17.02.2015 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

YALIYOMO<br />

No.<br />

Ukurasa.<br />

1. Yaliyomo-------------------------------------------------- i.<br />

2. Utangulizi------------------------------------------------- ii.<br />

3. Dibaji------------------------------------------------------- iv.<br />

4. Siri ya balaa------------------------------------------------ 1.<br />

5. Nini siri ya hizi balaa?------------------------------------ 4.<br />

6. Nini cha kufanya?------------------------------------------ 9.<br />

7. Sehemu ya pili “Wakati”----------------------------------- 15.<br />

8. Tukio la kiyama---------------------------------------------- 19<br />

9. Nyakati za Mnyezi Mungu---------------------------------- 24.<br />

i.


بسم<br />

هللا الر حمن الر حيم<br />

UTANGULIZI<br />

<strong>Al</strong>-hamdullilahi wal khayru wash-sharru bima<br />

shiyati Llah. <strong>Al</strong>lahu mma swalli a`laa habibika Seyyidna<br />

Muhammad wa alih waswahbihi ajmaina wat tabi ina lahum<br />

biihsa nin ilaa yawmid dina. Waba`ad:<br />

Inaonyesha kuwa watu wengi wanaishi bila kujua vipi kuishi.<br />

AJABU. Kufa kila mtu anajua, hata mtoto mdogo haitaji<br />

maelezo yoyote kwa suala hilo la kufa. Kutokana na illa hiyo,<br />

tumeonelea iko haja ya kuandika kijitabu kama hiki ambapo<br />

mtu anaweza kustafidi mengi katika suala la kuishi na<br />

kupambana na mitihani ambayo ndiyo hasa lengo lake. Baada<br />

ya kusoma kitabu hiki utashangaa kuona kuwa umefunukiwa<br />

na akili kiupana ambao labda ingekuchukua siku nyingi<br />

kuelewa hakika yake. Balaa, mitihani, fitna na majaribu ni<br />

neno moja ambalo katika kiswahili hatuna sawa yake. Na hata<br />

tukisema misukosuko haitoshelezi kuwa ndiyo balaa, kwa<br />

sababu misukosuko ni neno jingine kabisa. Mnyezi Mungu<br />

ametaja vifwatavyo kama fitna kubwa kwa mtu ; pesa, mke,<br />

watoto, mali, njaa, mauti, upungufu wa mali na kadhalika.<br />

Lakini wengi watashangazwa na listi hiyo pamoja na kuwa<br />

navyo vitu hivyo siku nyingi sana zilizokwisha kupitia<br />

maishani mwetu. Kila kitu kinategemea ilmu na hakuna lolote<br />

ambalo tunalifanza halina ilmu ndani yake.<br />

Qur an Suratul Twaha 20:50.<br />

"(Musa) akasema: “Mola wetu ni yule liyekipa<br />

kila kitu umbo lake kisha akakiongoza (kufuata kinachowafiki<br />

umbo lake hilo).”<br />

Bila ilmu hatuwezi kuongoza njia - Ndo maana Bwana Mtume<br />

SWA. katuambia:<br />

طَلب العلم فريضة على كل مسلم ومسلمة<br />

ii


(Kutafuta ilmu ni lazima kwa kila muislamu<br />

mume na mke).<br />

Na mambo yote yafanywayo bila ilmu ni yenye<br />

kurudishwa hayakubaliwi. Tutapungukiwa na shida nyingi<br />

tukijua jinsi gani Mnyezi Mungu anavyowajaribu waja<br />

wake na kuwa imara zama za mabalaa kwani:<br />

خيزه وشزه من هللا تعالي<br />

(kheri na shari zote zinatoka kwake Mnyezi<br />

Mungu SWT).<br />

(Amin).<br />

<strong>Al</strong>-<strong>Faqeer</strong>,<br />

Ahmad Sheikh,<br />

Majaalis<br />

Sinza,<br />

Shaaban 24 – 1415,<br />

25 – 1 – 1995.<br />

iii


DIBAJI<br />

بسم<br />

هللا الر حمن الر حيم<br />

Tunamshukuru Mwenyeenzi Mungu kwa fadhila zake na neema zake nyingi<br />

sana zisizohesabika. Na Swala na Salaam zimfikie Mtume Muhammad (SAW)<br />

pamoja na ali zake na awaridhiye maswahaba wake wote – Amin.<br />

Amma Baad : Amesema Mola katika Quran takatifu surati <strong>Al</strong> Ankabuut:<br />

Qur an 29 : 1 – 3.<br />

“Watu wanadhani kuwa wataachiwa pindi wakisema kuwa<br />

tumeamini bila ya kupata misukosuko. Hakika tuliwatiya<br />

katika misukosuko wale ambao waliyokuwa kabla yao wao,<br />

kwa yakini mwenyeenzi Mungu atawatambulisha wale walio<br />

wakweli na atawatambulisha wale ambao ni warongo”.<br />

Ni katika moja ya hekima zake Mwenyeenzi Mungu katika kuwapima waumini<br />

kwa viwango vya imani zao kwake yeye kwa kuwaletea aina mbali mbali za<br />

misukosuko na mabalaa. Na ingawa anavijua Kabla ya kuvipima viwango hivyo.<br />

Na Mwenyeenzi Mungu anafanya hivyo kwa kudhihirisha mapenzi yake kwa<br />

anayemleteya misukosuko na mabalaa, kama alivyosema Mtume Muhammad<br />

(SAW):<br />

ان هللا اذااحب عبدا ابتاله فاذاصبر نجاه واذارضا اصطفاه<br />

(Hakika Mwenyenzi Mungu akimpenda mja humpa mabalaa<br />

na kama akisubiri anamuokowa nayo na akiridhika nayo<br />

humchaguwa (kuwa mja wake wa karibu).<br />

Kwa hivyo basi, muumini wa kweli amewajabika kuridhika na hukumu ya<br />

Mwenyenzi Mungu kwake yeye hata ikiwa ina uchungu wa namna gani. Amesema<br />

Mtume Muhammad (SAW) katika <strong>Al</strong>-Hadithi <strong>Al</strong>- kudsiyy;<br />

من لم يزض تقضاى فا لىتجذر تا سوا ى<br />

iv


DIBAJI<br />

“Asiyeridhika na hukumu yangu, basi na<br />

awe na mola asiyekuwa mimi”.<br />

Kupendwa na Mwenyenzi Mungu kwa njia ya kuteremshiwa mabalaa na<br />

misukosuko ni moja wapo ya neema zake ambayo inazalisha ndani yake<br />

neema nyinginezo zilizo nzuri na muhimu kwa maisha ya muumini hapa<br />

duniani, ikiwemo neema na sifa ya subira. Na subira kama alivyosema Mtume<br />

Muhammad (SAW):-<br />

ا لصثز نصف ا ال ى مان<br />

Sote tunaelewa kuwa Mtume Muhammad (SAW) ni kipenzi cha<br />

Mwenyeenzi Mungu kuliko watu wote. Na katika historia ya maisha yake<br />

kama Mtume wa Mwenyeenzi Mungu alifiliwa na mke wake wa kwanza bibi<br />

Khadija RA na kufuatiliya kufa ami yake na mlezi wake Bwana Abiy twaalib<br />

katika mwaka mmoja. Na Bwana Mtume aliusiya kwa kuwita mwaka huo ni<br />

mwaka wa huzuni.<br />

Na alipokwenda mjini Twaaif katika mwaka huo huo kuwahubiriya watu<br />

wake ujumbe wa Mwenyeenzi Mungu wa Dini ya Islam walimpiga mawe na<br />

kuukataa. Na kwa kuwa ni kama alivyoamrishwa na Mwenyeenzi Mungu<br />

katika Qurani Takatifu Surat <strong>Al</strong> Ahkaaf kuwa awe mwenye subira: Qur an<br />

