12.07.2015 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS
  • No tags were found...

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Proposta de Dissertação de Mestrado DCTI, ISCTE - IUL 1Escolha de jogadas estudadas usando tecnologiasbaseadas em CBROrientador: Luís Mota1 IntroduçãoO futebol robótico é uma área de investigação e de divulgação científica emgrande expansão, devido à grande abrangência de temas de investigação quemotiva e também à sua componente lúdica e didáctica. A investigação nestaárea é fomentada por uma organização internacional (ver www.robocup.org)que organiza campeonatos e conferências numa base anual. Existem váriasligas, e.g. robots pequenos, simulação e humanoides, onde se abordam diferentesdesafios. Uma questão que tem atraído atenção a nível de investigaçãoé o desenvolvimento de jogadas estudadas (“Setplays”), a serem aplicadas emcircunstâncias particulares, por forma a explorar fraquezas do adversário.Exemplos de tal jogadas serão a marcação de bolas paradas, bem como situaçõesparticulares em jogo corrido. Tais jogadas são livremente definidasnuma linguagem específica. Esta capacidade é suportada por uma estruturade software já existente e em funcionamento em várias equipas de várias ligas.A sua plena aplicação depende, porém, da capacidade de escolher, emcada momento, a jogada mais apropriada à situação e ao adversário. Comesse fim foi criada uma ferramenta de avaliação de jogadas baseada em CBR(“Case Based Reasoning”). Esta ferramenta baseia a sua escolha em dadosagregados sobre o desempenho passado de cada jogada. Para melhoraro desempenho de esta ferramenta, deve-se alterar a manutenção desta informação,por forma a ter mais informação sobre cada execução individualde uma jogada. Dessa forma poderá proceder-se a novos processos de análisee consolidação da informação.2 Objectivo da DissertaçãoInvestigação sobre o desempenho de um sistema baseado em CBR para a escolhade jogadas estudadas, em tempo real, numa equipa de futebol robótico.Desenvolvimento de uma ferramenta de armazenamento, análise e consolidaçãode informação de base do sistema de CBR.


Mtungaji wa kitabu:<strong>Al</strong> Habib <strong>Al</strong> <strong>Faqeer</strong> Ahmad Sheikh.ii.


Yaliyomo:No.Ukurasa.1. Yaliyomo……………………………………………. iii2. Dibaji (Sheikh Ahmed Haydar)……………………… iv.3. Utangulizi…………………………………………… vii.4. Mkombozi wa wajinga……………………………... 1.5. Miaka mia sita baada ya Nabii Isa (AS)…………. 6.6. Ukiwa wa baba na mama…………………………. 7.7. Ummul Muuminina Bi Khadija………………….. 8.8. Kubaithiwa Unabii………………………………… 9.9. Malinganisho………………………………………. 10.10. Bwana wa Mabwana………………………………. 12.11. Miungoni mwa sifa za Bwana Mtume SAW……. 17.12. Mkombozi wa Umma…………………………….. 21.13. Khayril Bashar……………………………………. 25.14. Utukufu wa Bwana Mtume SAW……………….. 27.15. Na Muombeeni Amani…………………………... 29.16. Nuru……………..……………………………… 39.17. Vitabu tulivyotoa….………...……………………… 41.iii.


Dibaji:بسمهللا الر حمن الر حيمTunamshukuru Mweyeenzi Mungu (SWAT) kwa neemazake nyingi sana kwetu zikiwemo neema ya Islamu alizokuja nazoBwana wa Mabwana Mtume Muhammad (SAW).Na kuletwa kwake hapa duniani ni moja ya neema zakekwetu sisi kama alivyosema katika Qurani takatifu Suratil <strong>Al</strong>Imraan:Qur an: 3:164.“Hakika Mwenyeezi Mungu amewaneemeshaviumbe alipowaletea Mtume miongoni mwao(Binadamu) anawasomea aya zake na anawatakasana anawafundisha kitabu na hekima...” .Mtume Muhammad SAW) ni Bin Adam kama sisi, lakini sifaalizosifiwa na Mola wale katika Qurani Takatifu hakusifiwa nazoyeyote yule miongoni mwa Bin adam wenzake. AmesemaMwenyeezi Mungu katika Qurani Takatifu Suratil <strong>Al</strong> Qalamakimsifiya Mtume Muhammad (SAW)Qur an: <strong>Al</strong> Qalam:68:4.“Hakika yako wewe (Muhammad) ni Mwenyetabia nzuri sana”.Tabia nzuri peke yake ndiyo iliyokuwa ni kivutiokilichowavutiya watu wengi, na kilichowafanya wampende,wamuamini na kumsadiki Mtume Muhammad (SAW) kablahajapewa Utume kwa watu wote na Unabii wa mwisho. <strong>Al</strong>izaliwayatima kwa kufariki baba yake kabla ya kuzaliwa. Malezi mazurihalisi alilelewa, na Mola wake.iv.


Qur an: 93:6.“Hakukukuta yatima, akakupa makazi Mazuri”.Sifa zote nzuri zinazohusika na tabia nzuri, kama vileUaminifu, Upole, Subira, Usamehevu, Ukarimu, na nyinginezo.Ndiyo akaweza kutatuwa kabla hajapewa Utume tatizo kubwalililoibuka wakati Makureysh walipotaka kuliweka “Jiwe TakatifuJeusi” mahala pake walipomaliza kukarabati Msikiti Mtukufu waMakka ilibaki kidogo wapigane. Hatimaye wakakubaliana kuwaaliweke Mtume Muhammad (SAW) kutokana alikuwa ni mtumuaminifu.Uaminifu wake ndiyo sifa ya pekee aliyompendeza Ummul<strong>Al</strong> Muuminin bi Khadija aliyemuowa kutokana na sifa hiyo,alipomfanyiya biashara zake na kumpatiya faida nyingi sana.Amesema Mwenyeezi Mungu katika Qurani Takatifu:Qur an:93:8.“Na akakukuta fakiri akakutajirisha”.Bwana Zayd bin Harithah bin Sherhabiyl (R.a) ni Swahabawake aliyemleya mwenyewe Bwana Mtume (SAW) nyumbanikwake kabla ya Uislamu. <strong>Al</strong>itekwa nyara bado mdogo na Majangiliwa Baniy Kasr mjini Makka. Kabla Bwana Mtume (SAW)hajapewa utume, na anaishi na mkewe wa pekee Bibi Khadija (R.a).Majangili hao wakamuuza katika soko ya watumwa ya mjini Makkailiyoitwa Ukaadh, na aliyemnunua ni Bwana Hakiym bin Hizaambin Khuweyliyd na kumpa shangazi yake, Bibi Khadija bintiKhuweyliyd mke wa Bwana Mtume (SAW) na mama wa watotowake.Baba yake mzazi Zayd anamtafuta mji wote wa Makkakijana wake aliyetekwa nyara na kuuzwa kama mtumwa naakanunuliwa na kuishi nyumbani kwa kwa Bwana Mtume (SAW)kabla hajapewa Utume na baada ya kupewa Utume. <strong>Al</strong>ipojulishwakuwa yupo nyumbani kwa Bwana Mtume Muhammad (SAW)anaishi naye, na watu wanamwita Zayd bin Muhammad - NaBwana Mtume (SAW) hawakatalii hivo - Isipokuwa Mwenyeeziv.


Mungu Mwenyewe ndiye aliyewakataza katika Qurani TakatifuSuratil <strong>Al</strong> Ahzab (33,4) alikwenda nyumbani kwa Bwana Mtume(SAW) na akamuona mtoto wake Zayd ameshakuwa Muislamu, naalimkataliya kwenda naye nyumbani kwake alikokuwa akiishi nababa yake na mama yake, baada ya kushauriwa na Bwana Mtume(SAW), na akaoneleya bora kwake yeye aendelee kuishi na BwanaMtume Muhammad (SAW) Na alipotaka kuowa Bwana Mtume(SAW) alimuozesha mtoto wa Shangazi yake, Bibi Zaynab bintJahsh (Ra) na kuzaa naye mtoto mmoja mwanamume aliyeitwa kwajina la Usama. Amesema Mtume Muhammmad (SAW) kuhusuUsama:أحة أطاِحإٌاص إٌي ‏ِاػذافا طّح“Usama ni kipenzi changu baada ya Fatma”.Kukataa Bwana Zayd (Ra) kurudi nyumbani kwa wazaziwake na kuendelea kuishi na Bwana Mtume (SAW), na watuwalitumiya jina la Bwana Mtume (SAW) kama ndiyo baba yake, nakumuozesha mtoto wa shangazi yake, ni dalili za wazi za utukufuwa tabiya na kustahiki kuwa Bwana wa Mabwana aliyeletwakutimiza tabiya zilizo bora:تؼ ثد ألذُّ‏ ‏ِىارَ‏ األخالقاٌٍُٙ‏ تزحّره اٌٛاطؼح إرحُ‏ صاحة ‏٘ذا اٌراٌيفاٌّؼيذ اٌّغفٛر ٌٗاٌشيخ احّذ تٓ‏ اٌشيخ إٌّشئ اٌّجٍض اٌؼٍٝ‏ اٌمادرٜ‏ ‏ٚافض ػٍيٗ‏ِٓ تزواذه أه ػٍٝ‏ وً‏ شئ لذيز ‏ٚتاألجاتح ج ديز<strong>Al</strong> habib Sheikh:Ahmad Haydar MwinyimvuaDar es salaam - Tanzania.vi.


بسمهللا الر حمن الر حيمUTANGULIZI:<strong>Al</strong> Hamduli-llahi <strong>Al</strong>ostahiki sifa nyingi zote, miungonimwa ambazo ni kubwa, hakuna kama kule kutuumba sisi WanaAdamu, na kututengenezea ambayo kuyahisabu si kazi rahisi hatakidogo.Na Rehma na Amani zake Mola zimfikie alojaa fadhilakama bahari kwa ukubwa na wingi wake, nae akiwa na funguo zote,Bwana Mtume Muhammad SAW na Jamaa zake wote, pamoja nawalomfwata, walofwata hadi kufikia siku ya malipo.Baada ya utukuzo wa jina la Mnyezi Mungu, sifa zake nakumtakia Rehma Mtume wake ambae ni kipenzi kwake, ni lazimanikiri si mimi tu bali kila Muumini kwa Bwana Mtume MuhammadSAW ni Naby wa mwisho, ambae kupelekwa kwake ni tofautikisehemu na Mitume ilomtangulia. Yeye amepelekwa kwa viumbewote. Isitoshe, amekhusishwa kwa uongofu na Dini ya KWELI ilikuidhihirisha wazi wazi juu ya dini zote.Qur an: <strong>Al</strong> Fat: 48:28.“Yeye ndiye <strong>Al</strong>iyemtuma, (<strong>Al</strong>iyemleta) Mtume wakekwa uwongofu na dini iliyo ya haki ili aishindishejuu ya dini zote na Mwenyezi Mungu anatosha kuwashahidi”Kupelekwa kwake kwa viumbe, zaidi ya kua kama shahidina mbashiria kheri na ya kuwafaa viumbe, na kama muonyaji, yeyeni Taa ya kung`aa.Qur an:Ahzab:33:45-46.vii.


