You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
wa Mwenyi Ezi Mungu ananiamrisha nitaje Ismul-Jalala".<br />
Sayyidat <strong>Al</strong>awiyya huyu ndiye ambaye Sheikh Abdallah<br />
Darwesh alisema katika kumtaja kumpa cheo chake:<br />
"Wangegawika Muridi mimi ningekuwa pamoja na kikundi<br />
alichomo Sayyidati <strong>Al</strong>awiyya".<br />
Katika siku hizo alikwenda Sayyid kwenye Bustani ya<br />
mama yake ijulikanayo kwa jina la Buzini akakaa huko siku<br />
nyingi awemo ndani ya Khalwa (Muepukano na kila kitu kwa<br />
kushughulika na Mwenyi Ezi Mungu) Hapo ilimjilia kwa daraja<br />
kubwa hali wapatao Mawalii wakubwa ilirejea nayo Mironi<br />
akaingia nyumbani kwa Sheikh Abdallah Bin Himid, akabaki<br />
pamoja naye huko siku tatu bila ya kuingia huko nyumba yoyote.<br />
Baada ya hapo alitoka Sheikh Abdallah Bin Himid<br />
na Sayyid akapanda juu ya sakafu ya nyumba akafika ukingoni<br />
akaanguka, nduguye Sayyid alimchukua mpaka nyumbani kwa<br />
mama yake akabaki nyumbani kiasi ya miezi sita na Ahwal zake<br />
zikizidi hatuwezi kukisia aliyoyapata katika yajayo kutoka na<br />
Mwenyi Ezi Mungu pamoja na yanayoteremka na miminio<br />
alipokuwa katika hali hiyo mara yumo ndani ya صحو mara<br />
nyingine محو pengine huwa عينةkatika na pengine katika<br />
(Maneno haya hayafasirika kwani ni Istilahi za Mabwana حضو ر<br />
Masufi. Hayana maana ya lugha wenyewe wanatambua kwa<br />
Dhawq. Kuyaonja na ekspiriense. - Mfasiri). <strong>Al</strong>iendelea hata<br />
akapata ambayo hatwezi kuyatambua vilivyo na tunahemewa na<br />
kudiriki hakika yake.<br />
Jadhba hii ni mash-hur Ngazija kwa Muridi wote. Yeye<br />
Sayyid alisema wakati katika Jadhba yake "Mimi ni kitu Azizi<br />
mimi ni kitu kilichotokana na Mtume (S.A.W) na ni hasha<br />
Mtume kumpa baba yangu kitu kidhalilifu". <strong>Al</strong>isema:<br />
(Mwenyi Ezi Mungu atunufaishe kwa baraka zake ) "Ingekuwa<br />
bahari ni wino na miti kalamu ili kudhibiti niliyoyaona<br />
bahari ingekwisha na miti ingemalizika kabla ya kumalizika<br />
mambo niliyoyaona katika Jadhba yangu hii".<br />
Baada ya hapo alirejea kukaa na watu kama ada yake ya<br />
mwanzo akasafiri kwenda Hinzwani akateremka Mtsamudu.<br />
Sultan Abdallah alikuwa Bambao alimtaka Sayyid aende huko na<br />
yeye akenda pamoja na baadhi ya Muridi. Sultan Abdallah<br />
akampokea kwa taadhima na mtukuzo, na yeye alikuwa<br />
akijihisabu kuwa ni katika jumla ya Muridu. Katika baadhi ya<br />
10.