17.02.2015 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Mnyezi Mungu hataacha kuwajaribu waja ili kuona ni nani wa<br />

kweli mpaka dunia imalizike. Sasa wapi tutakwenda ambako hakuna<br />

Mitihani Fitna na Balaa?<br />

NINI CHA KUFANYA:<br />

Baada ya kwisha kupatapata siri ya Mabalaa sasa na<br />

tujiulize nini la kufanya ndani ya ule muda wa kusubiri?. Lazima<br />

turudi kwenye ile Aya ya 153 ya sura <strong>Al</strong> Baqrah ambapo<br />

tunashauriwa tujisaidie katika mambo yetu kwa Kusubiri na Kusali.<br />

La muhimu ni huko kusali. Kusali kuna maana si moja tu, ya<br />

kusimama, kurukuu na kusujudu. Lakini swala ina sehemu kubwa ya<br />

Dua, nayo ni maombi kwa Mnyezi Mungu. Swala ni Bridge (daraja)<br />

yenye kumuunganisha Mtu na Mola wake, na Ibada maalumu. Sala<br />

ni rehma, na ndiyo maana katika kumswalia Bwana Mtume SAW<br />

hakuna kusimama, kurukuu wala kusujudu, pia katika sala ya maiti.<br />

Kujisaidia mambo yetu kwa sala, tunapata kauli ya Bwana Mtume<br />

SAW kuwa:<br />

(Mnyezi Mungu amejaalia kila kitu silaha,<br />

na silaha ya muumini ni Dua).<br />

Mnyezi Mungu anafundisha vipi tutamuomba; amma kwa jina lake<br />

<strong>Al</strong>lahu au kwa jina lake Rahman Kwingine anatutaka tumuombe<br />

kwa unyenyekevu na kwa khofu, pengine kwa khofu na kwa kutumai<br />

(confidence) na kwa siri au kwa fakhri au kwa sauti ya juu wala si<br />

kwa sauti ya chini lakini baina yake. Qur an 17:57.<br />

“Hao wanaowaomba (wenyewe) wanatafuta<br />

ukaribiano na mola wao; (hata) walio karibu<br />

miungoni mwao (na Mungu, kama malaika wao<br />

wanafanya yaya haya) wanatumai rehma Zake<br />

na wanaogopa adhabu yake. Hakika adhabu ya<br />

Mola wako ni ya kuogopwa.”<br />

9

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!