You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
YALIYOMO<br />
No.<br />
Ukurasa.<br />
1. Yaliyomo-------------------------------------------------- i.<br />
2. Utangulizi------------------------------------------------- ii.<br />
3. Dibaji------------------------------------------------------- iv.<br />
4. Siri ya balaa------------------------------------------------ 1.<br />
5. Nini siri ya hizi balaa?------------------------------------ 4.<br />
6. Nini cha kufanya?------------------------------------------ 9.<br />
7. Sehemu ya pili “Wakati”----------------------------------- 15.<br />
8. Tukio la kiyama---------------------------------------------- 19<br />
9. Nyakati za Mnyezi Mungu---------------------------------- 24.<br />
i.
بسم<br />
هللا الر حمن الر حيم<br />
UTANGULIZI<br />
<strong>Al</strong>-hamdullilahi wal khayru wash-sharru bima<br />
shiyati Llah. <strong>Al</strong>lahu mma swalli a`laa habibika Seyyidna<br />
Muhammad wa alih waswahbihi ajmaina wat tabi ina lahum<br />
biihsa nin ilaa yawmid dina. Waba`ad:<br />
Inaonyesha kuwa watu wengi wanaishi bila kujua vipi kuishi.<br />
AJABU. Kufa kila mtu anajua, hata mtoto mdogo haitaji<br />
maelezo yoyote kwa suala hilo la kufa. Kutokana na illa hiyo,<br />
tumeonelea iko haja ya kuandika kijitabu kama hiki ambapo<br />
mtu anaweza kustafidi mengi katika suala la kuishi na<br />
kupambana na mitihani ambayo ndiyo hasa lengo lake. Baada<br />
ya kusoma kitabu hiki utashangaa kuona kuwa umefunukiwa<br />
na akili kiupana ambao labda ingekuchukua siku nyingi<br />
kuelewa hakika yake. Balaa, mitihani, fitna na majaribu ni<br />
neno moja ambalo katika kiswahili hatuna sawa yake. Na hata<br />
tukisema misukosuko haitoshelezi kuwa ndiyo balaa, kwa<br />
sababu misukosuko ni neno jingine kabisa. Mnyezi Mungu<br />
ametaja vifwatavyo kama fitna kubwa kwa mtu ; pesa, mke,<br />
watoto, mali, njaa, mauti, upungufu wa mali na kadhalika.<br />
Lakini wengi watashangazwa na listi hiyo pamoja na kuwa<br />
navyo vitu hivyo siku nyingi sana zilizokwisha kupitia<br />
maishani mwetu. Kila kitu kinategemea ilmu na hakuna lolote<br />
ambalo tunalifanza halina ilmu ndani yake.<br />
Qur an Suratul Twaha 20:50.<br />
"(Musa) akasema: “Mola wetu ni yule liyekipa<br />
kila kitu umbo lake kisha akakiongoza (kufuata kinachowafiki<br />
umbo lake hilo).”<br />
Bila ilmu hatuwezi kuongoza njia - Ndo maana Bwana Mtume<br />
SWA. katuambia:<br />
طَلب العلم فريضة على كل مسلم ومسلمة<br />
ii
(Kutafuta ilmu ni lazima kwa kila muislamu<br />
mume na mke).<br />
Na mambo yote yafanywayo bila ilmu ni yenye<br />
kurudishwa hayakubaliwi. Tutapungukiwa na shida nyingi<br />
tukijua jinsi gani Mnyezi Mungu anavyowajaribu waja<br />
wake na kuwa imara zama za mabalaa kwani:<br />
خيزه وشزه من هللا تعالي<br />
(kheri na shari zote zinatoka kwake Mnyezi<br />
Mungu SWT).<br />
(Amin).<br />
<strong>Al</strong>-<strong>Faqeer</strong>,<br />
Ahmad Sheikh,<br />
Majaalis<br />
Sinza,<br />
Shaaban 24 – 1415,<br />
25 – 1 – 1995.<br />
iii
DIBAJI<br />
بسم<br />
هللا الر حمن الر حيم<br />
Tunamshukuru Mwenyeenzi Mungu kwa fadhila zake na neema zake nyingi<br />
sana zisizohesabika. Na Swala na Salaam zimfikie Mtume Muhammad (SAW)<br />
pamoja na ali zake na awaridhiye maswahaba wake wote – Amin.<br />
Amma Baad : Amesema Mola katika Quran takatifu surati <strong>Al</strong> Ankabuut:<br />
Qur an 29 : 1 – 3.<br />
“Watu wanadhani kuwa wataachiwa pindi wakisema kuwa<br />
tumeamini bila ya kupata misukosuko. Hakika tuliwatiya<br />
katika misukosuko wale ambao waliyokuwa kabla yao wao,<br />
kwa yakini mwenyeenzi Mungu atawatambulisha wale walio<br />
wakweli na atawatambulisha wale ambao ni warongo”.<br />
Ni katika moja ya hekima zake Mwenyeenzi Mungu katika kuwapima waumini<br />
kwa viwango vya imani zao kwake yeye kwa kuwaletea aina mbali mbali za<br />
misukosuko na mabalaa. Na ingawa anavijua Kabla ya kuvipima viwango hivyo.<br />
Na Mwenyeenzi Mungu anafanya hivyo kwa kudhihirisha mapenzi yake kwa<br />
anayemleteya misukosuko na mabalaa, kama alivyosema Mtume Muhammad<br />
(SAW):<br />
ان هللا اذااحب عبدا ابتاله فاذاصبر نجاه واذارضا اصطفاه<br />
(Hakika Mwenyenzi Mungu akimpenda mja humpa mabalaa<br />
na kama akisubiri anamuokowa nayo na akiridhika nayo<br />
humchaguwa (kuwa mja wake wa karibu).<br />
Kwa hivyo basi, muumini wa kweli amewajabika kuridhika na hukumu ya<br />
Mwenyenzi Mungu kwake yeye hata ikiwa ina uchungu wa namna gani. Amesema<br />
Mtume Muhammad (SAW) katika <strong>Al</strong>-Hadithi <strong>Al</strong>- kudsiyy;<br />
من لم يزض تقضاى فا لىتجذر تا سوا ى<br />
iv
DIBAJI<br />
“Asiyeridhika na hukumu yangu, basi na<br />
awe na mola asiyekuwa mimi”.<br />
Kupendwa na Mwenyenzi Mungu kwa njia ya kuteremshiwa mabalaa na<br />
misukosuko ni moja wapo ya neema zake ambayo inazalisha ndani yake<br />
neema nyinginezo zilizo nzuri na muhimu kwa maisha ya muumini hapa<br />
duniani, ikiwemo neema na sifa ya subira. Na subira kama alivyosema Mtume<br />
Muhammad (SAW):-<br />
ا لصثز نصف ا ال ى مان<br />
Sote tunaelewa kuwa Mtume Muhammad (SAW) ni kipenzi cha<br />
Mwenyeenzi Mungu kuliko watu wote. Na katika historia ya maisha yake<br />
kama Mtume wa Mwenyeenzi Mungu alifiliwa na mke wake wa kwanza bibi<br />
Khadija RA na kufuatiliya kufa ami yake na mlezi wake Bwana Abiy twaalib<br />
katika mwaka mmoja. Na Bwana Mtume aliusiya kwa kuwita mwaka huo ni<br />
mwaka wa huzuni.<br />
Na alipokwenda mjini Twaaif katika mwaka huo huo kuwahubiriya watu<br />
wake ujumbe wa Mwenyeenzi Mungu wa Dini ya Islam walimpiga mawe na<br />
kuukataa. Na kwa kuwa ni kama alivyoamrishwa na Mwenyeenzi Mungu<br />
katika Qurani Takatifu Surat <strong>Al</strong> Ahkaaf kuwa awe mwenye subira: Qur an<br />
46:35.<br />
“ Subiri (ewe Muhammad) kama walivyosubiri Mitume<br />
Uwlu-<strong>Al</strong>-Azim. Nao ni: Mitume Nuhu, Ibrahim, Mussa<br />
na Isa (AS)”v<br />
Subira aliyokuwa nayo Mtume Muhammad (SAW) ndiyo iliyokuwa<br />
moja wapo ya silaha aliyotumia Mtume Muhammad (SAW) katika<br />
kuufanikisha kwa kuufikisha ujumbe wa Mwenyeenzi Mungu kwa watu wote<br />
kama Nabii wa mwisho na Mtume kwa watu wote.<br />
Mwenyenzi Mungu amkubaliye <strong>Al</strong> Marhuum Sheikh Ahmad Sheikh wa<br />
