You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
YALIYOMO:<br />
No.<br />
Uk.<br />
1. Yaliyomo………………………………………….……..iii.<br />
2. Dibaji……………………………………………………iv.<br />
3. Utangulizi…………………………….………..……...….vii.<br />
4. Nafsi………………………………………..………….…1.<br />
5. Roho/Nafsi…………………………………….…….……9.<br />
6. Tiba ya Nafsi Khabbith…………………………………..13.<br />
7. Akili……………………………………..……….…...…...19.<br />
8. Moyo………………………....……………..………...…...25.<br />
9. Jedwary la Nafsi…………………………………………...28.<br />
10. Jinsi ya kuachana na Mwili……………………...………...29.<br />
iii.
DIBAJI:<br />
Bismillahir Rahmanir Raheem.<br />
Baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu Mola wa ulimwengu,<br />
Mfalme wa siku ya malipo yeye peke yake ndiye anayesitahiki kuabudiwa<br />
na hakuzaa wala hakuzaliwa.<br />
Anasema Mwenyezi Mungu katika Kurani Takatifu Surat<br />
Yusuf Aya ya 53:<br />
“….Nami sitakasi Nafsi yangu, kwa hakika kila<br />
Nafsi ni yenye kuamrisha sana maovu isipokuwa<br />
ile ambayo Mola wangu ameirehemu”.<br />
Maneno haya ya katika Kurani Takatifu aliyoyaelezea kumueleza<br />
Mtume Muhammad (SAW) yanamhusu Mtume Yusuf Bin Yakuwb (AS)<br />
alipokua anajitetea kuwa hakumtaka mke wa Mfalme wa Misri.<br />
Anamhakikishia kuwa “Nafsi ni yenye kutuamrisha sana maovu”<br />
isipokuwa iliyorehemewa na yeye Mola. Na hii iliyorehemewa na Mola<br />
ndiyo Nafsi ambayo yenye muelekeo mzuri yenye kumtii Mwenyezi<br />
Mungu na kumuabudu na ndiyo inayoitwa “<strong>Al</strong> Mutmainna” aliyoitaja<br />
Mwenyezi Mungu katika Kurani Takatifu Surat <strong>Al</strong>fajr:<br />
Ewe Nafsi iliyotulia rejeya kwa Mola wako<br />
hali ya kuwa utaridhika (kwa utakayoyapata)<br />
na Mwenyezi Mungu aridhike na wewe, basi<br />
iv.
Kupigana Jihadi na Nafsi ni jukumu kubwa linalotukabili katika<br />
maisha yetu ya hapa Duniani. Mfano alivotupigia Sheikh Ahmad katika<br />
kitabu hiki Uk. 11 wa Sheikh Abdul – Kaader Jeylani (Q.A.S.A)<br />
kuwa alichukua miaka kumi na tano maporini akifanza majaribio<br />
kuishinda Nafsi yake. Na akaishinda na kuitawala barabara. Na kuitawala<br />
huko ni kufikia kilele cha ucha Mungu na akawa mmoja wa Mawalii wa<br />
Mwenyezi Mungu. Na kabla yake alikuwepo Walii nchini <strong>Al</strong>yaman jina<br />
lake Abuwmuslim <strong>Al</strong> khawalaniy aliyempinga <strong>Al</strong> aswad <strong>Al</strong> ansiy<br />
aliyekuwa akijidai Unabii na Utume wakati wa Mtume Muhammad<br />
(SAW) alikamatwa na wafuasi wa <strong>Al</strong> ansiy na wakamtiya katika shimo la<br />
moto ili aunguwe. Moto haukumuunguza wala haukumchubuwa kama<br />
ilivyotokea kwa Mtume Ibrahim (AS), hii ni karama alizozionyesha walii<br />
huyu Abuwmuslim kwa kuishinda Nafsi yake. Kwa hivyo basi na<br />
tujitahidi kuzipiga Jihadi Nafsi zetu kwa sababu ndizo<br />
zitakazotusababishiya kuingizwa ima Peponi au Motoni. Amesema<br />
Mwenyenzi Mungu katika Kurani Takatifu<br />
Surat <strong>Al</strong> – Imraan, 185 :-<br />
“Kila Nafsi itaonja mauti na bila shaka mtapewa ujira<br />
wenu kamili siku ya kiyama, na aliyewekwa mbali na moto<br />
na akaingizwa peponi, basi amefuzu, na maisha ya Dunia<br />
hii ni starehe idanganyayo”.<br />
Mwenyenzi Mungu amjaze kheri Sheikh Ahmad kwa juhudi zake<br />
za kuandika kitabu hiki kwa kuwanufaisha na kuwazindusha ndugu zake<br />
Waislamu.<br />
WAMA TAWFIYQIY ILLA BI LLAAH.<br />
AHMAD HAYDAR MWINYIMVUA,<br />
DAR ES SALAAM.<br />
vi.
Bismillahir Rahmanir Raheem.<br />
UTANGULIZI:<br />
<strong>Al</strong>-hamdulillah na si vingine bali ni ukweli usiokanushika kua<br />
Mnyezi Mungu ndiye pekee mstahiki wa kila Swifa njema na Rehma zake<br />
Mola pamoja na amani zimwendee mjumbe wake wa mwisho Bw. Mtume<br />
Muhammad (SAW ) Mwalimu mkuu mno, aliyefundisha Umma huu wa<br />
mwisho Ilimu zote tunazozijua kuanzia siku zile za jahilia mpaka leo hii<br />
ambapo huyu humfundisha huyu na kuendelea mpaka siku ya mwisho<br />
ambayo kiitikadi tunaimani kua ipo na itawadia tu bila khilafi wala<br />
khiyari.<br />
Suala lililochukua uzito katika kitabu hiki Akili ni moja<br />
miongoni mwa Mas-la mazito na lilo muhimu sana. Na mwenye akili<br />
hushughulishwa mno na yote yenye kutaalaki na Akili maana kama<br />
iwavyo vyovyote vile.<br />
Wana wa Elimu ya Viumbe vyenye Uhai (Biologists) wa kileo<br />
wanakubali kutoijua khassa Akili ni nini. Hatua moja kubwa walopiga<br />
katika suala zima la akili ni kua kwake Ubongo wa mbele ya kichwa<br />
(Cerebrium) ni kitovu cha akili. Hii imepatikana kutokana na majaribio<br />
ya muda mrefu.<br />
Wana sayansi hao wameelezea ndani ya vitabu kadhaa-wakadhaa<br />
mfano wa “The Exploring Biology” ambapo ndani yake wameelezea<br />
kua hatua moja kubwa walioifanza kutokana na majaribio kadhaa ni<br />
katika kugundua ya kua akili Mahir (ile ilo kusanya mambo matano –<br />
macho, pua, sikio, ulimi, na mikono) na hiyo ni akili (isio julikana kua<br />
kitu gani) ni vilowekwa katikati ya hiyo Cerebrium.<br />
Akili yenyewe ikiwa ni matenda kazi ya hiyo Cerebrium kama<br />
vile uhai ni matenda kazi ya nyanja muhimu za uhai (Protoplasm).<br />
Linapoulizwa suala la akili na wapi katika mwili wa mtu ambapo<br />
Mnyezi Mungu ameiweka. Wengi huona kua akili ipo kichwani, lakini<br />
Mwendawazimu pia anacho. Hakuna<br />
vii.
Mwendawazimu ambae hana kichwa lakini matendo yake siyo ya mtu<br />
mwenye akili.<br />
Akili bila shaka ni lazima tuijue amma sivyo haitokuwa rahisi<br />
kudai kua nayo. Kutokana na kujiingikiwa nayo wengi katika ndugu<br />
zangu tumeona kuwepo umuhimu mkubwa kuandika fatwa kwa njia ya<br />
kipetopeto.<br />
Hakuna shaka kabisa kua baada ya kupata hakika yake itakua<br />
tumepiga hatua kubwa kiasi ilobaki ni wewe kutafuta njia za kuiongeza.<br />
Njia zipo basi mwenye akili hataziacha bali atazitafuta kwa udi na<br />
uvumba, na usiku na mchana.<br />
Tunamuomba Mnyezi Mungu atunufaishe kwa kijitabu hiki na<br />
kutufungulia kila lenye kuhitajika katika kutujenga kua watu wenye Akili<br />
kweli.<br />
Nahisi siwezi kukwepa kuwashukuru wote ambao walioandaa<br />
darasa la kila Juma tano pale Ilala kwa Akh Fuad Batarfy, Sharif Karama,<br />
Ba <strong>Al</strong>ly Bin Mkhashshe, Seyyid Hussein<br />
El Bayti, Sheybob, Akh Said Okash, Moh’d Batarfy, Saleh Hariz, Ababili<br />
Abdallah na wengineo ambao si rahisi kuwaorodhesha majina yao hapa.<br />
Bidii yao katika kuzishughulikia nuskha hizi kuzichapisha katika<br />
Computer na kadhalika ni moja inayoonyesha wazi kua ni wenye kupenda<br />
ilmu. Na haidhaniwi kua mwenye raghba ya ilmu si mwenye akili.<br />
Mnyezi Mungu atawajaza ziada ya vile ilivyoelezwa kua ni bora kuliko<br />
wenye kupigana vita vya jihadi, na Mahujaji na wafanzao Umra.<br />
Huwatakia maghfira ( hao wapendao ilmu) Mbingu na Ardhi na<br />
bahari miti na wanyama, pia mawe, na kila chenye kuchomozewa jua juu<br />
yake, na huko akhera malipo yao anayajua Mnyezi Mungu Sub hana<br />
wa Taala.<br />
“Ishi hapa duniani ukiwa <strong>Al</strong>im au<br />
Mutaallimi (mwenye kujifunza), au<br />
Mustamian (mwenye kusikiliza ilmu)<br />
usiwe mtu wa nne utahiliki.”<br />
viii.
