17.02.2015 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

YALIYOMO:<br />

No.<br />

Uk.<br />

1. Yaliyomo………………………………………….……..iii.<br />

2. Dibaji……………………………………………………iv.<br />

3. Utangulizi…………………………….………..……...….vii.<br />

4. Nafsi………………………………………..………….…1.<br />

5. Roho/Nafsi…………………………………….…….……9.<br />

6. Tiba ya Nafsi Khabbith…………………………………..13.<br />

7. Akili……………………………………..……….…...…...19.<br />

8. Moyo………………………....……………..………...…...25.<br />

9. Jedwary la Nafsi…………………………………………...28.<br />

10. Jinsi ya kuachana na Mwili……………………...………...29.<br />

iii.


DIBAJI:<br />

Bismillahir Rahmanir Raheem.<br />

Baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu Mola wa ulimwengu,<br />

Mfalme wa siku ya malipo yeye peke yake ndiye anayesitahiki kuabudiwa<br />

na hakuzaa wala hakuzaliwa.<br />

Anasema Mwenyezi Mungu katika Kurani Takatifu Surat<br />

Yusuf Aya ya 53:<br />

“….Nami sitakasi Nafsi yangu, kwa hakika kila<br />

Nafsi ni yenye kuamrisha sana maovu isipokuwa<br />

ile ambayo Mola wangu ameirehemu”.<br />

Maneno haya ya katika Kurani Takatifu aliyoyaelezea kumueleza<br />

Mtume Muhammad (SAW) yanamhusu Mtume Yusuf Bin Yakuwb (AS)<br />

alipokua anajitetea kuwa hakumtaka mke wa Mfalme wa Misri.<br />

Anamhakikishia kuwa “Nafsi ni yenye kutuamrisha sana maovu”<br />

isipokuwa iliyorehemewa na yeye Mola. Na hii iliyorehemewa na Mola<br />

ndiyo Nafsi ambayo yenye muelekeo mzuri yenye kumtii Mwenyezi<br />

Mungu na kumuabudu na ndiyo inayoitwa “<strong>Al</strong> Mutmainna” aliyoitaja<br />

Mwenyezi Mungu katika Kurani Takatifu Surat <strong>Al</strong>fajr:<br />

Ewe Nafsi iliyotulia rejeya kwa Mola wako<br />

hali ya kuwa utaridhika (kwa utakayoyapata)<br />

na Mwenyezi Mungu aridhike na wewe, basi<br />

iv.


Kupigana Jihadi na Nafsi ni jukumu kubwa linalotukabili katika<br />

maisha yetu ya hapa Duniani. Mfano alivotupigia Sheikh Ahmad katika<br />

kitabu hiki Uk. 11 wa Sheikh Abdul – Kaader Jeylani (Q.A.S.A)<br />

kuwa alichukua miaka kumi na tano maporini akifanza majaribio<br />

kuishinda Nafsi yake. Na akaishinda na kuitawala barabara. Na kuitawala<br />

huko ni kufikia kilele cha ucha Mungu na akawa mmoja wa Mawalii wa<br />

Mwenyezi Mungu. Na kabla yake alikuwepo Walii nchini <strong>Al</strong>yaman jina<br />

lake Abuwmuslim <strong>Al</strong> khawalaniy aliyempinga <strong>Al</strong> aswad <strong>Al</strong> ansiy<br />

aliyekuwa akijidai Unabii na Utume wakati wa Mtume Muhammad<br />

(SAW) alikamatwa na wafuasi wa <strong>Al</strong> ansiy na wakamtiya katika shimo la<br />

moto ili aunguwe. Moto haukumuunguza wala haukumchubuwa kama<br />

ilivyotokea kwa Mtume Ibrahim (AS), hii ni karama alizozionyesha walii<br />

huyu Abuwmuslim kwa kuishinda Nafsi yake. Kwa hivyo basi na<br />

tujitahidi kuzipiga Jihadi Nafsi zetu kwa sababu ndizo<br />

zitakazotusababishiya kuingizwa ima Peponi au Motoni. Amesema<br />

Mwenyenzi Mungu katika Kurani Takatifu<br />

Surat <strong>Al</strong> – Imraan, 185 :-<br />

“Kila Nafsi itaonja mauti na bila shaka mtapewa ujira<br />

wenu kamili siku ya kiyama, na aliyewekwa mbali na moto<br />

na akaingizwa peponi, basi amefuzu, na maisha ya Dunia<br />

hii ni starehe idanganyayo”.<br />

Mwenyenzi Mungu amjaze kheri Sheikh Ahmad kwa juhudi zake<br />

za kuandika kitabu hiki kwa kuwanufaisha na kuwazindusha ndugu zake<br />

Waislamu.<br />

WAMA TAWFIYQIY ILLA BI LLAAH.<br />

AHMAD HAYDAR MWINYIMVUA,<br />

DAR ES SALAAM.<br />

vi.


Bismillahir Rahmanir Raheem.<br />

UTANGULIZI:<br />

<strong>Al</strong>-hamdulillah na si vingine bali ni ukweli usiokanushika kua<br />

Mnyezi Mungu ndiye pekee mstahiki wa kila Swifa njema na Rehma zake<br />

Mola pamoja na amani zimwendee mjumbe wake wa mwisho Bw. Mtume<br />

Muhammad (SAW ) Mwalimu mkuu mno, aliyefundisha Umma huu wa<br />

mwisho Ilimu zote tunazozijua kuanzia siku zile za jahilia mpaka leo hii<br />

ambapo huyu humfundisha huyu na kuendelea mpaka siku ya mwisho<br />

ambayo kiitikadi tunaimani kua ipo na itawadia tu bila khilafi wala<br />

khiyari.<br />

Suala lililochukua uzito katika kitabu hiki Akili ni moja<br />

miongoni mwa Mas-la mazito na lilo muhimu sana. Na mwenye akili<br />

hushughulishwa mno na yote yenye kutaalaki na Akili maana kama<br />

iwavyo vyovyote vile.<br />

Wana wa Elimu ya Viumbe vyenye Uhai (Biologists) wa kileo<br />

wanakubali kutoijua khassa Akili ni nini. Hatua moja kubwa walopiga<br />

katika suala zima la akili ni kua kwake Ubongo wa mbele ya kichwa<br />

(Cerebrium) ni kitovu cha akili. Hii imepatikana kutokana na majaribio<br />

ya muda mrefu.<br />

Wana sayansi hao wameelezea ndani ya vitabu kadhaa-wakadhaa<br />

mfano wa “The Exploring Biology” ambapo ndani yake wameelezea<br />

kua hatua moja kubwa walioifanza kutokana na majaribio kadhaa ni<br />

katika kugundua ya kua akili Mahir (ile ilo kusanya mambo matano –<br />

macho, pua, sikio, ulimi, na mikono) na hiyo ni akili (isio julikana kua<br />

kitu gani) ni vilowekwa katikati ya hiyo Cerebrium.<br />

Akili yenyewe ikiwa ni matenda kazi ya hiyo Cerebrium kama<br />

vile uhai ni matenda kazi ya nyanja muhimu za uhai (Protoplasm).<br />

Linapoulizwa suala la akili na wapi katika mwili wa mtu ambapo<br />

Mnyezi Mungu ameiweka. Wengi huona kua akili ipo kichwani, lakini<br />

Mwendawazimu pia anacho. Hakuna<br />

vii.


Mwendawazimu ambae hana kichwa lakini matendo yake siyo ya mtu<br />

mwenye akili.<br />

Akili bila shaka ni lazima tuijue amma sivyo haitokuwa rahisi<br />

kudai kua nayo. Kutokana na kujiingikiwa nayo wengi katika ndugu<br />

zangu tumeona kuwepo umuhimu mkubwa kuandika fatwa kwa njia ya<br />

kipetopeto.<br />

Hakuna shaka kabisa kua baada ya kupata hakika yake itakua<br />

tumepiga hatua kubwa kiasi ilobaki ni wewe kutafuta njia za kuiongeza.<br />

Njia zipo basi mwenye akili hataziacha bali atazitafuta kwa udi na<br />

uvumba, na usiku na mchana.<br />

Tunamuomba Mnyezi Mungu atunufaishe kwa kijitabu hiki na<br />

kutufungulia kila lenye kuhitajika katika kutujenga kua watu wenye Akili<br />

kweli.<br />

Nahisi siwezi kukwepa kuwashukuru wote ambao walioandaa<br />

darasa la kila Juma tano pale Ilala kwa Akh Fuad Batarfy, Sharif Karama,<br />

Ba <strong>Al</strong>ly Bin Mkhashshe, Seyyid Hussein<br />

El Bayti, Sheybob, Akh Said Okash, Moh’d Batarfy, Saleh Hariz, Ababili<br />

Abdallah na wengineo ambao si rahisi kuwaorodhesha majina yao hapa.<br />

Bidii yao katika kuzishughulikia nuskha hizi kuzichapisha katika<br />

Computer na kadhalika ni moja inayoonyesha wazi kua ni wenye kupenda<br />

ilmu. Na haidhaniwi kua mwenye raghba ya ilmu si mwenye akili.<br />

Mnyezi Mungu atawajaza ziada ya vile ilivyoelezwa kua ni bora kuliko<br />

wenye kupigana vita vya jihadi, na Mahujaji na wafanzao Umra.<br />

Huwatakia maghfira ( hao wapendao ilmu) Mbingu na Ardhi na<br />

bahari miti na wanyama, pia mawe, na kila chenye kuchomozewa jua juu<br />

yake, na huko akhera malipo yao anayajua Mnyezi Mungu Sub hana<br />

wa Taala.<br />

“Ishi hapa duniani ukiwa <strong>Al</strong>im au<br />

Mutaallimi (mwenye kujifunza), au<br />

Mustamian (mwenye kusikiliza ilmu)<br />

usiwe mtu wa nne utahiliki.”<br />

viii.