46:35.<br />

“ Subiri (ewe Muhammad) kama walivyosubiri Mitume<br />

Uwlu-<strong>Al</strong>-Azim. Nao ni: Mitume Nuhu, Ibrahim, Mussa<br />

na Isa (AS)”v<br />

Subira aliyokuwa nayo Mtume Muhammad (SAW) ndiyo iliyokuwa<br />

moja wapo ya silaha aliyotumia Mtume Muhammad (SAW) katika<br />

kuufanikisha kwa kuufikisha ujumbe wa Mwenyeenzi Mungu kwa watu wote<br />

kama Nabii wa mwisho na Mtume kwa watu wote.<br />

Mwenyenzi Mungu amkubaliye <strong>Al</strong> Marhuum Sheikh Ahmad Sheikh wa<br />

Majaalis – Sinza athari yake hii aliyetuachia na nyinginezo kwa manufaa ya<br />

ndugu zake Waislam, na alijaaliye Kaburi lake (Kibaha ) bustani miungoni<br />

mwa mabustani ya peponi- Amin.<br />

v<br />

Ahmad Haydar Mwinyimvua,<br />

Dar es salaam Tanzania.<br />

14 Ramadhani 1424,<br />

9 November, 2003.


بسم<br />

هللا الر حمن الر حيم<br />

SIRI YA BALAA:<br />

Bin Adam hana pahala ambapo hupata utakaso wa moyo kama<br />

anapofikwa na balaa. Mfano ambao ameuelezea Mnyezi Mungu<br />

mwenyewe ndani ya Qur an hakuna kama ule anapotokea mtu kuwamo<br />

ndani ya chombo baharini na ghafla ikaanza mchafuko wa hali ya hewa.<br />

Dharuba toka kila upande, mawimbi mazito na makubwa kama mlima<br />

hakuna nchi yeyote karibuni bali ni bahari pana tu, ambayo mwisho wa<br />

mandhari yake mtu kila upande ni ile ya maji kukamatana na mawingu<br />

tu. Mandhari hiyo lau tofauti ni ndogo na ile ya siifu (khasf: yaani:<br />

“ Quick sends” ), ambaye anayetumbukia ndani yake hukiona kifo ni<br />

chenye kumvaa bila ubishi wowote, lakini mtu hujiona kabisa anakufa<br />

na kukata tamaa ya kunusurika kama aliyoipitia Edmond Dause.<br />

<strong>Al</strong>isema:<br />

“The angry waves and the sight of dangerous<br />

rocks told me that death was near. and the<br />

thought of death made me afraid. I used all my<br />

powers as a man and as a sea man to ascape.<br />

But I did so because I was happy, because I<br />

didn`t coated death, and because I didn`t<br />

wish that I, a living thing made by the service<br />

of God, should became food for the birds and<br />

beasts of the sea……..”.<br />

“mawimbi ya ghadhabu na mandhari ya majabali ya<br />

hatari yaliniambia kuwa kifo kilikuwa kimekaribia, na<br />

mawazo ya kifo yalifanza niogope. Nilitumia uwezo<br />

wangu wote kama mwanamme na baharia hasa, ili<br />

kuikwepa ajali hiyo. Lakini nilifanya hivyo kwa sababu<br />

nilikuwa na furaha; kwa sababu sikuwa nimefunikwa na<br />

kifo. Na kwa sababu sikutegemea kuwa mimi kiumbe<br />

chenye uhai uliotengenezwa kwa huduma yake Mnyezi<br />

Mungu, nije kuwa chakula cha ndege na wanyama wa<br />

baharini…“<br />

1


Katika hali kama hiyo mwanaadamu humuomba Mnyezi Mungu kwa<br />

hali ya unyenyekevu na utakaso mkubwa kweli kweli. Qur an Surat<br />

Yunus: 10:22.<br />

“Yeye ndiye anayekuendesheni katika bara na baharini.<br />

Hata mnapokuwa katika majahazi na yanakwenda nao<br />

Kwa upepo mzuri na wakafurahi nao; mara upepo mkali<br />

Unayajia na mawimbi yanawajia kutoka kila upande, na<br />

wanaanza kufikiri ya kwamba wametingwa. ( Hapo ndipo)<br />

wanapomuomba Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia<br />

utii, (wakisema): “Ukituokoa katika haya, bila shaka tutakuwa<br />

miongoni mwa wanaoshukuru.”<br />

Lakini anapookolewa na akawasili katika ardhi salama kabisa hapo<br />

hapo humfanzia mola wake chungu ya washirika kama siye yeye<br />

aliyekiomba kwa hali ya Ikhlaas kubwa moyoni mwake. Quran Surat<br />

Hud 11:9 –10.<br />

2


“Na kama tukimuonjesha mwanaadamu rehema<br />

inayotokana nasi; kisha tukaiondoa kwake, mara<br />

moja anakuwa mwenye kukata tamaa kabisa na<br />

asiyekuwa na shukurani. Na kama tukimuonjesha<br />

neema baada ya dhara iliyompata mara husema:<br />

“Taabu zimekwisha ondoka kwangu”. (Wala<br />

hashughuliki kufanya mema wala kumshukuru<br />

Mnyezi Mungu). Basi huwa (sasa) ni mwenye<br />

kufurahi sana (na) mwenye kujivuna kabisa”.<br />

Pengine mtu hupewa balaa katika neema, naye mtu hufurahia<br />

na kukongoea kule kukirimiwa kwake. Na anapobalaiwa (tiwa balaa)<br />

katika upungufu wa neema, mara hupayuka akadai kuwa Mnyezi<br />

Mungu amemsahau. Qur an Surat Fajr 89:15-16.<br />

“Lakini mwanaadam, mola wake anapomfanyia<br />

mtihani akamtukuza na kumneemesha, basi husema :<br />

“Mola wangu amenitukuza;” (wala hashughuliki<br />

kufanya mema ili kutengeneza akhera yake). Na<br />

Anapomfanyia mtihani Akampunguzia rizki yake,<br />

husema: “Mola wangu amenidhalilisha, (nikifanya<br />

mema au mabaya ni sawa sawa, hatayashughulikia,<br />

basi naendelea kufanya mabaya)”<br />

3


Kwa nini yapatikane yote haya? Bila shaka sababu ya msingi si<br />

nyingine illa ni ile iliyoelezewa mwenye surat Mulk na nyingine kadhaa<br />

mwenye Qur an. Qur an Mulk 67:2.<br />

“Ambaye ameumba mauti na uhai ili kukujaribuni<br />

(kukufanyieni mtihani); ni nani miongoni mwenu<br />

mwenye vitendo vizuri zaidi. Naye ni mwenye nguvu<br />

( na) mwenye msamaha”.<br />

Katika katiba zake Mnyezi Mungu hapa duniani ni kuwajaribu<br />

waja wake. Kwa hali hii neema ni mtihani na nakma ni mtihani pia. Yule<br />

anayeneemeshwa, anatarajiwa kushukuru; na yule alonakamishwa<br />

anatarajiwa kusubiri. Asiyeweza hayo, basi Mnyezi Mungu anasema:<br />

“……….Na atafute Mola asiyekuwa Mnyezi Mungu na pa kuishi<br />

pasokua hapa duniani.” Hadithi hiyo ina mafumbo mazito ndani yake.<br />

NINI SIRI YA HIZI BALAA.<br />

Bwana Mtume S.A.W anatuambia:<br />

4


(Hakika Mnyezi Mungu alotukuka anapompenda<br />

mja wake humpa mabalaa. Basi akisubiri humuepusha<br />

na balaa hilo. Na akiridhia basi humchagua<br />

(kuwa mja wake).<br />

Hadithi hii inatupa maarifa mazuri ndani yake, nayo si<br />

mengine bali ni yale yanayotuwezesha kugundua siri ya kupendwa na<br />

