Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Al</strong> Habib Seyyid Omar Bin Seyyid Abdallah – Mwinyi baraka.<br />
i
Katika<br />
ulimwengu wa Uislamu<br />
(i)<br />
Muharram 1429 - January 2008<br />
Toleo la pili <strong>Al</strong>l rights reserved Second addition.<br />
ii.
Yaliyomo:<br />
No.<br />
Ukurasa.<br />
1. Yaliyomo……………………………………... iii.<br />
2. Dibaji………………………………………….. vi.<br />
3. Utangulizi……………………………………… vii.<br />
4. Sehemu ya kwanza…………………………… viii.<br />
5. Kuzaliwa kwangu na malezi yangu…………… 1.<br />
6. Kuanza kusoma………..……………………… 1.<br />
7. Kwenda Makerere…………………………….. 2.<br />
8. Miaka ya Uganda……………………………... 3.<br />
9. Kuanza kusomesha skuli ya Dole…………….. 3.<br />
10. Daawa Ilallah………………………………….. 8.<br />
11. Sehemu ya pili………………………………… 18.<br />
12. Picha ya <strong>Al</strong> habib Seyyid Omar – Mwinyi Baraka.. 31.<br />
13. Vitabu vilivyotoka……………………………… 32.<br />
iii
DIBAJI:<br />
<strong>Al</strong>-hamdul-lillah wa Swalatu was salaam alaa Khayru<br />
Khalqillah Sayyidna Muhammad wa A-lihi wa Swahbihi waman waala<br />
wa Baad.<br />
Hichi ni kitabu ambacho <strong>Al</strong>-habib Sayyid Omar Bin Abdallah<br />
mashuhuri kwa jina Mwinyi-Baraka katika wajukuu wa Sayyid Abubakkar<br />
Bin Salim-Mola-Enaat huko Hadharamut, kwa taabu alielezea<br />
mwenyewe akiwa amejinyoosha kwenye kitanda alipokua mgeni wa<br />
Bw. Mohamed Khan Shemeji yake na <strong>Al</strong>-mar-hum Swaahib El- Ishara<br />
Bw. Akram Mohd aliyefia Mwanza - Tanzania kati ya Mwaka 1988 na<br />
89 <strong>Al</strong>lahu Yarhamuhu wa Jamiil Muuminina wal Muuminaat.<br />
<strong>Al</strong>ikua akizungumza kwa shida sana pengine Dak. 10. Pengine<br />
ndo gha-ya Dak. 15. Kwa hiyo ilikuwa tukimfwata na Tepu Recorder<br />
mara kwa mara tukiwa na Akh. <strong>Al</strong>y Mzee Comorian toka Mkunguni<br />
kwa <strong>Al</strong>-marhumu Mohamed Bin Mahdi na wanawe kina Akh. Islam,<br />
Khamis na <strong>Al</strong>-marhumu Mahdy Mohamed Mahdy <strong>Al</strong>lahummaghfirlahum<br />
wa yarhamhum jamiia.<br />
<strong>Al</strong>-hamdu-lillah tuliwahi kumaliza kunasa na kunukuru yote<br />
kuhusu safari zake za Europe na Amerika kama itavoonekana ndani<br />
yake.<br />
Kwa vile lengo kubwa la safari zake tukiacha kusoma ilikua ni<br />
Jihadi katika Dini ya Mnyezi Mungu nayo si nyingine bali ni Uislamu,<br />
tumeonelea kukiita “Mwinyi Baraka katika Ulimwengu wa Uislamu<br />
– I ” tukitegemea kwa imani zote kua:<br />
(a) Kitazagaza maarifa mazuri kwa watakaokisoma<br />
(b)<br />
Kutakua angalau na kumbukumbu ya mmoja wa wanafalsafa<br />
wa Kisufi mkubwa lakini hakupata umashuhuri nchini kwao<br />
mpaka amekufa.<br />
(c) Tutafaulu Insha-allah kumjulisha yule ambae hakumjua<br />
mwanachuoni mkubwa huyo wa East-Africa na labda<br />
vi.
kumuigiza au kumtakia dua, kwani ipo hasara kubwa kwa kule<br />
kushindwa kumtumia vile ambavyo ingepasa.<br />
Tabia yake katika kujitupa chini na kujiona kua si kitu<br />
alifahamika vibaya kwa ambao hawakumjua, na hijabu ya wazi wazi<br />
kwa walomjua vizuri kabisa. Dalili kubwa ilionekana mara nyingi<br />
alipokuwepo Jijini hapa, si wengi walojua, kwa hiyo ilifikia mpaka<br />
anaondoka si wengi walokua na habari hata ile ya kuepo Jijini hadi<br />
kufikia mwezi mzima! mara kadhaa alipata mwaliko kwa mwanafunzi<br />
wake mkubwa, alipokua madarakani <strong>Al</strong>-hajj <strong>Al</strong>y Hassan Mwinyi-<br />
(Mzee Rukhsa )-Ikulu na alitutaka rukhsa aende au asiende.<br />
Ahlil Majaalis El Ula El Qa-diriyya hawataacha kulia kwa<br />
huzuni kila wakifikiria uamuzi aloutoa baada ya makubaliano kua<br />
angeandika tafsiri ya kite kwa lugha ya Kiswahili ya kitabu kitukufu<br />
Qur an baada ya kushindikana kuitoa tafsiri hiyo kwa njia ya TVZ,<br />
lakini pia Majaalis nao hawakuwahi kwa sababu aliomba aende<br />
Comorro akamshauri mkewe aje nae D‟Salaam nyumbani kwa <strong>Al</strong>marhumu<br />
Bw. Moh‟d Mhdy (A.Y) kinyume ya mambo ni kwamba<br />
kwenda kwake Comorro alikua ameshaitwa kwenda kukutana na ajali<br />
yake badala ya kuja tena D‟Salaam kwa ajili ya kazi ya tafsiri ambayo<br />
ilitarajiwa kuchukua miaka mitatu mizima.<br />
Na ilifikiriwa kutoa juzuu moja moja kama alivoanza hivo <strong>Al</strong>marhumu<br />
Sheikh Abdallah Swaleh El-Farsy (Ay).<br />
Bumbuwazi tulolipata bila ya kumuomba aanze na utangulizi<br />
na Surat El-Fa-tiha tu tulifunukiwa nalo baadae kabisa kua lau mtu<br />
angejua ghaibu basi kuzidisha kheri kwetu ingetumilikisha angalau na<br />
tafsiri ya Surat El-Fatiha ya <strong>Al</strong>-habib Sayyid Omary Abdallah Mwinyi<br />
Baraka (Rahmatullah layhi).<br />
Kwa sababu <strong>Al</strong>-habib alitudarisha vizuri sana kuhusu somo la<br />
Nafsi (Tizama kitabu chetu “Maana halisi ya Imani”) hatuoni haja<br />
yeyote ya kulaumu walokua na uwezo mkubwa na kueka kumbukumbu<br />
ya mwanachuoni huyo kabla na labda baada ya kufa kwake.<br />
Akielezea mwenyewe <strong>Al</strong>-habib kua kila alipokua Makka <strong>Al</strong>marahumu<br />
Bin Bazz alikuwa akimtanguliza… “Omar Swalisha”.<br />
Akimwambia: “Bwana Mtume SAW akisema, Ahlishsharafaa laa<br />
Ahlisharaf watu wa Sharaf hupitana kwa Sharaf. Walaa Yaa arifa<br />
Ahlish-sharaf wala hawawajui watu wa Sharaf Illa Dhawish Sharaf,<br />
Illa ambao ni watu wa Sharaf”.<br />
v.
Kwa niaba ya Majaalis natwaa fursa hii kuwashukuru mno<br />
vijana wa Darasa la kila Jumatano Baadal-Maghrib Mtaa wa Sadani<br />
Ilala baina kina Sharif Karama kwa juhudi yake kubwa katika<br />
kuziandaa kwa makini na uangalifu sana jumla ya makala hizo na<br />
kuzitoa katika Computer, kina Sharif El-Beyt Hussen, Fuad, Mohamed,<br />
Mkhashshe, Swahibul-Ishara Swaleh Hariz, Okashi, Mustafaa, kina<br />
Ababil Abdallah Twalib Arusha na wote wa Jalsa hiyo Mnyezi Mungu<br />
atawajazi Fid Dunia Wal A-khirah.<br />
AL-FAQEER.<br />
AHMAD SHEIKH.<br />
vi.
UTANGULIZI:<br />
<strong>Al</strong>-hamdu-lillahi Rabbil <strong>Al</strong>lamin, Was Swalaatu Was Salaam,<br />
<strong>Al</strong>a Asharafil Anbiya Wal Mursalin <strong>Al</strong>ladhi Unzila <strong>Al</strong>ayhi<br />
Lawlaa Nafarun Min Firqatin Kulli Twaa Fatin Layatafaqqahli<br />
Fil Diin Wa‟alaa <strong>Al</strong>ihit Twaahirina wa Aswaha-bihil<br />
Akramiin.<br />
(Amma Baad)<br />
Wemeniamrisha nsoweza kuwavunja na wakanitaka<br />
watu ambao naona uzito kwenda kinyume nao nieleze<br />
yatayosahilika katika safari zangu.<br />
Sasa naingia kufanya hayo kwa msaada wa Mnyezi<br />
Mungu na uwezo wake Laa-hawla Walaa Quwata Illa Billahil<br />
<strong>Al</strong>iyyil Adhim.<br />
OMAR ABDALLAH<br />
DAR ES SALAAM - TANZANIA<br />
1987<br />
vii.
S E H E M U<br />
YA<br />
K W A N Z A<br />
viii.
KUZALIWA KWANGU NA MALEZI YANGU:<br />
“Naona afadhali nielezee kwanza msingi wa malezi.<br />
Nilizaliwa Zanzibar mwisho mwaka 1917 yaani<br />
December kwa mujibu wa Sheikh, yeye atakuwa anamjua<br />
Mzee wangu vizuri kwani alikua ameoa kwao, kwa Babu na<br />
Mama wote Masharifu walozaliwa Ngazija. Babu Abu-Bakkar<br />
Bin Salim, Mama Lydiid Jamallilleye.<br />
Babu mkubwa Sayyid Abdul-Hassan baada ya miaka<br />
miwili yaani 1938 Baba yangu huyo alifariki-Mungu<br />
amrehemu. Na baada ya miaka mitano ya umri wangu mama<br />
alifariki - Mungu amlaze mahali pema . Nikalelewa na Mume<br />
wa Khaalal Ibin Khaalat wa Mama yangu Seyyid Abdul-<br />
Fattaah Bin Ahmed Jamalilley akiitwa sharifu Abudu.<br />
KUANZA KUSOMA:<br />
Nilipelekwa chuoni kwa <strong>Al</strong>-Mar-hum Seyyid Sheikh<br />
Bin Abdul-Rahman Babake Seyyid Hassan Sheikh nikawa<br />
nasoma, na Sala nimesoma kwa Bibi mkubwa mwana-Ashata<br />
kama alivokua akiitwa Aisha lakini wakimwita Mwana-<br />
Ashata.<br />
Nikabaki baada ya kuhitimu nasomesha watoto chuoni huko<br />
huko na Khalafu nikawa nakwenda nasomesha watoto chuoni kwa<br />
Sharifu Abudu, na wakati huo huo tena nikatiwa Skuli, lakini kwa<br />
sababu ya kukawia kuingia Skuli, sikupata Mnazi mmoja.<br />
Nikapelekwa Mwembe-ladu kutoka Kisiwandui asubuhi, ninarudi<br />
halafu nakwenda saa nane tena mpaka mwisho nikaja zangu Mnazimmoja.<br />
Baada ya kusoma miaka mitatu Mwembe-ladu na mwalimu<br />
wa mwanzo wa Skuli hiyo alikuwa Juma Mohamed, wakimwita<br />
Juma Mohamed Mushte - sijui kwanini Mwalimu Juma <strong>Al</strong>lahu-<br />
Yarham.<br />
1.
