Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Siku moja alipikiwa chakula Moroni, akasema: "Mwenye<br />
kula chakula hiki ataingia peponi, na mwenye kukila kwa nia<br />
yoyote atapata muradi wake". Akachukua kila mmoja katika<br />
walio kuwepo tonge tonge akawachukulia watu wa nyumbani.<br />
Palikuwa na mwanamke Tasa akala kwa nia Mwenyi Ezi Mungu<br />
ampe mtoto na Mungu akampa na hekaya hii inajulikana<br />
Ngazijah na imeenea kwenye watu wa huko.<br />
Baadaye alimpelekea Assayyid khabari asafiri<br />
aende Hinzwani Sayyid akamjibu kuwa, "hapana marikebu<br />
inayokwenda huko". Akamjibu "Andaeni safari kwani nyinyi<br />
mtasafiri kesho inshaallah". Wala hapakuwa merikebu pwani<br />
ilipokuja siku aliyowaambia kuwa safari yao itakuwa, alisikia<br />
mjini kuwa pamedhihiri jahazi ya matanga pwani lakini jahazi<br />
hiyo haikusogea mjini watu walitoka kuiangalia wakaikuta kama<br />
ilivyosemwa. Paliteremshwa Ngalawa kutoka Jahazini<br />
wakateremka baadhi ya waliokuwa na katika wao alikuwa<br />
mwenye Jahazi, Muhammed Bin Silim yeye alikua ana mke na<br />
marafiki Moroni ilipita kuwazuru tu. Assayyid alimuuliza<br />
mnaendea wapi? " akajibu Muwali" akasema "Sisi tunataka<br />
kusafiri pamoja na nyinyi" Jawabu ilikuwa kwa mapenzi na<br />
Ukarim akasafiri siku hiyo pamoja na Sheikh Abdallah <strong>Al</strong>i fundi<br />
na Ahmad Bin Nakhodha hata wakafika Muwali wakateremka<br />
baadae walisafiri kwenda Hinzwani katika Jahazi nyingineyo<br />
wakateremka Bamoni wakapita njia ya barabara hata wakifika<br />
Mtsamudu. Siku hiyo ilikuwa Ijumaa Mwezi 24 mfungo Tisa<br />
mwaka 1299 Hijriyya walipofika hapo alikutana na Ssayyid<br />
Ahmad <strong>Al</strong>-Kabir Muhammed <strong>Al</strong> Arab na Muhammed Abood na<br />
Abdu-Rab na wote wakawa katika Muridi wa Kishadhili.<br />
Baadaye Sayyid alijiweka kuwapa Ijaza kila alietaka wakachukua<br />
Ijaza kutokana naye watu namna nyingi, alikuwa husimamisha<br />
Daira msikiti wa Ijumaa kila usiku baada ya sala ya Isha. Watu<br />
wa msikitini walimwambia: "Ungeligura ukenda mahali pengine<br />
ingelikuwa bora kwani sisi tunashawishika ikisimamishwa Daira<br />
hapa na sisi tuna nyiradi hatuwezi kuzisoma". Kwa hiyo alihamia<br />
Masjid Ar-rhmani hakuwa akisimamisha Daira msikiti wa<br />
Ijumaa ila baada ya sala ya Ijumaa na sikukuu zote mbili.<br />
Baadae alielekea Wani ili kutoa Ijaza akakaa huko kiasi ya<br />
wiki walichukua Ijaza kwake aghlabu ya watu wa huko akampa<br />
Sheikh Muhammed Bin Abubakar Ukhalifa juu yao.<br />
7