You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
بسم<br />
هللا الر حمن الر حيم<br />
UTANGULIZI<br />
<strong>Al</strong>-hamdullilahi wal khayru wash-sharru bima<br />
shiyati Llah. <strong>Al</strong>lahu mma swalli a`laa habibika Seyyidna<br />
Muhammad wa alih waswahbihi ajmaina wat tabi ina lahum<br />
biihsa nin ilaa yawmid dina. Waba`ad:<br />
Inaonyesha kuwa watu wengi wanaishi bila kujua vipi kuishi.<br />
AJABU. Kufa kila mtu anajua, hata mtoto mdogo haitaji<br />
maelezo yoyote kwa suala hilo la kufa. Kutokana na illa hiyo,<br />
tumeonelea iko haja ya kuandika kijitabu kama hiki ambapo<br />
mtu anaweza kustafidi mengi katika suala la kuishi na<br />
kupambana na mitihani ambayo ndiyo hasa lengo lake. Baada<br />
ya kusoma kitabu hiki utashangaa kuona kuwa umefunukiwa<br />
na akili kiupana ambao labda ingekuchukua siku nyingi<br />
kuelewa hakika yake. Balaa, mitihani, fitna na majaribu ni<br />
neno moja ambalo katika kiswahili hatuna sawa yake. Na hata<br />
tukisema misukosuko haitoshelezi kuwa ndiyo balaa, kwa<br />
sababu misukosuko ni neno jingine kabisa. Mnyezi Mungu<br />
ametaja vifwatavyo kama fitna kubwa kwa mtu ; pesa, mke,<br />
watoto, mali, njaa, mauti, upungufu wa mali na kadhalika.<br />
Lakini wengi watashangazwa na listi hiyo pamoja na kuwa<br />
navyo vitu hivyo siku nyingi sana zilizokwisha kupitia<br />
maishani mwetu. Kila kitu kinategemea ilmu na hakuna lolote<br />
ambalo tunalifanza halina ilmu ndani yake.<br />
Qur an Suratul Twaha 20:50.<br />
"(Musa) akasema: “Mola wetu ni yule liyekipa<br />
kila kitu umbo lake kisha akakiongoza (kufuata kinachowafiki<br />
umbo lake hilo).”<br />
Bila ilmu hatuwezi kuongoza njia - Ndo maana Bwana Mtume<br />
SWA. katuambia:<br />
طَلب العلم فريضة على كل مسلم ومسلمة<br />
ii