Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
DIBAJI:<br />
Bismillahir Rahmanir Raheem.<br />
Baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu Mola wa ulimwengu,<br />
Mfalme wa siku ya malipo yeye peke yake ndiye anayesitahiki kuabudiwa<br />
na hakuzaa wala hakuzaliwa.<br />
Anasema Mwenyezi Mungu katika Kurani Takatifu Surat<br />
Yusuf Aya ya 53:<br />
“….Nami sitakasi Nafsi yangu, kwa hakika kila<br />
Nafsi ni yenye kuamrisha sana maovu isipokuwa<br />
ile ambayo Mola wangu ameirehemu”.<br />
Maneno haya ya katika Kurani Takatifu aliyoyaelezea kumueleza<br />
Mtume Muhammad (SAW) yanamhusu Mtume Yusuf Bin Yakuwb (AS)<br />
alipokua anajitetea kuwa hakumtaka mke wa Mfalme wa Misri.<br />
Anamhakikishia kuwa “Nafsi ni yenye kutuamrisha sana maovu”<br />
isipokuwa iliyorehemewa na yeye Mola. Na hii iliyorehemewa na Mola<br />
ndiyo Nafsi ambayo yenye muelekeo mzuri yenye kumtii Mwenyezi<br />
Mungu na kumuabudu na ndiyo inayoitwa “<strong>Al</strong> Mutmainna” aliyoitaja<br />
Mwenyezi Mungu katika Kurani Takatifu Surat <strong>Al</strong>fajr:<br />
Ewe Nafsi iliyotulia rejeya kwa Mola wako<br />
hali ya kuwa utaridhika (kwa utakayoyapata)<br />
na Mwenyezi Mungu aridhike na wewe, basi<br />
iv.