Majaalis – Sinza athari yake hii aliyetuachia na nyinginezo kwa manufaa ya<br />
ndugu zake Waislam, na alijaaliye Kaburi lake (Kibaha ) bustani miungoni<br />
mwa mabustani ya peponi- Amin.<br />
v<br />
Ahmad Haydar Mwinyimvua,<br />
Dar es salaam Tanzania.<br />
14 Ramadhani 1424,<br />
9 November, 2003.
بسم<br />
هللا الر حمن الر حيم<br />
SIRI YA BALAA:<br />
Bin Adam hana pahala ambapo hupata utakaso wa moyo kama<br />
anapofikwa na balaa. Mfano ambao ameuelezea Mnyezi Mungu<br />
mwenyewe ndani ya Qur an hakuna kama ule anapotokea mtu kuwamo<br />
ndani ya chombo baharini na ghafla ikaanza mchafuko wa hali ya hewa.<br />
Dharuba toka kila upande, mawimbi mazito na makubwa kama mlima<br />
hakuna nchi yeyote karibuni bali ni bahari pana tu, ambayo mwisho wa<br />
mandhari yake mtu kila upande ni ile ya maji kukamatana na mawingu<br />
tu. Mandhari hiyo lau tofauti ni ndogo na ile ya siifu (khasf: yaani:<br />
“ Quick sends” ), ambaye anayetumbukia ndani yake hukiona kifo ni<br />
chenye kumvaa bila ubishi wowote, lakini mtu hujiona kabisa anakufa<br />
na kukata tamaa ya kunusurika kama aliyoipitia Edmond Dause.<br />
<strong>Al</strong>isema:<br />
“The angry waves and the sight of dangerous<br />
rocks told me that death was near. and the<br />
thought of death made me afraid. I used all my<br />
powers as a man and as a sea man to ascape.<br />
But I did so because I was happy, because I<br />
didn`t coated death, and because I didn`t<br />
wish that I, a living thing made by the service<br />
of God, should became food for the birds and<br />
beasts of the sea……..”.<br />
“mawimbi ya ghadhabu na mandhari ya majabali ya<br />
hatari yaliniambia kuwa kifo kilikuwa kimekaribia, na<br />
mawazo ya kifo yalifanza niogope. Nilitumia uwezo<br />
wangu wote kama mwanamme na baharia hasa, ili<br />
kuikwepa ajali hiyo. Lakini nilifanya hivyo kwa sababu<br />
nilikuwa na furaha; kwa sababu sikuwa nimefunikwa na<br />
kifo. Na kwa sababu sikutegemea kuwa mimi kiumbe<br />
chenye uhai uliotengenezwa kwa huduma yake Mnyezi<br />
Mungu, nije kuwa chakula cha ndege na wanyama wa<br />
baharini…“<br />
1
Katika hali kama hiyo mwanaadamu humuomba Mnyezi Mungu kwa<br />
hali ya unyenyekevu na utakaso mkubwa kweli kweli. Qur an Surat<br />
Yunus: 10:22.<br />
“Yeye ndiye anayekuendesheni katika bara na baharini.<br />
Hata mnapokuwa katika majahazi na yanakwenda nao<br />
Kwa upepo mzuri na wakafurahi nao; mara upepo mkali<br />
Unayajia na mawimbi yanawajia kutoka kila upande, na<br />
wanaanza kufikiri ya kwamba wametingwa. ( Hapo ndipo)<br />
wanapomuomba Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia<br />
utii, (wakisema): “Ukituokoa katika haya, bila shaka tutakuwa<br />
miongoni mwa wanaoshukuru.”<br />
Lakini anapookolewa na akawasili katika ardhi salama kabisa hapo<br />
hapo humfanzia mola wake chungu ya washirika kama siye yeye<br />
aliyekiomba kwa hali ya Ikhlaas kubwa moyoni mwake. Quran Surat<br />
Hud 11:9 –10.<br />
2
“Na kama tukimuonjesha mwanaadamu rehema<br />
inayotokana nasi; kisha tukaiondoa kwake, mara<br />
moja anakuwa mwenye kukata tamaa kabisa na<br />
asiyekuwa na shukurani. Na kama tukimuonjesha<br />
neema baada ya dhara iliyompata mara husema:<br />
“Taabu zimekwisha ondoka kwangu”. (Wala<br />
hashughuliki kufanya mema wala kumshukuru<br />
Mnyezi Mungu). Basi huwa (sasa) ni mwenye<br />
kufurahi sana (na) mwenye kujivuna kabisa”.<br />
Pengine mtu hupewa balaa katika neema, naye mtu hufurahia<br />
na kukongoea kule kukirimiwa kwake. Na anapobalaiwa (tiwa balaa)<br />
katika upungufu wa neema, mara hupayuka akadai kuwa Mnyezi<br />
Mungu amemsahau. Qur an Surat Fajr 89:15-16.<br />
“Lakini mwanaadam, mola wake anapomfanyia<br />
mtihani akamtukuza na kumneemesha, basi husema :<br />
“Mola wangu amenitukuza;” (wala hashughuliki<br />
kufanya mema ili kutengeneza akhera yake). Na<br />
Anapomfanyia mtihani Akampunguzia rizki yake,<br />
husema: “Mola wangu amenidhalilisha, (nikifanya<br />
mema au mabaya ni sawa sawa, hatayashughulikia,<br />
basi naendelea kufanya mabaya)”<br />
3
Kwa nini yapatikane yote haya? Bila shaka sababu ya msingi si<br />
nyingine illa ni ile iliyoelezewa mwenye surat Mulk na nyingine kadhaa<br />
mwenye Qur an. Qur an Mulk 67:2.<br />
“Ambaye ameumba mauti na uhai ili kukujaribuni<br />
(kukufanyieni mtihani); ni nani miongoni mwenu<br />
mwenye vitendo vizuri zaidi. Naye ni mwenye nguvu<br />
( na) mwenye msamaha”.<br />
Katika katiba zake Mnyezi Mungu hapa duniani ni kuwajaribu<br />
waja wake. Kwa hali hii neema ni mtihani na nakma ni mtihani pia. Yule<br />
anayeneemeshwa, anatarajiwa kushukuru; na yule alonakamishwa<br />
anatarajiwa kusubiri. Asiyeweza hayo, basi Mnyezi Mungu anasema:<br />
“……….Na atafute Mola asiyekuwa Mnyezi Mungu na pa kuishi<br />
pasokua hapa duniani.” Hadithi hiyo ina mafumbo mazito ndani yake.<br />
NINI SIRI YA HIZI BALAA.<br />
Bwana Mtume S.A.W anatuambia:<br />
4
(Hakika Mnyezi Mungu alotukuka anapompenda<br />
mja wake humpa mabalaa. Basi akisubiri humuepusha<br />
na balaa hilo. Na akiridhia basi humchagua<br />
(kuwa mja wake).<br />