Hii ni kawli yake <strong>Al</strong>ayhi Afdhalus Swalatu Was Salaam, Bwana Mtume<br />

Muhammed (. S. A.W).<br />

<strong>Al</strong> <strong>Faqeer</strong> Ahmad sheikh,<br />

Majaalis El Ulaa,<br />

El Qadiriyya, Sinza<br />

Dar es salaam,<br />

Tanzania<br />

Swafar – 21<br />

9 may 2000.<br />

ix.


Nafsi na Sifa zake:<br />

<strong>Al</strong> hamdullilah, waswalaatu lilahi taala wa salaamuha ala rasulillah.<br />

(S.A.W).<br />

Amma baad, Suala la Nafsi hii ambayo tunayo ndani ya miili yetu<br />

ni kubwa na pia zito, kwa hiyo basi haitakuwa jambo la akili kulipita hivi<br />

hivi tu minighayri ya kujishughulisha na kulijua kwake.<br />

Bwana Mtume (S.A.W) amelisemea hivi:-<br />

“Man arafa nafsahu<br />

faqad arafa Rabbahu”<br />

“Mwenye kuijua nafsi yake bila<br />

shaka ameishamjua Mola wake”<br />

Sababu ya kusema hivi kumjua Mnyezi Mungu ni wajibu wake<br />

mtu wa kwanza katika uhai, na njia nyepesi ya kumjua mola ni katika mtu<br />

kuijua Nafsi yake.<br />

Kuijua Nafsi ni kujua makamu za Nafsi. Hii ina maana ya kujua<br />

manzili zake saba kwa swifa na matendo yake.<br />

Ya kwanza:<br />

Nafsi Ammaara.<br />

Ambayo Mnyezi Mungu Sub-haana wa Taalah ameisema ndani<br />

ya Qur an kama:- S:12:53<br />

1.


“Mimi sijitakasi nafsi yangu, kwa hakika (kila)<br />

nafsi ni yenye kuamrisha sana maovu, isipokuwa<br />

ile ambayo Mola wangu ameirehemu. Hakika Mola<br />

wangu ni mwingi wa kusamehe (na) mwingi<br />

wa kurehemu”<br />

Hii ndiyo nafsi ovu na khabbithi kupita zote, kwa mujibu wa kauli yake<br />

<strong>Al</strong>ayhis-swalaatu Llahi Taala waa-lihi.! “Nafsi hii ni khabbithi zaidi<br />

kuliko mashetwani sabini”<br />

Inakutosha kuangalia zile sifa zake, ili kuthibitisha kauli yake<br />

bwana Mtume S.A.W wewe mwenyewe uelewe ya kwamba kila<br />

unapojishughulisha na kuifuatilia kwa karibu zaidi ndiyo jihadi kubwa<br />

kwako na kukuingizia thawabu nyingi ndani yake.<br />

Sifa za Nafsi Ammaarah<br />

Kupenda kula sana<br />

Ubakhili<br />

Kuhangaika<br />

Kua na tamaa<br />

Kuwa na kiburi (Wall yadh Billah)<br />

Matamanio<br />

Hasada na<br />

Ghafla<br />

Sifa zote hizi ni zenye kumpeleka mtu kwenye kuhiliki kwa adilla<br />

na ushahidi madhubuti toka kwa Bwana Mtume <strong>Al</strong>ayhi<br />

swala waatul-Lahi wa salaamuhu.<br />

Ya pili: Nafsi Lawwaama.<br />

Hii ni Nafsi inayojilaumu laumu, Seyyid Umar Bin Abdallah Bin<br />

<strong>Al</strong>-ba-shaikh Abiibakar Bin Salum ( Mwinyi- Baraka) akisema :- “Haina<br />

njia nyingine, ni kujilaumu”<br />

Lakini Mnyezi Mungu ameisemea vizuri. Ameiapia:- 75:1-2<br />

2.


“Naapa kwa siku ya kiyama tena naapa kwa nafsi<br />

inayojilaumu. (Kuwa imefufuliwa na mtalipwa)”<br />

Sifa za Nafsi Lawwaama:<br />

Kujilaumu laumu.<br />

Fikra.<br />

Kujizuia (Qabdh).<br />

Ujubi<br />

Lalamika lalamika<br />

Asili ya kuwa na sifa hizo ni kwamba ni kutaka kujiondosha<br />

kabisa katika Nafsi Ammaara kwa vitendo vyake vyenye kwenda<br />

kinyume na maamrisho ya Mnyezi Mungu.<br />

Nafsi Mul-hama.<br />

Ya tatu:<br />

Nafsi zote takribani zimetajwa hakika zake mwenye Qur an. Hii<br />

imetajwa ndani ya:- Suratish-shams. 91:7-8-9-10.<br />

“Na kwa nafsi (roho na aliyeitengeneza kisha<br />

akaifahamisha uovu wake na wema wake. Bila<br />

shaka amefaulu aliyeitakasa ( Nafsi yake) na<br />

bila shaka amejihasiri alieiviza (Nafsi yake)”.<br />

3.


Sifa za Nafsi Mul-hama.<br />

Ilmu.<br />

Tawaadhui.<br />

Tawba.<br />

Subrah.<br />

Tahaamul - kuvumilia adha.<br />

Kiakili tu ukizilinganisha swifa hizo na zile za nafsi ya kwanza<br />

utaona ipo tofauti kubwa mno ndani yake. Ndani ya nafsi hizi unaona<br />

wazi kuwepo Uislamu ndani yake, kama unavyoweza kuona kuwepo<br />

ukafiri ndani ya nafsi ya kwanza. Hiyo ni hatua<br />

kubwa katika kujijua. Ni hatua kunjufu katika jihad ya nafsi<br />

ambayo Bwana Mtume (S.A.W) ameihimizia.<br />

Nafsi Mutmainna.<br />

Ya nne:<br />

Hii ndiyo Nafsi pekee ya kwanza iliyotulizana kabbisa, haina vituko<br />

ndani yake, na, “Iliyosemezwa na Mnyezi Mungu Khasa”. Qur an<br />

89:27.<br />

“Ewe Nafsi yenye kutua.”<br />

Huko ni kunadiwa na Mnyezi Mungu mwenyewe lakini bila shaka<br />

ukiweka mazingatio ya kweli utaona kuwa ni miujiza mikubwa imo<br />

mwenye mnada huu kwa wenye akili.<br />

4.


Sifa za Nafsi Mutmainna:<br />

Ukarimu.<br />

Tawakkul.<br />

Hikam.<br />

Ibaada<br />

Shukar na Ridhaa.<br />

Hizo ni miongoni mwa sifa nzuri mno ambapo mtu anakua nazo<br />

ndani ya Uhai wake hapa duniani. Mawalii wote bila shaka ni wakarimu<br />

kwa hiyo kila anaye tamassak na sifa hii basi ametammasak na sifa ya<br />

Mnyezi Mungu. Nasi tumeusiwa na Bwana Mtume S.A.W. tujitabiishe na<br />

sifa nzuri nzuri za Mnyezi Mungu. Amma katika kushukuru kuna Uislam<br />

mzima ndani yake.<br />

Nafsi Radhiya.<br />

Ya tano:<br />

Nafsi hii imetajwa mara tu baada ya Mutmainna ndani ya Suratil Fajar<br />

katika juzuu ya “Amma.” Nafsi iliyo ridhiya.<br />

Sifa za Nafsi Radhiya:<br />

Zuhdi (Kuipa nyongo dunia).<br />

Ikhlas.<br />

Wara`a.<br />

Kuacha yasomuhusu mtu.<br />

Wafaa`i – Kutekeleza.<br />

Miungoni mwa sifa njema ambazo zimeibeba Nafsi hii hamna kama<br />

Ikhlas ambayo Shaytwani anaikhofu mno. Qur an imesema hivyo siyo<br />

mwandishi. Pia katika msururu wa utajo wa Nafsi tatu hizo, hii ndiyo<br />

yenye kukamilisha yaani:-<br />

5.