“Kwa yaqini tumekutuma uwe shahidi na mtoaji wahabari nzuri na (tumekuleta uwe) muonyaji. Na uwemuitaji (wa watu) kwa Mwenyezi Mungu kwa idhiniyake na (uwe) taa itoayo Nuru”.Akiwa Mtume na Mjumbe wa Mnyezi Mungu alitofautiana nawenzie kwa mengi, yeye ni kiigizo chema juu ya viumbe.Qur an: Ahzab:33:21.“Bila shaka mnao mfano mwema (Ruwaza nzuri) kwaMtume wa Mnyezi Mungu kwa mwenye kumuogopaMwenyezi Mungu na siku ya mwisho na kumtaja MwenyeziMungu sana”.Hilo neno (Lakum) katika aya hiyo limeambiwa sisi,limehusishwa kwetu sisi, na hassa waumini katika viumbe naZAMAN za mwisho. Katika uzito wa maana zake inaonyesha wazikua lau kila mmoja alichukua tabia za Bwana Mtume SAWingeswiri watu wote kua kama mtu mmoja tu – Naby MuhammadSAW. Naye alikuwa na khulka ya Qur an.واْ‏ خٍمٗ‏ اٌمزاْ‏“<strong>Al</strong>ikuwa tabia zake kama Qur an”Hayo ni maneno aliyosema Ummul Muuminin Bi Ayshabinti Seyyidna Abu-bakaris Siddiq - R.a. alipoendewa na baadhi yaMaswahaba kuulizwa juu ya khulka ya Bwana Mtume SAW.Nabiyyil Ummiyyi:Kuja kwa Bwana Mtume SAW kama asiyejua kuandika walakusoma kiloandikwa:viii.


Qur an: <strong>Al</strong> Juma-a:62:2.“Yeye ndiye aliyeleta Mtume katika watu wasiojuakusoma, anayetokana na wao, awasomee Aya zakena kuwatakasa na kuwafunza kitabu na hikma(ilimu nyinginezo). Na kabla ya haya walikuwaKatika upotovu ulio dhwahiri”.Kuitengua sifa za wasomi, si wa zama hizo tu, bali wa zama ZOTEhadi kufikia kiyama. Na juu yake tumeambiwa:Qur an: <strong>Al</strong> Hashr:59:7.“…Na anachokupeni Mtume basi pokeeni, na anachokukatazaenijiepusheni nacho. Na muogopeni MwenyeziMungu; kwa yaqini Mwenyezi Mungu ni mkaliwa kuadhibu”.Na pia:Qur an:Nisai:4:80.“Mwenye kumtii Mtume amemtii Mwenyezi Mungu(kwani anayoamrisha Mtume yametoka kwa MwenyeziMungu)…”Katika kusemwa:Qur an:Yusufu:12:76.ix.


Ni wazi kua Bwana Mtume SAW amepewa Ilimu ambayohakupewa zaidi yake yeyote yule mpaka kufika kiyama. Na kwawalopewa Ilimu ndo wenye daraja kubwa mbele ya Mnyezi Mungu.Wapo baadhi ya watu mpaka leo ambao wanaona uzito kumwitaBwana Mtume SAW “Bwana” au “Seyyidna” .Kazi aloifanya katika kubalighisha Risala ya MnyeziMungu na kutufundisha Ilimu hii yote ilotapakaa, hakunaanaethubutu kusema ni ndogo. Pamoja na kusifiwa na wasiokuwaWaislamu kama wa kwanza katika watu mia waloleta mapinduzimakubwa katika kuwaendeleza Bin Adamu duniani, inawia ngumu,eti kumwita “Bwana” (Master au Lord) na hapo hapo kumuita <strong>Al</strong> hajAbubakkar Tafawa Balewa au Churchil, kama “Sir”, watu ambaowakilinganishwa wamefanza nini duniani hawafikii robo yaaliyoyafanza Bwana Mtume SAW. Hiyo isiwe ndo basi, lakini mtuafikie kukutolea uamuzi kua, kusema:“Ash-shahadu anla ilaha illa Llah wa Ash-haduanna Muhammada Rasulu Llah”.Au kusema:“<strong>Al</strong>lahu wa Rasulihi A`alam”Ni shrki.Neno “Bwana” ni wachache mno wasopendeleakunasibishwa nalo. Neno “Muadhamu”, na “Mtukufu” …. Kwaroho nyeupe tunayatumia mpaka hii leo (1988-89) kuwaitia waleambao Mnyezi Mungu amewaneemesha vyeo vya kidunia. Lakinilau utamnasibisha nayo Bwana Mtume SAW - <strong>Al</strong>lahu Akbarutatiwa kati husemi umeua!!Katika kijitabu hiki tumejaribu kwa kadiri ya ilmu yetuchache, kuonyesha kua Bwana Mtume SAW anastahili kuitwa“Bwana”. Mnyezi Mungu atunufaishe nacho.<strong>Al</strong> <strong>Faqeer</strong>,Ahmad Sheikh.x.


بسمهللا الر حمن الر حيمMKOMBOZI WA WAJINGA:Qur an:Zumar:39:9“…Je wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na walewasiojua?” Wanaotanabahi ni wale wenye akili tu.Ajabu katika ukweli wa mambo ni kwamba kila alimu anaemwalimu, wengi wetu. Lakini Bwana Mtume SAW alikuwaUmmiyyi (asiyejua kuandika wala kusoma, kilichoandikwa) mpakaalipofikia umri wa miaka 40. hapo ndipo alipoanza kufundishwa, naMnyezi Mungu mwenyewe kwa wasita tofauti na ule uliokusudiwahasa kwa viumbe:Qur an: 96:4.“..Amefundisha kwa wasita wa kalamu..”Lakini yeye ni kwa Roho Mtakatifu (Seyyidna Jibril A.S).“<strong>Al</strong>lamahu shadidul quwaa”.Matokeo yake ilikuwa kwamba Bwana Mtume alipata Ilimu ambayohakuna aliefikia robo yake. Na akafundisha ulimwengu mzimampaka leo hii.Malinganisho:1. Bwana Mtume SAW hakujua kuandika na kusoma tanguudogo wake - Wengi ya wa kileo huanza kujishughulishana Ilimu katika umri wa miaka 5, 6, hadi 7 na juu ya hivohakuna tegemeo la kupata robo ya Ilimu ya Ummiyyi(Illiterate) huyo.2. Bwana Mtume SAW alifundishwa na Mwenyezi Mungu kwa1.


Wasita wa Seyyidna Jibril A.S. – Kwa kiumbe mwingine kupatanafasi hiyo labda katika kufundishwa kutamka:Qur an:Ar-Rahman:55:3-4.……“..Amemuumba binaadamu..”… …“..Akamfundisha kutamka..”Na pia Il-ham kuhusiana na Furqan (Ilmu ya Upambanuzi).3. Bwana Mtume SAW – amewafundisha Majinni Ilmu naUislamu, na kwa uwezo mkubwa aliopewa pamoja naushujaa wa moyo alizungumza na viumbe vingine vyoteilipobidi.Wengi ya watu wasomi si wenye kumudu hayo, na penginekwa Imani dhaifu huenda akitokea kumuogopa Jinni au Mnyamamkali yeyote yule, kupita vile amuogopavo Mnyezi Mungu, na hayoni mambo ya ajabu mno.Kuja kwa Bwana Mtume Muhammad SAW duniani katikakarne ya sita baada ya Naby Isa A.S walimwengu duniani walikuwakatika giza zito la ujinga. Hakika hii haikanushiki kwa wajuaotarikh. Ilimu ya kila aina iko kwa Mnyezi Mungu. Naye ndiyeaiteremshae kwa viumbe kwa kupitia kwa Mitume – Ghalib.Katika zama hizo hizo mathalan aliyejua hakika ya duniaakatangaza kua ni Duara au inazunguuka aghlabu alihukumiwakufa. Kwa hio hakuwepo alimu yeyote wa kutokomeza ujinga ule,isipokuwa Bwana Mtume SAW. Mwenye fikra nzito ataona kua lausi Bwana Mtume SAW, sura ya walimwengu hii leo haingekuwailipofikia hata Kidogo.Seyyidna <strong>Al</strong>y bin Aby Twa-lib R.A akiwa kama lango la mjiwa ilmu (kutokana na hadithi aloisema Bwana Mtume (SAW):2.


أػطيد ػٍّا شرا فؼٍُ‏ اِزخ أْ‏ اػٍُ‏ إٌاص وافح ‏ٚػٍُ‏ اِزخاْ‏ أػٍُ‏ اٌخاص ‏ٚػٍُ‏ أِزخ أْ‏ ال اػٍُ‏ احادا“Nimepewa Ilmu koche koche, kuna Ilmu nieambiwaniwafundishe watu wote, kuna Ilmu nimeambiwaniwafundishe watu mahsusi na kuna Ilmu nimeambiwanisimfundishe mtu yeyote.”Inatutosha kuona mfano wa Ilmu kubwa alopewa katika hadithizake tu. Mwanachuoni mkubwa wa Kiislamu katika mambo yahadithi, Imamu Mohamed bin Ismail <strong>Al</strong>-Bukhar, aliekuepo bainamwaka 194 hadi 256 – (1215 - 1277AD), kwa jitihada yakealikusanya kiasi cha hadithi laki tatu (300,000) kati ya hizo,alizihifadhi laki (200,000). Katika juzuu kumi za vitabu vyake“Sahihi Bukhari” ameweka hadithi <strong>Al</strong>fu saba mia mbili na sabinina tano (7275) ambazo hazina shaka kabisa (Most anthentic ones).Wakati Imam Bukhari alihifadhi hadithi laki mbili, sisi wa kawaidatumo katika kuzitapia arubaini tu, zilosemwa kua ambayeatazihifadhi; basi huenda akaingizwa peponi; na papo nanga zingalizikikokota (Tazama Imam Nawawy- 40 ambacho vijana waUniversity – Dar es Salaam wamefanza jitihada kubwa kukifasirikwa lugha ya Kiswahili).Hatuna njia nyingine ya kuzidisha Ilmu baada ile alotuusianayo Bwana Mtume SAW:وٓ‏ ػاٌّا أٚ‏ ‏ِرؼٍّا اٚ‏ ‏ِظرّؼا ‏ٚالذىٓ‏ را تؼا فرٍٙه“Kuwa mwenye Ilmu, au mtafuta Ilmu, au MsikilizajiIlmu, Usiwe mtu wa nne utahiliki”Kama ile ya kuitumia (kuifanzia majaribio – Experimentation)kwani ndipo Mnyezi Mungu anapoingia kati ya mja akimfunuliazaidi:ِٓ ػًّ‏ تّا ػٍُ‏ ‏ٚرثٗ‏ هللا ػٍّا ٌُ يؼٍُ‏“Mwenye kuifanzia kazi Ilmu aloijua Mnyezi Munguhumrithisha Ilmu hakua akiijua”.Lakini ajabu ni kwamba baada ya Bwana Mtume SAWkutuelezahayo, bado tupo wengi wenye itikadi ziso na msingi4.