Hadithi hii inatupa maarifa mazuri ndani yake, nayo si<br />
mengine bali ni yale yanayotuwezesha kugundua siri ya kupendwa na<br />
Mnyezi Mungu imo ndani ya kujaribiwa. Tofauti na mapenzi ya<br />
binadamu anayekuletea kisababu, balaa basi huyo hakupendi. Na<br />
anayekukunjulia mkono basi huyo ndiyo anayekupenda na<br />
kukuhurumia<br />
Mnyezi Mungu anafahamisha mwenye Qur an 2: 155-156.<br />
“Na tutakutieni katika msukosuko wa (baadhi<br />
ya mambo haya); hofu na njaa na upungufu wa<br />
mali na watu na wa matunda. Na wapashe habari<br />
njema wanaosubiri. Ambao uwapatapo msiba<br />
husema: “hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na<br />
kwake yeye tutarejea (atatupa jaza yake).”<br />
Hiyo: “…Wape bishara njema wenye kusubiri…<br />
Wapashe habari njema…” Inagusia pale pale katika kutarajiwa<br />
yule alonakamishwa kuwa atasubiri. Kusubiri ndiyo jawabu la<br />
mtihani, au majaribio, au balaa.<br />
Bwana Mtume S.A.W. amesema:<br />
"....وماجزاءالصبر االالجنو<br />
5
(Hatukujua jaza (malipo) ya subra kingine<br />
chochote illa ni pepo tu.)<br />
Amesema pia katika hadithi nyingine kuwa:<br />
(Muumini hana, anachokosa akineemeshwa<br />
hushukuru (na si vingine,mwenye kushukuru<br />
huzidishiwa huzidishiwa),na akitahiniwa<br />
husubiri (na malipo ya subra ni pepo).<br />
Kwa hivyo huku anapata na huku anapata. Mnyezi Mungu anaonyesha<br />
ndani ya Qur an kuwa lau angekuwa anawapa kila mtu kwa ayafanyayo,<br />
basi wale wenye kumkufuru na kumshirikisha ndiyo angewapa nyumba<br />
nzuri nzuri za dhahabu na fedha na kadhalika kila wakitakacho. Kinyume<br />
nyume mambo yake Mnyezi Mungu. Sisi huona tukineemeshwa sana<br />
ndiyo eti tunapendwa mno, kumbe huwa ni hatari.<br />
Seyyidna Daud As alikaa mwaka mzima bila ya mtihani wa aina<br />
yeyote, basi alishtuka akamuuliza Mnyezi Mungu VIPI? Au amekuwa<br />
miongoni mwa waliochukiwa mbele yake Sub hana wa Taala?. Na ambao<br />
huwa na mitihani mikubwa kupita watu wote hakuna kama mitume. Basi<br />
na warithi wa mitume nao wasishtuke na kuanza kubabaika yanapowafika<br />
mabalaa. Qur an 2:214.<br />
“Mnadhani kuwa mtaingia peponi na hali<br />
hamjajiwa na mfano wa (yale yalowajia)<br />
wale waliopita kabla yenu? Yaliwapata<br />
6
mashaka na madhara na wakatetemeshwa<br />
sana hata mitume walioamini pamoja nao<br />
wakasema: “Nusura ya Mwenyezi Mungu itafika<br />
lini?”. Jueni kuwa nusura ya Mwenyezi Mungu<br />
iko karibu”.<br />
Zipo balaa za kujitafutia mtu mwenyewe- mathalan mtu<br />
kutumbukiza kidole mwenye sega la nyuki na wenyewe wamo ndani.<br />
Zipo balaa nyingine Mnyezi Mungu anaelezea mwenye Qur an<br />
2:195<br />
“Na toeni katika njia ya Mwenyezi Mungu, wala<br />
msijitie kwa mikono yenu katika maangamizi –<br />
zo. Na fanyeni wema, hakika Mwenyezi Mungu<br />
huwapenda wafanyao wema”.<br />
Na mifano kama hiyo mingi Mnyezi Mungu kwa rehma zake<br />
atukinge nayo. Mnyezi Mungu anafundisha tena jinsi ambavyo<br />
tutaweza kufaulu katika kukabiliana na mitahani yake. Ni kama<br />
anaetoa jawabu zake mbele kabla ya mitihani kuletwa: Qur an<br />
2:153<br />
7
“Enyi mliomini jisaidieni (katika mambo<br />
yenu) kwa subira na sala, bila shaka<br />
Mwenyezi Mungu yu pamoja na wanaosubiri.”<br />
Mnyezi Mungu ndiyo huba kubwa (The greatest love). Na kila<br />
anayependa hua hapendi kuwa (kukaa) mbali na mpenzi wake. Basi ikiwa<br />
amri ya mambo ndiyo iko hivyo, basi ni budi kuzidisha subra zetu kila<br />
siku. Fakhri iliyoje kwa watu kusikia kuwa Rais au Mfalme wa nchi yuko<br />
kwa fulani. Siyo yeye yuko kwa Rais au Mfalme, Aa! Rais au Mfalme ndo<br />
yuko kwake au yuko pamoja naye.<br />
Hakuna njia ambapo anafikilia mja katika bahri ya mapenzi yake<br />
kwa Mnyezi Mungu ila kwa kupitia mabalaa. Lakini kwa sababu nafsi ya<br />
neno lenyewe Balaa siyo kiswahili, uzito wake umekuwa na sura ya<br />
tofauti na vile lilivyo hasa. Katika lugha ya kiswahili Balaa inatupa<br />
tafhuma ya hatari isiyoweza kusubiria ndani yake. Na pia inapotafsiriwa<br />
kuwa ni Fitna ndiyo kabisa na inapotafsiriwa kuwa ni mitihani hapa<br />
kidogo ule mmeremeto wa ubaya unapungua kasi. Kadhalika Majaribio<br />
yote ikiwa ni neno lile lile lakini uzito unazidi kupungua, pamoja na kuwa<br />
kwake maneno yote hayo –Balaa, Fitna, Mitihani na Majaribio hakuna<br />
hata moja la kiswahili. Sasa ikiwa hatujapata neno la kiswahili kwa –<br />
“Balaa”- vipi tunaelewa tutakavyo tu. Mnyezi Mungu anatwambia: Qur<br />
an 47:31.<br />
“Na tutakufanyieni mitihani mpaka<br />
tuwadhihirishe (wajulikane ) wale<br />
wanaopigania dini miongoni mwenu na<br />
wanaosubiri, nasi tutadhihirisha habari<br />
zenu.”<br />
8
Mnyezi Mungu hataacha kuwajaribu waja ili kuona ni nani wa<br />
kweli mpaka dunia imalizike. Sasa wapi tutakwenda ambako hakuna<br />
Mitihani Fitna na Balaa?<br />
NINI CHA KUFANYA:<br />
Baada ya kwisha kupatapata siri ya Mabalaa sasa na<br />
tujiulize nini la kufanya ndani ya ule muda wa kusubiri?. Lazima<br />
turudi kwenye ile Aya ya 153 ya sura <strong>Al</strong> Baqrah ambapo<br />
tunashauriwa tujisaidie katika mambo yetu kwa Kusubiri na Kusali.<br />
