You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
ROHO/NAFSI<br />
Qur an: 17:85.<br />
“Na wanakuuliza habari ya roho. Sema, roho ni jambo<br />
lililohusika na Mola wangu (Mnyezi Mungu) nanyi<br />
hamkupewa katika ilmu (Ujuzi) ila kidogo kabisa”.<br />
Ushahidi wa aya hii ni wenye kuonyesha wazi wazi kua upo ujuzi<br />
wa Roho. Na pamoja na kua kidogo au kiduchu tu. Ndiyo makadirio<br />
ambayo Mnyezi Mungu ameonelea kua ni yenye kutosha kabisa kwa hapa<br />
duniani.<br />
Katika misemo yetu ya Kiswahili ni ule msemo:- “Maji ya kifuu ni<br />
Bahari ya chungu” (yaani yule mdudu mdogo na mwepesi sana – mdudu<br />
wa sukari pengine mdudu chungu).<br />
Huo ni mfano mmoja tosha kwa mtu mwenye akili ya kujisaidia nayo<br />
angalau kidogo tu; ni wazi kuwa hatahitaji maelezo marefu ya aina<br />
yoyote.<br />
Tukiangalia kwa mazingatio kauli ya Bw. Mtume S.A.W juu ya<br />
Rehma za Mnyezi Mungu tunaelewa fika kua ni “moja kwa mia moja”<br />
kwa jumla tangu dunia ianze mpaka kufikia kiyama. Bila shaka moja kwa<br />
mia ni sehemu ndogo mno, na hapo mpaka leo hii karne ya Ishirini na<br />
moja mwaka huu wa Elfu mbili watu bado wangali wanarehemeana bado.<br />
Na hasa ukiongezeka usemi wake kua:<br />
“Warehemuni walioko ardhini atakurehemuni<br />
aliyeko mbinguni”.<br />
9.