Nafsi Mardhiyya.<br />

ya sita:<br />

Nafsi hii imetajwa mara tu baada ya Nafsi Radhiya yaani ilo ridhiwa<br />

na Mola Sub-hana wa Taalah. Amma mtu akisha ridhiwa na Mnyezi<br />

Mungu basi hua hana haja ya kuogopa chochote tena.<br />

Sifa zake:<br />

Husnul khuluq – Tabia njema<br />

Lutf kwa viumbe.<br />

Taqarrab ila Llah – Kuacha yote yasiokuwa ya Mnyezi Mungu.<br />

Tafakkur - Katika utukufu na ukubwa wake Mola.<br />

Kuridhika na alokugawia Mnyezi Mungu Sub-hana wataala.<br />

Nafsi hiyo inatakiwa kurudi kwa Mola wake Radhiyya.<br />

Hali ya kuwa Mardhiyya hivyo basi, inatakiwa iingie katika kundi la waja<br />

wake Mnyezi Mungu.<br />

Waja wote ni wa Mnyezi Mungu lakini wapo ambao ni speshel.<br />

Amma katika walioukubali uja hakuna kama Bwana Mtume <strong>Al</strong>ayhi<br />

Afdhalu Swalaat Was-salaam.<br />

Mtume Muhammad S.A.W Ni mja wake na mjumbe wake. Mitume<br />

wengine wote wanamfwatia Nabii Muhammad .S. A W. kama Sayyidna<br />

Issa AS. ametajwa pia kama Abduhu warasuluhu lakini wamepitana<br />

kwa daraja na fadhila. Na pamoja na hayo yote pia Mtume SAW anasema<br />

ya kuwa…..“Hajifakharishi- Katika kuwa kwake Bwana wa watoto<br />

wote wa (Nabii Adam A.S.W).”<br />

Nafsi Kaamila.<br />

Ya saba:<br />

Pengine huitwa Nafsi Swafiyya, yaani iliyokuwa safi<br />

6.


kabisa. Kwa nini? Kwa kuwa sifa nzuri nzuri zote zimo ndani yake.<br />

Sifa zake:<br />

Sifa zote njema zilizotajwa katika Nafsi tano ukiacha Nafsi ya<br />

kwanza ambayo ni Ammara.<br />

Bwana Mtume S.A.W amesema:- “Kupigana na Nafsi ndiyo jihadi<br />

kubwa”<br />

Hakuna juu yake Jihadi nyingine yaani ile Jihadi ya Panga ambayo<br />

humfanya anayekufa ndani yake kuhisabiwa kuwa “yuko hai” haifui dafu<br />

kabisa hapa.<br />

Nafsi na makamu zake:<br />

Mpaka kufikia hapa bila shaka umeishaipatapata kiasi ambacho<br />

hakukupi shaka ndani ya moyo wako. Nini wamesema Maulamaa<br />

wakubwa wakubwa katika Uislam?.<br />

Wachache tu mfano wa akina Ghazzal, Busri na labda Habibi<br />

Ahmed Bin Abubakkar Bin Sumeit aliyekuwa Zanzibar katika karne ya<br />

kumi na nane mwishoni na kumi na tisa.<br />

Imam Ghazzal ameelezea vizuri sana mas-ala ya Nafsi, Roho na<br />

akili ndani ya vitabu vyake vya “Ihyaa ulumud deen”.<br />

Imam Busri ameelezea vizuri ndani ya “Burda” kitabu mashuhuri<br />

ambacho Waislamu wengi wanakijua na kukifanzia kazi katika matukio<br />

kadhaa wa kadhaa ndani ya uhai wa kila leo, katika Tawassul za kila<br />

siku. Yeye amesema kuwa:-<br />

“Nafsi ni kama mtoto mchanga ukimwacha<br />

atapondekea kunyonya na ukimzuia ataacha”.<br />

Nafsi haina cha ujana haina cha uzee, ikimshika mtu hua hasikii<br />

kitu katika waadhi wala nasaha. Tazama katika kuiachia kula sana kama<br />

Punda inavokutia uvivu na kadhalika.<br />

7.


Amma Habib Ahmed ndani ya Kitabu chake. “ kawkabur zaahir”,<br />

anasema.:- “ Nafsi ni kama smaku”. Chunguza smaku utaona inayo<br />

pande mbili. Upande wa kuvutia, upande wa kufukuzia. Ule wa kwanza<br />

ndiyo wenye kukufanza ukamili katika maovu na ule wakuzuia ndiyo<br />

unaokukataza kufanya maovu.<br />

Qur an 79.40-41<br />

“ Na amma yule anechelea kusimamishwa mbele ya<br />

Mola wake akaizuia nafsi yake na matamanio<br />

basi pepo ndio mashukio yake”<br />

Suala la kujizuia ni muhimu mno na ni Jihadi ya kila mmoja, kwa<br />

hiyo siyo mambo ya Sheytwani bali “Wewe binafsi yako”.<br />

Na kila unapoanza amali njema inakuwa inatakata sehemu kwa sehemu<br />

mpaka inang’aa kama Nuru, na hapo ndipo unapohesabika kua mtu<br />

kamili. Amma sivyo, basi wewe ni kama wanyama wengine wowote<br />

(mammals).<br />

Mnyezi Mungu atuwafikishe katika kheri.<br />

8.


ROHO/NAFSI<br />

Qur an: 17:85.<br />

“Na wanakuuliza habari ya roho. Sema, roho ni jambo<br />

lililohusika na Mola wangu (Mnyezi Mungu) nanyi<br />

hamkupewa katika ilmu (Ujuzi) ila kidogo kabisa”.<br />

Ushahidi wa aya hii ni wenye kuonyesha wazi wazi kua upo ujuzi<br />

wa Roho. Na pamoja na kua kidogo au kiduchu tu. Ndiyo makadirio<br />

ambayo Mnyezi Mungu ameonelea kua ni yenye kutosha kabisa kwa hapa<br />

duniani.<br />

Katika misemo yetu ya Kiswahili ni ule msemo:- “Maji ya kifuu ni<br />

Bahari ya chungu” (yaani yule mdudu mdogo na mwepesi sana – mdudu<br />

wa sukari pengine mdudu chungu).<br />

Huo ni mfano mmoja tosha kwa mtu mwenye akili ya kujisaidia nayo<br />

angalau kidogo tu; ni wazi kuwa hatahitaji maelezo marefu ya aina<br />

yoyote.<br />

Tukiangalia kwa mazingatio kauli ya Bw. Mtume S.A.W juu ya<br />

Rehma za Mnyezi Mungu tunaelewa fika kua ni “moja kwa mia moja”<br />

kwa jumla tangu dunia ianze mpaka kufikia kiyama. Bila shaka moja kwa<br />

mia ni sehemu ndogo mno, na hapo mpaka leo hii karne ya Ishirini na<br />

moja mwaka huu wa Elfu mbili watu bado wangali wanarehemeana bado.<br />

Na hasa ukiongezeka usemi wake kua:<br />

“Warehemuni walioko ardhini atakurehemuni<br />

aliyeko mbinguni”.<br />

9.


Basi kidogo hiyo ni yenye kutosha kabisa. Pengine ingekuwa ni<br />

Rehma mbili katika zile mia ndo ziloshushwa ungesema watu<br />

wangeshindwa kufanza mambo mengine yoyote bali wangekuwa<br />

wanarehemeana tu. Wapo watu wengine wanafikia kuikanusha kisirisiri<br />

au kipumbavu kiuchache wa ilmu. Aya hiyo: 17:85 wao wakidai kua<br />

hamna anaejua mambo ya roho illa Mnyezi Mungu .<br />

Mnyezi Mungu anaijua mno hiyo Roho; anasema kua ametupa ujuzi<br />

nayo lakini ni kuduchu. Si busara kuchukua kidogo ya Mnyezi Mungu<br />

ukaifanza kua ndo hiyo hiyo kwako wewe Mwanadamu, na huku ukidai<br />

kuamini kua: –<br />

“Hana anayefanana naye hata mmoja”.<br />

Kuna hatari ya kufikia kujichukua wewe kama <strong>Al</strong>im-Sameeun<br />

(Unaesikia ) Basweerun (Unaeona) na kadhalika, kua ndo hiyo hiyo ya<br />

Mnyezi Mungu (Mnyezi Mungu apishilie mbali fikra kama hizo kwetu).<br />

Mnyezi Mungu anamuona na kumsikia sisimizi michang’ato yake<br />

chini ya ardhi ndani ya giza la usiku, Je Shekhe, wewe wasikia hivo hivo?<br />

Mnyezi Mungu anayajua ya siri na yalofichika ndani ya siri katika vifua<br />

vya watu. Jee na wewe Sheikh ni hivo hivo? Basi Staghfiru kwa Mola<br />

wako na ukithirishe Kalima ya Tawheedi usije ukahiliki kwa kujifanya<br />

kichwa Mchungu. Uislamu unataka unyenyekevu (Sub-Mission).<br />

Na isisahaulike kua Bwana Mtume SAW amekataza malumbano na<br />

kwamba mwenye kuacha kulumbana (kubishana na hali ya kua yeye ndio<br />

mwenye haki basi (malipo yake) siku ya kiama Mnyezi Mungu<br />

atamjengea Nyumba ya Dhahabu). Na ikiwa kwa waliopewa Chuo (Ahlil-<br />

Kitab) Basi malumbano yawe “Bil-lati Hiya Ahsan” kwa njia ya wema<br />

sana. Kwa nini?; kwa sababu ni mara chache tunakumbuka kua mtu<br />

anapopinga jambo hua na maana ya kufru. Kwa hiyo basi huenda mtu<br />

akawa na Sijda yake usoni lakini ni Kafiri.<br />

10.