Hii ni kawli yake <strong>Al</strong>ayhi Afdhalus Swalatu Was Salaam, Bwana Mtume<br />
Muhammed (. S. A.W).<br />
<strong>Al</strong> <strong>Faqeer</strong> Ahmad sheikh,<br />
Majaalis El Ulaa,<br />
El Qadiriyya, Sinza<br />
Dar es salaam,<br />
Tanzania<br />
Swafar – 21<br />
9 may 2000.<br />
ix.
Nafsi na Sifa zake:<br />
<strong>Al</strong> hamdullilah, waswalaatu lilahi taala wa salaamuha ala rasulillah.<br />
(S.A.W).<br />
Amma baad, Suala la Nafsi hii ambayo tunayo ndani ya miili yetu<br />
ni kubwa na pia zito, kwa hiyo basi haitakuwa jambo la akili kulipita hivi<br />
hivi tu minighayri ya kujishughulisha na kulijua kwake.<br />
Bwana Mtume (S.A.W) amelisemea hivi:-<br />
“Man arafa nafsahu<br />
faqad arafa Rabbahu”<br />
“Mwenye kuijua nafsi yake bila<br />
shaka ameishamjua Mola wake”<br />
Sababu ya kusema hivi kumjua Mnyezi Mungu ni wajibu wake<br />
mtu wa kwanza katika uhai, na njia nyepesi ya kumjua mola ni katika mtu<br />
kuijua Nafsi yake.<br />
Kuijua Nafsi ni kujua makamu za Nafsi. Hii ina maana ya kujua<br />
manzili zake saba kwa swifa na matendo yake.<br />
Ya kwanza:<br />
Nafsi Ammaara.<br />
Ambayo Mnyezi Mungu Sub-haana wa Taalah ameisema ndani<br />
ya Qur an kama:- S:12:53<br />
1.
“Mimi sijitakasi nafsi yangu, kwa hakika (kila)<br />
nafsi ni yenye kuamrisha sana maovu, isipokuwa<br />
ile ambayo Mola wangu ameirehemu. Hakika Mola<br />
wangu ni mwingi wa kusamehe (na) mwingi<br />
wa kurehemu”<br />
Hii ndiyo nafsi ovu na khabbithi kupita zote, kwa mujibu wa kauli yake<br />
<strong>Al</strong>ayhis-swalaatu Llahi Taala waa-lihi.! “Nafsi hii ni khabbithi zaidi<br />
kuliko mashetwani sabini”<br />
Inakutosha kuangalia zile sifa zake, ili kuthibitisha kauli yake<br />
bwana Mtume S.A.W wewe mwenyewe uelewe ya kwamba kila<br />
unapojishughulisha na kuifuatilia kwa karibu zaidi ndiyo jihadi kubwa<br />
kwako na kukuingizia thawabu nyingi ndani yake.<br />
Sifa za Nafsi Ammaarah<br />
Kupenda kula sana<br />
Ubakhili<br />
Kuhangaika<br />
Kua na tamaa<br />
Kuwa na kiburi (Wall yadh Billah)<br />
Matamanio<br />
Hasada na<br />
Ghafla<br />
Sifa zote hizi ni zenye kumpeleka mtu kwenye kuhiliki kwa adilla<br />
na ushahidi madhubuti toka kwa Bwana Mtume <strong>Al</strong>ayhi<br />
swala waatul-Lahi wa salaamuhu.<br />
Ya pili: Nafsi Lawwaama.<br />
Hii ni Nafsi inayojilaumu laumu, Seyyid Umar Bin Abdallah Bin<br />
<strong>Al</strong>-ba-shaikh Abiibakar Bin Salum ( Mwinyi- Baraka) akisema :- “Haina<br />
njia nyingine, ni kujilaumu”<br />
Lakini Mnyezi Mungu ameisemea vizuri. Ameiapia:- 75:1-2<br />
2.
“Naapa kwa siku ya kiyama tena naapa kwa nafsi<br />
inayojilaumu. (Kuwa imefufuliwa na mtalipwa)”<br />
Sifa za Nafsi Lawwaama:<br />
Kujilaumu laumu.<br />
Fikra.<br />
Kujizuia (Qabdh).<br />
Ujubi<br />
Lalamika lalamika<br />
Asili ya kuwa na sifa hizo ni kwamba ni kutaka kujiondosha<br />
kabisa katika Nafsi Ammaara kwa vitendo vyake vyenye kwenda<br />
kinyume na maamrisho ya Mnyezi Mungu.<br />
Nafsi Mul-hama.<br />
Ya tatu:<br />
Nafsi zote takribani zimetajwa hakika zake mwenye Qur an. Hii<br />
imetajwa ndani ya:- Suratish-shams. 91:7-8-9-10.<br />
“Na kwa nafsi (roho na aliyeitengeneza kisha<br />
akaifahamisha uovu wake na wema wake. Bila<br />
shaka amefaulu aliyeitakasa ( Nafsi yake) na<br />
bila shaka amejihasiri alieiviza (Nafsi yake)”.<br />
3.
Sifa za Nafsi Mul-hama.<br />
Ilmu.<br />
Tawaadhui.<br />
Tawba.<br />
Subrah.<br />
Tahaamul - kuvumilia adha.<br />
Kiakili tu ukizilinganisha swifa hizo na zile za nafsi ya kwanza<br />
utaona ipo tofauti kubwa mno ndani yake. Ndani ya nafsi hizi unaona<br />
wazi kuwepo Uislamu ndani yake, kama unavyoweza kuona kuwepo<br />
ukafiri ndani ya nafsi ya kwanza. Hiyo ni hatua<br />
kubwa katika kujijua. Ni hatua kunjufu katika jihad ya nafsi<br />
ambayo Bwana Mtume (S.A.W) ameihimizia.<br />
Nafsi Mutmainna.<br />
Ya nne:<br />
Hii ndiyo Nafsi pekee ya kwanza iliyotulizana kabbisa, haina vituko<br />
ndani yake, na, “Iliyosemezwa na Mnyezi Mungu Khasa”. Qur an<br />
89:27.<br />
“Ewe Nafsi yenye kutua.”<br />
Huko ni kunadiwa na Mnyezi Mungu mwenyewe lakini bila shaka<br />
ukiweka mazingatio ya kweli utaona kuwa ni miujiza mikubwa imo<br />
mwenye mnada huu kwa wenye akili.<br />
4.
Sifa za Nafsi Mutmainna:<br />
Ukarimu.<br />
Tawakkul.<br />
Hikam.<br />
Ibaada<br />
Shukar na Ridhaa.<br />
Hizo ni miongoni mwa sifa nzuri mno ambapo mtu anakua nazo<br />
ndani ya Uhai wake hapa duniani. Mawalii wote bila shaka ni wakarimu<br />
kwa hiyo kila anaye tamassak na sifa hii basi ametammasak na sifa ya<br />
Mnyezi Mungu. Nasi tumeusiwa na Bwana Mtume S.A.W. tujitabiishe na<br />
sifa nzuri nzuri za Mnyezi Mungu. Amma katika kushukuru kuna Uislam<br />
mzima ndani yake.<br />
Nafsi Radhiya.<br />
Ya tano:<br />
Nafsi hii imetajwa mara tu baada ya Mutmainna ndani ya Suratil Fajar<br />
katika juzuu ya “Amma.” Nafsi iliyo ridhiya.<br />
Sifa za Nafsi Radhiya:<br />
Zuhdi (Kuipa nyongo dunia).<br />
Ikhlas.<br />
Wara`a.<br />
Kuacha yasomuhusu mtu.<br />
Wafaa`i – Kutekeleza.<br />
Miungoni mwa sifa njema ambazo zimeibeba Nafsi hii hamna kama<br />
Ikhlas ambayo Shaytwani anaikhofu mno. Qur an imesema hivyo siyo<br />
mwandishi. Pia katika msururu wa utajo wa Nafsi tatu hizo, hii ndiyo<br />
yenye kukamilisha yaani:-<br />
5.
