17.02.2015 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

<strong>Al</strong> Habib Seyyid Omar Bin Seyyid Abdallah – Mwinyi baraka.<br />

i


Katika<br />

ulimwengu wa Uislamu<br />

(i)<br />

Muharram 1429 - January 2008<br />

Toleo la pili <strong>Al</strong>l rights reserved Second addition.<br />

ii.


Yaliyomo:<br />

No.<br />

Ukurasa.<br />

1. Yaliyomo……………………………………... iii.<br />

2. Dibaji………………………………………….. vi.<br />

3. Utangulizi……………………………………… vii.<br />

4. Sehemu ya kwanza…………………………… viii.<br />

5. Kuzaliwa kwangu na malezi yangu…………… 1.<br />

6. Kuanza kusoma………..……………………… 1.<br />

7. Kwenda Makerere…………………………….. 2.<br />

8. Miaka ya Uganda……………………………... 3.<br />

9. Kuanza kusomesha skuli ya Dole…………….. 3.<br />

10. Daawa Ilallah………………………………….. 8.<br />

11. Sehemu ya pili………………………………… 18.<br />

12. Picha ya <strong>Al</strong> habib Seyyid Omar – Mwinyi Baraka.. 31.<br />

13. Vitabu vilivyotoka……………………………… 32.<br />

iii


DIBAJI:<br />

<strong>Al</strong>-hamdul-lillah wa Swalatu was salaam alaa Khayru<br />

Khalqillah Sayyidna Muhammad wa A-lihi wa Swahbihi waman waala<br />

wa Baad.<br />

Hichi ni kitabu ambacho <strong>Al</strong>-habib Sayyid Omar Bin Abdallah<br />

mashuhuri kwa jina Mwinyi-Baraka katika wajukuu wa Sayyid Abubakkar<br />

Bin Salim-Mola-Enaat huko Hadharamut, kwa taabu alielezea<br />

mwenyewe akiwa amejinyoosha kwenye kitanda alipokua mgeni wa<br />

Bw. Mohamed Khan Shemeji yake na <strong>Al</strong>-mar-hum Swaahib El- Ishara<br />

Bw. Akram Mohd aliyefia Mwanza - Tanzania kati ya Mwaka 1988 na<br />

89 <strong>Al</strong>lahu Yarhamuhu wa Jamiil Muuminina wal Muuminaat.<br />

<strong>Al</strong>ikua akizungumza kwa shida sana pengine Dak. 10. Pengine<br />

ndo gha-ya Dak. 15. Kwa hiyo ilikuwa tukimfwata na Tepu Recorder<br />

mara kwa mara tukiwa na Akh. <strong>Al</strong>y Mzee Comorian toka Mkunguni<br />

kwa <strong>Al</strong>-marhumu Mohamed Bin Mahdi na wanawe kina Akh. Islam,<br />

Khamis na <strong>Al</strong>-marhumu Mahdy Mohamed Mahdy <strong>Al</strong>lahummaghfirlahum<br />

wa yarhamhum jamiia.<br />

<strong>Al</strong>-hamdu-lillah tuliwahi kumaliza kunasa na kunukuru yote<br />

kuhusu safari zake za Europe na Amerika kama itavoonekana ndani<br />

yake.<br />

Kwa vile lengo kubwa la safari zake tukiacha kusoma ilikua ni<br />

Jihadi katika Dini ya Mnyezi Mungu nayo si nyingine bali ni Uislamu,<br />

tumeonelea kukiita “Mwinyi Baraka katika Ulimwengu wa Uislamu<br />

– I ” tukitegemea kwa imani zote kua:<br />

(a) Kitazagaza maarifa mazuri kwa watakaokisoma<br />

(b)<br />

Kutakua angalau na kumbukumbu ya mmoja wa wanafalsafa<br />

wa Kisufi mkubwa lakini hakupata umashuhuri nchini kwao<br />

mpaka amekufa.<br />

(c) Tutafaulu Insha-allah kumjulisha yule ambae hakumjua<br />

mwanachuoni mkubwa huyo wa East-Africa na labda<br />

vi.


kumuigiza au kumtakia dua, kwani ipo hasara kubwa kwa kule<br />

kushindwa kumtumia vile ambavyo ingepasa.<br />

Tabia yake katika kujitupa chini na kujiona kua si kitu<br />

alifahamika vibaya kwa ambao hawakumjua, na hijabu ya wazi wazi<br />

kwa walomjua vizuri kabisa. Dalili kubwa ilionekana mara nyingi<br />

alipokuwepo Jijini hapa, si wengi walojua, kwa hiyo ilifikia mpaka<br />

anaondoka si wengi walokua na habari hata ile ya kuepo Jijini hadi<br />

kufikia mwezi mzima! mara kadhaa alipata mwaliko kwa mwanafunzi<br />

wake mkubwa, alipokua madarakani <strong>Al</strong>-hajj <strong>Al</strong>y Hassan Mwinyi-<br />

(Mzee Rukhsa )-Ikulu na alitutaka rukhsa aende au asiende.<br />

Ahlil Majaalis El Ula El Qa-diriyya hawataacha kulia kwa<br />

huzuni kila wakifikiria uamuzi aloutoa baada ya makubaliano kua<br />

angeandika tafsiri ya kite kwa lugha ya Kiswahili ya kitabu kitukufu<br />

Qur an baada ya kushindikana kuitoa tafsiri hiyo kwa njia ya TVZ,<br />

lakini pia Majaalis nao hawakuwahi kwa sababu aliomba aende<br />

Comorro akamshauri mkewe aje nae D‟Salaam nyumbani kwa <strong>Al</strong>marhumu<br />

Bw. Moh‟d Mhdy (A.Y) kinyume ya mambo ni kwamba<br />

kwenda kwake Comorro alikua ameshaitwa kwenda kukutana na ajali<br />

yake badala ya kuja tena D‟Salaam kwa ajili ya kazi ya tafsiri ambayo<br />

ilitarajiwa kuchukua miaka mitatu mizima.<br />

Na ilifikiriwa kutoa juzuu moja moja kama alivoanza hivo <strong>Al</strong>marhumu<br />

Sheikh Abdallah Swaleh El-Farsy (Ay).<br />

Bumbuwazi tulolipata bila ya kumuomba aanze na utangulizi<br />

na Surat El-Fa-tiha tu tulifunukiwa nalo baadae kabisa kua lau mtu<br />

angejua ghaibu basi kuzidisha kheri kwetu ingetumilikisha angalau na<br />

tafsiri ya Surat El-Fatiha ya <strong>Al</strong>-habib Sayyid Omary Abdallah Mwinyi<br />

Baraka (Rahmatullah layhi).<br />

Kwa sababu <strong>Al</strong>-habib alitudarisha vizuri sana kuhusu somo la<br />

Nafsi (Tizama kitabu chetu “Maana halisi ya Imani”) hatuoni haja<br />

yeyote ya kulaumu walokua na uwezo mkubwa na kueka kumbukumbu<br />

ya mwanachuoni huyo kabla na labda baada ya kufa kwake.<br />

Akielezea mwenyewe <strong>Al</strong>-habib kua kila alipokua Makka <strong>Al</strong>marahumu<br />

Bin Bazz alikuwa akimtanguliza… “Omar Swalisha”.<br />

Akimwambia: “Bwana Mtume SAW akisema, Ahlishsharafaa laa<br />

Ahlisharaf watu wa Sharaf hupitana kwa Sharaf. Walaa Yaa arifa<br />

Ahlish-sharaf wala hawawajui watu wa Sharaf Illa Dhawish Sharaf,<br />

Illa ambao ni watu wa Sharaf”.<br />

v.


Kwa niaba ya Majaalis natwaa fursa hii kuwashukuru mno<br />

vijana wa Darasa la kila Jumatano Baadal-Maghrib Mtaa wa Sadani<br />

Ilala baina kina Sharif Karama kwa juhudi yake kubwa katika<br />

kuziandaa kwa makini na uangalifu sana jumla ya makala hizo na<br />

kuzitoa katika Computer, kina Sharif El-Beyt Hussen, Fuad, Mohamed,<br />

Mkhashshe, Swahibul-Ishara Swaleh Hariz, Okashi, Mustafaa, kina<br />

Ababil Abdallah Twalib Arusha na wote wa Jalsa hiyo Mnyezi Mungu<br />

atawajazi Fid Dunia Wal A-khirah.<br />

AL-FAQEER.<br />

AHMAD SHEIKH.<br />

vi.


UTANGULIZI:<br />

<strong>Al</strong>-hamdu-lillahi Rabbil <strong>Al</strong>lamin, Was Swalaatu Was Salaam,<br />

<strong>Al</strong>a Asharafil Anbiya Wal Mursalin <strong>Al</strong>ladhi Unzila <strong>Al</strong>ayhi<br />

Lawlaa Nafarun Min Firqatin Kulli Twaa Fatin Layatafaqqahli<br />

Fil Diin Wa‟alaa <strong>Al</strong>ihit Twaahirina wa Aswaha-bihil<br />

Akramiin.<br />

(Amma Baad)<br />

Wemeniamrisha nsoweza kuwavunja na wakanitaka<br />

watu ambao naona uzito kwenda kinyume nao nieleze<br />

yatayosahilika katika safari zangu.<br />

Sasa naingia kufanya hayo kwa msaada wa Mnyezi<br />

Mungu na uwezo wake Laa-hawla Walaa Quwata Illa Billahil<br />

<strong>Al</strong>iyyil Adhim.<br />

OMAR ABDALLAH<br />

DAR ES SALAAM - TANZANIA<br />

1987<br />

vii.


S E H E M U<br />

YA<br />

K W A N Z A<br />

viii.


KUZALIWA KWANGU NA MALEZI YANGU:<br />

“Naona afadhali nielezee kwanza msingi wa malezi.<br />

Nilizaliwa Zanzibar mwisho mwaka 1917 yaani<br />

December kwa mujibu wa Sheikh, yeye atakuwa anamjua<br />

Mzee wangu vizuri kwani alikua ameoa kwao, kwa Babu na<br />

Mama wote Masharifu walozaliwa Ngazija. Babu Abu-Bakkar<br />

Bin Salim, Mama Lydiid Jamallilleye.<br />

Babu mkubwa Sayyid Abdul-Hassan baada ya miaka<br />

miwili yaani 1938 Baba yangu huyo alifariki-Mungu<br />

amrehemu. Na baada ya miaka mitano ya umri wangu mama<br />

alifariki - Mungu amlaze mahali pema . Nikalelewa na Mume<br />

wa Khaalal Ibin Khaalat wa Mama yangu Seyyid Abdul-<br />

Fattaah Bin Ahmed Jamalilley akiitwa sharifu Abudu.<br />

KUANZA KUSOMA:<br />

Nilipelekwa chuoni kwa <strong>Al</strong>-Mar-hum Seyyid Sheikh<br />

Bin Abdul-Rahman Babake Seyyid Hassan Sheikh nikawa<br />

nasoma, na Sala nimesoma kwa Bibi mkubwa mwana-Ashata<br />

kama alivokua akiitwa Aisha lakini wakimwita Mwana-<br />

Ashata.<br />

Nikabaki baada ya kuhitimu nasomesha watoto chuoni huko<br />

huko na Khalafu nikawa nakwenda nasomesha watoto chuoni kwa<br />

Sharifu Abudu, na wakati huo huo tena nikatiwa Skuli, lakini kwa<br />

sababu ya kukawia kuingia Skuli, sikupata Mnazi mmoja.<br />

Nikapelekwa Mwembe-ladu kutoka Kisiwandui asubuhi, ninarudi<br />

halafu nakwenda saa nane tena mpaka mwisho nikaja zangu Mnazimmoja.<br />

Baada ya kusoma miaka mitatu Mwembe-ladu na mwalimu<br />

wa mwanzo wa Skuli hiyo alikuwa Juma Mohamed, wakimwita<br />

Juma Mohamed Mushte - sijui kwanini Mwalimu Juma <strong>Al</strong>lahu-<br />

Yarham.<br />

1.


