Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Kupigana Jihadi na Nafsi ni jukumu kubwa linalotukabili katika<br />
maisha yetu ya hapa Duniani. Mfano alivotupigia Sheikh Ahmad katika<br />
kitabu hiki Uk. 11 wa Sheikh Abdul – Kaader Jeylani (Q.A.S.A)<br />
kuwa alichukua miaka kumi na tano maporini akifanza majaribio<br />
kuishinda Nafsi yake. Na akaishinda na kuitawala barabara. Na kuitawala<br />
huko ni kufikia kilele cha ucha Mungu na akawa mmoja wa Mawalii wa<br />
Mwenyezi Mungu. Na kabla yake alikuwepo Walii nchini <strong>Al</strong>yaman jina<br />
lake Abuwmuslim <strong>Al</strong> khawalaniy aliyempinga <strong>Al</strong> aswad <strong>Al</strong> ansiy<br />
aliyekuwa akijidai Unabii na Utume wakati wa Mtume Muhammad<br />
(SAW) alikamatwa na wafuasi wa <strong>Al</strong> ansiy na wakamtiya katika shimo la<br />
moto ili aunguwe. Moto haukumuunguza wala haukumchubuwa kama<br />
ilivyotokea kwa Mtume Ibrahim (AS), hii ni karama alizozionyesha walii<br />
huyu Abuwmuslim kwa kuishinda Nafsi yake. Kwa hivyo basi na<br />
tujitahidi kuzipiga Jihadi Nafsi zetu kwa sababu ndizo<br />
zitakazotusababishiya kuingizwa ima Peponi au Motoni. Amesema<br />
Mwenyenzi Mungu katika Kurani Takatifu<br />
Surat <strong>Al</strong> – Imraan, 185 :-<br />
“Kila Nafsi itaonja mauti na bila shaka mtapewa ujira<br />
wenu kamili siku ya kiyama, na aliyewekwa mbali na moto<br />
na akaingizwa peponi, basi amefuzu, na maisha ya Dunia<br />
hii ni starehe idanganyayo”.<br />
Mwenyenzi Mungu amjaze kheri Sheikh Ahmad kwa juhudi zake<br />
za kuandika kitabu hiki kwa kuwanufaisha na kuwazindusha ndugu zake<br />
Waislamu.<br />
WAMA TAWFIYQIY ILLA BI LLAAH.<br />
AHMAD HAYDAR MWINYIMVUA,<br />
DAR ES SALAAM.<br />
vi.