La muhimu ni huko kusali. Kusali kuna maana si moja tu, ya<br />
kusimama, kurukuu na kusujudu. Lakini swala ina sehemu kubwa ya<br />
Dua, nayo ni maombi kwa Mnyezi Mungu. Swala ni Bridge (daraja)<br />
yenye kumuunganisha Mtu na Mola wake, na Ibada maalumu. Sala<br />
ni rehma, na ndiyo maana katika kumswalia Bwana Mtume SAW<br />
hakuna kusimama, kurukuu wala kusujudu, pia katika sala ya maiti.<br />
Kujisaidia mambo yetu kwa sala, tunapata kauli ya Bwana Mtume<br />
SAW kuwa:<br />
(Mnyezi Mungu amejaalia kila kitu silaha,<br />
na silaha ya muumini ni Dua).<br />
Mnyezi Mungu anafundisha vipi tutamuomba; amma kwa jina lake<br />
<strong>Al</strong>lahu au kwa jina lake Rahman Kwingine anatutaka tumuombe<br />
kwa unyenyekevu na kwa khofu, pengine kwa khofu na kwa kutumai<br />
(confidence) na kwa siri au kwa fakhri au kwa sauti ya juu wala si<br />
kwa sauti ya chini lakini baina yake. Qur an 17:57.<br />
“Hao wanaowaomba (wenyewe) wanatafuta<br />
ukaribiano na mola wao; (hata) walio karibu<br />
miungoni mwao (na Mungu, kama malaika wao<br />
wanafanya yaya haya) wanatumai rehma Zake<br />
na wanaogopa adhabu yake. Hakika adhabu ya<br />
Mola wako ni ya kuogopwa.”<br />
9
Wengine hufanza Tawasssul nyingi nyingi tu, kwa sababu<br />
Mnyezi Mungu ni mwenye kupenda kuombwa na huchukia asipoombwa.<br />
Kinyume na sisi. Tusipoombwa hufurahi, na tunachukia - illa wachache tu<br />
labda, tunapoombwa. Mnyezi Mungu anawataja waja wake wema kwa<br />
kutuambia: Qur an 51:19<br />
“Na katika mali zao ilikuwako haki ya kupewa<br />
maskini aombaye na ajizuiaye kuomba.”<br />
Pia katika Suratul Ma’arij 70:24-25.<br />
“Na ambao katika mali zao iko sehemu maalumu.<br />
Kwa ajili ya aombaye na anayejizuilia kuomba<br />
(japo muhitaji)”.<br />
Sisi tunajitoa katika sifa tukufu kama hizo kwa kuchukia kuombwa.<br />
Kwa hiyo kumuomba Mnyezi Mungu ndiyo jawabu tunapokuwa mwenye<br />
mabalaa. Siku nyingi zilizopita waliteseka baadhi ya watu kwa sababu ya<br />
kumuomba Mnyezi Mungu mpaka ikafikia kuambiwa: Qur an 22:40<br />
10
“Ambao wametolewa majumbani, (mjini) Mwao<br />
pasipo haki ila kwa sababu wanasema: “Mola<br />
wetu ni Mwenyezi Mungu.” Na kama Mwenyezi<br />
Mungu asingaliwakinga watu, baadhi yao kwa<br />
wengine, bila shaka yangalivujwa mahekalu na<br />
makanisa na nyumba nyingine za ibada na<br />
misikiti ambamo Jina la Mwenyezi Mungu<br />
hutajwa kwa wingi. Na bila shaka Mwenyezi<br />
Mungu humsaidia yule anayesaidia Dini Yake.<br />
Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na<br />
Mwenye kushinda.”<br />
Subra ikienda na dua na matendo mema, ndipo Mnyezi<br />
Mungu huepushia watu mabalaa yao. Na miongoni mwa jawabu<br />
hakuna kama ISTIKTHAAR (kufanza wingi ) mambo ya swadaka na<br />
ISTIGHFAAR (kutaka msamaha) kwake yeye Mnyezi Mungu.<br />
Mambo mawili hayo yanapata ( Support ) kutiwa nguvu na aya : Qur<br />
an 71:10-12<br />
"Nikawaambia: Ombeni msamaha kwa<br />
Mola wenu. Hakika yeye ni mwingi wa<br />
Msamaha. Atakuleteeni mawingu yanyeshayo<br />
mvua nyingi. Na atakupeni mali na watoto,<br />
na atakupeni mabustani, na atakufanyieni mito.”<br />
Vile vile Mnyezi Mungu amesema: Qur an Suratul Anfal 8:33<br />
11
“Lakini Mnyezi Mungu hakuwa wa kuadhibu<br />
maadamu wewe ( Nabii MUHAMMAD )<br />
umo pamoja nao ( Hapa Makka ), Wala Mnyezi<br />
Mungu hakuwa wa kuadhibu pia hali ya kuwa<br />
(Baadhi yao wamesilimu ) wanomba msamaha.”<br />
Mtu angetaka aambiwe na nani zaidi ya Mnyezi Mungu hakaik<br />
za namna hiyo ili asikie na kutekeleza. Tazama fadhila za ISTIGHFAAR<br />
zilivo pewa ubora na faida. Mnyezi Mungu anaacha kuwaadhibu<br />
washupavu watenda dhambi katika mji wanapopatikana wenye kuleta<br />
ISTIGHFAAR. Kutokana na wao Mnyezi Mungu anastahi kuwaadhibu –<br />
Ni madogo Hayo ? – Lakini ndiyo kwa vile watu hawataki kutambuwa<br />
wala kuwathamini.<br />
Jambo la pili ni swadaka ambapo Mnyezi Mungu<br />
katika hadithi aliyofahamisha Bwana Mtume SAW kuwa:<br />
الصدقة تدفع غضة الزب<br />
(Swadaka hukinga ghadhabu ya Mnyezi Mungu).<br />
Jee hatuoni fawaida zake ndani ya uhai na maisha<br />
yetu ya kila siku? Inataka mtu achunguze na kufanza<br />
majaribio, hiyo ni ibada tosha na ya uhakika (Creative<br />
worshiping).<br />
Jinsi gani Mnyezi Mungu anavyojaalia mitihani kwa<br />
waja wake. Mwenye mali mitihani yake mingi ni kwenye<br />
mali yake na dhidi ya hali yake, ndiyo kusema masikini.<br />
Wengi wenye mali walizipoteza kwa sababu ya<br />
kuwanyanyasa masikini. A`lim mtihani wake katika ilmu na<br />
dhidi yake kwa wajinga. Bwana Mtume SAW alisema kuwa:<br />
(Ilmu hupata maafa wakifundishwa wasiokuwa watu<br />
wake).<br />
12
Halkadhalika masikini na mahakimu nao wana mitihani yao.<br />
Watu wanne hao tumewaonyesha kwa kuwa wao ndio nguzo<br />
zilokamatia ulimwengu jinsi vile alivyosema Bwana Mtume SAW.<br />
Kwa ujumla Mnyezi Mungu hukinga balaa zetu na<br />
hupunguza ghadhabu zake kwetu kwa ajili ya swadaka. Basi jambo<br />
hilo lingefaa lidumishwe kwa sababu faida zake ni za kuonekanwa<br />
kwa macho hasa, na mambo yetu yamghadhibishayo Mnyezi Mungu<br />
