Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Na wale ambao zama Sheytwani anapowashika hukumbuka basi<br />
saa hiyo hiyo huwa wanaona (Mno) akili ndo huwa macho,<br />
ikamkumbuka na kumtaja Mnyezi Mungu.<br />
Na azingatie mtu juu ya vitu ambavo tunadai tunavijua mno na<br />
kutokana na kuvijua huko na mazoeya tunahisi ati havitupi taabu hata<br />
kidogo: Radio, Tepu, Tv, Magari, Kamera, Taa za Stimu, Kompyuta,<br />
Mobitel, Inter-net na kadhalika: jee viliteremka moja kwa moja toka<br />
Mbinguni kama mvua?.<br />
Hili ni suala tosha kukuwezesha kuichemsha Akili yako ambayo<br />
labda unatumia sehemu yake moja tu ya – kumi na sita (1/16). Daima<br />
usipoichemsha, itabaki hivyo hivyo mpaka kiyama ambapo itaonekana<br />
kua ulipewa Akili lakini hukuitumia!!.<br />
Sifa za mwenye Akili:<br />
Mnyezi Mungu aliyetukuka amejaalia kila kitu kua na swifa zake<br />
kwa makusudio maalumu ili kipate kujulikana kwa wepesi na<br />
kutambuliwa kwa njia iso na shaka hata kidogo. Halikadhalika Akili nayo<br />
imepewa swifa zake maalumu ambazo zinakujulisha wazi kua mwenyewe<br />
ni mtu mwenye Akili.<br />
Hizi ndo swifa za Akili kutokana na mafunzo alofundisha Bw.<br />
Mtume SAW, katika hadithi iliyopokelewa kutokana na Bi. Aisha (R.A)<br />
hakika amesema:-<br />
Akili inayo Swifa kumi (10) kati yake zimegawika ndani ya mafungu<br />
mawili:- Dhwahiri na Batwin.<br />
Dhwahiri Ni zile zilizo wazi wazi kabisa mtu akiziangalia anaziona,<br />
nazo ni :-<br />
1. Swamt: yaani ukimya, Bw. Mtume SAW katika Swifa hii<br />
pia amesema kua: “ Mwenye kuzidisha maneno yake<br />
basi huzidi kuanguka kwake” (Speech is Silver,<br />
Silence is Gold) (Kusema sema ni fedha na<br />
kunyamaa ni dhahabu – kinaong`arisha.)<br />
21.