Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Al</strong>irejea tena Mtsamudu, lakini hakukaa hapo mda mrefu<br />
akatakiwa kwenda Bombo akaenda pamoja na baadhi ya Muridi,<br />
akakaa huko siku kadha wa kadha aliwapa Ijaza huko watu wengi<br />
akafanya khalifa juu yao Sayyid Jaafar baadae alirejea Mtsamudu<br />
akadumu katika Masjid Ar hmani katika kumtaja Rabbu wake.<br />
Hakuwa akienda msikiti wa Ijumaa ila siku ya Ijumaa.<br />
Kupingwa na Sheikh Fadhil na Jawabu ya Sayyid na<br />
yaliyopita baina yao kwa ufupi.<br />
(Mungu awalie Radhi wote wawili na atunufaishe kwa wote)<br />
katika muda huu Sheikh Fadhili alimpinga Sayyid katika<br />
kuwapa Ijaza ya Tarika watu wa Hunzuwani pamoja na kuwa<br />
wao si Ahli kama alivyodai yeye hali ya kutoa Dalili kwa hadithi<br />
"Msiwape hekima wasiostahiki msije mkadhulumu" na katika<br />
hadithi nyingine au utimilifu wa hii au hadith khutba na mimi<br />
ndie Mufti wa Sawahil yote tangu Ras hafun mpaka Ras torfi na<br />
mimi nimezuia dhikri juu yenu au kuisoma mbele yangu. Seyyid<br />
alisimama akasema "Huna njia ya kuzuia dhikri", wakati huo<br />
zogo lilizuka kwa wingi msikitini watu walisimama na kelele<br />
zikaja juu. Kila mmoja akakamata silaha yake, Sayyid nae<br />
alinyanyua upanga wake Sayyid Abdallah Bin Sheikh alitoa nje<br />
upanga wake Sayyid Abdallah Bin Omar Khajar lake akelekea<br />
kwa Sayyid Abdallah Bin Omar aliyeitwa Abood Bin<br />
Muhammad Bin Omar, mtoto wa nduguye Abdallah Bin Omar ni<br />
katika Muridi wa Sayyid. Hapo hapo alimpiga kofi Ami yake<br />
kwa sababu ya wivu juu ya Sheikh wake hivi ndo anavyokuwa<br />
Muridi. Sultan Abdallah alikuwapo msikitini askari wake<br />
wakamzunguka Sayyid akatoka nje ya msikiti akanadi anaetaka<br />
Ijaza na ahudhurie wakahudhuria mbele yake wengi na yeye<br />
pamoja waliokua pamoja naye wanataka jina la Mwenyi Ezi<br />
Mungu. Baadae alitoa sauti akatoa nje upanga wake mbele ya<br />
Sultan Abdallah. Askari walipoona upanga walikimbia, Sayyid<br />
alimshika Sultan mkono akamwambia: "Sema <strong>Al</strong>lah" akawa<br />
anasema pamoja naye wakafuatana nyumbani na waliokuwapo<br />
waliwafuata na wote wanataja jina tukufu mpaka Sultan akaingia<br />
nyumbani kwake.<br />
Assayyid alielekea Mirontsi na kikundi katika Muridi wake<br />
walimfuata lakini hawakufika pamoja naye kwenye msikiti wa<br />
8.