Mnyezi Mungu imo ndani ya kujaribiwa. Tofauti na mapenzi ya<br />

binadamu anayekuletea kisababu, balaa basi huyo hakupendi. Na<br />

anayekukunjulia mkono basi huyo ndiyo anayekupenda na<br />

kukuhurumia<br />

Mnyezi Mungu anafahamisha mwenye Qur an 2: 155-156.<br />

“Na tutakutieni katika msukosuko wa (baadhi<br />

ya mambo haya); hofu na njaa na upungufu wa<br />

mali na watu na wa matunda. Na wapashe habari<br />

njema wanaosubiri. Ambao uwapatapo msiba<br />

husema: “hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na<br />

kwake yeye tutarejea (atatupa jaza yake).”<br />

Hiyo: “…Wape bishara njema wenye kusubiri…<br />

Wapashe habari njema…” Inagusia pale pale katika kutarajiwa<br />

yule alonakamishwa kuwa atasubiri. Kusubiri ndiyo jawabu la<br />

mtihani, au majaribio, au balaa.<br />

Bwana Mtume S.A.W. amesema:<br />

‏"....وماجزاءالصبر االالجنو<br />

5


(Hatukujua jaza (malipo) ya subra kingine<br />

chochote illa ni pepo tu.)<br />

Amesema pia katika hadithi nyingine kuwa:<br />

(Muumini hana, anachokosa akineemeshwa<br />

hushukuru (na si vingine,mwenye kushukuru<br />

huzidishiwa huzidishiwa),na akitahiniwa<br />

husubiri (na malipo ya subra ni pepo).<br />

Kwa hivyo huku anapata na huku anapata. Mnyezi Mungu anaonyesha<br />

ndani ya Qur an kuwa lau angekuwa anawapa kila mtu kwa ayafanyayo,<br />

basi wale wenye kumkufuru na kumshirikisha ndiyo angewapa nyumba<br />

nzuri nzuri za dhahabu na fedha na kadhalika kila wakitakacho. Kinyume<br />

nyume mambo yake Mnyezi Mungu. Sisi huona tukineemeshwa sana<br />

ndiyo eti tunapendwa mno, kumbe huwa ni hatari.<br />

Seyyidna Daud As alikaa mwaka mzima bila ya mtihani wa aina<br />

yeyote, basi alishtuka akamuuliza Mnyezi Mungu VIPI? Au amekuwa<br />

miongoni mwa waliochukiwa mbele yake Sub hana wa Taala?. Na ambao<br />

huwa na mitihani mikubwa kupita watu wote hakuna kama mitume. Basi<br />

na warithi wa mitume nao wasishtuke na kuanza kubabaika yanapowafika<br />

mabalaa. Qur an 2:214.<br />

“Mnadhani kuwa mtaingia peponi na hali<br />

hamjajiwa na mfano wa (yale yalowajia)<br />

wale waliopita kabla yenu? Yaliwapata<br />

6


mashaka na madhara na wakatetemeshwa<br />

sana hata mitume walioamini pamoja nao<br />

wakasema: “Nusura ya Mwenyezi Mungu itafika<br />

lini?”. Jueni kuwa nusura ya Mwenyezi Mungu<br />

iko karibu”.<br />

Zipo balaa za kujitafutia mtu mwenyewe- mathalan mtu<br />

kutumbukiza kidole mwenye sega la nyuki na wenyewe wamo ndani.<br />

Zipo balaa nyingine Mnyezi Mungu anaelezea mwenye Qur an<br />

2:195<br />

“Na toeni katika njia ya Mwenyezi Mungu, wala<br />

msijitie kwa mikono yenu katika maangamizi –<br />

zo. Na fanyeni wema, hakika Mwenyezi Mungu<br />

huwapenda wafanyao wema”.<br />

Na mifano kama hiyo mingi Mnyezi Mungu kwa rehma zake<br />

atukinge nayo. Mnyezi Mungu anafundisha tena jinsi ambavyo<br />

tutaweza kufaulu katika kukabiliana na mitahani yake. Ni kama<br />

anaetoa jawabu zake mbele kabla ya mitihani kuletwa: Qur an<br />

2:153<br />

7


“Enyi mliomini jisaidieni (katika mambo<br />

yenu) kwa subira na sala, bila shaka<br />

Mwenyezi Mungu yu pamoja na wanaosubiri.”<br />

Mnyezi Mungu ndiyo huba kubwa (The greatest love). Na kila<br />

anayependa hua hapendi kuwa (kukaa) mbali na mpenzi wake. Basi ikiwa<br />

amri ya mambo ndiyo iko hivyo, basi ni budi kuzidisha subra zetu kila<br />

siku. Fakhri iliyoje kwa watu kusikia kuwa Rais au Mfalme wa nchi yuko<br />

kwa fulani. Siyo yeye yuko kwa Rais au Mfalme, Aa! Rais au Mfalme ndo<br />

yuko kwake au yuko pamoja naye.<br />

Hakuna njia ambapo anafikilia mja katika bahri ya mapenzi yake<br />

kwa Mnyezi Mungu ila kwa kupitia mabalaa. Lakini kwa sababu nafsi ya<br />

neno lenyewe Balaa siyo kiswahili, uzito wake umekuwa na sura ya<br />

tofauti na vile lilivyo hasa. Katika lugha ya kiswahili Balaa inatupa<br />

tafhuma ya hatari isiyoweza kusubiria ndani yake. Na pia inapotafsiriwa<br />

kuwa ni Fitna ndiyo kabisa na inapotafsiriwa kuwa ni mitihani hapa<br />

kidogo ule mmeremeto wa ubaya unapungua kasi. Kadhalika Majaribio<br />

yote ikiwa ni neno lile lile lakini uzito unazidi kupungua, pamoja na kuwa<br />

kwake maneno yote hayo –Balaa, Fitna, Mitihani na Majaribio hakuna<br />

hata moja la kiswahili. Sasa ikiwa hatujapata neno la kiswahili kwa –<br />

“Balaa”- vipi tunaelewa tutakavyo tu. Mnyezi Mungu anatwambia: Qur<br />

an 47:31.<br />

“Na tutakufanyieni mitihani mpaka<br />

tuwadhihirishe (wajulikane ) wale<br />

wanaopigania dini miongoni mwenu na<br />

wanaosubiri, nasi tutadhihirisha habari<br />

zenu.”<br />

8


Mnyezi Mungu hataacha kuwajaribu waja ili kuona ni nani wa<br />

kweli mpaka dunia imalizike. Sasa wapi tutakwenda ambako hakuna<br />

Mitihani Fitna na Balaa?<br />

NINI CHA KUFANYA:<br />

Baada ya kwisha kupatapata siri ya Mabalaa sasa na<br />

tujiulize nini la kufanya ndani ya ule muda wa kusubiri?. Lazima<br />

turudi kwenye ile Aya ya 153 ya sura <strong>Al</strong> Baqrah ambapo<br />

tunashauriwa tujisaidie katika mambo yetu kwa Kusubiri na Kusali.<br />

La muhimu ni huko kusali. Kusali kuna maana si moja tu, ya<br />

kusimama, kurukuu na kusujudu. Lakini swala ina sehemu kubwa ya<br />

Dua, nayo ni maombi kwa Mnyezi Mungu. Swala ni Bridge (daraja)<br />

yenye kumuunganisha Mtu na Mola wake, na Ibada maalumu. Sala<br />

ni rehma, na ndiyo maana katika kumswalia Bwana Mtume SAW<br />

hakuna kusimama, kurukuu wala kusujudu, pia katika sala ya maiti.<br />

Kujisaidia mambo yetu kwa sala, tunapata kauli ya Bwana Mtume<br />

SAW kuwa:<br />

(Mnyezi Mungu amejaalia kila kitu silaha,<br />

na silaha ya muumini ni Dua).<br />

Mnyezi Mungu anafundisha vipi tutamuomba; amma kwa jina lake<br />

<strong>Al</strong>lahu au kwa jina lake Rahman Kwingine anatutaka tumuombe<br />