Zilikuwa Klas mbili halafu mwisho zikawa tatu, halafu<br />

nikaenda Gulioni. Nikaendelea na masomo Skuli na huku<br />

nikienda chuoni na kusomesha mpaka nakumbuka mwaka<br />

gani nilipotiwa Skuli, ilikua 1928.<br />

Nilipokua STD. 7 Sharifu Abudu akafariki na huku<br />

nimeshaanza kusoma soma kwa Seyyid Abal-Hassan na vile<br />

vile Nahaw. <strong>Al</strong>ivofariki nikabaki chuoni. Nimekiendesha<br />

chuo bila shaka mwenyewe ni Seyyid Abal-Hassan ninasalisha<br />

Msikiti wake Msikiti wa Sharifu Abudu Vikokotoni.<br />

KWENDA MAKERERE COLLEGE:<br />

Nikasomesha Mukhtasaraf pale baada ya Swalatil-Fajr nae<br />

Seyyid Abal-Hassan akawa anasomesha Umdatus Saaliki baada ya<br />

vitabu kadhaa wa kadhaa tulivokua tumeishasoma. Sera zote<br />

takribin, Mukhtasarat kwa Seyyid Abdul-Fattah tumewahi kuvisoma<br />

kwake. Nikaanza na Nahaw hapo, ilihudhuriwa na watu mahodari<br />

katika masomo hayo. Kama Seyyid Mustafa, Sheikh Mohamed<br />

Qamus baada ya Swalatil-Ishaa. Hatukumaliza kitabu mie nilikua<br />

nimeishakwenda Secondary School na nikapata kupelekwa<br />

Makerere nkaenda Makerere College.<br />

Nilikua na bahati nzuri ya kufanya Mitihani, siku zote nakua<br />

Fas aghlabu. Katika Primary yote na Secondary nilipasi vizuri. Na<br />

nikisoma mwenyewe vibuku vibuku na hasa palikuwepo magazine<br />

ikiitwa Islamic Review kulikua na Library ya Sunni Mkunazini<br />

nikipenda sana kusoma. Kulikuwepo kama zile nikipata sana sana<br />

kusoma kama habari za kina Khuwaja Kamalud-din nikiona raha<br />

kwenda kusoma.<br />

Makerere niliingia 1939 nikapata Diploma ya Education baada<br />

ya miaka miwili na nikakaa mwaka wa tatu kuspeshalaiz katika<br />

Biology.<br />

2.


MIAKA YA UGANDA:<br />

Miaka ya Uganda ilikuwa ya faida sana kwa kufwatana<br />

Waislamu huko. Kutwalii nao, wakija Makerere tukitwalii na<br />

Sheikh wao Sheikh Shuayb na mmoja Maallim Juma na wengineo,<br />

hasa Nahaw, na Sheikh Shuayb akisoma mantik, Ambayo niliwahi<br />

kusoma kidogo kwa Muhsin Bin <strong>Al</strong>y Barwani pamoja na mwanae<br />

<strong>Al</strong>y muhsin halafu mimi nikaendelea kwa Sheikh Sleiman Bin<br />

<strong>Al</strong>awy.<br />

KUA MWALIMU SHULE YA DOLE:<br />

Mwisho nikarudi Zanzibar nikawa Mwalimu wa Sayans na<br />

Religion (DINI) katika shule ya Dole pamoja na Teachers Training<br />

yake. Wakati huo ndio nikapata fursa ya kufundisha Vijana wengi<br />

ambao sasa wameshika madaraka makubwa kama President <strong>Al</strong>y<br />

Hassan Mwinyi Vice President Idriis Abdul-Wakyl na wengineo.<br />

Huku ninasomesha Dole na Beit-Raas.<br />

Skuli ile ya Dole ikawa Beit-Raas na kila nikija mjini<br />

ninasomesha msikiti wa Sharif Abudu, na daima nasoma kwa<br />

Sheikh Sleiman na Sheikh Muhsini. Na vitu vingi nimesoma kwa<br />

Sheikh Sleiman, Fanni. Hata mtu akiniuliza Elimu yako ya Dini<br />

umeipata kwa nani, ntamwambia kwa Sharif Abudu, Seyyid Abdul-<br />

Fattan. Secondary Seyyid Abal-Hassan na Seyyid Mustafa Bin<br />

Jafar ambaye ni Father in Law wangu (Mkwe wangu).<br />

Na ikiwa kuna ilimu inaweza kuhisabiwa pamoja kua ya Ki-<br />

University, basi Universtity niloipata huko huko kwetu basi ni<br />

Sheikh Sleiman, Seyyid Abal-Hassan, Sheikh Muhsin, Seyyid<br />

Mustafa Bin Jaafar ambae ni Father in Law wangu (Mkwe wangu)<br />

zote zinajulikana nimezipata kwao Shikh Sleiman <strong>Al</strong>awy Babake<br />

Sheikh Zamil alikua mwanachuoni aliyekusanya mambo mengi<br />

taabu kuyakuta kwa mtu mmoja yeyote.<br />

1951 nkapata Scholorship ya London kwenda kusoma Islamic<br />

and Comperative Law. Unasoma Law ya Kiingereza, Law ya<br />

kiafrica na bila shaka kwa wingi - Sheria ya Kiislam na katika ajabu<br />

za kusoma mtu huyo ni kua walimu wa sheria ya Kiislamu<br />

3.


walikuwa ni Waingereza, na wengine walikuwa ni maadui wa<br />

Islamu. Lakini ni Law ni Fiq-hi, lakini wapo walokuwa<br />

wakinisomesha vitabu kama Dr. <strong>Al</strong>y Hassan Abdul-Qadir Director<br />

wa Islamic Cultural Centre alikueko siku hizo - London University<br />

ilimkodi School of Oriental Studies ilimtaka awe akija akisomesha.<br />

Nikasoma Fiq-hi, Usulil-Fiqhi kwake, nikasoma na kiarabu zaidi<br />

kwa Wazungu.<br />

Somo hilo liliniletea hasa katika kusomeshwa na mmoja<br />

katika wakristo, walikua wakitaka kuuvunja Uislamu sana Imani.<br />

Na kutaka kuponda kisichopondeka kwa Bw. Mtume - SAW<br />

Anderson akiitwa. Tumepigizana kelele mara nyingi kwenye klasi.<br />

Na nilikuwa nikisoma kinamna ya peke yangu pengine<br />

mimi na Mwalimu tu, pengine Walimu wawili na miye mwanafunzi<br />

mmoja pengine walimu watatu na mwanafunzi ni miye mmoja. Na<br />

miye kila nikipata fursa nikipondana pondana. Pengine klasi inajaa<br />

mpaka watu wanakwenda kwenye Dining Hall – mahali pa kulia<br />

chakula – manake watu wanasoma Law walikuwa wakichukua kitu<br />

kinaitwa LLM au LLB na ISLAMIC LAW – yaani sheria ya<br />

Kiislamu ni moja katika subjects.<br />

Wote wakija kwake sasa wakipanga aje awasomeshe na siye<br />

sote tuko pamoja. Tukipigizana kelele sana kilichontokea katika<br />

fikra za mwanzo kabisa ni khabari ya alipokuja kwenye mambo ya<br />

ndoa katika sheria ya Kiislamu akapata fursa ya kutaja ndoa ya<br />

Sayyidatna Zeynab Mtume SAW akasema hivo wanavosema wao:-<br />

“Siku moja alimuoza Zeyd Bin Harith kwa sababu Zeyd Bin<br />

Harith alikua ni mtumwa wake Mtume akamwacha huru<br />

akamuoza Zeynab. Zeynab alikua mtoto wa Shangazi yake na<br />

walikuwa hawataki aolewe na mtu ambae aliwahi kua mtumwa.<br />

Lakini kwa kumstahi Mtume na kusemewa kwa Mtume<br />

akamuoa sasa Khalafu akaja akamwacha akamuoa Mtume.<br />

Ndoa yake yalosemwa ndani ya Qur-an.<br />

Aya Qur an ilokusudiwa hapo ni ile ilioko katika 33:37.<br />

“Na (wakumbushe) ulipomwambia yule ambaye Mnyezi<br />

Mungu amemneeshesha (kwa kumuafikia Uislamu) na wewe<br />

ukamneemesha (kwa kumpa kugusana naye ni Bw Zaid Bin Harith<br />

ulipomwambia “shikamana na Mkeo na umche Mnyezi Mungu<br />

(usimuache)”. Na ukaficha katika Nafsi yako aliyotaka Mnyezi<br />

Mungu kuyatoa (nayo ni kuwa Mnyezi Mungu amekuamrisha<br />

4.


umuoe wewe huyo mkewe atakapomuacha ili iondoke ile itikadi<br />

iliyokua ya kuwa mtoto wa kulea ni kama mtoto wa kumzaa) na<br />

ukawachelea watu, hali Mnyezi Mungu ndiye mwenye haki zaidi ya<br />

kumchelea. Basi alipokwisha Zaid haja yake na mwanamke huyo,<br />

tulikuoza wewe ili isiwe taabu kwa Waislamu kuwaowa wake wa<br />

watoto wao wa kupanga wanapokuwa hawana haja nao. Na amri ya<br />

Mnyezi Mungu ni yenye kutekelezwa”.<br />

Qur an: 33:37<br />

Ilikuaje wao wanasema kamuona akampenda akamwambia<br />

mwache nimuowe miye. Na hakika ya amri ni jambo ilikua Zayd<br />

akipata taabu sana nyumbani kwa Zeynab. Ilikua Mabibi wa<br />

Kikureish wanadharau yule Bibi aliyeolewa na mtu ambae alikua ni<br />

Mtumwa, nae ni mzalendo. Akimtaabisha Zeyd. Zeyd akitaabika<br />

akija akimwambia mtume “Niachie nimuache” akamwambia “ Kaa<br />

nae, Kaa nae”. mwisho akapewa Rukhsa, alipopewa rukhsa Zeyd<br />

akamwacha Mtume SAW akamuoa. Sababu mbili:-<br />

Kwanza:-<br />

Kwa kikureishi hapana rukhsa kumuoa mtu ambae<br />

alikua mke wa mtumwa wake, mtu ambae alikua<br />

mtumwa wake akamwacha huru halafu akawa mkewe<br />

akimwacha hapana rukhsa kumuoa. Azwaaj adiyaihi.<br />

Ili kuondoshwa hayo iwe anza wewe hapana atae<br />

thubutu mwingine kila mtu ataogopa asitukanwe<br />

asifanzweje - wewe anza.<br />

“Tulikuoza wewe ili isiwe taabu kwa Waislamu kuwaowa<br />

wake wa watoto wao wa kupanga wanapokuwa hawana<br />

haja nao. Na amri ya Mnyezi Mungu ni yenye kutekelezwa”.<br />

“Likay laa yakuna ararajun fii azwaaj ad-i yaaihi midhaa<br />

qadhaa minha watwaran wa kana amrullahi maf-u-la”<br />

Ya pili:- Ilikua ni tabu kwa Zeynab kuolewa na watu wengine<br />

baada ya kua kaolewa na mtu Ad-iyaai – alikua ni<br />

mtumwa sasa Mtume ASW amekua kilugha ya<br />

kisasa yeye ndo alo Run Life yake. Jambo gani zuri zaidi<br />

angelifanya kuliko kumchukua yeye akamuoa.<br />

5.