Lau kabla ya kubishia jambo ambalo amelisema ambae hana ushuhura<br />

katika Jamii, tungezingatia katika kawli aizungumziayo kua ni yake au ya<br />

Mnyezi Mungu ingekuwa rahisi kuyahukumu mambo kwa njia ya Amani<br />

na busara ya hali ya juu ambayo haingemgandamiza mtu. Ilmu iwe ya<br />

manufaa siyo ya fadhuli.<br />

<strong>Al</strong> Habib Seyyid Umar akisema:- “Suala la Nafsi / Roho si la<br />

kusemea kidogo tu kisha ukaliacha, utapoteza watu”. Yeye<br />

mwenyewe ilimchukua masaa matatu kuelezea juu ya Nafsi alipotoka<br />

Makerere University Uganda ambako alikua na kina Nyerere, Obote,<br />

Yusufu Lule na wengine kadhaa aliowataja ambao baadae walishika<br />

nyadhifa kubwa kubwa katika Serikali za Afrika Mashariki.<br />

Sheikh Abdul-Qa dir Jeylani (Q.A.S.A) alichukua miaka kumi na<br />

tano maporini akifanza majaribio ya kuishinda Nafsi na hatimae<br />

akaishinda na kuitawala barabara. Na miungoni mwa natija ni ile ya<br />

kufunguliwa mambo mengi makubwa makubwa yalojaa karama, yote<br />

hayo hayajaja kwa upendeleo bali Mujaahada.<br />

Na katika mda wote huo alikua akifunga kila siku - labda siku moja<br />

tu alifungua kwa sababu ya maskini mmoja alietaka kumuombea mtu Dua<br />

lakini kwa sharti ale nae pamoja, Basi alifungulia kwa ajili hiyo -<br />

Chambulecho <strong>Al</strong> Habib:-<br />

“Nini Swaumu ya miaka kumi na<br />

tano kwa Dua ya masikini huyu”.<br />

Nafsil Ammaara haina inapopata taabu kama katika Swaumu. Basi<br />

kwa apendae kupata Sa’ada ya Nafsi yake na aanze na tabiya hii ya<br />

kufunga funga.<br />

Swaumu za Twaa (Tatwa-w-u’e) kama vile Jumatatu na <strong>Al</strong>-Khamisi<br />

na siku za mwezi kumi na tatu kumi na nne na kumi na tano za kila<br />

mwezi. Huenda ukahisabiwa kama aliyefunga Dahar nzima. Kumbuka<br />

kauli ya <strong>Al</strong> - Mustwafa S.A.W:-……<br />

“Mwenye kufunga Ramadhani akafatanisha na Sittatish-<br />

Shawwaal (Siku sita za Shawwal) hua kama aliyefunga Dahar….”<br />

Sababu ni Basweet kwa kuchukua malipo ya kila jambo jema<br />

11.


Thawabu 10; Jumla ya siku thelathini na sita kwa Thawabu kumi<br />

inafanza siku za mwaka mzima (Dahar) yaani siku mia tatu na sitini, na<br />

hali kadhalika funga ya Ayyamul-Beydh 13, 14 na 15 ya kila mwezi kwa<br />

miezi kumi na mbili ya mwaka mzima inafanza siku 36 zenye Thawabu<br />

kila moja inakuja ile ile mia tatu na Sitini ambazo ndo Dahar. (Tazama<br />

Hikma ilivyo ajabu kiasi gani ndani yake).<br />

Amma katika Khatwir (mapenzi ya jambo lenye kuvutia moyoni)<br />

yake Bw. Mtume SAW <strong>Al</strong>ivutiwa mno na Swaumu ya Nabii Daudi<br />

Babake Nabiy-<strong>Al</strong>lah Suleiman A.S - ambae alikuwa akifunga siku moja<br />

na kula siku moja.<br />

Majaribio hayo yote hassa si vingine Illa ni yenye makusudio ya<br />

kumtengeneza mtu ili awe mwema na mwenye Swifa za kuwa<br />

Mtawala alokusudiwa na Mola Subhana wa Taala hapa Duniani (The<br />

divine’s viceregent).<br />

Njia nyepesi mno katika kushinda Nafsi hii ilokwisha<br />

kukudhihirikia ukhabith wake mda mrefu sasa tangu ubaleghe hadi hii leo<br />

hakuna kama kwenda kinyume ya swifa zake ambazo tayari<br />

umeishazifahamu .<br />

Maswahaba zake Bwana Mtume SAW, Radhya-<strong>Al</strong>lah Anhum<br />

wakifanza majaribio katika kila jambo lililohitaji muamalla zama za<br />

kuteremshwa wahyi toka kwa Mola wa ulimwengu zote.<br />

Tukumbuke la maana angalau moja katika natija na faida nzuri katika<br />

majaribio (Experimantations) nalo ni kuongezeka akili.<br />

Sasa hebu na tuangalie katika ya kuhitaji kuyafanzia kazi leo kabla kesho<br />

kuhusu hii Nafsi khabith.<br />

12.


Jinsi ya kuitibu Nafsi khabbith.<br />

Kupenda kula sana: Basi dhidi yake ni kufunga – Swawmu. Bw.<br />

Mtume SAW alisema:-<br />

“Sisi ni wale ambao hawali mpaka wawe na<br />

njaa na pindi tulapo basi hatushibi huondosha<br />

mkono hali ya kuwa hatukushiba na hatuna njaa”.<br />

Mfalme mmoja aliita matabibu ili wampe dawa ya kuondosha maradhi<br />

yote. Wakamwendea mabingwa katika fani ya Twiba toka Arabuni , India<br />

na Afrika (Sudan) Mwarabu alimwambia kuwa ni Habba Soda. Muhindi<br />

alimwambia kua ni maji ya moto Asubuhi kabla ya Stiftahi na usiku<br />

wakati wa kulala. Pakapita kimya kiasi ambacho kilimpelekea amuulize<br />

Twabib Mwafrika vipi mbona uko kimya au umeshindwa? Bwana<br />

Mwafrika akasema:- “Bwana Mfalme, ni kweli Habba Soda imesemewa<br />

na Bwana Mtume SAW kua inatibu maradhi yote ila mauti, na lau na<br />

mauti yangekuwa na dawa, basi Mnyezi Mungu angeweka mwenye<br />

Habba Soda. Amma kwa maji ya moto tumbo hulainika na mafuta<br />

mwilini huyeyuka hivo basi, mtu upunguza unene. Lakini dawa ya<br />

maradhi yote hakuna kama kula wakati mtu una njaa, na kuondosha<br />

mkono kabla hujashiba (na kuvimbiwa), njia hii huwa ni kinga kabla<br />

kujitibu.”<br />

(Preventetion is Better than Cure).<br />

Mfalme akasema kuaTwabib Mwafrika ameswibu na kuhibu yaani<br />

ndiye aliyepata.<br />

Ubakhili: Kinyume chake ni ukarimu – Sukhaa.<br />

Bakhili ni Aduwwal-Llah hata kama ni mchaji mtaabbadi<br />

Mkubwa, na karimu ni kipenzi cha Mnyezi Mungu hata kama<br />

ni faasik.<br />

Kuhangaika: Dhidi yake ni utulivu ambao unaandamana na Nafsi<br />

Mutmainna.<br />

13.


Kua na tamaa: Zingatia ule usemi “Tamaa mbele mauti nyuma”.<br />

Kinyume chake ni kinaa na kule kukinai ni utajiri mkubwa, anasema<br />

Mtume wa Mnyezi Mungu.<br />

Kuwa na kiburi: (Mola atuepushe nacho) Dhiddi ni kujitupa chini<br />

kua Mnyenyekevu.<br />

Hata ikibidi kufanza aina ya shughuli ambazo lau atakuona yeyote<br />

yule basi hatakosa kupata hisia kama za kudharauliwa. Hiyo ina kheyri<br />

zaidi kuliko kutukuzwa ukapata kiburi.<br />

Matamanio: Lau huanguka kwa kufunga Swawmu tu. Lakini ziada<br />

ni katika kuyakumbuka mno Mauti. Bwana Mtume SAW alieleza<br />

kua katika kuyakumbuka mauti imma itamfanza mtu apungunze<br />

maasi au atazidisha Ibada.<br />

Mfano utabiri wa Pope mwaka 1959 kua 1960 ingekua mwisho<br />

wa Dunia, wa Moshi Kilimanjaro walibakia Makanisani kuanzia Krismas<br />

mpaka January, ni wenye kutosha kuthibitisha ukweli wa kuyakumbuka<br />

mauti ni waadhi kamili, na ambae hawaidhiki kwa mauti, basi huyo hana<br />

waadhi.<br />

Hasad: Amma kuhusu Hasad ambayo Bw. Mtume SAW amesema:<br />

“Ni ugonjwa usio na Dawa”. Illa kuacha tu kule kuhusudu, mtu wa<br />

akili anatakiwa kuyazingatia sana maanani huenda akanusurika.<br />

Maisha ya hapa Duniani yamejaa majaribu, kwa hiyo mtu mwenye<br />

akili nae anatakiwa afanze majaribio kwa kila jema alolijua. Akili haina<br />

njia ya kuzidi kama katika mtu kua na ungi wa Tajiriba (Frequent<br />

Experimentation Culculation and So on and so Forth) katika<br />

majaribu makubwa tulonayo hasa katika zama zetu hizi hakuna kama<br />

“Wanawake”. Bwana Mtume SAW akisema :-<br />

14.


