You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
SAFARI YA PILI AMERIKA:<br />
“Tuliingia mji wa Nishilin na kila mtu akawekwa katika<br />
nyumba fulani, mimi nikawekwa katika Fiski University – pamoja<br />
na President wa Unit Squad Farsuk University pamoja na<br />
President wa hiyo Fiski University alikua ndo anahishimiwa kabisa<br />
New York na ni Mnegro. Hapo alikua na mkewe vile vile wote<br />
watu wahishimiwa sana. Ndo mwenye nyumba nzuri kubwa kabisa.<br />
Wakati wa kula akanambia “Jee! Grace?”; Wakristo<br />
husema kabla ya kula, inaitwa “Grace”, sisi Grace yetu ni:-<br />
“Bismillahir-Rahmanir-Raheem”. Hii ndo kwa ufupi, lakini watu<br />
wajuao kuna vitu zaidi katika vinavosemwa kabla ya kula, lakini<br />
hilo niliona ni refu na “Bismillahir-Rahmanir-Raheem” inatosha<br />
nikafasiri kwa Kiingereza:-<br />
“In the name of God the most compassionate the<br />
most merciful”.<br />
“O! hii sasa tutakua tukiitumia hii inatosha kabisa”. Na<br />
wanao wanafunzi walotoka nchi nyingine za Kiislamu katika<br />
University yao. Baada ya kula wakaniambia vile vile niseme kitu<br />
cha kushukuru kama wanavyofanya wao nikawaambia, siye yetu<br />
nyepesi tunasema:- “<strong>Al</strong>-hamdulillahi-Rabil-alameen”. “Haya<br />
sema” nikawaambia:-<br />
“<strong>Al</strong>l praises are due to God - the Lord the Evolver<br />
of the Universe the Sustainer of the Universe”.<br />
Tukakaa mwisho tukaondoka. Ajabu, namna walivyokaa na<br />
mimi kwa uzuri, mwisho wa mtu kukaa na mtu kwa uzuri sana, tena<br />
hawanijui mwanzo wala mwisho - tena kwa vizuri sana. Nikitaka<br />
kuondoka wemekataa, “Usiondoke”. Hatimae nikaondoka kama<br />
desturi ilivotengnezwa katika Programme.<br />
Nilipofika London nimewaandikia barua, katika barua<br />
nikasema nikatia maneno ya Kiarabu.<br />
“Maa Fil Maqaam Lidhyl Aql Wadhil Adab”<br />
19.