madhubuti mambo ya majaribio (Experimentation) ama ndani yamaabara (Laboratories) au nje, ni ya wazungu, kwa hiyo si yakujishughulisha nayo!!Kwa Muislamu ambae hajapata ukweli wa mambo badoataona hao wazungu kweli hayo ni mambo yao. Lakini ukweli nikwamba Ilmu ilioko Uropa leo ilipelekwa huko na Waislamu, nahata baadhi ya majina yamebaki mpaka leo vile vile katika Kiarabu:<strong>Al</strong> Kimya (Chemistry), <strong>Al</strong> jebra (<strong>Al</strong> gebra), <strong>Al</strong> musiqar (Music), <strong>Al</strong>ifBee Tee (<strong>Al</strong>phabeti) na kadhalika. <strong>Al</strong> habib Seyyid Umar binAbdallah mara nyingi akilipitia jambo hili kila alipozungumziamfano wa mada kama hizo popote duniani. Na akimtaja mno BishopGowa kama mmoja katika waandishi mashuhuri Uropa aliekikubalikua ni Waislamu ambao walipeleka Ilmu Ulaya.5.


Miaka mia sita baada ya Nabii Isa - A.S.Ni kutokana na historia ya maandishi au machimbo au yakupitia mdomo hadi mdomo, tunapata kujua yaliopita siku za kale.Inaaminika kua kati ya uzawa wa Naby Isa AS (Jesus Christ)na Muhammad SAW ilipita miaka mia tano na sabini na moja.<strong>Al</strong>ipokurubia kuondoka diniani huyo Naby Isa AS mwana waMaryam binti Imrani alinena kuwaambia Bani Israeli, manenoambayo yamehifadhiwa kumbukumbu yake mwenye Qur an kamahivi:Qur an:SUratil As saff:6:6.“Na (wakumbushe) aliposema (Nabii) Isa Ibn Maryam(Kuwaambia Mayahudi) enyi wana wa Israil mimi niMtume wa Mwenyezi Mungu kwenu nisadikishayeyaliyokuwa kabla yangu katika Taurati na kutoa habarinjema ya Mtume atakaye wajia nyuma yangu ambayejina lake litakuwa Ahmad (Muhammad na maanaya majina mawili yote haya ni moja. Maana yakemwenye kushukuriwa kwa maneno yake mazuri navitendo vyake vizuri na kila chake, kwani vyake vyoteni vizuri) lakini alipowajia kwa hoja zilizo wazi walisemahuu ni udanganyifu ulio dhahiri”Bishara ile ilidhihiri kweli; na hiyo ilikuwa miungoni mwa miujizayake Naby Isa AS. Kwa sababu miujiza sio yake mtu binafsi, bali niya Mnyezi Mungu.Mayahudi walijitahidi kila njia kupeleleza na kupangamauaji ya Mtume huyo kwa vile wao ndo walokijua ukweli wake,Lakini hawakufaulu; Bwana Mtume SAW alipatikana kamaalivyopanga Mwenyewe mwingi wa mipango Sub-hana wa Ta`ala.6.


Ukiwa wa Baba na Mama:Baba ya Bwana Mtume SAW, Bwana Abdullahi Ibn AbdulMut-Twalib alikuwa ameshafariki zama alipozaliwa mwanawe. Nakabla kubaleghe mama yake pia ilihama roho yake kurudi kwa Molawake.Bwana Mtume SAW alilelewa na babu na baadae Ammi yake,kama yatima pande zote mbili, lakini alitokea kua na adabu yamfano ambao, chambulecho <strong>Al</strong> habib Seyyid Umar:“Uliigizwa toka Cairo hadi China baadae”.Yeye alizidiriki baadhi ya zile sifa kumi zenye kujulisha mwenyeakili, angali akiwa mdogo:i. Upole,ii. Tafakkuri,iii. Ukweli.Upole na unyenyekevu. Ziloshamiri mno zikawavutia mnojamaa zake na wote alokutana nao, hakuna kama Ukweli naUaminifu. Kwa hivo alijulikana kama: “Muhammad Swa-diqulAmi-n” tangu utoto. Wakati alizungukwa na warongo na walaghai,yeye hakua kama wao. Wakati jamaa zake wakipendelea dhulma,uasharati, kamari na pombe, yeye aliepukana na matendo yale. Nawakati jamaa zake katika mazingira yao wakiabudu masanamu,yeye hakuwahi hata siku moja kuabudu wala kusheherekea karamuzao za kila mwaka. Kinyume yake yeye alikichukia kwa dhati yalematendo yao ya uovu hali ya kua mtoto.Utabiri wa Makuhani:Akiwa angali mtoto Seyyidna Muhammad SAWalionyesha sifa nyingi za utukufu. Na alipofwatana na Ammi yakeambae ni baba yake Seyyidna <strong>Al</strong>y Ibn Aby Twalib, katika misafaraya biashara kuelekea Sham, alionana na baadhi ya Makuhani waKinasara akatabiriwa kua Mtume alielezewa mwenye vitabu vyao.7.


Jambo hilo lilithibiti baadae alipofika umri wa miaka 40 lakini kamaalivotangulia kubashiri mwana wa Bi Maryam bint Imran:“Falama jaahu………..”Na kweli ndivyo alivokua.Ummul Muumini Bi Khadija Bint Khuwailid:Katika umri wa miaka 25 Bwana Mtume SAW aliacha kaziya kuchunga mbuzi kwa sababu aliajiriwa na Bi Khadija R.a kusafiri nabiashara kuelekea Sham. Kilichomvutia mno Bi Khadija R.a hakunakama ukweli na Uaminifu wa Bwana Mtume SAW .Twaba`an aliefwatana nae katika safari hiyo alietolewa naBibie awe kama mhudumu wake wa njiani – Bwana Maysara alizidishabaadhi ya maajabu aliyomuona nayo Bwana Mtume SAW, nayo piayalisaidia katika kumraghibisha Bi Khadija R.a aolewe nae.Qur an:Dhuhaa: 93:7-8.“Na akakukuta hujui kuongoza njia, akakuongoza.Na akakukuta fakiri akakutajirisha”.Bi Khadija R.a alimzidi Bwana Mtume SAW kwa miaka 15katika umri na lau baadae alioa wake kumi na moja, mmoja tu akiwando mdogo, yaani Bi Aisha Binti Seyyidna Abu-bakkaris Swidiq R.a.Lakini aliezaa nae watoto wengi ni huyo peke yake.Bi Khadija alibahatiwa watoto sita wawili wanaume; BwanaAbdallah na Qasim, na wanne wanawake: Bi Zaynab, Bi Rukiya BiFatmatiz Zahrai (hilo Zahrai kwa maana alieng`aa kwa kufanza Ibada –Rakaa alfu moj (1000) za Sunna kila siku mpaka kufa kwake, miezi sitabaada ya baba yake 632AD); na Bi Ummu Kulthumu, ambae pamoja naBi Rukiya walijulikana kama “Nureynin Naby SAW” na SeyyidnaOthman Bin Affan R.a kwa kuwaowa mmoja baada ya mwengine - Siochanjari.Mtoto wa saba wa Bwana Mtume SAW alitokana na UmmulMuuminin Maryatil Qibtwiyya R.a na aliitwa Bwana Ibrahim.8.


Kubaithiwa Unabii:Seyyidna Muhammad SAW alipotimia umri wa miakaarubaini aliteuliwa na kubaithiwa Unabii na Mjumbe wa mwishokatika ujao wa mitume ya Mnyezi Mungu:Qur an:Ahzab:33:40.“Muhammad si baba wa yeyote katika wanaume wenu,bali yeye ni Mtume wa Mungu na mwisho wa Mitume,Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu”.Na ndo kwa mara ya kwanza tangu azaliwe alitakiwa akariri baadhiya aya za Qur an zama Seyyidna Jibril As alipomtokea kwa sura zakutisha akamwambia asome:Qur an:`<strong>Al</strong>aq:96:1-5.“Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba. AmemuumbaMwanaadamu kwa pande la damu. Soma, na Molawako ni Karimu sana. Ambaye amemfundisha (binaadamuilimu zote hizi) kwa wasita (msaada) wakalamu; (zilizoandika vitabu, watu wakapata ilimu).Amemfundisha mwanaadamu (chungu ya) mambo alokuwahayajui”.9


Malinganisho:1. Miaka mia sita kabla kuja kwake alishatabiriwa na baadhi yawaja wema wa Mnyezi Mungu; na pia ikiwa mdogo alitabiriwana baadhi ya Makuhani kua Mtume. Mimi na wewe hatufikiiutukufu huo hata kwa miaka michache nyuma ya kuolewawazazi wetu. Baadhi ya watukukufu walitokea kupata fursa kamahizo.2. Bwana Mtume SAW akiwa yatima alitokea kua na tabia nzuri yakupigia mfano hassa:Qur an: Ahzab:33:21.“Bila shaka mnao mfano mwema (ruwaza nzuri) kwaMtume wa Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho nakumtaja Mwenyezi Mungu sana”.Qur an: Qalam:68:4.“Na bila shaka una tabia njema”.وفان تاٌؼٍُ‏ في األِي ‏ِؼجشذا فياٌجا٘اٌيح ‏ٚاٌرأدية في اٌيرُ‏“Inakutosheleza kua katika wakati wa jahiliakama ule, apatikane mtu ana Ilmu, ilikuwa nimiujiza peke yake. Ilikuwa ni miujiza tosha”.Na kupatikana adabu katika mtoto yatima katika wakati ule,ambapo watu walikuwa na ubeberu na itikadi za kuua binati zao10.


wakisadiki au wakiamini kwamba watakuja kufanza mambomabaya. Amma wakati mara nyingi yatima hulosa adabu aghlabu,haitegemewi hata angepata adabu kufikia ile ya Bwana MtumeSAW ambayo licha ya kusifiwa na watu ambapo ingehitaji kitabucha peke yake kuiandikia, lakini Mnyezi Mungu mwenyewekamsifia- Sisiwala tusiote ndoto kama hizo, kwani hazijalakiwa bado.3. Katika utoto wake hakusema uongo hata mara moja, hakuiba,hakua na sifa yeyote mbaya wala kuabudu sanamu aukusheherekea sikukuu zao. Sisi hatuna dhamana ya kusalimika,hasa ikizingatiwa akilini mambo ya watoto yalivo. Amma katikakuabudu, kwa mujibu wa neno “Ibada” linavyofahamika,hatukosi kuabudu Nafsi zetu, Mali, Wake, Watoto na kadhalika.Amma Mtume SAW hakuwa hivyo, kwa hivyo tunatofautianasana sana mno na yeye <strong>Al</strong> Mustafa.4. Bwana Mtume SAW alichaguliwa na Mnyezi Mungu awemjumbe wake wa mwisho; na alionana na Seyyidna Jibril (RohoMtakatifu) katika sura ambayo pamoja na kua kwake na Rohoya usafi kabisa alipata homa ya nderema. Mimi na wewe lautungekutana nae uso kwa macho, bila shaka yeyote hali ingezidiile ya Bwana Mtume SAW kwa zaidi ya mara kumi.11.


