You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
KUZALIWA KWANGU NA MALEZI YANGU:<br />
“Naona afadhali nielezee kwanza msingi wa malezi.<br />
Nilizaliwa Zanzibar mwisho mwaka 1917 yaani<br />
December kwa mujibu wa Sheikh, yeye atakuwa anamjua<br />
Mzee wangu vizuri kwani alikua ameoa kwao, kwa Babu na<br />
Mama wote Masharifu walozaliwa Ngazija. Babu Abu-Bakkar<br />
Bin Salim, Mama Lydiid Jamallilleye.<br />
Babu mkubwa Sayyid Abdul-Hassan baada ya miaka<br />
miwili yaani 1938 Baba yangu huyo alifariki-Mungu<br />
amrehemu. Na baada ya miaka mitano ya umri wangu mama<br />
alifariki - Mungu amlaze mahali pema . Nikalelewa na Mume<br />
wa Khaalal Ibin Khaalat wa Mama yangu Seyyid Abdul-<br />
Fattaah Bin Ahmed Jamalilley akiitwa sharifu Abudu.<br />
KUANZA KUSOMA:<br />
Nilipelekwa chuoni kwa <strong>Al</strong>-Mar-hum Seyyid Sheikh<br />
Bin Abdul-Rahman Babake Seyyid Hassan Sheikh nikawa<br />
nasoma, na Sala nimesoma kwa Bibi mkubwa mwana-Ashata<br />
kama alivokua akiitwa Aisha lakini wakimwita Mwana-<br />
Ashata.<br />
Nikabaki baada ya kuhitimu nasomesha watoto chuoni huko<br />
huko na Khalafu nikawa nakwenda nasomesha watoto chuoni kwa<br />
Sharifu Abudu, na wakati huo huo tena nikatiwa Skuli, lakini kwa<br />
sababu ya kukawia kuingia Skuli, sikupata Mnazi mmoja.<br />
Nikapelekwa Mwembe-ladu kutoka Kisiwandui asubuhi, ninarudi<br />
halafu nakwenda saa nane tena mpaka mwisho nikaja zangu Mnazimmoja.<br />
Baada ya kusoma miaka mitatu Mwembe-ladu na mwalimu<br />
wa mwanzo wa Skuli hiyo alikuwa Juma Mohamed, wakimwita<br />
Juma Mohamed Mushte - sijui kwanini Mwalimu Juma <strong>Al</strong>lahu-<br />
Yarham.<br />
1.