Nafsi Mardhiyya.<br />
ya sita:<br />
Nafsi hii imetajwa mara tu baada ya Nafsi Radhiya yaani ilo ridhiwa<br />
na Mola Sub-hana wa Taalah. Amma mtu akisha ridhiwa na Mnyezi<br />
Mungu basi hua hana haja ya kuogopa chochote tena.<br />
Sifa zake:<br />
Husnul khuluq – Tabia njema<br />
Lutf kwa viumbe.<br />
Taqarrab ila Llah – Kuacha yote yasiokuwa ya Mnyezi Mungu.<br />
Tafakkur - Katika utukufu na ukubwa wake Mola.<br />
Kuridhika na alokugawia Mnyezi Mungu Sub-hana wataala.<br />
Nafsi hiyo inatakiwa kurudi kwa Mola wake Radhiyya.<br />
Hali ya kuwa Mardhiyya hivyo basi, inatakiwa iingie katika kundi la waja<br />
wake Mnyezi Mungu.<br />
Waja wote ni wa Mnyezi Mungu lakini wapo ambao ni speshel.<br />
Amma katika walioukubali uja hakuna kama Bwana Mtume <strong>Al</strong>ayhi<br />
Afdhalu Swalaat Was-salaam.<br />
Mtume Muhammad S.A.W Ni mja wake na mjumbe wake. Mitume<br />
wengine wote wanamfwatia Nabii Muhammad .S. A W. kama Sayyidna<br />
Issa AS. ametajwa pia kama Abduhu warasuluhu lakini wamepitana<br />
kwa daraja na fadhila. Na pamoja na hayo yote pia Mtume SAW anasema<br />
ya kuwa…..“Hajifakharishi- Katika kuwa kwake Bwana wa watoto<br />
wote wa (Nabii Adam A.S.W).”<br />
Nafsi Kaamila.<br />
Ya saba:<br />
Pengine huitwa Nafsi Swafiyya, yaani iliyokuwa safi<br />
6.
kabisa. Kwa nini? Kwa kuwa sifa nzuri nzuri zote zimo ndani yake.<br />
Sifa zake:<br />
Sifa zote njema zilizotajwa katika Nafsi tano ukiacha Nafsi ya<br />
kwanza ambayo ni Ammara.<br />
Bwana Mtume S.A.W amesema:- “Kupigana na Nafsi ndiyo jihadi<br />
kubwa”<br />
Hakuna juu yake Jihadi nyingine yaani ile Jihadi ya Panga ambayo<br />
humfanya anayekufa ndani yake kuhisabiwa kuwa “yuko hai” haifui dafu<br />
kabisa hapa.<br />
Nafsi na makamu zake:<br />
Mpaka kufikia hapa bila shaka umeishaipatapata kiasi ambacho<br />
hakukupi shaka ndani ya moyo wako. Nini wamesema Maulamaa<br />
wakubwa wakubwa katika Uislam?.<br />
Wachache tu mfano wa akina Ghazzal, Busri na labda Habibi<br />
Ahmed Bin Abubakkar Bin Sumeit aliyekuwa Zanzibar katika karne ya<br />
kumi na nane mwishoni na kumi na tisa.<br />
Imam Ghazzal ameelezea vizuri sana mas-ala ya Nafsi, Roho na<br />
akili ndani ya vitabu vyake vya “Ihyaa ulumud deen”.<br />
Imam Busri ameelezea vizuri ndani ya “Burda” kitabu mashuhuri<br />
ambacho Waislamu wengi wanakijua na kukifanzia kazi katika matukio<br />
kadhaa wa kadhaa ndani ya uhai wa kila leo, katika Tawassul za kila<br />
siku. Yeye amesema kuwa:-<br />
“Nafsi ni kama mtoto mchanga ukimwacha<br />
atapondekea kunyonya na ukimzuia ataacha”.<br />
Nafsi haina cha ujana haina cha uzee, ikimshika mtu hua hasikii<br />
kitu katika waadhi wala nasaha. Tazama katika kuiachia kula sana kama<br />
Punda inavokutia uvivu na kadhalika.<br />
7.
Amma Habib Ahmed ndani ya Kitabu chake. “ kawkabur zaahir”,<br />
anasema.:- “ Nafsi ni kama smaku”. Chunguza smaku utaona inayo<br />
pande mbili. Upande wa kuvutia, upande wa kufukuzia. Ule wa kwanza<br />
ndiyo wenye kukufanza ukamili katika maovu na ule wakuzuia ndiyo<br />
unaokukataza kufanya maovu.<br />
Qur an 79.40-41<br />
“ Na amma yule anechelea kusimamishwa mbele ya<br />
Mola wake akaizuia nafsi yake na matamanio<br />
basi pepo ndio mashukio yake”<br />
Suala la kujizuia ni muhimu mno na ni Jihadi ya kila mmoja, kwa<br />
hiyo siyo mambo ya Sheytwani bali “Wewe binafsi yako”.<br />
Na kila unapoanza amali njema inakuwa inatakata sehemu kwa sehemu<br />
mpaka inang’aa kama Nuru, na hapo ndipo unapohesabika kua mtu<br />
kamili. Amma sivyo, basi wewe ni kama wanyama wengine wowote<br />
(mammals).<br />
Mnyezi Mungu atuwafikishe katika kheri.<br />
8.
ROHO/NAFSI<br />
Qur an: 17:85.<br />
“Na wanakuuliza habari ya roho. Sema, roho ni jambo<br />
lililohusika na Mola wangu (Mnyezi Mungu) nanyi<br />
hamkupewa katika ilmu (Ujuzi) ila kidogo kabisa”.<br />
Ushahidi wa aya hii ni wenye kuonyesha wazi wazi kua upo ujuzi<br />
wa Roho. Na pamoja na kua kidogo au kiduchu tu. Ndiyo makadirio<br />
ambayo Mnyezi Mungu ameonelea kua ni yenye kutosha kabisa kwa hapa<br />
duniani.<br />
Katika misemo yetu ya Kiswahili ni ule msemo:- “Maji ya kifuu ni<br />
Bahari ya chungu” (yaani yule mdudu mdogo na mwepesi sana – mdudu<br />
wa sukari pengine mdudu chungu).<br />
Huo ni mfano mmoja tosha kwa mtu mwenye akili ya kujisaidia nayo<br />
angalau kidogo tu; ni wazi kuwa hatahitaji maelezo marefu ya aina<br />
yoyote.<br />
Tukiangalia kwa mazingatio kauli ya Bw. Mtume S.A.W juu ya<br />
Rehma za Mnyezi Mungu tunaelewa fika kua ni “moja kwa mia moja”<br />
kwa jumla tangu dunia ianze mpaka kufikia kiyama. Bila shaka moja kwa<br />
mia ni sehemu ndogo mno, na hapo mpaka leo hii karne ya Ishirini na<br />
moja mwaka huu wa Elfu mbili watu bado wangali wanarehemeana bado.<br />
Na hasa ukiongezeka usemi wake kua:<br />
“Warehemuni walioko ardhini atakurehemuni<br />
aliyeko mbinguni”.<br />
9.
Basi kidogo hiyo ni yenye kutosha kabisa. Pengine ingekuwa ni<br />
Rehma mbili katika zile mia ndo ziloshushwa ungesema watu<br />
wangeshindwa kufanza mambo mengine yoyote bali wangekuwa<br />
wanarehemeana tu. Wapo watu wengine wanafikia kuikanusha kisirisiri<br />
au kipumbavu kiuchache wa ilmu. Aya hiyo: 17:85 wao wakidai kua<br />
hamna anaejua mambo ya roho illa Mnyezi Mungu .<br />
Mnyezi Mungu anaijua mno hiyo Roho; anasema kua ametupa ujuzi<br />
nayo lakini ni kuduchu. Si busara kuchukua kidogo ya Mnyezi Mungu<br />
ukaifanza kua ndo hiyo hiyo kwako wewe Mwanadamu, na huku ukidai<br />
kuamini kua: –<br />
“Hana anayefanana naye hata mmoja”.<br />
Kuna hatari ya kufikia kujichukua wewe kama <strong>Al</strong>im-Sameeun<br />
(Unaesikia ) Basweerun (Unaeona) na kadhalika, kua ndo hiyo hiyo ya<br />
Mnyezi Mungu (Mnyezi Mungu apishilie mbali fikra kama hizo kwetu).<br />
Mnyezi Mungu anamuona na kumsikia sisimizi michang’ato yake<br />
chini ya ardhi ndani ya giza la usiku, Je Shekhe, wewe wasikia hivo hivo?<br />
Mnyezi Mungu anayajua ya siri na yalofichika ndani ya siri katika vifua<br />
vya watu. Jee na wewe Sheikh ni hivo hivo? Basi Staghfiru kwa Mola<br />
wako na ukithirishe Kalima ya Tawheedi usije ukahiliki kwa kujifanya<br />
kichwa Mchungu. Uislamu unataka unyenyekevu (Sub-Mission).<br />
Na isisahaulike kua Bwana Mtume SAW amekataza malumbano na<br />
kwamba mwenye kuacha kulumbana (kubishana na hali ya kua yeye ndio<br />
mwenye haki basi (malipo yake) siku ya kiama Mnyezi Mungu<br />
atamjengea Nyumba ya Dhahabu). Na ikiwa kwa waliopewa Chuo (Ahlil-<br />
Kitab) Basi malumbano yawe “Bil-lati Hiya Ahsan” kwa njia ya wema<br />
sana. Kwa nini?; kwa sababu ni mara chache tunakumbuka kua mtu<br />
anapopinga jambo hua na maana ya kufru. Kwa hiyo basi huenda mtu<br />
akawa na Sijda yake usoni lakini ni Kafiri.<br />
10.
