Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
kwenda watoe kiasi kadhaa wa kadhaa na wakifika huko<br />
watatizamwa, watakua wageni wa Jumuiya ya Kimarekani moja<br />
wapo – wazungushwe wonyeshwe maisha ya Kimarekani yaliyo<br />
mema kwa mujibu wa vipimo vyao na mengine kwa vipimo vya<br />
watu wote.<br />
Kwa umri waliokua wakiutaka mimi nilikua nimekwisha kua<br />
mtu mzima lakini walipoona application yangu na kuniona<br />
wakanitia kati. Ilikuwa taabu kupata kipando tena, mwisho nikapata<br />
Greck Line ikanichukua mpaka Quebec, mji baada ya mji mpaka<br />
Batholomeo mpaka New York. Njiani bila shaka nikaona Niagara<br />
Falls. Shalalar Niagara – Mmiminiko wa maji katika mahali<br />
wanapokwenda watu kutizama. Pahala pa ajabu penye Nature –<br />
yaani umbo la ajabu.<br />
Bin Adam hajatia mkono wake, wenyewe tu linakwenda –<br />
lipo. Kutoka hapo ndo nkaenda Batholomeo – Batholomeo New<br />
York nkapokelewa na wenzangu wengine mmoja mmoja. Tena<br />
mmoja kutoka London tukakutana huko huko. Nimekwenda<br />
tukakutanika pamoja na Waislamu wawili watatu mmoja mtu wa<br />
Kimasr, mmoja wa Pakistan lakini sasa imekwisha kua kikatiba –<br />
Bangladesh tena. Na Dini nyinginezo na kabila nyinginezo.<br />
Tukachukuliwa kuzungushwa tukapitishwa States mbali mbali, na<br />
kila pahali tunapata fursa ya kupokewa kwa heshima na<br />
kuonyeshwa na kushughulikiwa, na wasaa wa kutoa fikra.<br />
Na bila shaka mtu Muislam kila akipata fursa jambo la<br />
mwanzo hutizama njia awaonyeshe watu nini Uislamu, nini faida<br />
zake nini ukweli wake, na <strong>Al</strong>-hamdulillah sikuziwacha fursa hizo.<br />
Hata unaona Naby Yusuf AS alipoulizwa habari za ndoto na wale<br />
watu wawili katika gereza kabla hajawajibu kawaambia.<br />
“Enyi Wafungwa wenzangu wawili Je! waungu wengi<br />
wanaofarikiana ndio bora (kuabudiwa) au Mnyezi<br />
Mungu mmoja mwenye nguvu (juu ya kila kitu)”.<br />
Qur an: 12:39<br />
“Inni Taraktu Millata Qawm Laa Yuuminun Billahi<br />
Wal-yawmil Akhir”<br />
Qur an: 12:39<br />
7.