26wewe kuelewa hiyo makosa imetoka wapi. Mwisho bwana mwenyekiti unapata hata unafungwa Jela pasipo wewe kuelewakwamba hili kosa limetoka wapi. Kwa mfano bwana mwenyekiti mimi mwenyewe, mwak wa 91, niliweza kufungwa nikuwaBungoma nikapigwa zaidi nikaumizwa pasipo kuelewa kosa kwa sababu nilibandikwa kosa mimi navuta bangi, na mimi katikamaisha yangu mimi zijavuta bangi, hata leo kwa hivyo nikaona bwana mwenyekiti sheria irekebishe mamlaka ambao policewako nayo katika raia, ningeomba sana iwapo Katiba itapitisha police wawe na uhakika wa kuweza kushika mwananchi kwasababu leo nikiongea nikiraramika pengine mwingine hajashikwa kesho mwingine atashikwa.Pili mwenyekiti, mimi maoni yangu ningeomba sana ikiwa mnataka rushwa Kenya iishe, ningeomba haya mwenyekiti, kwasababu mimi nimezaliwa huku, nimetembea Kenya hii nimeona kitukinaitwa chang’aa ihalalishwe na wapeane licence kwasababu hiyo licence wakipeana kwa mtu ambaye anatengeneza chang’aa police hatakuwa na nafasi ya kuenda kushika huyomtu, na hawa wamama ambao wanahangaishwa na pombe hizo watakuwa na nafasi ya kuweza kuuza hiyo pombe kwa sababuserikali itakuwa imepokea ushuru wake, na huyu mtu atakuwa anaendesha hiyo biashara kama biashara zingine ukiangaliapombe kama ya Kenya Brewery hao walipewa licence, na wanaendesha, kwa hivyo mimi maoni yangu ni kuona kwambamtilie maanani chang’aa iwekwe licence sababu rushwa hawawazi tena kupata, sababu police watazidi kuhangaisha watu zaidikuhusu chang’aa na wanapokea hongo nyingi sana na hata mahakama nyingi sana iko kwa police mahakama badia bwanamwenyekiti.Pengine nikienda mbio kwa sababu ya wakati, katika uhuru wa kuweza kuabudu, bwana mwenyekiti mimi ningeomba kamam<strong>kenya</strong> kama mwafrika iwe kama sheria sababu hata tukisoma bibilia ama Koran, Mungu ana ruhusu mwanamume kuoamwanamke isiwe mwenyekiti tafadhali kama sheria baadaye katika Kenya yetu hii ambayo tunataka uhuru tusije tukakuwa nanafasi ama mtu mwanamume kuoa mwingine, hiyo ni makosa sana hata kwa Mungu kwa sababu hata bibilia ama koranainasema ulawiti ni dhabi halafu mwanamke asikuwe na nafasi yake ama kuoa mwingine. Bwana mwenyekiti nikienda mbio mimininaomba sana unapata katika shida ya mashamba ambao wenzangu wametaja hapa mwenyekiti, mimi ninaweza kuwaninashamba langu la acre 10, na unaweza kupata tajiri anakuja ananinyang’anya hiyo shamba ambayo ni ya babu yangu, pasipomimi kuelewa sababu mimi sina pesa bwana mwenyekiti, huyu mtu atatumia unjanja fulani kuenda mahakamani, ama kuendakatika lands na anatumia makaratasi na anapata title deed mnapata hata mimi pengine baba aliweza kunipatia title deed. Lakiniutapata kuona kuwa huyu mwenyekiti mtu anakuja na pesa na ana nguvu, anaenda police unashtuka tu wanakufukuza kwashamba ambayo ni ya babu yako kwa kweli, hiyo kitu ina tuudhi tena ndio inaongeza vita katika Kenya hii ambayo tunaishisasa. Bwana mwenyekiti mimi maoni yangu muangalie hilo neno kwamba Katiba ipitishe mahakama ama lands isikuwe nauwezo wa kuweza kupeana title deed kwa shamba bila mwenyewe, tafadhali mwenyekiti muangalie kwa Kenya yetu ambavyovinakunja kwa vizazi ambazo zinakunja.Lingine bwana mwenyekiti ningeomba sana kama hawa <strong>of</strong>ficer wetu wa nyumbani wa utawala kama chief na assistant chief.Ningeomba sana kama nyinyi kama ma-Commissioner ambao mnachukua maoni yetu, kwa Kenya ambayo inakuja ningeombasana chief akuweko peke yake. Halafu assistant chief aondolowe kwa sababu huyo mtu ndio anaongeza fitina kati ya
27wananchi, kwa hivyo mwenyekiti mimi ninaona kwamba kama m<strong>kenya</strong> sababu mimi saa hii nina watoto niko mzazi lakiniunaweza kupata barua zingine bwana assistant anaweza kukuharakisha ama ana kupeleka hata kwa police pasipo wewekuelewa kwa sababu ana chuku Fulani kati ya wewe na yeye, yeye anaweza kutumia hiyo priority kwa sababu sasa yeye nimtawala anasema mimi ninajua huyu mtu lazima mumfanyie baadaye hivi unapata shida nyingi sana.Mwenyekiti nikimalizia mimi ningeomba sana uhuru wa kuabudu katika makanisa ukuweko sana kwa sababu mimi kamamkristo, mara nyingi nimepata shida, siku moja tulivamiwa na police katika kanisa tukapigwa marungu mpaka hatatukajeruhiwa. Mimi ningeomba sana sheria ipitishwe kanisa waheshimu kwa sababu Mungu ndio mkubwa kushinda sisi, hatakama kuna mtu amekosa, ama kwamba kuna makosa yoyote bwana mwenyekiti, police wangojee ibada