You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
askari ambao walitafuta baadhi ya watu wajulikanao<br />
wakawachukua baadhi yao. Walimtafuta As-Sayyid lakini yeye<br />
alijificha hawakuweza kutambua alipokuwa. Mitsamhuli<br />
ilikuwapo jahazi inakwenda Zanzibar, Sayyid alipanda usiku<br />
wakati ambao wanaomtafuta wameghafilika walipokuwa<br />
hawakumpataSayyid, nchi kavu wazungu walipanda kwenye<br />
jahazi ili watizame ikiwa hajajificha humo jahazini. Walipoingia<br />
jahazini wakaanza kupekua, palivuma upepo mkali na mawimbi<br />
yakachafuka, hapo hapo waliteremka bila ya kumuona, "Na wapi<br />
jicho pofu litaona jua?" wakati huo mnyororo uliofungiwa jahazi<br />
na nanga ulikatika na Jahazi ikaingia baharini matanga<br />
yakapandishwa na jahazi ikatweka kuelekea Zanzibar.<br />
Imewachukua Sayyid na Muridi wake wawili Ahmad<br />
Nakhodha na Abdul-R-rabb jahazi ilipokuwa mbali na nchi kavu<br />
Sayyid alisimama juu ya sitaha akababaika mmoja katika muridi<br />
wake akasema: "Eeh bwana wangu, umejitokeza watu watakuua<br />
iwe sababu ya sisi kuangamia", akajibu "Usihuzunike na sisi kwa<br />
kupenda Mwenyi Ezi Mungu baada ya salat aljumaa tutaingia<br />
Zanzibar. Safari yake ilikuwa jioni ya jumanne. Ikatokea vile vile<br />
kama alivyosema kwani waliingia Zanzibar baada ya salat<br />
aljumaa.<br />
<strong>Al</strong>iishi Sayyid Unguja hata mpaka alipotolewa Sultan<br />
Sayyid <strong>Al</strong>i Ngazija Dola ya kifaransa ndio iliyomtoa. Hapo<br />
alirejea Ngazija na hakusafiri kamwe. Hakuondoka huko hata<br />
Mwenyi Ezi Mungu akamchukua hali ya kuwa yeye Sayyid<br />
karidhia na karidhiwa.<br />
منا فيو رض هللا عنو<br />
12.