Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Bwana Mtume SAW amesema:-<br />
“Hufa Mtu Kwa Yale <strong>Al</strong>oishi Nayo, na<br />
hufufuliwa Mtu Kwa Yale <strong>Al</strong>okufa nayo”.<br />
Katika hoja hii wametokea walomili upande wa hakika ya<br />
Talqini (ile asomewayo maiti baada kwisha fukiwa) kua haina umuhimu<br />
kwake kwa sababu kama aliishi akiwa anamjua Mnyezi Mungu na Mtume<br />
wake, anaijua Dini aloridhiya Mola wake, Kibla chake, Imamu wake<br />
(yaani muongozo wake kwa maana ya (Qur an) na ndugu zake, basi<br />
hatahitaji kukumbushwa chochote.<br />
Na hali kadhalika ameishi hayajui hayo mpaka amekufa, basi hatoweza<br />
kujifunza chochote kutokana na Talqini. Anayeweza kujifunza ni yule<br />
aliye hai. Kwa upeo wa Taammul za kweli hutakosa kuona jinsi gani<br />
Moyo ulivo muhimu.<br />
Hebu na atizame na kutaammal mtu, ya vijana wadogo tu<br />
waliohifadhi Qur an yenye aya zisizopungua alfu sita mia sita na sitini na<br />
sita (6666) ndani ya nyoyo zao bila kukosea kitu!.<br />
Kwa msaada wa Moyo ndiyo tunajifunza na kuzihifadhi Ilimu na maarifa<br />
kadhaa wa kadhaa; jee hiyo si ajabu ilo kweya mipaka?.<br />
Suala linakuja, “Jee Moyo huo wenye maajabu makubwa kama<br />
hayo, ambao unamwezesha mtu kuyajibu masuala ya Munkar na<br />
Nakiir baada ya kufa – ukitokea kubakizwa Hospitali kwa<br />
uchunguzi wa sababu za kufa kwa marehemu vipi atakabil<br />
masuali ya Malaika hao. Yote aloyahifadhi moyoni mwake ndo<br />
yamebakia kwenye maabara za Hospitali vipi itakua hukmu ya<br />
maiti wake?”<br />
Hapo ndo maulamaa mfano wa kina Imam Ghazzali walipoenda<br />
kite zaidi na zaidi hadi kufikia kuona kua moyo ulokusudiwa hapo ni ule<br />
wa Nuru ambao pengine ndo mtu mwenyewe, na ambao ndani yake<br />
ndo Mnyezi Mungu ameiweka Akili. Sio Moyo ambao wengi wetu ndo<br />
kwa mazowea tunaojua, ukiwa na kazi ya kuendesha damu ukisaidiwa na<br />
mapafu!.<br />
26.