Sasa wamemgeuza badala ya kumsifu kua ni mtu mtukufu namna<br />

hii na hivi Firaq akampenda. Nikasema pale pale kwenye klas na<br />

tulikuwa watu wangapi watu wanne, mimi na huyo aliekua akieleza<br />

na Profesa wa African Law na mmoja akifanza kazi ya<br />

Administration katika Afrika na mmoja alikua Jaji India sasa alikua<br />

akisomesha English Law nikawaambia jambo:-<br />

Something for which you have aught you have to have<br />

praised him, respected him. You have taken the very<br />

theme blame him and to make it the cause of saying bad<br />

things about the profet.<br />

Jambo kama hili mtu atataka Udhuru vipi-<br />

“Idhaa mahaasin allatii ataytuha aadat dhunubihi<br />

Faqul-llii kayfa aatadhir”<br />

“Ikiwa mema yangu niliyoyafanya yanahisabiwa ndo<br />

madhambi sasa natoa udhuru vipi tena”<br />

“Aa, yamekwisha hayo ni moja katika mambo yalotokea katika<br />

klas. Mikutano hiyo wasokua Waislamu na vikundi vya Waislamu.<br />

Ndo mwanzo Vijana wa Kiislamu wanaanza kukusanyika pamoja<br />

na kukutana toka nchi za nje na mmoja mmoja wa kule na<br />

wanafanya mikutano wanasoma, wanazungumza – palikua na<br />

pahala panaitwa Aclistus Square, kwa Editor wa Islamic Review<br />

kwenye Laasiri watu wanakutana wanadiscuss. Inasomwa Maqra<br />

inatafsiriwa, inaelezwa na <strong>Al</strong>-hamdulillah ikielezwa wao hutaka na<br />

mie nitie langu.<br />

Ikaendelea hivo hivo mpaka nikapata safari ya Marekani na<br />

mie ni mwanafunzi wa U.K niko England. Na kule kule England<br />

bila shaka fursa zimetokea katika makanisa vikundi vya wakristo<br />

nami nakwenda kutoa khutba fanni ni wengi na wanafurahi wasikie<br />

khabari za Uislamu na hivi.<br />

Nakumbuka Wales nilitoa khutba moja very famous - sana<br />

ilijaa watu sana kabisa. London nilikua nipo hapo nikitoa khutba<br />

sasa itakuja safari ya Marekani.<br />

Nilipokua mwanafuzi London School of Oriental African<br />

Studies <strong>Al</strong>-Madrasati Qarasaatish-Sharqiyyat katika London<br />

University ilipatikana fursa ya kwenda States wanafunzi wanaotaka<br />

6.


kwenda watoe kiasi kadhaa wa kadhaa na wakifika huko<br />

watatizamwa, watakua wageni wa Jumuiya ya Kimarekani moja<br />

wapo – wazungushwe wonyeshwe maisha ya Kimarekani yaliyo<br />

mema kwa mujibu wa vipimo vyao na mengine kwa vipimo vya<br />

watu wote.<br />

Kwa umri waliokua wakiutaka mimi nilikua nimekwisha kua<br />

mtu mzima lakini walipoona application yangu na kuniona<br />

wakanitia kati. Ilikuwa taabu kupata kipando tena, mwisho nikapata<br />

Greck Line ikanichukua mpaka Quebec, mji baada ya mji mpaka<br />

Batholomeo mpaka New York. Njiani bila shaka nikaona Niagara<br />

Falls. Shalalar Niagara – Mmiminiko wa maji katika mahali<br />

wanapokwenda watu kutizama. Pahala pa ajabu penye Nature –<br />

yaani umbo la ajabu.<br />

Bin Adam hajatia mkono wake, wenyewe tu linakwenda –<br />

lipo. Kutoka hapo ndo nkaenda Batholomeo – Batholomeo New<br />

York nkapokelewa na wenzangu wengine mmoja mmoja. Tena<br />

mmoja kutoka London tukakutana huko huko. Nimekwenda<br />

tukakutanika pamoja na Waislamu wawili watatu mmoja mtu wa<br />

Kimasr, mmoja wa Pakistan lakini sasa imekwisha kua kikatiba –<br />

Bangladesh tena. Na Dini nyinginezo na kabila nyinginezo.<br />

Tukachukuliwa kuzungushwa tukapitishwa States mbali mbali, na<br />

kila pahali tunapata fursa ya kupokewa kwa heshima na<br />

kuonyeshwa na kushughulikiwa, na wasaa wa kutoa fikra.<br />

Na bila shaka mtu Muislam kila akipata fursa jambo la<br />

mwanzo hutizama njia awaonyeshe watu nini Uislamu, nini faida<br />

zake nini ukweli wake, na <strong>Al</strong>-hamdulillah sikuziwacha fursa hizo.<br />

Hata unaona Naby Yusuf AS alipoulizwa habari za ndoto na wale<br />

watu wawili katika gereza kabla hajawajibu kawaambia.<br />

“Enyi Wafungwa wenzangu wawili Je! waungu wengi<br />

wanaofarikiana ndio bora (kuabudiwa) au Mnyezi<br />

Mungu mmoja mwenye nguvu (juu ya kila kitu)”.<br />

Qur an: 12:39<br />

“Inni Taraktu Millata Qawm Laa Yuuminun Billahi<br />

Wal-yawmil Akhir”<br />

Qur an: 12:39<br />

7.


DAAWA ILALLAH:<br />

Mwisho akawatajia Mnyezi Mungu khalafu ndo akawafasiria<br />

tena. Hii ndo kazi ya Muislamu. Da-awa Ilallah siku zote kwa<br />

nyendo zake, kwa maneno yake, kwa vitendo vyake, kwa mawaidha<br />

yake kwa kila namna zake yeye anaupokea Uislamu. Anapita watu<br />

kwa njia nzuri kabisa, kwa hekma na mawaidha mazuri.<br />

“Id-u Ilaa Sabiili Rabbika Bilhikma wa Mawidhatan<br />

Hasana……..”<br />

“Kuja kwenye njia ya rabbu wako kwa hikma<br />

na mawaidha mazuri”.<br />

“…Wajaadilhum Billati Hiya Ahsan…”<br />

“Usishindane nao illa kwa namna iliyo njema kabisa”<br />

“…Qul Haadhihi Sabilli…”<br />

“Sema hii njia yangu”<br />

“…Ad-u-llahi <strong>Al</strong>la Baswiratu Anaa wa Mamit Tabaan”<br />

“Na ita kwa Mnyezi Mungu, juu ya utambuzi kwa fikra,<br />

kwa mipango kwa kujua ntafanya nini, na hii kazi hii mimi<br />

anaenifwata”.<br />

Basi ndo kazi ya Muislamu tena madamu yuko duniani hali<br />

haonywi basi atakua kama watu wabaya anajua ataepukana nayo<br />

kadri anavoweza. Mema anayajua atayafuata kadri anavyoweza.<br />

Lakini Mission yake kubwa ni Da‟awa Ilallah – Propagation kwa<br />

kiasi chake anachokijua na uwezo wake na uhodari wake na alicho<br />

nacho basi kila State ikitokea haya.<br />

Nakumbuka kuna State nyingine nikipata fursa mpaka<br />

kwenye Radio nikisikilizwa mtu aseme khabari za kwao. Bila shaka<br />

nikisema khabari za kwetu nayo ni Zanzibar na wao ni watu wa<br />

Dini nyingine. Anataka kujua Dini gani – Uislamu, Uislamu ni nini,<br />

unawaambia na kuwaeleza na unawafahamisha na kuwaonyesha vile<br />

utofauti uliopo baina ya Uislamu na Ukrito.<br />

Si kwa kuponda kiasi ya kua wajue tu nini kiliopo kilicho<br />

kikubwa kilicho tofautisha bila shaka, kikubwa kilichotofautisha ni<br />

8.


itikadi ya Wakristo kua Nabii Isa ana uungu. Waislamu wanakataa<br />

yeye ni Mtume tu pamoja na wengine Illa yeye kaitwa na Mnyezi<br />

Mungu:-<br />

“…Abdullahi wa Rasuluhu wa Ibni Ammatihi Wakalimatuhu<br />

<strong>Al</strong>-qa-ha Ilaa Maryam Waru-hum-minhu”.<br />

Basi mambo kama haya inapatikana fursa. Illa nakumbuka<br />

hivi hivi nilipofika Noxivil, ilisadifu Jumamosi wakaniambia kua<br />

kesho Jumapili tunakwenda katika Kanisa na wao kule ni katika<br />

wakubwa wa Kanisa, “Jee! utatufwata?” Nikawaambia<br />

intakufwateni, nyie mtakwenda na yenu na mimi ntakwenda na<br />

yangu.<br />

Nilipokwenda nkasikia mkubwa wao ananadi kua tumepata<br />

mgeni na si wa Dini yetu na tutampa yeye fursa atoe Sermon,<br />

Aprichi – haya jazaa kheyr. Nikasimama nikatoa nikaprich kitu<br />

kikubwa. Kulikua Nigroes wengi, ni mji wa Wanigroes walo na sura<br />

nzuri wanaoendesha mambo yao na kila namna. Basi nikawatajia<br />

bila shaka mwanzo wa usawa wa Kiislamu bila shaka mwanzo ule<br />

Uislamu hauna nani weusi nani weupe kama Kanisa – Msikiti wa<br />

weusi na weupe. Hapo ndo nkapatiwa fursa ya kuisoma kama<br />

kungineko, kokote kuisoma aya:-<br />

“Yaa Ayyuhanaas Innaa Khalaqna-kum Min<br />

Dhakarin wa Untha…”<br />

“Enyi watu hakika sisi tumekuumbeni wanaume na<br />

wanawake (wengine wakatafsiri) kutokana na yule yule<br />

mmoja (Naby Adam) na mwanamke yule yule mmoja<br />

(Hawwa)”.<br />

“…Wajaalna-kum Shuuban wa Qabaaila<br />

Litaarafu…”<br />

“…Tukakujaalieni “Nations” na “Tribes” na kabila<br />

kubwa na kabila ndogo ndogo mkaongeza nchi na<br />

kabila katika nchi mpate kujuana msaidiane (mjue<br />

namna ya kukaa pamoja msijiweke Divisions au<br />

Labour)”<br />

Qur an: 49:13.<br />

9.


“…Inna Akramakum Indallahi Atqa-kum”.<br />

“…Mtukufu wenu kwa Mnyezi Mungu ni yule mcha<br />

Mungu kuliko nyote. (Hali hii watu hufasiri wakaona<br />

kama hapana namna nyingine za kutukuzana illa ni<br />

utukufu tu)”.<br />

Qur an: 49:13<br />

Kuna maneno mengi ya Kiislamu “Akram” na si Akram tu<br />

kuna “Ashraf” haikusemwa “Inna Ashrakum” bila shaka<br />

Afdhwalakum maana yake mbali. Maana ya Qur an inakata<br />

kuzingatiwa – Kila neno lina maana yake na pahala pake na uzito<br />

wake.<br />

Na katika khutba nilizokua nikitoa huko Marekani kuonyesha<br />

Uislamu nilitumia aya hii kuonyesha kua sisi hatuna ugomvi na<br />

wakristo kwa kusoma:-<br />

“Qu-lu Amanna Billahi wa Maa Unzila A Layna wa<br />

Maa-Unzila Ila Ibrahima wa Isma-iila Wais-haaq<br />

wa Yaa-quuba Wamaa-utiya Musa wa Isa<br />

Wamaa Utiyyiina Min Rabbihim”.<br />

Inatwambia:-<br />

“Semeni:- Tumemuamini Mnyezi Mungu, tulicho<br />

teremshiwa na kilichoteremshwa kwa Ibrahim na Ismail na<br />

Is- haq na Yaaqub na wajukuu. (Wamaa Uutiya Musa) – na<br />

anayopewa Musa wa Isa – (Wamaa Uutiyyan – Nabiyyuna<br />

Min Rabbihim) wanayopewa na Mitume kutokana na<br />

Rabbu wao. Yote tumeyaamini kua yameletwa na Mungu:-<br />

(Laa Nufarraqu Baina Ahadin Mini- hum). Hatufariqishi<br />

baina yeyote katika wao, (Wa Nahnu Lahu Muslimu) na<br />

sisi kwa Mnyezi Mungu tumeslimu”.<br />

Qur an: 3:84.<br />

“Fain Amanu Bimithli Maa Amantum Bihi Faqadih<br />

Tada Wain-Tawallaw Fainna Maahum Fii Shiqa-qin<br />

Fasayakfiikahumullah wa Huwas-Samiiun <strong>Al</strong>iim”.<br />

Qur an: 2:137<br />

10.