kwa unyenyekevu na kwa khofu, pengine kwa khofu na kwa kutumai<br />

(confidence) na kwa siri au kwa fakhri au kwa sauti ya juu wala si<br />

kwa sauti ya chini lakini baina yake. Qur an 17:57.<br />

“Hao wanaowaomba (wenyewe) wanatafuta<br />

ukaribiano na mola wao; (hata) walio karibu<br />

miungoni mwao (na Mungu, kama malaika wao<br />

wanafanya yaya haya) wanatumai rehma Zake<br />

na wanaogopa adhabu yake. Hakika adhabu ya<br />

Mola wako ni ya kuogopwa.”<br />

9


Wengine hufanza Tawasssul nyingi nyingi tu, kwa sababu<br />

Mnyezi Mungu ni mwenye kupenda kuombwa na huchukia asipoombwa.<br />

Kinyume na sisi. Tusipoombwa hufurahi, na tunachukia - illa wachache tu<br />

labda, tunapoombwa. Mnyezi Mungu anawataja waja wake wema kwa<br />

kutuambia: Qur an 51:19<br />

“Na katika mali zao ilikuwako haki ya kupewa<br />

maskini aombaye na ajizuiaye kuomba.”<br />

Pia katika Suratul Ma’arij 70:24-25.<br />

“Na ambao katika mali zao iko sehemu maalumu.<br />

Kwa ajili ya aombaye na anayejizuilia kuomba<br />

(japo muhitaji)”.<br />

Sisi tunajitoa katika sifa tukufu kama hizo kwa kuchukia kuombwa.<br />

Kwa hiyo kumuomba Mnyezi Mungu ndiyo jawabu tunapokuwa mwenye<br />

mabalaa. Siku nyingi zilizopita waliteseka baadhi ya watu kwa sababu ya<br />

kumuomba Mnyezi Mungu mpaka ikafikia kuambiwa: Qur an 22:40<br />

10


“Ambao wametolewa majumbani, (mjini) Mwao<br />

pasipo haki ila kwa sababu wanasema: “Mola<br />

wetu ni Mwenyezi Mungu.” Na kama Mwenyezi<br />

Mungu asingaliwakinga watu, baadhi yao kwa<br />

wengine, bila shaka yangalivujwa mahekalu na<br />

makanisa na nyumba nyingine za ibada na<br />

misikiti ambamo Jina la Mwenyezi Mungu<br />

hutajwa kwa wingi. Na bila shaka Mwenyezi<br />

Mungu humsaidia yule anayesaidia Dini Yake.<br />

Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na<br />

Mwenye kushinda.”<br />

Subra ikienda na dua na matendo mema, ndipo Mnyezi<br />

Mungu huepushia watu mabalaa yao. Na miongoni mwa jawabu<br />

hakuna kama ISTIKTHAAR (kufanza wingi ) mambo ya swadaka na<br />

ISTIGHFAAR (kutaka msamaha) kwake yeye Mnyezi Mungu.<br />

Mambo mawili hayo yanapata ( Support ) kutiwa nguvu na aya : Qur<br />

an 71:10-12<br />

"Nikawaambia: Ombeni msamaha kwa<br />

Mola wenu. Hakika yeye ni mwingi wa<br />

Msamaha. Atakuleteeni mawingu yanyeshayo<br />

mvua nyingi. Na atakupeni mali na watoto,<br />

na atakupeni mabustani, na atakufanyieni mito.”<br />

Vile vile Mnyezi Mungu amesema: Qur an Suratul Anfal 8:33<br />

11


“Lakini Mnyezi Mungu hakuwa wa kuadhibu<br />

maadamu wewe ( Nabii MUHAMMAD )<br />

umo pamoja nao ( Hapa Makka ), Wala Mnyezi<br />

Mungu hakuwa wa kuadhibu pia hali ya kuwa<br />

(Baadhi yao wamesilimu ) wanomba msamaha.”<br />

Mtu angetaka aambiwe na nani zaidi ya Mnyezi Mungu hakaik<br />

za namna hiyo ili asikie na kutekeleza. Tazama fadhila za ISTIGHFAAR<br />

zilivo pewa ubora na faida. Mnyezi Mungu anaacha kuwaadhibu<br />

washupavu watenda dhambi katika mji wanapopatikana wenye kuleta<br />

ISTIGHFAAR. Kutokana na wao Mnyezi Mungu anastahi kuwaadhibu –<br />

Ni madogo Hayo ? – Lakini ndiyo kwa vile watu hawataki kutambuwa<br />

wala kuwathamini.<br />

Jambo la pili ni swadaka ambapo Mnyezi Mungu<br />

katika hadithi aliyofahamisha Bwana Mtume SAW kuwa:<br />

الصدقة تدفع غضة الزب<br />

(Swadaka hukinga ghadhabu ya Mnyezi Mungu).<br />

Jee hatuoni fawaida zake ndani ya uhai na maisha<br />

yetu ya kila siku? Inataka mtu achunguze na kufanza<br />

majaribio, hiyo ni ibada tosha na ya uhakika (Creative<br />

worshiping).<br />

Jinsi gani Mnyezi Mungu anavyojaalia mitihani kwa<br />

waja wake. Mwenye mali mitihani yake mingi ni kwenye<br />

mali yake na dhidi ya hali yake, ndiyo kusema masikini.<br />

Wengi wenye mali walizipoteza kwa sababu ya<br />

kuwanyanyasa masikini. A`lim mtihani wake katika ilmu na<br />

dhidi yake kwa wajinga. Bwana Mtume SAW alisema kuwa:<br />

(Ilmu hupata maafa wakifundishwa wasiokuwa watu<br />

wake).<br />

12


Halkadhalika masikini na mahakimu nao wana mitihani yao.<br />

Watu wanne hao tumewaonyesha kwa kuwa wao ndio nguzo<br />

zilokamatia ulimwengu jinsi vile alivyosema Bwana Mtume SAW.<br />

Kwa ujumla Mnyezi Mungu hukinga balaa zetu na<br />

hupunguza ghadhabu zake kwetu kwa ajili ya swadaka. Basi jambo<br />

hilo lingefaa lidumishwe kwa sababu faida zake ni za kuonekanwa<br />

kwa macho hasa, na mambo yetu yamghadhibishayo Mnyezi Mungu<br />

ni mengi. Mambo haya wapo wengi ambao hawana habari nayo<br />

pengine hizo swadaka huchukulia kuwa ndiyo ZAKA.<br />

Lakini tofauti ni kule kuwa swadaka ni ya hiyari, na zaka ni<br />

ya lazima. Swadaka unaweza kumpa mtu yeyote, lakini zaka ni<br />

lazima muislamu anaestahiki kule kupata zaka. Amma sivyo<br />

itakuwa haijaswihi na utakuwa hutahisabiwa kuwa umelipa, na<br />

itabidi kuirudishia tena.<br />

