You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
DIBAJI<br />
بسم<br />
هللا الر حمن الر حيم<br />
Tunamshukuru Mwenyeenzi Mungu kwa fadhila zake na neema zake nyingi<br />
sana zisizohesabika. Na Swala na Salaam zimfikie Mtume Muhammad (SAW)<br />
pamoja na ali zake na awaridhiye maswahaba wake wote – Amin.<br />
Amma Baad : Amesema Mola katika Quran takatifu surati <strong>Al</strong> Ankabuut:<br />
Qur an 29 : 1 – 3.<br />
“Watu wanadhani kuwa wataachiwa pindi wakisema kuwa<br />
tumeamini bila ya kupata misukosuko. Hakika tuliwatiya<br />
katika misukosuko wale ambao waliyokuwa kabla yao wao,<br />
kwa yakini mwenyeenzi Mungu atawatambulisha wale walio<br />
wakweli na atawatambulisha wale ambao ni warongo”.<br />
Ni katika moja ya hekima zake Mwenyeenzi Mungu katika kuwapima waumini<br />
kwa viwango vya imani zao kwake yeye kwa kuwaletea aina mbali mbali za<br />
misukosuko na mabalaa. Na ingawa anavijua Kabla ya kuvipima viwango hivyo.<br />
Na Mwenyeenzi Mungu anafanya hivyo kwa kudhihirisha mapenzi yake kwa<br />
anayemleteya misukosuko na mabalaa, kama alivyosema Mtume Muhammad<br />
(SAW):<br />
ان هللا اذااحب عبدا ابتاله فاذاصبر نجاه واذارضا اصطفاه<br />
(Hakika Mwenyenzi Mungu akimpenda mja humpa mabalaa<br />
na kama akisubiri anamuokowa nayo na akiridhika nayo<br />
humchaguwa (kuwa mja wake wa karibu).<br />
Kwa hivyo basi, muumini wa kweli amewajabika kuridhika na hukumu ya<br />
Mwenyenzi Mungu kwake yeye hata ikiwa ina uchungu wa namna gani. Amesema<br />
Mtume Muhammad (SAW) katika <strong>Al</strong>-Hadithi <strong>Al</strong>- kudsiyy;<br />
من لم يزض تقضاى فا لىتجذر تا سوا ى<br />
iv