Lau kabla ya kubishia jambo ambalo amelisema ambae hana ushuhura<br />
katika Jamii, tungezingatia katika kawli aizungumziayo kua ni yake au ya<br />
Mnyezi Mungu ingekuwa rahisi kuyahukumu mambo kwa njia ya Amani<br />
na busara ya hali ya juu ambayo haingemgandamiza mtu. Ilmu iwe ya<br />
manufaa siyo ya fadhuli.<br />
<strong>Al</strong> Habib Seyyid Umar akisema:- “Suala la Nafsi / Roho si la<br />
kusemea kidogo tu kisha ukaliacha, utapoteza watu”. Yeye<br />
mwenyewe ilimchukua masaa matatu kuelezea juu ya Nafsi alipotoka<br />
Makerere University Uganda ambako alikua na kina Nyerere, Obote,<br />
Yusufu Lule na wengine kadhaa aliowataja ambao baadae walishika<br />
nyadhifa kubwa kubwa katika Serikali za Afrika Mashariki.<br />
Sheikh Abdul-Qa dir Jeylani (Q.A.S.A) alichukua miaka kumi na<br />
tano maporini akifanza majaribio ya kuishinda Nafsi na hatimae<br />
akaishinda na kuitawala barabara. Na miungoni mwa natija ni ile ya<br />
kufunguliwa mambo mengi makubwa makubwa yalojaa karama, yote<br />
hayo hayajaja kwa upendeleo bali Mujaahada.<br />
Na katika mda wote huo alikua akifunga kila siku - labda siku moja<br />
tu alifungua kwa sababu ya maskini mmoja alietaka kumuombea mtu Dua<br />
lakini kwa sharti ale nae pamoja, Basi alifungulia kwa ajili hiyo -<br />
Chambulecho <strong>Al</strong> Habib:-<br />
“Nini Swaumu ya miaka kumi na<br />
tano kwa Dua ya masikini huyu”.<br />
Nafsil Ammaara haina inapopata taabu kama katika Swaumu. Basi<br />
kwa apendae kupata Sa’ada ya Nafsi yake na aanze na tabiya hii ya<br />
kufunga funga.<br />
Swaumu za Twaa (Tatwa-w-u’e) kama vile Jumatatu na <strong>Al</strong>-Khamisi<br />
na siku za mwezi kumi na tatu kumi na nne na kumi na tano za kila<br />
mwezi. Huenda ukahisabiwa kama aliyefunga Dahar nzima. Kumbuka<br />
kauli ya <strong>Al</strong> - Mustwafa S.A.W:-……<br />
“Mwenye kufunga Ramadhani akafatanisha na Sittatish-<br />
Shawwaal (Siku sita za Shawwal) hua kama aliyefunga Dahar….”<br />
Sababu ni Basweet kwa kuchukua malipo ya kila jambo jema<br />
11.
Thawabu 10; Jumla ya siku thelathini na sita kwa Thawabu kumi<br />
inafanza siku za mwaka mzima (Dahar) yaani siku mia tatu na sitini, na<br />
hali kadhalika funga ya Ayyamul-Beydh 13, 14 na 15 ya kila mwezi kwa<br />
miezi kumi na mbili ya mwaka mzima inafanza siku 36 zenye Thawabu<br />
kila moja inakuja ile ile mia tatu na Sitini ambazo ndo Dahar. (Tazama<br />
Hikma ilivyo ajabu kiasi gani ndani yake).<br />
Amma katika Khatwir (mapenzi ya jambo lenye kuvutia moyoni)<br />
yake Bw. Mtume SAW <strong>Al</strong>ivutiwa mno na Swaumu ya Nabii Daudi<br />
Babake Nabiy-<strong>Al</strong>lah Suleiman A.S - ambae alikuwa akifunga siku moja<br />
na kula siku moja.<br />
Majaribio hayo yote hassa si vingine Illa ni yenye makusudio ya<br />
kumtengeneza mtu ili awe mwema na mwenye Swifa za kuwa<br />
Mtawala alokusudiwa na Mola Subhana wa Taala hapa Duniani (The<br />
divine’s viceregent).<br />
Njia nyepesi mno katika kushinda Nafsi hii ilokwisha<br />
kukudhihirikia ukhabith wake mda mrefu sasa tangu ubaleghe hadi hii leo<br />
hakuna kama kwenda kinyume ya swifa zake ambazo tayari<br />
umeishazifahamu .<br />
Maswahaba zake Bwana Mtume SAW, Radhya-<strong>Al</strong>lah Anhum<br />
wakifanza majaribio katika kila jambo lililohitaji muamalla zama za<br />
kuteremshwa wahyi toka kwa Mola wa ulimwengu zote.<br />
Tukumbuke la maana angalau moja katika natija na faida nzuri katika<br />
majaribio (Experimantations) nalo ni kuongezeka akili.<br />
Sasa hebu na tuangalie katika ya kuhitaji kuyafanzia kazi leo kabla kesho<br />
kuhusu hii Nafsi khabith.<br />
12.
Jinsi ya kuitibu Nafsi khabbith.<br />
Kupenda kula sana: Basi dhidi yake ni kufunga – Swawmu. Bw.<br />
Mtume SAW alisema:-<br />
“Sisi ni wale ambao hawali mpaka wawe na<br />
njaa na pindi tulapo basi hatushibi huondosha<br />
mkono hali ya kuwa hatukushiba na hatuna njaa”.<br />
Mfalme mmoja aliita matabibu ili wampe dawa ya kuondosha maradhi<br />
yote. Wakamwendea mabingwa katika fani ya Twiba toka Arabuni , India<br />
na Afrika (Sudan) Mwarabu alimwambia kuwa ni Habba Soda. Muhindi<br />
alimwambia kua ni maji ya moto Asubuhi kabla ya Stiftahi na usiku<br />
wakati wa kulala. Pakapita kimya kiasi ambacho kilimpelekea amuulize<br />
Twabib Mwafrika vipi mbona uko kimya au umeshindwa? Bwana<br />
Mwafrika akasema:- “Bwana Mfalme, ni kweli Habba Soda imesemewa<br />
na Bwana Mtume SAW kua inatibu maradhi yote ila mauti, na lau na<br />
mauti yangekuwa na dawa, basi Mnyezi Mungu angeweka mwenye<br />
Habba Soda. Amma kwa maji ya moto tumbo hulainika na mafuta<br />
mwilini huyeyuka hivo basi, mtu upunguza unene. Lakini dawa ya<br />
maradhi yote hakuna kama kula wakati mtu una njaa, na kuondosha<br />
mkono kabla hujashiba (na kuvimbiwa), njia hii huwa ni kinga kabla<br />
kujitibu.”<br />
(Preventetion is Better than Cure).<br />
Mfalme akasema kuaTwabib Mwafrika ameswibu na kuhibu yaani<br />
ndiye aliyepata.<br />
Ubakhili: Kinyume chake ni ukarimu – Sukhaa.<br />
Bakhili ni Aduwwal-Llah hata kama ni mchaji mtaabbadi<br />
Mkubwa, na karimu ni kipenzi cha Mnyezi Mungu hata kama<br />
ni faasik.<br />
Kuhangaika: Dhidi yake ni utulivu ambao unaandamana na Nafsi<br />
Mutmainna.<br />
13.
Kua na tamaa: Zingatia ule usemi “Tamaa mbele mauti nyuma”.<br />
Kinyume chake ni kinaa na kule kukinai ni utajiri mkubwa, anasema<br />
Mtume wa Mnyezi Mungu.<br />
Kuwa na kiburi: (Mola atuepushe nacho) Dhiddi ni kujitupa chini<br />
kua Mnyenyekevu.<br />
Hata ikibidi kufanza aina ya shughuli ambazo lau atakuona yeyote<br />
yule basi hatakosa kupata hisia kama za kudharauliwa. Hiyo ina kheyri<br />
zaidi kuliko kutukuzwa ukapata kiburi.<br />
Matamanio: Lau huanguka kwa kufunga Swawmu tu. Lakini ziada<br />
ni katika kuyakumbuka mno Mauti. Bwana Mtume SAW alieleza<br />
kua katika kuyakumbuka mauti imma itamfanza mtu apungunze<br />
maasi au atazidisha Ibada.<br />
Mfano utabiri wa Pope mwaka 1959 kua 1960 ingekua mwisho<br />
wa Dunia, wa Moshi Kilimanjaro walibakia Makanisani kuanzia Krismas<br />
mpaka January, ni wenye kutosha kuthibitisha ukweli wa kuyakumbuka<br />
mauti ni waadhi kamili, na ambae hawaidhiki kwa mauti, basi huyo hana<br />
waadhi.<br />
Hasad: Amma kuhusu Hasad ambayo Bw. Mtume SAW amesema:<br />
“Ni ugonjwa usio na Dawa”. Illa kuacha tu kule kuhusudu, mtu wa<br />
akili anatakiwa kuyazingatia sana maanani huenda akanusurika.<br />
Maisha ya hapa Duniani yamejaa majaribu, kwa hiyo mtu mwenye<br />
akili nae anatakiwa afanze majaribio kwa kila jema alolijua. Akili haina<br />
njia ya kuzidi kama katika mtu kua na ungi wa Tajiriba (Frequent<br />
Experimentation Culculation and So on and so Forth) katika<br />
majaribu makubwa tulonayo hasa katika zama zetu hizi hakuna kama<br />
“Wanawake”. Bwana Mtume SAW akisema :-<br />
14.