Zilikuwa Klas mbili halafu mwisho zikawa tatu, halafu<br />
nikaenda Gulioni. Nikaendelea na masomo Skuli na huku<br />
nikienda chuoni na kusomesha mpaka nakumbuka mwaka<br />
gani nilipotiwa Skuli, ilikua 1928.<br />
Nilipokua STD. 7 Sharifu Abudu akafariki na huku<br />
nimeshaanza kusoma soma kwa Seyyid Abal-Hassan na vile<br />
vile Nahaw. <strong>Al</strong>ivofariki nikabaki chuoni. Nimekiendesha<br />
chuo bila shaka mwenyewe ni Seyyid Abal-Hassan ninasalisha<br />
Msikiti wake Msikiti wa Sharifu Abudu Vikokotoni.<br />
KWENDA MAKERERE COLLEGE:<br />
Nikasomesha Mukhtasaraf pale baada ya Swalatil-Fajr nae<br />
Seyyid Abal-Hassan akawa anasomesha Umdatus Saaliki baada ya<br />
vitabu kadhaa wa kadhaa tulivokua tumeishasoma. Sera zote<br />
takribin, Mukhtasarat kwa Seyyid Abdul-Fattah tumewahi kuvisoma<br />
kwake. Nikaanza na Nahaw hapo, ilihudhuriwa na watu mahodari<br />
katika masomo hayo. Kama Seyyid Mustafa, Sheikh Mohamed<br />
Qamus baada ya Swalatil-Ishaa. Hatukumaliza kitabu mie nilikua<br />
nimeishakwenda Secondary School na nikapata kupelekwa<br />
Makerere nkaenda Makerere College.<br />
Nilikua na bahati nzuri ya kufanya Mitihani, siku zote nakua<br />
Fas aghlabu. Katika Primary yote na Secondary nilipasi vizuri. Na<br />
nikisoma mwenyewe vibuku vibuku na hasa palikuwepo magazine<br />
ikiitwa Islamic Review kulikua na Library ya Sunni Mkunazini<br />
nikipenda sana kusoma. Kulikuwepo kama zile nikipata sana sana<br />
kusoma kama habari za kina Khuwaja Kamalud-din nikiona raha<br />
kwenda kusoma.<br />
Makerere niliingia 1939 nikapata Diploma ya Education baada<br />
ya miaka miwili na nikakaa mwaka wa tatu kuspeshalaiz katika<br />
Biology.<br />
2.
MIAKA YA UGANDA:<br />
Miaka ya Uganda ilikuwa ya faida sana kwa kufwatana<br />
Waislamu huko. Kutwalii nao, wakija Makerere tukitwalii na<br />
Sheikh wao Sheikh Shuayb na mmoja Maallim Juma na wengineo,<br />
hasa Nahaw, na Sheikh Shuayb akisoma mantik, Ambayo niliwahi<br />
kusoma kidogo kwa Muhsin Bin <strong>Al</strong>y Barwani pamoja na mwanae<br />
<strong>Al</strong>y muhsin halafu mimi nikaendelea kwa Sheikh Sleiman Bin<br />
<strong>Al</strong>awy.<br />
KUA MWALIMU SHULE YA DOLE:<br />
Mwisho nikarudi Zanzibar nikawa Mwalimu wa Sayans na<br />
Religion (DINI) katika shule ya Dole pamoja na Teachers Training<br />
yake. Wakati huo ndio nikapata fursa ya kufundisha Vijana wengi<br />
ambao sasa wameshika madaraka makubwa kama President <strong>Al</strong>y<br />
Hassan Mwinyi Vice President Idriis Abdul-Wakyl na wengineo.<br />
Huku ninasomesha Dole na Beit-Raas.<br />
Skuli ile ya Dole ikawa Beit-Raas na kila nikija mjini<br />
ninasomesha msikiti wa Sharif Abudu, na daima nasoma kwa<br />
Sheikh Sleiman na Sheikh Muhsini. Na vitu vingi nimesoma kwa<br />
Sheikh Sleiman, Fanni. Hata mtu akiniuliza Elimu yako ya Dini<br />
umeipata kwa nani, ntamwambia kwa Sharif Abudu, Seyyid Abdul-<br />
Fattan. Secondary Seyyid Abal-Hassan na Seyyid Mustafa Bin<br />
Jafar ambaye ni Father in Law wangu (Mkwe wangu).<br />
Na ikiwa kuna ilimu inaweza kuhisabiwa pamoja kua ya Ki-<br />
University, basi Universtity niloipata huko huko kwetu basi ni<br />
Sheikh Sleiman, Seyyid Abal-Hassan, Sheikh Muhsin, Seyyid<br />
Mustafa Bin Jaafar ambae ni Father in Law wangu (Mkwe wangu)<br />
zote zinajulikana nimezipata kwao Shikh Sleiman <strong>Al</strong>awy Babake<br />
Sheikh Zamil alikua mwanachuoni aliyekusanya mambo mengi<br />
taabu kuyakuta kwa mtu mmoja yeyote.<br />
1951 nkapata Scholorship ya London kwenda kusoma Islamic<br />
and Comperative Law. Unasoma Law ya Kiingereza, Law ya<br />
kiafrica na bila shaka kwa wingi - Sheria ya Kiislam na katika ajabu<br />
za kusoma mtu huyo ni kua walimu wa sheria ya Kiislamu<br />
3.
walikuwa ni Waingereza, na wengine walikuwa ni maadui wa<br />
Islamu. Lakini ni Law ni Fiq-hi, lakini wapo walokuwa<br />
wakinisomesha vitabu kama Dr. <strong>Al</strong>y Hassan Abdul-Qadir Director<br />
wa Islamic Cultural Centre alikueko siku hizo - London University<br />
ilimkodi School of Oriental Studies ilimtaka awe akija akisomesha.<br />
Nikasoma Fiq-hi, Usulil-Fiqhi kwake, nikasoma na kiarabu zaidi<br />
kwa Wazungu.<br />
Somo hilo liliniletea hasa katika kusomeshwa na mmoja<br />
katika wakristo, walikua wakitaka kuuvunja Uislamu sana Imani.<br />
Na kutaka kuponda kisichopondeka kwa Bw. Mtume - SAW<br />
Anderson akiitwa. Tumepigizana kelele mara nyingi kwenye klasi.<br />
Na nilikuwa nikisoma kinamna ya peke yangu pengine<br />
mimi na Mwalimu tu, pengine Walimu wawili na miye mwanafunzi<br />
mmoja pengine walimu watatu na mwanafunzi ni miye mmoja. Na<br />
miye kila nikipata fursa nikipondana pondana. Pengine klasi inajaa<br />
mpaka watu wanakwenda kwenye Dining Hall – mahali pa kulia<br />
chakula – manake watu wanasoma Law walikuwa wakichukua kitu<br />
kinaitwa LLM au LLB na ISLAMIC LAW – yaani sheria ya<br />
Kiislamu ni moja katika subjects.<br />
Wote wakija kwake sasa wakipanga aje awasomeshe na siye<br />
sote tuko pamoja. Tukipigizana kelele sana kilichontokea katika<br />
fikra za mwanzo kabisa ni khabari ya alipokuja kwenye mambo ya<br />
ndoa katika sheria ya Kiislamu akapata fursa ya kutaja ndoa ya<br />
Sayyidatna Zeynab Mtume SAW akasema hivo wanavosema wao:-<br />
“Siku moja alimuoza Zeyd Bin Harith kwa sababu Zeyd Bin<br />
Harith alikua ni mtumwa wake Mtume akamwacha huru<br />
akamuoza Zeynab. Zeynab alikua mtoto wa Shangazi yake na<br />
walikuwa hawataki aolewe na mtu ambae aliwahi kua mtumwa.<br />
Lakini kwa kumstahi Mtume na kusemewa kwa Mtume<br />
akamuoa sasa Khalafu akaja akamwacha akamuoa Mtume.<br />
Ndoa yake yalosemwa ndani ya Qur-an.<br />
Aya Qur an ilokusudiwa hapo ni ile ilioko katika 33:37.<br />
“Na (wakumbushe) ulipomwambia yule ambaye Mnyezi<br />
Mungu amemneeshesha (kwa kumuafikia Uislamu) na wewe<br />
ukamneemesha (kwa kumpa kugusana naye ni Bw Zaid Bin Harith<br />
ulipomwambia “shikamana na Mkeo na umche Mnyezi Mungu<br />
(usimuache)”. Na ukaficha katika Nafsi yako aliyotaka Mnyezi<br />
Mungu kuyatoa (nayo ni kuwa Mnyezi Mungu amekuamrisha<br />
4.
umuoe wewe huyo mkewe atakapomuacha ili iondoke ile itikadi<br />
iliyokua ya kuwa mtoto wa kulea ni kama mtoto wa kumzaa) na<br />
ukawachelea watu, hali Mnyezi Mungu ndiye mwenye haki zaidi ya<br />
kumchelea. Basi alipokwisha Zaid haja yake na mwanamke huyo,<br />
tulikuoza wewe ili isiwe taabu kwa Waislamu kuwaowa wake wa<br />
watoto wao wa kupanga wanapokuwa hawana haja nao. Na amri ya<br />
Mnyezi Mungu ni yenye kutekelezwa”.<br />
Qur an: 33:37<br />
Ilikuaje wao wanasema kamuona akampenda akamwambia<br />
mwache nimuowe miye. Na hakika ya amri ni jambo ilikua Zayd<br />
akipata taabu sana nyumbani kwa Zeynab. Ilikua Mabibi wa<br />
Kikureish wanadharau yule Bibi aliyeolewa na mtu ambae alikua ni<br />
Mtumwa, nae ni mzalendo. Akimtaabisha Zeyd. Zeyd akitaabika<br />
akija akimwambia mtume “Niachie nimuache” akamwambia “ Kaa<br />
nae, Kaa nae”. mwisho akapewa Rukhsa, alipopewa rukhsa Zeyd<br />
akamwacha Mtume SAW akamuoa. Sababu mbili:-<br />
Kwanza:-<br />
Kwa kikureishi hapana rukhsa kumuoa mtu ambae<br />
alikua mke wa mtumwa wake, mtu ambae alikua<br />
mtumwa wake akamwacha huru halafu akawa mkewe<br />
akimwacha hapana rukhsa kumuoa. Azwaaj adiyaihi.<br />
Ili kuondoshwa hayo iwe anza wewe hapana atae<br />
thubutu mwingine kila mtu ataogopa asitukanwe<br />
asifanzweje - wewe anza.<br />
“Tulikuoza wewe ili isiwe taabu kwa Waislamu kuwaowa<br />
wake wa watoto wao wa kupanga wanapokuwa hawana<br />
haja nao. Na amri ya Mnyezi Mungu ni yenye kutekelezwa”.<br />
“Likay laa yakuna ararajun fii azwaaj ad-i yaaihi midhaa<br />
qadhaa minha watwaran wa kana amrullahi maf-u-la”<br />
Ya pili:- Ilikua ni tabu kwa Zeynab kuolewa na watu wengine<br />
baada ya kua kaolewa na mtu Ad-iyaai – alikua ni<br />
mtumwa sasa Mtume ASW amekua kilugha ya<br />
kisasa yeye ndo alo Run Life yake. Jambo gani zuri zaidi<br />
angelifanya kuliko kumchukua yeye akamuoa.<br />
5.
