You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Lagha-b-masim-ba Law (Ingekuwa hawajafariki vichaka<br />
wasingepata visindika). Wal-ud fi ardhiha Naw-un minal hatwab<br />
(Na udi pahali pake ni namna tu ya mti katika miti na ukiondoka<br />
pale ndo unatiwa ndani ya moto unatoa harufu nzuri). Watu<br />
wakihimizwa sana kusafiri lakini safari haijaachwa kua taabu “Qitatun<br />
minal adhab” yuko mtu mmoja anasema:-<br />
“Balil Adha-b qit-a minals safar”<br />
“Bali adhabu ni sehemu ya safari”<br />
Na zamani ilikua raha yake kubwa ya safari mnafwatana<br />
mnakua ndugu wamoja, kitu kimoja, mnasaidiana mnashirikiana<br />
mnaona raha katika safari, mnokofika mnapokewa kwa wema, sasa<br />
watu wote kila mmoja kashughulika na lake. Hilo ni moja katika<br />
pahala pamoja tulipowekwa.<br />
Sasa tulipokua huko New York tuliwekwa nyumba inaitwa<br />
„International House‟. Siku moja nimekaa nje pale ninamuona<br />
Mmarekani mmoja kaingia na karatasi anadhania “Islam and<br />
Religion” (Islam na Dini) nikasema huyu amedhania Uislamu si<br />
Dini? nitajaribu kiasi nnachoweza kumfahamisha kua Uislam ni<br />
dini; tena ni dini kuliko dini nyingine zozote bali mbele ya Mnyezi<br />
Mungu hapana inayoweza kuitwa dini illa Uislamu.<br />
“Innad-Deena Indallahil Islam”<br />
“Hakika dini kwa Mnyezi Mungu ni Uislamu)”.<br />
Qur an: 3:19.<br />
Si kwa kua tunaambiwa na Qur an tu, lakini mafundisho yake na<br />
namna zake na maisha yake inaonyesha dini ya kweli, na kwa<br />
Mnyezi Mungu ni Uislamu.<br />
Basi nikaanza nnaingia ninamfahamisha tukenda mpaka<br />
njiani akaniambia: “Basi, basi, mimi ni Muislamu mwenzako, hii<br />
khutba nnakwenda kuitoa YMCA, na namna ulivonieleza, wewe,<br />
naona wewe utaeleza vizuri kuliko ntavoelezea mimi kwa hivo<br />
wewe utakwenda ukaitoe khutba hii na ili nisiikose hukai hapa tena<br />
utakuja kukaa nyumbani”.<br />
Nikamwambia si kitu lakini mimi nimewekwa hapa.<br />
Akawapigia simu walioniweka, yeye yule akataka kujua mie<br />
nimekubali, akanipigia simu akataka kujua Adresi, akapigiwa na<br />
21.