Bwana wa Mabwana:Mnyezi Mungu anatuonyesha vipi ilikuwa hali ya wale wanawakekatika karamu ya mke wa Mfalme Aziz walipomuona Naby Yusufkwa mara ya kwanza:Qur an:Suratil Yusuf:12:31.…“…Wakasema: Hasha lillahi! Huyu si mwanadamu;Hakuwa huyu ila ni Malaika Mtukufu”.Chambulecho <strong>Al</strong> Habib Seyyid Umar:“…Wamesema kua yeye si Bashari, Naby Yusuf. NaMnyezi Mungu kayaeleza ndani ya Qur an pasinakuyavunja. Hawa watu wanafikiri vipi, kwani Mtumeakiwa yeye si Bashari kama Bashari ndoumekwisha sema kua yeye ni Mungu. MnyeziMungu ni mwingine namna nyingine, watuwamejaribu kutaka kumvunja mtu huyu, makafiriwanamponda nawe unasaidia? Na watu ambaowasokuwa Waislamu wanamsemea!! Mtizameniyule nlokwambieni Bordley, mtazameni Carleyle,muandishi mkubwa, msemaji mkubwa waKiingereza. Ana buku lake “Heroes and heroworship”. Hero as a Profet – Akamtaja MuhammadSAW - As a Profet - Huna cha kumpondea Mtumehata kimoja Makafiri wamesalim amri…”Lakini yapo mambo mawili ya kuzingatia. Kwanza jambolilobashiriwa na Bwana Mtume SAW kua litatokea, basi hakunawa kulizuia. Yeye alisema utakuja wakati, watu watawalaumuwalotangulia (katika Maulamaa na kadhalika).Pili amesema:“Kila Umma ulikua na Fitna, na Fitna ya ummawangu ni Mali”.Basi kama mtu ameandikiwa Uongofu atafikiria mno – Manenoya Bwana Mtume SAW :12.


“Haamini mmoja wenu yeyote mpaka niwe mimi nimbora kuliko nafsi yake na mali yake …”Amesema Bwana Mtume SAW:“Anaa Seyyid auladu Adam walaa fakhar”“Mimi ni Bwana wa watoto wote wa Seyyidna Adam,wala sijifakharishi”.Ni wazi kua madam tunaamini kua alilotamka Bwana MtumeSAW halijatokana na matamanio ya nafsi yake, bali ni Wahyi – Nilazima tukubali kua – huo Ubwana alipewa na Mnyezi Mungu.Amma kwa kutokana na khulka zake amesema:“Walaa fakhar”.“Wala sijifakharishi”.Katika safari yake ya usiku mmoja ilopangwa na MnyeziMungu ili aonyeshwe baadhi ya maajabu ya Mola wake, alipoingiaEl Quds aliona Umma mkubwa. <strong>Al</strong>iambiwa na Seyyidna Jibril ASkua walikua ni Mitume yote ilotangulia. Na ilipokimiwa Salaakatangulizwa yeye kuwasalisha, ilionyesha wazi kua Cheo chake nikikubwa.Bwana Mtume SAW katika ofisi yake alikua Mfalme kamili,kwani yeye ndiye kichwa, utawala katika dola ya Kiislamu.<strong>Al</strong>ikuwa na wanavyuoni, Mawaziri, askari wa kivita, Khazina yaUmma wa Kiislamu, na Mahakama ambayo ilihukumu kwa mujibualivyoamua hakimu mkubwa Sub- hana wa Taala. Mahakama yakehaikutizama sura wala nasaba.Kutokana na tafhuma atayoipata mtu kutokana na pichaambayo ataipata kwa maelezo hayo peke yake, ataona kua hata hiyodaraja ya “Bwana” ilikua ni ndogo mno kunasibishwa nayo kamayeye.Na inapotokea mtu kupinga na kuleta aya zisolaikiana kabisakama zile za kusema eti ni: “Shirki kumtanguliza yeye katika baadhiya mambo ya Mnyezi Mungu”. Kama ya kuomba na kadhalika.Wakati anasema Mfano wa aya kama hii katika:Qur an: Suratit Tawba:9:99.13.


“Na katika Mabedui hao wako wanaomuaminiMwenyezi Mungu na siku ya mwisho, na wanaitakidikuwa wanayoyatoa ndiyo (sababu za)kuwasogeza kwa Mwenyezi Mungu, na za (kupatia)Dua za mitume. Sikieni! Hakika hayo ni(kweli kuwa ni) mambo ya kuwasogeza kwaMnyezi Mungu atawaingiza katika Rehma yake.Bila shaka Mwenyezi Mungu ni mwingi wa kusamehe(na) mwingi wa kurehemu”.Na katika sura hiyo hiyo:Qur an: Suratit Tawba:9:103.“Chukua swadaka katika mali zao uwasafishe nakuwatakasa kwa ajili ya hizo (Swadaka zao) nakuwataja kwa vizuri (mbele yangu) na uwaombeedua–Hakika kuwaombea kwako kutawapa utulivu(watengenekewe), na Mwenyezi Mungu ndiye asikiayena ajuaye”.Basi itaonyesha kule kukanusha kwake kumeambatana na jambojingine kabisa. Na si lingine, isipokuwa ni chuki.Basi hata hastahi kupaza sauti yake katika kusema: “ A!Muhammad ni mtu tu kama wewe!” Wale makafiri waliotamkamaneno kama hayo waliingia faragha kwa siri, kama ilivotokeakatika Surati:14.


Qur an: Ambiyai: 21:3.“Zimeghafilika nyoyo zao. Na wanasemezana kwasiri wale waliodhulumu (nafsi zao, wanaambizanahivi), ni nani huyu (Muhammad) isipokuwa ni Binadamutu kama nyinyi? Je, mnafika katika uchawi,(mnakiendea kiini macho) na hali nyinyi mnaona?”.Mtu kama hajajiuliza nafsi yake “Jee (kutokana na Ihsan)Bwana Mtume SAW angekuwa mbele yake angemfurahisha kwasuala kama hilo?”. Na huku anaambiwa kua Mtume ni bora kulikomuumini yeyote yule, na si ruhusa kuoa mkewe yeyote baada yake,kwa vile wake zake Bwana Mtume SAW ni mama wa waumini, jeeyeye Mwenyewe atakua ni nani kwetu?Lau tungetaka tuone mwenye Qur an kila jambo, basiingehitajia mara tatu bahari saba ziwe wino. Mathalan MnyeziMungu kaonyesha manufaa ya nyuki katika Jamii ya vidudu venyekuruka kwa mbawa, basi tuonyeshwe na Barkoa nae manufaa yake,na nyigu, kipepeo na kama hao!! Hiyo ingekuwa inda, na akilizimekosa kazi!.Unyenyekevu:Wakati Mnyezi Mungu alipoamrisha kuchinja, haijakua namaana kua anahaja ya damu kuinywa wala nyama kuila, lakini uleunyenyekevu wetu ambao hua ni Taqwa ndio unaomfikia yeye.Tizama vile makafiri walivojibu walipoambiwa watoe miungonimwa vile walivyoruzukiwa na Mnyezi Mungu:Qur an Suratil Yasin: 36:47.15.


“…Tuwalishe (tuwaruzuku) ambao Mwenyezi Munguangependa angewalisha yeye Mwenyewe…?”.Sisi hatutaraji kua hivo, lakini kama ni wapinzani basi mtu siangepinga suala la “Bwana” kwa Bwana Mtume SAW, lakiniangepata nafasi nzuri kutaka kusemea ibada ya kulizunguka jiwe, nakwenda mbio baina Safaa na Marwa, kusimama Arafa na jua kalilote lile pale ni kama upumbavu tu, na kufunga sio lazima, ilainapotokea shida ya uhaba wa chakula, basi watu wanawezakufunga ili kusevu chakula kisiishe haraka.Malinganisho:1. Inaaminika kua Bwana Mtume Muhammad SAW alizidiuzuri kuliko Naby Yusuf AS tafauti yao ni kwamba uzuriwa Bwana Mtume SAW hakuweza kutamanika. Lakini leo,lau utamnasibisha Bwana Mtume Muhammad SAW naMalaika, na lau ni kweli amewazidi Malaika eti utaambiwasi shirki tu bali ni kufru!.2. Dua ya Bwana Mtume SAW kwetu ni muhimu mno mbeleya Mnyezi Mungu kwa ukurba na kujibiwa, chambulecho<strong>Al</strong> Habib Seyyid Umar:“Huwezi kuondoka tu umwambie Mnyezi MunguAstaghfiru Llah Sharti wende kwa Mtume,umwambie nimekuja ya Rasulullah niombeekwa Mnyezi Mungu”. \Sisi hatukupewa cheo, na daraja kama hiyo.3. Katika Surat Anbiya 21:3 makafiri walikaa kandowakanong`onezana kwa siri, kusema: “A! Muhammad ninani, mtu tu kama wewe!”.4. Katika sifa za Bwana Mtume SAW zilivoandikwa kwenyeBiblia. Ameonyeshwa wazi wazi kua yey ni Mfalme wawafalme, Bwana wa mabwana!.Sisi eti sifa hizo hatikubaliani nazo kwa sababu ni Shirki.16.