Insha <strong>Al</strong>lah Mnyezi Mungu atuwafikishe katika<br />

kheri tuongokewe kwa yetu, sisi na waislamu wenzetu.<br />

Na tuweke matumaini ya dhati kuwa tutajibiwa kwa<br />

lolote tunaloliomba. Na ndio maana Mnyezi Mungu<br />

akatuambia kuwa: Hadithil Quds:<br />

“Lau wangekusanyika pahala pamoja watu<br />

wote wa mwanzo na wa mwisho, binaadam<br />

na majinni kila mmoja akaomba alitakalo<br />

kwa Mnyezi Mungu katika shida zake, basi<br />

Mnyezi Mungu angempa kila mmoja na<br />

isingekuwa imepungua chochote katika<br />

hazina yake”.<br />

Labda kiasi kile kile cha uzi uliotumbukizwa baharini,<br />

ukanyonya maji na kushirabu barabara.<br />

Huyo ndiye Mnyezi Mungu aliye mkarimu mno na mwenye huruma<br />

isiyomithilika kwa viumbe, Mkwasi mwenye kuneemesha waja wake<br />

atakavyo, wengine anawakunjulia wengine anawakadiria.<br />

Mambo yote tuloyataja na kufahamisha ndani humu ni yake<br />

na kule kuyatekeleza na kuyafuata ndiyo maana ya uislamu.<br />

Qur an 3 : 83<br />

13


“Je! Wanataka dini isiyokuwa ya<br />

Mnyezi Mungu, na hali kila kilichomo<br />

mbinguni na ardhini kinamtii yeye,<br />

kikipenda kisipende? Na kwake<br />

watarejeshwa wote”.<br />

14


Sehemu<br />

ya<br />

Pili<br />

15


WAKATI<br />

Na tarehe yetu yote ni daraja sekunde dakika na saa – SAA!<br />

Wakati umegawika katika mafungu matatu, manne :<br />

i. Uliopita ( Past )<br />

ii. Uliopo ( present )<br />

iii. Ujao ( future )<br />

iv. Milele ( Eternal or Eternity ).<br />

Waliopita huenda waliyajua ya kwetu kama: yajayo; na<br />

wajao hawajui ya kwetu wala waliopita na yajayo. Kwa hivyo<br />

sisi tumekuwa bora kuliko waliopita. Mnyezi Mungu anasema<br />

(ili kuthibitisha ubora wetu kwa kawli fupi kama hii): Qur an<br />

3:110.<br />

“Nyinyi (ndio mmekua ) umma bora (miongoni mwa<br />

nyumma) zilizoletwa kwa watu------“.<br />

Hadithi:<br />

Imetokana na Seyyidna Omar (R.A) alisema:<br />

“Siku moja tulikuwa tumekaa na Bwana Mtume<br />

SAW. Hapo alitokea mtu ambaye nguo zake<br />

zilikuwa nyeupe Pepe na nywele zake zilikuwa<br />

nyeusi sana; hakuwa na alama ya machofu<br />

ya safari na wala hapakuwa na hata mmoja<br />

katika sisi aliyemtambua. <strong>Al</strong>ienda akakaa karibu<br />

na Bwana Mtume SAW. Akiweka magoti yake<br />

karibu na magoti ya Bwana Mtume SAW aliweka<br />

viganja vyake juu ya mapaja yake, akasema<br />

“Ewe Muhammad nambie kuhusu Uislamu.”<br />

Mtume wa ALLAH SWT alisema: “Uislamu ni<br />

Kukiri kuwa hakuna Mungu isipokuwa ALLAH<br />

16


Na Muhammad ni Mjumbe wake, kusali, kutoa<br />

zaka, kufunga Ramadhani, na kwenda Ma<br />

kka ukiweza”. “Umesema kweli”, alisadikisha<br />

yule mgeni. Tulipigwa na mshangao kwa kumuuliza<br />

na kisha yeye muulizaji kusadikisha.<br />

Akauliza tena “Nambie kuhusu Imaan”. Akamjibu<br />

Ni kumwamini Mnyezi Mungu, Malaika<br />

Wake, vitabu Vyake, Mitume wake, Siku ya<br />

kiyama na kuamini kuwa kheri na shari zote<br />

Zinatoka kwake.” “Umesema kweli” akasadi-<br />

Kisha yule mgeni. Akauliza tena: “Hebu<br />

Nieleze juu ya Ihsan”. <strong>Al</strong>isema SAW: Ni kumuabudu<br />

Mnyezi Mungu kama vile unamuona japokuwa<br />

humuoni yeye anakuona.” Akauliza<br />

tena. “Niambie juu ya kiyama”. Bwana Mtume<br />

SAW alisema: “Anaeulizwa hajui zaidi<br />

Kuliko aneuliza”. Yule mgeni akasema: “Nambie<br />

alama zake”. <strong>Al</strong>isema SAW “Kijakazi atamz<br />

aa bwana wake na utaona wachunga wenda<br />

miguu chini, wenda uchi, mafukara (wasiokuwa<br />

na hata makazi) wakishindana kujenga majumba<br />

ya fakhri. Muda mfupi baada ya yule mgeni<br />

kuondoka, Bwana mtume SAW akauliza:<br />

“Ewe Omar jee unamjua ni nani yule aliekuwa<br />

akiuliza? “ Nilisema “Mnyezi Mungu na Mjumbe<br />

wake wanajua zaidi.” <strong>Al</strong>isema ni Jibril<br />

alikuja kuwafundisha Dini yenu (Kwa njia ya<br />

maswali)”.<br />

Imepokewa na Muslim.<br />

17


Wakati seyyidna Jibril AS (The holy ghost ) alipomshukia Bwana<br />

Mtume SAW ( katika karne ya saba) ili amfundishe DINI (ISLAM) kwa<br />

njia ya kumuuliza maswali, akawa anasadikisha kila alipojibiwa, swala<br />

lilikuwa moja zito sana. Lakini aliomba afahamishwe dalili zake tu baada<br />

ya kujibiwa kua “Hakuwa mwenye kuulizwa kwacho ( hicho kiyama)<br />

mwenye kujua kuliko muulizaji”. Bwana Mtume SAW alielezea dalili<br />

zake tu, nazo zilikuwa kama hivi:<br />

i. Mjakazi ( Amati – pia ni jam-u ya umma) yaani: mama.<br />

ii. Utaona wenda miguu chini na uchi, wachunga<br />

mbuzi (cowboys) wakipitana kwa majumba marefu marefu<br />

(Zama ambapo sky scrappers za USA hazikuwepo).<br />

iii. Wanawake wanapokosa haya na kuota mikia.<br />

iv. Qur an itapodharauliwa na kudhalilika.<br />

Bwana Mtume SAW aliendelea mno kuelezea watu juu ya dalili za kiyama baadae<br />

