17.02.2015 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Lagha-b-masim-ba Law (Ingekuwa hawajafariki vichaka<br />

wasingepata visindika). Wal-ud fi ardhiha Naw-un minal hatwab<br />

(Na udi pahali pake ni namna tu ya mti katika miti na ukiondoka<br />

pale ndo unatiwa ndani ya moto unatoa harufu nzuri). Watu<br />

wakihimizwa sana kusafiri lakini safari haijaachwa kua taabu “Qitatun<br />

minal adhab” yuko mtu mmoja anasema:-<br />

“Balil Adha-b qit-a minals safar”<br />

“Bali adhabu ni sehemu ya safari”<br />

Na zamani ilikua raha yake kubwa ya safari mnafwatana<br />

mnakua ndugu wamoja, kitu kimoja, mnasaidiana mnashirikiana<br />

mnaona raha katika safari, mnokofika mnapokewa kwa wema, sasa<br />

watu wote kila mmoja kashughulika na lake. Hilo ni moja katika<br />

pahala pamoja tulipowekwa.<br />

Sasa tulipokua huko New York tuliwekwa nyumba inaitwa<br />

„International House‟. Siku moja nimekaa nje pale ninamuona<br />

Mmarekani mmoja kaingia na karatasi anadhania “Islam and<br />

Religion” (Islam na Dini) nikasema huyu amedhania Uislamu si<br />

Dini? nitajaribu kiasi nnachoweza kumfahamisha kua Uislam ni<br />

dini; tena ni dini kuliko dini nyingine zozote bali mbele ya Mnyezi<br />

Mungu hapana inayoweza kuitwa dini illa Uislamu.<br />

“Innad-Deena Indallahil Islam”<br />

“Hakika dini kwa Mnyezi Mungu ni Uislamu)”.<br />

Qur an: 3:19.<br />

Si kwa kua tunaambiwa na Qur an tu, lakini mafundisho yake na<br />

namna zake na maisha yake inaonyesha dini ya kweli, na kwa<br />

Mnyezi Mungu ni Uislamu.<br />

Basi nikaanza nnaingia ninamfahamisha tukenda mpaka<br />

njiani akaniambia: “Basi, basi, mimi ni Muislamu mwenzako, hii<br />

khutba nnakwenda kuitoa YMCA, na namna ulivonieleza, wewe,<br />

naona wewe utaeleza vizuri kuliko ntavoelezea mimi kwa hivo<br />

wewe utakwenda ukaitoe khutba hii na ili nisiikose hukai hapa tena<br />

utakuja kukaa nyumbani”.<br />

Nikamwambia si kitu lakini mimi nimewekwa hapa.<br />

Akawapigia simu walioniweka, yeye yule akataka kujua mie<br />

nimekubali, akanipigia simu akataka kujua Adresi, akapigiwa na<br />

21.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!