17.02.2015 Views

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

Read - Al-Faqeer

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

mwenye kutizamwa kwa jicho la kusaidiwa na kutengenezewa<br />

kutokana na bwana Muumbaji khalafu alisafiri kwenda Zanzibar<br />

akakutana na Sheikh Uways na akachukua Tarika ya Qadiria<br />

kutokana naye akarejea Ngazija baadaye akenda Nzwani wakati<br />

huo anadhikri kwa Tarika ya Qadiriya wala hakumpa yeyote Ijaza<br />

ya Tarika hiyo, bali baadhi ya nyakati alikuwa hujitenga faragha<br />

akadhikiri peke yake baadae hurejea kwa wapenzi wake.<br />

<strong>Al</strong>iporejea Ngazija haikuchukua muda mrefu ila alifika<br />

Sheikh Abdallah Darwesh alikuwa kafuatana na ndugu yake<br />

Sayyid Abdal Rahman Bin Sheikh na mama yake Sayyidat<br />

Mwana Mkuu wakaja katika jahazi moja.<br />

Sayyid alikutana na Sheikh Abdallah Darwesh alie<br />

mchukulia amana na pakapatikana baina yao mahaba kwa<br />

mtizamano wa mwanzo.<br />

Hayo yalitokea kwa hekima ya Mwenye Ezi Mungu<br />

aliyeumba akatengeneza kila jambo na vipawa vya kukusudiwa.<br />

Sheikh Abdallah alitelemka kwenye kisiwa cha Ngazija<br />

akaingia katika vingi katika vijiji vyake. <strong>Al</strong>ipokuwa anazunguka<br />

katika vijiji hivyo aliona katika baadhi ya njia zake ndege wawili,<br />

mmoja akatoa ubait huu:<br />

شرتث شراب السر مه خمر الصفاء<br />

Wapili nae akatoa ubait huu:<br />

فسكرت لو حقا ومالي منا زعا<br />

Sheikh akaongeza juu ya ubait huu Abyat nyingine kama ilivyo<br />

katika kasida ijulikanayo Ubait wa mwanzo wa qasida hiyo ni:<br />

سقاء في سعاىاالحثية فلم ارى<br />

سواه علي اال طالقا فىاكون المع<br />

mpaka mwisho.<br />

Baadae Sheikh Abdallah alifanya makazi mahali alipozaliwa.<br />

Itsandaa mjini (Huko ndiko alipozaliwa mrithi wa Ahwal za<br />

Mawalii na Maqamat yao Seyyidna <strong>Al</strong>-Habib Omar Bin Ahmad<br />

Bin Sumeit رضوان هللا عايو na baba yake alizaliwa huko huko,<br />

babu yake <strong>Al</strong>-Habib Abubakar ndiye aliyetoka Shibam<br />

Hadhramaut kuja Ngazija- Mfasiri).<br />

Huko kwao Itsandaa Sheikh Abdallah alifungua chuo<br />

cha kusomesha watoto kur-an tukufu na baadhi ya vyuo vidogo<br />

vidogo. Baadhi ya watoto walikua wakikhitimu kuran takatifu<br />

kwa muda wa chini ya miezi sita kwa baraka zake hata wengi<br />

4

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!