ni mengi. Mambo haya wapo wengi ambao hawana habari nayo<br />
pengine hizo swadaka huchukulia kuwa ndiyo ZAKA.<br />
Lakini tofauti ni kule kuwa swadaka ni ya hiyari, na zaka ni<br />
ya lazima. Swadaka unaweza kumpa mtu yeyote, lakini zaka ni<br />
lazima muislamu anaestahiki kule kupata zaka. Amma sivyo<br />
itakuwa haijaswihi na utakuwa hutahisabiwa kuwa umelipa, na<br />
itabidi kuirudishia tena.<br />
Insha <strong>Al</strong>lah Mnyezi Mungu atuwafikishe katika<br />
kheri tuongokewe kwa yetu, sisi na waislamu wenzetu.<br />
Na tuweke matumaini ya dhati kuwa tutajibiwa kwa<br />
lolote tunaloliomba. Na ndio maana Mnyezi Mungu<br />
akatuambia kuwa: Hadithil Quds:<br />
“Lau wangekusanyika pahala pamoja watu<br />
wote wa mwanzo na wa mwisho, binaadam<br />
na majinni kila mmoja akaomba alitakalo<br />
kwa Mnyezi Mungu katika shida zake, basi<br />
Mnyezi Mungu angempa kila mmoja na<br />
isingekuwa imepungua chochote katika<br />
hazina yake”.<br />
Labda kiasi kile kile cha uzi uliotumbukizwa baharini,<br />
ukanyonya maji na kushirabu barabara.<br />
Huyo ndiye Mnyezi Mungu aliye mkarimu mno na mwenye huruma<br />
isiyomithilika kwa viumbe, Mkwasi mwenye kuneemesha waja wake<br />
atakavyo, wengine anawakunjulia wengine anawakadiria.<br />
Mambo yote tuloyataja na kufahamisha ndani humu ni yake<br />
na kule kuyatekeleza na kuyafuata ndiyo maana ya uislamu.<br />
Qur an 3 : 83<br />
13
“Je! Wanataka dini isiyokuwa ya<br />
Mnyezi Mungu, na hali kila kilichomo<br />
mbinguni na ardhini kinamtii yeye,<br />
kikipenda kisipende? Na kwake<br />
watarejeshwa wote”.<br />
14
Sehemu<br />
ya<br />
Pili<br />
15
WAKATI<br />
Na tarehe yetu yote ni daraja sekunde dakika na saa – SAA!<br />
Wakati umegawika katika mafungu matatu, manne :<br />
i. Uliopita ( Past )<br />
ii. Uliopo ( present )<br />
iii. Ujao ( future )<br />
iv. Milele ( Eternal or Eternity ).<br />
Waliopita huenda waliyajua ya kwetu kama: yajayo; na<br />
wajao hawajui ya kwetu wala waliopita na yajayo. Kwa hivyo<br />
sisi tumekuwa bora kuliko waliopita. Mnyezi Mungu anasema<br />
(ili kuthibitisha ubora wetu kwa kawli fupi kama hii): Qur an<br />
3:110.<br />
“Nyinyi (ndio mmekua ) umma bora (miongoni mwa<br />
nyumma) zilizoletwa kwa watu------“.<br />
Hadithi:<br />
Imetokana na Seyyidna Omar (R.A) alisema:<br />
“Siku moja tulikuwa tumekaa na Bwana Mtume<br />
SAW. Hapo alitokea mtu ambaye nguo zake<br />
zilikuwa nyeupe Pepe na nywele zake zilikuwa<br />
nyeusi sana; hakuwa na alama ya machofu<br />
ya safari na wala hapakuwa na hata mmoja<br />
katika sisi aliyemtambua. <strong>Al</strong>ienda akakaa karibu<br />
na Bwana Mtume SAW. Akiweka magoti yake<br />
karibu na magoti ya Bwana Mtume SAW aliweka<br />
viganja vyake juu ya mapaja yake, akasema<br />
“Ewe Muhammad nambie kuhusu Uislamu.”<br />
Mtume wa ALLAH SWT alisema: “Uislamu ni<br />
Kukiri kuwa hakuna Mungu isipokuwa ALLAH<br />
16
Na Muhammad ni Mjumbe wake, kusali, kutoa<br />
zaka, kufunga Ramadhani, na kwenda Ma<br />
kka ukiweza”. “Umesema kweli”, alisadikisha<br />
yule mgeni. Tulipigwa na mshangao kwa kumuuliza<br />
na kisha yeye muulizaji kusadikisha.<br />
Akauliza tena “Nambie kuhusu Imaan”. Akamjibu<br />
Ni kumwamini Mnyezi Mungu, Malaika<br />
Wake, vitabu Vyake, Mitume wake, Siku ya<br />
kiyama na kuamini kuwa kheri na shari zote<br />
Zinatoka kwake.” “Umesema kweli” akasadi-<br />
Kisha yule mgeni. Akauliza tena: “Hebu<br />
Nieleze juu ya Ihsan”. <strong>Al</strong>isema SAW: Ni kumuabudu<br />
Mnyezi Mungu kama vile unamuona japokuwa<br />
humuoni yeye anakuona.” Akauliza<br />
tena. “Niambie juu ya kiyama”. Bwana Mtume<br />
SAW alisema: “Anaeulizwa hajui zaidi<br />
Kuliko aneuliza”. Yule mgeni akasema: “Nambie<br />
alama zake”. <strong>Al</strong>isema SAW “Kijakazi atamz<br />
aa bwana wake na utaona wachunga wenda<br />
miguu chini, wenda uchi, mafukara (wasiokuwa<br />
na hata makazi) wakishindana kujenga majumba<br />
ya fakhri. Muda mfupi baada ya yule mgeni<br />
kuondoka, Bwana mtume SAW akauliza:<br />
“Ewe Omar jee unamjua ni nani yule aliekuwa<br />
akiuliza? “ Nilisema “Mnyezi Mungu na Mjumbe<br />
wake wanajua zaidi.” <strong>Al</strong>isema ni Jibril<br />
alikuja kuwafundisha Dini yenu (Kwa njia ya<br />
maswali)”.<br />
Imepokewa na Muslim.<br />
17
Wakati seyyidna Jibril AS (The holy ghost ) alipomshukia Bwana<br />
Mtume SAW ( katika karne ya saba) ili amfundishe DINI (ISLAM) kwa<br />
njia ya kumuuliza maswali, akawa anasadikisha kila alipojibiwa, swala<br />
lilikuwa moja zito sana. Lakini aliomba afahamishwe dalili zake tu baada<br />
ya kujibiwa kua “Hakuwa mwenye kuulizwa kwacho ( hicho kiyama)<br />
mwenye kujua kuliko muulizaji”. Bwana Mtume SAW alielezea dalili<br />
zake tu, nazo zilikuwa kama hivi:<br />
i. Mjakazi ( Amati – pia ni jam-u ya umma) yaani: mama.<br />
ii. Utaona wenda miguu chini na uchi, wachunga<br />
mbuzi (cowboys) wakipitana kwa majumba marefu marefu<br />
(Zama ambapo sky scrappers za USA hazikuwepo).<br />
iii. Wanawake wanapokosa haya na kuota mikia.<br />
iv. Qur an itapodharauliwa na kudhalilika.<br />
Bwana Mtume SAW aliendelea mno kuelezea watu juu ya dalili za kiyama baadae<br />
