17.02.2015 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

ROHO/NAFSI<br />

Qur an: 17:85.<br />

“Na wanakuuliza habari ya roho. Sema, roho ni jambo<br />

lililohusika na Mola wangu (Mnyezi Mungu) nanyi<br />

hamkupewa katika ilmu (Ujuzi) ila kidogo kabisa”.<br />

Ushahidi wa aya hii ni wenye kuonyesha wazi wazi kua upo ujuzi<br />

wa Roho. Na pamoja na kua kidogo au kiduchu tu. Ndiyo makadirio<br />

ambayo Mnyezi Mungu ameonelea kua ni yenye kutosha kabisa kwa hapa<br />

duniani.<br />

Katika misemo yetu ya Kiswahili ni ule msemo:- “Maji ya kifuu ni<br />

Bahari ya chungu” (yaani yule mdudu mdogo na mwepesi sana – mdudu<br />

wa sukari pengine mdudu chungu).<br />

Huo ni mfano mmoja tosha kwa mtu mwenye akili ya kujisaidia nayo<br />

angalau kidogo tu; ni wazi kuwa hatahitaji maelezo marefu ya aina<br />

yoyote.<br />

Tukiangalia kwa mazingatio kauli ya Bw. Mtume S.A.W juu ya<br />

Rehma za Mnyezi Mungu tunaelewa fika kua ni “moja kwa mia moja”<br />

kwa jumla tangu dunia ianze mpaka kufikia kiyama. Bila shaka moja kwa<br />

mia ni sehemu ndogo mno, na hapo mpaka leo hii karne ya Ishirini na<br />

moja mwaka huu wa Elfu mbili watu bado wangali wanarehemeana bado.<br />

Na hasa ukiongezeka usemi wake kua:<br />

“Warehemuni walioko ardhini atakurehemuni<br />

aliyeko mbinguni”.<br />

9.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!