Miungoni mwa sifa za Bwana MtumeMuhammad SAW:Walomsifu Bwana Mtume SAW wakiwa ni mabingwawa fanni nyingi za ilmu hawakufika mwisho. Akili za wenye akilihazikutatanishwa na jambo lolote zito kama suala la Bwana MtumeMuhammad SAW (<strong>Al</strong>ayhis swala-tu was salaam). Miungoni mwasifa chache tu za Bwana huyo ni:1. Kapokea Wahyi toka kwa Mnyezi Mungu.2. kakamilika kwa tabia njema.3. Mikono yake ilijaa barka na ilitoa chem chem za maji.4. Hakua na kivuli.5. Hakua na athar alipotembea kwenye mchanga.6. Uso wake ulijaa Nuru.7. Kati ya mabega yake alikua na Muhuri ulokitoa Nuru.8. Haukujulikana urefu wake.9. Haukujulikana upeo wa nguvu zake.10. Ameoa wake wengi kwa Rukhsa ya Mnyezi Mungu.11. Akimtangulia kila Mtu kumtolea salam.12. <strong>Al</strong>ikuwa akicheka katika kila maudhi alofanyiwa yeye.13. <strong>Al</strong>ikuwa akighadhibika katika kila lilokua la kumuudhi<strong>Al</strong>lah.14. Jasho lake likinukia badala ya kunuka.15. Akiona mbele yake kama nyuma, pembeni na chini yake.16. Akiona gizani kama mwangani.17. Hakupata kumnyanyasa masikini.18. Hakuwa mwenye kukataa jambo la sawa.19. Akishauriana na watu katika mambo mengi.20. <strong>Al</strong>ikisali mno Sunna za usiku mpaka ikivimba miguu yake.21. Akiwapenda mno yatima.22. Akiwatumikia ahli zake kwa haraka haraka.23. <strong>Al</strong>ikitolewa salam na mawe na miti kila alipoipitia.24. <strong>Al</strong>izungumza na Paa (Ghazzali).25. <strong>Al</strong>isubiria misuko suko yote kwa ajii ya dini ya MnyeziMungu.26. <strong>Al</strong>iwahutubia Majinni juu ya Uislamu.27. <strong>Al</strong>ionana na Mitume yote ilopita.28. <strong>Al</strong>iona pepo na moto na Malaika wenye kuzisimamia.17.


29. <strong>Al</strong>iona mengi mfano wa Kursy, Arshi, Hijabu, na Nuru zarangi ambazo hapa duniani hazipo kabisa.30. <strong>Al</strong>imuona na kumpanda Buraki.31. <strong>Al</strong>iiona dunia katika dhati ya umbo lake la awali na sasa.32. <strong>Al</strong>iona mifano ya watu katika hali ya adhabu zao yawmulqiyamazitakavokua.33. Akisali alipotoka usingizini bila kua na haja ya kutawadha.34. <strong>Al</strong>ikua yakilala macho yake, moyo ukimsab-bih Molawake.35. <strong>Al</strong>ifutiwa dhambi zake zote zilotangulia na zilofwatanyuma yake.36. <strong>Al</strong>ikifanza kazi zake kwa mikono yake.37. <strong>Al</strong>ikua Muadilifu.38. <strong>Al</strong>ikua akipenda kutoa – Sakhii.39. <strong>Al</strong>ikua akiwaandikia barua Wafalme akiwataka wasilimu(ambao hawakua Waislamu).40. <strong>Al</strong>ijenga umma wa Kiislamu na Dola ya Kiislamu.41. <strong>Al</strong>itabiri ambayo ni miungoni mwa yalona-sib wakati wamwisho kabisa.42. Amepasuliwa kifua chake na kusafishwa uchafu wa moyowake.43. Akila alipokuwa na njaa tu, mara moja kila siku tatu.44. Hakuinama alipopita popote pafupi.45. Akiwapenda Mafakiri na Masikini na kukaa nao.46. Akifatwa nyuma na Malaika wa Kiruhani.47. Akirai mno ahadi.48. Hakuzidiwa na yeyote kwa ushujaa.49. Hakuzidiwa na yeyote kwa Ilmu.50. Hakuzidiwa na yeyote kwa Akili.51. Hakuzidiwa na yeyote kwa Busara.52. Hakuzidiwa na yeyote kwa Taf-huma.53. Hakuzidiwa na yeyote kwa Imani.54. Hakuzidiwa na yeyote kwa Taqwa.55. Hakuzidiwa na yeyote kwa Unyenyekevu.56. Hakuzidiwa na yeyote kwa upole.57. Hakuzidiwa na yeyote kwa haya.58. Hakuzidiwa na yeyote kwa utulivu.18.


59. Hakuzidiwa na yeyote kwa ustahamilivu.60. Hakuzidiwa na yeyote kwa Urahimu.61. Hakuzidiwa na yeyote kwa Kuridhia.62. Hakuzidiwa na yeyote kwa Hikma.63. Hakuzidiwa na yeyote kwa Kuabudu.64. Hakuzidiwa na yeyote kwa kumjua Mnyezi Mungu.65. Hakuzidiwa na yeyote kwa Kujijua Nafsi yake.66. <strong>Al</strong>isemeshwa na chakula kilichotiwa sumu.67. Hakupendelea mali wala dunia.68. Hakupendelea ujinga pamoja na kua Ummiyyi.69. Akipenda kufikirifikiri mara nyingi.70. Akipenda ukweli hata katika mizaha.71. <strong>Al</strong>iepukana na kila aina ya uchafu.72. <strong>Al</strong>ipendwa hata na adui zake.73. Hakuogopa chochote illa Mnyezi Mungu.74. Hakupata kutuliwa na nzi mwilini.75. Kanzu yake haikueka mstari kiunoni hata mara moja.76. <strong>Al</strong>ikua na khulka ilonasibiana na kitabu cha MnyeziMungu.77. Akitoa na kupokea kwa mkono wake wa kulia.78. <strong>Al</strong>ikua akiombea mno umati wake na hasa walokufa.79. Akiwapenda jirani zake hata Yahudi.80. Akizuru wagonjwa.81. Akienda kuzika maskini.82. Akimpa alomyima.83. Akimfikia aliyempiga pande yeye.84. Akihudhuria alipoalikwa na maskini.85. Hakua akieka undani au kinyongo.86. Akiwahurumia sana kina mama hasa wafiwa na waumezao.87. <strong>Al</strong>iwakomboa wanawake kutoka katika unyonge.88. Akija-hid kuondosha ubaguzi na Ubwana.89. Akipenda kueka usawa kati ya watu.90. <strong>Al</strong>ikuwa rafiki ya wote, na kila mmoja alikua akiona yeyendiye rafiki yake mkubwa.91. Hajapata kuhudhuria harusi hata ya Binti yake.92. Watu wakisilimu kwa wema wake.19.


93. Ni jemedari hodari wa vita.94 Katokana na wazazi walotwahirika na uchafu wa ainayeyote.95. Akiwaamrisha wakeze kuwahudumia majeruhi vitani.96. Akishika gao la mchanga akitupia adui vitani kamaguruneti.97. <strong>Al</strong>ieka udugu mzito kati ya Islamu na Islamu.98. <strong>Al</strong>ikuwa mkweli tangu utotoni.99. <strong>Al</strong>ikuwa Mwaminifu.100. <strong>Al</strong>ikuwa Mfaswaha na mwenye hoja kali.Katika jumla ya sifa hizo, na aitazame mwenye kutizama,aseme yeye anayo moja yeyote tangu udogo wake bila kukosananayo hata mara moja.Hizo ni miungoni tu mwa sifa za Bwana Mtume SAW, siozote. Na papo ingemuhitaji mtu wa Taqwa kubwa sana kuhozibaadhi yake kwa taabu pia.20.


Mkombozi wa umma ulimwenguni:Mtu yeyote mja mwenye akili akikaa kitako kimya kwatadabburi ilo nzito kidogo kuyapima mambo jinsi yalivokuwa miaka1500 iliyopita hatakosa kuona picha yenye mifano kama hiiifwatayo:-Kijana katika nyumba yake anao labda wake watano, wanne,watatu au wawili. Kama ni watatu, basi mmoja ni mama yake mzazina wawili ni mama zake wa kambo. Kama kawaida labdaungemuuliza, angekwambia: “Hawa wake zangu nimewarithi kwababa yangu”.Mmoja kati ya wawili amejifungua mototo wa kike, naeamembeba akiwa na jembe anakwenda kumzika mzima mzima. Nakila aliemuona basi, licha ya kumkongowea lakini wanamsifiakamwe kua hatua aloichukua ni ya kikabaila na kiungwana hasa.Masikini ameenda kukopa kwa mwenye kujiweza na bintiyake kigori, anamwacha pale hadi ambapo angelipa ile deni; katikajumla ya shuruti, ni ile ya riba kiasi maalumu kila alipochelewakulisalimisha deni lile.Mwingine mwenye nguvu amemtwaa kwa nguvu mdeni wakealiechelewa kumlipa mpaka zikamfikia mara tatu, nne juu, kwahivyo amepitisha hukumu kumuuza hadharani.Mtu amefikwa na balaa yeyote ile, anajitupa chini ya sanamula bahati mbaya akiliomba limuondoshee au lisimamishe mikosiyake juu yake, na alipoondoka hapo aliondoka na imani mpya kuamambo yamekwisha.Upande mwingine kundi la watu wakiwa na furaha,wamemtwaa binti mzuri, wamemvalisha vizuri, wamempandishajuu ya farasi aliepambwa vile vile, wanamsindikiza binti huyokumtoa muhanga kwa mungu mkubwa. Hapo penye sanamu pakiwandio mwisho wa maandamano, yupo mchinjaji maalumu; hiyo ndiyokazi yake, kila mwaka. Baada ya waadhi mfupi msichana yulehulazwa kifudi fudi chini ya sanamu na kukatwa kichwa chake kwapanga kali sana nyuma ya shingo yake.Mandhari ya mgeni akitanga tanga kutafuta ambaeangemsaidia kupata mali yake aloiweka amana kwa mzalendo.Mwenye nguvu ameamua kumuua dhaifu, kwa sababu yakumvunjia hishma yake. Labda yule dhaifu anayo haki yake kwake,21.


