17.02.2015 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Halkadhalika masikini na mahakimu nao wana mitihani yao.<br />

Watu wanne hao tumewaonyesha kwa kuwa wao ndio nguzo<br />

zilokamatia ulimwengu jinsi vile alivyosema Bwana Mtume SAW.<br />

Kwa ujumla Mnyezi Mungu hukinga balaa zetu na<br />

hupunguza ghadhabu zake kwetu kwa ajili ya swadaka. Basi jambo<br />

hilo lingefaa lidumishwe kwa sababu faida zake ni za kuonekanwa<br />

kwa macho hasa, na mambo yetu yamghadhibishayo Mnyezi Mungu<br />

ni mengi. Mambo haya wapo wengi ambao hawana habari nayo<br />

pengine hizo swadaka huchukulia kuwa ndiyo ZAKA.<br />

Lakini tofauti ni kule kuwa swadaka ni ya hiyari, na zaka ni<br />

ya lazima. Swadaka unaweza kumpa mtu yeyote, lakini zaka ni<br />

lazima muislamu anaestahiki kule kupata zaka. Amma sivyo<br />

itakuwa haijaswihi na utakuwa hutahisabiwa kuwa umelipa, na<br />

itabidi kuirudishia tena.<br />

Insha <strong>Al</strong>lah Mnyezi Mungu atuwafikishe katika<br />

kheri tuongokewe kwa yetu, sisi na waislamu wenzetu.<br />

Na tuweke matumaini ya dhati kuwa tutajibiwa kwa<br />

lolote tunaloliomba. Na ndio maana Mnyezi Mungu<br />

akatuambia kuwa: Hadithil Quds:<br />

“Lau wangekusanyika pahala pamoja watu<br />

wote wa mwanzo na wa mwisho, binaadam<br />

na majinni kila mmoja akaomba alitakalo<br />

kwa Mnyezi Mungu katika shida zake, basi<br />

Mnyezi Mungu angempa kila mmoja na<br />

isingekuwa imepungua chochote katika<br />

hazina yake”.<br />

Labda kiasi kile kile cha uzi uliotumbukizwa baharini,<br />

ukanyonya maji na kushirabu barabara.<br />

Huyo ndiye Mnyezi Mungu aliye mkarimu mno na mwenye huruma<br />

isiyomithilika kwa viumbe, Mkwasi mwenye kuneemesha waja wake<br />

atakavyo, wengine anawakunjulia wengine anawakadiria.<br />

Mambo yote tuloyataja na kufahamisha ndani humu ni yake<br />

na kule kuyatekeleza na kuyafuata ndiyo maana ya uislamu.<br />

Qur an 3 : 83<br />

13

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!