You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
MAISHA YAKE.<br />
Sasa naanzia:<br />
Utajo wa kuzaliwa kwake Mwenyi Ezi Mungu atakase siri<br />
yake Bwana <strong>Al</strong>-Maarufu alizaliwa mwaka Saf 1270 Hijra katika<br />
mtaa wa Bajanani, Moroni Ngazija.<br />
<strong>Al</strong>izaliwa katika nyumba iitwayo "Shashanyongo". Baba<br />
yake ndiye aliyemlea. <strong>Al</strong>isoma kuran Ngazija akawa anasoma<br />
kwa Tajwidi.<br />
Baadaye Baba yake alimpeleka Zanzibar si kwa<br />
jingine lolote ila kutafuta ilmu. <strong>Al</strong>ikaa Unguja kiasi ya miaka<br />
mine, takriban akazijua vilivyo fani za Tajwidi, Fiqih, Nahw na<br />
kiasi cha kutosha katika ilmu za hadithi na kuran. Ilmu zote hizi<br />
alizichukua kutokana na mjomba wake Sayyid <strong>Al</strong>i Bin Sultan<br />
Ahmad.<br />
Wakati wa safari yake, Babu yake upande wa mama<br />
yake Sultan Ahmad alimwambia; "Tutafutie ilmu ya haqiq<br />
(undani wa mambo yaliyohusiana na Uungu) kwani sisi hatujui<br />
vilivyo".<br />
Baada ya kusoma ilmu hizo alirejea Ngazija, akashughulika<br />
kukunjua ilmu zote hizi na kuita watu kwa Mwenyi Ezi Mungu<br />
katika msikiti wa Ijumaa. <strong>Al</strong>ianza kusomesha katika tafsiri ya<br />
kuran Jalalain katika wanafunzi wake waliosoma kwake fanni ni<br />
mwalimu wake wa Tajwidi Musa Bin Ahmad.<br />
Muhimu:<br />
Baba yake Sayyid, Mungu amuie Radhi ilikuwa<br />
hakupata mtoto mwanaume. Basi alipohiji akakusudia Madina<br />
kumzuru babu yake, Rehema ya Mwenyi Ezi Mungu na Amani<br />
yake ziwe juu yake, alimuomba Mwenyi Ezi Mungu katika Quba<br />
la mtume (SAW) amruzuku mtoto mwanaume kwa mke wake<br />
mlahirifu Mwana mkuu Bint Sultan Ahmad. <strong>Al</strong>iweka nadhiri<br />
hapo ikiwa Mwenyi Ezi Mungu kamruzuku mtoto mwanamme<br />
1.