Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Halkadhalika masikini na mahakimu nao wana mitihani yao.<br />
Watu wanne hao tumewaonyesha kwa kuwa wao ndio nguzo<br />
zilokamatia ulimwengu jinsi vile alivyosema Bwana Mtume SAW.<br />
Kwa ujumla Mnyezi Mungu hukinga balaa zetu na<br />
hupunguza ghadhabu zake kwetu kwa ajili ya swadaka. Basi jambo<br />
hilo lingefaa lidumishwe kwa sababu faida zake ni za kuonekanwa<br />
kwa macho hasa, na mambo yetu yamghadhibishayo Mnyezi Mungu<br />
ni mengi. Mambo haya wapo wengi ambao hawana habari nayo<br />
pengine hizo swadaka huchukulia kuwa ndiyo ZAKA.<br />
Lakini tofauti ni kule kuwa swadaka ni ya hiyari, na zaka ni<br />
ya lazima. Swadaka unaweza kumpa mtu yeyote, lakini zaka ni<br />
lazima muislamu anaestahiki kule kupata zaka. Amma sivyo<br />
itakuwa haijaswihi na utakuwa hutahisabiwa kuwa umelipa, na<br />
itabidi kuirudishia tena.<br />
Insha <strong>Al</strong>lah Mnyezi Mungu atuwafikishe katika<br />
kheri tuongokewe kwa yetu, sisi na waislamu wenzetu.<br />
Na tuweke matumaini ya dhati kuwa tutajibiwa kwa<br />
lolote tunaloliomba. Na ndio maana Mnyezi Mungu<br />
akatuambia kuwa: Hadithil Quds:<br />
“Lau wangekusanyika pahala pamoja watu<br />
wote wa mwanzo na wa mwisho, binaadam<br />
na majinni kila mmoja akaomba alitakalo<br />
kwa Mnyezi Mungu katika shida zake, basi<br />
Mnyezi Mungu angempa kila mmoja na<br />
isingekuwa imepungua chochote katika<br />
hazina yake”.<br />
Labda kiasi kile kile cha uzi uliotumbukizwa baharini,<br />
ukanyonya maji na kushirabu barabara.<br />
Huyo ndiye Mnyezi Mungu aliye mkarimu mno na mwenye huruma<br />
isiyomithilika kwa viumbe, Mkwasi mwenye kuneemesha waja wake<br />
atakavyo, wengine anawakunjulia wengine anawakadiria.<br />
Mambo yote tuloyataja na kufahamisha ndani humu ni yake<br />
na kule kuyatekeleza na kuyafuata ndiyo maana ya uislamu.<br />
Qur an 3 : 83<br />
13