Sasa wamemgeuza badala ya kumsifu kua ni mtu mtukufu namna<br />
hii na hivi Firaq akampenda. Nikasema pale pale kwenye klas na<br />
tulikuwa watu wangapi watu wanne, mimi na huyo aliekua akieleza<br />
na Profesa wa African Law na mmoja akifanza kazi ya<br />
Administration katika Afrika na mmoja alikua Jaji India sasa alikua<br />
akisomesha English Law nikawaambia jambo:-<br />
Something for which you have aught you have to have<br />
praised him, respected him. You have taken the very<br />
theme blame him and to make it the cause of saying bad<br />
things about the profet.<br />
Jambo kama hili mtu atataka Udhuru vipi-<br />
“Idhaa mahaasin allatii ataytuha aadat dhunubihi<br />
Faqul-llii kayfa aatadhir”<br />
“Ikiwa mema yangu niliyoyafanya yanahisabiwa ndo<br />
madhambi sasa natoa udhuru vipi tena”<br />
“Aa, yamekwisha hayo ni moja katika mambo yalotokea katika<br />
klas. Mikutano hiyo wasokua Waislamu na vikundi vya Waislamu.<br />
Ndo mwanzo Vijana wa Kiislamu wanaanza kukusanyika pamoja<br />
na kukutana toka nchi za nje na mmoja mmoja wa kule na<br />
wanafanya mikutano wanasoma, wanazungumza – palikua na<br />
pahala panaitwa Aclistus Square, kwa Editor wa Islamic Review<br />
kwenye Laasiri watu wanakutana wanadiscuss. Inasomwa Maqra<br />
inatafsiriwa, inaelezwa na <strong>Al</strong>-hamdulillah ikielezwa wao hutaka na<br />
mie nitie langu.<br />
Ikaendelea hivo hivo mpaka nikapata safari ya Marekani na<br />
mie ni mwanafunzi wa U.K niko England. Na kule kule England<br />
bila shaka fursa zimetokea katika makanisa vikundi vya wakristo<br />
nami nakwenda kutoa khutba fanni ni wengi na wanafurahi wasikie<br />
khabari za Uislamu na hivi.<br />
Nakumbuka Wales nilitoa khutba moja very famous - sana<br />
ilijaa watu sana kabisa. London nilikua nipo hapo nikitoa khutba<br />
sasa itakuja safari ya Marekani.<br />
Nilipokua mwanafuzi London School of Oriental African<br />
Studies <strong>Al</strong>-Madrasati Qarasaatish-Sharqiyyat katika London<br />
University ilipatikana fursa ya kwenda States wanafunzi wanaotaka<br />
6.
kwenda watoe kiasi kadhaa wa kadhaa na wakifika huko<br />
watatizamwa, watakua wageni wa Jumuiya ya Kimarekani moja<br />
wapo – wazungushwe wonyeshwe maisha ya Kimarekani yaliyo<br />
mema kwa mujibu wa vipimo vyao na mengine kwa vipimo vya<br />
watu wote.<br />
Kwa umri waliokua wakiutaka mimi nilikua nimekwisha kua<br />
mtu mzima lakini walipoona application yangu na kuniona<br />
wakanitia kati. Ilikuwa taabu kupata kipando tena, mwisho nikapata<br />
Greck Line ikanichukua mpaka Quebec, mji baada ya mji mpaka<br />
Batholomeo mpaka New York. Njiani bila shaka nikaona Niagara<br />
Falls. Shalalar Niagara – Mmiminiko wa maji katika mahali<br />
wanapokwenda watu kutizama. Pahala pa ajabu penye Nature –<br />
yaani umbo la ajabu.<br />
Bin Adam hajatia mkono wake, wenyewe tu linakwenda –<br />
lipo. Kutoka hapo ndo nkaenda Batholomeo – Batholomeo New<br />
York nkapokelewa na wenzangu wengine mmoja mmoja. Tena<br />
mmoja kutoka London tukakutana huko huko. Nimekwenda<br />
tukakutanika pamoja na Waislamu wawili watatu mmoja mtu wa<br />
Kimasr, mmoja wa Pakistan lakini sasa imekwisha kua kikatiba –<br />
Bangladesh tena. Na Dini nyinginezo na kabila nyinginezo.<br />
Tukachukuliwa kuzungushwa tukapitishwa States mbali mbali, na<br />
kila pahali tunapata fursa ya kupokewa kwa heshima na<br />
kuonyeshwa na kushughulikiwa, na wasaa wa kutoa fikra.<br />
Na bila shaka mtu Muislam kila akipata fursa jambo la<br />
mwanzo hutizama njia awaonyeshe watu nini Uislamu, nini faida<br />
zake nini ukweli wake, na <strong>Al</strong>-hamdulillah sikuziwacha fursa hizo.<br />
Hata unaona Naby Yusuf AS alipoulizwa habari za ndoto na wale<br />
watu wawili katika gereza kabla hajawajibu kawaambia.<br />
“Enyi Wafungwa wenzangu wawili Je! waungu wengi<br />
wanaofarikiana ndio bora (kuabudiwa) au Mnyezi<br />
Mungu mmoja mwenye nguvu (juu ya kila kitu)”.<br />
Qur an: 12:39<br />
“Inni Taraktu Millata Qawm Laa Yuuminun Billahi<br />
Wal-yawmil Akhir”<br />
Qur an: 12:39<br />
7.
DAAWA ILALLAH:<br />
Mwisho akawatajia Mnyezi Mungu khalafu ndo akawafasiria<br />
tena. Hii ndo kazi ya Muislamu. Da-awa Ilallah siku zote kwa<br />
nyendo zake, kwa maneno yake, kwa vitendo vyake, kwa mawaidha<br />
yake kwa kila namna zake yeye anaupokea Uislamu. Anapita watu<br />
kwa njia nzuri kabisa, kwa hekma na mawaidha mazuri.<br />
“Id-u Ilaa Sabiili Rabbika Bilhikma wa Mawidhatan<br />
Hasana……..”<br />
“Kuja kwenye njia ya rabbu wako kwa hikma<br />
na mawaidha mazuri”.<br />
“…Wajaadilhum Billati Hiya Ahsan…”<br />
“Usishindane nao illa kwa namna iliyo njema kabisa”<br />
“…Qul Haadhihi Sabilli…”<br />
“Sema hii njia yangu”<br />
“…Ad-u-llahi <strong>Al</strong>la Baswiratu Anaa wa Mamit Tabaan”<br />
“Na ita kwa Mnyezi Mungu, juu ya utambuzi kwa fikra,<br />
kwa mipango kwa kujua ntafanya nini, na hii kazi hii mimi<br />
anaenifwata”.<br />
Basi ndo kazi ya Muislamu tena madamu yuko duniani hali<br />
haonywi basi atakua kama watu wabaya anajua ataepukana nayo<br />
kadri anavoweza. Mema anayajua atayafuata kadri anavyoweza.<br />
Lakini Mission yake kubwa ni Da‟awa Ilallah – Propagation kwa<br />
kiasi chake anachokijua na uwezo wake na uhodari wake na alicho<br />
nacho basi kila State ikitokea haya.<br />
Nakumbuka kuna State nyingine nikipata fursa mpaka<br />
kwenye Radio nikisikilizwa mtu aseme khabari za kwao. Bila shaka<br />
nikisema khabari za kwetu nayo ni Zanzibar na wao ni watu wa<br />
Dini nyingine. Anataka kujua Dini gani – Uislamu, Uislamu ni nini,<br />
unawaambia na kuwaeleza na unawafahamisha na kuwaonyesha vile<br />
utofauti uliopo baina ya Uislamu na Ukrito.<br />
Si kwa kuponda kiasi ya kua wajue tu nini kiliopo kilicho<br />
kikubwa kilicho tofautisha bila shaka, kikubwa kilichotofautisha ni<br />
8.
itikadi ya Wakristo kua Nabii Isa ana uungu. Waislamu wanakataa<br />
yeye ni Mtume tu pamoja na wengine Illa yeye kaitwa na Mnyezi<br />
Mungu:-<br />
“…Abdullahi wa Rasuluhu wa Ibni Ammatihi Wakalimatuhu<br />
<strong>Al</strong>-qa-ha Ilaa Maryam Waru-hum-minhu”.<br />
Basi mambo kama haya inapatikana fursa. Illa nakumbuka<br />
hivi hivi nilipofika Noxivil, ilisadifu Jumamosi wakaniambia kua<br />
kesho Jumapili tunakwenda katika Kanisa na wao kule ni katika<br />
wakubwa wa Kanisa, “Jee! utatufwata?” Nikawaambia<br />
intakufwateni, nyie mtakwenda na yenu na mimi ntakwenda na<br />
yangu.<br />
Nilipokwenda nkasikia mkubwa wao ananadi kua tumepata<br />
mgeni na si wa Dini yetu na tutampa yeye fursa atoe Sermon,<br />
Aprichi – haya jazaa kheyr. Nikasimama nikatoa nikaprich kitu<br />
kikubwa. Kulikua Nigroes wengi, ni mji wa Wanigroes walo na sura<br />
nzuri wanaoendesha mambo yao na kila namna. Basi nikawatajia<br />
bila shaka mwanzo wa usawa wa Kiislamu bila shaka mwanzo ule<br />
Uislamu hauna nani weusi nani weupe kama Kanisa – Msikiti wa<br />
weusi na weupe. Hapo ndo nkapatiwa fursa ya kuisoma kama<br />
kungineko, kokote kuisoma aya:-<br />
“Yaa Ayyuhanaas Innaa Khalaqna-kum Min<br />
Dhakarin wa Untha…”<br />
“Enyi watu hakika sisi tumekuumbeni wanaume na<br />
wanawake (wengine wakatafsiri) kutokana na yule yule<br />
mmoja (Naby Adam) na mwanamke yule yule mmoja<br />
(Hawwa)”.<br />
“…Wajaalna-kum Shuuban wa Qabaaila<br />
Litaarafu…”<br />
“…Tukakujaalieni “Nations” na “Tribes” na kabila<br />
kubwa na kabila ndogo ndogo mkaongeza nchi na<br />
kabila katika nchi mpate kujuana msaidiane (mjue<br />
namna ya kukaa pamoja msijiweke Divisions au<br />
Labour)”<br />
Qur an: 49:13.<br />
9.
“…Inna Akramakum Indallahi Atqa-kum”.<br />
“…Mtukufu wenu kwa Mnyezi Mungu ni yule mcha<br />
Mungu kuliko nyote. (Hali hii watu hufasiri wakaona<br />
kama hapana namna nyingine za kutukuzana illa ni<br />
utukufu tu)”.<br />
Qur an: 49:13<br />
Kuna maneno mengi ya Kiislamu “Akram” na si Akram tu<br />
kuna “Ashraf” haikusemwa “Inna Ashrakum” bila shaka<br />
Afdhwalakum maana yake mbali. Maana ya Qur an inakata<br />
kuzingatiwa – Kila neno lina maana yake na pahala pake na uzito<br />
wake.<br />
Na katika khutba nilizokua nikitoa huko Marekani kuonyesha<br />
Uislamu nilitumia aya hii kuonyesha kua sisi hatuna ugomvi na<br />
wakristo kwa kusoma:-<br />
“Qu-lu Amanna Billahi wa Maa Unzila A Layna wa<br />
Maa-Unzila Ila Ibrahima wa Isma-iila Wais-haaq<br />
wa Yaa-quuba Wamaa-utiya Musa wa Isa<br />
Wamaa Utiyyiina Min Rabbihim”.<br />
Inatwambia:-<br />
“Semeni:- Tumemuamini Mnyezi Mungu, tulicho<br />
teremshiwa na kilichoteremshwa kwa Ibrahim na Ismail na<br />
Is- haq na Yaaqub na wajukuu. (Wamaa Uutiya Musa) – na<br />
anayopewa Musa wa Isa – (Wamaa Uutiyyan – Nabiyyuna<br />
Min Rabbihim) wanayopewa na Mitume kutokana na<br />
Rabbu wao. Yote tumeyaamini kua yameletwa na Mungu:-<br />
(Laa Nufarraqu Baina Ahadin Mini- hum). Hatufariqishi<br />
baina yeyote katika wao, (Wa Nahnu Lahu Muslimu) na<br />
sisi kwa Mnyezi Mungu tumeslimu”.<br />
Qur an: 3:84.<br />
“Fain Amanu Bimithli Maa Amantum Bihi Faqadih<br />
Tada Wain-Tawallaw Fainna Maahum Fii Shiqa-qin<br />
Fasayakfiikahumullah wa Huwas-Samiiun <strong>Al</strong>iim”.<br />
Qur an: 2:137<br />
10.