kiasi cha kujenga picha kama hii:<br />
v. Mbali itapokuwa karibu. - ( Ibara hii inadhihirisha umuhimu<br />
wa usafiri kwa vyombo viendavyo mbio kuliko ngamia na<br />
farasi - Kwani wakati farasi anakimbia mfano wa masafa ya<br />
maili sitini kwa saa, roketi itafunika masafa yenye maili<br />
ishirini na tano elfu kwa muda huo huo), na mara mbili ya<br />
roketi, challenger inakwenda maili hamsini elfu katika saa<br />
moja.<br />
vi. Chuma kitapotamka.- ( Mfano wa redio, simu na Telex ambazo<br />
hazikuwepo katika zama zile ).<br />
vii. Mtu mweusi kutawala – ( labda katika zama zile mtawala<br />
mweusi alikuwa ni Mfalme Nagash wa Ethiopia, na katika karne<br />
ya kumi na tisa dunia imejaa watawala weusi, aliyajuaje Bwana<br />
Mtume Muhammad SAW haya?).<br />
18
TUKIO LA KIYAMA:<br />
Tofauti kati ya mwislamu na kafiri ni kuamini mambo ya ghayb ( fact<br />
in exisence) mwislamu ni lazima aamini kiyama kuwa kitakuja bila<br />
shaka yeyote (without any doubt) lau sio lazima kujua kuja kwake.<br />
Qur an Naziat 79:42-44<br />
“Wanakuuliza kiyama kutokea kwake<br />
kutakua lini?. Uko wapi na kuweza<br />
kutaja (wakati wa kuja kiyama ). Mwisho<br />
(wa ujuzi ) wake uko kwa Mola wako.”<br />
Mnyezi Mungu anamweleza Mtume wake Nabii Muhammad<br />
SAW kwa kawli ya wazi wazi kua kipo, hicho kiyama, lakini wale tu<br />
wanaokiogopa ambao watakumbushika, wengine laa !. Na katika dalili<br />
za wazi wazi ambazo ni muhimu kuzijua kwa jicho la mazingatio ya<br />
hali ya juu kabisa ni hizi:<br />
1. Kudhihiri Mahdi<br />
2. Kutokea kwa Dajjaal (Atazaliwa akiwa na jicho moja<br />
kama walivyokuwa kawmu NISA. (Amerika katika noti<br />
yao ya dola 100 ambapo inaonyesha picha ya jicho moja,<br />
utadhani walipata habari zake).<br />
Huyo mlaghai mkubwa jitu moja lenye fitna kubwa kabisa,<br />
ambaye atadai uungu kama alivyodai Firauni wa zama za Nabii Mussa<br />
AS, na tofauti ya muda wa Firauni miaka mia nne, Dajjaal atadumu<br />
duniani kwa muda wa siku arubaini ambazo ni tofauti na siku ya<br />
kawaida. Siku kumi za mwanzo kila siku moja itakuwa kama mwaka<br />
(kwa hiyo ni miaka kumi) siku kumi za pili kila siku moja kama mwezi.<br />
Siku kumi za tatu kila siku yake ni kama wiki moja Na siku kumi za<br />
mwisho kila siku ni kama siku ya kawaida.<br />
Kwa hiyo, siku kumi za mwanzo ni kama miaka kumi. Kumi la pili ni kama<br />
miezi kumi. Kumi la tatu ni siku sabini, ( yaani miezi miwili na siku kumi). Na kumi la<br />
nne ni siku kumi. Jumla ni miaka kumi na mbili na siku ishirini.<br />
19
Dajjaal ataingia kila nchi duniani kudanganya na kufitinisha watu.<br />
Ulaghai atoutumia kama vile kumfufua aliekufa siku nyingi na kuleta<br />
mvua na kuotesha mazao mashambani utavutia watu mno kiasi cha<br />
kumwamini kuwa mungu. Yeye atakuwa na pepo na moto. Wataomkubali<br />
atawatia ndani ya pepo yake, wataomkataa atawatia motoni. Lakini ukweli<br />
wa mambo ni kinyume nyume. Watoingizwa peponi ndiyo watoingia<br />
motoni, na wale watoingia motoni ndiyo watoingia pepo ya Mnyezi<br />
Mungu wa kweli. Nchi pekee ambazo hataingia Dajjaal ni Makka na<br />
Madina.<br />
3. Kuteremka seyyidna Isa AS. (Ambaye<br />
atakuja kumpiga vita na kumuondoa (huyo<br />
Dajjaal). Baadaye ataishi siyo kama Mtume, bali<br />
kama mja mwema aliye mchaji ). – Ataoa ataishi<br />
miaka arubaini atakufa, na Madina katika Rawdha<br />
karibu ya Bwana Mtume SAW ndipo atazikwa.<br />
4. Kutokea Juju wa Majuju. (Ambao Dhyl Qarneyn)<br />
aliyewafungia ndani ya ukuta fulani tangu siku hizo hadi leo<br />
hii bila shaka.<br />
5. Kutokea kwa Dabba. (Mnyama wa ajabu ). Mnyama huyu<br />
atawasemeza watu yale ambayo wanakataa kuyakinisha.<br />
Hakika hii .inafahamishwa kwetu na Qur an ya Mnyezi<br />
Mungu; kwa kila mtu kujipatia mwangaza wa mbele kabla<br />
kuwadia wakati wake ambao kutokea karne hii ya ishirini na<br />
moja sio mbali tena.<br />
Tunaanza kuzoeshwa kumzowea mnyama huyo kabla ya kufika<br />
kwake ili tu, tusifikie mshtuko ambao unaweza kuitoa roho ya mtu mbichi<br />
mbichi. Mfano wa “Mapi show” Unajihusisha vizuri sana.<br />
Mnyama huyo atakuwa na mwendo mkali mno, hatakikosa<br />
atakachokifukuza wala hakitampata kitachomfukuza. Ataandika usoni<br />
mwa muumini: “huyu ni mtu wa peponi”. Na uso wa mtu huyo utang`aa<br />
sana. Na katika uso wa mtu wa motoni ataandika: “huyu ni ka fir” na uso<br />
wake utapiga weusi. Na leo praktizi za kujitia weusi zimeanza hali ya<br />
kuwa huyo Dabba wenyewe hajaja. Dabba atakuwa miungoni mwa dalili<br />
za mwisho tena.<br />
6. Kuchomoza jua magharibi ya ardhi:<br />
Hii ni ishara ya wazi wazi yenye kuogofya ( kuogopesha)<br />
mno – <strong>Al</strong>lahu Akbar. Bila ya shaka ionekanapo hitilafu<br />
katika maumbile bin adam hushangaa,<br />
20
hushtuka na pengine humiliki hali fulani akataka afanze<br />
ambalo uwezo wake ungeruhusu.<br />
Viumbe vyote vimezoea kuona jua likichomoza toka mashariki ya<br />
dunia kwenda magharibi. Lakini siku hiyo litachomoza toka magharibi<br />
na kuja zake hadi katikati ( kama inavyokuwa saa sita, saa za kulingana<br />