kiasi cha kujenga picha kama hii:<br />

v. Mbali itapokuwa karibu. - ( Ibara hii inadhihirisha umuhimu<br />

wa usafiri kwa vyombo viendavyo mbio kuliko ngamia na<br />

farasi - Kwani wakati farasi anakimbia mfano wa masafa ya<br />

maili sitini kwa saa, roketi itafunika masafa yenye maili<br />

ishirini na tano elfu kwa muda huo huo), na mara mbili ya<br />

roketi, challenger inakwenda maili hamsini elfu katika saa<br />

moja.<br />

vi. Chuma kitapotamka.- ( Mfano wa redio, simu na Telex ambazo<br />

hazikuwepo katika zama zile ).<br />

vii. Mtu mweusi kutawala – ( labda katika zama zile mtawala<br />

mweusi alikuwa ni Mfalme Nagash wa Ethiopia, na katika karne<br />

ya kumi na tisa dunia imejaa watawala weusi, aliyajuaje Bwana<br />

Mtume Muhammad SAW haya?).<br />

18


TUKIO LA KIYAMA:<br />

Tofauti kati ya mwislamu na kafiri ni kuamini mambo ya ghayb ( fact<br />

in exisence) mwislamu ni lazima aamini kiyama kuwa kitakuja bila<br />

shaka yeyote (without any doubt) lau sio lazima kujua kuja kwake.<br />

Qur an Naziat 79:42-44<br />

“Wanakuuliza kiyama kutokea kwake<br />

kutakua lini?. Uko wapi na kuweza<br />

kutaja (wakati wa kuja kiyama ). Mwisho<br />

(wa ujuzi ) wake uko kwa Mola wako.”<br />

Mnyezi Mungu anamweleza Mtume wake Nabii Muhammad<br />

SAW kwa kawli ya wazi wazi kua kipo, hicho kiyama, lakini wale tu<br />

wanaokiogopa ambao watakumbushika, wengine laa !. Na katika dalili<br />

za wazi wazi ambazo ni muhimu kuzijua kwa jicho la mazingatio ya<br />

hali ya juu kabisa ni hizi:<br />

1. Kudhihiri Mahdi<br />

2. Kutokea kwa Dajjaal (Atazaliwa akiwa na jicho moja<br />

kama walivyokuwa kawmu NISA. (Amerika katika noti<br />

yao ya dola 100 ambapo inaonyesha picha ya jicho moja,<br />

utadhani walipata habari zake).<br />

Huyo mlaghai mkubwa jitu moja lenye fitna kubwa kabisa,<br />

ambaye atadai uungu kama alivyodai Firauni wa zama za Nabii Mussa<br />

AS, na tofauti ya muda wa Firauni miaka mia nne, Dajjaal atadumu<br />

duniani kwa muda wa siku arubaini ambazo ni tofauti na siku ya<br />

kawaida. Siku kumi za mwanzo kila siku moja itakuwa kama mwaka<br />

(kwa hiyo ni miaka kumi) siku kumi za pili kila siku moja kama mwezi.<br />

Siku kumi za tatu kila siku yake ni kama wiki moja Na siku kumi za<br />

mwisho kila siku ni kama siku ya kawaida.<br />

Kwa hiyo, siku kumi za mwanzo ni kama miaka kumi. Kumi la pili ni kama<br />

miezi kumi. Kumi la tatu ni siku sabini, ( yaani miezi miwili na siku kumi). Na kumi la<br />

