Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
2. Hilm: Upole.<br />
3. Tawadhu’i : Yaani ule Unyenyekevu ikiwa ni ile hali ya kujitupa<br />
chini na hata kama Mnyezi Mungu amekufanza kuwa<br />
Mfalme mbele za watu kwani hapo hasa ndo pahala<br />
pake. Amesema Bw. Mtume SAW “Mwenye kujiweka<br />
chini, Basi Mnyezi Mungu humrufaisha ( Humnyanyua<br />
humpandisha juu)”.<br />
4. Kuamrisha mema.<br />
5. Kukataza mabaya: Daima hutakia wenzake mambo ya<br />
kheri kila anapokueko baina ya watu.<br />
<strong>Al</strong>- Habib Sayyid Umar akiwa katika safari za Ulaya kwenye<br />
meli, safari hiyo alijiwa na kijana wa kizungu akawa anamtolea nasaha<br />
na kumueleza juu ya Mnyezi Mungu na kumsomea <strong>Al</strong>-Hamdu na<br />
Qul-Huwallahu kwa taabu. <strong>Al</strong>-Habib alimuuliza ni mda gani tangu<br />
amekua Mwislam? akamwambia miezi sita. Lakini aliahidi kwa Mnyezi<br />
Mungu kua akikutana na mtu yoyote atamwelezea juu ya Mola Sub-hana<br />
Wataala, na hali kadhalika katika kukataza Mabaya ambayo watu<br />
huyafanza, uzuri zaidi ni kuwahi kabla ili mtu aweze kujiandaa na<br />
kuyakwepa.<br />
Sifa za batwin:<br />
6. Tafakkur: Yaani hali ya kufikirifikiri hasa katika dalil nyingi<br />
zilizojaa na kutapakaa katika maumbile, kuanzia mbingu<br />
na viliomo juu na ndani yake. Ardhi na viliomo ndani<br />
yake, mfano wa milima, wanyama, majani, maji na<br />
madini mbali mbali. Kwa mtu wa Tafakkur bila shaka<br />
ndani ya Machache hayo angeweza kuandika vitabu vya<br />
Ilimu fani mbali mbali tele na nyingi ni zenye umuhimu<br />
kweli kweli ndani ya maisha ya hapa duniani.<br />
22.