayana maana ya lugha wenyewe wanatambua kwa<br />

Dhawq. Kuyaonja na ekspiriense. - Mfasiri). <strong>Al</strong>iendelea hata<br />

akapata ambayo hatwezi kuyatambua vilivyo na tunahemewa na<br />

kudiriki hakika yake.<br />

Jadhba hii ni mash-hur Ngazija kwa Muridi wote. Yeye<br />

Sayyid alisema wakati katika Jadhba yake "Mimi ni kitu Azizi<br />

mimi ni kitu kilichotokana na Mtume (S.A.W) na ni hasha<br />

Mtume kumpa baba yangu kitu kidhalilifu". <strong>Al</strong>isema:<br />

(Mwenyi Ezi Mungu atunufaishe kwa baraka zake ) "Ingekuwa<br />

bahari ni wino na miti kalamu ili kudhibiti niliyoyaona<br />

bahari ingekwisha na miti ingemalizika kabla ya kumalizika<br />

mambo niliyoyaona katika Jadhba yangu hii".<br />

Baada ya hapo alirejea kukaa na watu kama ada yake ya<br />

mwanzo akasafiri kwenda Hinzwani akateremka Mtsamudu.<br />

Sultan Abdallah alikuwa Bambao alimtaka Sayyid aende huko na<br />

yeye akenda pamoja na baadhi ya Muridi. Sultan Abdallah<br />

akampokea kwa taadhima na mtukuzo, na yeye alikuwa<br />

akijihisabu kuwa ni katika jumla ya Muridu. Katika baadhi ya<br />

10.


siku alimwonyesha mkono Sayyid kwa kutaka kumpa<br />

mapesa. Sayyid alisema: "Nimepokea zawadi yako, lakini<br />

sasa sina haja ya kitu basi kaa nayo mpaka wakati wa haja".<br />

Baadae alifika Sheikh Abdallah bin Himid kutoka<br />

Ngazija akakutana na Sayyid akampa khabari ya kifo cha<br />

Sayyidat Fatuma Bint Sheikh Ahmad. Ukhti yake Sayyid<br />

baba mmoja mama mmoja, alimuomba arejee Ngazija.<br />

akakubali akasafiri pamoja. Hii ndio safari ya mwisho ya<br />

Hinzwani hakurejea tena.<br />

Baada ya kufika Ngazija, watu wa huko walikhtalifiana<br />

na mfalme wao Sultan Sayyid <strong>Al</strong>i Bin Sultan Sayyid Omar<br />

<strong>Al</strong>-Masily walimtaka Sayyid awe pamoja nao na<br />

walimkhubiri kuwa watamuuzulu Sayyid <strong>Al</strong>i. Wakati huo<br />

ada ilikurubia kutoa kabisa hukumu za sheria iliyo<br />

tahirishwa jambo ambalo haridhii nalo Mwenyi Ezi Mungu<br />

na Mjumbe wake. Sayyid mara nyingi alikuwa akiyataja<br />

lakini hakumpata wa kunusuru sheria kwa hiyo alipotakiwa<br />

awe pamoja na alietaka kumuuzulu Sultan Sayyid <strong>Al</strong>i,<br />

waliomtaka walimpa miadi madhubuti kuwa watabatilisha<br />

ada yenye kwenda kinyume na sheria, watasimamisha<br />

sheria imara. <strong>Al</strong>iwakubalia na ikawa sababu kubwa ya<br />

kusalimika Sulatn Sayyid <strong>Al</strong>i nafsi yake kwani wale<br />

waliotaka kumuuzulu, walikusudia kumuua, lakini Sayyid<br />

hakuwaachia bali alibaki anawarairai na anawachukua kwa<br />

upole na kuwalainishia maneno kwa kumuonea huruma<br />

mtoto wa ndugu mama yake (Hakika ya mambo alihisi<br />

kuwa kisharia hakustahiki kuuliwa. Ingelikuwa sii hivyo<br />

angeliwaachia wakamuua kwani yeye ni wa mbele katika<br />

ambao hawatizami mhusiano mbele ya sheria ya Mungu -<br />

Mfasiri).<br />

Azma ya kumuuzulu iliposhika nguvu walimuamrisha<br />

khatibu asimtaje katika khutba ya <strong>Al</strong>jumua na yeye alukhutubu<br />

pasina kumuombea dua, ilipothibiti kwa Sultan Sayyid <strong>Al</strong>i kuwa<br />

waliloliazimia na jambo la matatizo alisafiri kwa kujificha mpaka<br />

Muali, na kutoka huko mpaka Maote akaifikishia dolla ya<br />

kifaransa yaliyomfika. Dola ya kifaransa iliandalia marikebo<br />

ikachukua idadi ya askari marekebo iliingia Ngazija ikateremsha<br />

11.