nne ni siku kumi. Jumla ni miaka kumi na mbili na siku ishirini.<br />

19


Dajjaal ataingia kila nchi duniani kudanganya na kufitinisha watu.<br />

Ulaghai atoutumia kama vile kumfufua aliekufa siku nyingi na kuleta<br />

mvua na kuotesha mazao mashambani utavutia watu mno kiasi cha<br />

kumwamini kuwa mungu. Yeye atakuwa na pepo na moto. Wataomkubali<br />

atawatia ndani ya pepo yake, wataomkataa atawatia motoni. Lakini ukweli<br />

wa mambo ni kinyume nyume. Watoingizwa peponi ndiyo watoingia<br />

motoni, na wale watoingia motoni ndiyo watoingia pepo ya Mnyezi<br />

Mungu wa kweli. Nchi pekee ambazo hataingia Dajjaal ni Makka na<br />

Madina.<br />

3. Kuteremka seyyidna Isa AS. (Ambaye<br />

atakuja kumpiga vita na kumuondoa (huyo<br />

Dajjaal). Baadaye ataishi siyo kama Mtume, bali<br />

kama mja mwema aliye mchaji ). – Ataoa ataishi<br />

miaka arubaini atakufa, na Madina katika Rawdha<br />

karibu ya Bwana Mtume SAW ndipo atazikwa.<br />

4. Kutokea Juju wa Majuju. (Ambao Dhyl Qarneyn)<br />

aliyewafungia ndani ya ukuta fulani tangu siku hizo hadi leo<br />

hii bila shaka.<br />

5. Kutokea kwa Dabba. (Mnyama wa ajabu ). Mnyama huyu<br />

atawasemeza watu yale ambayo wanakataa kuyakinisha.<br />

Hakika hii .inafahamishwa kwetu na Qur an ya Mnyezi<br />

Mungu; kwa kila mtu kujipatia mwangaza wa mbele kabla<br />

kuwadia wakati wake ambao kutokea karne hii ya ishirini na<br />

moja sio mbali tena.<br />

Tunaanza kuzoeshwa kumzowea mnyama huyo kabla ya kufika<br />

kwake ili tu, tusifikie mshtuko ambao unaweza kuitoa roho ya mtu mbichi<br />

mbichi. Mfano wa “Mapi show” Unajihusisha vizuri sana.<br />

Mnyama huyo atakuwa na mwendo mkali mno, hatakikosa<br />

atakachokifukuza wala hakitampata kitachomfukuza. Ataandika usoni<br />

mwa muumini: “huyu ni mtu wa peponi”. Na uso wa mtu huyo utang`aa<br />

sana. Na katika uso wa mtu wa motoni ataandika: “huyu ni ka fir” na uso<br />

wake utapiga weusi. Na leo praktizi za kujitia weusi zimeanza hali ya<br />

kuwa huyo Dabba wenyewe hajaja. Dabba atakuwa miungoni mwa dalili<br />

za mwisho tena.<br />

6. Kuchomoza jua magharibi ya ardhi:<br />

Hii ni ishara ya wazi wazi yenye kuogofya ( kuogopesha)<br />

mno – <strong>Al</strong>lahu Akbar. Bila ya shaka ionekanapo hitilafu<br />

katika maumbile bin adam hushangaa,<br />

20


hushtuka na pengine humiliki hali fulani akataka afanze<br />

ambalo uwezo wake ungeruhusu.<br />

Viumbe vyote vimezoea kuona jua likichomoza toka mashariki ya<br />

dunia kwenda magharibi. Lakini siku hiyo litachomoza toka magharibi<br />

na kuja zake hadi katikati ( kama inavyokuwa saa sita, saa za kulingana<br />

kinvuli ), na litarudi huko huko maghribi.<br />

7. Utapodhihiri moshi: Moshi uliokusudiwa hapa ni ambao<br />

utaenea dunia nzima. Moshi huu utakuwepo duniani muda wa<br />

siku arubaini. Moshi utakuwa ukitoka puani, machoni na<br />

kwenye duburi ( tupu ya nyuma ) ya kila kafir mpaka<br />

ataonekana kama mlevi.<br />

Hali hii ya kuonekana watu walevi na hali hawakunywa pombe,<br />

bali ni adhabu ya Mnyezi Mungu ni kali. Imetajwa ndani ya Qur an<br />

ikiashiria juu ya dalili za kiama vile zitavyojionyesha. Taathira ya<br />

moshi kwa muumini itakuwa kama mafua mafua tu hivi. –<br />

Hizi ni miungoni mwa taabira ( prophecies ) alizozielezea Bwana<br />

Mtume SAW. Na kila mtu ni muhimu azijue mapema na kuwafundisha<br />

watoto wake.<br />

8. Kuharibika <strong>Al</strong> Kaaba: Baada ya kufa nabii Isa AS. Na<br />

kuzikwa Madina, <strong>Al</strong> kaaba itaharibika juu ya mikono ya<br />

Habash.<br />

Katika karne ya saba wakati wa uzawa wa Bwana Mtume SAW<br />

<strong>Al</strong> kaaba ilitaka kuharibiwa na Abraha – Ambaye alikuwa mfalme<br />

muhabesh aliyeweka jeshi lake Yemen. Mnyezi Mungu alituma jeshi la<br />

ndege -Ababiil - wakiwa na vijiwe midomoni idadi ya jeshi zima la<br />

Abraha, wakawa kama majani yaliyotafunwa na kisha yakatemwa.<br />

Baada ya tukio hilo hakuna nchi yeyote duniani iliyojasiri kutaka<br />

kuihujumu nyumba ya Mnyezi Mungu mpaka hii leo. Lakini<br />

ipo kawli toka kwa Bwana Mtume SAW kuwa katika akheriz zaman<br />

madola makubwa ya dunia yatapata kishawishi kutaka kuihujumu<br />

lakini Mnyezi Mungu atawateremshia mabalaa mjini mwao washindwe<br />

kujitambua nafsi zao. Hakika ya <strong>Al</strong> kaaba inabaki kuwa ni nyumba ya<br />

Mnyezi Mungu ambayo iliyojengwa na Seyyidna Ibrahim ASW.<br />

akisaidiana na mwanawe Seyyidna Ismail AS. Na ni pahala pa amani<br />

siku zote, na hilo limetimia tangu wakati wa seyyidna Ibrahim ASW<br />

mpaka leo, si chini ya miaka elfu sita iliyokwishapita.<br />

21


9. Kunyanyuliwa Qur an: Qur an ndiyo kitabu cha mwisho<br />

kwa wanaadam duniani, na kiliteremshwa kwa Bwana<br />

Mtume Muhammad SAW katika karne ya saba, wakati<br />

dunia ilikuwa imezama katika ujaahili. Ikiitwa “Dark age”.<br />

Bwana Mtume ndiyo Mtume wa mwisho aliyeteremkiwa na roho<br />

mtakatifu (The holy ghost ) naye hakuwa msomi wala kuandika hakuwa<br />

anajua. Hakika hiyo ilikuwa hoja kubwa na yenye nguvu kweli. Lakini<br />

haikusaidia kuwafanya wapinzani wa uislamu wajizuie kumtuhumu kuwa<br />

ameiandika yeye. Ajabu ni kwamba wenye ilmu hata wakikusanyika<br />

pamoja kuandika mfano wake wasingeweza na wala hawataweza<br />

Pambano liko wazi kama watapatikana wa kuandika wajitokeze.<br />

Wengine wamemsingizia kuwa Bwana Mtume SAW alijitangazia<br />

utume yeye mwenyewe. Kwa wenye kujua vipi mitume<br />

inavyotayarishwa, madai kama haya hayawapi taabu kwa vile<br />

yaliyodaiwa na majaahili waliorubuniwa na mabwana zao watafanya<br />

nini?. Miungoni mwa kawli zake Bwana Mtume SAW kuhusu mfano<br />

kama huo uliobeba kichwa cha maneno, ni ule wenye kuelezea kuwa:<br />

“Zitakuja zama hautabaki uislamu illa jina<br />

lake tu, na haitabaki Qur an illa maandishi<br />

yake tu ( Rasmuhu )”.<br />

Usemi huo unaonyesha kuwa zama hizo ( na huenda zimeshafika )<br />

watu hawatajishughulisha na kusoma Qur an, kwa hiyo Qur an itafanana<br />

na nyumba iliyohamwa - lakini kunyanyuliwa Qur an ni yenye uzito<br />

tofauti kabisa, kwani hata vifuani haitakuwepo na katika kurudi watu wa<br />

ardhini kuwa makafiri hiyo ndiyo hatari zaidi. Mfano wa kuidharau Qur<br />

an mpaka kufikia wazee kuwashughulikia mno watoto wao kwa masomo<br />

ya kizungu kuliko Qur an ambayo ni rahisi mno, ni moja miungoni mwa<br />

dalili za wazi ambazo zinatuonyesha wapi tunakwenda!.<br />

Pia kupuuza sala kwa nyudhuru za nguo chafu na kila siku<br />

tunazifua kwa masabuni chungu mbovu. Vipi Bwana Mtume SAW<br />

asemee juu ya sala kuwa ndiyo nguzo kuu ya uislamu, kwa hivyo<br />

mwenye kuisimamisha (Iqamu swalat ), basi amesimamisha dini<br />

(Uislamu ), na mwenye kuitupa akaipuuza, basi ameivunja dini. - Halafu<br />

mtu ajifanze hamnazo na kwa makusudi aiche hiyo sala?. Basi kama<br />

imedaiwa kuwa watu wa ardhini watarudi kuwa makafiri, basi, ni wazi<br />

kuwa zoezi lake limeshatwaa nafasi.<br />

22


Amma kwa dalili za kiyama, kila muislamu anajua kwa hiyo siyo<br />

rahisi kuvutiwa na hadithi za dhana dhana na kudanganya watu. Mfano<br />

wa utabiri wa Pop wa 1959 kuwa mwaka 1960 ingekuwa mwisho wa<br />

dunia. Miaka arubaini baadaye utabiri wa Nishel Nostrodamus kwa july<br />

4 na kama hizo. Kiama hakitatokea ila chini ya bendera ya uislam.<br />

Kiama hakitatokea mpaka akosekane katika uso wa ardhi ambaye<br />

anasema: “<strong>Al</strong>lah, <strong>Al</strong>lah"; Lau baadhi ya dalili zimeisha jitokeza,<br />