kinvuli ), na litarudi huko huko maghribi.<br />
7. Utapodhihiri moshi: Moshi uliokusudiwa hapa ni ambao<br />
utaenea dunia nzima. Moshi huu utakuwepo duniani muda wa<br />
siku arubaini. Moshi utakuwa ukitoka puani, machoni na<br />
kwenye duburi ( tupu ya nyuma ) ya kila kafir mpaka<br />
ataonekana kama mlevi.<br />
Hali hii ya kuonekana watu walevi na hali hawakunywa pombe,<br />
bali ni adhabu ya Mnyezi Mungu ni kali. Imetajwa ndani ya Qur an<br />
ikiashiria juu ya dalili za kiama vile zitavyojionyesha. Taathira ya<br />
moshi kwa muumini itakuwa kama mafua mafua tu hivi. –<br />
Hizi ni miungoni mwa taabira ( prophecies ) alizozielezea Bwana<br />
Mtume SAW. Na kila mtu ni muhimu azijue mapema na kuwafundisha<br />
watoto wake.<br />
8. Kuharibika <strong>Al</strong> Kaaba: Baada ya kufa nabii Isa AS. Na<br />
kuzikwa Madina, <strong>Al</strong> kaaba itaharibika juu ya mikono ya<br />
Habash.<br />
Katika karne ya saba wakati wa uzawa wa Bwana Mtume SAW<br />
<strong>Al</strong> kaaba ilitaka kuharibiwa na Abraha – Ambaye alikuwa mfalme<br />
muhabesh aliyeweka jeshi lake Yemen. Mnyezi Mungu alituma jeshi la<br />
ndege -Ababiil - wakiwa na vijiwe midomoni idadi ya jeshi zima la<br />
Abraha, wakawa kama majani yaliyotafunwa na kisha yakatemwa.<br />
Baada ya tukio hilo hakuna nchi yeyote duniani iliyojasiri kutaka<br />
kuihujumu nyumba ya Mnyezi Mungu mpaka hii leo. Lakini<br />
ipo kawli toka kwa Bwana Mtume SAW kuwa katika akheriz zaman<br />
madola makubwa ya dunia yatapata kishawishi kutaka kuihujumu<br />
lakini Mnyezi Mungu atawateremshia mabalaa mjini mwao washindwe<br />
kujitambua nafsi zao. Hakika ya <strong>Al</strong> kaaba inabaki kuwa ni nyumba ya<br />
Mnyezi Mungu ambayo iliyojengwa na Seyyidna Ibrahim ASW.<br />
akisaidiana na mwanawe Seyyidna Ismail AS. Na ni pahala pa amani<br />
siku zote, na hilo limetimia tangu wakati wa seyyidna Ibrahim ASW<br />
mpaka leo, si chini ya miaka elfu sita iliyokwishapita.<br />
21
9. Kunyanyuliwa Qur an: Qur an ndiyo kitabu cha mwisho<br />
kwa wanaadam duniani, na kiliteremshwa kwa Bwana<br />
Mtume Muhammad SAW katika karne ya saba, wakati<br />
dunia ilikuwa imezama katika ujaahili. Ikiitwa “Dark age”.<br />
Bwana Mtume ndiyo Mtume wa mwisho aliyeteremkiwa na roho<br />
mtakatifu (The holy ghost ) naye hakuwa msomi wala kuandika hakuwa<br />
anajua. Hakika hiyo ilikuwa hoja kubwa na yenye nguvu kweli. Lakini<br />
haikusaidia kuwafanya wapinzani wa uislamu wajizuie kumtuhumu kuwa<br />
ameiandika yeye. Ajabu ni kwamba wenye ilmu hata wakikusanyika<br />
pamoja kuandika mfano wake wasingeweza na wala hawataweza<br />
Pambano liko wazi kama watapatikana wa kuandika wajitokeze.<br />
Wengine wamemsingizia kuwa Bwana Mtume SAW alijitangazia<br />
utume yeye mwenyewe. Kwa wenye kujua vipi mitume<br />
inavyotayarishwa, madai kama haya hayawapi taabu kwa vile<br />
yaliyodaiwa na majaahili waliorubuniwa na mabwana zao watafanya<br />
nini?. Miungoni mwa kawli zake Bwana Mtume SAW kuhusu mfano<br />
kama huo uliobeba kichwa cha maneno, ni ule wenye kuelezea kuwa:<br />
“Zitakuja zama hautabaki uislamu illa jina<br />
lake tu, na haitabaki Qur an illa maandishi<br />
yake tu ( Rasmuhu )”.<br />
Usemi huo unaonyesha kuwa zama hizo ( na huenda zimeshafika )<br />
watu hawatajishughulisha na kusoma Qur an, kwa hiyo Qur an itafanana<br />
na nyumba iliyohamwa - lakini kunyanyuliwa Qur an ni yenye uzito<br />
tofauti kabisa, kwani hata vifuani haitakuwepo na katika kurudi watu wa<br />
ardhini kuwa makafiri hiyo ndiyo hatari zaidi. Mfano wa kuidharau Qur<br />
an mpaka kufikia wazee kuwashughulikia mno watoto wao kwa masomo<br />
ya kizungu kuliko Qur an ambayo ni rahisi mno, ni moja miungoni mwa<br />
dalili za wazi ambazo zinatuonyesha wapi tunakwenda!.<br />
Pia kupuuza sala kwa nyudhuru za nguo chafu na kila siku<br />
tunazifua kwa masabuni chungu mbovu. Vipi Bwana Mtume SAW<br />
asemee juu ya sala kuwa ndiyo nguzo kuu ya uislamu, kwa hivyo<br />
mwenye kuisimamisha (Iqamu swalat ), basi amesimamisha dini<br />
(Uislamu ), na mwenye kuitupa akaipuuza, basi ameivunja dini. - Halafu<br />
mtu ajifanze hamnazo na kwa makusudi aiche hiyo sala?. Basi kama<br />
imedaiwa kuwa watu wa ardhini watarudi kuwa makafiri, basi, ni wazi<br />
kuwa zoezi lake limeshatwaa nafasi.<br />
22
Amma kwa dalili za kiyama, kila muislamu anajua kwa hiyo siyo<br />
rahisi kuvutiwa na hadithi za dhana dhana na kudanganya watu. Mfano<br />
wa utabiri wa Pop wa 1959 kuwa mwaka 1960 ingekuwa mwisho wa<br />
dunia. Miaka arubaini baadaye utabiri wa Nishel Nostrodamus kwa july<br />
4 na kama hizo. Kiama hakitatokea ila chini ya bendera ya uislam.<br />
Kiama hakitatokea mpaka akosekane katika uso wa ardhi ambaye<br />
anasema: “<strong>Al</strong>lah, <strong>Al</strong>lah"; Lau baadhi ya dalili zimeisha jitokeza,<br />
mfano wa kwenda uchi, wanawake kukosa haya, wanawake kuwa na<br />
mikia, na nundu kama ya ngamia kichwani, mbali kuwa karibu, vyuma<br />
kuzungumza na mtu mweusi kutawala. Lakini hizo tisa bado kuanza<br />
hata moja. Mambo yatakapokuwa tayari, bila shaka yeyote tutaanza<br />
kuzishuhudia moja baada ya moja kama tutakuwepo.<br />
