Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
mwenye kutizamwa kwa jicho la kusaidiwa na kutengenezewa<br />
kutokana na bwana Muumbaji khalafu alisafiri kwenda Zanzibar<br />
akakutana na Sheikh Uways na akachukua Tarika ya Qadiria<br />
kutokana naye akarejea Ngazija baadaye akenda Nzwani wakati<br />
huo anadhikri kwa Tarika ya Qadiriya wala hakumpa yeyote Ijaza<br />
ya Tarika hiyo, bali baadhi ya nyakati alikuwa hujitenga faragha<br />
akadhikiri peke yake baadae hurejea kwa wapenzi wake.<br />
<strong>Al</strong>iporejea Ngazija haikuchukua muda mrefu ila alifika<br />
Sheikh Abdallah Darwesh alikuwa kafuatana na ndugu yake<br />
Sayyid Abdal Rahman Bin Sheikh na mama yake Sayyidat<br />
Mwana Mkuu wakaja katika jahazi moja.<br />
Sayyid alikutana na Sheikh Abdallah Darwesh alie<br />
mchukulia amana na pakapatikana baina yao mahaba kwa<br />
mtizamano wa mwanzo.<br />
Hayo yalitokea kwa hekima ya Mwenye Ezi Mungu<br />
aliyeumba akatengeneza kila jambo na vipawa vya kukusudiwa.<br />
Sheikh Abdallah alitelemka kwenye kisiwa cha Ngazija<br />
akaingia katika vingi katika vijiji vyake. <strong>Al</strong>ipokuwa anazunguka<br />
katika vijiji hivyo aliona katika baadhi ya njia zake ndege wawili,<br />
mmoja akatoa ubait huu:<br />
شرتث شراب السر مه خمر الصفاء<br />
Wapili nae akatoa ubait huu:<br />
فسكرت لو حقا ومالي منا زعا<br />
Sheikh akaongeza juu ya ubait huu Abyat nyingine kama ilivyo<br />
katika kasida ijulikanayo Ubait wa mwanzo wa qasida hiyo ni:<br />
سقاء في سعاىاالحثية فلم ارى<br />
سواه علي اال طالقا فىاكون المع<br />
mpaka mwisho.<br />
Baadae Sheikh Abdallah alifanya makazi mahali alipozaliwa.<br />
Itsandaa mjini (Huko ndiko alipozaliwa mrithi wa Ahwal za<br />
Mawalii na Maqamat yao Seyyidna <strong>Al</strong>-Habib Omar Bin Ahmad<br />
Bin Sumeit رضوان هللا عايو na baba yake alizaliwa huko huko,<br />
babu yake <strong>Al</strong>-Habib Abubakar ndiye aliyetoka Shibam<br />
Hadhramaut kuja Ngazija- Mfasiri).<br />
Huko kwao Itsandaa Sheikh Abdallah alifungua chuo<br />
cha kusomesha watoto kur-an tukufu na baadhi ya vyuo vidogo<br />
vidogo. Baadhi ya watoto walikua wakikhitimu kuran takatifu<br />
kwa muda wa chini ya miezi sita kwa baraka zake hata wengi<br />
4