“Basi watu hao (Manasara na Mayahudi) kama mnavoamini<br />
(nyinyi) itakua kweli wameongoka na wakikengeuka<br />
(wakikupa mgongo, nyongo) basi wao wapo<br />
katika upinzani tu. Basi Mnyezi Mungu atakulinda na<br />
shari yao, nao hawatakudhuruni kitu-(Wa Huwa-<br />
Samiiun <strong>Al</strong>ym) na ndo mwenye kusikia na mwenye<br />
kujua. (Sibghata – llahi) – hiyo radhi ya Mnyezi<br />
Mungu kisha ipanga katika nyoyo za waja, hiyo<br />
Sibghat llahi ni Babtism ya Mungu Ka-precise kua<br />
ambae kwa Wakristo Sharti Abatizwe.<br />
Padri ambatize mtu. Na unaona katika Uislamu laa - Mungu<br />
mwenyewe anakubatiza. Mambo ya Roho hayo Bin Adam<br />
mwenzake hayagusi. Mnyezi Mungu anasema, ukimwamini kuna<br />
Mjarad wa kuamini namna hiyo tu. Kama inavohitajiwa uamini<br />
Mungu mwenyewe. Amma kubatiza.<br />
“…Waman Ahsan Mina-llahi Swibghata wa Nahnu<br />
Lahu A-bidu-n”.<br />
“Na mimi mwema zaidi kuliko Mnyezi Mungu<br />
kwa Swibgha, na sisi kwa yeye ni wenye kumuabudu”.<br />
Qur an: 2:138.<br />
Mtu mwengine akutengenezee wende ukamuabudu<br />
mwengine. Akufanye unafaa-kuabudu, wende ukamuabudu<br />
mwengine. Huyo huyo unofaa kumuabudu ndiye ataekutengeneza<br />
akupokee, atengeneze mambo yako, kuonyesha Utolerence wa<br />
Uislamu, kukaa pamoja na watu wa dini nyingine kama Qur an<br />
inavyosema:-<br />
“Walaa Tujaadil Ahlil – kitaab Illa Billati<br />
Hiya Ahsan”.<br />
“Usijadiliane na watu wa chuo illa kwa namna iliyo<br />
nzuri (watu wa chuo Yahudi na Kristo) ilaa kwa namna<br />
iliyo nzuri kabisa”.<br />
Qur an: 29:46<br />
Haya katika Radio, katika Maklasi, katika mashangwe katika<br />
kila pahala mtu akipata fursa anatoa aya hizo na aya zinginezo<br />
11.
waafikianazo.<br />
“Wa Qu-lu A-manna Billahi Unzila Ilayna Wamaa<br />
Unzila Ilykum Wailaahana Wailaahukum<br />
Wa-hid Wanahnu Lahu Muslimuun”.<br />
“Na useme tumeamini ambacho kilichoteremshwa<br />
kwetu na kilichotelemshwa kwenu nyinyi<br />
na Mungu wetu na Mungu wenu ni mmoja na<br />
sisi kwa yeye peke yake tumesilimu”.<br />
Qur an: 3:84<br />
Hiyo ndiyo Qur an tukufu tuliitumia sana. Nikitoa khutba<br />
katika Lottery Clubs katika Clubs za namna kwa namna na vikundi<br />
vya wanawake, mjini na mashambani kuna Associations za<br />
wanawake na mambo yao hayo, nkawaambia khutba.<br />
Mtu bila shaka nkaonyesha kuona wapi katika Uislamu<br />
katika hayo nkawaambia ulietajwa kwa uzuri katika Qur an kuliko<br />
zaidi kuliko Sayydatna Maryam na wanadhania kua yeye anavunjwa<br />
na Uislamu. Waislamu ni mtu wao mamake Mtume na anatajwa<br />
ndani ya Qur an vizuri kabisa.<br />
Sadatna Maryam na alivotajwa vizuri katika Qur an hakua si<br />
chochote illa ni Mamake Naby Isa aliyeambiwa kua amemzaa hali<br />
ya kua yu Bikra inatosha sikwambii miujiza yake. Tunda, siku si<br />
zake mengine na wema wake katika Lottery inataka wasaa kusema<br />
na Politician wakubwa wakubwa. Kusema na watu juu ya mambo<br />
makubwa unawaambia hatari ya Colourbar Discrimination si kwa<br />
kuwatukana wala kuwaogopa, kuwaambia hatari unafanya hatari<br />
yaani kama jeuri.<br />
Mmarekani mmoja anainua kidole namwambia Mmarekani<br />
aache Colorbar aache kwa mmoja Myahudi alikua katika Group<br />
yetu akaja akawaambia mngekua mnajiona we mwenyewe<br />
unapokua unasema-ajabu. Na alil-hasil fursa hizo zimechukulika<br />
Insha-<strong>Al</strong>lah zisifutike ziwe zimethbitika.<br />
Khutba kadhaa wa kadhaa nimejaribu kuzikumbuka mambo<br />
makhsusi yalosemwa–Maelezo makhsusi yalokamatana na Uislamu<br />
ambao ulikua nao – Hawafahamu nimejaribu kuwafahamisha kadiri<br />
ya uwezo nimekwenda hata tukafika pahala, hapo kuna Camp kuna<br />
vijana wa Jamal – kadhaa wa kadhaa wameekwa hapo wageni wa<br />
Vice Chairman wa Serikali ya Kimarekani, tukachanganishwa<br />
12.
nao sasa yule aliyetuchukua Marekani akasema kwamba: “Naona<br />
kama kwamba Jumapili hii Wakristo wasiende Kanisani – badala<br />
yake watachanganyika na Waislamu na Mayahudi pamoja wafanye<br />
jambo la kiibada pamoja.<br />
Kila mtu asome kitu katika Dini yake. Mayahudi wasome<br />
Taurati, Wakristo wasome Zaburi na Dua ya Zaburi na Waislamu<br />
wasome Qur-an. Mambo yafanyike ki-njia ambayo Wayahudi<br />
hawatowaudhi Waislamu wala Wakristo. Na Wakristo watafute vile<br />
vile kwamba hawatakwenda kinyume na Waislamu na Wayahudi”<br />
Wakatupa shauri hilo, mimi nikamwambia yule Kijana wa<br />
Kimasri Muegyptian kua apande ahubiri, yeye afanye kazi ile, lakini<br />
akakataa . Mimi nikamwambia: “Lakini lini wataisikia Qur an na<br />
hatuna woga wowote wa kuonyesha kua Qur-an ndio sawa<br />
kuonyesha kua Qur-an itafunikwa au itazidiwa kabisa ndo sawa<br />
kuonyesha kua ndo kitabu cha Mnyezi Mungu hasa cha kweli<br />
kweli”. <strong>Al</strong>ipokataa mimi nikafanya, wale walosoma vitabu vyao na<br />
dua zao hapana alothibitika. Quran iliposomwa na aya gani<br />
ilosomwa.<br />
“Walaa Tastawi-l Hasanatu Walas Sayyiatu Id-Faa<br />
Billati Hiya Ahsan Faidhal Ladhi Bainaka wa<br />
Baynahu Ada-Watan wa Maaka Annahu Waliyyul<br />
Hamiid Yulaqi Qa-ha Illa-ladhiina Swabaru<br />
Wamaa Yulaqqa-ha Illa Dhu-Hadh-Dhin Adhiim”.<br />
Hiyo ndiyo Qur an, ni Aya mbili hizo zilizosomwa. Haiwi sawa<br />
Kiingereza ikifasiriwa:-<br />
“It can never be equal evils and virtue it will never be equal”.<br />
Tenda kwa lilo zuri kabisa jema kabisa, mtu akifanya ovu hutafuta<br />
lilo jema kabisa atende. Push away what whatever is the best<br />
what is the worst and all of a sudden that one who was your<br />
bitter enemy between you and him you will discover he has<br />
turned into a faithfull friend almost – irreletive. Mlipe mema<br />
mara utamuona amebadilika amekua rafiki mwema. Wala<br />
hawakutanishwi na hayo illa wenye kusubiri wala hawakutanishwi<br />
na hayo illa wenye fungu kubwa kwa Mungu.<br />
“Laa Ilaha Illallah wa Maa yulaqqa-ha Illal ladhina<br />
13.
Swabaru wa Maa Yulaqqa ha Illa Dhuhadh-dhu<br />
Adhiim”.<br />
Wameathirika utastaajabu kabisa, ajabu mmoja Mmarekani<br />
akanijia akaniambia: “Is that the Qur an?” Nikamwambi: “O<br />
yes, there is a lot in that”. Nkamwambia-mmekawia kujua.<br />
Ni moja katika mambo yalotokea halafu akanijia yule<br />
Muegyptian akaniambia “You, anta adhym, anta tahmil<br />
elamaana”. Nikamwambia: “<strong>Al</strong>hamdu-Lillah”. Basi<br />
tukaondoka hapo tukasogea mbele pengine. Mtu asome aya<br />
katika katibu chake inahitajia asome na Dua ya Kitabu chake<br />
mimi nilichagua Aya hii:-<br />
“Rabbana Laa Tua-khidhna innasiina Aw-kh-twaana<br />
Rabbana wala tahmil elayna iswran kamaa hamal<br />
tahu ala-lladhina min Qablina Rabbana wala tahmilna<br />
maa Laa Twa-qata Lala bihi wa af anna-waghfir lana<br />
war hamna Anta Mawla-na fan-Swurna alal-qawmil –<br />
ka firiina”.<br />
“Bwana wetu, e! Rabbu wetu usitupatilize tukisahu au<br />
Tukikosa e! (Rabbu wetu) usituchukulie uzito kama<br />
ulivowachukulia walio kabla yetu usitubebeshe<br />
tusioweza kuyachukua yalo mazito kwetu ya Rabb<br />
utuafu utughafirie uturehemu we ndo ulo tawalia<br />
mambo yetu utunusuru juu ya watu (Qawm) yenye<br />
kukufuru”.<br />
Hiyo Amerika katika Camp ile ilikusanya watu namna kwa<br />
namna. O! our Lord, kwa hakika nilifasiri Lord, hapana neno<br />
jingine lililotumika sana kwa Rabbana kama Lord, lakini haina<br />
maana ya Lord peke yake yaani ina maana nyingine. Creator<br />
Envoilver Lord Prossessor – kila kitu kimo katika neno Rabb –<br />
Avenger – mtengenezaji, kama sisi, kwa kiswahili utasema<br />
mtengenezaji, katutengenezea yote. Rabb ukifasiri, “Bwana”<br />
haitoshi hata kidogo au si Wafaransa “Laa tua-khidhna in nasiina<br />
aw-akhtwaana”.<br />
Maana Muislamu makosa yake yanakuja kwa kusahau,<br />
anarukwa na akili anasahau. Huo ndio Uungu, anasahau Pepo<br />
anasahau alokatazwa kwa kufanya makosa kama ilivyodhihiri kwa<br />
14.