lakini ameenda kuitaka wakati yeye alikuwa ndani ya starehe zakesaa zile.Mwingine amemuasi mkewe, amemuweka kwenye kibanda,si wa chakula cha maana wala nguo. Yeye hana haja nae walahamuachi, bali akimuacha hivo hivo hadi kufa.Mtu mwingine amerundika pombe na wanawake anastarehekwa mali ya yatima ambao hawajui lolote, na pengine wa katikadhiki kubwa hapo kwao.Kundi la watu limeacha kazi zao kumzunguka mshairiakimsifu mwenye pesa, na Fulani bin Fulani, huku wakianguavicheko na kudhihaki.Wengine wameeka rubaa kuzungumza juu ya biashara, wizi,na vita. Silaha gani waongeze, na farasi wangapi zingepaswakununuliwa; pengine kikoa hichi kingerudiwa siku kadhaa wakadhaa kabla kuwafikiana.Mtu mwingine anaburuzana na mwanamke kwa nguvuhadharani na pengine amemjeruhi na kumchania nguo. Juu yakupiga kelele na kuomba msaada, waapi! Hakuna ambaeangeshituka hata kidogo.Mmoja miungoni mwao ameinuka akiwa aliyechukizwa mnona tabia za kinyama namna zile. Akasimama imara pamoja nakuonwa eti ni mwenye kujisumbua nafsi yake bure. Kusimamadhiddi ya wengi waovu? Mbona ni sawa na kujitia katika mamboyasokuhusu ndewe wala sikio? Yamekuhusu nini, si kungojautendewe wewe?Siku ya kwanza na ya pili ya kutetea kwake haikua sawa nasiku ya tatu na zilofwata. Walikuwepo kama yeye ambao hawakuawakipendelea mambo yale, lakini walikua wamejificha na saa hiyobasi walijitokeza wakajumuika.Kila siku nguvu yao ilikizidi na kuzidi mpaka kufikia hatuaambayo uonevu ulipungua, na dhulma ikawa kama ngeni.He! Taratibu yakaanza kutoeka na kusambaratika. Matendoyote yale yalo kionekana kua ya kawaida sasa yakawa hayapokabisa. Mihanga ya kuuawa wasichana kila mwaka ikatoweka, kwasababu hapajakuwepo tena ismu ya sanamu.Tabia ya kuzika binati wadogo mara walipozaliwaikasimama na kupita, ikabaki ni hadithi tu ambazo hazikuaminikamara moja hivi. Mandhari ikaonekana ya kistaarabu badala yakishenzi na kinyama nyama. Na pengine yule yule alie akiabudu22.


mungu wake kutokana na tende yake mwenyewe, lakinialiitengeneza sanamu, alipoila tende katika wakati ule wamabadiliko makubwa aliangua kicheko kikubwa. <strong>Al</strong>iuhisiupumbavu wake wa zamani zilizopita akajiona kama aliepigahatua kubwa na muhimu sana katika maendeleo ya bin Adamuduniani.Mtu alijihisi kua na uhuru uliokamilika hasa, kwanihakuogopea mali yake kua ingepokwa au kuhatarika saayeyote ile ya mchana au usiku.A!! pongezi ilioje!! Sifa aina gani ungestahili eweuliosimama imara kuondosha udhalimu ukaleta maisha ya rahakama haya!!. Ikiwa jaza ya hisani ni hisani, basi tungemuita“Bwana” yule hadharani kushauriana pamoja, tungeamuakumfanyia nini “Bwana” yule?.Lakini badala ya kukubali yote ambayo waliamua kumpakama tunzo kubwa la heshima, yeye aliwaambia: “Malipo ya pekeeambayo nnayataka toka kwenu ni kusema kwenu: Laila-ha illaLlah yamekwisha”. Mfadhili huyo, si Mwingine isipokua niBwana Mtume Muhammad Sallal lahu <strong>Al</strong>ayhi Wasallam.Kazi aliyofanya akiwa kama taa ilowashwa na MnyeziMungu katika wakati uliofaa hasa, uliacha dunia nzima iliokuagizani (Dark ages) ubakie kwenye Nuru.Qur an:Ahzab: 33:45-46.“Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu! kwa yakini sisitumekutuma (tumekulete uwe) shahidi na mtoaji wahabari nzuri, na muonyaji. Na uwe muitaji (wa watu)kwa Mwenyezi Mungu, kwa idhini yake, na (uwe) taaitoayo nuru”.Kazi aliyofanya ikanufaisha ulimwengu mzima, ni ambayosi ya kusahaulika tu, bali hakuna, wala hatatokea mfano wake wakumudu kuifanya mpaka mwisho wa dunia.23


Basi ikiwa kwa kazi kuu kama hiyo mahakama ya waamuzi,wameona hastahili kutunukiwa heshima ya Mtawala mkuu,Maulana, jina la heshima la mtu wa cheo kikuu Fulani (Lord) nahali wanapewa ambao kwa malinganisho ya kazi walizofanya hata sirobo. Pia wameona haifai kutunzwa heshima ya Bwana au Sharifu(Sir), wakati wamepewa duniani baada yake kwa kazi ambazo sikubwa.Na pia hawezi kupewa Bwana, Fundi, Stadi, Mjuzi (Master),cheo cha mwisho kabisa ambacho kibinadamu watu wanapeanatena bila lolote wala chochote. Basi mahakama ya waamuziwangempa cheo wakifikiriacho wao kua kingemfaa kwa kazialioifanya.24.


Khayril Bashar:Kutokana na jinsi watu wafanzapo zile kazi zao kwa ustadiuliokithiri, maarifa ya wengine kwa kawaida huruka tukasema“Yule bwana ni Stadi, Mwalimu mkuu, (Professor)!”, Ammaanapoitenda kwa kinjia ambayo mtu mwingine wa kawaida hawezikuifikia, basi husema “Bwana yule amebahatiwa (Gifted)!”. Naakitokea kufanza kazi fulani kiajabu kupita kiasi, husema “Bwanayule ni Mchawi!!”.Amerika na baadhi ya nchi nyingine za Uropa ziliwachukuakarne kadhaa za kutawaliwa mpaka kuja kupata uhuru. Hivi hivibaadhi ya nchi za Asia na Afrika. Na baada kujitawala ilichukuamiaka mingi sana kudumisha mataifa yao.Bwana Mtume Muhammad SAW ilimchukua miaka ishirinina tatu kufikiza ujumbe wa Mnyezi Mungu duniani. Na katika mudahuo huo alikomboa dunia nzima kutoka katika giza zito. Ndani yamiaka 23 alielimisha watu, <strong>Al</strong>itengeneza Umma, na kujenga dola yaKiislamu duniani.Katika tabaka mbili za watu:1. Waumini wa kweli walifurahikiwa mno kuona kua BwanaMtume SAW alitimiza kazi alokabidhiwa na Mola wake.2. Wapinzani wa haki walimtafutia waloweza kumtafutiawakamsambikizia kusema “a! hakua Muhammad ila nimchawi; Mshairi, na mtu tu kama watu wengine”.3. Hakika ni kitu cha mwisho kila siku. Na katika kupimiamambo kwa adala, wakati ni hakika kwamba tumuonapo mtukakwea katika vituko viovu, basi humwita Firauni auShetwani au Afiriti!. Amma akiwa shujaa mwenye nguvu,basi hutumia jina Simba au Chuma cha Pua au Jabali!!. Yotehayo ni kutokana na kushindwa kufikia mfano wake katikakumuigiza.Amma Bwana Mtume SAW sifa zake tu hakuna aliefikiakikamilifu kuziigiza – Lakini hakuna jina lolote lililotolewa.Matendo yake, na kazi kubwa aloifanya katika miaka ishirini natatu, hakuna mpaka leo alomudu kuitenda na papo hakuna jina.Wapenzi wake wenye akili timamu, na ilmu zenye upeo wahaja hasa, wamepima wakamsema“Muhammad ni Mtu lakini Si kama watu wengine”Ajabu ni kwamba wengine imewachoma kiasi chaKuyapima maneno hayo kwa ijtihada zao, na njia zao wakatoa fatwa25.


kua kawli kama hizo ni Shirki. “Mtu Fulani ni kama Simba auMulku Sleyman bin Daud”, Hayo si mazito. “Fulani mtukufu,Muadhamu, ni wa pekee!!” Hayo si shirki!!.Watu hawa walau ya kua na ilmu, wanapofikia uamuzi kamahuo, hua na lengo gani nyuma ya Bwana Mtume SAW?. BwanaMtume SAW amehofia mno ulamaa wanapoigeukia dunia,wakaipenda, na wanapovutika kwa MALI!!!Na tumuombe Mnyezi Mungu kwa Jaha ya Bwana MtumeSAW atuingize katika hekma zake na atuzidishie Ilmu pamoja nakuturuzuku fahamu, kwani bila ta-fuhma njema Ilmu haijasimama.Wa sallal Lahu wa Sallam alaa khayru khalqillahiKulli-himi Sydna MUHAMMAD.26.


Utukufu wa Bwana Mtume MuhammadSAW:اٌحّذ هلل رب اٌؼاٌّيٓ‏ اٌذٜ‏ ارطً‏ ‏ٔثيٕا ‏ِحّذ رحّح ‏ٌٍؼاٌّيٓ‏‏ٚجؼً‏ اِرٗ‏ خيز اِح أخزجد ‏ٌٍٕاص أجّؼيٓ.‏ ثُ‏ اٌصالج‏ٚاٌظالَ‏ػٍيٗ‏ ‏)خيز خٍك هللا(‏ ‏ٚاٌٗ‏ ‏ٚصحثٗ‏ ٚ )ِٓ ‏ٚاالٖ(‏ اٌراتؼيٓ.‏Amma baad.Utukufu wa Bwana Mtume Muhammad SAW hauhitajimaelezo yenye sherehe ndefu, kwani uko wazi kabbisa, labda kwamtu alopungukiwa na Imani ndani ya moyo wake na kadhalikamahaba.Tungependa kwa umoja wetu tuzungumzie juu ya aya mbili tokaSuratil Ahzab.Ya kwanza:Qur an: Ahzab:33:43.“Yeye (Mwenyezi Mungu) ndiye anayekurehemuni, naMalaika wake (wanakuombeeni dua) ili kukutoeni katikagiza (kwa kukupelekeni) katika nuru, naye ni mwenyekuwarehemu sana Waislamu”.Inataka mtu azingatie sana aweze hata kujiuliza yeye ana kitugani muhimu mno hata afikie Mnyezi Mungu, Kumswalia - Yaanikumrehemu- na Malaika wa Mnyezi Mungu washughulikekumuombea dua ili atolewe kwenye giza aekwe kwenye Nuru? Nikwa kitu gani kikubwa mno hassa hata ufanyiwe yote hayo? Unapembe za chuma, una panga za Radi?27.