23
NYAKATI ZA MNYEZI MUNGU:<br />
Mnyezi Mungu ndiye aliyeutoa wakati ambao yeye haumuhusu<br />
kitu chochote. Wakati wanasayansi wanaitakidi kuwa ili ufanzike wakati<br />
ni budi kuweko ( vitu vitatu ) Nafasi yaani Volume. Mnyezi mungu<br />
kaenea kila pahala, kwa nafasi haimhusu chochote. Masafa yaani<br />
Distance ( hapa na kule ), Mnyezi Mungu haitaji masafa. Na ili upatikane<br />
wakati vile vile ni lazima kuwepo Kasi yaani Speed, au mwendo, ( bila<br />
ya shaka ni wa kuzunguka). Kwa hoja hii wamehusisha maumbo yaliyoko<br />
mbinguni ambayo yote ni yenye kuzunguka. Mnyezi Mungu haimpasii<br />
jambo hilo hata siku moja. Mnyezi Mungu ameelezea juu ya wakati katika<br />
Qur an: Suratus sajadah 32:5<br />
“Anapitisha mambo yote yaliyo baina ya<br />
mbingu na ardhi, kisha yanapanda kwake<br />
kwa siku moja tu ambayo kipimo chake ni<br />
miaka elfu mnayotumia nyinyi katika<br />
kuhisabu kwenu”.<br />
Katika mfumo huo mwenye akili timamu hatakosa kuona hizi saa<br />
24 zetu ni fupi mno kiasi cha kumaanisha kuwa saa 1 yake ni miaka 41. 16<br />
au miaka 42.4. Tukitizama katika sura ya pili inayoelezea wakati. Tutaona<br />
ndani ya: Quran suratul ma`arij 70:4<br />
“Malaika na roho hupanda kwake katika<br />
siku ambayo muda wake ni miaka elfu<br />
hamsini”.<br />
24
Katika sura hii tunaona kuwa saa moja yake ni sawa na miaka<br />
2083-2088. Mtu mwenye akili timamu hakosi kuona kuwa katika saa<br />
yake hiyo ni kiasi ambacho kinamfikia Nabii Zakari AS, Yunus AS, nk.<br />
Mtu akitafakuri juu ya mtoto wa digi digi aliozaliwa na baada ya saa<br />
moja tu anaenda mbio na mama yake, wakati binadamu labda miaka<br />
miwili na zaidi ndio aje kumudu zoezi hilo, basi ni sawa na kusema:<br />
“Saa moja ya digi digi ni sawa na miaka<br />
miwili ya mwanaadam”.<br />
Ndani ya nyakati mbili hizi mtu yoyote mwenye akili<br />
hatokosa kuona kuwa suala la: “kupitwa na wakati”, kama<br />
ilivyozoeleka mno kwa vijana wa leo, ni kama upumbavu<br />
mtupu. Msemo huu unawaandama masikini wa kutafakari<br />
katika jamii.<br />
Katika wakati wa kwanza na wa pili walioudiriki ni Seyyidna<br />
Adam ASW na Mama Hawwa AS. Katika wanaadamu. Na pia<br />
wamediriki huu wakati wetu wa masaa 24. Wakaishi hadi miaka 1001<br />
(elfu moja na moja ) hapa duniani.<br />
Wanasayansi waliochunguza na wakakubaliana kuwa ndiyo<br />
hakika kwamba mwanga wa jua unatembea miaka 186 elfu kwa sekunde<br />
moja, nyota aina ya GALAXY katika muda huo huo inakwenda kiasi<br />
cha maili 105 ya mwanga, ambapo kila mwaka wake mmoja ni sawa na<br />
miaka Trillion sita (6, 000,000,000,000,000,000 ). Suala la kupitwa na<br />
wakati hapa ni la kipumbavu kabisa.<br />
Mfano wa Betilquise ( Beyt jawzaa ), nyota moja<br />
kubwa mno, imethibitishwa kielimu ( Science ). Mwanga<br />
wa jua kwa spidi yake ya 186,000 maili kwa sekunde,<br />
itakuwa kiasi cha miaka 32 elfu kufikia mara moja na si tena<br />
illa baada ya miaka elfu 32 mingine. Na papo zipo nyakati<br />
ambazo haziwezi kuingia ndani ya akili ya mtu. Dakika<br />
moja ni sawa na miaka mia tano ya anga.<br />
Na upo huo wakati wa milele ambao ndani ya akili<br />
ya mtu haufikirikiki kabisa. Mnyezi Mungu ndiye anayejua<br />
– Wallahu ya`alam bi swa waah.<br />
WABILLAHIT TAWFEEQ.<br />
25
<strong>Al</strong> habib <strong>Al</strong> <strong>Faqeer</strong> Ahmad Sheikh Mohamed Sheikh Msiha,<br />
amezaliwa Singida mkoa wa Dodoma, mwaka 1938. Amepata elimu ya<br />
sekula Unguja na amebahatika kupata elimu ya juu katika chuo maarufu<br />
Afrika ya Mashariki Makerere Uganda.<br />
Elimu yake ya Dini ameipata hapo hapo Unguja toka kwa Masheikh<br />
mbali mbali, baadhi yao ni:<br />
Sheikh Sleiman <strong>Al</strong>wi (Muhib Rasul) (<strong>Al</strong> Marhum).<br />
Sheikh Seyyid Mansab.<br />
Maalim Himid (<strong>Al</strong> marhum).<br />
Maalim Hemed Muhamed El Buhry.<br />
Sheikh Seyyid Qamus.<br />
Sheikh Muawwiya Ibn Abdul Rahman.<br />
Sheikh <strong>Al</strong>ly Muhamed Comorian.<br />
Sheikh Ibrahim Mzee Ahd.<br />
Sheikh Haj Mzee Ahmad Msiha.<br />
Amma Elimu ya Nafsi na Roho Amepata Ijaza yake toka kwa A`limu<br />
mkubwa Duniani <strong>Al</strong> Habib Sayyid Omar Bin Abdallah (Mwinyi<br />
Baraka).<br />
Sheikh Ahmad amewahi kufanya kazi katika jeshi la Polisi<br />
Tanzania Bara katika mikoa mbali mbali mpaka alipostahafu.<br />
Katika umri wake wote Sheikh Ahmad alijahid katika kuendeleza<br />
Uislamu kwa kusomesha na kuandika vitabu vya mada na maudhui<br />
mbali mbali katika Uislamu. Pia alianzisha Majaalis Sehemu mbali<br />
ambazo ziko mpaka leo, Mtaa wa Pemba, Sinza, Bungoni, kijito nyama,<br />
Sadani (Ilala) na Kibaha (Misugusugu) ambapo ndipo ilipo Dhwarihi<br />
yake (alipozikwa).<br />
Sheikh Ahmad ametwawafu 27. 8. 2001. ( Mwezi 7 jumadda thany<br />
1421 H.R.). Akiwa na umri wa miaka 63, vile vile alivyokuwa akiomba<br />
aishi umri ule ule alioshi kipenzi chake Bwana Mtume Muhammad<br />
SAW.<br />
Insha <strong>Al</strong>lah Mnyezi Mungu amjaze kheri na alitie Nuru kaburi lake<br />
(Amin).<br />
Majaalis El Ulaa El Qadiriyya,<br />
Sinza Dar es Salam.