Babu yetu, Mzee wetu Adam. Akikumbuka anarejea anasikitika na<br />
anamuomba Mungu asimchukulie. Muislamu mwema, kinyume<br />
mbaya hutampa kufanya ni fahari huyakimbilia akayatengenezea<br />
tena.<br />
Basi unataka ujue kua hapana haya kwa kucha kwa Dini zao<br />
nyingineo, kwanza kwa Kikatholic lazima wende wakamtafute<br />
Priest. Akupe kurudi halafu ndo usamehewe kwa wasta wake.<br />
Wanaita wenyewe To Confess! kukubali ubaya wake mtu.<br />
Kiislamu hapana, unakubaliwa na Mnyezi Mungu na<br />
unamuomba asikuchukulie. Basi mpaka mwisho hapo ikaja<br />
mizunguko tena tulikokwenda.<br />
Sasa si sharti niseme kwa mujibu wa taratibu uliopita lakini<br />
kwa namna yoyote ile kwa kiasi ntavyokumbuka tulipofika New<br />
York usiku tulichukuliwa tukatiwa katika Meli tukaitizame New<br />
York kwa nje Baharini. Inatisha, ina haiba inapendeza Sky Scrapers.<br />
Majumba ya mamia makumi kwa makumi, Ghorofa mia na kitu<br />
Mataa jumba la United Nations, na hii inaathir sana kuonyesha Bin<br />
Adam vipi anaweza kutumia uwezo aliopewa akafanya kazi akafikia<br />
hali ile.<br />
Jitihada yao yote watu fikra nzuri juu ya Marekani na kwa<br />
sababu hiyo ndo maana nyumba tulizokaa nyingi mimi nafsi yangu,<br />
nyumba nilizokaa ni kumi na nane. Kumi na sita ndani yake hakuna<br />
hata tone la ulevi, na wanavunja ulevi vile vile, ili kutaka<br />
kutuonyesha ya kua wako watu hawalewi huo Amerika. Akili yao<br />
imewaambia ulevi una hatari na si wa kutumiwa kwa sababu ya<br />
uzima, kwa sababu ya akili, kwa sababu ya mwili.<br />
Basi na huku vile vile kila wanalolipata na kutufanyia wema<br />
kwa kadiri wanavoweza katika majumba. Na hivi hata huko South<br />
Atlanta imewekwa nao kwenyewe kulikuwa ndo wakati huo<br />
kwenye Racial Discrimination kubwa – Colorbar – na niliwekwa<br />
katika nyumba ya mmoja katika weupe wenye hadhi lakini alikua<br />
haamini hayo.<br />
Wakanitazama vizuri, mwisho wakanifulia nguo zangu.<br />
Wakaniniuliza wenyewe nguo zako za taka ziko wapi, hebu lete.<br />
Ndivo walivo hao juu ya majumba hayo, watu namna nyingi katika<br />
nchi moja na wako wengine wakikutizama unaona kua<br />
wanakutizama kwa jicho la adhabu.<br />
Basi tukenda tukafika New york tukaingia katika meli<br />
tukaingia katika Bahari. Nilipoona nikakumbuka Qur an kama Aya<br />
15.
<strong>Al</strong>iyoitumia Sayyidnal Imma Sheikh Abdo Bakathir Abdallah Bin<br />
Mohamed Bakathir Sheikhe wa Mashekhe zetu <strong>Al</strong>eyhum<br />
Ridhwaanullah, alipokuja akaonyeshwa Aeroplane mwanzo inapita<br />
Aeroplane watu katika Zawiya yake akatolewa alipoiona<br />
hakutaharaki wala lolote alisema.<br />
“Falamma nasuu maa dhukkiru bihi fatahna lahlim<br />
Abwa-ba shiy hatta idhaa farihu bi maa uwtu<br />
akhadhnahum baghtatan faidha-hum mublisun<br />
faqutwi a daabiral qawmul ladhiina dhwalamu-wal<br />
hamdu Lillahi Rabbil A-lamina”<br />
Ikanijia Aya hiyo na nikaisoma:-<br />
“Waliposahau hayo walionyeshwa kwayo tuliwafungulia<br />
Milango ya kila kitu (<strong>Al</strong>lah Akbar) hata walipokwisha<br />
furahi kwa waliyopewa tuliwachukua kwa ghafla (Adhabu<br />
ikaja kwa ghafla) waka haribikiwa kwa ghafla”<br />
Kama tunavoona mambo ya Kiulaya huja yakenda kama bofu<br />
likawa juu hivi mara likapasuka vita au nini au nini.<br />
“…Faidhaahun Mublisuun”. mara wamekata tamaa hata kusema<br />
hawawezi. Wamekaa tu nyuma ya watu wenye kudhulumu wenye<br />
kuweka mambo si pahali pao ndo maana ya dhulma. “Dhulma”<br />
wanaweka kitu si mahali pake <strong>Al</strong>-Hamdulillah. Basi nilipotizama<br />
pale ilinijia Aya hiyo nikaisoma:-<br />
“Falamma nasuu maa dhukrini bihi fatahna lahum<br />
abwaaba kulli shiy hatta idhaa farihu bima uwtu<br />
akhadha hum baghttan faidha-hum mublisuna<br />
faqutwia daabral qawmil ladhiina dhwalamu wal<br />
Hamdu lillahi Rabbil A-lamiina”<br />
Yule Muegyptain akamwambia yule Mmarekani:<br />
“Mwambie akutafsirie Aya hiyo”. Nikaona taabu kubwa. Hawa<br />
wenyewe masikini wanataka waonyeshe kua hapana watu kama<br />
wao. Wamefika pakubwa pa kukua, hii Aya inaonyesha wapuuzi<br />
kabisa na wako katika hatari. Nikamwambia: “Haya we mtajie”,<br />
16.
Akaniambia: “Hapana usikubali”. Akashikilia, nikamsafiria<br />
akanywea. “Basi twende zetuni” Imekua yale aliyoyataka siyo yale<br />
aliyoyapata. Qur an mimi sina mastaajabu na kua kuna kitu<br />
kushinda Qur an na iko pale hata kitu kimoja. Kila kitu kiko pale.<br />
Haya tuliporudi New York tena.<br />
Sasa mimi nafikiri kua afadhali sehemu hii niifanye Part one<br />
hii niliokwisha sema nikae nifikiri namna ya kukaabili sehemu<br />
nyingine. Safari hii ya Amerika ilikua safari ndefu ina karibia miezi<br />
mitatu, kwa hiyo ndiyo ina mambo kadhaa wa kadhaa”.<br />
17.
SEHEMU<br />
YA<br />
PILI<br />
18.
SAFARI YA PILI AMERIKA:<br />
“Tuliingia mji wa Nishilin na kila mtu akawekwa katika<br />
nyumba fulani, mimi nikawekwa katika Fiski University – pamoja<br />
na President wa Unit Squad Farsuk University pamoja na<br />
President wa hiyo Fiski University alikua ndo anahishimiwa kabisa<br />
New York na ni Mnegro. Hapo alikua na mkewe vile vile wote<br />
watu wahishimiwa sana. Ndo mwenye nyumba nzuri kubwa kabisa.<br />
Wakati wa kula akanambia “Jee! Grace?”; Wakristo<br />
husema kabla ya kula, inaitwa “Grace”, sisi Grace yetu ni:-<br />
“Bismillahir-Rahmanir-Raheem”. Hii ndo kwa ufupi, lakini watu<br />
wajuao kuna vitu zaidi katika vinavosemwa kabla ya kula, lakini<br />
hilo niliona ni refu na “Bismillahir-Rahmanir-Raheem” inatosha<br />
nikafasiri kwa Kiingereza:-<br />
“In the name of God the most compassionate the<br />
most merciful”.<br />
“O! hii sasa tutakua tukiitumia hii inatosha kabisa”. Na<br />
wanao wanafunzi walotoka nchi nyingine za Kiislamu katika<br />
University yao. Baada ya kula wakaniambia vile vile niseme kitu<br />
cha kushukuru kama wanavyofanya wao nikawaambia, siye yetu<br />
nyepesi tunasema:- “<strong>Al</strong>-hamdulillahi-Rabil-alameen”. “Haya<br />
sema” nikawaambia:-<br />
“<strong>Al</strong>l praises are due to God - the Lord the Evolver<br />
of the Universe the Sustainer of the Universe”.<br />
Tukakaa mwisho tukaondoka. Ajabu, namna walivyokaa na<br />
mimi kwa uzuri, mwisho wa mtu kukaa na mtu kwa uzuri sana, tena<br />
hawanijui mwanzo wala mwisho - tena kwa vizuri sana. Nikitaka<br />
kuondoka wemekataa, “Usiondoke”. Hatimae nikaondoka kama<br />
desturi ilivotengnezwa katika Programme.<br />
Nilipofika London nimewaandikia barua, katika barua<br />
nikasema nikatia maneno ya Kiarabu.<br />
“Maa Fil Maqaam Lidhyl Aql Wadhil Adab”<br />
19.
“Hapana katika kukaa moja kwa moja usisafiri kwa mwenye akili na<br />
mwenye adabu, anaetafuta adabu namna ya kuishi vizuri duniani.<br />
Safiri, katika safari kuna faida tano:-<br />
i. Tafrijil Ham - Kutokwa na hamu,<br />
ii. Wa Kasbil Maaisha - Na kuchuma maisha. Mimi hapa<br />
nimeondoka na suti mbili nzuri<br />
kabisa - first class - katika maduka<br />
yaliyo bora kabisa.<br />
iii. Wa Ilmun - Na Ilmu. Huyo alikua Sociologist<br />
mkubwa ana vitabu kadhaa<br />
vya Sociology.<br />
iv. Wa a-dabun - Na adabu, namna ya kujua kukaa na<br />
watu na kusema na watu.<br />
v. Wa Sub-hati Maajidin-Na Sub-ha ya Watu Watukufu.<br />
Watafrijil Ham, Waktisaabul Maa-i-sha, wa Ilmun, wa<br />
A-da-bun, Nikaja nikafasiri kwa Kiingereza, halafu katika barua ile<br />
nikaandika kwa Kiingereza, mambo yote matano hayo nimeyakuta<br />
katika nyumba moja, nikamwambia:-<br />
“Is n‟t it wonderful that one could find all those five<br />
under one roof?.<br />
“<strong>Al</strong>aysa Ha-dha Ajaban Annal Insaan Yajid Hadhal<br />
Khamsa Tah-ta Saqf Wahid?”.<br />
Akaniletea barua akasema:- “Usiseme hivyo, kwenu kwa pili huku, njoo<br />
tena”. Mimi sikwenda njia hizo tena, nilikwenda Amerika tena lakini<br />
sikwenda upande huo, ni ajabu mtu kuyakuta yote matano haya mahali<br />
pamoja. Na ziko nyingine zinahimizwa kusafiri kama:-<br />
“Sa-firu fainna fil Asfa-ri tajid iwadhan<br />
amman tufa-riquhu”.<br />
“Safiri utapata badala ya yule uliyemfariki”.<br />
Wa Ansub (Ujitayarishe) Fa Inna Ladhatil Maaisha (Utamu wa<br />
maisha), Fin nusub (katika tabu), Inni ra-aytu fi Khisaai fil maai<br />
yufsiduhu (Mimi naona kusimama maji huyafisidi), In-sa-la Twabahu<br />
(Hua mema yakichuruzika yakiteremka), Twa-ba (Hua mema<br />
na yakitulizana huharibika), Muftalasatwal usud law laa Firaqu<br />
20,
Lagha-b-masim-ba Law (Ingekuwa hawajafariki vichaka<br />
wasingepata visindika). Wal-ud fi ardhiha Naw-un minal hatwab<br />
(Na udi pahali pake ni namna tu ya mti katika miti na ukiondoka<br />
pale ndo unatiwa ndani ya moto unatoa harufu nzuri). Watu<br />
wakihimizwa sana kusafiri lakini safari haijaachwa kua taabu “Qitatun<br />
minal adhab” yuko mtu mmoja anasema:-<br />
“Balil Adha-b qit-a minals safar”<br />
“Bali adhabu ni sehemu ya safari”<br />
Na zamani ilikua raha yake kubwa ya safari mnafwatana<br />
mnakua ndugu wamoja, kitu kimoja, mnasaidiana mnashirikiana<br />
mnaona raha katika safari, mnokofika mnapokewa kwa wema, sasa<br />
watu wote kila mmoja kashughulika na lake. Hilo ni moja katika<br />
pahala pamoja tulipowekwa.<br />
Sasa tulipokua huko New York tuliwekwa nyumba inaitwa<br />
„International House‟. Siku moja nimekaa nje pale ninamuona<br />
Mmarekani mmoja kaingia na karatasi anadhania “Islam and<br />
Religion” (Islam na Dini) nikasema huyu amedhania Uislamu si<br />
Dini? nitajaribu kiasi nnachoweza kumfahamisha kua Uislam ni<br />
dini; tena ni dini kuliko dini nyingine zozote bali mbele ya Mnyezi<br />
Mungu hapana inayoweza kuitwa dini illa Uislamu.<br />
“Innad-Deena Indallahil Islam”<br />
“Hakika dini kwa Mnyezi Mungu ni Uislamu)”.<br />
Qur an: 3:19.<br />
Si kwa kua tunaambiwa na Qur an tu, lakini mafundisho yake na<br />
namna zake na maisha yake inaonyesha dini ya kweli, na kwa<br />
Mnyezi Mungu ni Uislamu.<br />
Basi nikaanza nnaingia ninamfahamisha tukenda mpaka<br />
njiani akaniambia: “Basi, basi, mimi ni Muislamu mwenzako, hii<br />
khutba nnakwenda kuitoa YMCA, na namna ulivonieleza, wewe,<br />
naona wewe utaeleza vizuri kuliko ntavoelezea mimi kwa hivo<br />
wewe utakwenda ukaitoe khutba hii na ili nisiikose hukai hapa tena<br />
utakuja kukaa nyumbani”.<br />
Nikamwambia si kitu lakini mimi nimewekwa hapa.<br />
Akawapigia simu walioniweka, yeye yule akataka kujua mie<br />
nimekubali, akanipigia simu akataka kujua Adresi, akapigiwa na<br />
21.