Just find out, for what specific reason should<strong>Al</strong> Might God, bless you and so His Angels?Bila shaka ukiweza kulipata jibu, utatulia na kuzidisha Ihtiramuyako kwa Mola wako.Aya ya pili:Ni ile iliyoko kwenye:Qur an: Ahzab:33:56.“Hakika Mwenyezi Mungu anamteremshia RehmaMtume na Malaika wake wanamuombea dua kwavile vitendo vizuri alivyovifanya). Basi enyi Waislamu(mliopata neema hii ya kufundishwa haya na Mtume)Msalieni (Mtume, muombeeni Rehma) Na muombeeniamani”.28


Na Muombeeni Amani:‏ِحّذ ٚ اٌٗ‏صٍٝ‏ ػٍٝ‏ اٌٍُٙ‏ ‏ٚاٌذيٓ‏ ‏ِا تذا تٗ‏اٌشزع شزع احّذ وثذر فٝ‏ وّاٌٗ‏تذا جّاي اٌّصطفٝ‏ اٌُ‏ ذز جثّأٗ‏ذّاَ‏ اٌحً‏ الِغ تزؤيح حثيثٗ‏ثُ‏ اٌّحة ػاشك دػاْ‏ فٝ‏ ‏ِٕٙاجٗ‏جٍيً‏ جاء تٍٙذٜ‏ ‏ِا فٝ‏ اٌٛرٜ‏ وّثٍٗ‏حٍيُ‏ حاس حٍّٗ‏ أثيائٗ‏خراَ‏ خيار خٍك احّ‏ ذ اال ألجً‏ خٍمٗ‏‏ٌٛالٖ‏ ‏ِا تذا اٌٛرٜ‏ ‏ٌمائٗ‏‏ِزادٔا ‏ِحّذ ‏ِحّٛدٔا ػذٔاْ‏ اصً‏ جذٖ‏‏ٔٛر األٔاَ‏ صفٛٔا ػٍٝ‏ إٌثٝ‏ ٚ اٌٗ‏ثُ‏ اٌصالج ‏ٚاٌظالَ‏ ‏ٚاٌصحة ‏ِغ ذثاػٗ‏يؼُ‏ آي اٌّصطفٝ‏ Sheikh Abdul Qadir Jaylan (QSA) amefikia kusema:٘ٛ اٌّخرار اٌذٜ‏ فاق وً‏ شيء‏ٌٚٛال هللا ‏ِؼثٛد ‏ٌيؼثذ“Yeye ndo Mteule Mtengwa ambaye amekipita kilakitu na lau si Mnyezi Mungu kuwa ndo Muabudiwaangeabudiwa thamma angeabudiwa (yeye <strong>Al</strong>Mustwafa)”.29.


Imam Mohamed Busry amesema:ٌٛ ‏ٔظثد لذرٖ‏ اياذٗ‏ ػظّاأحٝ‏ اطّٗ‏ حيٓ‏ يذػٝ‏ دارص اٌزُِ‏“Lau lingenasibishwa jana lake katika Utukufu naukubwa, basi lingetosha jina lake tu peke yakekufufua mifupa ya maiti ilogeuka mchanga”.Qur an:“Annaby aula bil Muuminina min anfusihim”“The greatest of man”Sheikh Yusuf <strong>Al</strong>y katika translation yake ya Qur an kwa kiingerezaanasema:“God and his Angels honour and bless the Holyprophet as the greatest of Men. We asked tohonour and bless him all the more, because hetook upon himself to suffer the sorrows andaffliction of this life in order to guide us toGod`s mercy and the highest inner life”.Katika kuambiwa hapa kua:“Mnyezi Mungu na Malaika wana muenzi, wanamuheshimu kamamkubwa kuliko watu wote… Ni bora kuliko watu wote nk”.Ipo dalili kubwa yenye maana nzito.30.


Amemuadabisha kwa matendo mazuri mpaka yeye mwenyeweakamsifu:Qur an:<strong>Al</strong> Qalam:68:4.“Kwa hakika ni mwenye tabia njema”Na amejaalia kila anapotajwa Mnyezi Mungu pia anatajwa nayeye: Qur an:<strong>Al</strong>am Nashrah:94:4.“Na tukaunyanyua utajo wako”.Kwa watu waliokomaa akili na mahaba kwa Mtume wao, BwanaMtume SAW vile alivotupenda sisi kweli kweli – Kunaonekanawazi katika kawli yake Mnyezi Mungu katika aya za mwisho zaSuratil Tawba.Qur an:Tawba:9:128.Amekufikieni Mjumbe aliye jinsi moja na nyinyiyanamuhuzunusha yanayokutaabisheni, anakuhangaikieni(na) kwa walioamini ni mpole na mwenyehuruma”.Yule asiyekuwa na Ilmu yenye kuangalia kwa macho mawili twabaanhapo hawezi kuona kitu, kwa hivyo atakidhibisha nakukanusha haya – Lakini baada ya Mnyezi Mungu kutwambia kua:Tusiwahisabu wale waliofishwa wakiwa katika kuitetea dini yaMnyezi Mungu kua wamekufa, basi imekwea imani ni itikadi yaAshikina kua Bwana Mtume SAW yuko hai kama mwanzo.Aya hiyo haijamalizikia kwa Masahaba peke yao, laa hasha;bali, hata sisi yale yanayotutaabisha yana muhuzunisha pia. Kwavipi? Kwa sababu amali zetu za kila siku zinapitishwa kwake na hiloni jambo la ajabu sana kwa wale ambao akili zao ni nzima sio walewanaoangalia mauti kwa jicho moja – Kwa sababu mioyo ya watu31.


kama hao imejaa maarifa ya khulaswa kua Bwana Mtume SAWalizaliwa Makka na kupewa Utume hapo Makka. Na akaha-jirkwenda Madina. Wao hawana khabari yeyote juu ya undani wakauli yake Mnyezi Mungu:Qur an:<strong>Al</strong> Imran:3:169.“Wala usiwadhani wale waliouawa katika njia yaMwenyezi Mungu kuwa ni wafu (maiti). Bali wahai, wanaruzukiwa kwa mola wao”.Na yataacha wapi kumuhuzunisha mambo yetu wakatianasema kua zile amali zetu zikisha onyeshwa kwake naeakaziangalia:“Nikizikuta za kheri, basi namuhimidia Mnyezi Mungu,na nikizikuta zisokua za kheri nawaombea Maghfirakwa Mnyezi Mungu” .Jee mtu aliyekwisha kufa yumo ndani ya kaburi penginemifupa imeshageuka mchanga (na lau ardhi haili miili ya Mitume)ana haja gani na wakosaji walo mwenye uhai wa duniani?Wewe hushituki kuona kua kila uvutapo makamba yako,Bwana Mtume SAW awe anazilegeza kwa kukuombea Maghfirampaka hii leo?!! <strong>Al</strong>lahu Akbar!!.Aya mbili za ndani ya Suratil Ahzab ni lazima zimpe shidayule anaesimama kidete kupinga Swalaatu alan Naby SAW na hukuakidai kua yeye ni Muislamu, Muislamu wa nani? Chambulecho <strong>Al</strong>Habib Seyyid Umar Mwinyi Baraka!!Katika kazi kubwa aloifanya Bwana Mtume SAW ni kulekuibainisha ile Qur an kwetu ili tuweze kuifahamu baraab-bar yalematakwa yake. Mnyezi Mungu ameteremsha Qur an naam, lakiniKuibainisha ilikua kazi ya Bwana Mtume SAW.32.


Qur an: <strong>Al</strong> Nahl: 16:64.“Na hatukuteremsha kitabu (hiki Qur an) isipokuwauwabainishie yale ambayo wanakhitalafiana, na(pia kiwe) uwongozi na Rehma kwa watu wanaoamini”Kwa aya hizo na nyinginezo mfano wa hiyo ni yenye kuonyeshakua ipo haja ya kuona jinsi gani alivobainisha kwetu haya ya Quran. Na hilo halipatikani ila ndani ya hadithi zake Bwana MtumeSAW ambazo zimehifadhiwa madhubuti kabisa.Na yote aliyoyasema Bwana Mtume SAW bila shakayamesemwa na yeye Mnyezi Mungu na ndo maana akatwambiakua:Qur an:An Naisa: 4:80.……“Mwenye kumtwii Mjumbe (wa Mwenyezi Munguyaani Bwana Mtume SAW) bila shaka (atakuwaamemtwii Mwenyezi Mungu…”Vile vile Mnyezi Mungu anasema katika Qur an:Qur an:An Nisa:4:115.33.


“Na atakaemuasi Mtume baada ya kumdhhirikiaUongofu na akafuata njia isiyokuwa ya Waislamututamgeuza alikogeukia mwenyewe na tutamuingizaJahannamu napo ni mahala pabaya kabisa pa mtukurudia”.Yeyote mwenye akili nzima ni lazima aone kua kabla yakuletwa Bwana Mtume SAW hakuna aliyejua lolote kuhusu sheriaza Mnyezi Mungu. Kutokana na yeye <strong>Al</strong> Mustwafa SAW ndiotumejua Shahada mbili na Kalimati Tawheed. Kusimamisha Swala,Kutoa Zakaat, Kufunga na Kuhiji Makka.Hangekuwa Bwana Mtume SAW kutubainishia juu ya mambohayo kinaga naga leo hatungeweza kuutekeleza Uislamu kwasababu Qur an haikubainisha vipi kutoa Shahada na nini cha kusemandani yake, vipi kukaa tahiyaatu na ya kusema ndani yake, vipikutoa Salaam – na nini la kufanya endapo mtu amepitiwa ndani yaSwala au amepunguza au kuzidisha jambo – na kama hayo, ambayoQur an peke yake haitoshelezi.Hayo ambayo hayakuelezwa ndani ya Qur an, baliyamebainishwa na Bwana Mtume SAW wewe huyataki!! Basiunaswali kivyako?Namna gani tutatoa Zakaa na mali ziko za namna kwa namna,pamoja na kubainishiwa, Zakaa zinatolewe Ramadhani hadiRamadhani hata kama mtu ameanza biashara miezi mitatu tu nyumaya Ramadhani; na papo atampa Muislamu jina la Pagan, Mshirikinana kadhalika. Au atatoa kwa kufwata sura za watu; na pengineasiwe na haja kabisa ya watumikiao zile Zakaa nk. Bwana MtumeSAW.Na hiyo Hijja ndo kabisa pamoja na kutajwa juu ya kutufulakini haitoshi kufahamisha vipi na namna gani. Kwa hiyo lazimapawepo haja kubwa ya kumfwata Bwana Mtume SAW. Na ambayeana muasi, basi atakua anamuasi Mnyezi Mungu, na amuasiyeMnyezi Mungu huyo si Muumini wala si Muislamu – na hukmuyake ni kukatwa kichwa.Tukirudi katika Mada kuhusu Aya ya 43 na 56 ya Suratil Ahzab,tutaona kua hakuna tofauti ya maana illa ile ya kutakiwa sisitumtakie Rehma na Amani Bwana Mtume SAW. Lakini kamaMnyezi Mungu na Malaika wanamtakia yeye (<strong>Al</strong> Mustwafa)Rehma, basi pia Mnyezi Mungu na Malaika wake wanatutakia sisiRehma sasa ugomvi unakujaje mpaka wengine wasimame kati ya34.