ikwishe halafuwaweze kuitisha mtu huyo ambaye wanamtaka ama hawa watu na waweze kuwauliza ama kuwachukua, kuliko police kuingiakatika kanisa na kuvamia wale waumini na kuwapiga hata unaweza kupata wanapiga Pastor, ni kitu cha aibu sana, wanararuahata Kola ya shingo ni kitu kingine kichefu bwana mwenyekiti, tuangalie hilo kama Kenya ambayo tulipata uhuru. Linginekatika upande wa utawala bwana mwenyekiti, Rais ambaye anakunja, mimi siwezi kusema kwa leo ambaye atakunja asikuwena wajibu wa kutuchagulia kiongozi, sisi kama wa Kenya wenyewe ama kama raia tuweze kuchagua kiongozi ambaye anawezakutuongoza na muhula wa Raisi wa kuongoza uwe miaka kumi, ikiwa yeye ni mzuri, kwa tano tutamuongezea, hata kama yeyeatakuwa kama dhahabu, lulu hatuwezi kumuongeza zaidi ya kumi, tafadhali bwana mwenyekiti, asante Sababu niseme hivyomwenyekiti tukitaka maendeleo kwa mfano, ya kutujenga un…..Interjection Com Nunow: one more minute give us your last two points,George: Asante mwenyekiti, mimi katika upande wa Rais ndio mimi nitabakia, Rais ambaye tunaweza kumchagua kwa miakamitano, akuwe na wajibu wa kuweza kuangalia Kenya mahali ambayo haijaendelea iaiinue, ni wajibu wangu sana ambao miminina waomba Commission hii iangalie hio neno baadaye ili huyo Rais mahali yule ambaye alikuwa anaongoza kama aliazishamirandi kama ameshastaafu ama ametoka yeye achukue hiyo miradi akiendeleza mfano mashule, mahospitali, na hatamakanisa. Asante mwenyekiti.Com.Nunow: Thank you asanti George tafadhali ujiadikishe pale, Zainabu Muyoti,Zainabu Muyoti: Kwa majina naitwa Zainabu Muyoti natoka Mungatii sub-location, Buhayo East Location.Preamble: Katika jina la mwenyezi Mungu Katiba yetu idumu, hii ni Katiba ya watu wa Kenya. Tunakumbuka mashunjaawaliopigania uhuru wetu hasa wanawake waliotunza masilahi ya wanaume wakiwa msituni. Bwana mwenyekiti, lugha ambayoilitumika kwa vile vijitabu, ya marekebisho ya taifa ya kiswahili ilikuwa ngumu sana kwa watu wa bara kuelewa. Ilitakikanampaka mtu awe na kamusi labda ndio ataweza kuelewa vifungu vingine.
- Page 1 and 2: CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMIS
- Page 3 and 4: 3Mungu wetu umetuongoza na wakati h
- Page 5 and 6: 5wanakaribisha wageni vizuri sana,
- Page 7 and 8: 7wanataka kuzungumzia hayo maandish
- Page 9 and 10: 9Legislature. A patient should have
- Page 11 and 12: 11the death sentence should be outl
- Page 13 and 14: 13and another person has no plot to
- Page 15 and 16: 15Christine Omondi: My names are Ch
- Page 17 and 18: 17police force the GSU which is of
- Page 19 and 20: 19Godfrey: My understanding is that
- Page 21 and 22: 21to one foot from the water along
- Page 23 and 24: 23Josiah: Nataka watu maskini wapew
- Page 25: 25The Attorney General, the speaker
- Page 29 and 30: 29road blocks sasa hawa watu wa mat
- Page 31 and 32: 31nilijifunza agriculture British R
- Page 33 and 34: 33Primary schools, na saa hii hulip
- Page 35 and 36: 35Com.Nunow: Asante sana bwana Makh
- Page 37 and 38: 37Andrew: Efe badidi ba inyuma enoT
- Page 39 and 40: 39Andrew: mbara nibiakhuba mbu omun
- Page 41 and 42: 41kurudi kwa kazi. Mtu anayetaka ka
- Page 43 and 44: 43Secondly is the early marriages t
- Page 45 and 46: 45secretary akikufa au Minister ame
- Page 47 and 48: 47kwa korti. Watu wanasukuma na mpa
- Page 49 and 50: 49not unduly interfere with the oth
- Page 51 and 52: 51waislamu na wasio waislamu au wai
- Page 53 and 54: 53huku wanapata mishahara minono, n
- Page 55 and 56: 55know exactly what they stand for,
- Page 57 and 58: 574. Too many road blocks which do
- Page 59 and 60: 59zikichukua miaka mingi, watu weng
- Page 61 and 62: 61Point number three, is on somebod
- Page 63 and 64: 63Cornelia: Hilo linakuwa na mimi n
- Page 65 and 66: 65and he will also be part of the E
- Page 67 and 68: 67covered, but I would like highlig
- Page 69 and 70: 692 Electoral Commissioners, those
- Page 71 and 72: 71one has failed us terribly.The Ex
- Page 73 and 74: 73President being above the law. He
- Page 75 and 76: 75Jonathan: Eliakhubiri omundu akho
- Page 77 and 78:
77huko nyuma mimi ndie nina-deal na
- Page 79 and 80:
79official one Identity card that c
- Page 81 and 82:
81Jambo lingine la kumalizia nasema
- Page 83 and 84:
83serikali vile unafanya hivi, mtot
- Page 85 and 86:
85tafadhali wanasiasa, au viongozi
- Page 87 and 88:
87nitasema tu neno moja ya assistan