You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Moyo.<br />
Kwa Kiarabu Moyo ni Qalb; yaani kitu cha kubadilika badilika,<br />
leo hivi kesho vile. Na kutokana na maana hiyo Mapinduzi ni Inqilaab.<br />
Pia ni yenye kukokotezwa kumuomba Mnyezi Mungu mwenye<br />
kuzipindua nyoyo kila siku baina ya vidole vyake viwili – azithibitishe<br />
nyoyo zetu ndani ya Twa`a yake.<br />
Moyo umefananishwa au nasibishwa na Arshi yake Mnyezi<br />
Mungu; kwani mambo yote huanzia hapo. Kadhalika ndani ya Moyo<br />
ndipo panapoanza mambo yetu yote, na mengi tunashangalia sana hivi<br />
leo. Tunayaona ya ajabu, na hiyo peke yake ni Ajabu. Mnyezi Mungu<br />
hajaumba sanaa ya ajabu kuliko Mtu, na papo mtu huyo huyo anaona vitu<br />
vingine alivyovitengeneza yeye mwenyewe kua ni Ajabu. Bwana Mtume<br />
SAW amesema katika hadithi ambayo ni mashuhuri sana kua:-<br />
“Ndani ya mwili lipo pande la nyama Jeusi; likitengemaa<br />
basi hutengemaa mwili mzima, na likifisidika basi<br />
hufisidika mwili wote; (Basi haliwi pande hilo la nyama ila<br />
kua ni Moyo)”<br />
Pia amesema SAW:-<br />
“Hakika amali zote ni zenye kutegemea nia yake mtu; na<br />
nia pahala pake ni moyoni”.<br />
Na Mnyezi Mungu haangalii sura za watu wala watoto wao na<br />
mali zao, lakini Mnyezi Mungu anaangalia nyoyo za watu na matendo<br />
yao. Fikra zote za maana ambazo mtu huzihangaikia, huanza Moyoni.<br />
Mambo yote aliyoyakusanya mtu ni kutokana na Moyo. Mambo mfano<br />
wa Ilimu au Ujuzi wowote kila alichohifadhi, kila chenye kuhitaji<br />
kumbukumbu na kadhalika.<br />
25.