“Basi watu hao (Manasara na Mayahudi) kama mnavoamini<br />

(nyinyi) itakua kweli wameongoka na wakikengeuka<br />

(wakikupa mgongo, nyongo) basi wao wapo<br />

katika upinzani tu. Basi Mnyezi Mungu atakulinda na<br />

shari yao, nao hawatakudhuruni kitu-(Wa Huwa-<br />

Samiiun <strong>Al</strong>ym) na ndo mwenye kusikia na mwenye<br />

kujua. (Sibghata – llahi) – hiyo radhi ya Mnyezi<br />

Mungu kisha ipanga katika nyoyo za waja, hiyo<br />

Sibghat llahi ni Babtism ya Mungu Ka-precise kua<br />

ambae kwa Wakristo Sharti Abatizwe.<br />

Padri ambatize mtu. Na unaona katika Uislamu laa - Mungu<br />

mwenyewe anakubatiza. Mambo ya Roho hayo Bin Adam<br />

mwenzake hayagusi. Mnyezi Mungu anasema, ukimwamini kuna<br />

Mjarad wa kuamini namna hiyo tu. Kama inavohitajiwa uamini<br />

Mungu mwenyewe. Amma kubatiza.<br />

“…Waman Ahsan Mina-llahi Swibghata wa Nahnu<br />

Lahu A-bidu-n”.<br />

“Na mimi mwema zaidi kuliko Mnyezi Mungu<br />

kwa Swibgha, na sisi kwa yeye ni wenye kumuabudu”.<br />

Qur an: 2:138.<br />

Mtu mwengine akutengenezee wende ukamuabudu<br />

mwengine. Akufanye unafaa-kuabudu, wende ukamuabudu<br />

mwengine. Huyo huyo unofaa kumuabudu ndiye ataekutengeneza<br />

akupokee, atengeneze mambo yako, kuonyesha Utolerence wa<br />

Uislamu, kukaa pamoja na watu wa dini nyingine kama Qur an<br />

inavyosema:-<br />

“Walaa Tujaadil Ahlil – kitaab Illa Billati<br />

Hiya Ahsan”.<br />

“Usijadiliane na watu wa chuo illa kwa namna iliyo<br />

nzuri (watu wa chuo Yahudi na Kristo) ilaa kwa namna<br />

iliyo nzuri kabisa”.<br />

Qur an: 29:46<br />

Haya katika Radio, katika Maklasi, katika mashangwe katika<br />

kila pahala mtu akipata fursa anatoa aya hizo na aya zinginezo<br />

11.


waafikianazo.<br />

“Wa Qu-lu A-manna Billahi Unzila Ilayna Wamaa<br />

Unzila Ilykum Wailaahana Wailaahukum<br />

Wa-hid Wanahnu Lahu Muslimuun”.<br />

“Na useme tumeamini ambacho kilichoteremshwa<br />

kwetu na kilichotelemshwa kwenu nyinyi<br />

na Mungu wetu na Mungu wenu ni mmoja na<br />

sisi kwa yeye peke yake tumesilimu”.<br />

Qur an: 3:84<br />

Hiyo ndiyo Qur an tukufu tuliitumia sana. Nikitoa khutba<br />

katika Lottery Clubs katika Clubs za namna kwa namna na vikundi<br />

vya wanawake, mjini na mashambani kuna Associations za<br />

wanawake na mambo yao hayo, nkawaambia khutba.<br />

Mtu bila shaka nkaonyesha kuona wapi katika Uislamu<br />

katika hayo nkawaambia ulietajwa kwa uzuri katika Qur an kuliko<br />

zaidi kuliko Sayydatna Maryam na wanadhania kua yeye anavunjwa<br />

na Uislamu. Waislamu ni mtu wao mamake Mtume na anatajwa<br />

ndani ya Qur an vizuri kabisa.<br />

Sadatna Maryam na alivotajwa vizuri katika Qur an hakua si<br />

chochote illa ni Mamake Naby Isa aliyeambiwa kua amemzaa hali<br />

ya kua yu Bikra inatosha sikwambii miujiza yake. Tunda, siku si<br />

zake mengine na wema wake katika Lottery inataka wasaa kusema<br />

na Politician wakubwa wakubwa. Kusema na watu juu ya mambo<br />

makubwa unawaambia hatari ya Colourbar Discrimination si kwa<br />

kuwatukana wala kuwaogopa, kuwaambia hatari unafanya hatari<br />

yaani kama jeuri.<br />

Mmarekani mmoja anainua kidole namwambia Mmarekani<br />

aache Colorbar aache kwa mmoja Myahudi alikua katika Group<br />

yetu akaja akawaambia mngekua mnajiona we mwenyewe<br />

unapokua unasema-ajabu. Na alil-hasil fursa hizo zimechukulika<br />

Insha-<strong>Al</strong>lah zisifutike ziwe zimethbitika.<br />

Khutba kadhaa wa kadhaa nimejaribu kuzikumbuka mambo<br />

makhsusi yalosemwa–Maelezo makhsusi yalokamatana na Uislamu<br />

ambao ulikua nao – Hawafahamu nimejaribu kuwafahamisha kadiri<br />

ya uwezo nimekwenda hata tukafika pahala, hapo kuna Camp kuna<br />

vijana wa Jamal – kadhaa wa kadhaa wameekwa hapo wageni wa<br />

Vice Chairman wa Serikali ya Kimarekani, tukachanganishwa<br />

12.


nao sasa yule aliyetuchukua Marekani akasema kwamba: “Naona<br />

kama kwamba Jumapili hii Wakristo wasiende Kanisani – badala<br />

yake watachanganyika na Waislamu na Mayahudi pamoja wafanye<br />

jambo la kiibada pamoja.<br />

Kila mtu asome kitu katika Dini yake. Mayahudi wasome<br />

Taurati, Wakristo wasome Zaburi na Dua ya Zaburi na Waislamu<br />

wasome Qur-an. Mambo yafanyike ki-njia ambayo Wayahudi<br />

hawatowaudhi Waislamu wala Wakristo. Na Wakristo watafute vile<br />

vile kwamba hawatakwenda kinyume na Waislamu na Wayahudi”<br />

Wakatupa shauri hilo, mimi nikamwambia yule Kijana wa<br />

Kimasri Muegyptian kua apande ahubiri, yeye afanye kazi ile, lakini<br />

akakataa . Mimi nikamwambia: “Lakini lini wataisikia Qur an na<br />

hatuna woga wowote wa kuonyesha kua Qur-an ndio sawa<br />

kuonyesha kua Qur-an itafunikwa au itazidiwa kabisa ndo sawa<br />

kuonyesha kua ndo kitabu cha Mnyezi Mungu hasa cha kweli<br />

kweli”. <strong>Al</strong>ipokataa mimi nikafanya, wale walosoma vitabu vyao na<br />

dua zao hapana alothibitika. Quran iliposomwa na aya gani<br />

ilosomwa.<br />

“Walaa Tastawi-l Hasanatu Walas Sayyiatu Id-Faa<br />

Billati Hiya Ahsan Faidhal Ladhi Bainaka wa<br />

Baynahu Ada-Watan wa Maaka Annahu Waliyyul<br />

Hamiid Yulaqi Qa-ha Illa-ladhiina Swabaru<br />

Wamaa Yulaqqa-ha Illa Dhu-Hadh-Dhin Adhiim”.<br />

Hiyo ndiyo Qur an, ni Aya mbili hizo zilizosomwa. Haiwi sawa<br />

Kiingereza ikifasiriwa:-<br />

“It can never be equal evils and virtue it will never be equal”.<br />

Tenda kwa lilo zuri kabisa jema kabisa, mtu akifanya ovu hutafuta<br />

lilo jema kabisa atende. Push away what whatever is the best<br />

what is the worst and all of a sudden that one who was your<br />

bitter enemy between you and him you will discover he has<br />

turned into a faithfull friend almost – irreletive. Mlipe mema<br />

mara utamuona amebadilika amekua rafiki mwema. Wala<br />

hawakutanishwi na hayo illa wenye kusubiri wala hawakutanishwi<br />

na hayo illa wenye fungu kubwa kwa Mungu.<br />

“Laa Ilaha Illallah wa Maa yulaqqa-ha Illal ladhina<br />

13.


Swabaru wa Maa Yulaqqa ha Illa Dhuhadh-dhu<br />

Adhiim”.<br />

Wameathirika utastaajabu kabisa, ajabu mmoja Mmarekani<br />

akanijia akaniambia: “Is that the Qur an?” Nikamwambi: “O<br />

yes, there is a lot in that”. Nkamwambia-mmekawia kujua.<br />

Ni moja katika mambo yalotokea halafu akanijia yule<br />

Muegyptian akaniambia “You, anta adhym, anta tahmil<br />

elamaana”. Nikamwambia: “<strong>Al</strong>hamdu-Lillah”. Basi<br />

tukaondoka hapo tukasogea mbele pengine. Mtu asome aya<br />

katika katibu chake inahitajia asome na Dua ya Kitabu chake<br />

mimi nilichagua Aya hii:-<br />

“Rabbana Laa Tua-khidhna innasiina Aw-kh-twaana<br />

Rabbana wala tahmil elayna iswran kamaa hamal<br />

tahu ala-lladhina min Qablina Rabbana wala tahmilna<br />

maa Laa Twa-qata Lala bihi wa af anna-waghfir lana<br />

war hamna Anta Mawla-na fan-Swurna alal-qawmil –<br />

ka firiina”.<br />

“Bwana wetu, e! Rabbu wetu usitupatilize tukisahu au<br />

Tukikosa e! (Rabbu wetu) usituchukulie uzito kama<br />

ulivowachukulia walio kabla yetu usitubebeshe<br />

tusioweza kuyachukua yalo mazito kwetu ya Rabb<br />

utuafu utughafirie uturehemu we ndo ulo tawalia<br />

mambo yetu utunusuru juu ya watu (Qawm) yenye<br />

kukufuru”.<br />

Hiyo Amerika katika Camp ile ilikusanya watu namna kwa<br />

namna. O! our Lord, kwa hakika nilifasiri Lord, hapana neno<br />

jingine lililotumika sana kwa Rabbana kama Lord, lakini haina<br />

maana ya Lord peke yake yaani ina maana nyingine. Creator<br />

Envoilver Lord Prossessor – kila kitu kimo katika neno Rabb –<br />

Avenger – mtengenezaji, kama sisi, kwa kiswahili utasema<br />

mtengenezaji, katutengenezea yote. Rabb ukifasiri, “Bwana”<br />

haitoshi hata kidogo au si Wafaransa “Laa tua-khidhna in nasiina<br />

aw-akhtwaana”.<br />

Maana Muislamu makosa yake yanakuja kwa kusahau,<br />

anarukwa na akili anasahau. Huo ndio Uungu, anasahau Pepo<br />

anasahau alokatazwa kwa kufanya makosa kama ilivyodhihiri kwa<br />

14.