“Sijakuachieni baada yangu fitna ashaddu<br />

kuliko wanawake”<br />

Tuondoshe au tupunguze habari za: “Aa!! Sikataka mwenyewe!” <strong>Al</strong>-<br />

Habib (Mwinyi Baraka) akisema :- “Itafaa wapi si kataka<br />

mwenyewe“. Ni nzuri mtu kua mwema hasa anapokua kijana aliyejaa<br />

Ghururi ambazo daima humzunguka kweli kweli. Wakati wa ujana ndo<br />

aghlabu huvutiwa na mambo ya ajabu ajabu ya maisha ya ghururi.<br />

“Haingii peponi ambae ndani ya moyo<br />

wake ana punje ndogo ya kiburi.<br />

Kadhalika Ubakhili umuaduisha (humfanza awe adui wa Mnyezi<br />

Mungu ) Na pia adui wa Nafsi yake yeye mwenyewe. Na vipi mtu huyo<br />

kua rafiki ya mwingine? Amma ni kweli kua:<br />

“Sakhii alie Faasik ni Mahbub mbele za Mnyezi<br />

Mungu, kuliko Bakhili mchaji Mungu”.<br />

Juwa ewe mtafuta matukufu kwa Mnyezi Mungu Mtukufu ya kua<br />

Mnyezi Mungu anapotaka kufanza mmoja ya waja wake kua Walii<br />

(Rafiki) Basi, humpamba kwa sifa hiyo ya ukarimu na tabiya njema.<br />

Tumeishaona jumla ya sifa njema katika Nafsi sita, sifa ambazo ni<br />

zenye kumtosha mtu kujipamba nazo ili afanikishe katika kua mja wa<br />

Mnyezi Mungu wa kweli kweli.<br />

Na mtu anapofikia kua kipenzi cha Mnyezi Mungu basi hua hana<br />

hofu juu yake na kila siku hua ni mtu wa mafanikio mazuri. Kila<br />

analolitaka Mnyezi Mungu atampa thamma atampa. Hivyo ndivyo<br />

asemavyo yeye mwenyewe Sub-Hana wa Taala katika hadithi takatifu<br />

(Hadithil- Qudsi)<br />

Kila unaemsikia kua ni walii basi kafikia Daraja hiyo kwa<br />

maagizo hayo yaliyomo mwenye Hadithil-Quds, na kwa kumpenda mno<br />

Bw. Mtume Muhammad <strong>Al</strong>ayhi Swalawatullah Wa Salamuhu. Nasi<br />

Inshaallahu Taala tupate Tawfiqi ya kweli ndani ya kupigana jihadi<br />

kubwa hii dhiddi ya Nafsi vile alivyotuusia Bwana wa Mabwana, Bwana<br />

wa Watoto wote wa Sayyidna<br />

15.


Adam . ASW. Bwana Mtume S.A.W. amesema:<br />

“Lau ningechaguzwa juu ya Utume ninataka kitu<br />

gani nisingechangua isio kua tabiya njema kwani<br />

kila cha ziada (Fadhila) ni chenye kuondoka na<br />

kwisha, isipokuwa sifa njema; Kwani hizo hubaki<br />

na wewe (milele)”.<br />

Ni nani baada ya Mnyezi Mungu na Mtume wake mkweli wa<br />

mambo kuhusu yote yamuhusuyo mtu hapa Duniani? Swifa nzuri na tabia<br />

njema ndo zimfanzazo mtu kuonekanwa mtu amma sivyo, mtu hua ni<br />

mnyama tu (Mammals-Biologists wanasema).<br />

Na pengine mtu huzidiwa na Wanyama kibaadhi ya sifa. Matendo<br />

yote ayafanzayo mtu pia Mnyama huyafanza pamoja na kutokuwa na<br />

akili. Lakini wakati asiyekuwa na akili anamsabihi Mola muumba na<br />

kuswali swala ambayo Mnyezi Mungu na huyo Mnyama anaijua, basi<br />

mwenye akili mtu hua chini ya Mnyama. Na hivyo ndivyo ilivyosimuliwa<br />

mwenye:<br />

Qur- An- 7:179.<br />

“ Na bila shaka tumewaumbia Moto wa Jahan-nam<br />

Wengi katika Majini na wanadamu (kwa sababu<br />

hii) Nyoyo wanazo lakini hawafahamu kwazo<br />

(hawataki kufahamu kwazo) na macho wanayo<br />

lakini hawaoni kwayo na masikio wanayo, lakini<br />

hawasikii kwayo. Hao ni kama Wanyama, bali wao<br />

ni wapotofu ( Wapotevu) zaidi – hao ndio<br />

walioghafilika”.<br />

16.


Suala la pepo na Moto si suala la mtu kujipangia, amma sivyo hangeingia<br />

yeyote Motoni. Lakini suala la kufananishwa mtu ambaye Mnyezi Mungu<br />

amemtukuza kupita viumbe vyote hapa Duniani aje kufananishwa na<br />

Mnyama asiye na akili na papo awe mpotevu zaidi, hilo ni tusi zito sana.<br />

Mambo ya kweli kama haya inataka mtu aweze kuyazingatia na<br />

kuazimia azma ya kweli kujibadilisha kwa kadri ya uwezo wake pamoja<br />

na kumuomba Mnyezi Mungu amuongoze kwa Rehma zake.<br />

Mnyezi Mungu anajua sana jinsi uzito wa Mitihani yake ulivyo kwa<br />

mtu katika mapambano yake na Nafsi yake, Matamanio, Dunia na<br />

Sheytwani, Basi, hakuna haja ya kukata tamaa na Rehma zake Sub-Hana<br />

Wataala.<br />

Tazama vile Mnyezi Mungu atuambiavyo katika: Qur an 39:53<br />

“Sema, “Enyi waja wangu mliojidhulumu Nafsi<br />

zenu, msikate tamaa na Rehema ya Mwenyezi<br />

Mungu bila shaka Mwenyezi Mungu husamehe<br />

Dhambi zote. Hakika yeye ni mwingi wa kusamehe<br />

(na) mwingi wa kurehemu”.<br />

<strong>Al</strong> –Habib (Mwinyi Baraka), Akisema: “Hakuna dhambi<br />

inayomshinda kuisamehe ila Shirk”. Kawli hii ukiitia maanani<br />

unapata matumaini ya moyo kua Mnyezi Mungu ni mzuri mwenye<br />

huruma mno kuliko Mama kwa kichanga chake.<br />

Tusisahau pia vile alivyotuusia Bwana Mtume S.A.W. katika<br />

maneno yaliyojaa hikma ndani yake kua:<br />

“Mtu ni hadithi (Mazungumzo tu) baada yake,<br />

basi (Tu) jitengenezee hadith nzuri kwa<br />

watakaokuja kusimulia (Baadae)”<br />

17.


Tena na tena na tumuombe Mnyezi Mungu atupe Tawfiqi na mioyo yenye<br />

nguvu katika kuishinda mitihani yake kwa wingi wa Subra na shukurani<br />

kwa Jaha ya Bwana Mtume Muhammad Swallallahu Taala <strong>Al</strong>ayhi wa<br />

<strong>Al</strong>ihit-wahiraati-Ummahaatil Muslimiina. DUNIANI. (Amin).<br />

18.


AKILI:<br />

Ni Nuru ya kung’aza, Mnyezi Mungu ameiweka ndani ya Moyo<br />

wa mtu na daima hunga’ara kwenye ubongo ambao uko kichwani katika<br />

mtu.<br />

Mfano wa karibu kabisa ambao mtu wa kawaida anaweza<br />

akaipata-pata kirahisi ni ule wa Projector na Screen katika kufanza<br />

kazi pamoja, bila ya ushirikiano si rahisi. Ndo kusema tumuonapo mtu<br />

kaharibikiwa basi huwa hiyo Johari ya akili ndo iliyoathirika kwa hiyo<br />

huo ubongo wenye Awnsi kumi na sita hua haufanzi kazi kabisa.<br />

Bw.Mtume SAW amesema:-<br />

“Usimlilie aliyekufa mlilie ambae amepungukiwa<br />

na akili yake”.<br />

Chombo pekee kilo Azizi kwa mtu hakuna kama Akili, na hiyo<br />

ndiyo yenye kutafautisha baina ya mtu na Mnyama.<br />

Ukifungua Qur an utaona sehemu nyingi imetajwa Akili. Na ni<br />

kutokana na matendo gani hasa ndo mazingatio ya dhati<br />

yanapochukuliwa. Aya ifwatayo ina mengi ya kuzingatia<br />

Qur an 2:164:-<br />

19.


