17.02.2015 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Kupigana Jihadi na Nafsi ni jukumu kubwa linalotukabili katika<br />

maisha yetu ya hapa Duniani. Mfano alivotupigia Sheikh Ahmad katika<br />

kitabu hiki Uk. 11 wa Sheikh Abdul – Kaader Jeylani (Q.A.S.A)<br />

kuwa alichukua miaka kumi na tano maporini akifanza majaribio<br />

kuishinda Nafsi yake. Na akaishinda na kuitawala barabara. Na kuitawala<br />

huko ni kufikia kilele cha ucha Mungu na akawa mmoja wa Mawalii wa<br />

Mwenyezi Mungu. Na kabla yake alikuwepo Walii nchini <strong>Al</strong>yaman jina<br />

lake Abuwmuslim <strong>Al</strong> khawalaniy aliyempinga <strong>Al</strong> aswad <strong>Al</strong> ansiy<br />

aliyekuwa akijidai Unabii na Utume wakati wa Mtume Muhammad<br />

(SAW) alikamatwa na wafuasi wa <strong>Al</strong> ansiy na wakamtiya katika shimo la<br />

moto ili aunguwe. Moto haukumuunguza wala haukumchubuwa kama<br />

ilivyotokea kwa Mtume Ibrahim (AS), hii ni karama alizozionyesha walii<br />

huyu Abuwmuslim kwa kuishinda Nafsi yake. Kwa hivyo basi na<br />

tujitahidi kuzipiga Jihadi Nafsi zetu kwa sababu ndizo<br />

zitakazotusababishiya kuingizwa ima Peponi au Motoni. Amesema<br />

Mwenyenzi Mungu katika Kurani Takatifu<br />

Surat <strong>Al</strong> – Imraan, 185 :-<br />

“Kila Nafsi itaonja mauti na bila shaka mtapewa ujira<br />

wenu kamili siku ya kiyama, na aliyewekwa mbali na moto<br />

na akaingizwa peponi, basi amefuzu, na maisha ya Dunia<br />

hii ni starehe idanganyayo”.<br />

Mwenyenzi Mungu amjaze kheri Sheikh Ahmad kwa juhudi zake<br />

za kuandika kitabu hiki kwa kuwanufaisha na kuwazindusha ndugu zake<br />

Waislamu.<br />

WAMA TAWFIYQIY ILLA BI LLAAH.<br />

AHMAD HAYDAR MWINYIMVUA,<br />

DAR ES SALAAM.<br />

vi.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!