Babu yetu, Mzee wetu Adam. Akikumbuka anarejea anasikitika na<br />

anamuomba Mungu asimchukulie. Muislamu mwema, kinyume<br />

mbaya hutampa kufanya ni fahari huyakimbilia akayatengenezea<br />

tena.<br />

Basi unataka ujue kua hapana haya kwa kucha kwa Dini zao<br />

nyingineo, kwanza kwa Kikatholic lazima wende wakamtafute<br />

Priest. Akupe kurudi halafu ndo usamehewe kwa wasta wake.<br />

Wanaita wenyewe To Confess! kukubali ubaya wake mtu.<br />

Kiislamu hapana, unakubaliwa na Mnyezi Mungu na<br />

unamuomba asikuchukulie. Basi mpaka mwisho hapo ikaja<br />

mizunguko tena tulikokwenda.<br />

Sasa si sharti niseme kwa mujibu wa taratibu uliopita lakini<br />

kwa namna yoyote ile kwa kiasi ntavyokumbuka tulipofika New<br />

York usiku tulichukuliwa tukatiwa katika Meli tukaitizame New<br />

York kwa nje Baharini. Inatisha, ina haiba inapendeza Sky Scrapers.<br />

Majumba ya mamia makumi kwa makumi, Ghorofa mia na kitu<br />

Mataa jumba la United Nations, na hii inaathir sana kuonyesha Bin<br />

Adam vipi anaweza kutumia uwezo aliopewa akafanya kazi akafikia<br />

hali ile.<br />

Jitihada yao yote watu fikra nzuri juu ya Marekani na kwa<br />

sababu hiyo ndo maana nyumba tulizokaa nyingi mimi nafsi yangu,<br />

nyumba nilizokaa ni kumi na nane. Kumi na sita ndani yake hakuna<br />

hata tone la ulevi, na wanavunja ulevi vile vile, ili kutaka<br />

kutuonyesha ya kua wako watu hawalewi huo Amerika. Akili yao<br />

imewaambia ulevi una hatari na si wa kutumiwa kwa sababu ya<br />

uzima, kwa sababu ya akili, kwa sababu ya mwili.<br />

Basi na huku vile vile kila wanalolipata na kutufanyia wema<br />

kwa kadiri wanavoweza katika majumba. Na hivi hata huko South<br />

Atlanta imewekwa nao kwenyewe kulikuwa ndo wakati huo<br />

kwenye Racial Discrimination kubwa – Colorbar – na niliwekwa<br />

katika nyumba ya mmoja katika weupe wenye hadhi lakini alikua<br />

haamini hayo.<br />

Wakanitazama vizuri, mwisho wakanifulia nguo zangu.<br />

Wakaniniuliza wenyewe nguo zako za taka ziko wapi, hebu lete.<br />

Ndivo walivo hao juu ya majumba hayo, watu namna nyingi katika<br />

nchi moja na wako wengine wakikutizama unaona kua<br />

wanakutizama kwa jicho la adhabu.<br />

Basi tukenda tukafika New york tukaingia katika meli<br />

tukaingia katika Bahari. Nilipoona nikakumbuka Qur an kama Aya<br />

15.


<strong>Al</strong>iyoitumia Sayyidnal Imma Sheikh Abdo Bakathir Abdallah Bin<br />

Mohamed Bakathir Sheikhe wa Mashekhe zetu <strong>Al</strong>eyhum<br />

Ridhwaanullah, alipokuja akaonyeshwa Aeroplane mwanzo inapita<br />

Aeroplane watu katika Zawiya yake akatolewa alipoiona<br />

hakutaharaki wala lolote alisema.<br />

“Falamma nasuu maa dhukkiru bihi fatahna lahlim<br />

Abwa-ba shiy hatta idhaa farihu bi maa uwtu<br />

akhadhnahum baghtatan faidha-hum mublisun<br />

faqutwi a daabiral qawmul ladhiina dhwalamu-wal<br />

hamdu Lillahi Rabbil A-lamina”<br />

Ikanijia Aya hiyo na nikaisoma:-<br />

“Waliposahau hayo walionyeshwa kwayo tuliwafungulia<br />

Milango ya kila kitu (<strong>Al</strong>lah Akbar) hata walipokwisha<br />

furahi kwa waliyopewa tuliwachukua kwa ghafla (Adhabu<br />

ikaja kwa ghafla) waka haribikiwa kwa ghafla”<br />

Kama tunavoona mambo ya Kiulaya huja yakenda kama bofu<br />

likawa juu hivi mara likapasuka vita au nini au nini.<br />

“…Faidhaahun Mublisuun”. mara wamekata tamaa hata kusema<br />

hawawezi. Wamekaa tu nyuma ya watu wenye kudhulumu wenye<br />

kuweka mambo si pahali pao ndo maana ya dhulma. “Dhulma”<br />

wanaweka kitu si mahali pake <strong>Al</strong>-Hamdulillah. Basi nilipotizama<br />

pale ilinijia Aya hiyo nikaisoma:-<br />

“Falamma nasuu maa dhukrini bihi fatahna lahum<br />

abwaaba kulli shiy hatta idhaa farihu bima uwtu<br />

akhadha hum baghttan faidha-hum mublisuna<br />

faqutwia daabral qawmil ladhiina dhwalamu wal<br />

Hamdu lillahi Rabbil A-lamiina”<br />

Yule Muegyptain akamwambia yule Mmarekani:<br />

“Mwambie akutafsirie Aya hiyo”. Nikaona taabu kubwa. Hawa<br />

wenyewe masikini wanataka waonyeshe kua hapana watu kama<br />

wao. Wamefika pakubwa pa kukua, hii Aya inaonyesha wapuuzi<br />

kabisa na wako katika hatari. Nikamwambia: “Haya we mtajie”,<br />

16.


Akaniambia: “Hapana usikubali”. Akashikilia, nikamsafiria<br />

akanywea. “Basi twende zetuni” Imekua yale aliyoyataka siyo yale<br />

aliyoyapata. Qur an mimi sina mastaajabu na kua kuna kitu<br />

kushinda Qur an na iko pale hata kitu kimoja. Kila kitu kiko pale.<br />

Haya tuliporudi New York tena.<br />

Sasa mimi nafikiri kua afadhali sehemu hii niifanye Part one<br />

hii niliokwisha sema nikae nifikiri namna ya kukaabili sehemu<br />

nyingine. Safari hii ya Amerika ilikua safari ndefu ina karibia miezi<br />

mitatu, kwa hiyo ndiyo ina mambo kadhaa wa kadhaa”.<br />

17.


SEHEMU<br />

YA<br />

PILI<br />

18.


SAFARI YA PILI AMERIKA:<br />

“Tuliingia mji wa Nishilin na kila mtu akawekwa katika<br />

nyumba fulani, mimi nikawekwa katika Fiski University – pamoja<br />

na President wa Unit Squad Farsuk University pamoja na<br />

President wa hiyo Fiski University alikua ndo anahishimiwa kabisa<br />

New York na ni Mnegro. Hapo alikua na mkewe vile vile wote<br />

watu wahishimiwa sana. Ndo mwenye nyumba nzuri kubwa kabisa.<br />

Wakati wa kula akanambia “Jee! Grace?”; Wakristo<br />

husema kabla ya kula, inaitwa “Grace”, sisi Grace yetu ni:-<br />

“Bismillahir-Rahmanir-Raheem”. Hii ndo kwa ufupi, lakini watu<br />

wajuao kuna vitu zaidi katika vinavosemwa kabla ya kula, lakini<br />

hilo niliona ni refu na “Bismillahir-Rahmanir-Raheem” inatosha<br />

nikafasiri kwa Kiingereza:-<br />

“In the name of God the most compassionate the<br />

most merciful”.<br />

“O! hii sasa tutakua tukiitumia hii inatosha kabisa”. Na<br />

wanao wanafunzi walotoka nchi nyingine za Kiislamu katika<br />

University yao. Baada ya kula wakaniambia vile vile niseme kitu<br />

cha kushukuru kama wanavyofanya wao nikawaambia, siye yetu<br />

nyepesi tunasema:- “<strong>Al</strong>-hamdulillahi-Rabil-alameen”. “Haya<br />

sema” nikawaambia:-<br />

“<strong>Al</strong>l praises are due to God - the Lord the Evolver<br />

of the Universe the Sustainer of the Universe”.<br />

Tukakaa mwisho tukaondoka. Ajabu, namna walivyokaa na<br />

mimi kwa uzuri, mwisho wa mtu kukaa na mtu kwa uzuri sana, tena<br />

hawanijui mwanzo wala mwisho - tena kwa vizuri sana. Nikitaka<br />

kuondoka wemekataa, “Usiondoke”. Hatimae nikaondoka kama<br />

desturi ilivotengnezwa katika Programme.<br />

Nilipofika London nimewaandikia barua, katika barua<br />

nikasema nikatia maneno ya Kiarabu.<br />

“Maa Fil Maqaam Lidhyl Aql Wadhil Adab”<br />

19.