“Sijakuachieni baada yangu fitna ashaddu<br />
kuliko wanawake”<br />
Tuondoshe au tupunguze habari za: “Aa!! Sikataka mwenyewe!” <strong>Al</strong>-<br />
Habib (Mwinyi Baraka) akisema :- “Itafaa wapi si kataka<br />
mwenyewe“. Ni nzuri mtu kua mwema hasa anapokua kijana aliyejaa<br />
Ghururi ambazo daima humzunguka kweli kweli. Wakati wa ujana ndo<br />
aghlabu huvutiwa na mambo ya ajabu ajabu ya maisha ya ghururi.<br />
“Haingii peponi ambae ndani ya moyo<br />
wake ana punje ndogo ya kiburi.<br />
Kadhalika Ubakhili umuaduisha (humfanza awe adui wa Mnyezi<br />
Mungu ) Na pia adui wa Nafsi yake yeye mwenyewe. Na vipi mtu huyo<br />
kua rafiki ya mwingine? Amma ni kweli kua:<br />
“Sakhii alie Faasik ni Mahbub mbele za Mnyezi<br />
Mungu, kuliko Bakhili mchaji Mungu”.<br />
Juwa ewe mtafuta matukufu kwa Mnyezi Mungu Mtukufu ya kua<br />
Mnyezi Mungu anapotaka kufanza mmoja ya waja wake kua Walii<br />
(Rafiki) Basi, humpamba kwa sifa hiyo ya ukarimu na tabiya njema.<br />
Tumeishaona jumla ya sifa njema katika Nafsi sita, sifa ambazo ni<br />
zenye kumtosha mtu kujipamba nazo ili afanikishe katika kua mja wa<br />
Mnyezi Mungu wa kweli kweli.<br />
Na mtu anapofikia kua kipenzi cha Mnyezi Mungu basi hua hana<br />
hofu juu yake na kila siku hua ni mtu wa mafanikio mazuri. Kila<br />
analolitaka Mnyezi Mungu atampa thamma atampa. Hivyo ndivyo<br />
asemavyo yeye mwenyewe Sub-Hana wa Taala katika hadithi takatifu<br />
(Hadithil- Qudsi)<br />
Kila unaemsikia kua ni walii basi kafikia Daraja hiyo kwa<br />
maagizo hayo yaliyomo mwenye Hadithil-Quds, na kwa kumpenda mno<br />
Bw. Mtume Muhammad <strong>Al</strong>ayhi Swalawatullah Wa Salamuhu. Nasi<br />
Inshaallahu Taala tupate Tawfiqi ya kweli ndani ya kupigana jihadi<br />
kubwa hii dhiddi ya Nafsi vile alivyotuusia Bwana wa Mabwana, Bwana<br />
wa Watoto wote wa Sayyidna<br />
15.
Adam . ASW. Bwana Mtume S.A.W. amesema:<br />
“Lau ningechaguzwa juu ya Utume ninataka kitu<br />
gani nisingechangua isio kua tabiya njema kwani<br />
kila cha ziada (Fadhila) ni chenye kuondoka na<br />
kwisha, isipokuwa sifa njema; Kwani hizo hubaki<br />
na wewe (milele)”.<br />
Ni nani baada ya Mnyezi Mungu na Mtume wake mkweli wa<br />
mambo kuhusu yote yamuhusuyo mtu hapa Duniani? Swifa nzuri na tabia<br />
njema ndo zimfanzazo mtu kuonekanwa mtu amma sivyo, mtu hua ni<br />
mnyama tu (Mammals-Biologists wanasema).<br />
Na pengine mtu huzidiwa na Wanyama kibaadhi ya sifa. Matendo<br />
yote ayafanzayo mtu pia Mnyama huyafanza pamoja na kutokuwa na<br />
akili. Lakini wakati asiyekuwa na akili anamsabihi Mola muumba na<br />
kuswali swala ambayo Mnyezi Mungu na huyo Mnyama anaijua, basi<br />
mwenye akili mtu hua chini ya Mnyama. Na hivyo ndivyo ilivyosimuliwa<br />
mwenye:<br />
Qur- An- 7:179.<br />
“ Na bila shaka tumewaumbia Moto wa Jahan-nam<br />
Wengi katika Majini na wanadamu (kwa sababu<br />
hii) Nyoyo wanazo lakini hawafahamu kwazo<br />
(hawataki kufahamu kwazo) na macho wanayo<br />
lakini hawaoni kwayo na masikio wanayo, lakini<br />
hawasikii kwayo. Hao ni kama Wanyama, bali wao<br />
ni wapotofu ( Wapotevu) zaidi – hao ndio<br />
walioghafilika”.<br />
16.
Suala la pepo na Moto si suala la mtu kujipangia, amma sivyo hangeingia<br />
yeyote Motoni. Lakini suala la kufananishwa mtu ambaye Mnyezi Mungu<br />
amemtukuza kupita viumbe vyote hapa Duniani aje kufananishwa na<br />
Mnyama asiye na akili na papo awe mpotevu zaidi, hilo ni tusi zito sana.<br />
Mambo ya kweli kama haya inataka mtu aweze kuyazingatia na<br />
kuazimia azma ya kweli kujibadilisha kwa kadri ya uwezo wake pamoja<br />
na kumuomba Mnyezi Mungu amuongoze kwa Rehma zake.<br />
Mnyezi Mungu anajua sana jinsi uzito wa Mitihani yake ulivyo kwa<br />
mtu katika mapambano yake na Nafsi yake, Matamanio, Dunia na<br />
Sheytwani, Basi, hakuna haja ya kukata tamaa na Rehma zake Sub-Hana<br />
Wataala.<br />
Tazama vile Mnyezi Mungu atuambiavyo katika: Qur an 39:53<br />
“Sema, “Enyi waja wangu mliojidhulumu Nafsi<br />
zenu, msikate tamaa na Rehema ya Mwenyezi<br />
Mungu bila shaka Mwenyezi Mungu husamehe<br />
Dhambi zote. Hakika yeye ni mwingi wa kusamehe<br />
(na) mwingi wa kurehemu”.<br />
<strong>Al</strong> –Habib (Mwinyi Baraka), Akisema: “Hakuna dhambi<br />
inayomshinda kuisamehe ila Shirk”. Kawli hii ukiitia maanani<br />
unapata matumaini ya moyo kua Mnyezi Mungu ni mzuri mwenye<br />
huruma mno kuliko Mama kwa kichanga chake.<br />
Tusisahau pia vile alivyotuusia Bwana Mtume S.A.W. katika<br />
maneno yaliyojaa hikma ndani yake kua:<br />
“Mtu ni hadithi (Mazungumzo tu) baada yake,<br />
basi (Tu) jitengenezee hadith nzuri kwa<br />
watakaokuja kusimulia (Baadae)”<br />
17.
Tena na tena na tumuombe Mnyezi Mungu atupe Tawfiqi na mioyo yenye<br />
nguvu katika kuishinda mitihani yake kwa wingi wa Subra na shukurani<br />
kwa Jaha ya Bwana Mtume Muhammad Swallallahu Taala <strong>Al</strong>ayhi wa<br />
<strong>Al</strong>ihit-wahiraati-Ummahaatil Muslimiina. DUNIANI. (Amin).<br />
18.
AKILI:<br />
Ni Nuru ya kung’aza, Mnyezi Mungu ameiweka ndani ya Moyo<br />
wa mtu na daima hunga’ara kwenye ubongo ambao uko kichwani katika<br />
mtu.<br />
Mfano wa karibu kabisa ambao mtu wa kawaida anaweza<br />
akaipata-pata kirahisi ni ule wa Projector na Screen katika kufanza<br />
kazi pamoja, bila ya ushirikiano si rahisi. Ndo kusema tumuonapo mtu<br />
kaharibikiwa basi huwa hiyo Johari ya akili ndo iliyoathirika kwa hiyo<br />
huo ubongo wenye Awnsi kumi na sita hua haufanzi kazi kabisa.<br />
Bw.Mtume SAW amesema:-<br />
“Usimlilie aliyekufa mlilie ambae amepungukiwa<br />
na akili yake”.<br />
Chombo pekee kilo Azizi kwa mtu hakuna kama Akili, na hiyo<br />
ndiyo yenye kutafautisha baina ya mtu na Mnyama.<br />
Ukifungua Qur an utaona sehemu nyingi imetajwa Akili. Na ni<br />
kutokana na matendo gani hasa ndo mazingatio ya dhati<br />
yanapochukuliwa. Aya ifwatayo ina mengi ya kuzingatia<br />
Qur an 2:164:-<br />
19.
