17.02.2015 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Moyo.<br />

Kwa Kiarabu Moyo ni Qalb; yaani kitu cha kubadilika badilika,<br />

leo hivi kesho vile. Na kutokana na maana hiyo Mapinduzi ni Inqilaab.<br />

Pia ni yenye kukokotezwa kumuomba Mnyezi Mungu mwenye<br />

kuzipindua nyoyo kila siku baina ya vidole vyake viwili – azithibitishe<br />

nyoyo zetu ndani ya Twa`a yake.<br />

Moyo umefananishwa au nasibishwa na Arshi yake Mnyezi<br />

Mungu; kwani mambo yote huanzia hapo. Kadhalika ndani ya Moyo<br />

ndipo panapoanza mambo yetu yote, na mengi tunashangalia sana hivi<br />

leo. Tunayaona ya ajabu, na hiyo peke yake ni Ajabu. Mnyezi Mungu<br />

hajaumba sanaa ya ajabu kuliko Mtu, na papo mtu huyo huyo anaona vitu<br />

vingine alivyovitengeneza yeye mwenyewe kua ni Ajabu. Bwana Mtume<br />

SAW amesema katika hadithi ambayo ni mashuhuri sana kua:-<br />

“Ndani ya mwili lipo pande la nyama Jeusi; likitengemaa<br />

basi hutengemaa mwili mzima, na likifisidika basi<br />

hufisidika mwili wote; (Basi haliwi pande hilo la nyama ila<br />

kua ni Moyo)”<br />

Pia amesema SAW:-<br />

“Hakika amali zote ni zenye kutegemea nia yake mtu; na<br />

nia pahala pake ni moyoni”.<br />

Na Mnyezi Mungu haangalii sura za watu wala watoto wao na<br />

mali zao, lakini Mnyezi Mungu anaangalia nyoyo za watu na matendo<br />

yao. Fikra zote za maana ambazo mtu huzihangaikia, huanza Moyoni.<br />

Mambo yote aliyoyakusanya mtu ni kutokana na Moyo. Mambo mfano<br />

wa Ilimu au Ujuzi wowote kila alichohifadhi, kila chenye kuhitaji<br />

kumbukumbu na kadhalika.<br />

25.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!