“Hapana katika kukaa moja kwa moja usisafiri kwa mwenye akili na<br />

mwenye adabu, anaetafuta adabu namna ya kuishi vizuri duniani.<br />

Safiri, katika safari kuna faida tano:-<br />

i. Tafrijil Ham - Kutokwa na hamu,<br />

ii. Wa Kasbil Maaisha - Na kuchuma maisha. Mimi hapa<br />

nimeondoka na suti mbili nzuri<br />

kabisa - first class - katika maduka<br />

yaliyo bora kabisa.<br />

iii. Wa Ilmun - Na Ilmu. Huyo alikua Sociologist<br />

mkubwa ana vitabu kadhaa<br />

vya Sociology.<br />

iv. Wa a-dabun - Na adabu, namna ya kujua kukaa na<br />

watu na kusema na watu.<br />

v. Wa Sub-hati Maajidin-Na Sub-ha ya Watu Watukufu.<br />

Watafrijil Ham, Waktisaabul Maa-i-sha, wa Ilmun, wa<br />

A-da-bun, Nikaja nikafasiri kwa Kiingereza, halafu katika barua ile<br />

nikaandika kwa Kiingereza, mambo yote matano hayo nimeyakuta<br />

katika nyumba moja, nikamwambia:-<br />

“Is n‟t it wonderful that one could find all those five<br />

under one roof?.<br />

“<strong>Al</strong>aysa Ha-dha Ajaban Annal Insaan Yajid Hadhal<br />

Khamsa Tah-ta Saqf Wahid?”.<br />

Akaniletea barua akasema:- “Usiseme hivyo, kwenu kwa pili huku, njoo<br />

tena”. Mimi sikwenda njia hizo tena, nilikwenda Amerika tena lakini<br />

sikwenda upande huo, ni ajabu mtu kuyakuta yote matano haya mahali<br />

pamoja. Na ziko nyingine zinahimizwa kusafiri kama:-<br />

“Sa-firu fainna fil Asfa-ri tajid iwadhan<br />

amman tufa-riquhu”.<br />

“Safiri utapata badala ya yule uliyemfariki”.<br />

Wa Ansub (Ujitayarishe) Fa Inna Ladhatil Maaisha (Utamu wa<br />

maisha), Fin nusub (katika tabu), Inni ra-aytu fi Khisaai fil maai<br />

yufsiduhu (Mimi naona kusimama maji huyafisidi), In-sa-la Twabahu<br />

(Hua mema yakichuruzika yakiteremka), Twa-ba (Hua mema<br />

na yakitulizana huharibika), Muftalasatwal usud law laa Firaqu<br />

20,


Lagha-b-masim-ba Law (Ingekuwa hawajafariki vichaka<br />

wasingepata visindika). Wal-ud fi ardhiha Naw-un minal hatwab<br />

(Na udi pahali pake ni namna tu ya mti katika miti na ukiondoka<br />

pale ndo unatiwa ndani ya moto unatoa harufu nzuri). Watu<br />

wakihimizwa sana kusafiri lakini safari haijaachwa kua taabu “Qitatun<br />

minal adhab” yuko mtu mmoja anasema:-<br />

“Balil Adha-b qit-a minals safar”<br />

“Bali adhabu ni sehemu ya safari”<br />

Na zamani ilikua raha yake kubwa ya safari mnafwatana<br />

mnakua ndugu wamoja, kitu kimoja, mnasaidiana mnashirikiana<br />

mnaona raha katika safari, mnokofika mnapokewa kwa wema, sasa<br />

watu wote kila mmoja kashughulika na lake. Hilo ni moja katika<br />

pahala pamoja tulipowekwa.<br />

Sasa tulipokua huko New York tuliwekwa nyumba inaitwa<br />

„International House‟. Siku moja nimekaa nje pale ninamuona<br />

Mmarekani mmoja kaingia na karatasi anadhania “Islam and<br />

Religion” (Islam na Dini) nikasema huyu amedhania Uislamu si<br />

Dini? nitajaribu kiasi nnachoweza kumfahamisha kua Uislam ni<br />

dini; tena ni dini kuliko dini nyingine zozote bali mbele ya Mnyezi<br />

Mungu hapana inayoweza kuitwa dini illa Uislamu.<br />

“Innad-Deena Indallahil Islam”<br />

“Hakika dini kwa Mnyezi Mungu ni Uislamu)”.<br />

Qur an: 3:19.<br />

Si kwa kua tunaambiwa na Qur an tu, lakini mafundisho yake na<br />

namna zake na maisha yake inaonyesha dini ya kweli, na kwa<br />

Mnyezi Mungu ni Uislamu.<br />

Basi nikaanza nnaingia ninamfahamisha tukenda mpaka<br />

njiani akaniambia: “Basi, basi, mimi ni Muislamu mwenzako, hii<br />

khutba nnakwenda kuitoa YMCA, na namna ulivonieleza, wewe,<br />

naona wewe utaeleza vizuri kuliko ntavoelezea mimi kwa hivo<br />

wewe utakwenda ukaitoe khutba hii na ili nisiikose hukai hapa tena<br />

utakuja kukaa nyumbani”.<br />

Nikamwambia si kitu lakini mimi nimewekwa hapa.<br />

Akawapigia simu walioniweka, yeye yule akataka kujua mie<br />

nimekubali, akanipigia simu akataka kujua Adresi, akapigiwa na<br />

21.


simu kua niko huko nyumbani nnakokwenda nkakae. Bila shaka<br />

nikakaa akaja na mimi nikaenda nikahamia. Namna tulivyozoeana<br />

kwa muda mchache. Akastaajabu vipi Mmarekani si Muislamu ama<br />

mnaona leo udugu wa Kiislamu, nikamwambia laa ni udugu wa<br />

Kiislamu:<br />

“Innamal Muuminanuna Ikhwana”<br />

(Hakika si jinginelo ni kuwa waumini wote ni ndugu)<br />

“Fa Aslehu baina Akhawaykum”<br />

“Patanisheni baina ndugu zenu”<br />

Qur an: 49:10.<br />

“Wat Taqul Llaha……..”<br />

“Na wamche Mnyezi Mungu”.<br />

Nikamuuliza wakati mmoja alikueko, ajabu, akiitwa Bwana<br />

kheri ni jamaa yake Marehemu Maallim Mohamed Ahmed wa<br />

Zanzibar anafanya kazi Melini. Nilipopata kuja London nikamuuliza<br />

pana watu wa Kingazija huko. Akanipa Adresi, Mohamed Ahmed<br />

Jae. “Laa Ilaaha Illal Lah” Akanipa Adresi kwa kua nikienda<br />

Amerika nitajaribu kuuliza nayo ni kuuliza tu. Lakini pahali kama<br />

Amerika, Umtafute mtu wapi!.<br />

Huyu nilipomuona Muislamu nikasema nitamuuliza alaa<br />

kulli hali. “Oo! yule Mzanzibari?” Hakujua kuwa ni Mngazija au<br />

Mnini – maadam katoka Zanzabar basi ni Mzanzibari akasema<br />

“Utamuona lakini kwanza twende tukakae nyumbani asije<br />

akakuchukua. Tukakaa akatengeneza khutba yake, akamaliza.<br />

Akaniambia “leo tutakwenda, <strong>Al</strong>khamisi usiku utamuona pahala”.<br />

Tukaenda katika majumba ya Sky Scrapers moja za New York tena<br />

kuna Maulidi wanasoma kila <strong>Al</strong>khamisi tukafika kwenye “Yaa<br />

Naby Salaam <strong>Al</strong>ayka Yaa Rasul Salaam <strong>Al</strong>ayka” nikamwambia:<br />

“Amma wewe Yaa Naby umefika mbali mpaka Huku!”.<br />

Baada ya Maulidi yule Mzee yuko hapo. Huyo Mzee<br />

mwenyewe Mruwada wa Jumbe Fumu. Nikamwita huyo mtu wa<br />

huko nikisikia mtu ananiambia. “Huyu mtu wa huku lakini<br />

anaonyesha Mngazija”. Nikamwambia: “Wee nani?” akaniambia<br />

“Mimi Mruwada wa Jumbe Fumu”. “Nani jamaa zako?”<br />

22.


“Mahmudu wa Jumbe Fumu, ni katika walionilea Mimi, anaitwa<br />

Mahmudu wa Jumbe Fumu na wamenikhusu kwa upande wa<br />

ukeni”.<br />

Mtu akiitwa: Mahmudu Bin Kimwana Jumbe Fumu au<br />

Abdul-ghanii wa Jumbe ndo mwanzo akiitwa wa Jumbe Fum.<br />

Nikamwambia: “Hawa ndugu zako ndo walonilea!”. Basi pale pale<br />

akaanza kujifakharisha kwa wale – “Huyu mwanangu” – “This is<br />

my son I have rasied him, my Brothers have raised him”<br />

wamemnyanyua - yaani wamemlea – “He must come and stay with<br />

me (Aje nyumbani akae na miye), Na hivo twende zetu sasa hivi”<br />

Nikamwambia” “Haiyumkiniki nimechukuliwa kwa hishma na kwa<br />

azma, na azma zenyewe bado hazijatekelezeka, itakuwaje!” - Laa<br />

Ilaaha Illa llah - akakubali.<br />

Basi tukaenda mpaka baada kutengenezwa tena ikatiwa<br />

tukenda Maulidini, tukaenda tukafanya ile khutba ikawa Ghas-ya<br />

kwenye khutba. Kuonyesha nini Uislamu, ni kama khutba ile<br />

niliotoa katika – King Abdul-Azeez University – “What is Islam”<br />

Hii nimesema: “The real meaning of Islam” lakini ile nimesema<br />

na watu si Waislamu – iko tofauti sana.<br />

Katika niliowaonyesha usawa katika Uislamu na umoja na<br />

undugu nime Emphasise sana na yale niliokua nikielezea huko<br />

nyuma huko, na kwengineko kama: “Qu-lu, a-manaa Billahi<br />

wama unzila ilayna” (sema tumeamini Mnyezi Mungu na<br />

yaloteremshwa kwetu) – na hiyo – “Yaa ayyuhaa Naas inna<br />

khalaqna-Kum min dhakarin wa untha” – Sote ni namna hiyo<br />

hatujui sisi tofauti ya Rangi wala Nchi wala Nasabu – wala nini.<br />

Ikiwa kuna watu hawatumii, hawataki, pale mbali, lakini<br />

Uislamu umeamrisha kama hawaongei mawazo mengine ambayo<br />

watu hawayataki au hawawezi kuyafwata lakini wamejua Uislamu<br />

umeamrisha.<br />

Katika kuuliza ilipokuja katika usawa, kwenye usawa<br />

ilivokwisha ikaja suala, Akainuka Mnegro mmoja akasema “Wewe<br />

unasema katika Uislamu unasomesha Usawa mbona kuna watumwa<br />

katika Uislamu unakubali tu?” Nikamwambia “Ukristo<br />

hayakubaliwi hayo au hapana? wewe Mnigro umekujaje huku<br />

Amerika? umetekwa, umetiwa kamba, umetiwa katika atlantic<br />

Ocean, umefanywa mtumwa kwa nguvu, na hivi umeletwa huku,<br />

umeelimishwa umefanywaje!” Aaa! wakamvamia Wanegro<br />

wenzake wakamwambia – “We ndo wa kusema maneno namna<br />

23.


hiyo, maneno gani hayo!”. Nililetewa barua kua walisilim watu kwa<br />

sababu ya khutba zile zilotolewa YMCA.<br />

Tukarudi England lakini ilitokea ilikua na hamu sana kurudi<br />

kwa Meli. Kwa Meli kutoka New York mpaka Southampton, nilikua<br />

kila nnapokwenda naambiwa hapana Meli asilani sasa shauri gani?<br />

hata siku moja hiyo tukalala nikaona “Queen Elizabeth” Meli<br />

kubwa lile linakuja New York kutoka Southmpton (London)<br />

asubuhi nikaambiwa kua siku ya pili au ya tatu kuna safari, kuna<br />

Queen Elizabeth ipo, inatoka New York inakwenda London.<br />

Basi nikapanda Queen Elizabeth toka New York kwenda<br />

London bila shaka kwanza unafika Southampton. Meli pandikizi la<br />

Meli naona ni katika Meli kubwa zilokuweko wakati wake duniani.<br />

Ilikuepo “United States” ilikuwepo “France, Normandee”<br />

ilikuwepo Queen Elizabeth na Queen Mary!<br />

Sasa safarini tumo ndani ya Queen Elizabeth nikaona katika<br />

Atlantic Ocean Baharini kama Jabali katika Bahari nikauliza<br />

nkasema “Kuna Jabali katika Atlantic Ocean?” nikambiwa “Laa, ile<br />

ni Queen Mery inatoka Southampton inakwenda New York?.<br />

“Aajib, ni kama Qur-an ilivosema, Quran inasemaje?”<br />

“Walahul Jawaaril, Manshaa-ji Fil Bahri Kal<br />

Aalaam”<br />

“Na vitokuja kuzaliwa (havipo sasa) (Vitakuja kuzaliwa)<br />

katika bahari vitakua utadhani jabal”.<br />

Qur an: 55:24<br />

Nikaona Quran haijabakisha kitu “Walahuljawaaril Munsha-a-ti<br />

kal Aalaam fa Biayyi a-Laai Rabbikum a-tukadhdhiba (Ipi<br />

katika Miujiza ya Mwenyezi Mungu mnaikadhibisha?).<br />

Hata safari moja neno husemwa pamoja na neno jingine.<br />

alikuja Sheikh Shuayb, ndo alokua Mwanachuoni Mkubwa kabisa<br />

Uganda akaja Unguja. Kwanza alichukua Uislamu tu kwa Sheikh<br />

Abdus-Swamad, mmoja alikua zamani – Zama za Seyyid Ma-jid<br />

akenda kule. Mimi nimemkuta Mzee – Sheikh akaja akawa anataka<br />

kusoma hasa akataka kusoma “Mantiq” na ndo alosimamia Maulidi<br />

sana baada ya Shekh Abdur-Rahman Bin Aqeed – <strong>Al</strong>oyatia Maulid<br />

Uganda wakasilimu watu kwa maelfu siku hiyo.<br />

Mwanzo wa kusomwa Maulidi walisilimu watu kwa maelfu.<br />

24.