“Hakika katika kuumbwa kwa mbingu na ardhi,<br />
na katika kuandamizana usiku na mchana na katika<br />
(mwendo wa) vyombo ambavyo hupita katika bahari<br />
kwa (kuchukua vitu) vifaavyo watu, na (katika<br />
kumiminika ) maji aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu<br />
kutoka Mawinguni na kwa (Maji) hayo akaihuisha ardhi<br />
baada ya kufa kwake Na akaeneza humo (Ulimwenguni<br />
kwa ajili ya maji hayo) kila aina ya Wanyama, na katika<br />
mabadiliko ya upepo na mawingu yanayoamrishwa<br />
kupita baina ya mbingu na ardhi, Bila ya shaka<br />
(Katika haya) zimo Ishara kwa watu wenye akili<br />
(kuwa yuko Mwenyezi Mungu na ni mmoja).<br />
Na kweli ikiwa tofauti ya pekee kubwa kati ya mtu na Mnyama ni<br />
akili ni wazi kua Mnyama hawezi kua na habari yeyote ya vyombo<br />
vinavyotembea baharini, kinachobadilisha usiku na mchana na kadhalika,<br />
basi mtu ambae hana habari ya hayo yote bila shaka hataachana futi moja<br />
na Mnyama mwenyewe. Hilo ni tusi kubwa ambalo ukimweleza mtu basi<br />
mtapigana sana pengine akwambie: “… ngoja leo ndo utauona huo<br />
unyama wangu…”<br />
Akili imesemwa kua inazidi na kupungua. Kuzidi kwake ni<br />
kutokana na wingi wa majaribio katika mambo mbali mbali ambayo<br />
umeanza kuyajua hivi sasa. Na humo humo Mnyezi Mungu<br />
anakufundisha yeye mwenyewe ambayo hukua unayajua.<br />
Ni ajabu kubwa kwa mwenye akili, lakini kwa asiyekuwa na akili hataona<br />
chochote cha maana ndani yake.<br />
Amma kupungua kwake akili ni zama za kufanza makosa akili<br />
huondoka, na ndo maana ya kauli yake Bw. Mtume SAW kua:-<br />
“Hawi muumini anaiba, zama zile za kuiba (kwake)<br />
kua ni muumin, au anazini zama zile za kuzini kua ni<br />
muumin, au anauwa zama zile akiuwa kua ni muumin”.<br />
20.
Na wale ambao zama Sheytwani anapowashika hukumbuka basi<br />
saa hiyo hiyo huwa wanaona (Mno) akili ndo huwa macho,<br />
ikamkumbuka na kumtaja Mnyezi Mungu.<br />
Na azingatie mtu juu ya vitu ambavo tunadai tunavijua mno na<br />
kutokana na kuvijua huko na mazoeya tunahisi ati havitupi taabu hata<br />
kidogo: Radio, Tepu, Tv, Magari, Kamera, Taa za Stimu, Kompyuta,<br />
Mobitel, Inter-net na kadhalika: jee viliteremka moja kwa moja toka<br />
Mbinguni kama mvua?.<br />
Hili ni suala tosha kukuwezesha kuichemsha Akili yako ambayo<br />
labda unatumia sehemu yake moja tu ya – kumi na sita (1/16). Daima<br />
usipoichemsha, itabaki hivyo hivyo mpaka kiyama ambapo itaonekana<br />
kua ulipewa Akili lakini hukuitumia!!.<br />
Sifa za mwenye Akili:<br />
Mnyezi Mungu aliyetukuka amejaalia kila kitu kua na swifa zake<br />
kwa makusudio maalumu ili kipate kujulikana kwa wepesi na<br />
kutambuliwa kwa njia iso na shaka hata kidogo. Halikadhalika Akili nayo<br />
imepewa swifa zake maalumu ambazo zinakujulisha wazi kua mwenyewe<br />
ni mtu mwenye Akili.<br />
Hizi ndo swifa za Akili kutokana na mafunzo alofundisha Bw.<br />
Mtume SAW, katika hadithi iliyopokelewa kutokana na Bi. Aisha (R.A)<br />
hakika amesema:-<br />
Akili inayo Swifa kumi (10) kati yake zimegawika ndani ya mafungu<br />
mawili:- Dhwahiri na Batwin.<br />
Dhwahiri Ni zile zilizo wazi wazi kabisa mtu akiziangalia anaziona,<br />
nazo ni :-<br />
1. Swamt: yaani ukimya, Bw. Mtume SAW katika Swifa hii<br />
pia amesema kua: “ Mwenye kuzidisha maneno yake<br />
basi huzidi kuanguka kwake” (Speech is Silver,<br />
Silence is Gold) (Kusema sema ni fedha na<br />
kunyamaa ni dhahabu – kinaong`arisha.)<br />
21.
2. Hilm: Upole.<br />
3. Tawadhu’i : Yaani ule Unyenyekevu ikiwa ni ile hali ya kujitupa<br />
chini na hata kama Mnyezi Mungu amekufanza kuwa<br />
Mfalme mbele za watu kwani hapo hasa ndo pahala<br />
pake. Amesema Bw. Mtume SAW “Mwenye kujiweka<br />
chini, Basi Mnyezi Mungu humrufaisha ( Humnyanyua<br />
humpandisha juu)”.<br />
4. Kuamrisha mema.<br />
5. Kukataza mabaya: Daima hutakia wenzake mambo ya<br />
kheri kila anapokueko baina ya watu.<br />
<strong>Al</strong>- Habib Sayyid Umar akiwa katika safari za Ulaya kwenye<br />
meli, safari hiyo alijiwa na kijana wa kizungu akawa anamtolea nasaha<br />
na kumueleza juu ya Mnyezi Mungu na kumsomea <strong>Al</strong>-Hamdu na<br />
Qul-Huwallahu kwa taabu. <strong>Al</strong>-Habib alimuuliza ni mda gani tangu<br />
amekua Mwislam? akamwambia miezi sita. Lakini aliahidi kwa Mnyezi<br />
Mungu kua akikutana na mtu yoyote atamwelezea juu ya Mola Sub-hana<br />
Wataala, na hali kadhalika katika kukataza Mabaya ambayo watu<br />
huyafanza, uzuri zaidi ni kuwahi kabla ili mtu aweze kujiandaa na<br />
kuyakwepa.<br />
Sifa za batwin:<br />
6. Tafakkur: Yaani hali ya kufikirifikiri hasa katika dalil nyingi<br />
zilizojaa na kutapakaa katika maumbile, kuanzia mbingu<br />
na viliomo juu na ndani yake. Ardhi na viliomo ndani<br />
yake, mfano wa milima, wanyama, majani, maji na<br />
madini mbali mbali. Kwa mtu wa Tafakkur bila shaka<br />
ndani ya Machache hayo angeweza kuandika vitabu vya<br />
Ilimu fani mbali mbali tele na nyingi ni zenye umuhimu<br />
kweli kweli ndani ya maisha ya hapa duniani.<br />
22.
Bwana Mtume SAW amesema:<br />
“kutafakkur katika maumbile ya Mnyezi Mungu<br />
saa moja ni bora kuliko Ibada (ya sunna) ya<br />
mwaka mzima”.<br />
7. Ibra: Katika maajabu mazito ya akili, swifa hii imetiya<br />
fora kwani katika maisha yake huenda mwenye<br />
akili ndogo akamwelewa vibaya na kumtabiri<br />
ambavyo sivyo alivyo – pengine aseme ni<br />
mchawi.<br />
8. Khofu: Kumkhofu, kumuogopa Mnyezi Mungu peke yake. Amma<br />
kwa yule asie mkhofu Mnyezi Mungu. Basi itafaa kumkhofu<br />
zaidi, kwani haachi kutomuogopa Mnyezi Mungu illa moto<br />
mdogo au mwendawazimu peke yao hao. Inatosha kuonyesha<br />
kua mtu anamkhofu Mnyezi<br />
Mungu kwa kutekeleza kwa kadiri ya uwezo wake yale yote<br />
aloamrishwa ayafanze na kuacha yale yote alokatazwa nayo.<br />
Haiwezi kua ni khofu “eti mbona havui nguo<br />
akatembea uchi au kuhujumu watu.” Wazimu upo<br />
aina saba akichunguza lazima atapata ncha<br />
ilonasibiana nae, na anaemjua mwendawazimu<br />
kisha usimkhofu basi ipo hatari ya kua yeye ni zaidi.<br />
9. Kuyaadhimisha madhambi:<br />
Yaani ayaone mazito hata, yawe madogo vipi kwani hawezi<br />
akajua ni dhambi ipi aifanzayo ambayo itamfanza Mola wake<br />
achukie na kumfuta katika waja wake warehemewa. Zingatia<br />
juu ya moto mkubwa ambao mwanzo wake ni cheche ndogo<br />
ndogo kabisa<br />
10 Kudhalilisha nafsi:<br />
23.
Abadan.<br />
Nafsi kila siku inataka makuu na kutambuliwa na wewe<br />
kua inayo haki kwako, ni kama vitimbi vya mtoto mdogo<br />
nyumbani kwao na hasa wanapokuwepo wageni. Na kama<br />
ilivyo maalumu nafsi ukiitukuza ni lazima mwisho wake<br />
itakuliza, kwani daima haikutizamii maslahi kwako<br />
Nafsi ilokusudiwa hapa si ingine bali ile <strong>Al</strong> ammara.<br />
Mnyezi Mungu ameelezea kua daima ni yenye kuamrisha<br />
maovu tu haibadiliki hata siku<br />
moja. Kwa kifupi mwenye Akili lazima awe na mifano<br />
iliyotajwa kwenye swifa kumi hizo. Na si rahisi kwa<br />
asiekuwa nazo kudai kua na Akili.<br />
Tunamuomba Mnyezi Mungu mjuzi wa kila jambo atufungulie<br />
Tafhuma katika kuielewa na kuitumia vyema Akili jambo ambalo Mola<br />
Sub-hanalaah amelisema kua ni azizi. Kwani hakuna baada Nuru ya<br />
Bwana Mtume SAW, jambo azizi kuliko<br />
A K I L I.<br />
24.
