Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Basi kidogo hiyo ni yenye kutosha kabisa. Pengine ingekuwa ni<br />
Rehma mbili katika zile mia ndo ziloshushwa ungesema watu<br />
wangeshindwa kufanza mambo mengine yoyote bali wangekuwa<br />
wanarehemeana tu. Wapo watu wengine wanafikia kuikanusha kisirisiri<br />
au kipumbavu kiuchache wa ilmu. Aya hiyo: 17:85 wao wakidai kua<br />
hamna anaejua mambo ya roho illa Mnyezi Mungu .<br />
Mnyezi Mungu anaijua mno hiyo Roho; anasema kua ametupa ujuzi<br />
nayo lakini ni kuduchu. Si busara kuchukua kidogo ya Mnyezi Mungu<br />
ukaifanza kua ndo hiyo hiyo kwako wewe Mwanadamu, na huku ukidai<br />
kuamini kua: –<br />
“Hana anayefanana naye hata mmoja”.<br />
Kuna hatari ya kufikia kujichukua wewe kama <strong>Al</strong>im-Sameeun<br />
(Unaesikia ) Basweerun (Unaeona) na kadhalika, kua ndo hiyo hiyo ya<br />
Mnyezi Mungu (Mnyezi Mungu apishilie mbali fikra kama hizo kwetu).<br />
Mnyezi Mungu anamuona na kumsikia sisimizi michang’ato yake<br />
chini ya ardhi ndani ya giza la usiku, Je Shekhe, wewe wasikia hivo hivo?<br />
Mnyezi Mungu anayajua ya siri na yalofichika ndani ya siri katika vifua<br />
vya watu. Jee na wewe Sheikh ni hivo hivo? Basi Staghfiru kwa Mola<br />
wako na ukithirishe Kalima ya Tawheedi usije ukahiliki kwa kujifanya<br />
kichwa Mchungu. Uislamu unataka unyenyekevu (Sub-Mission).<br />
Na isisahaulike kua Bwana Mtume SAW amekataza malumbano na<br />
kwamba mwenye kuacha kulumbana (kubishana na hali ya kua yeye ndio<br />
mwenye haki basi (malipo yake) siku ya kiama Mnyezi Mungu<br />
atamjengea Nyumba ya Dhahabu). Na ikiwa kwa waliopewa Chuo (Ahlil-<br />
Kitab) Basi malumbano yawe “Bil-lati Hiya Ahsan” kwa njia ya wema<br />
sana. Kwa nini?; kwa sababu ni mara chache tunakumbuka kua mtu<br />
anapopinga jambo hua na maana ya kufru. Kwa hiyo basi huenda mtu<br />
akawa na Sijda yake usoni lakini ni Kafiri.<br />
10.