mfano wa kwenda uchi, wanawake kukosa haya, wanawake kuwa na<br />

mikia, na nundu kama ya ngamia kichwani, mbali kuwa karibu, vyuma<br />

kuzungumza na mtu mweusi kutawala. Lakini hizo tisa bado kuanza<br />

hata moja. Mambo yatakapokuwa tayari, bila shaka yeyote tutaanza<br />

kuzishuhudia moja baada ya moja kama tutakuwepo.<br />

23


NYAKATI ZA MNYEZI MUNGU:<br />

Mnyezi Mungu ndiye aliyeutoa wakati ambao yeye haumuhusu<br />

kitu chochote. Wakati wanasayansi wanaitakidi kuwa ili ufanzike wakati<br />

ni budi kuweko ( vitu vitatu ) Nafasi yaani Volume. Mnyezi mungu<br />

kaenea kila pahala, kwa nafasi haimhusu chochote. Masafa yaani<br />

Distance ( hapa na kule ), Mnyezi Mungu haitaji masafa. Na ili upatikane<br />

wakati vile vile ni lazima kuwepo Kasi yaani Speed, au mwendo, ( bila<br />

ya shaka ni wa kuzunguka). Kwa hoja hii wamehusisha maumbo yaliyoko<br />

mbinguni ambayo yote ni yenye kuzunguka. Mnyezi Mungu haimpasii<br />

jambo hilo hata siku moja. Mnyezi Mungu ameelezea juu ya wakati katika<br />

Qur an: Suratus sajadah 32:5<br />

“Anapitisha mambo yote yaliyo baina ya<br />

mbingu na ardhi, kisha yanapanda kwake<br />

kwa siku moja tu ambayo kipimo chake ni<br />

miaka elfu mnayotumia nyinyi katika<br />

kuhisabu kwenu”.<br />

Katika mfumo huo mwenye akili timamu hatakosa kuona hizi saa<br />

24 zetu ni fupi mno kiasi cha kumaanisha kuwa saa 1 yake ni miaka 41. 16<br />

au miaka 42.4. Tukitizama katika sura ya pili inayoelezea wakati. Tutaona<br />

ndani ya: Quran suratul ma`arij 70:4<br />

“Malaika na roho hupanda kwake katika<br />

siku ambayo muda wake ni miaka elfu<br />

hamsini”.<br />

24


Katika sura hii tunaona kuwa saa moja yake ni sawa na miaka<br />

2083-2088. Mtu mwenye akili timamu hakosi kuona kuwa katika saa<br />

yake hiyo ni kiasi ambacho kinamfikia Nabii Zakari AS, Yunus AS, nk.<br />

Mtu akitafakuri juu ya mtoto wa digi digi aliozaliwa na baada ya saa<br />

moja tu anaenda mbio na mama yake, wakati binadamu labda miaka<br />

miwili na zaidi ndio aje kumudu zoezi hilo, basi ni sawa na kusema:<br />

“Saa moja ya digi digi ni sawa na miaka<br />

miwili ya mwanaadam”.<br />

Ndani ya nyakati mbili hizi mtu yoyote mwenye akili<br />

hatokosa kuona kuwa suala la: “kupitwa na wakati”, kama<br />

ilivyozoeleka mno kwa vijana wa leo, ni kama upumbavu<br />

mtupu. Msemo huu unawaandama masikini wa kutafakari<br />

katika jamii.<br />

Katika wakati wa kwanza na wa pili walioudiriki ni Seyyidna<br />

Adam ASW na Mama Hawwa AS. Katika wanaadamu. Na pia<br />

wamediriki huu wakati wetu wa masaa 24. Wakaishi hadi miaka 1001<br />

(elfu moja na moja ) hapa duniani.<br />

Wanasayansi waliochunguza na wakakubaliana kuwa ndiyo<br />

hakika kwamba mwanga wa jua unatembea miaka 186 elfu kwa sekunde<br />

moja, nyota aina ya GALAXY katika muda huo huo inakwenda kiasi<br />

cha maili 105 ya mwanga, ambapo kila mwaka wake mmoja ni sawa na<br />

miaka Trillion sita (6, 000,000,000,000,000,000 ). Suala la kupitwa na<br />

wakati hapa ni la kipumbavu kabisa.<br />

Mfano wa Betilquise ( Beyt jawzaa ), nyota moja<br />

kubwa mno, imethibitishwa kielimu ( Science ). Mwanga<br />

wa jua kwa spidi yake ya 186,000 maili kwa sekunde,<br />

itakuwa kiasi cha miaka 32 elfu kufikia mara moja na si tena<br />

illa baada ya miaka elfu 32 mingine. Na papo zipo nyakati<br />

ambazo haziwezi kuingia ndani ya akili ya mtu. Dakika<br />

moja ni sawa na miaka mia tano ya anga.<br />

Na upo huo wakati wa milele ambao ndani ya akili<br />

ya mtu haufikirikiki kabisa. Mnyezi Mungu ndiye anayejua<br />

– Wallahu ya`alam bi swa waah.<br />

WABILLAHIT TAWFEEQ.<br />

25


<strong>Al</strong> habib <strong>Al</strong> <strong>Faqeer</strong> Ahmad Sheikh Mohamed Sheikh Msiha,<br />

amezaliwa Singida mkoa wa Dodoma, mwaka 1938. Amepata elimu ya<br />

sekula Unguja na amebahatika kupata elimu ya juu katika chuo maarufu<br />

Afrika ya Mashariki Makerere Uganda.<br />

Elimu yake ya Dini ameipata hapo hapo Unguja toka kwa Masheikh<br />

mbali mbali, baadhi yao ni:<br />

Sheikh Sleiman <strong>Al</strong>wi (Muhib Rasul) (<strong>Al</strong> Marhum).<br />

Sheikh Seyyid Mansab.<br />

Maalim Himid (<strong>Al</strong> marhum).<br />

Maalim Hemed Muhamed El Buhry.<br />

Sheikh Seyyid Qamus.<br />

Sheikh Muawwiya Ibn Abdul Rahman.<br />

Sheikh <strong>Al</strong>ly Muhamed Comorian.<br />

Sheikh Ibrahim Mzee Ahd.<br />

Sheikh Haj Mzee Ahmad Msiha.<br />

Amma Elimu ya Nafsi na Roho Amepata Ijaza yake toka kwa A`limu<br />

mkubwa Duniani <strong>Al</strong> Habib Sayyid Omar Bin Abdallah (Mwinyi<br />

Baraka).<br />

Sheikh Ahmad amewahi kufanya kazi katika jeshi la Polisi<br />

Tanzania Bara katika mikoa mbali mbali mpaka alipostahafu.<br />

Katika umri wake wote Sheikh Ahmad alijahid katika kuendeleza<br />

Uislamu kwa kusomesha na kuandika vitabu vya mada na maudhui<br />

mbali mbali katika Uislamu. Pia alianzisha Majaalis Sehemu mbali<br />

ambazo ziko mpaka leo, Mtaa wa Pemba, Sinza, Bungoni, kijito nyama,<br />

Sadani (Ilala) na Kibaha (Misugusugu) ambapo ndipo ilipo Dhwarihi<br />

yake (alipozikwa).<br />

Sheikh Ahmad ametwawafu 27. 8. 2001. ( Mwezi 7 jumadda thany<br />

1421 H.R.). Akiwa na umri wa miaka 63, vile vile alivyokuwa akiomba<br />

aishi umri ule ule alioshi kipenzi chake Bwana Mtume Muhammad<br />

SAW.<br />

Insha <strong>Al</strong>lah Mnyezi Mungu amjaze kheri na alitie Nuru kaburi lake<br />

(Amin).<br />

Majaalis El Ulaa El Qadiriyya,<br />

Sinza Dar es Salam.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!