You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
“Enyi mliomini jisaidieni (katika mambo<br />
yenu) kwa subira na sala, bila shaka<br />
Mwenyezi Mungu yu pamoja na wanaosubiri.”<br />
Mnyezi Mungu ndiyo huba kubwa (The greatest love). Na kila<br />
anayependa hua hapendi kuwa (kukaa) mbali na mpenzi wake. Basi ikiwa<br />
amri ya mambo ndiyo iko hivyo, basi ni budi kuzidisha subra zetu kila<br />
siku. Fakhri iliyoje kwa watu kusikia kuwa Rais au Mfalme wa nchi yuko<br />
kwa fulani. Siyo yeye yuko kwa Rais au Mfalme, Aa! Rais au Mfalme ndo<br />
yuko kwake au yuko pamoja naye.<br />
Hakuna njia ambapo anafikilia mja katika bahri ya mapenzi yake<br />
kwa Mnyezi Mungu ila kwa kupitia mabalaa. Lakini kwa sababu nafsi ya<br />
neno lenyewe Balaa siyo kiswahili, uzito wake umekuwa na sura ya<br />
tofauti na vile lilivyo hasa. Katika lugha ya kiswahili Balaa inatupa<br />
tafhuma ya hatari isiyoweza kusubiria ndani yake. Na pia inapotafsiriwa<br />
kuwa ni Fitna ndiyo kabisa na inapotafsiriwa kuwa ni mitihani hapa<br />
kidogo ule mmeremeto wa ubaya unapungua kasi. Kadhalika Majaribio<br />
yote ikiwa ni neno lile lile lakini uzito unazidi kupungua, pamoja na kuwa<br />
kwake maneno yote hayo –Balaa, Fitna, Mitihani na Majaribio hakuna<br />
hata moja la kiswahili. Sasa ikiwa hatujapata neno la kiswahili kwa –<br />
“Balaa”- vipi tunaelewa tutakavyo tu. Mnyezi Mungu anatwambia: Qur<br />
an 47:31.<br />
“Na tutakufanyieni mitihani mpaka<br />
tuwadhihirishe (wajulikane ) wale<br />
wanaopigania dini miongoni mwenu na<br />
wanaosubiri, nasi tutadhihirisha habari<br />
zenu.”<br />
8