Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Dajjaal ataingia kila nchi duniani kudanganya na kufitinisha watu.<br />
Ulaghai atoutumia kama vile kumfufua aliekufa siku nyingi na kuleta<br />
mvua na kuotesha mazao mashambani utavutia watu mno kiasi cha<br />
kumwamini kuwa mungu. Yeye atakuwa na pepo na moto. Wataomkubali<br />
atawatia ndani ya pepo yake, wataomkataa atawatia motoni. Lakini ukweli<br />
wa mambo ni kinyume nyume. Watoingizwa peponi ndiyo watoingia<br />
motoni, na wale watoingia motoni ndiyo watoingia pepo ya Mnyezi<br />
Mungu wa kweli. Nchi pekee ambazo hataingia Dajjaal ni Makka na<br />
Madina.<br />
3. Kuteremka seyyidna Isa AS. (Ambaye<br />
atakuja kumpiga vita na kumuondoa (huyo<br />
Dajjaal). Baadaye ataishi siyo kama Mtume, bali<br />
kama mja mwema aliye mchaji ). – Ataoa ataishi<br />
miaka arubaini atakufa, na Madina katika Rawdha<br />
karibu ya Bwana Mtume SAW ndipo atazikwa.<br />
4. Kutokea Juju wa Majuju. (Ambao Dhyl Qarneyn)<br />
aliyewafungia ndani ya ukuta fulani tangu siku hizo hadi leo<br />
hii bila shaka.<br />
5. Kutokea kwa Dabba. (Mnyama wa ajabu ). Mnyama huyu<br />
atawasemeza watu yale ambayo wanakataa kuyakinisha.<br />
Hakika hii .inafahamishwa kwetu na Qur an ya Mnyezi<br />
Mungu; kwa kila mtu kujipatia mwangaza wa mbele kabla<br />
kuwadia wakati wake ambao kutokea karne hii ya ishirini na<br />
moja sio mbali tena.<br />
Tunaanza kuzoeshwa kumzowea mnyama huyo kabla ya kufika<br />
kwake ili tu, tusifikie mshtuko ambao unaweza kuitoa roho ya mtu mbichi<br />
mbichi. Mfano wa “Mapi show” Unajihusisha vizuri sana.<br />
Mnyama huyo atakuwa na mwendo mkali mno, hatakikosa<br />
atakachokifukuza wala hakitampata kitachomfukuza. Ataandika usoni<br />
mwa muumini: “huyu ni mtu wa peponi”. Na uso wa mtu huyo utang`aa<br />
sana. Na katika uso wa mtu wa motoni ataandika: “huyu ni ka fir” na uso<br />
wake utapiga weusi. Na leo praktizi za kujitia weusi zimeanza hali ya<br />
kuwa huyo Dabba wenyewe hajaja. Dabba atakuwa miungoni mwa dalili<br />
za mwisho tena.<br />
6. Kuchomoza jua magharibi ya ardhi:<br />
Hii ni ishara ya wazi wazi yenye kuogofya ( kuogopesha)<br />
mno – <strong>Al</strong>lahu Akbar. Bila ya shaka ionekanapo hitilafu<br />
katika maumbile bin adam hushangaa,<br />
20