simu kua niko huko nyumbani nnakokwenda nkakae. Bila shaka<br />
nikakaa akaja na mimi nikaenda nikahamia. Namna tulivyozoeana<br />
kwa muda mchache. Akastaajabu vipi Mmarekani si Muislamu ama<br />
mnaona leo udugu wa Kiislamu, nikamwambia laa ni udugu wa<br />
Kiislamu:<br />
“Innamal Muuminanuna Ikhwana”<br />
(Hakika si jinginelo ni kuwa waumini wote ni ndugu)<br />
“Fa Aslehu baina Akhawaykum”<br />
“Patanisheni baina ndugu zenu”<br />
Qur an: 49:10.<br />
“Wat Taqul Llaha……..”<br />
“Na wamche Mnyezi Mungu”.<br />
Nikamuuliza wakati mmoja alikueko, ajabu, akiitwa Bwana<br />
kheri ni jamaa yake Marehemu Maallim Mohamed Ahmed wa<br />
Zanzibar anafanya kazi Melini. Nilipopata kuja London nikamuuliza<br />
pana watu wa Kingazija huko. Akanipa Adresi, Mohamed Ahmed<br />
Jae. “Laa Ilaaha Illal Lah” Akanipa Adresi kwa kua nikienda<br />
Amerika nitajaribu kuuliza nayo ni kuuliza tu. Lakini pahali kama<br />
Amerika, Umtafute mtu wapi!.<br />
Huyu nilipomuona Muislamu nikasema nitamuuliza alaa<br />
kulli hali. “Oo! yule Mzanzibari?” Hakujua kuwa ni Mngazija au<br />
Mnini – maadam katoka Zanzabar basi ni Mzanzibari akasema<br />
“Utamuona lakini kwanza twende tukakae nyumbani asije<br />
akakuchukua. Tukakaa akatengeneza khutba yake, akamaliza.<br />
Akaniambia “leo tutakwenda, <strong>Al</strong>khamisi usiku utamuona pahala”.<br />
Tukaenda katika majumba ya Sky Scrapers moja za New York tena<br />
kuna Maulidi wanasoma kila <strong>Al</strong>khamisi tukafika kwenye “Yaa<br />
Naby Salaam <strong>Al</strong>ayka Yaa Rasul Salaam <strong>Al</strong>ayka” nikamwambia:<br />
“Amma wewe Yaa Naby umefika mbali mpaka Huku!”.<br />
Baada ya Maulidi yule Mzee yuko hapo. Huyo Mzee<br />
mwenyewe Mruwada wa Jumbe Fumu. Nikamwita huyo mtu wa<br />
huko nikisikia mtu ananiambia. “Huyu mtu wa huku lakini<br />
anaonyesha Mngazija”. Nikamwambia: “Wee nani?” akaniambia<br />
“Mimi Mruwada wa Jumbe Fumu”. “Nani jamaa zako?”<br />
22.
“Mahmudu wa Jumbe Fumu, ni katika walionilea Mimi, anaitwa<br />
Mahmudu wa Jumbe Fumu na wamenikhusu kwa upande wa<br />
ukeni”.<br />
Mtu akiitwa: Mahmudu Bin Kimwana Jumbe Fumu au<br />
Abdul-ghanii wa Jumbe ndo mwanzo akiitwa wa Jumbe Fum.<br />
Nikamwambia: “Hawa ndugu zako ndo walonilea!”. Basi pale pale<br />
akaanza kujifakharisha kwa wale – “Huyu mwanangu” – “This is<br />
my son I have rasied him, my Brothers have raised him”<br />
wamemnyanyua - yaani wamemlea – “He must come and stay with<br />
me (Aje nyumbani akae na miye), Na hivo twende zetu sasa hivi”<br />
Nikamwambia” “Haiyumkiniki nimechukuliwa kwa hishma na kwa<br />
azma, na azma zenyewe bado hazijatekelezeka, itakuwaje!” - Laa<br />
Ilaaha Illa llah - akakubali.<br />
Basi tukaenda mpaka baada kutengenezwa tena ikatiwa<br />
tukenda Maulidini, tukaenda tukafanya ile khutba ikawa Ghas-ya<br />
kwenye khutba. Kuonyesha nini Uislamu, ni kama khutba ile<br />
niliotoa katika – King Abdul-Azeez University – “What is Islam”<br />
Hii nimesema: “The real meaning of Islam” lakini ile nimesema<br />
na watu si Waislamu – iko tofauti sana.<br />
Katika niliowaonyesha usawa katika Uislamu na umoja na<br />
undugu nime Emphasise sana na yale niliokua nikielezea huko<br />
nyuma huko, na kwengineko kama: “Qu-lu, a-manaa Billahi<br />
wama unzila ilayna” (sema tumeamini Mnyezi Mungu na<br />
yaloteremshwa kwetu) – na hiyo – “Yaa ayyuhaa Naas inna<br />
khalaqna-Kum min dhakarin wa untha” – Sote ni namna hiyo<br />
hatujui sisi tofauti ya Rangi wala Nchi wala Nasabu – wala nini.<br />
Ikiwa kuna watu hawatumii, hawataki, pale mbali, lakini<br />
Uislamu umeamrisha kama hawaongei mawazo mengine ambayo<br />
watu hawayataki au hawawezi kuyafwata lakini wamejua Uislamu<br />
umeamrisha.<br />
Katika kuuliza ilipokuja katika usawa, kwenye usawa<br />
ilivokwisha ikaja suala, Akainuka Mnegro mmoja akasema “Wewe<br />
unasema katika Uislamu unasomesha Usawa mbona kuna watumwa<br />
katika Uislamu unakubali tu?” Nikamwambia “Ukristo<br />
hayakubaliwi hayo au hapana? wewe Mnigro umekujaje huku<br />
Amerika? umetekwa, umetiwa kamba, umetiwa katika atlantic<br />
Ocean, umefanywa mtumwa kwa nguvu, na hivi umeletwa huku,<br />
umeelimishwa umefanywaje!” Aaa! wakamvamia Wanegro<br />
wenzake wakamwambia – “We ndo wa kusema maneno namna<br />
23.
hiyo, maneno gani hayo!”. Nililetewa barua kua walisilim watu kwa<br />
sababu ya khutba zile zilotolewa YMCA.<br />
Tukarudi England lakini ilitokea ilikua na hamu sana kurudi<br />
kwa Meli. Kwa Meli kutoka New York mpaka Southampton, nilikua<br />
kila nnapokwenda naambiwa hapana Meli asilani sasa shauri gani?<br />
hata siku moja hiyo tukalala nikaona “Queen Elizabeth” Meli<br />
kubwa lile linakuja New York kutoka Southmpton (London)<br />
asubuhi nikaambiwa kua siku ya pili au ya tatu kuna safari, kuna<br />
Queen Elizabeth ipo, inatoka New York inakwenda London.<br />
Basi nikapanda Queen Elizabeth toka New York kwenda<br />
London bila shaka kwanza unafika Southampton. Meli pandikizi la<br />
Meli naona ni katika Meli kubwa zilokuweko wakati wake duniani.<br />
Ilikuepo “United States” ilikuwepo “France, Normandee”<br />
ilikuwepo Queen Elizabeth na Queen Mary!<br />
Sasa safarini tumo ndani ya Queen Elizabeth nikaona katika<br />
Atlantic Ocean Baharini kama Jabali katika Bahari nikauliza<br />
nkasema “Kuna Jabali katika Atlantic Ocean?” nikambiwa “Laa, ile<br />
ni Queen Mery inatoka Southampton inakwenda New York?.<br />
“Aajib, ni kama Qur-an ilivosema, Quran inasemaje?”<br />
“Walahul Jawaaril, Manshaa-ji Fil Bahri Kal<br />
Aalaam”<br />
“Na vitokuja kuzaliwa (havipo sasa) (Vitakuja kuzaliwa)<br />
katika bahari vitakua utadhani jabal”.<br />
Qur an: 55:24<br />
Nikaona Quran haijabakisha kitu “Walahuljawaaril Munsha-a-ti<br />
kal Aalaam fa Biayyi a-Laai Rabbikum a-tukadhdhiba (Ipi<br />
katika Miujiza ya Mwenyezi Mungu mnaikadhibisha?).<br />
Hata safari moja neno husemwa pamoja na neno jingine.<br />
alikuja Sheikh Shuayb, ndo alokua Mwanachuoni Mkubwa kabisa<br />
Uganda akaja Unguja. Kwanza alichukua Uislamu tu kwa Sheikh<br />
Abdus-Swamad, mmoja alikua zamani – Zama za Seyyid Ma-jid<br />
akenda kule. Mimi nimemkuta Mzee – Sheikh akaja akawa anataka<br />
kusoma hasa akataka kusoma “Mantiq” na ndo alosimamia Maulidi<br />
sana baada ya Shekh Abdur-Rahman Bin Aqeed – <strong>Al</strong>oyatia Maulid<br />
Uganda wakasilimu watu kwa maelfu siku hiyo.<br />
Mwanzo wa kusomwa Maulidi walisilimu watu kwa maelfu.<br />
24.