Moyo.<br />
Kwa Kiarabu Moyo ni Qalb; yaani kitu cha kubadilika badilika,<br />
leo hivi kesho vile. Na kutokana na maana hiyo Mapinduzi ni Inqilaab.<br />
Pia ni yenye kukokotezwa kumuomba Mnyezi Mungu mwenye<br />
kuzipindua nyoyo kila siku baina ya vidole vyake viwili – azithibitishe<br />
nyoyo zetu ndani ya Twa`a yake.<br />
Moyo umefananishwa au nasibishwa na Arshi yake Mnyezi<br />
Mungu; kwani mambo yote huanzia hapo. Kadhalika ndani ya Moyo<br />
ndipo panapoanza mambo yetu yote, na mengi tunashangalia sana hivi<br />
leo. Tunayaona ya ajabu, na hiyo peke yake ni Ajabu. Mnyezi Mungu<br />
hajaumba sanaa ya ajabu kuliko Mtu, na papo mtu huyo huyo anaona vitu<br />
vingine alivyovitengeneza yeye mwenyewe kua ni Ajabu. Bwana Mtume<br />
SAW amesema katika hadithi ambayo ni mashuhuri sana kua:-<br />
“Ndani ya mwili lipo pande la nyama Jeusi; likitengemaa<br />
basi hutengemaa mwili mzima, na likifisidika basi<br />
hufisidika mwili wote; (Basi haliwi pande hilo la nyama ila<br />
kua ni Moyo)”<br />
Pia amesema SAW:-<br />
“Hakika amali zote ni zenye kutegemea nia yake mtu; na<br />
nia pahala pake ni moyoni”.<br />
Na Mnyezi Mungu haangalii sura za watu wala watoto wao na<br />
mali zao, lakini Mnyezi Mungu anaangalia nyoyo za watu na matendo<br />
yao. Fikra zote za maana ambazo mtu huzihangaikia, huanza Moyoni.<br />
Mambo yote aliyoyakusanya mtu ni kutokana na Moyo. Mambo mfano<br />
wa Ilimu au Ujuzi wowote kila alichohifadhi, kila chenye kuhitaji<br />
kumbukumbu na kadhalika.<br />
25.
Bwana Mtume SAW amesema:-<br />
“Hufa Mtu Kwa Yale <strong>Al</strong>oishi Nayo, na<br />
hufufuliwa Mtu Kwa Yale <strong>Al</strong>okufa nayo”.<br />
Katika hoja hii wametokea walomili upande wa hakika ya<br />
Talqini (ile asomewayo maiti baada kwisha fukiwa) kua haina umuhimu<br />
kwake kwa sababu kama aliishi akiwa anamjua Mnyezi Mungu na Mtume<br />
wake, anaijua Dini aloridhiya Mola wake, Kibla chake, Imamu wake<br />
(yaani muongozo wake kwa maana ya (Qur an) na ndugu zake, basi<br />
hatahitaji kukumbushwa chochote.<br />
Na hali kadhalika ameishi hayajui hayo mpaka amekufa, basi hatoweza<br />
kujifunza chochote kutokana na Talqini. Anayeweza kujifunza ni yule<br />
aliye hai. Kwa upeo wa Taammul za kweli hutakosa kuona jinsi gani<br />
Moyo ulivo muhimu.<br />
Hebu na atizame na kutaammal mtu, ya vijana wadogo tu<br />
waliohifadhi Qur an yenye aya zisizopungua alfu sita mia sita na sitini na<br />
sita (6666) ndani ya nyoyo zao bila kukosea kitu!.<br />
Kwa msaada wa Moyo ndiyo tunajifunza na kuzihifadhi Ilimu na maarifa<br />
kadhaa wa kadhaa; jee hiyo si ajabu ilo kweya mipaka?.<br />
Suala linakuja, “Jee Moyo huo wenye maajabu makubwa kama<br />
hayo, ambao unamwezesha mtu kuyajibu masuala ya Munkar na<br />
Nakiir baada ya kufa – ukitokea kubakizwa Hospitali kwa<br />
uchunguzi wa sababu za kufa kwa marehemu vipi atakabil<br />
masuali ya Malaika hao. Yote aloyahifadhi moyoni mwake ndo<br />
yamebakia kwenye maabara za Hospitali vipi itakua hukmu ya<br />
maiti wake?”<br />
Hapo ndo maulamaa mfano wa kina Imam Ghazzali walipoenda<br />
kite zaidi na zaidi hadi kufikia kuona kua moyo ulokusudiwa hapo ni ule<br />
wa Nuru ambao pengine ndo mtu mwenyewe, na ambao ndani yake<br />
ndo Mnyezi Mungu ameiweka Akili. Sio Moyo ambao wengi wetu ndo<br />
kwa mazowea tunaojua, ukiwa na kazi ya kuendesha damu ukisaidiwa na<br />
mapafu!.<br />
26.
Amma ilaaka kati yake na Moyo uloachwa Hospitalini ni yenye<br />
kujulikana na Mnyezi Mungu peke yake, kwani Moyo wa<br />
Hospitali unaweza ukaoza kwa vile asili yake ni udongo uliodhihiri<br />
kama nyama. Lakini moyo wa Nuru ni wa swifa za juu ambao<br />
umekusudiwa maisha ya milele na si wenye Kufa hata siku moja.<br />
Ajabu kubwa jinsi unavyoshirikiana na Akili na Ubongo katika matenda<br />
kazi zake ndani ya maisha yetu ya kila siku!!.<br />
Mambo kama haya ndo anotakiwa mtu, na hasa vijana<br />
wajishughulishe nayo ili kujiandaa kupokea matukufu toka kwa Mnyezi<br />
Mungu, alotukuka.<br />
Vijana ndo wenye nafasi nzuri ya kukaribishwa chini ya kivuli cha<br />
Mnyezi Mungu siku ambayo hapatakuwepo kivuli illa hicho ikiwa<br />
watapondokea katika kumtii Mnyezi Mungu tu peke yake wakaacha balaa<br />
na ghasia chungu nzima zilizowazingira maishani mwao.<br />
Inshallah baada ya kujua moyo huo wenye asrari zisoidadi,<br />
huenda mambo yetu yakawa na mwelekeo wa mabadiliko mazuri.<br />
Wafaqanal Lahu lima yuhibbu wa yardha.<br />
27.
Makamu za Nafsi.<br />
No<br />
Nafsi Sifa Nyuradi<br />
1.<br />
2.<br />
3.<br />
4.<br />
5.<br />
6.<br />
7.<br />
<strong>Al</strong> Ammara.<br />
Lawwama.<br />
Mul hama.<br />
Mutmainna.<br />
Radhiyya.<br />
Mardhiyya.<br />
Kamila.<br />
Kupenda kula sana, Ubakhili,<br />
Kuhangaika,<br />
Kua na tamaa, Kuwa na<br />
kiburi (Wall yadh Billah).<br />
Matamanio, Hasada na<br />
Ghafla.<br />
Lalamikalamika, Kujilaumu<br />
laumu, Fikra, Kujizuia<br />
(Qabdh), Ujubi.<br />
Ilmu,Tawaadhui, Tawba.<br />
Subrah,Taamul - kuvumilia<br />
adha.<br />
Ukarimu,Tawakkul, Hikam,<br />
Ibaada, Shukar na Ridhaa.<br />
Zuhdi (Kuipa nyongo dunia),<br />
Ikhlas, War-l, Kuacha<br />
yasomuhusu mtu, Wafaai.<br />
Husnul khuluq – Tabia<br />
njema, Lutf kwa viumbe,<br />
Taqarrab illa Llah – Kuacha<br />
yote yasiokuwa ya<br />
M/Mungu, Tafakkur- Katika<br />
utukufu na ukubwa wake<br />
Mola.<br />
Kuridhika na alokugawia<br />
M/Mungu Sub-hana wataala.<br />
Sifa zote njema zilizotajwa<br />
katika nafsi tano, Ukiacha<br />
nafsi ya kwanza ambayo ni<br />
Ammara.<br />
La ilaha illa<br />
Llah.<br />
<strong>Al</strong>lah.<br />
Huwa.<br />
(Ismuh Dhwamir).<br />
Hayyu.<br />
Ahad<br />
A`ziz<br />
Wadud.<br />
28.
Namna au mambo muhimu katika<br />
zoezi la kuachana na mwili.<br />
Muhadhiri: <strong>Al</strong> <strong>Faqeer</strong> Ahmad Sheikh.<br />
Katika suala zima la kujigawa kuna mambo makubwa ya kuzingatia<br />
mawili: Transmission and Receiving.<br />
What we require to consider, in which way did we receive<br />
that message and then we are going to deal with it. If the<br />
transmission was spiritual: then we must act accordingly.<br />
Otherwise the message will be VOID. No spiritual message<br />
shall ever be valid in another way. Look; take this example of<br />
material in which a Human-being was created – SOIL. But we<br />
taking bath every now and then! And yet we are not dissolving -<br />
Why? – Ask your mind.<br />
Katika mambo haya saba ndio msingi wa kuachana na<br />
mwili – Separation:<br />
1. Lazima kudumu na udhu kwa masaa 24.<br />
2. Kuwa na tumbo jepesi – Mtu na aepukane na mambo ya kula<br />
kupita kiasi. Na hapa ni budi kutumia hadithi ya Bwana Mtume<br />
S.A.W pale aliposema: “Sisi hatuna haja ya Twabibu, kwa<br />
sababu hatuli mpaka tusikie njaa. Na pale tukila hatuli<br />
tukashiba”.<br />
29.