Watu walivosikia Matwari na nini, wamekimbilia<br />

kusikiliza na waliposikia khutba na kuona wameyumba,<br />

wamefanyaje, walipoondoka pale watu kwa maelfu wamekua<br />

Wailsamu. Hata wakataka kushitakiwa kua wamepiga ngoma<br />

kwa jina la Dini. Ikafanywa kesi – Seyyid Ahmed Ibn<br />

Abdur-Rahman akafanya, akasimamisha, akashinda.<br />

Basi tangu wakati huo wanaingia watu ndani ya<br />

Uislamu kwa Maulidi na Matwari. Wanavalia watu<br />

wanakwenda waganda wanavaa vizuri mpaka huenda<br />

wanakutana kutwa wanakaa pamoja wanasoma Maulidi,<br />

wanakula wanawafikiana, wanasilimu, wanaalika wakubwa<br />

wa nchi wanasheherekea.<br />

Mwanzo nilimuona Iddi Ameen huko katika Maulidi namna<br />

hayo pamoja na yule President – <strong>Al</strong>otolewa Karibu, walikuja<br />

pamoja punde baada ya Revolution ya Mutesa kabaka Mutesa –<br />

Mkutano mkubwa Sub-hana watu wanoshughulika na Uislamu na<br />

mambo ya kheri wanastarehe sana.<br />

Twayyib, basi alikuja Unguja ye Sheikh Shuyb lakini kaja<br />

baada ya kua kasoma namna hiyo tangu hapo – Fiqihi, kasoma na<br />

Nahaw, kasoma namna hiyo kasoma Mantiq na kiasi alivosoma,<br />

akaja mwisho akaja akachukua Twariqatish Sha-dhiliya<br />

Shurtwiya kwa Seyyyid <strong>Al</strong>y Bin Ammi yangu.<br />

Vile vile Seyyid Mohamed Bin Shekh El-Maaruf, Seyyid<br />

<strong>Al</strong>y ye yuko hapa hapa Babake She Hamadi. Hao wote Baba zao<br />

ndugu – yeye Seyyid <strong>Al</strong>y Bin Sheikh Seyyid Abdur-Rahaman na<br />

Babangu. Hata Sheikh Shuayb alipata kuniambia: “Nchi hii kama<br />

mmeekewa nyiye, Sayyid Abdur-Rahman kaja kaleta Maulidi,<br />

Sayyid <strong>Al</strong>y kaleta Twariqa-Sha-dhiliya, wewe umekuja<br />

umenisomesha”.<br />

Basi akaja nikamchukua Beyti-Ras kama unavojua baadhi<br />

ya watu – kumejengwa Msikiti mkubwa – mkubwa kwa sababu ya<br />

Watoto wa Boarding. Zamani Boarding ilikuwa Dole, na mimi<br />

nilianza kusomesha Dole mbali kidogo, Meli kumi unakwenda kwa<br />

mutkari halafu unakwenda kwa miguu. Au Bakhti yake upate gari<br />

ikuchukua mpaka juu huku pakiitwa Dole.<br />

Ikahamishwa halafu ikaja hapa Pwani Beyti-Rasi pahala<br />

Seyyid Saeed Bin Sultan alifikia hapo akitoka Oman, Zamani<br />

mwanzo akifika hapo pakajengwa skuli kubwa – Skuli Techers<br />

25.


Trining na Primary ni Dole Class na ikabidi uwepo Msikiti. Sheikh<br />

Shuayb alipokuja nikamchukua Msikitini nikamtaka atoe Mawaidha<br />

– Hodari wa kusema sana, Faswih na anajua kuchagua maneno, na<br />

nini; na mtu kakulia Uganda lakini anasema Kiswahili vizuri kabisa.<br />

Kaja akasema, pale ni iko karibu na bahari pale, ile Skuli na Msikiti<br />

uko karibu na Bahari, anawaonyesha ukweli wa Uislamu.<br />

Anawaambia “Tazama Qur an inavokwambieni unaona Meli<br />

zinavopitapita hapa nyiye mnastaajabu kua wazungu wamezua zile.<br />

Zile Mnyezi Mungu ameziumba kwa hikma yake; Akawasomea:<br />

“Walahul jawa-ril munsha-atifil fil bahri kal<br />

A‟<strong>Al</strong>aam”<br />

<strong>Al</strong>lahu yar-ham Sheikh Shuayb. Hiyo ndo ya njiani kwenda<br />

Southampton nikarudi nikaenda zangu London kuendelea na<br />

masomo.<br />

Kukaa London yametokea mambo mengi bila shaka,<br />

Mahudhurio Mikutano ya Waislamu, kufurahikia Maulidi, Sifa za<br />

Maulidi kuzifurahikia kushughulika kwa mambo kadhaa hata katika<br />

mambo niloyakumbuka siku za mwanzo mwanzo nilipokwenda<br />

nkayashughulikia.<br />

Mlokuemo katika Dini ni Miraji ilifanzwa London na mtu<br />

alochaguliwa atoe khutba mbele hapo – alikuwa Seyyid Ahmed Bin<br />

Kirami wa India akisomesha Skuli of Oriental African Studies.<br />

Nilikutana na Maalim Zuberi <strong>Al</strong>lahu yar-ham tukenda. Akasema<br />

akatoa khutba na kuonyesha Miraji kua imetokea na hawezi kuitia<br />

wasi wasi, mtu anajua uwezo wa Mnyezi Mungu na Mnyezi Mungu<br />

kusudi kaonyesha kua mambo haya si mambo ya kidesturi kwa<br />

kuanza kutaja kisa, kasema:-<br />

“Sub-hana ladhi asra bi abdihi layla, minal<br />

masjidil haram ilal masjidil-aqswaa”.<br />

Tazama Mnyezi Mungu kaanza kwa kusema “Sub-hana”<br />

katakasika na kila lisilo Laykiana na yeye – yaani msije mkajipima<br />

nyiye mkaona madam nyiye hamtaweza kujifanyia mambo haya<br />

ndo basi hayakufanyika. Haya yamefanywa na yule ambaye<br />

ametakasika na kila lisilolaikiana na yeye Kampeleka usiku mmoja<br />

Mtumwa wake, huyo Abdi wake Asra biabdih Yaani msiri wake<br />

alokiriana nae, yeye kamkiri kua ni Rabb na Rabb kamkiri kua<br />

yeye<br />

26.


ni Abdi wake – Anampa siri zake anamwendesha sio mwendo<br />

anaowaendesha watu wengine.<br />

Imetoka: “Masjidil Haraam Ilal Masjidil Aqswa <strong>Al</strong>ladhii<br />

ba-rakna hawlahu”. Akasema mpaka akalia akaliza watu<br />

nakumbuka ni katika mambo nlomuandikia <strong>Al</strong>-Habib Barua<br />

nilipokua kule na kitu kingine nilichomuandikia ni mkutano wangu<br />

na Yusuf <strong>Al</strong>y, Mkutano wangu na Yusuf <strong>Al</strong>y alo Translate Quran,<br />

na Translation yake ndo inohishimiwa sana.<br />

Nilikwenda nkamtafuta nnamuulizia nkaambiwa yuko<br />

England, wapi,! ikabidi nizunguuke nnamtafuta hata nkapambana,<br />

nkaambiwa nenda mahali fulani labda utamkuta.<br />

Hapo nkenda nkaonana nae - Ni klabu ya watu wanofanya<br />

kazi katika Empire, Empire Club. Nilipokwenda nikaonana na<br />

Receptionist akaniambia: “Je nani, yule Mzee anokaa pale afanzi<br />

lolote anajikalia tu?” Nikamwambia: unaona ni wewe tu kua<br />

kajikalia, ni yeye nnahaja nae. Nkaenda nkaja siku nyingine<br />

nikampata nikamwambi: “Nna haja na wewe”. Akaniambia: “Ndo<br />

wewe ndo unaekuja hapa ukiniuliza nimeambiwa?” nikamwambia<br />

“Naam” “Njoo unataka nini - Come <strong>Al</strong>ong what do you want?”<br />

“Sit down” Nkamwambia: “I have read your translation of the<br />

Quran and I was very much Impressed, very much indeed I<br />

Admire you”. I thought since you are here - still I must come<br />

and see you”. He was Old man <strong>Al</strong>most mystical, kua sufi mkubwa<br />

kawa na Mnyezi Mungu tu hata kusema na watu hasemi na watu.<br />

Akanambia “Naam - Yes you are right”. Nkamwambia: “Nadhani<br />

ulivokua ukiandika tafsiri ile umemuona usingizini Mtume mara<br />

nyingi”. Akanambia:-<br />

“Yes, and I saw him, I felt this was coming from<br />

Heaven to tell me what I should Write and I wrote<br />

that tranlation it took me three years to write the<br />

translation. I was going round and round, I was<br />

busy writing the translation and I visited almost<br />

every place mentioned in the Qur an in my attempt<br />

to write that translation”<br />

Nikamwambia: “What are you doing here, you are so old?”<br />

akanijibu: “Yes where shall I go? Lahor used to be a city of<br />

Islam, Now It‟s no longer. I have a small room here by myself<br />

27.


and literaly intersted in europe and here its easy for people to<br />

contact me”<br />

Ni ajabu namna ninavyoyakumbuka maneno yake,<br />

nimeyakumbuka very cleary na kwa kuya-repeat lakini nikayasema<br />

kwa namna clearly na Admiration yangu imenisaidia<br />

niyakumbuke maneno ndo ilivyo hivyo.<br />

Nikamwambia: “wewe ni mtu wa wapi asili yako wapi”<br />

akanambia: “Mimi ni mtu wa Yemen, Northern Yemen, Baba<br />

yangu alikua mtu wa huko, akaja India akawa mtu wa huko. Na si<br />

yeye tu bali hata Babu yake pia waliishi huko wakaowa, wakaishi<br />

huko”.<br />

Nikamwambia: “How did you manage to combine both<br />

types of Education – Islamic and European secular and<br />

Religion?” Akanambia: “Okey yes, I had a wise Father a learned<br />

person whose wisdom was greater than his knowladge, he told<br />

me: “learn anything you want but mind you would never find".<br />

He is wise who takes what is truth and leaves what is the<br />

incidental”.<br />

Hiyo ndo jawabu yake sasa nkasema kua – “Qur an<br />

imekusaidia sana. Watu walikaa kwa uovu na wewe, lakini Qu ran<br />

imekusaidia namna ya kukabiliana na watu. Aya gani imekusaidia<br />

sana kuliko aya zote?” Akanambia: “Suratil Fati-ha”.<br />

“There is northing like <strong>Al</strong>-hamdu, in the whole of<br />

World litrature”.<br />

Akawa anaingia, anaisoma akaisoma yote, akaisoma kama<br />

asili ilivyo, halafu akaifasiri. Halafu nikaona huyu Mzee leo<br />

nisimweke sana halafu nikija tena ataniona huyu mtu matata. Huyu<br />

afadhali nimuondoe njiani, nikamwambia leo basi afadhali tupige<br />

Fat-ha. “Unataka nini?” Nikamwambia: “General” akatia Fat-ha<br />

tukasoma <strong>Al</strong>-hamdu, akasoma yeye kwa sauti, unaona maana mpya<br />

inakuja kwa msomo wake Yusuf <strong>Al</strong>y <strong>Al</strong>lahu yar-ham.<br />

Siku nyingine tena nikamwambia vipi kwa sababu yeye ni<br />

Mwalimu wangu nikimuona mtu alokua akinisomesha Islamic Law<br />

mzungu Christian English akinistaajabisha nkamwambia: “Vipi<br />

duniani kuwa Prejudice namna hii. Mtu namna ile anatarajiwa<br />

aseme kitu haki tupu”.<br />

28.


