17.02.2015 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Bwana Mtume SAW amesema:-<br />

“Hufa Mtu Kwa Yale <strong>Al</strong>oishi Nayo, na<br />

hufufuliwa Mtu Kwa Yale <strong>Al</strong>okufa nayo”.<br />

Katika hoja hii wametokea walomili upande wa hakika ya<br />

Talqini (ile asomewayo maiti baada kwisha fukiwa) kua haina umuhimu<br />

kwake kwa sababu kama aliishi akiwa anamjua Mnyezi Mungu na Mtume<br />

wake, anaijua Dini aloridhiya Mola wake, Kibla chake, Imamu wake<br />

(yaani muongozo wake kwa maana ya (Qur an) na ndugu zake, basi<br />

hatahitaji kukumbushwa chochote.<br />

Na hali kadhalika ameishi hayajui hayo mpaka amekufa, basi hatoweza<br />

kujifunza chochote kutokana na Talqini. Anayeweza kujifunza ni yule<br />

aliye hai. Kwa upeo wa Taammul za kweli hutakosa kuona jinsi gani<br />

Moyo ulivo muhimu.<br />

Hebu na atizame na kutaammal mtu, ya vijana wadogo tu<br />

waliohifadhi Qur an yenye aya zisizopungua alfu sita mia sita na sitini na<br />

sita (6666) ndani ya nyoyo zao bila kukosea kitu!.<br />

Kwa msaada wa Moyo ndiyo tunajifunza na kuzihifadhi Ilimu na maarifa<br />

kadhaa wa kadhaa; jee hiyo si ajabu ilo kweya mipaka?.<br />

Suala linakuja, “Jee Moyo huo wenye maajabu makubwa kama<br />

hayo, ambao unamwezesha mtu kuyajibu masuala ya Munkar na<br />

Nakiir baada ya kufa – ukitokea kubakizwa Hospitali kwa<br />

uchunguzi wa sababu za kufa kwa marehemu vipi atakabil<br />

masuali ya Malaika hao. Yote aloyahifadhi moyoni mwake ndo<br />

yamebakia kwenye maabara za Hospitali vipi itakua hukmu ya<br />

maiti wake?”<br />

Hapo ndo maulamaa mfano wa kina Imam Ghazzali walipoenda<br />

kite zaidi na zaidi hadi kufikia kuona kua moyo ulokusudiwa hapo ni ule<br />

wa Nuru ambao pengine ndo mtu mwenyewe, na ambao ndani yake<br />

ndo Mnyezi Mungu ameiweka Akili. Sio Moyo ambao wengi wetu ndo<br />

kwa mazowea tunaojua, ukiwa na kazi ya kuendesha damu ukisaidiwa na<br />

mapafu!.<br />

26.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!