Jambo lingine la kuzingatia, ni aina ya chakula. Ni vyema<br />
kuepukana na vyakula vyote vyenye kutia nyege. (Ashki ya<br />
kufanya tendo la ndoa) na ikiwezekana ni bora mtu ajiepushe na<br />
vyakula vinavyotokana na Roho.<br />
3. Tuondoe woga kwa viumbe: Mtu na ajaribu kutoka usiku mpevu<br />
nje ya mji na alale popote bila ya kuogopa kuwa linaweza<br />
kutokea jambo dhidi yake.<br />
4. Mtu na aendelee kumtaja Mnyezi Mungu mara kwa mara. Na<br />
amkimbize Sheytwani Ibilisi kwa kutamka Kalimat Tawheed.<br />
Na pale anapoitamka Kalimat hiyo ni budi itoke ndani ya Roho.<br />
Kwa hakika ya mambo ya Kiroho hupatikana kwa kuyafanya<br />
Kiroho hayo mambo yenyewe.<br />
5. Mtu na aangalie Wakati. Hasa kati ya majira ya saa kumi na saa<br />
kumi na moja za <strong>Al</strong> fajir. Basi, atakuta kuna Wakati umesimama<br />
hauendi kama nyakati nyingine. Si vingine juu ya hakika ya<br />
jambo hilo, isipokuwa Mnyezi Mungu SWT anadhihiri katika<br />
wingu na Dunia akinadi : Je! Nani mwenye haja zake ili<br />
nimkidhie?, Nani mwenye haja ya kufutiwa Dhambi zake<br />
Nimfutie? Nani mwenye kutaka Pepo yangu Nimpatie?”.<br />
Wengi ya watu wanakuwa wamelala katika wakati huo. Basi<br />
kama wewe umefanikiwa juu ya jambo hilo ukawa hadhiri, basi<br />
nyanyuka na utarakai – Rakaa mbili za wakati huo ni bora<br />
kuliko Dunia na vilivyomo.<br />
6. Jitahidi kujiweka katika hali ya kati ya kuwa macho na kua<br />
katika Usingizi. Na ni katika hali hiyo ambapo unaweza<br />
kufungukiwa na mambo mengi – kwani ukifanikiwa jambo hilo<br />
utakuwa ukimiliki Coscious Mind na Sub–Conscious Mind. Na<br />
moja kati ya mambo yaliyo muhimu kabisa katika ku-develop ili<br />
uweze kujigawa.<br />
7. Shart lingine kubwa kabisa ni kumwogopa Mnyezi Mungu<br />
Kikweli kweli. Ndipo ambapo yeye Mnyezi Mungu atakiogopesha<br />
kila kiumbe dhidi yako. Na ndio maana ikapendelewa mtu afanye<br />
Haluwa zake nje ya mji.<br />
30.
Mahali ambapo ataweza kuziepuka sauti za watu. Jambo hili<br />
litampelekea mtu kuweza kuidhibiti barabara Nafsi yake. Na ile<br />
akili yenye nguvu Sub Conscious Mind inaingia kazini katika<br />
zile sehemu za hatari hatari. Hivyo ili kuizowesha kutumika akili<br />
hiyo budi kutingishwa tingishwa. Wengi katika watu hutumia<br />
kiasi cha 1/16. cha akili alopewa na ndio maana Bwana Mtume<br />
SAW akasema: “Watu wamelala”. Kwani sehemu kubwa ya<br />
akili zetu hatuzitumii. Hivyo na ajitahidi kila mmoja wetu<br />
kujipandisha Daraja kwa kuyafanzia kazi yale anayojua, ili angaa<br />
tuweze kutumia japo 3/16. ya akili zetu. Na papo ukifikia kutumia<br />
kiasi hicho, wengi katika watu watakupanga wewe katika kundi la<br />
wenda wazimu. Ama watakuona umechanganyikiwa (Ndio maana<br />
unasema au unatenda yasiyowezekana). Kwa kuwa maono yako<br />
yatakuwa mbali na maono ya watu wengine, na ni kweli utakuwa<br />
ukiviona vitu kwa asili yake, siyo kwa mfano ambao wengi wetu<br />
tumezoea kuona. Utakuwa unaishi katika ulimwengu wa Hakika<br />
na muda mrefu utakuwa katika jitihada za kumridhisha Mnyezi<br />
Mungu, na hapo ndipo penye kufuzu.<br />
“Hakika yetu sisi Hatukuwaumba Majini na Watu ila<br />
kwa kuniabudu Mimi. (Kunitambua mimi)”.<br />
31.
Mtungaji:<br />
(<strong>Al</strong> marhum)<br />
AL- FAQEER AL - HABIB AHMAD SHEIKH<br />
32.
Vitabu vilivyokwishatoka ni:<br />
*1. Maana halisi ya Imaan. (i) (1 st , 2nd & 3rd addition).<br />
*2. Njia nyepesi ya kuijua nafsi yako.<br />
*3. Njia nyepesi ya kujua kitu juu ya uongofu.<br />
*4. Knowledge vision & ecstacy.<br />
*5. Mwinyi Baraka katika ulimwengu wa kiislamu (i) .<br />
*6. Waislamu na Sayansi - Ulu-m.<br />
*7. Kuhifadhi Burda.<br />
*8. Maana halisi ya Imaan (ii).<br />
*9. Muhammad SAW katika ulimwengu wa ghayb.<br />
*10. Siri ya Balaa.<br />
*11. El makhlouq (Viumbe)<br />
*12. Njia nyepesi ya kujua kitu juu ya uongofu. (2nd addition)<br />
*13. Manaqib ya <strong>Al</strong> habbib Sayyeid <strong>Al</strong> Ma`aruf.<br />
*14. Some aspects of concepts of facility in medevial Islamic<br />
Philosophy by Mwinyibaraka.<br />
*15. Njia nyepesi ya kuijua Nafsi yako. (2nd addition).<br />
Vitabu ambavyo tunategemea kuvitoa muda si mrefu<br />
(Insha <strong>Al</strong>lah) ni:<br />
*1. Waislamu na Sayansi - Ulu-m. (2nd addition)<br />
*2. Mwinyi Baraka katika ulimwengu wa kiislamu (ii).<br />
*3. Muhammad SAW katika ulimwengu wa Ghayb.<br />
Kwa maulizo kuhusu vitabu wasiliana nasi:<br />
Majaalis El Ulaa - El Qadiriyya Sinza,<br />
33.<br />
P.o. Box 15170,<br />
Tel: 0747 483553<br />
Tel: 0748 595958.<br />
Tel: 0744 023703.<br />
Tel: 0741 235091.<br />
Tel: 0744 299597.<br />
Dar es salaam.
<strong>Al</strong> habib <strong>Al</strong> <strong>Faqeer</strong> Ahmed Sheikh Mohamed Sheikh Msiha, amezaliwa<br />
Singida mkoa wa Dodoma, mwaka 1938. Amepata elimu ya sekula Unguja na<br />
amebahatika kupata elimu ya juu katika chuo maarufu Afrika ya Mashariki<br />
Makerere Uganda.<br />
Elimu yake ya Dini ameipata hapo hapo Unguja toka kwa Masheikh mbali mbali,<br />
baadhi yao ni:<br />
Sheikh Sleiman <strong>Al</strong>wi (Muhib Rasul) (<strong>Al</strong> Marhum).<br />
Sheikh Seyyid Mansab.<br />
Maalim Himid (<strong>Al</strong> marhum).<br />
Maalim Hemed Muhamed El Buhry.<br />
Sheikh Seyyid Qamus.<br />
Sheikh Muawwiya Ibn Abdul Rahman.<br />
Sheikh <strong>Al</strong>ly Muhamed Comorian.<br />
Sheikh Ibrahim Mzee Ahd.<br />
Sheikh Haj Mzee Ahmad Msiha.<br />
Amma Elimu ya Nafsi na Roho Amepata Ijaza yake toka kwa A`limu mkubwa<br />
Duniani <strong>Al</strong> Habib Sayyid Omar Bin Abdallah (Mwinyi Baraka).<br />
Sheikh Ahmad amewahi kufanya kazi katika jeshi la Polisi Tanzania Bara<br />
katika mikoa mbali mbali mpaka alipostahafu.<br />
Katika umri wake wote Sheikh Ahmad alijahid katika kuendeleza Uislamu<br />
kwa kusomesha na kuandika vitabu vya mada na maudhui mbali mbali katika<br />
Uislamu. Pia alianzisha Majaalis Sehemu mbali ambazo ziko mpaka leo, Mtaa wa<br />
Pemba, Sinza, Bungoni, kijito nyama, Sadani (Ilala) na Kibaha (Misugusugu)<br />
ambapo ndipo ilipo Dhwarihi yake (alipozikwa).<br />
Sheikh Ahmad ametwawafu 27. 8. 2001. ( Mwezi 7 jumadda thany 1421<br />
H.R.). Akiwa na umri wa miaka 63, vile vile alivyokuwa akiomba aishi umri ule<br />
ule alioshi kipenzi chake Bwana Mtume Muhammad SAW.<br />
Insha <strong>Al</strong>lah Mnyezi Mungu amjaze kheri na alitie Nuru kaburi lake (Amin).<br />
Khalifa: Sheikh Issa Othman,<br />
Majaalis El Ulaa El Qadiriyya, Sinza Dar es Salam.