“What don‟t you – you mustn`t be surprised to see<br />

people with prejudices… you and I have our own,<br />

let others have their own prejudices”.<br />

Katika maneno alonambia hapa basi tukaendelea hivo hivo<br />

tukicheka, tunazungumza.<br />

Wakati mwingine nikamuona hasemi asilani. Nakaa kimya<br />

namuuliza naona hajanitambua! Ananiambia “Nakutambua si yule<br />

anokuja hapa. “You come here from time” Nikajua leo hayupo<br />

afadhali niende zangu. Msafara wangu wote na yeye hapo<br />

nilipokwambieni karibu na Trafalgel Square. Afadhali niende zangu<br />

nikamwacha. Hayo ndo mambo yalopita nilipokua London.<br />

Mambo mengi yamepita ya mfahamisho baina ya Waislamu<br />

na Wakristo. Pameambiwa katika yalokamatana na Science,<br />

mengine yamekamatana na Politics. Mie kila nkipata nafasi<br />

kuonyesha Uislamu unasema nini nasema, naandamana na mikutano<br />

ya Eastend na mengineyo. Na siku zile kulikuwepo mahali<br />

panaitwa East African House ilikodiwa na nchi za East Afrika,<br />

vijana hupata mahali pa kwenda kupumzika, pakapatikana na<br />

mjumbe wa kukaa nikahamia huko huko. Pahali pazuri karibu na<br />

katikati ya London.<br />

Muda mwingi nilioupitisha London niliupitisha na mimi<br />

nakaa hapo, na halafu, unajua tena Waislamu na vikundi vyao, na<br />

tukikutana wengine wanatualika. Tulikua pamoja na Salim akiitwa<br />

Bwana Awadh Bin Salum Masud alikua akipenda mambo hayo ya<br />

dini, huyazungumza na kuyaeleza.<br />

Anakwenda tunakutana na watu wa Pakistan wapi wapi,<br />

wazee wengine wametoka Suudia Hijaaz. Wamekuja Madaktari,<br />

wazee wengine Madaktari wa zamani wa asili huja mara moja tu,<br />

<strong>Al</strong>ha-sil siku za fursa. Mpaka mwisho ikapita miaka ilopita<br />

tukafanya mtihani miaka 1 – 3 nilikaa kwa sababu ya kusoma hivo<br />

nikafanya mtihani ikabidi nirudi kwetu East – Africa.<br />

Lakini wakati nilikueko Ulaya kila Vication nilichukua fursa<br />

kwenda Ulaya. Nikisikia kuna Group mpya ya watu wanakwenda<br />

“Europe” nami „nikiwajoin‟ tukiingia pamoja kwenda kutembea,<br />

kwenda kutizama Qur an inasema nini. “Siru Fil-ardhi” (nendeni<br />

kwenye ardhi) “Fandhuru” (mtizame) “Kayfa Baada-alkhalq”<br />

(Mnyezi Mungu vipi kaanza kuumba) “Thumma <strong>Al</strong>lahu Yanshiu<br />

Nashatal Ukhra” (Baada ya hapo Mnyezi Mungu anazua mzuo<br />

29.


mwingine kabisa sio ule alioumba mwanzo). Mnyezi Mungu ni<br />

“Latwiif” anajua kabisa undani wa mambo namna ya kutengeneza<br />

na kufanya. “Yarham Man Yashaa” (Anamrehemu amtakae) “Wa<br />

maa antum bi muujiziina fil ardh” (Na nyiye si wenye kumshinda<br />

Mnyezi Mungu kwenye ardhi). Hizo safari zangu za Europe<br />

nimezifanya ngapi, tunakwenda kunapotolewa Notice hapa na huko<br />

katika University halafu unapeleka Application yako kama<br />

umekubaliwa unakuwemo.<br />

Zote mbili nimekwenda nami simjui mtu yeyote, wote watu<br />

wageni namna kwa namna. Bali kuna moja tukaenda tukapita njia<br />

moja zote bila shaka watu wanachukulia mpaka Paris. Hii moja<br />

tukaenda mpaka Spain, Tukarudi France, tukaingia nchi nyingine za<br />

Europe lakini kwa hiyo kwa njia hiyo nikaona nchi zote za Europe<br />

zote Western Countries. Zote nikazipita, kuzitambua na kuziona.<br />

Safari nyingine ndo ntakuja nende kwenye nchi za Eastern<br />

Countries.<br />

Katika fursa kubwa na faida nilizopata nilipokuwepo<br />

England mara ya mwanzo ni kuingia ndani ya msafara<br />

uliotengenezwa kuzunguuka Europe, ndani ya Coach inakwenda<br />

mbio mbio na kwa raha. Nilikua ndani yake, hii ilitengenezwa na<br />

mmoja katika Walimu wa London University, tukaenda tukapita<br />

English Channel tukaenda France tukafika mpaka Paris tukakaa<br />

baada ya Paris tukateremka kwenda Spain. Tukaenda tukafika<br />

Spain. Hiyo Spain kwa wakati mkubwa ilikuwa nchi ya Kiislamu,<br />

Endlus Waislamu wakatawala, wakajenga, wakakaa wakazaliana<br />

ikawa kama nchi ya Kiislamu.<br />

Kila nchi watu wakawahusudu, wakatamani wawe kama<br />

wao, wakawaiga kama huku. Mwisho walivyokuja watu wakaja<br />

wakawaiga Wazungu – hata wanaandika waandishi wa Kiulaya,<br />

wengine wakasema kua wazee wa wakati ule walikua Wakristo<br />

wakisema: “Ama tumepigwa. Watoto wameharibika namna hii,<br />

wanafwata mambo ya Kiislamu na Kiarabu na kuvaa Kiislamu<br />

na hivi”. Na ustaarabu wao wote kama siye tunavopiga kelele<br />

kuhusu uzungu, na wao walikua namna hivyo hivyo.<br />

Waffaqana llahu Limaa Yuhibb wayardha<br />

Wal - Hamdu Lillahi Rabbil a-lameen.<br />

30.


Katika<br />

ulimwengu<br />

wa<br />

Uislamu<br />

(i)<br />

31.


Vitabu vilivyokwishatoka ni:<br />

*1. Maana halisi ya Imaan. (i) (1 st , 2nd & 3rd addition).<br />

*2. Njia nyepesi ya kuijua nafsi yako.<br />

*3. Njia nyepesi ya kujua kitu juu ya uongofu.<br />

*4. Knowledge vision & ecstacy.<br />

*5. Mwinyi Baraka katika ulimwengu wa Uislamu (i) .<br />

*6. Waislamu na Sayansi - Ulu-m.<br />

*7. Kuhifadhi Burda.<br />

*8. Maana halisi ya Imaan (ii).<br />

*9. Muhammad SAW katika ulimwengu wa ghayb.<br />

*10. Siri ya Balaa.<br />

*11. El makhlouq (Viumbe)<br />

*12. Njia nyepesi ya kujua kitu juu ya uongofu. (2nd addition)<br />

*13. Manaqib ya <strong>Al</strong> habbib Sayyeid <strong>Al</strong> Ma`aruf.<br />

*14. Some aspects of concepts of facility in medevial Islamic<br />

Philosophy by Mwinyibaraka.<br />

*15 maana halisi ya Imaani I (3rd. Addittion)<br />

*15. Njia nyepesi ya kuijua Nafsi yako. (2nd addition).<br />

*16. Mwinyi Baraka katika ulimwengu wa Uislamu ii.<br />

*17. Maana halisi ya Imaani ii (2 nd . Addition)<br />

*18. Mwinyi Baraka katika Ulimwengu wa Uislamu i (2 nd . Addi.).<br />

Vitabu ambavyo tunategemea kuvitoa muda si mrefu<br />

(Insha <strong>Al</strong>lah) ni:<br />

*1. Muhammad SAW Bwana wa Mabwana<br />

*2. Waislamu na Sayansi - Ulu-m. (2nd addition)<br />

*3. Muhammad SAW katika ulimwengu wa Ghayb.<br />

Kwa maulizo kuhusu vitabu wasiliana nasi:<br />

Majaalis El Ulaa - El Qadiriyya Sinza,<br />

P.o. Box 15170,<br />

Tel: 0747 483 553<br />

Tel: 0748 595 958.<br />

Tel: 0744 023 703.<br />

Tel: 0741 235 091.<br />

Tel: 0744 299 597.<br />

Dar es salaam.<br />

32.


<strong>Al</strong> habib Seyyid Umar bin Abdallah bin Seyyid Ahmad <strong>Al</strong> Sheikh Abu<br />

Bakar bin Salim (Mwinyi Baraka ). Amezaliwa Zanzibar katika mwaka<br />

1918. Naye alikuwa ni miongoni mwa vijana walionyanyukia katika malezi<br />

kamili ya Uislamu. <strong>Al</strong>ipomaliza masomo yake ya mwanzo katika Qur an<br />

<strong>Al</strong>iendelea kuhudhuria Majaalis za jioni katika misikiti mbalimbali mjini hapo.<br />

<strong>Al</strong>ikuwa ni kijana ambaye uwezo wake katika kuhifadhi Qur an na uzingatiaji<br />

katika masomo ya skuli ulikuwa ni wakupigia mfano. Katika skuli, masomo<br />

yake ya msingi na yale ya sekondari aliyapata katika shule za kawaida za<br />

Serikali ya Zanzibar.<br />

Baada ya kufanya vyema katika masomo ya Cambridge, aliweza kuendelea<br />

katika Chuo kikuu cha Makerere Uganda. Kwa muda wa miaka mitatu<br />

alikuwepo chuoni hapo kuweza kuhitimu Shahada ya: “Diploma in Bias and<br />

Biology”. Mara baada ya kuhitimu masomo yake, alirejea Zanzibar ambapo<br />

alianza kufundisha masomo ya Dini ya Uislamu, na pia alifundisha Biology<br />

katika Vyuo Vya Waalimu Dole na Beitil El Rass.<br />

Kwenye miaka ya hamsini mwanzoni, <strong>Al</strong> Habib alienda tena kusoma<br />

London Uingereza katika School of Oriental And African Studies. Ambapo<br />

alipewa Shahada ya Diploma katika Islamic and Comperative Law. Na pia<br />

alitunukiwa Shahada ya Diploma katika Lugha ya Kiarabu. <strong>Al</strong>iporejea tena<br />

Unguja katika mwaka 1955, <strong>Al</strong> Habib aliteuliwa kushika Wadhifa mwingine<br />

tena Principal katika Muslim Academy, kuanzia mwaka 1960 – 1963. kisha<br />

alipatiwa Schoolarship kutoka Commonwealth kwenda Oxford Univesity<br />

Uingereza. Huko alifaulu vyema katika masomo yake “Comperative Religion<br />

And Philosophy”. Hapo akatunukiwa Degree ya Ph.D.<br />

<strong>Al</strong> habib Umar alikuwa ni miongoni mwa masheikh wanaotuminiwa<br />

katika kuzilea Roho/Nafsi za waumini. Ambao pia wanajulikana kuwa ni<br />

Masheikh wa Kisufi (Taswauf). Miungini mwa Masheikh zake ni pamoja na <strong>Al</strong><br />

Habib Umar Bin Abu Bakar Bin Sumeity, na pia <strong>Al</strong> Habib Ahmad Bin Hussein<br />

Bin Abu Bakar Bin Salim.<br />

Siku ya tarehe tatu March 1988, Sawa na Mwezi 17, Rajab, 1408, Mwaka<br />

wa Kiislamu ilikuwa ni siku nzito iliyojaa majonzi kwa wale wote waliokuwa<br />

wakimfahamu <strong>Al</strong> Habib Umar Bin Abdallah (Mwinyi Baraka). Kwani<br />

<strong>Al</strong>itwawafu akiwa huko katika Visiwa vya Comoro.<br />

“Tunamuomba Mwenyezi Mungu Sub hanahu Wata`ala, ainyanyue<br />

juu Roho yake, Yeye pamoja na Masheikh wote wengine, Maulamaa<br />

pamoja na watu wema wote ambao wametangulia katika Imaan”.<br />

“Amin”

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!