You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
DIBAJI<br />
“Asiyeridhika na hukumu yangu, basi na<br />
awe na mola asiyekuwa mimi”.<br />
Kupendwa na Mwenyenzi Mungu kwa njia ya kuteremshiwa mabalaa na<br />
misukosuko ni moja wapo ya neema zake ambayo inazalisha ndani yake<br />
neema nyinginezo zilizo nzuri na muhimu kwa maisha ya muumini hapa<br />
duniani, ikiwemo neema na sifa ya subira. Na subira kama alivyosema Mtume<br />
Muhammad (SAW):-<br />
ا لصثز نصف ا ال ى مان<br />
Sote tunaelewa kuwa Mtume Muhammad (SAW) ni kipenzi cha<br />
Mwenyeenzi Mungu kuliko watu wote. Na katika historia ya maisha yake<br />
kama Mtume wa Mwenyeenzi Mungu alifiliwa na mke wake wa kwanza bibi<br />
Khadija RA na kufuatiliya kufa ami yake na mlezi wake Bwana Abiy twaalib<br />
katika mwaka mmoja. Na Bwana Mtume aliusiya kwa kuwita mwaka huo ni<br />
mwaka wa huzuni.<br />
Na alipokwenda mjini Twaaif katika mwaka huo huo kuwahubiriya watu<br />
wake ujumbe wa Mwenyeenzi Mungu wa Dini ya Islam walimpiga mawe na<br />
kuukataa. Na kwa kuwa ni kama alivyoamrishwa na Mwenyeenzi Mungu<br />
katika Qurani Takatifu Surat <strong>Al</strong> Ahkaaf kuwa awe mwenye subira: Qur an<br />
46:35.<br />
“ Subiri (ewe Muhammad) kama walivyosubiri Mitume<br />
Uwlu-<strong>Al</strong>-Azim. Nao ni: Mitume Nuhu, Ibrahim, Mussa<br />
na Isa (AS)”v<br />
Subira aliyokuwa nayo Mtume Muhammad (SAW) ndiyo iliyokuwa<br />
moja wapo ya silaha aliyotumia Mtume Muhammad (SAW) katika<br />
kuufanikisha kwa kuufikisha ujumbe wa Mwenyeenzi Mungu kwa watu wote<br />
kama Nabii wa mwisho na Mtume kwa watu wote.<br />
Mwenyenzi Mungu amkubaliye <strong>Al</strong> Marhuum Sheikh Ahmad Sheikh wa<br />
Majaalis – Sinza athari yake hii aliyetuachia na nyinginezo kwa manufaa ya<br />
ndugu zake Waislam, na alijaaliye Kaburi lake (Kibaha ) bustani miungoni<br />
mwa mabustani ya peponi- Amin.<br />
v<br />
Ahmad Haydar Mwinyimvua,<br />
Dar es salaam Tanzania.<br />
14 Ramadhani 1424,<br />
9 November, 2003.