askari ambao walitafuta baadhi ya watu wajulikanao<br />

wakawachukua baadhi yao. Walimtafuta As-Sayyid lakini yeye<br />

alijificha hawakuweza kutambua alipokuwa. Mitsamhuli<br />

ilikuwapo jahazi inakwenda Zanzibar, Sayyid alipanda usiku<br />

wakati ambao wanaomtafuta wameghafilika walipokuwa<br />

hawakumpataSayyid, nchi kavu wazungu walipanda kwenye<br />

jahazi ili watizame ikiwa hajajificha humo jahazini. Walipoingia<br />

jahazini wakaanza kupekua, palivuma upepo mkali na mawimbi<br />

yakachafuka, hapo hapo waliteremka bila ya kumuona, "Na wapi<br />

jicho pofu litaona jua?" wakati huo mnyororo uliofungiwa jahazi<br />

na nanga ulikatika na Jahazi ikaingia baharini matanga<br />

yakapandishwa na jahazi ikatweka kuelekea Zanzibar.<br />

Imewachukua Sayyid na Muridi wake wawili Ahmad<br />

Nakhodha na Abdul-R-rabb jahazi ilipokuwa mbali na nchi kavu<br />

Sayyid alisimama juu ya sitaha akababaika mmoja katika muridi<br />

wake akasema: "Eeh bwana wangu, umejitokeza watu watakuua<br />

iwe sababu ya sisi kuangamia", akajibu "Usihuzunike na sisi kwa<br />

kupenda Mwenyi Ezi Mungu baada ya salat aljumaa tutaingia<br />

Zanzibar. Safari yake ilikuwa jioni ya jumanne. Ikatokea vile vile<br />

kama alivyosema kwani waliingia Zanzibar baada ya salat<br />

aljumaa.<br />

<strong>Al</strong>iishi Sayyid Unguja hata mpaka alipotolewa Sultan<br />

Sayyid <strong>Al</strong>i Ngazija Dola ya kifaransa ndio iliyomtoa. Hapo<br />

alirejea Ngazija na hakusafiri kamwe. Hakuondoka huko hata<br />

Mwenyi Ezi Mungu akamchukua hali ya kuwa yeye Sayyid<br />

karidhia na karidhiwa.<br />

منا فيو رض هللا عنو<br />

12.


Mtoto wa <strong>Al</strong> habbib Sayyeid Muhammed <strong>Al</strong> Ma`aruf aliyezaliwa<br />

Zanzibar.<br />

13.


<strong>Al</strong> habbib Sayyeid Muhammed Bin Sayyeid <strong>Al</strong>liy <strong>Al</strong> Ma`aruf.<br />

15.


Mfasiri kwa Kiswahili mtoto wa ndugu yake Sayyeid <strong>Al</strong> Ma`aruf.<br />

<strong>Al</strong> habbib Nassib Sayyeid Umar Bin Sayyeid Abdallah<br />

Mwinyibaraka.<br />

17


Khalifa wa mwanzo wa Majaalis-el ulaa – Mwinyi Baraka-<br />

Uwesia – Qa-diriyya. <strong>Al</strong> <strong>Faqeer</strong> Sheikh Ahmad Bin Sheikh<br />

Muhammed Msiha.<br />

18


Vitabu vilivyokwishatoka ni:<br />

*1. Maana halisi ya Imaan. (i) (1 st , 2nd & 3rd addition).<br />

*2. Njia nyepesi ya kuijua nafsi yako.<br />

*3. Njia nyepesi ya kujua kitu juu ya uongofu.<br />

*4. Knowledge vision & ecstacy.<br />

*5. Mwinyi Baraka katika ulimwengu wa kiislamu.<br />

*6. Waislamu na Sayansi - Ulu-m.<br />

*7. Kuhifadhi Burda.<br />

*8. Maana halisi ya Imaan (ii).<br />

*9. Muhammad SAW katika ulimwengu wa ghayb.<br />

*10. Siri ya Balaa.<br />

*11. El makhlouq (Viumbe)<br />

*12. Njia nyepesi ya kujua juu ya uongofu. (2nd addition)<br />

*13. Manaqib ya <strong>Al</strong> habbib Sayyeid <strong>Al</strong> Ma`aruf.<br />

Vitabu ambavyo tunategemea kuvitoa muda si mrefu<br />

(Insha <strong>Al</strong>lah) ni:<br />

*1. Waislamu na Sayansi - Ulu-m. (2nd addition)<br />

*2. Njia nyepesi ya kuijua nafsi yako. (2nd addition).<br />

*3. Mwinyi Baraka katika ulimwengu wa kiislamu ( 2nd. add).<br />

*4. Njia nyepesi ya kujua kitu juu ya Uongofu.<br />

*5. Some aspects of concepts of facility in medevial Islamic<br />

Philosophy by Mwinyibaraka.<br />

Kwa maulizo kuhusu vitabu wasiliana nasi:<br />

Majaalis El Ulaa-MwinyiBaraka-Uwesia- El Qadiriyya Sinza,<br />

P.o. Box 15170,<br />

Tel: 0747483553<br />

Tel: 0748595958.<br />

Tel: 0744 023703.<br />

Tel: 0741 235091.<br />

Tel: 0744 299597.<br />

Dar es salaam.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!