“Hakika katika kuumbwa kwa mbingu na ardhi,<br />

na katika kuandamizana usiku na mchana na katika<br />

(mwendo wa) vyombo ambavyo hupita katika bahari<br />

kwa (kuchukua vitu) vifaavyo watu, na (katika<br />

kumiminika ) maji aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu<br />

kutoka Mawinguni na kwa (Maji) hayo akaihuisha ardhi<br />

baada ya kufa kwake Na akaeneza humo (Ulimwenguni<br />

kwa ajili ya maji hayo) kila aina ya Wanyama, na katika<br />

mabadiliko ya upepo na mawingu yanayoamrishwa<br />

kupita baina ya mbingu na ardhi, Bila ya shaka<br />

(Katika haya) zimo Ishara kwa watu wenye akili<br />

(kuwa yuko Mwenyezi Mungu na ni mmoja).<br />

Na kweli ikiwa tofauti ya pekee kubwa kati ya mtu na Mnyama ni<br />

akili ni wazi kua Mnyama hawezi kua na habari yeyote ya vyombo<br />

vinavyotembea baharini, kinachobadilisha usiku na mchana na kadhalika,<br />

basi mtu ambae hana habari ya hayo yote bila shaka hataachana futi moja<br />

na Mnyama mwenyewe. Hilo ni tusi kubwa ambalo ukimweleza mtu basi<br />

mtapigana sana pengine akwambie: “… ngoja leo ndo utauona huo<br />

unyama wangu…”<br />

Akili imesemwa kua inazidi na kupungua. Kuzidi kwake ni<br />

kutokana na wingi wa majaribio katika mambo mbali mbali ambayo<br />

umeanza kuyajua hivi sasa. Na humo humo Mnyezi Mungu<br />

anakufundisha yeye mwenyewe ambayo hukua unayajua.<br />

Ni ajabu kubwa kwa mwenye akili, lakini kwa asiyekuwa na akili hataona<br />

chochote cha maana ndani yake.<br />

Amma kupungua kwake akili ni zama za kufanza makosa akili<br />

huondoka, na ndo maana ya kauli yake Bw. Mtume SAW kua:-<br />

“Hawi muumini anaiba, zama zile za kuiba (kwake)<br />

kua ni muumin, au anazini zama zile za kuzini kua ni<br />

muumin, au anauwa zama zile akiuwa kua ni muumin”.<br />

20.


Na wale ambao zama Sheytwani anapowashika hukumbuka basi<br />

saa hiyo hiyo huwa wanaona (Mno) akili ndo huwa macho,<br />

ikamkumbuka na kumtaja Mnyezi Mungu.<br />

Na azingatie mtu juu ya vitu ambavo tunadai tunavijua mno na<br />

kutokana na kuvijua huko na mazoeya tunahisi ati havitupi taabu hata<br />

kidogo: Radio, Tepu, Tv, Magari, Kamera, Taa za Stimu, Kompyuta,<br />

Mobitel, Inter-net na kadhalika: jee viliteremka moja kwa moja toka<br />

Mbinguni kama mvua?.<br />

Hili ni suala tosha kukuwezesha kuichemsha Akili yako ambayo<br />

labda unatumia sehemu yake moja tu ya – kumi na sita (1/16). Daima<br />

usipoichemsha, itabaki hivyo hivyo mpaka kiyama ambapo itaonekana<br />

kua ulipewa Akili lakini hukuitumia!!.<br />

Sifa za mwenye Akili:<br />

Mnyezi Mungu aliyetukuka amejaalia kila kitu kua na swifa zake<br />

kwa makusudio maalumu ili kipate kujulikana kwa wepesi na<br />

kutambuliwa kwa njia iso na shaka hata kidogo. Halikadhalika Akili nayo<br />

imepewa swifa zake maalumu ambazo zinakujulisha wazi kua mwenyewe<br />

ni mtu mwenye Akili.<br />

Hizi ndo swifa za Akili kutokana na mafunzo alofundisha Bw.<br />

Mtume SAW, katika hadithi iliyopokelewa kutokana na Bi. Aisha (R.A)<br />

hakika amesema:-<br />

Akili inayo Swifa kumi (10) kati yake zimegawika ndani ya mafungu<br />

mawili:- Dhwahiri na Batwin.<br />

Dhwahiri Ni zile zilizo wazi wazi kabisa mtu akiziangalia anaziona,<br />

nazo ni :-<br />

1. Swamt: yaani ukimya, Bw. Mtume SAW katika Swifa hii<br />

pia amesema kua: “ Mwenye kuzidisha maneno yake<br />

basi huzidi kuanguka kwake” (Speech is Silver,<br />

Silence is Gold) (Kusema sema ni fedha na<br />

kunyamaa ni dhahabu – kinaong`arisha.)<br />

21.


2. Hilm: Upole.<br />

3. Tawadhu’i : Yaani ule Unyenyekevu ikiwa ni ile hali ya kujitupa<br />

chini na hata kama Mnyezi Mungu amekufanza kuwa<br />

Mfalme mbele za watu kwani hapo hasa ndo pahala<br />

pake. Amesema Bw. Mtume SAW “Mwenye kujiweka<br />

chini, Basi Mnyezi Mungu humrufaisha ( Humnyanyua<br />

humpandisha juu)”.<br />

4. Kuamrisha mema.<br />

5. Kukataza mabaya: Daima hutakia wenzake mambo ya<br />

kheri kila anapokueko baina ya watu.<br />

<strong>Al</strong>- Habib Sayyid Umar akiwa katika safari za Ulaya kwenye<br />

meli, safari hiyo alijiwa na kijana wa kizungu akawa anamtolea nasaha<br />

na kumueleza juu ya Mnyezi Mungu na kumsomea <strong>Al</strong>-Hamdu na<br />

Qul-Huwallahu kwa taabu. <strong>Al</strong>-Habib alimuuliza ni mda gani tangu<br />

amekua Mwislam? akamwambia miezi sita. Lakini aliahidi kwa Mnyezi<br />

Mungu kua akikutana na mtu yoyote atamwelezea juu ya Mola Sub-hana<br />

Wataala, na hali kadhalika katika kukataza Mabaya ambayo watu<br />

huyafanza, uzuri zaidi ni kuwahi kabla ili mtu aweze kujiandaa na<br />

kuyakwepa.<br />

Sifa za batwin:<br />

6. Tafakkur: Yaani hali ya kufikirifikiri hasa katika dalil nyingi<br />

zilizojaa na kutapakaa katika maumbile, kuanzia mbingu<br />

na viliomo juu na ndani yake. Ardhi na viliomo ndani<br />

yake, mfano wa milima, wanyama, majani, maji na<br />

madini mbali mbali. Kwa mtu wa Tafakkur bila shaka<br />

ndani ya Machache hayo angeweza kuandika vitabu vya<br />

Ilimu fani mbali mbali tele na nyingi ni zenye umuhimu<br />

kweli kweli ndani ya maisha ya hapa duniani.<br />

22.


Bwana Mtume SAW amesema:<br />

“kutafakkur katika maumbile ya Mnyezi Mungu<br />

saa moja ni bora kuliko Ibada (ya sunna) ya<br />

mwaka mzima”.<br />

7. Ibra: Katika maajabu mazito ya akili, swifa hii imetiya<br />

fora kwani katika maisha yake huenda mwenye<br />

akili ndogo akamwelewa vibaya na kumtabiri<br />

ambavyo sivyo alivyo – pengine aseme ni<br />

mchawi.<br />

8. Khofu: Kumkhofu, kumuogopa Mnyezi Mungu peke yake. Amma<br />

kwa yule asie mkhofu Mnyezi Mungu. Basi itafaa kumkhofu<br />

zaidi, kwani haachi kutomuogopa Mnyezi Mungu illa moto<br />

mdogo au mwendawazimu peke yao hao. Inatosha kuonyesha<br />

kua mtu anamkhofu Mnyezi<br />

Mungu kwa kutekeleza kwa kadiri ya uwezo wake yale yote<br />

aloamrishwa ayafanze na kuacha yale yote alokatazwa nayo.<br />

Haiwezi kua ni khofu “eti mbona havui nguo<br />

akatembea uchi au kuhujumu watu.” Wazimu upo<br />

aina saba akichunguza lazima atapata ncha<br />

ilonasibiana nae, na anaemjua mwendawazimu<br />

kisha usimkhofu basi ipo hatari ya kua yeye ni zaidi.<br />

9. Kuyaadhimisha madhambi:<br />

Yaani ayaone mazito hata, yawe madogo vipi kwani hawezi<br />

akajua ni dhambi ipi aifanzayo ambayo itamfanza Mola wake<br />

achukie na kumfuta katika waja wake warehemewa. Zingatia<br />

juu ya moto mkubwa ambao mwanzo wake ni cheche ndogo<br />

ndogo kabisa<br />

10 Kudhalilisha nafsi:<br />

23.


Abadan.<br />

Nafsi kila siku inataka makuu na kutambuliwa na wewe<br />

kua inayo haki kwako, ni kama vitimbi vya mtoto mdogo<br />

nyumbani kwao na hasa wanapokuwepo wageni. Na kama<br />

ilivyo maalumu nafsi ukiitukuza ni lazima mwisho wake<br />

itakuliza, kwani daima haikutizamii maslahi kwako<br />

Nafsi ilokusudiwa hapa si ingine bali ile <strong>Al</strong> ammara.<br />

Mnyezi Mungu ameelezea kua daima ni yenye kuamrisha<br />

maovu tu haibadiliki hata siku<br />

moja. Kwa kifupi mwenye Akili lazima awe na mifano<br />

iliyotajwa kwenye swifa kumi hizo. Na si rahisi kwa<br />

asiekuwa nazo kudai kua na Akili.<br />

Tunamuomba Mnyezi Mungu mjuzi wa kila jambo atufungulie<br />

Tafhuma katika kuielewa na kuitumia vyema Akili jambo ambalo Mola<br />

Sub-hanalaah amelisema kua ni azizi. Kwani hakuna baada Nuru ya<br />

Bwana Mtume SAW, jambo azizi kuliko<br />

A K I L I.<br />

24.


