17.02.2015 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Siku moja alipikiwa chakula Moroni, akasema: "Mwenye<br />

kula chakula hiki ataingia peponi, na mwenye kukila kwa nia<br />

yoyote atapata muradi wake". Akachukua kila mmoja katika<br />

walio kuwepo tonge tonge akawachukulia watu wa nyumbani.<br />

Palikuwa na mwanamke Tasa akala kwa nia Mwenyi Ezi Mungu<br />

ampe mtoto na Mungu akampa na hekaya hii inajulikana<br />

Ngazijah na imeenea kwenye watu wa huko.<br />

Baadaye alimpelekea Assayyid khabari asafiri<br />

aende Hinzwani Sayyid akamjibu kuwa, "hapana marikebu<br />

inayokwenda huko". Akamjibu "Andaeni safari kwani nyinyi<br />

mtasafiri kesho inshaallah". Wala hapakuwa merikebu pwani<br />

ilipokuja siku aliyowaambia kuwa safari yao itakuwa, alisikia<br />

mjini kuwa pamedhihiri jahazi ya matanga pwani lakini jahazi<br />

hiyo haikusogea mjini watu walitoka kuiangalia wakaikuta kama<br />

ilivyosemwa. Paliteremshwa Ngalawa kutoka Jahazini<br />

wakateremka baadhi ya waliokuwa na katika wao alikuwa<br />

mwenye Jahazi, Muhammed Bin Silim yeye alikua ana mke na<br />

marafiki Moroni ilipita kuwazuru tu. Assayyid alimuuliza<br />

mnaendea wapi? " akajibu Muwali" akasema "Sisi tunataka<br />

kusafiri pamoja na nyinyi" Jawabu ilikuwa kwa mapenzi na<br />

Ukarim akasafiri siku hiyo pamoja na Sheikh Abdallah <strong>Al</strong>i fundi<br />

na Ahmad Bin Nakhodha hata wakafika Muwali wakateremka<br />

baadae walisafiri kwenda Hinzwani katika Jahazi nyingineyo<br />

wakateremka Bamoni wakapita njia ya barabara hata wakifika<br />

Mtsamudu. Siku hiyo ilikuwa Ijumaa Mwezi 24 mfungo Tisa<br />

mwaka 1299 Hijriyya walipofika hapo alikutana na Ssayyid<br />

Ahmad <strong>Al</strong>-Kabir Muhammed <strong>Al</strong> Arab na Muhammed Abood na<br />

Abdu-Rab na wote wakawa katika Muridi wa Kishadhili.<br />

Baadaye Sayyid alijiweka kuwapa Ijaza kila alietaka wakachukua<br />

Ijaza kutokana naye watu namna nyingi, alikuwa husimamisha<br />

Daira msikiti wa Ijumaa kila usiku baada ya sala ya Isha. Watu<br />

wa msikitini walimwambia: "Ungeligura ukenda mahali pengine<br />

ingelikuwa bora kwani sisi tunashawishika ikisimamishwa Daira<br />

hapa na sisi tuna nyiradi hatuwezi kuzisoma". Kwa hiyo alihamia<br />

Masjid Ar-rhmani hakuwa akisimamisha Daira msikiti wa<br />

Ijumaa ila baada ya sala ya Ijumaa na sikukuu zote mbili.<br />

Baadae alielekea Wani ili kutoa Ijaza akakaa huko kiasi ya<br />

wiki walichukua Ijaza kwake aghlabu ya watu wa huko akampa<br />

Sheikh Muhammed Bin Abubakar Ukhalifa juu yao.<br />

7

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!