You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
بسم<br />
هللا الر حمن الر حيم<br />
SIRI YA BALAA:<br />
Bin Adam hana pahala ambapo hupata utakaso wa moyo kama<br />
anapofikwa na balaa. Mfano ambao ameuelezea Mnyezi Mungu<br />
mwenyewe ndani ya Qur an hakuna kama ule anapotokea mtu kuwamo<br />
ndani ya chombo baharini na ghafla ikaanza mchafuko wa hali ya hewa.<br />
Dharuba toka kila upande, mawimbi mazito na makubwa kama mlima<br />
hakuna nchi yeyote karibuni bali ni bahari pana tu, ambayo mwisho wa<br />
mandhari yake mtu kila upande ni ile ya maji kukamatana na mawingu<br />
tu. Mandhari hiyo lau tofauti ni ndogo na ile ya siifu (khasf: yaani:<br />
“ Quick sends” ), ambaye anayetumbukia ndani yake hukiona kifo ni<br />
chenye kumvaa bila ubishi wowote, lakini mtu hujiona kabisa anakufa<br />
na kukata tamaa ya kunusurika kama aliyoipitia Edmond Dause.<br />
<strong>Al</strong>isema:<br />
“The angry waves and the sight of dangerous<br />
rocks told me that death was near. and the<br />
thought of death made me afraid. I used all my<br />
powers as a man and as a sea man to ascape.<br />
But I did so because I was happy, because I<br />
didn`t coated death, and because I didn`t<br />
wish that I, a living thing made by the service<br />
of God, should became food for the birds and<br />
beasts of the sea……..”.<br />
“mawimbi ya ghadhabu na mandhari ya majabali ya<br />
hatari yaliniambia kuwa kifo kilikuwa kimekaribia, na<br />
mawazo ya kifo yalifanza niogope. Nilitumia uwezo<br />
wangu wote kama mwanamme na baharia hasa, ili<br />
kuikwepa ajali hiyo. Lakini nilifanya hivyo kwa sababu<br />
nilikuwa na furaha; kwa sababu sikuwa nimefunikwa na<br />
kifo. Na kwa sababu sikutegemea kuwa mimi kiumbe<br />
chenye uhai uliotengenezwa kwa huduma yake Mnyezi<br />
Mungu, nije kuwa chakula cha ndege na wanyama wa<br />
baharini…“<br />
1