Moyo.<br />

Kwa Kiarabu Moyo ni Qalb; yaani kitu cha kubadilika badilika,<br />

leo hivi kesho vile. Na kutokana na maana hiyo Mapinduzi ni Inqilaab.<br />

Pia ni yenye kukokotezwa kumuomba Mnyezi Mungu mwenye<br />

kuzipindua nyoyo kila siku baina ya vidole vyake viwili – azithibitishe<br />

nyoyo zetu ndani ya Twa`a yake.<br />

Moyo umefananishwa au nasibishwa na Arshi yake Mnyezi<br />

Mungu; kwani mambo yote huanzia hapo. Kadhalika ndani ya Moyo<br />

ndipo panapoanza mambo yetu yote, na mengi tunashangalia sana hivi<br />

leo. Tunayaona ya ajabu, na hiyo peke yake ni Ajabu. Mnyezi Mungu<br />

hajaumba sanaa ya ajabu kuliko Mtu, na papo mtu huyo huyo anaona vitu<br />

vingine alivyovitengeneza yeye mwenyewe kua ni Ajabu. Bwana Mtume<br />

SAW amesema katika hadithi ambayo ni mashuhuri sana kua:-<br />

“Ndani ya mwili lipo pande la nyama Jeusi; likitengemaa<br />

basi hutengemaa mwili mzima, na likifisidika basi<br />

hufisidika mwili wote; (Basi haliwi pande hilo la nyama ila<br />

kua ni Moyo)”<br />

Pia amesema SAW:-<br />

“Hakika amali zote ni zenye kutegemea nia yake mtu; na<br />

nia pahala pake ni moyoni”.<br />

Na Mnyezi Mungu haangalii sura za watu wala watoto wao na<br />

mali zao, lakini Mnyezi Mungu anaangalia nyoyo za watu na matendo<br />

yao. Fikra zote za maana ambazo mtu huzihangaikia, huanza Moyoni.<br />

Mambo yote aliyoyakusanya mtu ni kutokana na Moyo. Mambo mfano<br />

wa Ilimu au Ujuzi wowote kila alichohifadhi, kila chenye kuhitaji<br />

kumbukumbu na kadhalika.<br />

25.


Bwana Mtume SAW amesema:-<br />

“Hufa Mtu Kwa Yale <strong>Al</strong>oishi Nayo, na<br />

hufufuliwa Mtu Kwa Yale <strong>Al</strong>okufa nayo”.<br />

Katika hoja hii wametokea walomili upande wa hakika ya<br />

Talqini (ile asomewayo maiti baada kwisha fukiwa) kua haina umuhimu<br />

kwake kwa sababu kama aliishi akiwa anamjua Mnyezi Mungu na Mtume<br />

wake, anaijua Dini aloridhiya Mola wake, Kibla chake, Imamu wake<br />

(yaani muongozo wake kwa maana ya (Qur an) na ndugu zake, basi<br />

hatahitaji kukumbushwa chochote.<br />

Na hali kadhalika ameishi hayajui hayo mpaka amekufa, basi hatoweza<br />

kujifunza chochote kutokana na Talqini. Anayeweza kujifunza ni yule<br />

aliye hai. Kwa upeo wa Taammul za kweli hutakosa kuona jinsi gani<br />

Moyo ulivo muhimu.<br />

Hebu na atizame na kutaammal mtu, ya vijana wadogo tu<br />

waliohifadhi Qur an yenye aya zisizopungua alfu sita mia sita na sitini na<br />

sita (6666) ndani ya nyoyo zao bila kukosea kitu!.<br />

Kwa msaada wa Moyo ndiyo tunajifunza na kuzihifadhi Ilimu na maarifa<br />

kadhaa wa kadhaa; jee hiyo si ajabu ilo kweya mipaka?.<br />

Suala linakuja, “Jee Moyo huo wenye maajabu makubwa kama<br />

hayo, ambao unamwezesha mtu kuyajibu masuala ya Munkar na<br />

Nakiir baada ya kufa – ukitokea kubakizwa Hospitali kwa<br />

uchunguzi wa sababu za kufa kwa marehemu vipi atakabil<br />

masuali ya Malaika hao. Yote aloyahifadhi moyoni mwake ndo<br />

yamebakia kwenye maabara za Hospitali vipi itakua hukmu ya<br />

maiti wake?”<br />

Hapo ndo maulamaa mfano wa kina Imam Ghazzali walipoenda<br />

kite zaidi na zaidi hadi kufikia kuona kua moyo ulokusudiwa hapo ni ule<br />

wa Nuru ambao pengine ndo mtu mwenyewe, na ambao ndani yake<br />

ndo Mnyezi Mungu ameiweka Akili. Sio Moyo ambao wengi wetu ndo<br />

kwa mazowea tunaojua, ukiwa na kazi ya kuendesha damu ukisaidiwa na<br />

mapafu!.<br />

26.


Amma ilaaka kati yake na Moyo uloachwa Hospitalini ni yenye<br />

kujulikana na Mnyezi Mungu peke yake, kwani Moyo wa<br />

Hospitali unaweza ukaoza kwa vile asili yake ni udongo uliodhihiri<br />

kama nyama. Lakini moyo wa Nuru ni wa swifa za juu ambao<br />

umekusudiwa maisha ya milele na si wenye Kufa hata siku moja.<br />

Ajabu kubwa jinsi unavyoshirikiana na Akili na Ubongo katika matenda<br />

kazi zake ndani ya maisha yetu ya kila siku!!.<br />

Mambo kama haya ndo anotakiwa mtu, na hasa vijana<br />

wajishughulishe nayo ili kujiandaa kupokea matukufu toka kwa Mnyezi<br />

Mungu, alotukuka.<br />

Vijana ndo wenye nafasi nzuri ya kukaribishwa chini ya kivuli cha<br />

Mnyezi Mungu siku ambayo hapatakuwepo kivuli illa hicho ikiwa<br />

watapondokea katika kumtii Mnyezi Mungu tu peke yake wakaacha balaa<br />

na ghasia chungu nzima zilizowazingira maishani mwao.<br />

Inshallah baada ya kujua moyo huo wenye asrari zisoidadi,<br />

huenda mambo yetu yakawa na mwelekeo wa mabadiliko mazuri.<br />

Wafaqanal Lahu lima yuhibbu wa yardha.<br />

27.


Makamu za Nafsi.<br />

No<br />

Nafsi Sifa Nyuradi<br />

1.<br />

2.<br />

3.<br />

4.<br />

5.<br />

6.<br />

7.<br />

<strong>Al</strong> Ammara.<br />

Lawwama.<br />

Mul hama.<br />

Mutmainna.<br />

Radhiyya.<br />

Mardhiyya.<br />

Kamila.<br />

Kupenda kula sana, Ubakhili,<br />

Kuhangaika,<br />

Kua na tamaa, Kuwa na<br />

kiburi (Wall yadh Billah).<br />

Matamanio, Hasada na<br />

Ghafla.<br />

Lalamikalamika, Kujilaumu<br />

laumu, Fikra, Kujizuia<br />

(Qabdh), Ujubi.<br />

Ilmu,Tawaadhui, Tawba.<br />

Subrah,Taamul - kuvumilia<br />

adha.<br />

Ukarimu,Tawakkul, Hikam,<br />

Ibaada, Shukar na Ridhaa.<br />

Zuhdi (Kuipa nyongo dunia),<br />

Ikhlas, War-l, Kuacha<br />

yasomuhusu mtu, Wafaai.<br />

Husnul khuluq – Tabia<br />

njema, Lutf kwa viumbe,<br />

Taqarrab illa Llah – Kuacha<br />

yote yasiokuwa ya<br />

M/Mungu, Tafakkur- Katika<br />

utukufu na ukubwa wake<br />

Mola.<br />

Kuridhika na alokugawia<br />

M/Mungu Sub-hana wataala.<br />

Sifa zote njema zilizotajwa<br />

katika nafsi tano, Ukiacha<br />

nafsi ya kwanza ambayo ni<br />

Ammara.<br />

La ilaha illa<br />

Llah.<br />

<strong>Al</strong>lah.<br />

Huwa.<br />

(Ismuh Dhwamir).<br />

Hayyu.<br />

Ahad<br />

A`ziz<br />

Wadud.<br />

28.


Namna au mambo muhimu katika<br />

zoezi la kuachana na mwili.<br />

Muhadhiri: <strong>Al</strong> <strong>Faqeer</strong> Ahmad Sheikh.<br />

Katika suala zima la kujigawa kuna mambo makubwa ya kuzingatia<br />

mawili: Transmission and Receiving.<br />

What we require to consider, in which way did we receive<br />

that message and then we are going to deal with it. If the<br />

transmission was spiritual: then we must act accordingly.<br />

Otherwise the message will be VOID. No spiritual message<br />

shall ever be valid in another way. Look; take this example of<br />

material in which a Human-being was created – SOIL. But we<br />

taking bath every now and then! And yet we are not dissolving -<br />

Why? – Ask your mind.<br />

Katika mambo haya saba ndio msingi wa kuachana na<br />

mwili – Separation:<br />

1. Lazima kudumu na udhu kwa masaa 24.<br />

2. Kuwa na tumbo jepesi – Mtu na aepukane na mambo ya kula<br />

kupita kiasi. Na hapa ni budi kutumia hadithi ya Bwana Mtume<br />

S.A.W pale aliposema: “Sisi hatuna haja ya Twabibu, kwa<br />

sababu hatuli mpaka tusikie njaa. Na pale tukila hatuli<br />

tukashiba”.<br />

29.