Watu walivosikia Matwari na nini, wamekimbilia<br />
kusikiliza na waliposikia khutba na kuona wameyumba,<br />
wamefanyaje, walipoondoka pale watu kwa maelfu wamekua<br />
Wailsamu. Hata wakataka kushitakiwa kua wamepiga ngoma<br />
kwa jina la Dini. Ikafanywa kesi – Seyyid Ahmed Ibn<br />
Abdur-Rahman akafanya, akasimamisha, akashinda.<br />
Basi tangu wakati huo wanaingia watu ndani ya<br />
Uislamu kwa Maulidi na Matwari. Wanavalia watu<br />
wanakwenda waganda wanavaa vizuri mpaka huenda<br />
wanakutana kutwa wanakaa pamoja wanasoma Maulidi,<br />
wanakula wanawafikiana, wanasilimu, wanaalika wakubwa<br />
wa nchi wanasheherekea.<br />
Mwanzo nilimuona Iddi Ameen huko katika Maulidi namna<br />
hayo pamoja na yule President – <strong>Al</strong>otolewa Karibu, walikuja<br />
pamoja punde baada ya Revolution ya Mutesa kabaka Mutesa –<br />
Mkutano mkubwa Sub-hana watu wanoshughulika na Uislamu na<br />
mambo ya kheri wanastarehe sana.<br />
Twayyib, basi alikuja Unguja ye Sheikh Shuyb lakini kaja<br />
baada ya kua kasoma namna hiyo tangu hapo – Fiqihi, kasoma na<br />
Nahaw, kasoma namna hiyo kasoma Mantiq na kiasi alivosoma,<br />
akaja mwisho akaja akachukua Twariqatish Sha-dhiliya<br />
Shurtwiya kwa Seyyyid <strong>Al</strong>y Bin Ammi yangu.<br />
Vile vile Seyyid Mohamed Bin Shekh El-Maaruf, Seyyid<br />
<strong>Al</strong>y ye yuko hapa hapa Babake She Hamadi. Hao wote Baba zao<br />
ndugu – yeye Seyyid <strong>Al</strong>y Bin Sheikh Seyyid Abdur-Rahaman na<br />
Babangu. Hata Sheikh Shuayb alipata kuniambia: “Nchi hii kama<br />
mmeekewa nyiye, Sayyid Abdur-Rahman kaja kaleta Maulidi,<br />
Sayyid <strong>Al</strong>y kaleta Twariqa-Sha-dhiliya, wewe umekuja<br />
umenisomesha”.<br />
Basi akaja nikamchukua Beyti-Ras kama unavojua baadhi<br />
ya watu – kumejengwa Msikiti mkubwa – mkubwa kwa sababu ya<br />
Watoto wa Boarding. Zamani Boarding ilikuwa Dole, na mimi<br />
nilianza kusomesha Dole mbali kidogo, Meli kumi unakwenda kwa<br />
mutkari halafu unakwenda kwa miguu. Au Bakhti yake upate gari<br />
ikuchukua mpaka juu huku pakiitwa Dole.<br />
Ikahamishwa halafu ikaja hapa Pwani Beyti-Rasi pahala<br />
Seyyid Saeed Bin Sultan alifikia hapo akitoka Oman, Zamani<br />
mwanzo akifika hapo pakajengwa skuli kubwa – Skuli Techers<br />
25.
Trining na Primary ni Dole Class na ikabidi uwepo Msikiti. Sheikh<br />
Shuayb alipokuja nikamchukua Msikitini nikamtaka atoe Mawaidha<br />
– Hodari wa kusema sana, Faswih na anajua kuchagua maneno, na<br />
nini; na mtu kakulia Uganda lakini anasema Kiswahili vizuri kabisa.<br />
Kaja akasema, pale ni iko karibu na bahari pale, ile Skuli na Msikiti<br />
uko karibu na Bahari, anawaonyesha ukweli wa Uislamu.<br />
Anawaambia “Tazama Qur an inavokwambieni unaona Meli<br />
zinavopitapita hapa nyiye mnastaajabu kua wazungu wamezua zile.<br />
Zile Mnyezi Mungu ameziumba kwa hikma yake; Akawasomea:<br />
“Walahul jawa-ril munsha-atifil fil bahri kal<br />
A‟<strong>Al</strong>aam”<br />
<strong>Al</strong>lahu yar-ham Sheikh Shuayb. Hiyo ndo ya njiani kwenda<br />
Southampton nikarudi nikaenda zangu London kuendelea na<br />
masomo.<br />
Kukaa London yametokea mambo mengi bila shaka,<br />
Mahudhurio Mikutano ya Waislamu, kufurahikia Maulidi, Sifa za<br />
Maulidi kuzifurahikia kushughulika kwa mambo kadhaa hata katika<br />
mambo niloyakumbuka siku za mwanzo mwanzo nilipokwenda<br />
nkayashughulikia.<br />
Mlokuemo katika Dini ni Miraji ilifanzwa London na mtu<br />
alochaguliwa atoe khutba mbele hapo – alikuwa Seyyid Ahmed Bin<br />
Kirami wa India akisomesha Skuli of Oriental African Studies.<br />
Nilikutana na Maalim Zuberi <strong>Al</strong>lahu yar-ham tukenda. Akasema<br />
akatoa khutba na kuonyesha Miraji kua imetokea na hawezi kuitia<br />
wasi wasi, mtu anajua uwezo wa Mnyezi Mungu na Mnyezi Mungu<br />
kusudi kaonyesha kua mambo haya si mambo ya kidesturi kwa<br />
kuanza kutaja kisa, kasema:-<br />
“Sub-hana ladhi asra bi abdihi layla, minal<br />
masjidil haram ilal masjidil-aqswaa”.<br />
Tazama Mnyezi Mungu kaanza kwa kusema “Sub-hana”<br />
katakasika na kila lisilo Laykiana na yeye – yaani msije mkajipima<br />
nyiye mkaona madam nyiye hamtaweza kujifanyia mambo haya<br />
ndo basi hayakufanyika. Haya yamefanywa na yule ambaye<br />
ametakasika na kila lisilolaikiana na yeye Kampeleka usiku mmoja<br />
Mtumwa wake, huyo Abdi wake Asra biabdih Yaani msiri wake<br />
alokiriana nae, yeye kamkiri kua ni Rabb na Rabb kamkiri kua<br />
yeye<br />
26.
ni Abdi wake – Anampa siri zake anamwendesha sio mwendo<br />
anaowaendesha watu wengine.<br />
Imetoka: “Masjidil Haraam Ilal Masjidil Aqswa <strong>Al</strong>ladhii<br />
ba-rakna hawlahu”. Akasema mpaka akalia akaliza watu<br />
nakumbuka ni katika mambo nlomuandikia <strong>Al</strong>-Habib Barua<br />
nilipokua kule na kitu kingine nilichomuandikia ni mkutano wangu<br />
na Yusuf <strong>Al</strong>y, Mkutano wangu na Yusuf <strong>Al</strong>y alo Translate Quran,<br />
na Translation yake ndo inohishimiwa sana.<br />
Nilikwenda nkamtafuta nnamuulizia nkaambiwa yuko<br />
England, wapi,! ikabidi nizunguuke nnamtafuta hata nkapambana,<br />
nkaambiwa nenda mahali fulani labda utamkuta.<br />
Hapo nkenda nkaonana nae - Ni klabu ya watu wanofanya<br />
kazi katika Empire, Empire Club. Nilipokwenda nikaonana na<br />
Receptionist akaniambia: “Je nani, yule Mzee anokaa pale afanzi<br />
lolote anajikalia tu?” Nikamwambia: unaona ni wewe tu kua<br />
kajikalia, ni yeye nnahaja nae. Nkaenda nkaja siku nyingine<br />
nikampata nikamwambi: “Nna haja na wewe”. Akaniambia: “Ndo<br />
wewe ndo unaekuja hapa ukiniuliza nimeambiwa?” nikamwambia<br />
“Naam” “Njoo unataka nini - Come <strong>Al</strong>ong what do you want?”<br />
“Sit down” Nkamwambia: “I have read your translation of the<br />
Quran and I was very much Impressed, very much indeed I<br />
Admire you”. I thought since you are here - still I must come<br />
and see you”. He was Old man <strong>Al</strong>most mystical, kua sufi mkubwa<br />
kawa na Mnyezi Mungu tu hata kusema na watu hasemi na watu.<br />
Akanambia “Naam - Yes you are right”. Nkamwambia: “Nadhani<br />
ulivokua ukiandika tafsiri ile umemuona usingizini Mtume mara<br />
nyingi”. Akanambia:-<br />
“Yes, and I saw him, I felt this was coming from<br />
Heaven to tell me what I should Write and I wrote<br />
that tranlation it took me three years to write the<br />
translation. I was going round and round, I was<br />
busy writing the translation and I visited almost<br />
every place mentioned in the Qur an in my attempt<br />
to write that translation”<br />
Nikamwambia: “What are you doing here, you are so old?”<br />
akanijibu: “Yes where shall I go? Lahor used to be a city of<br />
Islam, Now It‟s no longer. I have a small room here by myself<br />
27.
and literaly intersted in europe and here its easy for people to<br />
contact me”<br />
Ni ajabu namna ninavyoyakumbuka maneno yake,<br />
nimeyakumbuka very cleary na kwa kuya-repeat lakini nikayasema<br />
kwa namna clearly na Admiration yangu imenisaidia<br />
niyakumbuke maneno ndo ilivyo hivyo.<br />
Nikamwambia: “wewe ni mtu wa wapi asili yako wapi”<br />
akanambia: “Mimi ni mtu wa Yemen, Northern Yemen, Baba<br />
yangu alikua mtu wa huko, akaja India akawa mtu wa huko. Na si<br />
yeye tu bali hata Babu yake pia waliishi huko wakaowa, wakaishi<br />
huko”.<br />
Nikamwambia: “How did you manage to combine both<br />
types of Education – Islamic and European secular and<br />
Religion?” Akanambia: “Okey yes, I had a wise Father a learned<br />
person whose wisdom was greater than his knowladge, he told<br />
me: “learn anything you want but mind you would never find".<br />
He is wise who takes what is truth and leaves what is the<br />
incidental”.<br />
Hiyo ndo jawabu yake sasa nkasema kua – “Qur an<br />
imekusaidia sana. Watu walikaa kwa uovu na wewe, lakini Qu ran<br />
imekusaidia namna ya kukabiliana na watu. Aya gani imekusaidia<br />
sana kuliko aya zote?” Akanambia: “Suratil Fati-ha”.<br />
“There is northing like <strong>Al</strong>-hamdu, in the whole of<br />
World litrature”.<br />
Akawa anaingia, anaisoma akaisoma yote, akaisoma kama<br />
asili ilivyo, halafu akaifasiri. Halafu nikaona huyu Mzee leo<br />
nisimweke sana halafu nikija tena ataniona huyu mtu matata. Huyu<br />
afadhali nimuondoe njiani, nikamwambia leo basi afadhali tupige<br />
Fat-ha. “Unataka nini?” Nikamwambia: “General” akatia Fat-ha<br />
tukasoma <strong>Al</strong>-hamdu, akasoma yeye kwa sauti, unaona maana mpya<br />
inakuja kwa msomo wake Yusuf <strong>Al</strong>y <strong>Al</strong>lahu yar-ham.<br />
Siku nyingine tena nikamwambia vipi kwa sababu yeye ni<br />
Mwalimu wangu nikimuona mtu alokua akinisomesha Islamic Law<br />
mzungu Christian English akinistaajabisha nkamwambia: “Vipi<br />
duniani kuwa Prejudice namna hii. Mtu namna ile anatarajiwa<br />
aseme kitu haki tupu”.<br />
28.
