You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Nafsi Mardhiyya.<br />
ya sita:<br />
Nafsi hii imetajwa mara tu baada ya Nafsi Radhiya yaani ilo ridhiwa<br />
na Mola Sub-hana wa Taalah. Amma mtu akisha ridhiwa na Mnyezi<br />
Mungu basi hua hana haja ya kuogopa chochote tena.<br />
Sifa zake:<br />
Husnul khuluq – Tabia njema<br />
Lutf kwa viumbe.<br />
Taqarrab ila Llah – Kuacha yote yasiokuwa ya Mnyezi Mungu.<br />
Tafakkur - Katika utukufu na ukubwa wake Mola.<br />
Kuridhika na alokugawia Mnyezi Mungu Sub-hana wataala.<br />
Nafsi hiyo inatakiwa kurudi kwa Mola wake Radhiyya.<br />
Hali ya kuwa Mardhiyya hivyo basi, inatakiwa iingie katika kundi la waja<br />
wake Mnyezi Mungu.<br />
Waja wote ni wa Mnyezi Mungu lakini wapo ambao ni speshel.<br />
Amma katika walioukubali uja hakuna kama Bwana Mtume <strong>Al</strong>ayhi<br />
Afdhalu Swalaat Was-salaam.<br />
Mtume Muhammad S.A.W Ni mja wake na mjumbe wake. Mitume<br />
wengine wote wanamfwatia Nabii Muhammad .S. A W. kama Sayyidna<br />
Issa AS. ametajwa pia kama Abduhu warasuluhu lakini wamepitana<br />
kwa daraja na fadhila. Na pamoja na hayo yote pia Mtume SAW anasema<br />
ya kuwa…..“Hajifakharishi- Katika kuwa kwake Bwana wa watoto<br />
wote wa (Nabii Adam A.S.W).”<br />
Nafsi Kaamila.<br />
Ya saba:<br />
Pengine huitwa Nafsi Swafiyya, yaani iliyokuwa safi<br />
6.