Jambo lingine la kuzingatia, ni aina ya chakula. Ni vyema<br />

kuepukana na vyakula vyote vyenye kutia nyege. (Ashki ya<br />

kufanya tendo la ndoa) na ikiwezekana ni bora mtu ajiepushe na<br />

vyakula vinavyotokana na Roho.<br />

3. Tuondoe woga kwa viumbe: Mtu na ajaribu kutoka usiku mpevu<br />

nje ya mji na alale popote bila ya kuogopa kuwa linaweza<br />

kutokea jambo dhidi yake.<br />

4. Mtu na aendelee kumtaja Mnyezi Mungu mara kwa mara. Na<br />

amkimbize Sheytwani Ibilisi kwa kutamka Kalimat Tawheed.<br />

Na pale anapoitamka Kalimat hiyo ni budi itoke ndani ya Roho.<br />

Kwa hakika ya mambo ya Kiroho hupatikana kwa kuyafanya<br />

Kiroho hayo mambo yenyewe.<br />

5. Mtu na aangalie Wakati. Hasa kati ya majira ya saa kumi na saa<br />

kumi na moja za <strong>Al</strong> fajir. Basi, atakuta kuna Wakati umesimama<br />

hauendi kama nyakati nyingine. Si vingine juu ya hakika ya<br />

jambo hilo, isipokuwa Mnyezi Mungu SWT anadhihiri katika<br />

wingu na Dunia akinadi : Je! Nani mwenye haja zake ili<br />

nimkidhie?, Nani mwenye haja ya kufutiwa Dhambi zake<br />

Nimfutie? Nani mwenye kutaka Pepo yangu Nimpatie?”.<br />

Wengi ya watu wanakuwa wamelala katika wakati huo. Basi<br />

kama wewe umefanikiwa juu ya jambo hilo ukawa hadhiri, basi<br />

nyanyuka na utarakai – Rakaa mbili za wakati huo ni bora<br />

kuliko Dunia na vilivyomo.<br />

6. Jitahidi kujiweka katika hali ya kati ya kuwa macho na kua<br />

katika Usingizi. Na ni katika hali hiyo ambapo unaweza<br />

kufungukiwa na mambo mengi – kwani ukifanikiwa jambo hilo<br />

utakuwa ukimiliki Coscious Mind na Sub–Conscious Mind. Na<br />

moja kati ya mambo yaliyo muhimu kabisa katika ku-develop ili<br />

uweze kujigawa.<br />

7. Shart lingine kubwa kabisa ni kumwogopa Mnyezi Mungu<br />

Kikweli kweli. Ndipo ambapo yeye Mnyezi Mungu atakiogopesha<br />

kila kiumbe dhidi yako. Na ndio maana ikapendelewa mtu afanye<br />

Haluwa zake nje ya mji.<br />

30.


Mahali ambapo ataweza kuziepuka sauti za watu. Jambo hili<br />

litampelekea mtu kuweza kuidhibiti barabara Nafsi yake. Na ile<br />

akili yenye nguvu Sub Conscious Mind inaingia kazini katika<br />

zile sehemu za hatari hatari. Hivyo ili kuizowesha kutumika akili<br />

hiyo budi kutingishwa tingishwa. Wengi katika watu hutumia<br />

kiasi cha 1/16. cha akili alopewa na ndio maana Bwana Mtume<br />

SAW akasema: “Watu wamelala”. Kwani sehemu kubwa ya<br />

akili zetu hatuzitumii. Hivyo na ajitahidi kila mmoja wetu<br />

kujipandisha Daraja kwa kuyafanzia kazi yale anayojua, ili angaa<br />

tuweze kutumia japo 3/16. ya akili zetu. Na papo ukifikia kutumia<br />

kiasi hicho, wengi katika watu watakupanga wewe katika kundi la<br />

wenda wazimu. Ama watakuona umechanganyikiwa (Ndio maana<br />

unasema au unatenda yasiyowezekana). Kwa kuwa maono yako<br />

yatakuwa mbali na maono ya watu wengine, na ni kweli utakuwa<br />

ukiviona vitu kwa asili yake, siyo kwa mfano ambao wengi wetu<br />

tumezoea kuona. Utakuwa unaishi katika ulimwengu wa Hakika<br />

na muda mrefu utakuwa katika jitihada za kumridhisha Mnyezi<br />

Mungu, na hapo ndipo penye kufuzu.<br />

“Hakika yetu sisi Hatukuwaumba Majini na Watu ila<br />

kwa kuniabudu Mimi. (Kunitambua mimi)”.<br />

31.


Mtungaji:<br />

(<strong>Al</strong> marhum)<br />

AL- FAQEER AL - HABIB AHMAD SHEIKH<br />

32.


Vitabu vilivyokwishatoka ni:<br />

*1. Maana halisi ya Imaan. (i) (1 st , 2nd & 3rd addition).<br />

*2. Njia nyepesi ya kuijua nafsi yako.<br />

*3. Njia nyepesi ya kujua kitu juu ya uongofu.<br />

*4. Knowledge vision & ecstacy.<br />

*5. Mwinyi Baraka katika ulimwengu wa kiislamu (i) .<br />

*6. Waislamu na Sayansi - Ulu-m.<br />

*7. Kuhifadhi Burda.<br />

*8. Maana halisi ya Imaan (ii).<br />

*9. Muhammad SAW katika ulimwengu wa ghayb.<br />

*10. Siri ya Balaa.<br />

*11. El makhlouq (Viumbe)<br />

*12. Njia nyepesi ya kujua kitu juu ya uongofu. (2nd addition)<br />

*13. Manaqib ya <strong>Al</strong> habbib Sayyeid <strong>Al</strong> Ma`aruf.<br />

*14. Some aspects of concepts of facility in medevial Islamic<br />

Philosophy by Mwinyibaraka.<br />

*15. Njia nyepesi ya kuijua Nafsi yako. (2nd addition).<br />

Vitabu ambavyo tunategemea kuvitoa muda si mrefu<br />

(Insha <strong>Al</strong>lah) ni:<br />

*1. Waislamu na Sayansi - Ulu-m. (2nd addition)<br />

*2. Mwinyi Baraka katika ulimwengu wa kiislamu (ii).<br />

*3. Muhammad SAW katika ulimwengu wa Ghayb.<br />

Kwa maulizo kuhusu vitabu wasiliana nasi:<br />

Majaalis El Ulaa - El Qadiriyya Sinza,<br />

33.<br />

P.o. Box 15170,<br />

Tel: 0747 483553<br />

Tel: 0748 595958.<br />

Tel: 0744 023703.<br />

Tel: 0741 235091.<br />

Tel: 0744 299597.<br />

Dar es salaam.


<strong>Al</strong> habib <strong>Al</strong> <strong>Faqeer</strong> Ahmed Sheikh Mohamed Sheikh Msiha, amezaliwa<br />

Singida mkoa wa Dodoma, mwaka 1938. Amepata elimu ya sekula Unguja na<br />

amebahatika kupata elimu ya juu katika chuo maarufu Afrika ya Mashariki<br />

Makerere Uganda.<br />

Elimu yake ya Dini ameipata hapo hapo Unguja toka kwa Masheikh mbali mbali,<br />

baadhi yao ni:<br />

Sheikh Sleiman <strong>Al</strong>wi (Muhib Rasul) (<strong>Al</strong> Marhum).<br />

Sheikh Seyyid Mansab.<br />

Maalim Himid (<strong>Al</strong> marhum).<br />

Maalim Hemed Muhamed El Buhry.<br />

Sheikh Seyyid Qamus.<br />

Sheikh Muawwiya Ibn Abdul Rahman.<br />

Sheikh <strong>Al</strong>ly Muhamed Comorian.<br />

Sheikh Ibrahim Mzee Ahd.<br />

Sheikh Haj Mzee Ahmad Msiha.<br />

Amma Elimu ya Nafsi na Roho Amepata Ijaza yake toka kwa A`limu mkubwa<br />

Duniani <strong>Al</strong> Habib Sayyid Omar Bin Abdallah (Mwinyi Baraka).<br />

Sheikh Ahmad amewahi kufanya kazi katika jeshi la Polisi Tanzania Bara<br />

katika mikoa mbali mbali mpaka alipostahafu.<br />

Katika umri wake wote Sheikh Ahmad alijahid katika kuendeleza Uislamu<br />

kwa kusomesha na kuandika vitabu vya mada na maudhui mbali mbali katika<br />

Uislamu. Pia alianzisha Majaalis Sehemu mbali ambazo ziko mpaka leo, Mtaa wa<br />

Pemba, Sinza, Bungoni, kijito nyama, Sadani (Ilala) na Kibaha (Misugusugu)<br />

ambapo ndipo ilipo Dhwarihi yake (alipozikwa).<br />

Sheikh Ahmad ametwawafu 27. 8. 2001. ( Mwezi 7 jumadda thany 1421<br />

H.R.). Akiwa na umri wa miaka 63, vile vile alivyokuwa akiomba aishi umri ule<br />

ule alioshi kipenzi chake Bwana Mtume Muhammad SAW.<br />

Insha <strong>Al</strong>lah Mnyezi Mungu amjaze kheri na alitie Nuru kaburi lake (Amin).<br />

Khalifa: Sheikh Issa Othman,<br />

Majaalis El Ulaa El Qadiriyya, Sinza Dar es Salam.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!