“What don‟t you – you mustn`t be surprised to see<br />
people with prejudices… you and I have our own,<br />
let others have their own prejudices”.<br />
Katika maneno alonambia hapa basi tukaendelea hivo hivo<br />
tukicheka, tunazungumza.<br />
Wakati mwingine nikamuona hasemi asilani. Nakaa kimya<br />
namuuliza naona hajanitambua! Ananiambia “Nakutambua si yule<br />
anokuja hapa. “You come here from time” Nikajua leo hayupo<br />
afadhali niende zangu. Msafara wangu wote na yeye hapo<br />
nilipokwambieni karibu na Trafalgel Square. Afadhali niende zangu<br />
nikamwacha. Hayo ndo mambo yalopita nilipokua London.<br />
Mambo mengi yamepita ya mfahamisho baina ya Waislamu<br />
na Wakristo. Pameambiwa katika yalokamatana na Science,<br />
mengine yamekamatana na Politics. Mie kila nkipata nafasi<br />
kuonyesha Uislamu unasema nini nasema, naandamana na mikutano<br />
ya Eastend na mengineyo. Na siku zile kulikuwepo mahali<br />
panaitwa East African House ilikodiwa na nchi za East Afrika,<br />
vijana hupata mahali pa kwenda kupumzika, pakapatikana na<br />
mjumbe wa kukaa nikahamia huko huko. Pahali pazuri karibu na<br />
katikati ya London.<br />
Muda mwingi nilioupitisha London niliupitisha na mimi<br />
nakaa hapo, na halafu, unajua tena Waislamu na vikundi vyao, na<br />
tukikutana wengine wanatualika. Tulikua pamoja na Salim akiitwa<br />
Bwana Awadh Bin Salum Masud alikua akipenda mambo hayo ya<br />
dini, huyazungumza na kuyaeleza.<br />
Anakwenda tunakutana na watu wa Pakistan wapi wapi,<br />
wazee wengine wametoka Suudia Hijaaz. Wamekuja Madaktari,<br />
wazee wengine Madaktari wa zamani wa asili huja mara moja tu,<br />
<strong>Al</strong>ha-sil siku za fursa. Mpaka mwisho ikapita miaka ilopita<br />
tukafanya mtihani miaka 1 – 3 nilikaa kwa sababu ya kusoma hivo<br />
nikafanya mtihani ikabidi nirudi kwetu East – Africa.<br />
Lakini wakati nilikueko Ulaya kila Vication nilichukua fursa<br />
kwenda Ulaya. Nikisikia kuna Group mpya ya watu wanakwenda<br />
“Europe” nami „nikiwajoin‟ tukiingia pamoja kwenda kutembea,<br />
kwenda kutizama Qur an inasema nini. “Siru Fil-ardhi” (nendeni<br />
kwenye ardhi) “Fandhuru” (mtizame) “Kayfa Baada-alkhalq”<br />
(Mnyezi Mungu vipi kaanza kuumba) “Thumma <strong>Al</strong>lahu Yanshiu<br />
Nashatal Ukhra” (Baada ya hapo Mnyezi Mungu anazua mzuo<br />
29.
mwingine kabisa sio ule alioumba mwanzo). Mnyezi Mungu ni<br />
“Latwiif” anajua kabisa undani wa mambo namna ya kutengeneza<br />
na kufanya. “Yarham Man Yashaa” (Anamrehemu amtakae) “Wa<br />
maa antum bi muujiziina fil ardh” (Na nyiye si wenye kumshinda<br />
Mnyezi Mungu kwenye ardhi). Hizo safari zangu za Europe<br />
nimezifanya ngapi, tunakwenda kunapotolewa Notice hapa na huko<br />
katika University halafu unapeleka Application yako kama<br />
umekubaliwa unakuwemo.<br />
Zote mbili nimekwenda nami simjui mtu yeyote, wote watu<br />
wageni namna kwa namna. Bali kuna moja tukaenda tukapita njia<br />
moja zote bila shaka watu wanachukulia mpaka Paris. Hii moja<br />
tukaenda mpaka Spain, Tukarudi France, tukaingia nchi nyingine za<br />
Europe lakini kwa hiyo kwa njia hiyo nikaona nchi zote za Europe<br />
zote Western Countries. Zote nikazipita, kuzitambua na kuziona.<br />
Safari nyingine ndo ntakuja nende kwenye nchi za Eastern<br />
Countries.<br />
Katika fursa kubwa na faida nilizopata nilipokuwepo<br />
England mara ya mwanzo ni kuingia ndani ya msafara<br />
uliotengenezwa kuzunguuka Europe, ndani ya Coach inakwenda<br />
mbio mbio na kwa raha. Nilikua ndani yake, hii ilitengenezwa na<br />
mmoja katika Walimu wa London University, tukaenda tukapita<br />
English Channel tukaenda France tukafika mpaka Paris tukakaa<br />
baada ya Paris tukateremka kwenda Spain. Tukaenda tukafika<br />
Spain. Hiyo Spain kwa wakati mkubwa ilikuwa nchi ya Kiislamu,<br />
Endlus Waislamu wakatawala, wakajenga, wakakaa wakazaliana<br />
ikawa kama nchi ya Kiislamu.<br />
Kila nchi watu wakawahusudu, wakatamani wawe kama<br />
wao, wakawaiga kama huku. Mwisho walivyokuja watu wakaja<br />
wakawaiga Wazungu – hata wanaandika waandishi wa Kiulaya,<br />
wengine wakasema kua wazee wa wakati ule walikua Wakristo<br />
wakisema: “Ama tumepigwa. Watoto wameharibika namna hii,<br />
wanafwata mambo ya Kiislamu na Kiarabu na kuvaa Kiislamu<br />
na hivi”. Na ustaarabu wao wote kama siye tunavopiga kelele<br />
kuhusu uzungu, na wao walikua namna hivyo hivyo.<br />
Waffaqana llahu Limaa Yuhibb wayardha<br />
Wal - Hamdu Lillahi Rabbil a-lameen.<br />
30.
Katika<br />
ulimwengu<br />
wa<br />
Uislamu<br />
(i)<br />
31.
Vitabu vilivyokwishatoka ni:<br />
*1. Maana halisi ya Imaan. (i) (1 st , 2nd & 3rd addition).<br />
*2. Njia nyepesi ya kuijua nafsi yako.<br />
*3. Njia nyepesi ya kujua kitu juu ya uongofu.<br />
*4. Knowledge vision & ecstacy.<br />
*5. Mwinyi Baraka katika ulimwengu wa Uislamu (i) .<br />
*6. Waislamu na Sayansi - Ulu-m.<br />
*7. Kuhifadhi Burda.<br />
*8. Maana halisi ya Imaan (ii).<br />
*9. Muhammad SAW katika ulimwengu wa ghayb.<br />
*10. Siri ya Balaa.<br />
*11. El makhlouq (Viumbe)<br />
*12. Njia nyepesi ya kujua kitu juu ya uongofu. (2nd addition)<br />
*13. Manaqib ya <strong>Al</strong> habbib Sayyeid <strong>Al</strong> Ma`aruf.<br />
*14. Some aspects of concepts of facility in medevial Islamic<br />
Philosophy by Mwinyibaraka.<br />
*15 maana halisi ya Imaani I (3rd. Addittion)<br />
*15. Njia nyepesi ya kuijua Nafsi yako. (2nd addition).<br />
*16. Mwinyi Baraka katika ulimwengu wa Uislamu ii.<br />
*17. Maana halisi ya Imaani ii (2 nd . Addition)<br />
*18. Mwinyi Baraka katika Ulimwengu wa Uislamu i (2 nd . Addi.).<br />
Vitabu ambavyo tunategemea kuvitoa muda si mrefu<br />
(Insha <strong>Al</strong>lah) ni:<br />
*1. Muhammad SAW Bwana wa Mabwana<br />
*2. Waislamu na Sayansi - Ulu-m. (2nd addition)<br />
*3. Muhammad SAW katika ulimwengu wa Ghayb.<br />
Kwa maulizo kuhusu vitabu wasiliana nasi:<br />
Majaalis El Ulaa - El Qadiriyya Sinza,<br />
P.o. Box 15170,<br />
Tel: 0747 483 553<br />
Tel: 0748 595 958.<br />
Tel: 0744 023 703.<br />
Tel: 0741 235 091.<br />
Tel: 0744 299 597.<br />
Dar es salaam.<br />
32.
<strong>Al</strong> habib Seyyid Umar bin Abdallah bin Seyyid Ahmad <strong>Al</strong> Sheikh Abu<br />
Bakar bin Salim (Mwinyi Baraka ). Amezaliwa Zanzibar katika mwaka<br />
1918. Naye alikuwa ni miongoni mwa vijana walionyanyukia katika malezi<br />
kamili ya Uislamu. <strong>Al</strong>ipomaliza masomo yake ya mwanzo katika Qur an<br />
<strong>Al</strong>iendelea kuhudhuria Majaalis za jioni katika misikiti mbalimbali mjini hapo.<br />
<strong>Al</strong>ikuwa ni kijana ambaye uwezo wake katika kuhifadhi Qur an na uzingatiaji<br />
katika masomo ya skuli ulikuwa ni wakupigia mfano. Katika skuli, masomo<br />
yake ya msingi na yale ya sekondari aliyapata katika shule za kawaida za<br />
Serikali ya Zanzibar.<br />
Baada ya kufanya vyema katika masomo ya Cambridge, aliweza kuendelea<br />
katika Chuo kikuu cha Makerere Uganda. Kwa muda wa miaka mitatu<br />
alikuwepo chuoni hapo kuweza kuhitimu Shahada ya: “Diploma in Bias and<br />
Biology”. Mara baada ya kuhitimu masomo yake, alirejea Zanzibar ambapo<br />
alianza kufundisha masomo ya Dini ya Uislamu, na pia alifundisha Biology<br />
katika Vyuo Vya Waalimu Dole na Beitil El Rass.<br />
Kwenye miaka ya hamsini mwanzoni, <strong>Al</strong> Habib alienda tena kusoma<br />
London Uingereza katika School of Oriental And African Studies. Ambapo<br />
alipewa Shahada ya Diploma katika Islamic and Comperative Law. Na pia<br />
alitunukiwa Shahada ya Diploma katika Lugha ya Kiarabu. <strong>Al</strong>iporejea tena<br />
Unguja katika mwaka 1955, <strong>Al</strong> Habib aliteuliwa kushika Wadhifa mwingine<br />
tena Principal katika Muslim Academy, kuanzia mwaka 1960 – 1963. kisha<br />
alipatiwa Schoolarship kutoka Commonwealth kwenda Oxford Univesity<br />
Uingereza. Huko alifaulu vyema katika masomo yake “Comperative Religion<br />
And Philosophy”. Hapo akatunukiwa Degree ya Ph.D.<br />
<strong>Al</strong> habib Umar alikuwa ni miongoni mwa masheikh wanaotuminiwa<br />
katika kuzilea Roho/Nafsi za waumini. Ambao pia wanajulikana kuwa ni<br />
Masheikh wa Kisufi (Taswauf). Miungini mwa Masheikh zake ni pamoja na <strong>Al</strong><br />
Habib Umar Bin Abu Bakar Bin Sumeity, na pia <strong>Al</strong> Habib Ahmad Bin Hussein<br />
Bin Abu Bakar Bin Salim.<br />
Siku ya tarehe tatu March 1988, Sawa na Mwezi 17, Rajab, 1408, Mwaka<br />
wa Kiislamu ilikuwa ni siku nzito iliyojaa majonzi kwa wale wote waliokuwa<br />
wakimfahamu <strong>Al</strong> Habib Umar Bin Abdallah (Mwinyi Baraka). Kwani<br />
<strong>Al</strong>itwawafu akiwa huko katika Visiwa vya Comoro.<br />
“Tunamuomba Mwenyezi Mungu Sub hanahu Wata`ala, ainyanyue<br />
juu Roho yake, Yeye pamoja na Masheikh wote wengine, Maulamaa<br />
pamoja na watu wema wote ambao wametangulia katika Imaan”.<br />
“Amin”