Mnyezi Mungu na watu kuzuia jambo la kuswaliwa Bwana MtumeSAW isemwe kua ni Bid-a au jambo lisilofaa?Wale wale wenye kupinga Swalatu alan Naby SAW lazimawawe na hoja zao amma kwa Muraaja`a kwa vile imesha semwakuaQur an:An Nisa:4:59.….…..“Na kama mkikhitalifiana juu ya jambo lolote basilirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume”.(Ambapo hao hawathamini ya Mtume ndo kusemawanaitoa sehemu nzima ya aya hiyo – ambapo nihatari).Na wajitazame ule msimamo wao katika aya kama ile isemayoQur an:<strong>Al</strong> Ahzab:33:36.“Mwislamu mwanaumme wala Mwislamu mwa-Namke hana khiyari katika mambo ambayoMwennyezi Mungu na Mtume wake wameshakidhia(kata shauri/Hukmu)juu yake…..”.Qur an inampa Mtume SAW fursa ya kupitisha hukmu na sisitunasimame kati kuiangusha fursa hiyo. Sijui mshindi atakua nani!!Chambulecho <strong>Al</strong> Habib Seyyid Umar Mwinyi Baraka:-“Wazungu – Orientalists sio Waislamu wamemsemeavizuri kweli kweli, wewe Muislamu unungana naMakafiri kumpinga – Kumpiga vita Mtume?!!”35


Haya wanayoyafanya hawa wenye kumpiga vita Bwana MtumeSAW waelewe kua wanafanya ya kumuudhi Mnyezi Mungu badalaya kuitetea Dini na kumtetea Mtume wake. Hebu na aangalie mtukauli ya Mnyezi Mnugu.Qur an: Hashr:59:7.……“…Na anayokupeni Mtume chukueni, na anayokukatazeninayo, basi yawacheni…”.Na kauli zake Bwana Mtume SAW:‏ٌمذذزود ‏ٌىُ‏ ‏ِا أْ‏ ذّظىرُ‏ تّٙا فٍٓ‏ ذضٍٛااتذا اٌمزاْ‏ ‏ٚطٕرٝ‏“Bila shaka nimekuachieni vizito viwili Qur an naSunna zangu – ambapo mkikamatana navyo, basihamtapotea abadan”.Ajitazame mtu huyo kweli atakua Mwislamu kwa kuyaacha yaBwana Mtume SAW? Laa ilaha Illal Llahu. Basi kila mtu anajionaNafsi yake – Na Mnyezi Mungu anatwambia.Qur an:An Nisa:4:115.“Na atakaemuasi Mtume baada ya kumdhhirikiaUongofu na akafuata njia isiyokuwa ya Waislamu36.


tutamgeuza alikogeukia mwenyewe na tutamuingizaJahannamu napo ni mahala pabaya kabisa pa mtukurudia”.Na haya hawayaoni? Ikiwa wao ni wenye kufwata Qur anbasi yaloandikwa mwenye ya hiyo si mengine bali ni Qur an. Nahuyo Rasuli aliyetajwa hapo ni Bwana Mtume Muhammad SAW.Na wala hicho kipande kinachomwelezea yeye hajakipachika yeye –kwa sababu hakuna awezae kuleta mfano wa Qur an hata aya moja –na hiyo ni Open challenge - yeyote anaeweza kutoa hoja zake naatoke mbele aje aeleze, na aite mashahidi wake, asiyekua MnyeziMungu. Na thama hawatafanza hivyo na hawawezi na hawatawezakufanza hivyo, basi na wauchelee huo moto ambao kuni zake niwatu na mawe.Qur an:Baqara:2:23.“Na ikiwa mna shaka kwa hayo tuliyomteremshiaMtumwa wetu (kuwa hakuteremshiwa na MwenyeziMungu), basi leteni sura moja iliyofanywa na (mtu) aliyemfano wake, na muwaite waungu wenu bighairi ya MwenyeziMungu (wakusaidieni); ikiwa mnasema kweli”.Qur an:Baqara:2:24.“Na msipofanya – na hakika hamtafanya kamwe –basi uogopeni moto ambao kuni zake ni watu na mawe,uliowekewa makafiri”.37.


Mnyezi Mungu ametoa mara tatu mifano kama hiyo ndani ya Quran na aya nyingine ni:Qur an:Israil:17:88.“Sema: hata wakikusanyika watu (wote) na Majinniili kuleta mfano wa hii Qur an, basi hawangaliwezakuleta mfano wake; hata kama watasaidiana (vipi)wao kwa wao”.Bwana Mtume SAW anasema:“Ambae hamstahi Mnyezi Mungu, basi na afanze ayatakayo.Hiyo siyo ruhusa lakini, ni fumbo.Wafaqqanallah ala maa yuhibu wayardha.38.


بسمهللا الر حمن الر حيمNuru:Nuru ile ile ilong`aza ndani ya pango la Hirandiyo hiyo hiyo ilosambaza Waislamu Dunia nzimaleo, na kesho na bila kutarajiwa kukoma au kutindikajambo hilo hadi kiyama.Kesho – zama Nuru ilipoingia ndani yaMapales na kung`za kwa mmoja wao mfano waMarmadulle Pickthall - 1913 - Lord G. Bennerd Shawalipoendewa ili atoe ushauri juu ya namna ya kufaakuuzuia Uislamu kuzidi kuzagaa, yeye aliwaambia:–“…Kama vile Uislamu ulivyoingia England leona ndivyo hivo hivo kesho, na hakunaataeuzuia...”“…Like Islamu has entered England today andso tomorrow and no body should stop it!!.”Na kweli ilishindikana mpaka leo miaka 85 imepita.39.


Muharram 1429 - January 2008.Toleo la kwanza <strong>Al</strong>l rights reserved First addition.40.


Vitabu vilivyokwishatoka ni:*1. Maana halisi ya Imaan. (i) (1 st , 2nd & 3rd addition).*2. Njia nyepesi ya kuijua nafsi yako.*3. Njia nyepesi ya kujua kitu juu ya uongofu.*4. Knowledge vision & ecstacy.*5. Mwinyi Baraka katika ulimwengu wa kiislamu (i) .*6. Waislamu na Sayansi - Ulu-m.*7. Kuhifadhi Burda.*8. Maana halisi ya Imaan (ii).*9. Muhammad SAW katika ulimwengu wa ghayb.*10. Siri ya Balaa.*11. El makhlouq (Viumbe)*12. Njia nyepesi ya kujua kitu juu ya uongofu. (2nd addition)*13. Manaqib ya <strong>Al</strong> habbib Sayyeid <strong>Al</strong> Ma`aruf.*14. Some aspects of concepts of facility in medevial IslamicPhilosophy by Mwinyibaraka.*15. Njia nyepesi ya kuijua Nafsi yako. (2nd addition).*16. Sayyidna Muhammad SAW Bwana wa Mabwana.Vitabu ambavyo tunategemea kuvitoa muda si mrefu(Insha <strong>Al</strong>lah) ni:*1. Waislamu na Sayansi - Ulu-m. (2nd addition)*2. Mwinyi Baraka katika ulimwengu wa kiislamu (i) . 2 nd . Add.*3. Muhammad SAW katika ulimwengu wa Ghayb.Kwa maulizo kuhusu vitabu wasiliana nasi:Majaalis El Ulaa - El Qadiriyya Sinza,P.o. Box 15170,Tel: 0747 483 553Tel: 0748 595 958.Tel: 0744 023 703.Tel: 0741 235 091.Tel: 0744 299 597.Dar es salaam.41.


Ujumbe waAhly Majaalis:Assalam <strong>Al</strong>aykum:Ndugu Msomaji lengo la kitabu hiki siyo biashara;Madhumuni makubwa ni kuwa Waislamu wanufaike namafundisho ya Dini yao, kwani si wengi waliobahatika kupataIlmu ya madrasa eidha ukubwani au wakati wa utoto wao.Kutokana na gharama za uchapishaji kuwa kubwa ndiyoimetubidi tukiuze kitabu hiki ili kufidia gharama na tuendeleekutoa vitabu vingine.Kama Muislamu yeyote atakuwa yuko tayari kutoagharama za uchapishaji ili avitowe bure au kwa kuviuza kwagharama nafuu vitabu hivi, basi sisi tuko tayari. Awasilianenasi ili tufanikishe hilo kwa ajili ya <strong>Al</strong>lah.42.


<strong>Al</strong> habib <strong>Al</strong> <strong>Faqeer</strong> Ahmad Sheikh Mohamed Sheikh Msiha, amezaliwaSingida mkoa wa Dodoma, mwaka 1938. Amepata elimu ya sekula Unguja naamebahatika kupata elimu ya juu katika chuo maarufu Afrika ya MasharikiMakerere Uganda.Elimu yake ya Dini ameipata hapo hapo Unguja toka kwa Masheikh mbalimbali, baadhi yao ni:Sheikh Sleiman <strong>Al</strong>wi (Muhib Rasul) (<strong>Al</strong> Marhum).Sheikh Seyyid Mansab.Maalim Himid (<strong>Al</strong> marhum).Maalim Hemed Muhamed El Buhry.Sheikh Seyyid Qamus.Sheikh Muawwiya Ibn Abdul Rahman.Sheikh <strong>Al</strong>ly Muhamed Comorian.Sheikh Ibrahim Mzee Ahd.Sheikh Haj Mzee Ahmad Msiha.Amma Elimu ya Nafsi na Roho Amepata Ijaza yake toka kwa A`limu mkubwaDuniani <strong>Al</strong> Habib Sayyid Omar Bin Abdallah (Mwinyi Baraka).Sheikh Ahmad amewahi kufanya kazi katika jeshi la Polisi Tanzania Barakatika mikoa mbali mbali mpaka alipostahafu.Katika umri wake wote Sheikh Ahmad alijahid katika kuendeleza Uislamukwa kusomesha na kuandika vitabu vya mada na maudhui mbali mbali katikaUislamu. Pia alianzisha Majaalis Sehemu mbali ambazo ziko mpaka leo, Mtaawa Pemba, Sinza, Bungoni, kijito nyama, Sadani (Ilala) na Kibaha (Misugusugu)ambapo ndipo ilipo Dhwarihi yake (alipozikwa).Sheikh Ahmad ametwawafu 27. 8. 2001. ( Mwezi 7 jumadda thany 1421H.R.). Akiwa na umri wa miaka 63, vile vile alivyokuwa akiomba aishi umri uleule alioshi kipenzi chake Bwana Mtume Muhammad SAW.Insha <strong>Al</strong>lah Mnyezi Mungu amjaze kheri na alitie Nuru kaburi lake(Amin).Majaalis El Ulaa El Qadiriyya,Sinza Dar es Salam.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!